Swahili na Waswahili

Swahili na Waswahili
Waswahili na Mswahili Rachel Siwa...Pamoja Daima!!

Thursday 18 June 2020

Kikombe Cha Asubuhi; Tunamshukuru Mungu kwa kumaliza Kitabu cha Amosi,Leo Tunaanza Kitabu cha Obadia....1

Shalom,Habari za Asubuhi,Hamjambo,Mmeamkaje?

Tunamshukuru Mungu kwa kutupa kibali cha
 kupitia kitabu cha "AMOSI
"
Ni matumaini yangu kuna mengi tumejifunza/kufaidika
na kutupa mwanga/kuelewa kwenye kitabu hiki...

Leo tunapokwenda anza kupitia Kitabu cha"OBADIA"tunamuomba Mungu wetu akatupe kibali,macho ya rohoni
 na akili ya kuelewa katika kujifunza NENO lake...
Ee Mungu  tunaomba ukatuongoze...!!

Tumshukuru Mungu wetu katika yote...Mungu wetu Baba yetu,Muumba wetu Muumba wa Mbingu na Nchi
Muumba wa vyote vilivyomo vinavyoonekana na visivyoonekana
Mungu wa walio hai,Mungu  mwenye huruma,Mungu wa upendo
Mungu wa Abrahamu,Isaka na Yakobo...


Asante kwa wema na fadhili zako kwetu
Asante kwa ulinzi wako kwetu wakati wote
Asante kwa kutuchagua tena na kutupa
kibali cha kuendelea kuiona leo hii
Asante kwa pumzi/uzima,afya na kuwatayari kwa majukumu yetu

Neema yako yatutosha ee Mungu wetu....!!

Dhoruba iliendelea kuvuma na kesho yake wakaanza kutupa nje shehena ya meli. Siku ya tatu, wakaanza pia kutupa majini vifaa vya meli kwa mikono yao wenyewe.
Baba wa Mbinguni tunakuja mbele zako tukijinyenyekeza,
tukijishusha na kujiachilia mikononi mwako

Mungu wetu tunaomba utusamehe dhambi zetu zote 
Baba wa Mbinguni nasi tunaomba ukatupe neema
ya kuweza kuwasamehe wale wote waliotukosea
Usitutie majaribuni Mungu wetu tunaomba utuepushe
na yule mwovu na kazi zake zote
Jehovah ututakase miili yetu na akili zetu
Baba wa Mbinguni tunaomba utufunike kwa Damu
ya Bwana na Mwokozi wetu Yesu Kristo wa Nazareti
yeye aliteseka kwanza ili sisi tupate kupona....


Kwa muda wa siku nyingi hatukuweza kuona jua wala nyota; dhoruba iliendelea kuvuma sana, hata matumaini yote ya kuokoka yakatuishia.
Mungu wetu tunaomba ukabariki kazi za mikono yetu
Baba wa Mbinguni tunaomba ukatupe ubunifu na maarifa katika utendaji
Jehovah nasi tukatende sawasawa na mapenzi yako
Yahweh tunaomba ukabariki ridhiki zetu ziingiazo/zitokazo
Mungu wetu nasi tunaomna ukatupe neema ya kuweza kuwabariki wenye kuhitaji
Tusipungukiwe katika mahitaji yetu
Baba wa Mbinguni tunaomba ukatupe kama inavyokupendeza wewe...


Yahweh tunayaweka maisha yetu mikononi mwako
Mungu wetu tunaomba ukabariki nyumba/ndoa zetu,
Jehovah tunaomba ulinzi wako kwetu na kwa vyote tunavyovimiliki
Yahweh tunaomba ukatubariki tuingiapo/tutokapo
Mungu wetu tunaomba ukavibariki vyote tunavyoenda kugusa/kutumia
Baba wa Mbinguni ukavitakase kwa Damu ya Bwana wetu Yesu Kristo
Mungu wetu ukatamalaki na kutuatamia
Baba wa Mbinguni tukawe salama rohoni
Yahwe ukatupe akili ya kutambua mema na mabaya
Mfalme wa amani amani yako ikatawale katika maisha yetu
Mungu wetu ukatupe macho ya kuona,masikio ya kusikia sauti yako na kuitii..
Baba wa Mbinguni  tunaomba ukatupe neema ya kufuata
njia zako,tukasimamie Neno lako,amri na sheria zako
siku zote za maisha yetu...
Ukatuguse kwa mkono wako wenye nguvu,ukatufanye chombo chema
ee Mungu wetu nasi tukatumike kama inavyokupendeza wewe
Roho Mtakatifu akatuongoze katika yote na tukawe na kiasi....

Baada ya kukaa muda mrefu bila kula chakula, Paulo alisimama kati yao, akasema, “Waheshimiwa, ingalikuwa afadhali kama mngalinisikiliza na kuacha kusafiri kutoka Krete. Kama mngalifanya hivyo tungaliiepuka shida hii na hasara hizi zote.
Tazama watoto wako wenye shida/tabu,wote wanaopitia magumu/majaribu mbalimbali
Mungu wetu tunaomba ukawaguse kwa mkono wako wenye nguvu
kila mmoja na mahitaji yake
Mungu wetu tunaomba ukawasamehe pale walipo kwenda kinyume nawe
Yahweh tunaomba ukawape neema ya kuweza kujiombea,kufuata njia zako nazo zikawaweke huru...
Baba wa Mbinguni tunayaweka haya yote mikononi mwako
Kwakuwa Ufalme ni wako Nguvu na Utukufu hata Milele...
Amina...!!


Asanteni sana wapendwa katika Kristo Yesu kwakuwa nami,Baba wa Mbinguni aendelee kuwatendea sawasawa na mapenzi yake...
Nawapenda.

1Maono ya Obadia. Mambo aliyosema Bwana Mwenyezi-Mungu kuhusu taifa la Edomu.
Mwenyezi-Mungu ataadhibu Edomu
Tumepata habari kutoka kwa Mwenyezi-Mungu;
mjumbe ametumwa kati ya mataifa:
“Inukeni! Twende tukapigane na Edomu!”
2Mwenyezi-Mungu aliambia taifa la Edomu:
“Nitakufanya mdogo miongoni mwa mataifa,
utadharauliwa kabisa na wote.
3Kiburi chako kimekudanganya:
Kwa kuwa mji wako mkuu ni ngome ya miamba imara
na makao yako yapo juu milimani,
hivyo wajisemea,
‘Nani awezaye kunishusha chini?’
4Hata ukiruka juu kama tai,
ukafanya makao yako kati ya nyota,
mimi nitakushusha chini tu.
Nasema mimi Mwenyezi-Mungu.
5“Kama wezi au wanyang'anyi wangekujia usiku,
je, wasingechukua tu kiasi cha kuwatosha?
Ikiwa wavunaji zabibu wangekujia,
je, wasingekuachia kiasi kidogo tu?
Lakini wewe, adui zako wamekuangamiza kabisa.
6Enyi wazawa wa Esau, mali zenu zimetekwa;
hazina zenu zote zimeporwa!
7Washirika wenzenu wamewadanganya,
wamewafukuza nchini mwenu.
Mliopatana nao wamewashinda vitani,
rafiki wa kutegemewa ndio waliokutegea mitego,
nawe hukuelewa yaliyokuwa yanatendeka.
8Mimi Mwenyezi-Mungu nakuuliza hivi:
Je, siku hiyo, sitawaangamiza wenye hekima kutoka Edomu
na wenye maarifa kutoka mlima Esau?
9Ewe Temani, mashujaa wako watatishika
na kila mtu atauawa mlimani Esau.
Sababu za Edomu kuadhibiwa
10“Kwa sababu ya matendo maovu
mliyowatendea ndugu zenu wazawa wa Yakobo,
mtaaibishwa na kuangamizwa milele.
11Siku ile mlisimama kando mkitazama tu,
wakati wageni walipopora utajiri wao,
naam, wageni walipoingia malango yao
na kugawana utajiri wa Yerusalemu kwa kura.
Kwa hiyo nanyi mlitenda kama wazawa wao.
12Msingalifurahia siku hiyo ndugu zenu walipokumbwa na mikasa;
msingaliwacheka Wayuda
na kuona fahari wakati walipoangamizwa;
msingalijigamba wenzenu walipokuwa wanataabika.
13Msingeliingia katika mji wa watu wangu,
siku walipokumbwa na maafa;
msingelipora mali zao, siku hiyo ya maafa yao.
14Msingelisimama kwenye njia panda
na kuwakamata wakimbizi wao;
wala msingeliwakabidhi kwa adui zao
wale waliobaki hai.
Mungu atayahukumu mataifa
15“Siku inakaribia ambapo mimi Mwenyezi-Mungu
nitayahukumu mataifa yote.
Kama mlivyowatendea wengine, ndivyo mtakavyotendewa,
mtalipwa kulingana na matendo yenu.
16Maana, kama walivyokunywa kikombe cha ghadhabu yangu
kwenye mlima wangu mtakatifu
ndivyo na mataifa jirani yatakavyokunywa;
watakunywa na kupepesuka,
wataangamia kana kwamba hawakuwahi kuwapo duniani.
Waisraeli watashinda
17“Lakini mlimani Siyoni watakuwapo wale waliosalimika
nao utakuwa mlima mtakatifu.
Wazawa wa Yakobo wataimiliki tena nchi iliyokuwa yao.
18Wazawa wa Yakobo watakuwa kama moto
na wazawa wa Yosefu kama miali ya moto.
Watawaangamiza wazawa wa Esau
kama vile moto uteketezavyo mabua makavu,
asinusurike hata mmoja wao.
Mimi, Mwenyezi-Mungu, nimesema.
19Wale wanaokaa Negebu wataumiliki mlima Esau;
wale wanaokaa Shefela wataimiliki nchi ya Wafilisti.
Waisraeli watamiliki nchi za Efraimu na Samaria
na watu wa Benyamini wataimiliki nchi ya Gileadi.
20Waisraeli walio uhamishoni Hala
wataimiliki Foinike hadi Sarepta.
Watu wa Yerusalemu walio uhamishoni Sefaradi
wataimiliki miji ya Negebu.
21Waokoaji watapanda juu ya mlima Siyoni
ili kuutawala mlima Esau;
naye Mwenyezi-Mungu atakuwa ndiye Mfalme.”

Obadia1;1-21

Biblia Habari Njema kwa Watu Wote(BHN)

"Swahili Na Waswahili"Mbarikiwe

Wednesday 17 June 2020

Kikombe Cha Asubuhi; Amosi 9...

Shalom,Habari za Asubuhi,Hamjambo,Mmeamkaje?

Tumshukuru Mungu katika yote....

Mungu wetu Baba yetu,Muumba wetu Muumba wa Mbingu na Nchi
Muumba wa vyote vilivyomo vinavyoonekana na visivyoonekana
Mungu wa walio hai,Mungu  mwenye huruma,Mungu wa upendo
Mungu wa Abrahamu,Isaka na Yakobo...
Asante kwa wema na fadhili zako kwetu
Asante kwa ulinzi wako kwetu wakati wote
Asante kwa kutuchagua tena na kutupa
kibali cha kuendelea kuiona leo hii
Asante kwa pumzi/uzima,afya na kuwatayari kwa majukumu yetu

Neema yako yatutosha ee Mungu wetu....!!

Basi, upepo mzuri wa kusi ulianza kuvuma, nao wakadhani wamefanikiwa lengo lao; hivyo wakangoa nanga, wakaiendesha meli karibu sana na pwani ya Krete. Lakini haukupita muda, upepo mkali uitwao “Upepo wa Kaskazi” ulianza kuvuma kutoka kisiwani.
Baba wa Mbinguni tunakuja mbele zako,
Tukijinyenyekeza,tukijiachilia mikononi mwako
Mungu wetu tunamomba utusamehe dhambi zetu
Baba wa Mbinguni nasi tunaomba ukatupe neema
 ya kuweza kuwasamehe wale wote waliotukosea

Usitutie majaribuni Mungu wetu tunaomba utuepushe
na yule mwovu na kazi zake zote
Jehovah ututakase miili yetu na akili zetu
Baba wa Mbinguni tunaomba utufunike kwa Damu
ya Bwana na Mwokozi wetu Yesu Kristo wa Nazareti
yeye aliteseka kwanza ili sisi tupate kupona....

Upepo uliipiga ile meli, na kwa kuwa hatukuweza kuukabili, tukaiacha ikokotwe na huo upepo. Kisiwa kimoja kiitwacho Kauda kilitukinga kidogo na ule upepo; na tulipopita kusini mwake tulifaulu, ingawa kwa shida, kuusalimisha ule mtumbwi wa meli.
Mungu wetu tunaomba ukabariki kazi za mikono yetu
Baba wa Mbinguni tunaomba ukatupe ubunifu na maarifa katika utendaji
Jehovah nasi tukatende sawasawa na mapenzi yako
Yahweh tunaomba ukabariki ridhiki zetu ziingiazo/zitokazo
Mungu wetu nasi tunaomna ukatupe neema ya kuweza kuwabariki wenye kuhitaji
Tusipungukiwe katika mahitaji yetu
Baba wa Mbinguni tunaomba ukatupe kama inavyokupendeza wewe...


Yahweh tunayaweka maisha yetu mikononi mwako
Mungu wetu tunaomba ukabariki nyumba/ndoa zetu,
Jehovah tunaomba ulinzi wako kwetu na kwa vyote tunavyovimiliki
Yahweh tunaomba ukatubariki tuingiapo/tutokapo
Mungu wetu tunaomba ukavibariki vyote tunavyoenda kugusa/kutumia
Baba wa Mbinguni ukavitakase kwa Damu ya Bwana wetu Yesu Kristo
Mungu wetu ukatamalaki na kutuatamia
Baba wa Mbinguni tukawe salama rohoni
Yahwe ukatupe akili ya kutambua mema na mabaya
Mfalme wa amani amani yako ikatawale katika maisha yetu
Mungu wetu ukatupe macho ya kuona,masikio ya kusikia sauti yako na kuitii..
Baba wa Mbinguni  tunaomba ukatupe neema ya kufuata
njia zako,tukasimamie Neno lako,amri na sheria zako
siku zote za maisha yetu...
Ukatuguse kwa mkono wako wenye nguvu,ukatufanye chombo chema
ee Mungu wetu nasi tukatumike kama inavyokupendeza wewe
Roho Mtakatifu akatuongoze katika yote na tukawe na kiasi....

Wale wanamaji waliuvuta mtumbwi ndani, kisha wakaizungushia meli kamba na kuifunga kwa nguvu. Waliogopa kwamba wangeweza kukwama kwenye ufuko wa bahari, pwani ya Libia. Kwa hiyo walishusha matanga na kuiacha meli ikokotwe na upepo.
Tazama watoto wako wenye shida/tabu,wote wanaopitia magumu/majaribu mbalimbali
Mungu wetu tunaomba ukawaguse kwa mkono wako wenye nguvu
kila mmoja na mahitaji yake
Mungu wetu tunaomba ukawasamehe pale walipo kwenda kinyume nawe
Yahweh tunaomba ukawape neema ya kuweza kujiombea,kufuata njia zako nazo zikawaweke huru...
Baba wa Mbinguni tunayaweka haya yote mikononi mwako
Kwakuwa Ufalme ni wako Nguvu na Utukufu hata Milele...
Amina...!!


Asanteni sana wapendwa katika Kristo Yesu kwakuwa nami,Baba wa Mbinguni aendelee kuwatendea sawasawa na mapenzi yake...

Nawapenda.

Adhabu ya Mungu
1Nilimwona Mwenyezi-Mungu amesimama kando ya madhabahu, naye akaniamuru:
“Zipige hizo nguzo za hekalu
mpaka misingi yake itikisike.
Zivunje hizo nguzo ziwaangukie watu vichwani.
Wale watakaosalia nitawaua kwa upanga;
hakuna hata mmoja wao atakayenusurika,
naam, hakuna atakayetoroka.
2Wajapojichimbia njia ya kwenda kuzimu,
huko nitawachukua kwa mkono wangu;
wajapopanda mbinguni,
nitawaporomosha chini.
3Wajapojificha juu ya mlima Karmeli,
huko nitawasaka na kuwachukua;
wajapojificha mbali nami vilindini mwa bahari,
humo nitaliamuru joka la baharini liwaume.
4Wajapochukuliwa mateka na adui zao,
huko nitatoa amri wauawe kwa upanga.
Nitawachunga kwa makini sana
niwatendee mabaya na si mema.”
5Bwana Mwenyezi-Mungu wa majeshi,
anaigusa ardhi nayo inatetemeka
na wakazi wake wanaomboleza;
dunia nzima inapanda na kushuka
kama kujaa na kupwa kwa mto Nili wa Misri.
6Mwenyezi-Mungu amejenga makao yake mbinguni,
nayo dunia akaifunika kwa anga;
huyaita maji ya bahari,
na kuyamwaga juu ya nchi kavu.
Mwenyezi-Mungu, ndilo jina lake!
Marekebisho baada ya uharibifu
7Mwenyezi-Mungu asema hivi:
“Kwangu mimi, nyinyi Waisraeli,
hamna tofauti yoyote na watu wa Kushi!9:7 Kushi: Eneo ambalo sasa ni Ethiopia na sehemu ya Sudani.
Niliwatoa Wafilisti kutoka Krete,
na Waashuru kutoka Kiri,
kama nilivyowatoa nyinyi kutoka Misri.
8Mimi, Bwana Mwenyezi-Mungu nautazama ufalme wenye dhambi,
na nitauangamiza kabisa kutoka duniani.
Lakini sitawaangamiza wazawa wote wa Yakobo.
9“Tazama, nitatoa amri,
na kuwapepeta Waisraeli kati ya mataifa
kama mtu achekechavyo nafaka
niwakamate wote wasiofaa.
10Wenye dhambi miongoni mwa watu wangu,
watafia vitani kwa upanga;
hao ndio wasemao:
‘Maafa hayatatukumba wala kutupata!’
11“Siku yaja nitakapoisimika nyumba ya Daudi iliyoanguka;
nitazitengeneza kuta zake,
na kusimika upya magofu yake.
Nitaijenga upya kama ilivyokuwa hapo zamani.
12Nao Waisraeli watamiliki mabaki ya Edomu
na mataifa yote yaliyokuwa yangu.
Mimi Mwenyezi-Mungu nimesema,
na nitafanya hivyo.
13“Wakati waja kwa hakika,
ambapo mara baada ya kulima
mavuno yatakuwa tayari kuvunwa;
mara baada ya kupanda mizabibu
utafuata wakati wa kuvuna zabibu.
Milima itabubujika divai mpya,
navyo vilima vitatiririka divai.
14Nitarekebisha hali ya watu wangu Waisraeli.
Watajenga miji yao iliyoharibiwa na kuishi humo;
watapanda mizabibu na kunywa divai yake;
watalima mashamba na kula mazao yake.
15Nitawasimika katika nchi yao,
wala hawatang'olewa tena
kutoka katika nchi niliyowapa.
Mimi Mwenyezi-Mungu nimesema.”


Amosi9;1-15

Biblia Habari Njema kwa Watu Wote(BHN)

"Swahili Na Waswahili"Mbarikiwe

Tuesday 16 June 2020

Kikombe Cha Asubuhi; Amosi 8...

Shalom,Habari za Asubuhi,Hamjambo,Mmeamkaje?

Tumshukuru Mungu wetu katika yote...

Asante  Mungu wetu kwa wema na fadhili zako kwetu
Asante kwa ulinzi wako kwetu wakati wote
Asante kwa kutuchagua tena na kutupa
kibali cha kuendelea kuiona leo hii
Asante kwa pumzi/uzima,afya na kuwatayari kwa majukumu yetu


Utukuzwe ee Mungu wetu,usifiwe Baba wa Mbinguni

Neema yako yatutosha  Mungu wetu..!

Muda mrefu ulikuwa umepita, na hata siku ya kufunga ilikuwa imekwisha pita. Sasa ilikuwa hatari sana kusafiri kwa meli. Basi, Paulo aliwapa onyo: “Waheshimiwa, nahisi kwamba safari hii itakuwa ya shida na hasara nyingi si kwa shehena na meli tu, bali pia kwa maisha yetu.”
Baba wa Mbinguni tunakuja mbele zako tukijinyenyekeza,
tukijishusha na kujiachilia mikononi mwako

Mungu wetu tunaomba utusamehe dhambi zetu zote
Baba wa Mbinguni nasi tunaomba utupe neema ya kuweza kuwasamehe wale wote waliotukosea,Usitutie majaribuni Mungu wetu tunaomba utuepushe na yule mwovu na kazi zake zote,Jehovah ututakase miili yetu na akili zetu Baba wa Mbinguni tunaomba utufunike kwa  Damu ya Bwana na Mwokozi wetu Yesu Kristo wa Nazareti,
Yeye aliteseka kwanza ili sisi tupate kupona....

Lakini yule ofisa alivutiwa zaidi na maoni ya nahodha na ya mwenye meli kuliko yale aliyosema Paulo.
Mungu wetu tunaomba ukabariki kazi za mikono yetu
Baba wa Mbinguni tunaomba ukatupe ubunifu na maarifa 
katika utendaji
Jehovah nasi tukatende sawasawa na mapenzi yako
Baba wa Mbinguni tunaomba ukabariki ridhiki zetu
ziingiazo/zitokazo
Mungu wetu nasi tunaomba ukatupe neema ya kuweza
kuwabariki wenye kuhitaji
Yahweh tusipungukiwe katika mahitaji yetu
Mungu wetu ukatupe kama inavyokupendeza wewe



Jehovah tunayaweka maisha yetu mikononi mwako
Baba wa Mbinguni tunaomba ukabariki nyumba/ndoa zetu,
watoto,wazazi wetu,familia/ndugu na wote wanaotuzunguka
Jehovah tunaomba ulinzi wako kwetu na kwa vyote tunavyo vimiliki
Yahweh tunaomba ukatubariki tuingiapo/tutokapo
Mungu wetu tunaomba ukavibariki vyote tunavyoenda kugusa/kutumia
Baba wa Mbinguni ukavitakase kwa Damu ya Bwana wetu Yesu Kristo
Mungu wetu ukatamalaki na kutuatamia
Baba wa Mbinguni tukawe salama rohoni
Mfalme wa amani amani yako ikatawale katika maisha yetu
Mungu wetu ukatupe macho ya kuona na masikio ya kusikia 
sauti yako na kuitii
Baba wa Mbinguni tunaomba ukatupe neema ya kufuata njia zako
Yahweh tukasimamie Neno lako amri na sheria zako siku zote 
za maisha yetu

Mungu  wetu ukaonekane katika maisha yetu popote tupitapo na ikajulikane kwamba upo 

Neema zako zikawe nasi Nuru yako ikaangaze katika maisha yetu
Ukatufanye barua njema ee Mungu wetu nasi tukasomeke kama
inavyokupendeza wewe
Roho Mtakatifu akatuongoze katika yote na tukawe na kiasi...

Kwa kuwa bandari hiyo haikuwa mahali pazuri pa kukaa wakati wa baridi, wengi walipendelea kuendelea na safari, ikiwezekana mpaka Foinike. Foinike ni bandari ya Krete inayoelekea kusini-magharibi na kaskazini-magharibi; na huko wangeweza kukaa wakati wa baridi.
Tazama wenye shida/tabu,Mungu wetu tunaomba
 ukawaguse kila mmoja na mahitaji yake
Baba wa Mbinguni tunaomba ukawasamehe pale walipokwenda
kinyume nawe
Mungu wetu ukawape neema ya kujiombea,macho ya rohoni,masikio yakusikia sauti yako,wakafuate njia zako nazo zikawaweke huru
Mungu wetu tunaomba ukasikie kulia kwao
Baba wa Mbinguni tunomba ukawafute machozi yao
Nuru yako ikaangaze katika maisha yao
Mungu wetu tunaomba ukawatendee sawasawa na mapenzi yako
Kwakuwa Ufalme ni wako Nguvu na Utukufu hata Milele
Amina....!!!


Wapendwa katika Kristo Yesu asanteni sana
kwakuwanami/kunisoma

Mungu Baba aendelee kuwabariki na kuwatendea
kama inavyompendeza yeye
Amani ya Bwana wetu Yesu Kristo na upendo wa Mungu Baba
ukae nanyi daima....

Nawapenda.


Maono ya nne: Kikapu cha matunda
1Bwana Mwenyezi-Mungu alinijalia maono mengine: Niliona kikapu kilichojaa matunda ya kiangazi. 2Naye Mwenyezi-Mungu akaniuliza: “Amosi, unaona nini?” Nami nikamjibu, “Naona kikapu cha matunda ya kiangazi.”8:2 Maneno “matunda ya kiangazi” na neno “mwisho” katika Kiebrania yanakaribiana sana kimatamshi. Kisha Mwenyezi-Mungu akaniambia:
“Mwisho umewafikia watu wangu wa Israeli.
Sitavumilia tena maovu yao.
3Siku hiyo, nyimbo za ikulu zitakuwa maombolezo.
Kutakuwa na maiti nyingi,
nazo zitatupwa nje kimyakimya.”8:3 nje kimyakimya: Au “nje. Kimya!”
Mungu ataiadhibu Israeli
4Sikilizeni enyi mnaowakandamiza wanyonge
na kuwaletea maangamizi fukara wa nchi.
5Mnajisemea mioyoni mwenu:
“Sikukuu ya mwezi mwandamo itakwisha lini
ili tuanze tena kuuza nafaka yetu?
Siku ya Sabato itakwisha lini
ili tupate kuuza ngano yetu?
Tutatumia vipimo hafifu vya wastani na uzito,
tutadanganya watu kwa mizani isizo sawa,
6hata kuuza ngano hafifu kwa bei kubwa.
Tutaweza kununua watu fukara kwa fedha,
na wahitaji kwa jozi ya kandambili.”
7Mwenyezi-Mungu, fahari ya Yakobo, ameapa:
“Hakika, sitayasahau matendo yao maovu.
8Kwa hiyo, dunia itatetemeka
na kila mtu nchini ataomboleza.
Nchi yote itayumbayumba;
itapanda na kushuka,
kama yanavyojaa na kupwa maji ya mto Nili!”
9Bwana Mwenyezi-Mungu asema,
“Siku hiyo nitalifanya jua litue adhuhuri,
na kuijaza nchi giza mchana.
10Sherehe zenu nitazigeuza kuwa kilio,
na nyimbo zenu za furaha kuwa maombolezo.
Nitawafanya nyote mvae magunia kwa huzuni
na kunyoa vipara vichwa vyenu,
kama kuomboleza kifo cha mtoto wa pekee;
na siku ya mwisho itakuwa ya uchungu mkubwa.”
11Bwana Mwenyezi-Mungu asema,
“Siku zaja ambapo nitaleta njaa nchini.
Lakini sio njaa na kiu ya chakula na maji,
bali njaa ya kusikia maneno ya Mwenyezi-Mungu.
12Watu watatangatanga kutoka bahari hata bahari,
kutoka upande wa kaskazini mpaka mashariki.
Watakimbia huko na huko wakitafuta neno la Mwenyezi-Mungu,
lakini hawatalipata.
13“Siku hiyo, hata vijana wenye afya,
wa kiume kwa wa kike,
watazimia kwa kiu.
14Wale wanaoapa kwa mungu wa uongo wa Samaria,
na kusema: ‘Kwa nafsi ya mungu wako ee Dani’;
na, ‘Kwa nafsi ya mungu wa Beer-sheba’,
wote wataanguka na hawatainuka tena kamwe.”

Amosi8;1-14

Biblia Habari Njema kwa Watu Wote(BHN)

"Swahili Na Waswahili"Mbarikiwe

Monday 15 June 2020

Kikombe Cha Asubuhi; Amosi 7...

Shalom,Habari za Asubuhi,Hamjambo,Mmeamkaje?

Haleluyah ni siku/wiki nyingine tena Mungu wetu ametuchagua

na kutupa kibali cha kuendelea kuiona leo hii
Si kwamba sisi tumetenda mema sana wala si kwa nguvu zetu
si kwa utashi wetu wala si kwa akili zetu si kwamba sisi
ni wazuri mno si kwa uwezo wetu sisi kuwa hivi tulivyo leo hii
Ni kwa rehema/neema zake ni kwa mapenzi yake Mungu wetu....

Tumshukuru Mungu wetu katika yote...

Asante Mungu wetu kwa wema na fadhili zako kwetu
Asante kwa ulinzi wako kwetu wakati wote
Asante kwa pumzi/uzima,afya na kuwa tayari kwa majukumu yetu
Sifa na Utukufu tunakurudshia Mungu wetu....!!

Kutoka huko tuliendelea na safari, lakini kwa kuwa upepo ulikuwa unavuma kwa kasi kutujia kwa mbele, tulipitia upande wa kisiwa cha Kupro ambapo upepo haukuwa mwingi. Halafu tulivuka bahari ya Kilikia na Pamfulia, tukatia nanga Mura, mji wa Lukia.
Tazama jana imepita ee Mungu wetu leo ni siku mpya na kesho ni siku nyingine Jehovah tunakuja mbele zako tukijinyenyekeza,tukijishusha na kujiachilia mikononi mwako
 Mungu wetu tunaomba utusamehe dhambi zetu zote tulizozifanya kwakuwaza,kwakunena,kwakutenda,kwakujua/kutojua
Baba wa Mbinguni nasi tunaomba utupe neema ya kuweza kuwasamehe wale wote waliotukosea
Jehovah usitutie majaribuni Mungu wetu tunaomba utuepushe na yule mwovu na kazi zake zote
Yahweh tunaomba ututakase miili yetu na akili zetu
Baba wa Mbinguni utufunike kwa Damu ya Bwana na Mwokozi wetu Yesu Kristo wa Nazareti
yeye aliteseka kwanza ili sisi tupate kupona

Kwakupigwa kwake sisi tumepata kupona....

Hapo yule ofisa alikuta meli moja ya Aleksandria iliyokuwa inakwenda Italia, na hivyo akatupandisha ndani. Kwa muda wa siku nyingi tulisafiri polepole, na kwa shida tulifika karibu na Nido. Kwa sababu upepo ulikuwa bado unatupinga, tuliendelea mbele moja kwa moja tukapitia upande wa Krete karibu na rasi Salmone ambapo upepo haukuwa mwingi.
Yahweh tunaomba ukabariki kazi za mikono yetu

Baba wa Mbinguni tunaomba ukatupe ubunifu na maarifa 
katika utendaji
Jehovah nasi tukatende sawasawa na mapenzi yako
Baba wa Mbinguni tunaomba ukabariki ridhiki zetu
ziingiazo/zitokazo
Mungu wetu nasi tunaomba ukatupe neema ya kuweza
kuwabariki wenye kuhitaji
Yahweh tusipungukiwe katika mahitaji yetu
Mungu wetu ukatupe kama inavyokupendeza wewe

Baba wa Mbinguni tunayaweka maisha yetu mikononi mwako
Mungu wetu tunaomba ukabariki nyumba/ndoa zetu,
watoto,wazazi wetu,familia/ndugu na wote wanaotuzunguka
Jehovah tunaomba ulinzi wako kwetu na kwa vyote tunavyo vimiliki
Yahweh tunaomba ukatubariki tuingiapo/tutokapo
Mungu wetu tunaomba ukavibariki vyote tunavyoenda kugusa/kutumia
Baba wa Mbinguni ukavitakase kwa Damu ya Bwana wetu Yesu Kristo
Mungu wetu ukatamalaki na kutuatamia
Baba wa Mbinguni tukawe salama rohoni
Mfalme wa amani amani yako ikatawale katika maisha yetu
Mungu wetu ukatupe macho ya kuona na masikio ya kusikia 
sauti yako na kuitii
Baba wa Mbinguni tunaomba ukatupe neema ya kufuata njia zako
Yahweh tukasimamie Neno lako amri na sheria zako siku zote 
za maisha yetu
Mungu wetu ukaonekane katika maisha yetu
Neema zako zikawe nasi Nuru yako ikaangaze katika maisha yetu
ukatuguse kwa mkono wako wenye nguvu
Ukatufanye chombo chema ee Mungu wetu nasi tukatumike kama
inavyokupendeza wewe
Roho Mtakatifu akatuongoze katika yote na tukawe na kiasi...

Tulipita kando yake polepole tukafika mahali paitwapo “Bandari Nzuri,” karibu na mji wa Lasea.
Mungu wetu tunawaweka mikononi mwako wenye shida/tabu,wote wanaopitia magumu/majaribu mbalimbali
Mungu wetu tunaomba ukawaguse kwa mkono wako wenye nguvu
 kila mmoja na mahitaji yake 
Mungu wetu tunaomba ukawasamehe pale walipokwenda kinyume nawe
Baba wa Mbinguni ukawape neema ya kujiombea,kufuata njia zako
wakasimamie Neno lako nalo likawaweke huru
Mungu wetu tunaomba ukasikie kuomba kwetu
Mungu wetu ukawatendee sawasawa na mapenzi yako
Kwakuwa Ufalme ni wako Nguvu na Utukufu hata Milele
Amina...!!


Asanteni sana wapendwa katika Kristo Yesu kwakuwa nami
Mungu Baba aendelee kuwabariki na kuwatendea 
kama inavyompendeza yeye....
Nawapenda.


MAONO YA HUKUMU
Maono ya kwanza: Nzige
1Siku moja, Bwana Mwenyezi-Mungu alinijalia maono: Nilimwona Mungu anaumba nzige kundi zima, mara baada ya watu kumaliza kukata nyasi kwa ajili ya wanyama wa mfalme. Wakati huo, nyasi zilikuwa ndio zinaanza kuchipua tena. 2Niliwaona nzige hao wakila na kumaliza kila jani katika nchi. Ndipo nikasema:
“Ee Bwana Mwenyezi-Mungu, nakusihi utuhurumie!
Wazawa wa Yakobo watawezaje kuishi?
Wao ni wadogo mno!”
3Basi, Bwana Mwenyezi-Mungu akabadili nia yake,
akasema, “Haitakuwa hivyo!”
Maono ya pili: Moto
4Bwana Mwenyezi-Mungu alinijalia maono mengine: Nilimwona Bwana Mwenyezi-Mungu akiuita moto wa hukumu ya kuwaadhibu watu. Moto huo uliunguza vilindi vikuu vya bahari, ukaanza kuiteketeza nchi kavu. 5Ndipo nikasema:
“Ee Bwana Mwenyezi-Mungu, nakusihi uache kuadhibu!
Wazawa wa Yakobo watawezaje kuishi?
Wao ni wadogo mno!”
6Basi, Mwenyezi-Mungu akabadili nia yake,
akasema: “Hili pia halitatukia.”
Maono ya tatu: Timazi
7Mwenyezi-Mungu alinijalia tena maono mengine: Nilimwona Mwenyezi-Mungu amesimama karibu na ukuta, ameshika mkononi mwake uzi wenye timazi. 8Naye akaniuliza: “Amosi, unaona nini?” Nikamjibu, “Naona timazi.” Kisha Mwenyezi-Mungu akasema:
“Tazama! Naweka timazi kati ya watu wangu Waisraeli.
Sitavumilia tena maovu yao.
9Huko vilimani ambako wazawa wa Isaka hutambikia,
kutafanywa kuwa uharibifu mtupu
na maskani ya Waisraeli yatakuwa magofu.
Nitaushambulia kwa vita ukoo wa mfalme Yeroboamu.”
Amosi na Amazia
10Basi, Amazia kuhani wa mji wa Betheli, akampelekea mfalme Yeroboamu wa Israeli habari hizi: “Amosi analeta fitina juu yako katika ufalme wa Israeli. Hotuba zake ni hatari kwa nchi hii. 11Anachosema ni hiki:
‘Yeroboamu atakufa kwa upanga
nao Waisraeli watapelekwa uhamishoni,
mbali kabisa na nchi yao.’”
12Kisha Amazia akamwambia Amosi, “Sasa tumekuchoka, ewe nabii! Nenda zako! Rudi katika nchi ya Yuda, ukatoe unabii huko upate na ujira wako hukohuko. 13Usitoe tena unabii hapa mjini Betheli, kwa kuwa hapa ni maskani ya ibada ya mfalme; ni hekalu la utawala huu.”
14Amosi akamjibu Amazia, “Mimi si nabii wa kuajiriwa, wala si mmoja wa kikundi cha manabii. Mimi ni mchungaji na mtunza mikuyu. 15Mwenyezi-Mungu alinitoa katika kazi yangu hiyo ya uchungaji, akaniamuru nije kuwaambia unabii watu wake wa Israeli.
16Nawe basi, ewe Amazia,
sikiliza neno la Mwenyezi-Mungu:
Wewe waniambia nisitoe unabii dhidi ya Israeli,
wala nisihubiri dhidi ya wazawa wa Isaka.
17Kwa hiyo, Mwenyezi-Mungu asema hivi:
‘Mkeo atakuwa malaya mjini,
na wanao wa kiume na kike watauawa vitani.
Ardhi yako itagawanywa na kupewa wengine,
nawe binafsi utafia katika nchi najisi,
nao Waisraeli hakika watapelekwa uhamishoni,
mbali kabisa na nchi yao.’”


Amosi7;1-17

Biblia Habari Njema kwa Watu Wote(BHN)

"Swahili Na Waswahili"Mbarikiwe