Swahili na Waswahili

Swahili na Waswahili
Waswahili na Mswahili Rachel Siwa...Pamoja Daima!!

Thursday 28 May 2020

Kikombe Cha Asubuhi; Hosea 12..


Shalom,Habari za Asubuhi,Hamjambo,Mmeamkaje?

Tumshukuru Mungu katika yote....

Mungu wetu Baba yetu,Muumba wetu Muumba wa Mbingu na Nchi
Muumba wa vyote vilivyomo vinavyoonekana na visivyoonekana
Mungu wa walio hai,Mungu  mwenye huruma,Mungu wa upendo
Mungu wa Abrahamu,Isaka na Yakobo...
Asante kwa wema na fadhili zako kwetu
Asante kwa ulinzi wako kwetu wakati wote
Asante kwa kutuchagua tena na kutupa
kibali cha kuendelea kuiona leo hii
Asante kwa pumzi/uzima,afya na kuwatayari kwa majukumu yetu

Neema yako yatutosha ee Mungu wetu....!!

Mwenyezi-Mungu asema: “Piga kelele, wala usijizuie; paza sauti yako kama tarumbeta. Watangazie watu wangu makosa yao, waambie wazawa wa Yakobo dhambi zao. Siku hata siku wananijia kuniabudu, wanatamani kujua mwongozo wangu, kana kwamba wao ni taifa litendalo haki, taifa lisilosahau sheria za Mungu wao. Wananitaka niamue kwa haki, na kutamani kukaa karibu na Mungu.
Baba wa Mbinguni tunakuja mbele zako,
Tukijinyenyekeza,tukijiachilia mikononi mwako
Mungu wetu tunamomba utusamehe dhambi zetu
Baba wa Mbinguni nasi tunaomba ukatupe neema
 ya kuweza kuwasamehe wale wote waliotukosea

Usitutie majaribuni Mungu wetu tunaomba utuepushe
na yule mwovu na kazi zake zote
Jehovah ututakase miili yetu na akili zetu
Baba wa Mbinguni tunaomba utufunike kwa Damu
ya Bwana na Mwokozi wetu Yesu Kristo wa Nazareti
yeye aliteseka kwanza ili sisi tupate kupona....

“Nyinyi mnaniuliza: ‘Mbona tunafunga lakini wewe huoni? Mbona tunajinyenyekesha, lakini wewe hujali?’ “Ukweli ni kwamba wakati mnapofunga, mnatafuta tu furaha yenu wenyewe, na kuwakandamiza wafanyakazi wenu!
Mungu wetu tunaomba ukabariki kazi za mikono yetu
Baba wa Mbinguni tunaomba ukatupe ubunifu na maarifa katika utendaji
Jehovah nasi tukatende sawasawa na mapenzi yako
Yahweh tunaomba ukabariki ridhiki zetu ziingiazo/zitokazo
Mungu wetu nasi tunaomna ukatupe neema ya kuweza kuwabariki wenye kuhitaji
Tusipungukiwe katika mahitaji yetu
Baba wa Mbinguni tunaomba ukatupe kama inavyokupendeza wewe...


Yahweh tunayaweka maisha yetu mikononi mwako
Mungu wetu tunaomba ukabariki nyumba/ndoa zetu,
Jehovah tunaomba ulinzi wako kwetu na kwa vyote tunavyovimiliki
Yahweh tunaomba ukatubariki tuingiapo/tutokapo
Mungu wetu tunaomba ukavibariki vyote tunavyoenda kugusa/kutumia
Baba wa Mbinguni ukavitakase kwa Damu ya Bwana wetu Yesu Kristo
Mungu wetu ukatamalaki na kutuatamia
Baba wa Mbinguni tukawe salama rohoni
Yahwe ukatupe akili ya kutambua mema na mabaya
Mfalme wa amani amani yako ikatawale katika maisha yetu
Mungu wetu ukatupe macho ya kuona,masikio ya kusikia sauti yako na kuitii..
Baba wa Mbinguni  tunaomba ukatupe neema ya kufuata
njia zako,tukasimamie Neno lako,amri na sheria zako
siku zote za maisha yetu...
Ukatuguse kwa mkono wako wenye nguvu,ukatufanye chombo chema
ee Mungu wetu nasi tukatumike kama inavyokupendeza wewe
Roho Mtakatifu akatuongoze katika yote na tukawe na kiasi....

Mnafunga, na kugombana na kupigana ngumi. Mkifunga namna hiyo maombi yenu hayatafika kwangu juu. Mfungapo, nyinyi mnajitaabisha; mnaviinamisha vichwa vyenu kama unyasi, na kulalia nguo za magunia na majivu. Je, huo ndio mnaouita mfungo? Je, hiyo ni siku inayokubaliwa nami?
Tazama watoto wako wenye shida/tabu,wote wanaopitia magumu/majaribu mbalimbali
Mungu wetu tunaomba ukawaguse kwa mkono wako wenye nguvu
kila mmoja na mahitaji yake
Mungu wetu tunaomba ukawasamehe pale walipo kwenda kinyume nawe
Yahweh tunaomba ukawape neema ya kuweza kujiombea,kufuata njia zako nazo zikawaweke huru...
Baba wa Mbinguni tunayaweka haya yote mikononi mwako
Kwakuwa Ufalme ni wako Nguvu na Utukufu hata Milele...
Amina...!!


Asanteni sana wapendwa katika Kristo Yesu kwakuwa nami,Baba wa Mbinguni aendelee kuwatendea sawasawa na mapenzi yake...

Nawapenda.

1Watu wa Efraimu wananirundikia uongo,
na Waisraeli udanganyifu.
Watu wa Yuda, wananiasi mimi Mungu Mtakatifu.
2“Watu wa Efraimu wanachunga upepo
kutwa nzima wanafukuza upepo wa mashariki.
Wanazidisha uongo na ukatili,
wanafanya mkataba na Ashuru
na kupeleka mafuta Misri.”
3Mwenyezi-Mungu ana mashtaka dhidi ya Yuda;
atawaadhibu wazawa wa Yakobo kadiri ya makosa yao,
na kuwalipa kadiri ya matendo yao.
4Yakobo akiwa bado tumboni mwa mama yake,
alimshika kisigino kaka yake.
Na alipokuwa mtu mzima
alishindana na Mungu.
5Alipambana na malaika, akamshinda;
alilia machozi na kuomba ahurumiwe.
Huko Betheli, alikutana na Mungu,
huko Mungu aliongea naye.
6Mwenyezi-Mungu, wa majeshi,
Mwenyezi-Mungu, ndilo jina lake.
Lakini nyinyi mrudieni Mungu wenu.
Zingatieni upendo na haki,
mtumainieni Mungu wenu daima.
7“Efraimu ni sawa na mfanyabiashara
atumiaye mizani danganyifu,
apendaye kudhulumu watu.
8Efraimu amesema,
‘Mimi ni tajiri!
Mimi nimejitajirisha!
Hamna ubaya kupata faida.
Hata hivyo, hilo si kosa!’”
9Mwenyezi-Mungu asema, “Mimi ni Mwenyezi-Mungu, Mungu wako;
mimi ndimi niliyekutoa nchini Misri!
Mimi nitakukalisha tena katika mahema,
kama ufanyavyo sasa kwa siku chache tu,
wakati wa sikukuu ya vibanda.
10Mimi niliongea na manabii;
ni mimi niliyewapa maono mengi,
na kwa njia yao natangaza mpango wangu.
11Huko Gileadi ni mahali pa dhambi;
huko Gilgali walitambika fahali,
kwa hiyo madhabahu zao zitakuwa marundo ya mawe kwenye mitaro shambani.”
12Yakobo alikimbia nchi ya Aramu
akiwa huko alifanya kazi apate mke,
akachunga kondoo ili apate mke.
13Kwa nabii Mwenyezi-Mungu aliwatoa Waisraeli nchini Misri,
na kwa nabii Mungu aliwahifadhi.
14Waefraimu wamemchukiza Mwenyezi-Mungu sana.
Lakini Mwenyezi-Mungu atawalipiza makosa yao,
atawaadhibu kwa mambo maovu waliyotenda.

Hosea12;1-14

Biblia Habari Njema kwa Watu Wote(BHN)

"Swahili Na Waswahili"Mbarikiwe

No comments: