Swahili na Waswahili

Swahili na Waswahili
Waswahili na Mswahili Rachel Siwa...Pamoja Daima!!

Tuesday 19 May 2020

Kikombe Cha Asubuhi; Hosea 5..


Shalom,Habari za Asubuhi,Hamjambo,Mmeamkaje?

Tumshukuru Mungu katika yote....

Mungu wetu Baba yetu,Muumba wetu Muumba wa Mbingu na Nchi
Muumba wa vyote vilivyomo vinavyoonekana na visivyoonekana
Mungu wa walio hai,Mungu  mwenye huruma,Mungu wa upendo
Mungu wa Abrahamu,Isaka na Yakobo...
Asante kwa wema na fadhili zako kwetu
Asante kwa ulinzi wako kwetu wakati wote
Asante kwa kutuchagua tena na kutupa
kibali cha kuendelea kuiona leo hii
Asante kwa pumzi/uzima,afya na kuwatayari kwa majukumu yetu

Neema yako yatutosha ee Mungu wetu....!!

Basi, kwa vile ahadi ya kuingia mahali pa pumziko bado ipo, na tuogope ili yeyote kati yenu asije akashindwa kupata pumziko hilo. Maana Habari Njema imehubiriwa kwetu kama vile ilivyohubiriwa kwa hao watu wa kale. Lakini ujumbe huo haukuwafaa chochote, maana waliusikia lakini hawakuupokea kwa imani.
Baba wa Mbinguni tunakuja mbele zako,
Tukijinyenyekeza,tukijiachilia mikononi mwako
Mungu wetu tunamomba utusamehe dhambi zetu
Baba wa Mbinguni nasi tunaomba ukatupe neema
 ya kuweza kuwasamehe wale wote waliotukosea

Usitutie majaribuni Mungu wetu tunaomba utuepushe
na yule mwovu na kazi zake zote
Jehovah ututakase miili yetu na akili zetu
Baba wa Mbinguni tunaomba utufunike kwa Damu
ya Bwana na Mwokozi wetu Yesu Kristo wa Nazareti
yeye aliteseka kwanza ili sisi tupate kupona....

Basi, sisi tunaoamini tunapata pumziko hilo aliloahidi Mungu. Kama alivyosema: “Nilikasirika, nikaapa: ‘Hawataingia mahali pangu pa pumziko.’” Mungu alisema hayo ingawa kazi yake ilikuwa imekwisha malizika tangu alipoumba ulimwengu.
Mungu wetu tunaomba ukabariki kazi za mikono yetu
Baba wa Mbinguni tunaomba ukatupe ubunifu na maarifa katika utendaji
Jehovah nasi tukatende sawasawa na mapenzi yako
Yahweh tunaomba ukabariki ridhiki zetu ziingiazo/zitokazo
Mungu wetu nasi tunaomna ukatupe neema ya kuweza kuwabariki wenye kuhitaji
Tusipungukiwe katika mahitaji yetu
Baba wa Mbinguni tunaomba ukatupe kama inavyokupendeza wewe...


Yahweh tunayaweka maisha yetu mikononi mwako
Mungu wetu tunaomba ukabariki nyumba/ndoa zetu,
Jehovah tunaomba ulinzi wako kwetu na kwa vyote tunavyovimiliki
Yahweh tunaomba ukatubariki tuingiapo/tutokapo
Mungu wetu tunaomba ukavibariki vyote tunavyoenda kugusa/kutumia
Baba wa Mbinguni ukavitakase kwa Damu ya Bwana wetu Yesu Kristo
Mungu wetu ukatamalaki na kutuatamia
Baba wa Mbinguni tukawe salama rohoni
Yahwe ukatupe akili ya kutambua mema na mabaya
Mfalme wa amani amani yako ikatawale katika maisha yetu
Mungu wetu ukatupe macho ya kuona,masikio ya kusikia sauti yako na kuitii..
Baba wa Mbinguni  tunaomba ukatupe neema ya kufuata
njia zako,tukasimamie Neno lako,amri na sheria zako
siku zote za maisha yetu...
Ukatuguse kwa mkono wako wenye nguvu,ukatufanye chombo chema
ee Mungu wetu nasi tukatumike kama inavyokupendeza wewe
Roho Mtakatifu akatuongoze katika yote na tukawe na kiasi....

Maana Maandiko yasema mahali fulani kuhusu siku ya saba: “Mungu alipumzika siku ya saba, akaacha kazi zake zote.”
Tazama watoto wako wenye shida/tabu,wote wanaopitia magumu/majaribu mbalimbali
Mungu wetu tunaomba ukawaguse kwa mkono wako wenye nguvu
kila mmoja na mahitaji yake
Mungu wetu tunaomba ukawasamehe pale walipo kwenda kinyume nawe
Yahweh tunaomba ukawape neema ya kuweza kujiombea,kufuata njia zako nazo zikawaweke huru...
Baba wa Mbinguni tunayaweka haya yote mikononi mwako
Kwakuwa Ufalme ni wako Nguvu na Utukufu hata Milele...
Amina...!!


Asanteni sana wapendwa katika Kristo Yesu kwakuwa nami,Baba wa Mbinguni aendelee kuwatendea sawasawa na mapenzi yake...

Nawapenda.

Wakufunzi wabaya wa Israeli
1“Haya! Sikilizeni enyi makuhani!
Tegeni sikio, enyi Waisraeli!
Sikilizeni enyi ukoo wa kifalme!
Nyinyi mlipaswa kuzingatia haki,
badala yake mmekuwa mtego huko Mizpa,
mmekuwa wavu wa kuwanasa huko Tabori.
2Mmechimba shimo refu la kuwanasa huko Shitimu.
Lakini mimi nitawaadhibuni nyote.
3Nawajua watu wa Efraimu,
Waisraeli hawakufichika kwangu.
Nyinyi watu wa Efraimu mmefanya uzinzi,
watu wote wa Israeli wamejitia najisi.
Hosea aonya dhidi ya ibada za miungu
4“Matendo yao yanawazuia wasimrudie Mungu wao.
Mioyoni mwao wamejaa uzinzi;
hawanijui mimi Mwenyezi-Mungu.
5Kiburi cha Waisraeli chaonekana wazi;
watu wa Efraimu watajikwaa katika hatia yao,
nao watu wa Yuda watajikwaa pamoja nao.
6Watakwenda na makundi yao ya kondoo na ng'ombe,
kumtafuta Mwenyezi-Mungu;
lakini hawataweza kumpata,
kwa sababu amejitenga nao.
7Wamevunja uaminifu kwa Mwenyezi-Mungu,
wamezaa watoto walio haramu.
Mwezi mwandamo utawaangamiza,
pamoja na mashamba yao.
Vita kati ya Yuda na Israeli
8“Pigeni baragumu huko Gibea,
na tarumbeta huko Rama.
Pigeni king'ora huko Beth-aveni.
Enyi watu wa Benyamini, adui yenu yuko nyuma!
9Siku nitakapotoa adhabu
Efraimu itakuwa kama jangwa!
Ninachotangaza miongoni mwa makabila ya Israeli,
ni jambo litakalotukia kwa hakika.
10Viongozi wa Yuda wamekuwa
wenye kubadili mipaka ya ardhi.
Mimi nitawamwagia hasira yangu kama maji.
11Efraimu ameteswa,
haki zake zimetwaliwa;
kwani alipania kufuata upuuzi.
12Hivyo mimi Mungu niko kama nondo kwa Efraimu,
kama donda baya kwa watu wa Yuda.
13Watu wa Efraimu walipogundua ugonjwa wao,
naam, watu wa Yuda walipogundua donda lao,
watu wa Efraimu walikwenda Ashuru
kuomba msaada kwa mfalme mkuu;
lakini yeye hakuweza kuwatibu,
hakuweza kuponya donda lenu.
14Maana mimi nitakuwa kama simba kwa Efraimu,
kama mwanasimba kwa watu wa Yuda.
Mimi mwenyewe nitawararua na kuondoka,
nitawachukua na hakuna atakayewaokoa.
15Nitarudi mahali pangu na kujitenga nao
mpaka wakiri kosa lao na kunirudia.
Taabu zao zitawafundisha wanitafute, wakisema:



Hosea5;1-15

Biblia Habari Njema kwa Watu Wote(BHN)

"Swahili Na Waswahili"Mbarikiwe

No comments: