Swahili na Waswahili

Swahili na Waswahili
Waswahili na Mswahili Rachel Siwa...Pamoja Daima!!

Friday 17 August 2012

Kisa cha Leo ni Emu-Three na Mbio za Sakafuni,Huishia Ukingoni!!!!


Mbio za sakafuni,huishia ukingoni 4

Waungwana leo nimewaletea Mswahili; Emu-Three na Diary Yangu[Yake]
ANASEMA;Hii ni blog maalum kwa kumbukumbu za maisha 
(diaries), 
visa na matukio na yale unayopenda kuchangia na wenzako (mijadala),
 maneno ya hekima,
 kusaidiana na pia kutoa dukuduku lako (kilio chako). 
Soma na uchangie chochote kwa 
kutoa maoni (comments) yako,
 au tutumie kisa chako, au lolote lenye mafunzo ili tuliweke hewani.

Tupitie Kisa hiki kidogo, hii ni Sehemu ya 4:Kila mfanyakazi tunayemchukua hakai hapa nyumbani, sasa nimechoka kabisa kutafuta mfanyakazi wa nyumbani, naona ni heri nijifanyie kazi zangu mwenyewe, kwanza nililelewa kama mfanyakzia wa nyumbani…’akasema mke wangu.

Kipindi hicho maisha yetu yapo juu, tuna kila kitu, …lakini maisha ya ndani yalikuwa na mitihani yake, na ilionyesha wazi kuwa tulihitaji msaidizi, ili na yeye apate muda wa kufuatilia miradi yetu.Niliinuakichwa na kumtizama kwa macho ya huruma,maanaalikuwa mtu wa pilikapilika, shughuli zandani, shughuli zamiradi, shughuli za kijamii, zote alikuwa akijitahidi kujumuika nazo.

Nilimwangalia na kutabasamu, na hapo nikakumbuka siku za nyuma, wakati akiwa binti, wakati nampigania kumpata, ilikuwa kama kampeni za siasa ambazo nilikuwa nikipambana nazo, na hata siku anaingia kwangu kama mke wangu sikuamini.
‘Unanikumbusha mbali sana mke wangu, sijui kama ningekukosa ingelikwuaje…’nikasema.Inaendelea;kuanzia Sehemu ya 1-hii ya 4 na Kuendelea na Kisa hiki ingia;http://miram3.blogspot.co.uk
Mpendwa Unalolote la kuongezea kwa mwandishi huyu?Maoni,Ushauri na Kuelimishana kwa Upendo.Karibu sana.


Hongera sana Emu-Three kwa Kazi zako,Mungu Azidi kukubariki sana sana kwa Kazi za Mikono yako na kila lililo Jema.Tunakutakia Swaumu Njema!!!!!

"Swahili NA Waswahili" Pamoja Daima.

1 comment:

Yasinta Ngonyani said...

Hakika huyo ndugu wetu ni mukali si mchezo na kama ulivyosema mama swahili Na Waswahili Mungu azidi kukubariki sana sana kwa kazi zamikono yako na azizi kukupa moyo. Pamoja daima!!