Swahili na Waswahili

Swahili na Waswahili
Waswahili na Mswahili Rachel Siwa...Pamoja Daima!!

Wednesday 15 July 2020

Kikombe Cha Asubuhi; Sefania 2...

Shalom,Habari za Asubuhi,Hamjambo,Mmeamkaje?

Tumshukuru Mungu wetu katika yote...

Asante  Mungu wetu kwa wema na fadhili zako kwetu
Asante kwa ulinzi wako kwetu wakati wote
Asante kwa kutuchagua tena na kutupa
kibali cha kuendelea kuiona leo hii
Asante kwa pumzi/uzima,afya na kuwatayari kwa majukumu yetu


Utukuzwe ee Mungu wetu,usifiwe Baba wa Mbinguni

Neema yako yatutosha  Mungu wetu..!

Neno lako ni taa ya kuniongoza, na mwanga katika njia yangu. Nimeapa na kuthibitisha kiapo changu, kwamba nitashika maagizo yako adili.
Baba wa Mbinguni tunakuja mbele zako tukijinyenyekeza,
tukijishusha na kujiachilia mikononi mwako

Mungu wetu tunaomba utusamehe dhambi zetu zote
Baba wa Mbinguni nasi tunaomba utupe neema ya kuweza kuwasamehe wale wote waliotukosea,Usitutie majaribuni Mungu wetu tunaomba utuepushe na yule mwovu na kazi zake zote,Jehovah ututakase miili yetu na akili zetu Baba wa Mbinguni tunaomba utufunike kwa  Damu ya Bwana na Mwokozi wetu Yesu Kristo wa Nazareti,
Yeye aliteseka kwanza ili sisi tupate kupona....

Ee Mwenyezi-Mungu, ninateseka mno; unijalie uhai kama ulivyoahidi. Ee Mwenyezi-Mungu, upokee sala yangu ya shukrani; na kunifundisha maagizo yako. Maisha yangu yamo hatarini daima, lakini siisahau sheria yako.
Mungu wetu tunaomba ukabariki kazi za mikono yetu
Baba wa Mbinguni tunaomba ukatupe ubunifu na maarifa 
katika utendaji
Jehovah nasi tukatende sawasawa na mapenzi yako
Baba wa Mbinguni tunaomba ukabariki ridhiki zetu
ziingiazo/zitokazo
Mungu wetu nasi tunaomba ukatupe neema ya kuweza
kuwabariki wenye kuhitaji
Yahweh tusipungukiwe katika mahitaji yetu
Mungu wetu ukatupe kama inavyokupendeza wewe



Jehovah tunayaweka maisha yetu mikononi mwako
Baba wa Mbinguni tunaomba ukabariki nyumba/ndoa zetu,
watoto,wazazi wetu,familia/ndugu na wote wanaotuzunguka
Jehovah tunaomba ulinzi wako kwetu na kwa vyote tunavyo vimiliki
Yahweh tunaomba ukatubariki tuingiapo/tutokapo
Mungu wetu tunaomba ukavibariki vyote tunavyoenda kugusa/kutumia
Baba wa Mbinguni ukavitakase kwa Damu ya Bwana wetu Yesu Kristo
Mungu wetu ukatamalaki na kutuatamia
Baba wa Mbinguni tukawe salama rohoni
Mfalme wa amani amani yako ikatawale katika maisha yetu
Mungu wetu ukatupe macho ya kuona na masikio ya kusikia 
sauti yako na kuitii
Baba wa Mbinguni tunaomba ukatupe neema ya kufuata njia zako
Yahweh tukasimamie Neno lako amri na sheria zako siku zote 
za maisha yetu

Mungu  wetu ukaonekane katika maisha yetu popote tupitapo na ikajulikane kwamba upo 

Neema zako zikawe nasi Nuru yako ikaangaze katika maisha yetu
Ukatufanye barua njema ee Mungu wetu nasi tukasomeke kama
inavyokupendeza wewe
Roho Mtakatifu akatuongoze katika yote na tukawe na kiasi...

Waovu wamenitegea mitego, lakini sikiuki kanuni zako. Maamuzi yako ni riziki kubwa kwangu milele; hayo ni furaha ya moyo wangu. Nimekusudia kwa moyo wote kufuata masharti yako milele.
Tazama wenye shida/tabu,Mungu wetu tunaomba
 ukawaguse kila mmoja na mahitaji yake
Baba wa Mbinguni tunaomba ukawasamehe pale walipokwenda
kinyume nawe
Mungu wetu ukawape neema ya kujiombea,macho ya rohoni,masikio yakusikia sauti yako,wakafuate njia zako nazo zikawaweke huru
Mungu wetu tunaomba ukasikie kulia kwao
Baba wa Mbinguni tunomba ukawafute machozi yao
Nuru yako ikaangaze katika maisha yao
Mungu wetu tunaomba ukawatendee sawasawa na mapenzi yako
Kwakuwa Ufalme ni wako Nguvu na Utukufu hata Milele
Amina....!!!


Wapendwa katika Kristo Yesu asanteni sana
kwakuwanami/kunisoma

Mungu Baba aendelee kuwabariki na kuwatendea
kama inavyompendeza yeye
Amani ya Bwana wetu Yesu Kristo na upendo wa Mungu Baba
ukae nanyi daima....

Nawapenda.

Mwito wa toba
1Kusanyikeni, kusanyikeni enyi taifa la watu wasio na aibu,
2kabla hamjapeperushwa mbali kama makapi,2:2 kabla … makapi: Makala ya Kiebrania si dhahiri.
kabla haijawajia siku ya hasira kali ya Mwenyezi-Mungu,
kabla haijawajia siku ya ghadhabu ya Mwenyezi-Mungu.
3Mtafuteni Mwenyezi-Mungu enyi wanyenyekevu wote nchini,
enyi mnaozitii amri zake.
Tafuteni uadilifu, tafuteni unyenyekevu;
labda mtaiepa siku ya ghadhabu ya Mwenyezi-Mungu.
Maangamizi kwa mataifa ya jirani
4Mji wa Gaza utahamwa,
Ashkeloni utakuwa tupu.
Wakazi wa Ashdodi watatimuliwa mchana,
na wale wa Ekroni watang'olewa.
5Ole wenu wakazi wa nchi za pwani,
watu mnaoishi huko Krete!
Mwenyezi-Mungu ametamka dhidi yenu
enyi wakazi wa Kanaani, nchi ya Filistia:
Mimi nitawaangamiza asibaki hata mkazi mmoja!
6Nanyi nchi za pwani mtafanywa kuwa malisho;
mtakuwa vibanda vya wachungaji
na mazizi ya kondoo.
7Nchi ya pwani itamilikiwa na mabaki ya ukoo wa Yuda.
Watachunga mifugo yao huko.
Nyumba za mji wa Ashkeloni
zitakuwa mahali pao pa kulala.
Maana Mwenyezi-Mungu, Mungu wao atawakumbuka
na kuwarudishia hali yao njema.
8“Nimeyasikia masuto ya Moabu
na dhihaka za Waamoni;
jinsi walivyowasuta watu wangu,
na kujigamba kuiteka nchi yao.
9Kwa hiyo, niishivyo mimi Mwenyezi-Mungu wa majeshi,
mimi Mungu wa Israeli,
Moabu itakuwa kama Sodoma
na Amoni itakuwa kama Gomora.
Nchi zake zitakuwa za viwavi na mashimo ya chumvi,
zitakuwa ukiwa milele.
Watu wangu watakaobaki wataziteka nyara,
watu wa taifa langu waliosalia watazimiliki.”
10Hayo yatakuwa malipo ya kiburi chao,
kwa sababu waliwadhihaki na kujigamba
dhidi ya watu wa Mwenyezi-Mungu wa majeshi.
11Mwenyezi-Mungu atakuwa wa kutisha dhidi yao;
miungu yote ya dunia ataikondesha.
Mataifa yote duniani yatamsujudia;
kila taifa katika mahali pake.
12Nanyi watu wa Kushi pia
mtauawa kwa upanga wake.
13Mwenyezi-Mungu atanyosha mkono wake kaskazini,
na kuiangamiza nchi ya Ashuru.
Ataufanya mji wa Ninewi kuwa ukiwa,
kuwa mahali pakavu kama jangwa.
14Makundi ya mifugo yatalala humo,
kadhalika kila mnyama wa porini.
Tai na yangeyange na korongo wataishi juu ya nguzo zake,
bundi watalia kwenye madirisha yake,
kunguru watalia kwenye vizingiti,
maana nyumba zake za mierezi zitakuwa tupu.
15Je, huu ndio mji uliojivuna na kuishi kwa usalama,
mji uliojisemea, “Ni mimi tu, hakuna mwingine!”
Jinsi gani umekuwa mtupu
na makao ya wanyama wa mwituni!
Kila apitaye karibu atauzomea na kuudharau.

Sefania2;1-15

Biblia Habari Njema kwa Watu Wote(BHN)

"Swahili Na Waswahili"Mbarikiwe

Tuesday 14 July 2020

Kikombe Cha Asubuhi; Tunamshukuru Mungu kwa kumaliza Kitabu cha Habakuki,Leo Tunaanza Kitabu cha Sefania....1

Shalom,Habari za Asubuhi,Hamjambo,Mmeamkaje?

Tunamshukuru Mungu kwa kutupa kibali cha
 kupitia kitabu cha "Habakuki
"
Ni matumaini yangu kuna mengi tumejifunza/kufaidika
na kutupa mwanga/kuelewa kwenye kitabu hiki...

Leo tunapokwenda anza kupitia Kitabu cha"Sefania"tunamuomba Mungu wetu akatupe kibali,macho ya rohoni
 na akili ya kuelewa katika kujifunza NENO lake...
Ee Mungu  tunaomba ukatuongoze...!!
Tumshukuru Mungu wetu katika yote...Mungu wetu Baba yetu,Muumba wetu Muumba wa Mbingu na Nchi
Muumba wa vyote vilivyomo vinavyoonekana na visivyoonekana
Mungu wa walio hai,Mungu  mwenye huruma,Mungu wa upendo
Mungu wa Abrahamu,Isaka na Yakobo...


Asante kwa wema na fadhili zako kwetu
Asante kwa ulinzi wako kwetu wakati wote
Asante kwa kutuchagua tena na kutupa
kibali cha kuendelea kuiona leo hii
Asante kwa pumzi/uzima,afya na kuwatayari kwa majukumu yetu

Neema yako yatutosha ee Mungu wetu....!!

Naipenda sana sheria yako! Naitafakari mchana kutwa! Amri yako iko nami daima, yanipa hekima kuliko maadui zangu.
Baba wa Mbinguni tunakuja mbele zako tukijinyenyekeza,
tukijishusha na kujiachilia mikononi mwako

Mungu wetu tunaomba utusamehe dhambi zetu zote 
Baba wa Mbinguni nasi tunaomba ukatupe neema
ya kuweza kuwasamehe wale wote waliotukosea
Usitutie majaribuni Mungu wetu tunaomba utuepushe
na yule mwovu na kazi zake zote
Jehovah ututakase miili yetu na akili zetu
Baba wa Mbinguni tunaomba utufunike kwa Damu
ya Bwana na Mwokozi wetu Yesu Kristo wa Nazareti
yeye aliteseka kwanza ili sisi tupate kupona....

Ninaelewa kuliko waalimu wangu wote, kwa kuwa nayatafakari maamuzi yako. Nawapita wazee kwa busara yangu, kwa sababu nazishika kanuni zako. Najizuia nisifuate njia mbaya, nipate kulizingatia neno lako.
Mungu wetu tunaomba ukabariki kazi za mikono yetu
Baba wa Mbinguni tunaomba ukatupe ubunifu na maarifa katika utendaji
Jehovah nasi tukatende sawasawa na mapenzi yako
Yahweh tunaomba ukabariki ridhiki zetu ziingiazo/zitokazo
Mungu wetu nasi tunaomna ukatupe neema ya kuweza kuwabariki wenye kuhitaji
Tusipungukiwe katika mahitaji yetu
Baba wa Mbinguni tunaomba ukatupe kama inavyokupendeza wewe...


Yahweh tunayaweka maisha yetu mikononi mwako
Mungu wetu tunaomba ukabariki nyumba/ndoa zetu,
Jehovah tunaomba ulinzi wako kwetu na kwa vyote tunavyovimiliki
Yahweh tunaomba ukatubariki tuingiapo/tutokapo
Mungu wetu tunaomba ukavibariki vyote tunavyoenda kugusa/kutumia
Baba wa Mbinguni ukavitakase kwa Damu ya Bwana wetu Yesu Kristo
Mungu wetu ukatamalaki na kutuatamia
Baba wa Mbinguni tukawe salama rohoni
Yahwe ukatupe akili ya kutambua mema na mabaya
Mfalme wa amani amani yako ikatawale katika maisha yetu
Mungu wetu ukatupe macho ya kuona,masikio ya kusikia sauti yako na kuitii..
Baba wa Mbinguni  tunaomba ukatupe neema ya kufuata
njia zako,tukasimamie Neno lako,amri na sheria zako
siku zote za maisha yetu...
Ukatuguse kwa mkono wako wenye nguvu,ukatufanye chombo chema
ee Mungu wetu nasi tukatumike kama inavyokupendeza wewe
Roho Mtakatifu akatuongoze katika yote na tukawe na kiasi....

Sikukiuka maagizo yako, maana wewe mwenyewe ulinifundisha. Maneno yako ni matamu sana kwangu; naam, ni matamu kuliko asali! Kwa kanuni zako napata hekima, kwa hiyo nachukia kila mwenendo mbaya.
Tazama watoto wako wenye shida/tabu,wote wanaopitia magumu/majaribu mbalimbali
Mungu wetu tunaomba ukawaguse kwa mkono wako wenye nguvu
kila mmoja na mahitaji yake
Mungu wetu tunaomba ukawasamehe pale walipo kwenda kinyume nawe
Yahweh tunaomba ukawape neema ya kuweza kujiombea,kufuata njia zako nazo zikawaweke huru...
Baba wa Mbinguni tunayaweka haya yote mikononi mwako
Kwakuwa Ufalme ni wako Nguvu na Utukufu hata Milele...
Amina...!!


Asanteni sana wapendwa katika Kristo Yesu kwakuwa nami,Baba wa Mbinguni aendelee kuwatendea sawasawa na mapenzi yake...
Nawapenda.

1Neno la Mwenyezi-Mungu lililomjia Sefania mwana wa Kushi, mwana wa Gedalia, mwana wa Amenia, mwana wa Hezekia, wakati wa utawala wa mfalme Yosia mwana wa Amoni, mfalme wa Yuda:
2Mwenyezi-Mungu asema:
“Nitavifagilia mbali viumbe vyote duniani:
3Wanadamu, wanyama, ndege wa angani
na samaki wa baharini;
vyote nitaviangamiza.
Waovu1:3 waovu: Kiebrania: Wanaokwaza. nitawaangamiza kabisa;
wanadamu nitawafagilia mbali duniani.
4Nitaunyosha mkono wangu dhidi ya nchi ya Yuda,
kadhalika na wakazi wote wa mji wa Yerusalemu.
Nitaangamiza mabaki yote ya Baali kutoka nchi hii,
na hakuna atakayetambua jina lao.
5Nitawaangamiza wote wanaosujudu juu ya paa,
wakiabudu jeshi la mbinguni.
Nitawaangamiza wale wanaoniabudu
na kuapa kwa jina langu,
hali wanaapa pia kwa jina la mungu Milkomu.
6Nitawaangamiza wote walioniacha mimi Mwenyezi-Mungu
wote walioacha kunitafuta na kuniuliza shauri.”
7Nyamazeni mbele ya Bwana Mwenyezi-Mungu,
kwani siku ya Mwenyezi-Mungu iko karibu.
Mwenyezi-Mungu ameandaa tambiko,
nao aliowaalika amewateua.
8Mwenyezi-Mungu asema hivi:
“Katika siku ile ya karamu yangu,
nitawaadhibu viongozi wa watu hao,
kadhalika na wana wa mfalme
pamoja na wote wanaoiga desturi za kigeni.
9Siku hiyo nitawaadhibu wote:
Wanaoruka kizingiti cha nyumba kama wapagani,
wanaojaza nyumba ya bwana wao1:9 nyumba ya bwana wao: Au hekalu la mungu wao. vitu vya dhuluma na wizi.
10“Siku hiyo, nasema mimi Mwenyezi-Mungu,
Kutasikika kilio kutoka Lango la Samaki,
maombolezo kutoka Mtaa wa Pili,
na mlio mkubwa kutoka milimani.
11Lieni enyi wakazi wa Makteshi!
Wafanyabiashara wote wameangamia,
wote wapimao fedha wamefutiliwa mbali.
12Wakati huo nitaupekua mji wa Yerusalemu kwa taa,
nitawaadhibu wanaoishi wametulia kama machicha ya divai,
wote ambao husema mioyoni mwao:
‘Mwenyezi-Mungu hatafanya kitu: Chema au kibaya.’
13Utajiri wao utanyakuliwa,
na nyumba zao zitaachwa tupu!
Watajijengea nyumba, lakini hawataishi humo.
Watapanda mizabibu, lakini hawatakunywa divai yake.”
14Ile siku kubwa ya Mwenyezi-Mungu imekaribia,
iko karibu na inakuja mbio.
Mlio wa siku ya Mwenyezi-Mungu ni wa uchungu;
hapo, shujaa atalia kwa sauti.
15Siku hiyo itakuwa siku ya ghadhabu,
ni siku ya dhiki na uchungu,
siku ya giza na huzuni;
siku ya uharibifu na maangamizi,
siku ya mawingu na giza nene.
16Siku hiyo ni ya mlio wa tarumbeta ya vita,
dhidi ya miji yenye ngome na kuta ndefu.
17Kwa kuwa watu wamemkosea Mwenyezi-Mungu,
yeye atawaletea dhiki kubwa,
hivyo kwamba watatembea kama vipofu.
Damu yao itamwagwa kama vumbi,
na miili yao kama mavi.
18Fedha yao wala dhahabu yao havitaweza kuwaokoa
katika siku hiyo ya ghadhabu ya Mwenyezi-Mungu.
Kwa moto wa wivu wake
dunia yote itateketezwa.
Kwa ukamilifu na kwa namna ya kutisha
atawafanya wakazi wote duniani watoweke.


Sefania1;1-18

Biblia Habari Njema kwa Watu Wote(BHN)

"Swahili Na Waswahili"Mbarikiwe

Monday 13 July 2020

Kikombe Cha Asubuhi; Habakuki 3...

Shalom,Habari za Asubuhi,Hamjambo,Mmeamkaje?

Haleluyah ni siku/wiki nyingine tena Mungu wetu ametuchagua

na kutupa kibali cha kuendelea kuiona leo hii
Si kwamba sisi tumetenda mema sana wala si kwa nguvu zetu
si kwa utashi wetu wala si kwa akili zetu si kwamba sisi
ni wazuri mno si kwa uwezo wetu sisi kuwa hivi tulivyo leo hii
Ni kwa rehema/neema zake ni kwa mapenzi yake Mungu wetu....

Tumshukuru Mungu wetu katika yote...
Asante Mungu wetu kwa wema na fadhili zako kwetu
Asante kwa ulinzi wako kwetu wakati wote
Asante kwa pumzi/uzima,afya na kuwa tayari kwa majukumu yetu
Sifa na Utukufu tunakurudshia Mungu wetu....!!

Neno lako, ee Mwenyezi-Mungu, ladumu milele; limethibitika juu mbinguni. Uaminifu wako wadumu vizazi vyote, umeiweka dunia mahali pake nayo yadumu.
Tazama jana imepita ee Mungu wetu leo ni siku mpya na kesho ni siku nyingine Jehovah tunakuja mbele zako tukijinyenyekeza,tukijishusha na kujiachilia mikononi mwako
 Mungu wetu tunaomba utusamehe dhambi zetu zote tulizozifanya kwakuwaza,kwakunena,kwakutenda,kwakujua/kutojua
Baba wa Mbinguni nasi tunaomba utupe neema ya kuweza kuwasamehe wale wote waliotukosea
Jehovah usitutie majaribuni Mungu wetu tunaomba utuepushe na yule mwovu na kazi zake zote
Yahweh tunaomba ututakase miili yetu na akili zetu
Baba wa Mbinguni utufunike kwa Damu ya Bwana na Mwokozi wetu Yesu Kristo wa Nazareti
yeye aliteseka kwanza ili sisi tupate kupona

Kwakupigwa kwake sisi tumepata kupona....

Kwa amri yako viumbe vyote vipo leo, maana vitu vyote ni watumishi wako. Kama sheria yako isingekuwa furaha yangu, ningalikwisha angamia kwa taabu zangu. Sitasahau kamwe kanuni zako, maana kwa hizo umenipa uhai.
Yahweh tunaomba ukabariki kazi za mikono yetu

Baba wa Mbinguni tunaomba ukatupe ubunifu na maarifa 
katika utendaji
Jehovah nasi tukatende sawasawa na mapenzi yako
Baba wa Mbinguni tunaomba ukabariki ridhiki zetu
ziingiazo/zitokazo
Mungu wetu nasi tunaomba ukatupe neema ya kuweza
kuwabariki wenye kuhitaji
Yahweh tusipungukiwe katika mahitaji yetu
Mungu wetu ukatupe kama inavyokupendeza wewe

Baba wa Mbinguni tunayaweka maisha yetu mikononi mwako
Mungu wetu tunaomba ukabariki nyumba/ndoa zetu,
watoto,wazazi wetu,familia/ndugu na wote wanaotuzunguka
Jehovah tunaomba ulinzi wako kwetu na kwa vyote tunavyo vimiliki
Yahweh tunaomba ukatubariki tuingiapo/tutokapo
Mungu wetu tunaomba ukavibariki vyote tunavyoenda kugusa/kutumia
Baba wa Mbinguni ukavitakase kwa Damu ya Bwana wetu Yesu Kristo
Mungu wetu ukatamalaki na kutuatamia
Baba wa Mbinguni tukawe salama rohoni
Mfalme wa amani amani yako ikatawale katika maisha yetu
Mungu wetu ukatupe macho ya kuona na masikio ya kusikia 
sauti yako na kuitii
Baba wa Mbinguni tunaomba ukatupe neema ya kufuata njia zako
Yahweh tukasimamie Neno lako amri na sheria zako siku zote 
za maisha yetu
Mungu wetu ukaonekane katika maisha yetu
Neema zako zikawe nasi Nuru yako ikaangaze katika maisha yetu
ukatuguse kwa mkono wako wenye nguvu
Ukatufanye chombo chema ee Mungu wetu nasi tukatumike kama
inavyokupendeza wewe
Roho Mtakatifu akatuongoze katika yote na tukawe na kiasi...


Mimi ni wako, uniokoe, maana nimejitahidi kuzishika kanuni zako. Waovu wanivizia wapate kuniua; lakini mimi natafakari masharti yako. Nimetambua kila kitu hufikia kikomo, lakini amri yako ni kamilifu.
Mungu wetu tunawaweka mikononi mwako wenye shida/tabu,wote wanaopitia magumu/majaribu mbalimbali
Mungu wetu tunaomba ukawaguse kwa mkono wako wenye nguvu
 kila mmoja na mahitaji yake 
Mungu wetu tunaomba ukawasamehe pale walipokwenda kinyume nawe
Baba wa Mbinguni ukawape neema ya kujiombea,kufuata njia zako
wakasimamie Neno lako nalo likawaweke huru
Mungu wetu tunaomba ukasikie kuomba kwetu
Mungu wetu ukawatendee sawasawa na mapenzi yako
Kwakuwa Ufalme ni wako Nguvu na Utukufu hata Milele
Amina...!!


Asanteni sana wapendwa katika Kristo Yesu kwakuwa nami
Mungu Baba aendelee kuwabariki na kuwatendea 
kama inavyompendeza yeye....
Nawapenda.

Sala ya Habakuki
1Sala ya nabii Habakuki:
2Ee Mwenyezi-Mungu, nimesikia juu ya fahari yako,
juu ya matendo yako, nami naogopa.
Uyafanye tena mambo hayo wakati wetu;
uyafanye yajulikane wakati huu wetu.
Ukasirikapo tafadhali ukumbuke huruma yako!
3Mungu amekuja kutoka Temani,
Mungu mtakatifu kutoka mlima Parani.
Utukufu wake umetanda pote mbinguni,
nayo dunia imejaa sifa zake.
4Mng'ao wake ni kama wa jua;
miali imetoka mkononi mwake
ambamo nguvu yake yadhihirishwa.
5Maradhi yanatangulia mbele yake,
nyuma yake yanafuata maafa.
6Akisimama dunia hutikisika;
akiyatupia jicho mataifa, hayo hutetemeka.
Milima ya milele inavunjwavunjwa,
vilima vya kudumu vinadidimia;
humo zimo njia zake za kale na kale.
7Niliwaona watu wa Kushani wakiteseka,
na watu wa Midiani wakitetemeka.
8Ee Mwenyezi-Mungu, je, umeikasirikia mito?
Je, umeyakasirikia maji ya bahari,
hata ukaendesha farasi wako,
na magari ya vita kupata ushindi?
9Uliuweka tayari uta wako,
ukaweka mishale yako kwenye kamba.
Uliipasua ardhi kwa mito.
10Milima ilikuona, ikanyauka;
mafuriko ya maji yakapita humo.
Vilindi vya bahari vilinguruma,
na kurusha juu mawimbi yake.
11Jua na mwezi vilikaa kimya katika makazi yao,
vilipoona miali ya mishale yako ikienda kasi,
naam, vilipouona mkuki wako ukimetameta.
12Kwa ghadhabu ulipita juu ya nchi,
uliyakanyaga mataifa kwa hasira yako.
13Ulitoka kwenda kuwaokoa watu wako,
kumwokoa yule uliyemweka wakfu kwa mafuta.
Ulimponda kiongozi wa jamii ya waovu,
ukawaangamiza kabisa wafuasi wake.
14Amiri jeshi ulimchoma mishale yako,
jeshi lilipokuja kama kimbunga kututawanya,
wakijigamba kuwaangamiza maskini mafichoni mwao.
15Kwa farasi wako ulitembea juu ya bahari,
bahari inayosukwasukwa na mawimbi.
16Nasikia hayo nami ninashtuka mwilini,
midomo yangu inatetemeka kwa hofu;
mifupa yangu inateguka,
miguu yangu inatetemeka.
Ninangojea kwa utulivu siku ile ya maafa,
ambayo inawajia wale wanaotushambulia.
17Hata kama mitini isipochanua maua,
wala mizabibu kuzaa zabibu;
hata kama mizeituni isipozaa zeituni,
na mashamba yasipotoa chakula;
hata kama kondoo wakitoweka zizini,
na mifugo kukosekana mazizini,
18mimi nitaendelea kumfurahia Mwenyezi-Mungu
nitamshangilia Mungu anayeniokoa.
19Bwana, Mwenyezi-Mungu ndiye nguvu yangu,
huiimarisha miguu yangu kama ya paa,
huniwezesha kupita juu milimani.



Habakuki3;1-19

Biblia Habari Njema kwa Watu Wote(BHN)

"Swahili Na Waswahili"Mbarikiwe

Friday 10 July 2020

Kikombe Cha Asubuhi; Habakuki 2...

Shalom,Habari za Asubuhi,Hamjambo,Mmeamkaje?

Tumshukuru Mungu katika yote....

Mungu wetu Baba yetu,Muumba wetu Muumba wa Mbingu na Nchi
Muumba wa vyote vilivyomo vinavyoonekana na visivyoonekana
Mungu wa walio hai,Mungu  mwenye huruma,Mungu wa upendo
Mungu wa Abrahamu,Isaka na Yakobo...
Asante kwa wema na fadhili zako kwetu
Asante kwa ulinzi wako kwetu wakati wote
Asante kwa kutuchagua tena na kutupa
kibali cha kuendelea kuiona leo hii
Asante kwa pumzi/uzima,afya na kuwatayari kwa majukumu yetu

Neema yako yatutosha ee Mungu wetu....!!

Niko hoi kwa kukungojea uniokoe; naweka tumaini langu katika neno lako. Macho yangu yanafifia nikingojea ulichoahidi. Nauliza: “Utakuja lini kunifariji?”
Baba wa Mbinguni tunakuja mbele zako,
Tukijinyenyekeza,tukijiachilia mikononi mwako
Mungu wetu tunamomba utusamehe dhambi zetu
Baba wa Mbinguni nasi tunaomba ukatupe neema
 ya kuweza kuwasamehe wale wote waliotukosea

Usitutie majaribuni Mungu wetu tunaomba utuepushe
na yule mwovu na kazi zake zote
Jehovah ututakase miili yetu na akili zetu
Baba wa Mbinguni tunaomba utufunike kwa Damu
ya Bwana na Mwokozi wetu Yesu Kristo wa Nazareti
yeye aliteseka kwanza ili sisi tupate kupona....

Nimekunjamana kama kiriba katika moshi, hata hivyo sijasahau masharti yako. Mimi mtumishi wako nitasubiri mpaka lini? Utawaadhibu lini wale wanaonidhulumu? Wenye kiburi wamenichimbia mashimo, watu ambao hawafuati sheria yako.
Mungu wetu tunaomba ukabariki kazi za mikono yetu
Baba wa Mbinguni tunaomba ukatupe ubunifu na maarifa katika utendaji
Jehovah nasi tukatende sawasawa na mapenzi yako
Yahweh tunaomba ukabariki ridhiki zetu ziingiazo/zitokazo
Mungu wetu nasi tunaomna ukatupe neema ya kuweza kuwabariki wenye kuhitaji
Tusipungukiwe katika mahitaji yetu
Baba wa Mbinguni tunaomba ukatupe kama inavyokupendeza wewe...


Yahweh tunayaweka maisha yetu mikononi mwako
Mungu wetu tunaomba ukabariki nyumba/ndoa zetu,
Jehovah tunaomba ulinzi wako kwetu na kwa vyote tunavyovimiliki
Yahweh tunaomba ukatubariki tuingiapo/tutokapo
Mungu wetu tunaomba ukavibariki vyote tunavyoenda kugusa/kutumia
Baba wa Mbinguni ukavitakase kwa Damu ya Bwana wetu Yesu Kristo
Mungu wetu ukatamalaki na kutuatamia
Baba wa Mbinguni tukawe salama rohoni
Yahwe ukatupe akili ya kutambua mema na mabaya
Mfalme wa amani amani yako ikatawale katika maisha yetu
Mungu wetu ukatupe macho ya kuona,masikio ya kusikia sauti yako na kuitii..
Baba wa Mbinguni  tunaomba ukatupe neema ya kufuata
njia zako,tukasimamie Neno lako,amri na sheria zako
siku zote za maisha yetu...
Ukatuguse kwa mkono wako wenye nguvu,ukatufanye chombo chema
ee Mungu wetu nasi tukatumike kama inavyokupendeza wewe
Roho Mtakatifu akatuongoze katika yote na tukawe na kiasi....

Amri zako zote ni za kuaminika; watu wananitesa bila haki; unisaidie! Karibu wangefaulu kuniangamiza, lakini mimi sijavunja kanuni zako. Unisalimishe kadiri ya fadhili zako, nipate kuzingatia maamuzi uliyotamka.
Tazama watoto wako wenye shida/tabu,wote wanaopitia magumu/majaribu mbalimbali
Mungu wetu tunaomba ukawaguse kwa mkono wako wenye nguvu
kila mmoja na mahitaji yake
Mungu wetu tunaomba ukawasamehe pale walipo kwenda kinyume nawe
Yahweh tunaomba ukawape neema ya kuweza kujiombea,kufuata njia zako nazo zikawaweke huru...
Baba wa Mbinguni tunayaweka haya yote mikononi mwako
Kwakuwa Ufalme ni wako Nguvu na Utukufu hata Milele...
Amina...!!


Asanteni sana wapendwa katika Kristo Yesu kwakuwa nami,Baba wa Mbinguni aendelee kuwatendea sawasawa na mapenzi yake...

Nawapenda.

1Mimi nitasimama mahali pa kuchungulia,
na kukaa juu mnarani;
nitakaa macho nione ataniambia nini,
atajibu nini kuhusu lalamiko langu.”
Mungu anamjibu Habakuki
2Kisha, Mwenyezi-Mungu akanijibu hivi:
“Yaandike maono haya;
yaandike wazi juu ya vibao,
anayepitia hapo apate kuyasoma.
3 Taz Ebr 10:37 Maono haya yanangoja wakati wa kufaa;
ni maono ya ukweli juu ya mwisho.
Kama yaonekana kuchelewa, uyasubiri;
hakika yatafika, wala hayatachelewa.
4Andika:
‘Waangalie wenye kiburi, hao wataangamia;
lakini waadilifu wataishi kwa kumwamini Mungu.’”
Waovu wataangamia
5Zaidi ya hayo, divai hupotosha;
mtu mwenye kiburi hatadumu.
Yuko tayari kuwameza wengine kama Kuzimu;
kama vile kifo, hatosheki na kitu.
Hujikusanyia mataifa yote,
na watu wote kama mali yake.
6Kila mtu atamdhihaki mtu wa namna hiyo
na kumtungia misemo ya dhihaka:
“Ole wako unayejirundikia visivyo vyako,
na kuchukua rehani mali za watu lakini hulipi!
Utaendelea kufanya hivyo hadi lini?
7Siku moja wadeni wako watainuka ghafla,
wale wanaokutetemesha wataamka.
Ndipo utakuwa mateka wao.
8Wewe umeyapora mataifa mengi,
lakini wote wanaosalimika watakupora wewe,
kwa mauaji na dhuluma uliyoitendea dunia,
naam, uliyoifanyia miji na wakazi wake wote.
9“Ole wako unayejitajirisha kwa hasara ya mwingine,
ujengaye nyumba yako juu milimani
ukidhani kuwa salama mbali na madhara.
10Lakini kwa mipango yako umeiaibisha jamaa yako.
Kwa kuyaangamiza mataifa mengi,
umeyaangamiza maisha yako mwenyewe.
11Ndiyo maana hata mawe yatalalamika ukutani,
na boriti za nyumba zitayaunga mkono.
12“Ole wako unayejenga mji kwa mauaji
unayesimika jiji kwa maovu!
13Mwenyezi-Mungu wa majeshi husababisha
juhudi za watu zipotelee motoni,
na mataifa yajishughulishe bure.
14 Taz Isa 11:9 Utukufu wa Mwenyezi-Mungu utaenea pote duniani,
kama vile maji yaeneavyo baharini.
15Ole wako unayewalewesha jirani zako,
na kutia sumu katika divai yao
ili upate kuwaona wamekaa uchi.
16Utajaa aibu badala ya heshima.
Utakunywa wewe mwenyewe na kupepesuka!
Mwenyezi-Mungu mwenyewe atakulevya,
na aibu itaifunika heshima yako!
17Maovu uliyoitenda Lebanoni yatakuvamia wewe;
uliwaua wanyama, wanyama nao watakutisha.
Yote hayo yatakupata wewe,
kwa mauaji na dhuluma uliyoitendea dunia,
naam, uliyoifanyia miji na wakazi wake wote.
18“Chafaa nini kinyago alichotengeneza mtu?
Sanamu ni madini yaliyoyeyushwa,
ni kitu cha kueneza udanganyifu!
Mtengeneza sanamu hutumaini alichotengeneza mwenyewe,
kinyago ambacho hakiwezi hata kusema!
19Ole wake mtu aliambiaye gogo: ‘Amka!’
Au jiwe bubu ‘Inuka!’
Je, sanamu yaweza kumfundisha mtu?
Tazama imepakwa dhahabu na fedha,
lakini haina uhai wowote.”
20Lakini Mwenyezi-Mungu yumo katika hekalu lake takatifu;
dunia yote na ikae kimya mbele yake.

Habakuki2;1-20

Biblia Habari Njema kwa Watu Wote(BHN)

"Swahili Na Waswahili"Mbarikiwe