Swahili na Waswahili

Swahili na Waswahili
Waswahili na Mswahili Rachel Siwa...Pamoja Daima!!

Friday 22 May 2020

Kikombe Cha Asubuhi; Hosea 8..

Shalom,Habari za Asubuhi,Hamjambo,Mmeamkaje?

Tumshukuru Mungu wetu katika yote...

Asante  Mungu wetu kwa wema na fadhili zako kwetu
Asante kwa ulinzi wako kwetu wakati wote
Asante kwa kutuchagua tena na kutupa
kibali cha kuendelea kuiona leo hii
Asante kwa pumzi/uzima,afya na kuwatayari kwa majukumu yetu


Utukuzwe ee Mungu wetu,usifiwe Baba wa Mbinguni

Neema yako yatutosha  Mungu wetu..!

Basi, tuzingatie kwa makini imani tunayoiungama. Maana tunaye Kuhani Mkuu aliyeingia mpaka mbinguni; Yesu, Mwana wa Mungu.
Baba wa Mbinguni tunakuja mbele zako tukijinyenyekeza,
tukijishusha na kujiachilia mikononi mwako

Mungu wetu tunaomba utusamehe dhambi zetu zote
Baba wa Mbinguni nasi tunaomba utupe neema ya kuweza kuwasamehe wale wote waliotukosea,Usitutie majaribuni Mungu wetu tunaomba utuepushe na yule mwovu na kazi zake zote,Jehovah ututakase miili yetu na akili zetu Baba wa Mbinguni tunaomba utufunike kwa  Damu ya Bwana na Mwokozi wetu Yesu Kristo wa Nazareti,
Yeye aliteseka kwanza ili sisi tupate kupona....

Huyu Kuhani Mkuu wetu anaelewa kabisa unyonge wetu; yeye mwenyewe alijaribiwa kama sisi kwa kila namna lakini hakutenda dhambi.
Mungu wetu tunaomba ukabariki kazi za mikono yetu
Baba wa Mbinguni tunaomba ukatupe ubunifu na maarifa 
katika utendaji
Jehovah nasi tukatende sawasawa na mapenzi yako
Baba wa Mbinguni tunaomba ukabariki ridhiki zetu
ziingiazo/zitokazo
Mungu wetu nasi tunaomba ukatupe neema ya kuweza
kuwabariki wenye kuhitaji
Yahweh tusipungukiwe katika mahitaji yetu
Mungu wetu ukatupe kama inavyokupendeza wewe



Jehovah tunayaweka maisha yetu mikononi mwako
Baba wa Mbinguni tunaomba ukabariki nyumba/ndoa zetu,
watoto,wazazi wetu,familia/ndugu na wote wanaotuzunguka
Jehovah tunaomba ulinzi wako kwetu na kwa vyote tunavyo vimiliki
Yahweh tunaomba ukatubariki tuingiapo/tutokapo
Mungu wetu tunaomba ukavibariki vyote tunavyoenda kugusa/kutumia
Baba wa Mbinguni ukavitakase kwa Damu ya Bwana wetu Yesu Kristo
Mungu wetu ukatamalaki na kutuatamia
Baba wa Mbinguni tukawe salama rohoni
Mfalme wa amani amani yako ikatawale katika maisha yetu
Mungu wetu ukatupe macho ya kuona na masikio ya kusikia 
sauti yako na kuitii
Baba wa Mbinguni tunaomba ukatupe neema ya kufuata njia zako
Yahweh tukasimamie Neno lako amri na sheria zako siku zote 
za maisha yetu

Mungu  wetu ukaonekane katika maisha yetu popote tupitapo na ikajulikane kwamba upo 

Neema zako zikawe nasi Nuru yako ikaangaze katika maisha yetu
Ukatufanye barua njema ee Mungu wetu nasi tukasomeke kama
inavyokupendeza wewe
Roho Mtakatifu akatuongoze katika yote na tukawe na kiasi...

Basi, na tukikaribie bila hofu kiti cha enzi cha Mungu mwenye neema, tupokee huruma na neema ya kutusaidia wakati wa shida.
Tazama wenye shida/tabu,Mungu wetu tunaomba
 ukawaguse kila mmoja na mahitaji yake
Baba wa Mbinguni tunaomba ukawasamehe pale walipokwenda
kinyume nawe
Mungu wetu ukawape neema ya kujiombea,macho ya rohoni,masikio yakusikia sauti yako,wakafuate njia zako nazo zikawaweke huru
Mungu wetu tunaomba ukasikie kulia kwao
Baba wa Mbinguni tunomba ukawafute machozi yao
Nuru yako ikaangaze katika maisha yao
Mungu wetu tunaomba ukawatendee sawasawa na mapenzi yako
Kwakuwa Ufalme ni wako Nguvu na Utukufu hata Milele
Amina....!!!


Wapendwa katika Kristo Yesu asanteni sana
kwakuwanami/kunisoma

Mungu Baba aendelee kuwabariki na kuwatendea
kama inavyompendeza yeye
Amani ya Bwana wetu Yesu Kristo na upendo wa Mungu Baba
ukae nanyi daima....

Nawapenda.

Makosa makuu ya Israeli
1“Pigeni baragumu!
Adui anakuja kama tai
kuivamia nyumba ya Mwenyezi-Mungu,
kwa kuwa wamelivunja agano langu
na kuiasi sheria yangu.
2Waisraeli hunililia wakisema:
‘Mungu wetu, sisi tunakujua.’
3Lakini Israeli amepuuza mambo mema,
kwa hiyo, sasa adui watamfuatia.
4“Walijiwekea wafalme bila kibali changu,
walijiteulia viongozi ambao sikuwatambua.
Wamejitengenezea miungu ya fedha na dhahabu,
jambo ambalo litawaangamiza.
5Watu wa Samaria, naichukia sanamu yenu ya ndama.
Hasira yangu inawaka dhidi yenu.
Mtaendelea mpaka lini kuwa na hatia?
6Nanyi Waisraeli ni hivyohivyo!8:6 Nanyi … hivyohivyo: Labda iwe hivyo. Kiebrania: Tena kutoka Israeli.
Na sanamu yenu hiyo fundi ndiye aliyeitengeneza.
Yenyewe si Mungu hata kidogo.
Naam! Sanamu ya ndama ya Samaria itavunjwavunjwa!
7“Wanapanda upepo, watavuna kimbunga!
Mimea yao ya nafaka iliyo mashambani
haitatoa nafaka yoyote.
Na hata kama ikizaa,
mazao yake yataliwa na wageni.
8Waisraeli wamemezwa;
sasa wamo kati ya mataifa mengine,
kama chombo kisicho na faida yoyote;
9kwa kuwa wamekwenda kuomba msaada Ashuru.
Efraimu ni punda anayetangatanga peke yake;
Efraimu amekodisha wapenzi wake.
10Wametafuta wapenzi kati ya watu wa mataifa,
lakini mimi nitawakusanya mara.
Na hapo watasikia uzito wa mzigo,
ambao mfalme wa wakuu8:10 Mfalme wa wakuu: Jina lingine la mfalme wa Ashuru. aliwatwika.
11“Watu wa Efraimu wamejijengea madhabahu nyingi,
na madhabahu hizo zimewazidishia dhambi.
12Hata kama ningewaandikia sheria zangu mara nyingi,
wao wangeziona kuwa kitu cha kigeni tu.
13Wanapenda kutoa tambiko,
na kula nyama yake;
lakini mimi Mwenyezi-Mungu sipendezwi hata kidogo.
Mimi nayakumbuka makosa yao;
nitawaadhibu kwa dhambi zao;
nitawarudisha utumwani Misri.
14Waisraeli wamemsahau Muumba wao,
wakajijengea majumba ya fahari;
watu wa Yuda wamejiongezea miji ya ngome,
lakini mimi nitaipelekea moto miji hiyo,
na kuziteketeza ngome zao.”

Hosea8;1-14

Biblia Habari Njema kwa Watu Wote(BHN)

"Swahili Na Waswahili"Mbarikiwe

No comments: