Swahili na Waswahili

Swahili na Waswahili
Waswahili na Mswahili Rachel Siwa...Pamoja Daima!!

Thursday 21 May 2020

Kikombe Cha Asubuhi; Hosea 7..


Shalom,Habari za Asubuhi,Hamjambo,Mmeamkaje?

Tumshukuru Mungu katika yote....

Mungu wetu Baba yetu,Muumba wetu Muumba wa Mbingu na Nchi
Muumba wa vyote vilivyomo vinavyoonekana na visivyoonekana
Mungu wa walio hai,Mungu  mwenye huruma,Mungu wa upendo
Mungu wa Abrahamu,Isaka na Yakobo...
Asante kwa wema na fadhili zako kwetu
Asante kwa ulinzi wako kwetu wakati wote
Asante kwa kutuchagua tena na kutupa
kibali cha kuendelea kuiona leo hii
Asante kwa pumzi/uzima,afya na kuwatayari kwa majukumu yetu

Neema yako yatutosha ee Mungu wetu....!!

Basi, tujitahidi kuingia katika pumziko hilo, ili asiwepo yeyote miongoni mwetu atakayekataa kutii kama walivyofanya wao.
Baba wa Mbinguni tunakuja mbele zako,
Tukijinyenyekeza,tukijiachilia mikononi mwako
Mungu wetu tunamomba utusamehe dhambi zetu
Baba wa Mbinguni nasi tunaomba ukatupe neema
 ya kuweza kuwasamehe wale wote waliotukosea

Usitutie majaribuni Mungu wetu tunaomba utuepushe
na yule mwovu na kazi zake zote
Jehovah ututakase miili yetu na akili zetu
Baba wa Mbinguni tunaomba utufunike kwa Damu
ya Bwana na Mwokozi wetu Yesu Kristo wa Nazareti
yeye aliteseka kwanza ili sisi tupate kupona....

Neno la Mungu ni hai na lina nguvu; ni kali kuliko upanga wenye makali kuwili. Hukata kabisa mpaka mahali ambapo moyo na roho hukutana, mpaka pale vikutanapo viungo vya mwili na uboho. Neno hilo huchambua nia na fikira za mioyo ya watu.
Mungu wetu tunaomba ukabariki kazi za mikono yetu
Baba wa Mbinguni tunaomba ukatupe ubunifu na maarifa katika utendaji
Jehovah nasi tukatende sawasawa na mapenzi yako
Yahweh tunaomba ukabariki ridhiki zetu ziingiazo/zitokazo
Mungu wetu nasi tunaomna ukatupe neema ya kuweza kuwabariki wenye kuhitaji
Tusipungukiwe katika mahitaji yetu
Baba wa Mbinguni tunaomba ukatupe kama inavyokupendeza wewe...


Yahweh tunayaweka maisha yetu mikononi mwako
Mungu wetu tunaomba ukabariki nyumba/ndoa zetu,
Jehovah tunaomba ulinzi wako kwetu na kwa vyote tunavyovimiliki
Yahweh tunaomba ukatubariki tuingiapo/tutokapo
Mungu wetu tunaomba ukavibariki vyote tunavyoenda kugusa/kutumia
Baba wa Mbinguni ukavitakase kwa Damu ya Bwana wetu Yesu Kristo
Mungu wetu ukatamalaki na kutuatamia
Baba wa Mbinguni tukawe salama rohoni
Yahwe ukatupe akili ya kutambua mema na mabaya
Mfalme wa amani amani yako ikatawale katika maisha yetu
Mungu wetu ukatupe macho ya kuona,masikio ya kusikia sauti yako na kuitii..
Baba wa Mbinguni  tunaomba ukatupe neema ya kufuata
njia zako,tukasimamie Neno lako,amri na sheria zako
siku zote za maisha yetu...
Ukatuguse kwa mkono wako wenye nguvu,ukatufanye chombo chema
ee Mungu wetu nasi tukatumike kama inavyokupendeza wewe
Roho Mtakatifu akatuongoze katika yote na tukawe na kiasi....


Hakuna kiumbe chochote kilichofichika mbele ya Mungu; kila kitu kimefunuliwa wazi mbele ya macho yake yeye ambaye kwake tutapaswa kutoa hoja ya matendo yetu.
Tazama watoto wako wenye shida/tabu,wote wanaopitia magumu/majaribu mbalimbali
Mungu wetu tunaomba ukawaguse kwa mkono wako wenye nguvu
kila mmoja na mahitaji yake
Mungu wetu tunaomba ukawasamehe pale walipo kwenda kinyume nawe
Yahweh tunaomba ukawape neema ya kuweza kujiombea,kufuata njia zako nazo zikawaweke huru...
Baba wa Mbinguni tunayaweka haya yote mikononi mwako
Kwakuwa Ufalme ni wako Nguvu na Utukufu hata Milele...
Amina...!!


Asanteni sana wapendwa katika Kristo Yesu kwakuwa nami,Baba wa Mbinguni aendelee kuwatendea sawasawa na mapenzi yake...

Nawapenda.

1Kila nikitaka kuwarekebisha watu wangu,
ninapotaka kuwaponya Waisraeli,
uovu wa watu wa Efraimu hufunuliwa,
matendo mabaya ya Samaria hujitokeza.
Wao huongozwa na udanganyifu,
kwenye nyumba wezi huvunja
nje barabarani wanyang'anyi huvamia.
2Hawafikiri hata kidogo kwamba mimi
nayakumbuka maovu yao yote.
Sasa maovu yao yamewabana.
Yote waliyotenda yako mbele yangu.
Uhaini katika ikulu
3“Wanamfurahisha mfalme kwa maovu yao
wanawafurahisha wakuu kwa uhaini wao.
4Wote ni wazinzi;
wao ni kama tanuri iliyowashwa moto
ambao mwokaji hauchochei tangu akande unga
mpaka mkate utakapoumuka.
5Kwenye sikukuu ya mfalme,
waliwalewesha sana maofisa wake;
naye mfalme akashirikiana na wahuni.
6Kama tanuri iwakavyo,
mioyo yao huwaka kwa hila;
usiku kucha hasira yao hufuka moshi,
ifikapo asubuhi, hulipuka kama miali ya moto.
7Wote wamewaka hasira kama tanuri,
na wanawaangamiza watawala wao.
Wafalme wao wote wameanguka,
wala hakuna anayeniomba msaada.
Israeli anategemea mataifa mengine
8“Efraimu amechanganyika na watu wa mataifa.
Anaonekana kama mkate ambao haukugeuzwa.
9Wageni wamezinyonya nguvu zake,
wala yeye mwenyewe hajui;
mvi zimetapakaa kichwani mwake,
lakini mwenyewe hana habari.
10Kiburi cha Waisraeli chashuhudia dhidi yao,
hawanirudii mimi Mwenyezi-Mungu, Mungu wao;
wala hawanitafuti kwa matukio hayo yote.
11Efraimu ni kama njiwa, mjinga asiye na akili;
mara yuko Misri, mara Ashuru kuomba.
12Watakapokwenda nitatandaza wavu wangu niwanase,
nitawaangusha chini kama ndege wa angani;
nitamwaadhibu kadiri ya ripoti ya maovu yao.
13Ole wao kwa kuwa wameniacha!
Maangamizi na yawapate, maana wameniasi.
Nilitaka kuwakomboa,
lakini wanazua uongo dhidi yangu.
14“Wananililia, lakini si kwa moyo.
Wanagaagaa na kujikatakata vitandani mwao,
kusudi nisikilize dua zao za nafaka na divai;
lakini wanabaki waasi dhidi yangu.
15Mimi ndimi niliyeiimarisha mikono yao,
lakini wanafikiria maovu dhidi yangu.
16Wanaigeukia miungu batili,
wako kama uta uliolegea.
Viongozi wao watakufa kwa upanga,
kwa sababu ya maneno yao ya kiburi.
Kwa hiyo, watadharauliwa nchini Misri.

Hosea7;1-16

Biblia Habari Njema kwa Watu Wote(BHN)

"Swahili Na Waswahili"Mbarikiwe

No comments: