Swahili na Waswahili

Swahili na Waswahili
Waswahili na Mswahili Rachel Siwa...Pamoja Daima!!
Showing posts with label Hongera. Show all posts
Showing posts with label Hongera. Show all posts

Monday 1 August 2011

Siku kama ya Leo Rachel-Siwa Alizaliwa!!!!!!!!

Siku kama ya leo, Familia ya Bibi na Bwana M.S. Kiwinga walibahatika kupata mtoto  wa kike ;Rachel-siwa.
Nawashukuru sana Wazazi wangu kwa Malezi yenu mema na  yote mliyonitendea.
Pia nakushukuru sana kaka yangu R.Kiwinga kwa kupokea ulezi na kunitunza, Tangu pale Baba alipofariki mpaka pale uliponikabidhi kwa Mume,Sina cha kukulipa bali sitoacha kukuombea.


Ahsante sana Mume wangu Issac kwa yote na kuwapamoja siku zote mpaka 27/07/11 yaani j'tano iliyopita tumetimiza miaka 15 ya ndoa yetu,Mungu atubariki sana katika maisha yetu.

Basi niwashukuru Ndugu,Jamaa,Marafiki zangu woooooteee, kwa Yote,kwani nikiandika hapa hapatatosha.


NENO LA LEO; Nijaposema kwa lugha za wanadamu na za malaika,kama sina Upendo,nimekuwa shaba iliyo na upatu uvumao.Tena nijapokuwa na unabii,na kujua siri zote na maarifa yote,nijapokuwa na imani timilifu kiasi cha kuweza kuhamisha milima, kama sina Upendo,si  kitu mimi.Tena nikitoa mali zangu zote kuwalisha maskini, tena nikijitoa mwili wangu niungue moto, kama sina Upendo, hainifaidii kitu. Upendo Hufadhili; Upendo Hauhusudu; Upendo Hautakabari; Haujivuni; Haukosi kuwa na adabu; Hautafuti mambo yake; Hauoni uchungu; Hauhesabu mabaya; Haufurahii udhalimu,bali Hufurahia pamoja na kweli.!!!


MUNGU ATUBARIKI SOTE!!!!!!!!!

Tuesday 26 July 2011

Kaka Joel Ahitimu!!!!!!!!!

                          Kaka Joel mwenye Furaha.
                                 Duhh sitakuwa nao tena rafiki zangu,hii sasa mbaya kwangu!
                        Dada Jolen akimpongeza kaka.
               Nimeshakuwa mwanakijiji sasa!


Kaka Joel Amehitimu Nursery tayari kwa kuanza/kuingia Reception hapo September.
Joel!! Baba na Mama pamoja na Familia ya Mwasanjala na Shushu,Wanakutakia kila lililo jema katika safari yako ya kutafuta Elimu.


Rafiki[dada] yako kipenzi Tracey anakutakia mema katika masomo yako!


Nasi SwahilinaWaswahili tunakuombea Mungu awe pamoja nawe katika yote.


Mpendwa wewe ulipitia VIDUDU/Nursery?...Je unakumbukumbu gani katika hayo ni Uji,Nyimbo,Kulialia,Ulikutana na watoto Wababe au wewe ndiyo ulikuwa Mbabe!!!!!!


Karibuni sana Waungwana katika Yote!!!!!!!!

Sunday 17 July 2011

Sandra Atimiza miaka 13!!!!!!

                                 Sandra-Neema, akishangaa duh13!

                         Leo natimiza 13,kweli siku hazigandi,kaka Brian akihakikisha.
                    Sandra na Tracey, mwenzangu tumekuwa sasa.
                 Wageni kutoka Birmingham nao walikuwepo.
                               Dada Damari akisimamia watoto wa Swahili Fellowship.
                   Joel,Jolin na Tracey katika poziiiiii.
                     Manjula,Eireen,Shambara na mgeni wao hawakukosa.
                        Miriam na kaka Ebeneza nao walikuwepo.
                                      Sandra &Tracey wakishukuru wageni kwakuwa nao pamoja.
                   Mama na Sandra Tunamalizia.
Familia ya Isaac tuna Mshukuru sana Mungu kwa Yote aliyotutendea,Pia tunawashukuru wote mlio jumuika nasi kwa namna moja au nyingine.Shukrani za pekee kwa Uongozi wa Watoto wetu Coventry Swahili Fellowship,Chini ya Mwenyekiti Da'Mija na msaidizi wake da'Damari.
Mungu awabariki  wote na Tunawapenda sana.

Thursday 30 June 2011

Leo Anita Nyotu Atimiza Miaka 5!!!!!!

                                    Dada Anita katika tabasamu.

                               Keki ikikatwa.
                                    Baba akilishwa.
                        Mama akilwalikuwa wanatupata  Live.ishwa, huko Kenya
                                Mama Soph akituwakilisha Wazazi tuliokuwepo.
                             Watoto wasipo onja keki ,hakitaeleweka hapo.
                        Hapa ndipo penyewe kwa Watoto.
                             Hapa tulilegeza mikanda,Nyama choma kwa ugali,wenyewe waita[SIMA].
                            Baba na Mama wakitoa zawadi.
                                         Sandra&Tracey wakitoa chao.
                           Dada Soph&Ruth na  kaka Joseph & Nick walito chao.
                              Saviour & Tiffany walito zawadi yao.
                                 kaka James na wadogo zake nao walitoa yao.
                 Shosho[bibi] na familia huko Kenya tuliungana nao moja kwa moja,Kama unavyoona!!
                      Hali ya hewa leo ilikuwa inaruhusu kucheza nje!
                                Michezo ndiyo kama hiyo ni mwendo wa kuruka.
                                 Picha ya pamoja,hizi baada ya miaka 10 duhh.
                           Bibi ya Nyotu [mke wa Nyotu] Akitoa shukrani kwa waliofanikisha siku hii.
                        Bila kuwasahau Nyumbani Kenya kwa kuwa pamoja.


Nami kwa niaba ya wote tulioshiriki tunasema Ahsante sana.Pia kwa kujali muda,
Tuliambiwa saa 5 mpaka saa 8 mchana, na ilikuwa hivyo, mwenye kwenda kazini haya,
mwenye kuwahi kumpika mumewe [bwana] haya!!!!!!!

Sunday 19 June 2011

Leo ni Siku ya wa BABA!!!!!!!!

                                  Sandra & Tracey na Baba yao.[Faraja Yangu ].
                                        Joel & Jolen na Baba yao.
                                         Arianna na BABA!!.
.
                                     Baba Paulina.
                                        Sabrina na BABA.
                                      Jawahiri na BABA.
                                       Anna-Harrieth na BABA.
Nawatakia Kheri wa BABAWote popote mlipo, Mungu awabariki sana.
Tuwe bega kwa bega katika malezi ya watoto,Kama si Baba tusingeitwa mama.
Pia Shukrani kwa baba yangu Mpendwa [R.I.P]


Kama una Picha au salamu kwa BABA  yeyote Rukhsaaaaaa!!!! Tuma kupitia Rasca@hotmail.co.uk


Wapendwa kina BABA wa leo/kisasa  na Wazamani,  Kundi lipi linaongoza Kutelekeza Watoto/Familia?
Na Sababu ni nini, Nyumba ndogo, Ulevi,Ujana,Umimi au...........

Saturday 11 June 2011

Siku kama ya Leo Mash-P Alizaliwa!!!!!!!

Hongera  kaka Mash-p kwa kuongeza mwaka mwingine! Tunakutakia kila la kheri na baraka katika Yote.
Mungu akuongezee Miaka mingine Mingi.

Tuesday 31 May 2011

Siku kama ya Leo dada Upendo Penza Alizaliwa!!!!!!!!

Dada/Mdogo wetu Upendo[Mwana Penza].Siku kama ya leo alizaliwa na kuongeza idadi ya watoto wa Familia ya Bibi na Bwana J,Penza.Pia idadi ya Wajukuu wa Penza.Upendo ana Upendo na Mtu wa Vichekesho na Utani mwingi sana,Pia ana huruma na niwakujitoa sana kwa kila jambo,Liwe la Familia,Marafiki na Majirani. Kama mwanafamilia ninakuwa na wakati mzuri sana kuwa nae popote,  Hasa kwenye mikusanyiko ya kifamilia,Hata ikiwa ya majonzi basi baada ya muda kidogo  mtacheka tuu.
      Upendo, Tunakutakia kila la kheri na baraka katika maisha yako na uwe na wakati mzuri leo na siku zote.


Je mpenzi msomaji eti jina linaendana na Matendo ya mtu?kama vile ukimpatia mtoto jina la Shida na kweli Shida zitamuandama? au Imani za Waswahili/Watu?.


Monday 23 May 2011

Tracey atimiza miaka 10!!!!!!!!!!!!!

 Tracey-Sarah, Ametizimiza miaka 10,hapo amepozi akitafakali duhh nimekuwa dada sasa.

 Yaani mimi ndiyo nimefika maika hii?



 Kikosi kamili cha Watoto wa Coventry Christian Swahili Fellowship,Kikiongozwa na dada mkuu dada Damari Kihauka chini ya Mwenyekiti da Mija. Nitakueleza Siku nyingine mambo mengi kuhusu kikosi hiki!!!!!!

 Tracey na dada Damari wakitayarisha Keki ili kila mmoja apate.



                                       


                      Tracey akipokea zawadi maalum kutoka kwa kaka Joel.
 Wamama nao hawakuwa nyuma,kwaniaba ya Wazazi wote wa Swahili Felloship.

                                   dada Tracey-Sarah anasema Asanteni sana na Mungu awabariki!!!!!!!