Swahili na Waswahili

Swahili na Waswahili
Waswahili na Mswahili Rachel Siwa...Pamoja Daima!!

Friday 12 June 2020

Kikombe Cha Asubuhi; Amosi 6...

Shalom,Habari za Asubuhi,Hamjambo,Mmeamkaje?

Tumshukuru Mungu katika yote....

Mungu wetu Baba yetu,Muumba wetu Muumba wa Mbingu na Nchi
Muumba wa vyote vilivyomo vinavyoonekana na visivyoonekana
Mungu wa walio hai,Mungu  mwenye huruma,Mungu wa upendo
Mungu wa Abrahamu,Isaka na Yakobo...
Asante kwa wema na fadhili zako kwetu
Asante kwa ulinzi wako kwetu wakati wote
Asante kwa kutuchagua tena na kutupa
kibali cha kuendelea kuiona leo hii
Asante kwa pumzi/uzima,afya na kuwatayari kwa majukumu yetu

Neema yako yatutosha ee Mungu wetu....!!

Walipokwisha amua tusafiri mpaka Italia, walimweka Paulo pamoja na wafungwa wengine chini ya ulinzi wa Yulio aliyekuwa ofisa wa jeshi katika kikosi kiitwacho “Kikosi cha Augusto.”
Baba wa Mbinguni tunakuja mbele zako,
Tukijinyenyekeza,tukijiachilia mikononi mwako
Mungu wetu tunamomba utusamehe dhambi zetu
Baba wa Mbinguni nasi tunaomba ukatupe neema
 ya kuweza kuwasamehe wale wote waliotukosea

Usitutie majaribuni Mungu wetu tunaomba utuepushe
na yule mwovu na kazi zake zote
Jehovah ututakase miili yetu na akili zetu
Baba wa Mbinguni tunaomba utufunike kwa Damu
ya Bwana na Mwokozi wetu Yesu Kristo wa Nazareti
yeye aliteseka kwanza ili sisi tupate kupona....

Tulipanda meli ya Adiramito iliyokuwa inasafiri na kupitia bandari kadhaa za mkoa wa Asia, tukaanza safari. Aristarko, mwenyeji wa Makedonia kutoka Thesalonike, alikuwa pamoja nasi.
Mungu wetu tunaomba ukabariki kazi za mikono yetu
Baba wa Mbinguni tunaomba ukatupe ubunifu na maarifa katika utendaji
Jehovah nasi tukatende sawasawa na mapenzi yako
Yahweh tunaomba ukabariki ridhiki zetu ziingiazo/zitokazo
Mungu wetu nasi tunaomna ukatupe neema ya kuweza kuwabariki wenye kuhitaji
Tusipungukiwe katika mahitaji yetu
Baba wa Mbinguni tunaomba ukatupe kama inavyokupendeza wewe...


Yahweh tunayaweka maisha yetu mikononi mwako
Mungu wetu tunaomba ukabariki nyumba/ndoa zetu,
Jehovah tunaomba ulinzi wako kwetu na kwa vyote tunavyovimiliki
Yahweh tunaomba ukatubariki tuingiapo/tutokapo
Mungu wetu tunaomba ukavibariki vyote tunavyoenda kugusa/kutumia
Baba wa Mbinguni ukavitakase kwa Damu ya Bwana wetu Yesu Kristo
Mungu wetu ukatamalaki na kutuatamia
Baba wa Mbinguni tukawe salama rohoni
Yahwe ukatupe akili ya kutambua mema na mabaya
Mfalme wa amani amani yako ikatawale katika maisha yetu
Mungu wetu ukatupe macho ya kuona,masikio ya kusikia sauti yako na kuitii..
Baba wa Mbinguni  tunaomba ukatupe neema ya kufuata
njia zako,tukasimamie Neno lako,amri na sheria zako
siku zote za maisha yetu...
Ukatuguse kwa mkono wako wenye nguvu,ukatufanye chombo chema
ee Mungu wetu nasi tukatumike kama inavyokupendeza wewe
Roho Mtakatifu akatuongoze katika yote na tukawe na kiasi....

Kesho yake tulitia nanga katika bandari ya Sidoni. Yulio alimtendea Paulo vizuri kwa kumruhusu awaone rafiki zake na kupata mahitaji yake.
Tazama watoto wako wenye shida/tabu,wote wanaopitia magumu/majaribu mbalimbali
Mungu wetu tunaomba ukawaguse kwa mkono wako wenye nguvu
kila mmoja na mahitaji yake
Mungu wetu tunaomba ukawasamehe pale walipo kwenda kinyume nawe
Yahweh tunaomba ukawape neema ya kuweza kujiombea,kufuata njia zako nazo zikawaweke huru...
Baba wa Mbinguni tunayaweka haya yote mikononi mwako
Kwakuwa Ufalme ni wako Nguvu na Utukufu hata Milele...
Amina...!!


Asanteni sana wapendwa katika Kristo Yesu kwakuwa nami,Baba wa Mbinguni aendelee kuwatendea sawasawa na mapenzi yake...

Nawapenda.

Adhabu kwa sababu ya kujiamini
1Ole wenu nyinyi mnaostarehe huko Siyoni,
nanyi mnaojiona salama mlimani Samaria!
Nyinyi mwaonekana kuwa viongozi wa taifa maarufu
ambao Waisraeli wote huwategemea.
2Haya! Nendeni Kalne mkaangalie kila mahali,
tokeni huko mwende hadi mji ule mkubwa wa Hamathi,
kisha teremkeni hadi Gathi kwa Wafilisti.
Je, falme zao si bora kuliko zenu
na eneo lao si bora kuliko lenu?”
3Nyinyi mnajaribu kuifukuza siku mbaya.
Lakini mnauleta karibu utawala dhalimu.
4Ole wenu mnaolala juu ya vitanda vya pembe za ndovu
na kujinyosha juu ya masofa,
mkila nyama za wanakondoo na ndama!
5Nyinyi mnapenda kuimba ovyo na sauti ya vinubi
na kubuni ala mpya za muziki mkimwiga mfalme Daudi.
6Mnakunywa divai kwa mabakuli,
na kujipaka marashi mazuri mno.
Lakini hamhuzuniki hata kidogo
juu ya kuangamia kwa wazawa wa Yosefu.
7Kwa hiyo mtakuwa wa kwanza kwenda uhamishoni,
na karamu za wenye kustarehe zitatoweka.
8Bwana Mwenyezi-Mungu ameapa kwa nafsi yake;
Mwenyezi-Mungu, Mungu wa majeshi asema:
“Nachukizwa mno na kiburi cha wazawa wa Yakobo;
tena nayachukia majumba yao ya fahari.
Mji wao na vyote vilivyomo nitawapa adui zao.”
9Kama wakibaki watu kumi katika nyumba moja, wote watakufa. 10Na atakapokuja mjomba wa aliyekufa kuitoa maiti nje aichome, akamwuliza yeyote atakayekuwako ndani pembeni mwa nyumba, “Je kuna mtu mwingine pamoja nawe?” Naye atamjibu, “La! Hamna!” Naye atamwambia, “Nyamaza kimya! Tusilitaje hata jina la Mwenyezi-Mungu.”6:10 maana ya aya hii katika Kiebrania si dhahiri.
11Tazama! Mwenyezi-Mungu anatoa amri,
nalo jumba kubwa labomoka vipandevipande,
na nyumba ndogo kusagikasagika.
12Je, farasi waweza kupiga mbio miambani?
Je, watu huilima bahari kwa ng'ombe?
Lakini nyinyi mmeigeuza haki kuwa sumu,
na tunda la uadilifu kuwa uchungu.
13Nyinyi mnashangilia juu ya Lodebari,6:13 Lodebari: Matumizi ya jina hili katika Kiebrania ni kama neno lenye maana “kitu batili” au “upuuzi.”
na kusema mmeuteka Karnaimu6:13 Karnaimu: Maana ya jina la mji huu mdogo ni “pembe” nazo ni alama ya nguvu. kwa nguvu zenu wenyewe.
14Mwenyezi-Mungu wa majeshi asema hivi:
“Enyi Waisraeli,
kweli nitaleta taifa moja lije kuwashambulia,
nalo litawatesa nyinyi kuanzia Lebo-hamathi kaskazini,
hadi kijito cha Araba, upande wa kusini.”

Amosi6;1-14

Biblia Habari Njema kwa Watu Wote(BHN)

"Swahili Na Waswahili"Mbarikiwe

Thursday 11 June 2020

Kikombe Cha Asubuhi; Amosi 5...

Shalom,Habari za Asubuhi,Hamjambo,Mmeamkaje?

Tumshukuru Mungu wetu katika yote...

Asante  Mungu wetu kwa wema na fadhili zako kwetu
Asante kwa ulinzi wako kwetu wakati wote
Asante kwa kutuchagua tena na kutupa
kibali cha kuendelea kuiona leo hii
Asante kwa pumzi/uzima,afya na kuwatayari kwa majukumu yetu


Utukuzwe ee Mungu wetu,usifiwe Baba wa Mbinguni

Neema yako yatutosha  Mungu wetu..!

Kijana msichana aweza kusahau mapambo yake au bibi arusi mavazi yake? Lakini watu wangu wamenisahau kwa muda wa siku zisizohesabika. Kweli wewe ni bingwa wa kutafuta wapenzi! Hata wanawake wabaya huwafundisha njia zako.
Baba wa Mbinguni tunakuja mbele zako tukijinyenyekeza,
tukijishusha na kujiachilia mikononi mwako

Mungu wetu tunaomba utusamehe dhambi zetu zote
Baba wa Mbinguni nasi tunaomba utupe neema ya kuweza kuwasamehe wale wote waliotukosea,Usitutie majaribuni Mungu wetu tunaomba utuepushe na yule mwovu na kazi zake zote,Jehovah ututakase miili yetu na akili zetu Baba wa Mbinguni tunaomba utufunike kwa  Damu ya Bwana na Mwokozi wetu Yesu Kristo wa Nazareti,
Yeye aliteseka kwanza ili sisi tupate kupona....

Nguo zako zina damu ya maskini wasio na hatia, japo hukuwakuta wakivunja nyumba yako. “Lakini licha ya hayo yote, wewe wasema: ‘Mimi sina hatia; hakika hasira yake imegeuka mbali nami.’ Lakini mimi nitakuhukumu kwa sababu unasema: ‘Sikutenda dhambi.’
Mungu wetu tunaomba ukabariki kazi za mikono yetu
Baba wa Mbinguni tunaomba ukatupe ubunifu na maarifa 
katika utendaji
Jehovah nasi tukatende sawasawa na mapenzi yako
Baba wa Mbinguni tunaomba ukabariki ridhiki zetu
ziingiazo/zitokazo
Mungu wetu nasi tunaomba ukatupe neema ya kuweza
kuwabariki wenye kuhitaji
Yahweh tusipungukiwe katika mahitaji yetu
Mungu wetu ukatupe kama inavyokupendeza wewe



Jehovah tunayaweka maisha yetu mikononi mwako
Baba wa Mbinguni tunaomba ukabariki nyumba/ndoa zetu,
watoto,wazazi wetu,familia/ndugu na wote wanaotuzunguka
Jehovah tunaomba ulinzi wako kwetu na kwa vyote tunavyo vimiliki
Yahweh tunaomba ukatubariki tuingiapo/tutokapo
Mungu wetu tunaomba ukavibariki vyote tunavyoenda kugusa/kutumia
Baba wa Mbinguni ukavitakase kwa Damu ya Bwana wetu Yesu Kristo
Mungu wetu ukatamalaki na kutuatamia
Baba wa Mbinguni tukawe salama rohoni
Mfalme wa amani amani yako ikatawale katika maisha yetu
Mungu wetu ukatupe macho ya kuona na masikio ya kusikia 
sauti yako na kuitii
Baba wa Mbinguni tunaomba ukatupe neema ya kufuata njia zako
Yahweh tukasimamie Neno lako amri na sheria zako siku zote 
za maisha yetu

Mungu  wetu ukaonekane katika maisha yetu popote tupitapo na ikajulikane kwamba upo 

Neema zako zikawe nasi Nuru yako ikaangaze katika maisha yetu
Ukatufanye barua njema ee Mungu wetu nasi tukasomeke kama
inavyokupendeza wewe
Roho Mtakatifu akatuongoze katika yote na tukawe na kiasi...

Kwa nini unajirahisisha hivi, ukibadilibadili mwenendo wako? Utaaibishwa na Misri, kama ulivyoaibishwa na Ashuru. Na huko pia utatoka, mikono kichwani kwa aibu. Mimi Mwenyezi-Mungu nimewakataa wale uliowategemea, wala hutafanikiwa kwa msaada wao.
Tazama wenye shida/tabu,Mungu wetu tunaomba
 ukawaguse kila mmoja na mahitaji yake
Baba wa Mbinguni tunaomba ukawasamehe pale walipokwenda
kinyume nawe
Mungu wetu ukawape neema ya kujiombea,macho ya rohoni,masikio yakusikia sauti yako,wakafuate njia zako nazo zikawaweke huru
Mungu wetu tunaomba ukasikie kulia kwao
Baba wa Mbinguni tunomba ukawafute machozi yao
Nuru yako ikaangaze katika maisha yao
Mungu wetu tunaomba ukawatendee sawasawa na mapenzi yako
Kwakuwa Ufalme ni wako Nguvu na Utukufu hata Milele
Amina....!!!


Wapendwa katika Kristo Yesu asanteni sana
kwakuwanami/kunisoma

Mungu Baba aendelee kuwabariki na kuwatendea
kama inavyompendeza yeye
Amani ya Bwana wetu Yesu Kristo na upendo wa Mungu Baba
ukae nanyi daima....

Nawapenda.

Maombolezo ya Amosi
1Sikilizeni maombolezo yangu juu yenu,
enyi Waisraeli:
2Umeanguka na hutainuka tena
ewe binti Israeli!
Umeachwa pweke nchini mwako,
hamna hata mtu wa kukuinua.
3Maana Bwana Mwenyezi-Mungu asema hivi:
“Watu 1,000 watatoka mjini kwenda kupigana
lakini watarejea 100 tu;
wataondoka watu 100 wa kijiji kimoja
lakini watanusurika watu kumi tu.”
4Mwenyezi-Mungu awaambia hivi Waisraeli:
“Nitafuteni mimi nanyi mtaishi!
5Lakini msinitafute huko Betheli
wala msiende Gilgali
wala msivuke kwenda Beer-sheba.
Maana wakazi wa Gilgali,
hakika watachukuliwa uhamishoni,
na Betheli utaangamizwa!”
6Mtafuteni Mwenyezi-Mungu, nanyi mtaishi!
La sivyo, atawalipukia wazawa wa Yosefu kama moto;
moto utawateketeza wakazi wa Betheli
na hakuna mtu atakayeweza kuuzima.
7Tahadhari enyi mnaogeuza haki kuwa uchungu,
na kuuona uadilifu kuwa kama takataka!
8Huyo aliyezifanya Kilimia na sayari Orioni,
ambaye huligeuza giza nene kuwa mchana,
na mchana kuwa usiku;
yeye ambaye ayaitaye pamoja maji ya bahari
na kuyamwaga juu ya nchi kavu,
Mwenyezi-Mungu ndilo jina lake.
9Yeye ndiye anayewaangamiza wenye nguvu,
na kuziharibu ngome zao.
10Nyinyi huwachukia watetezi wa haki
na wenye kusema ukweli mahakamani.
11Nyinyi mnawakandamiza fukara
na kuwatoza kodi ya ngano kupita kiasi.
Mnajijengea nyumba za mawe ya kuchonga,
lakini nyinyi hamtaishi humo;
mnalima bustani nzuri za mizabibu,
lakini hamtakunywa divai yake.
12Maana mimi najua wingi wa makosa yenu
na ukubwa wa dhambi zenu;
nyinyi mnawatesa watu wema,
mnapokea rushwa
na kuzuia fukara wasipate haki mahakamani.
13Basi, kutakuwa na wakati mbaya
ambao hata mwenye busara atanyamaza.
14Tafuteni kutenda mema na si mabaya,
ili nyinyi mpate kuishi
naye Mwenyezi-Mungu wa majeshi
awe pamoja nanyi kama mnavyosema.
15Chukieni uovu, pendeni wema,
na kudumisha haki mahakamani.
Yamkini Mwenyezi-Mungu wa majeshi atawafadhili watu wa Yosefu waliobaki.
16Basi, Mwenyezi-Mungu, Mungu wa majeshi,
naam, Mwenyezi-Mungu asema:
“Patakuwa na kilio kila mahali mitaani;
watu wataomboleza: ‘Ole! Ole!’
Wakulima wataitwa waje kuomboleza,
na mabingwa wa kuomboleza waje kufanya matanga.
17Patakuwa na kilio katika mashamba yote ya mizabibu;
maana nitapita kati yenu kuwaadhibu.
Nasema mimi Mwenyezi-Mungu.”
Siku ya Mwenyezi-Mungu
18Ole wenu nyinyi mnaoingojea kwa hamu
siku ya Mwenyezi-Mungu!
Kwa nini mnaitaka sana siku hiyo?
Siku hiyo, itakuwa siku ya giza na sio ya mwanga!
19Mambo yatakuwa kama mtu aliyekimbia simba,
halafu akakumbana na dubu!
Au kama mtu anayerudi nyumbani kwake,
akatia mkono ukutani, akaumwa na nyoka.
20Siku ya Mwenyezi-Mungu itakuwa giza, na sio mwanga;
itakuwa huzuni bila uangavu wowote.
21Mwenyezi-Mungu asema hivi:
“Nazichukia na kuzidharau sikukuu zenu;
siifurahii mikutano yenu ya kidini.
22Mjaponitolea sadaka zenu za kuteketezwa na za nafaka,
mimi sitakubali kuzipokea;
na sadaka zenu za amani za wanyama wanono
mimi sitaziangalia kabisa.
23Ondoeni mbele yangu kelele za nyimbo zenu!
Sitaki kusikiliza muziki wa vinubi vyenu!
24Lakini acheni haki itiririke kama maji,
uadilifu uwe kama mto usiokauka.
25“Enyi Waisraeli, wakati ule mlipokuwa kule jangwani kwa miaka arubaini, je, mliniletea tambiko na sadaka hata mara moja? 26Je, wakati huo mlibeba kama sasa vinyago vya mungu wenu Sakuthi mfalme wenu na vinyago vya Kaiwani mungu wenu wa nyota, vitu ambavyo mlijitengenezea wenyewe? 27Kwa hiyo nitawapeleka uhamishoni, mbali kuliko Damasko! Hayo amesema Mwenyezi-Mungu, ambaye jina lake ni Mungu wa Majeshi.

Amosi5;1-27

Biblia Habari Njema kwa Watu Wote(BHN)

"Swahili Na Waswahili"Mbarikiwe

Wednesday 10 June 2020

Kikombe Cha Asubuhi; Amosi 4...

Shalom,Habari za Asubuhi,Hamjambo,Mmeamkaje?

Tumshukuru Mungu katika yote....

Mungu wetu Baba yetu,Muumba wetu Muumba wa Mbingu na Nchi
Muumba wa vyote vilivyomo vinavyoonekana na visivyoonekana
Mungu wa walio hai,Mungu  mwenye huruma,Mungu wa upendo
Mungu wa Abrahamu,Isaka na Yakobo...
Asante kwa wema na fadhili zako kwetu
Asante kwa ulinzi wako kwetu wakati wote
Asante kwa kutuchagua tena na kutupa
kibali cha kuendelea kuiona leo hii
Asante kwa pumzi/uzima,afya na kuwatayari kwa majukumu yetu

Neema yako yatutosha ee Mungu wetu....!!

Mbona mnanilalamikia? Nyinyi nyote mmeniasi. Mimi Mwenyezi-Mungu nimesema.
Baba wa Mbinguni tunakuja mbele zako,
Tukijinyenyekeza,tukijiachilia mikononi mwako
Mungu wetu tunamomba utusamehe dhambi zetu
Baba wa Mbinguni nasi tunaomba ukatupe neema
 ya kuweza kuwasamehe wale wote waliotukosea

Usitutie majaribuni Mungu wetu tunaomba utuepushe
na yule mwovu na kazi zake zote
Jehovah ututakase miili yetu na akili zetu
Baba wa Mbinguni tunaomba utufunike kwa Damu
ya Bwana na Mwokozi wetu Yesu Kristo wa Nazareti
yeye aliteseka kwanza ili sisi tupate kupona....

Niliwaadhibu watu wako bila kufanikiwa, wao wenyewe walikataa kukosolewa. Upanga wako uliwamaliza manabii wako kama simba mwenye uchu.
Mungu wetu tunaomba ukabariki kazi za mikono yetu
Baba wa Mbinguni tunaomba ukatupe ubunifu na maarifa katika utendaji
Jehovah nasi tukatende sawasawa na mapenzi yako
Yahweh tunaomba ukabariki ridhiki zetu ziingiazo/zitokazo
Mungu wetu nasi tunaomna ukatupe neema ya kuweza kuwabariki wenye kuhitaji
Tusipungukiwe katika mahitaji yetu
Baba wa Mbinguni tunaomba ukatupe kama inavyokupendeza wewe...


Yahweh tunayaweka maisha yetu mikononi mwako
Mungu wetu tunaomba ukabariki nyumba/ndoa zetu,
Jehovah tunaomba ulinzi wako kwetu na kwa vyote tunavyovimiliki
Yahweh tunaomba ukatubariki tuingiapo/tutokapo
Mungu wetu tunaomba ukavibariki vyote tunavyoenda kugusa/kutumia
Baba wa Mbinguni ukavitakase kwa Damu ya Bwana wetu Yesu Kristo
Mungu wetu ukatamalaki na kutuatamia
Baba wa Mbinguni tukawe salama rohoni
Yahwe ukatupe akili ya kutambua mema na mabaya
Mfalme wa amani amani yako ikatawale katika maisha yetu
Mungu wetu ukatupe macho ya kuona,masikio ya kusikia sauti yako na kuitii..
Baba wa Mbinguni  tunaomba ukatupe neema ya kufuata
njia zako,tukasimamie Neno lako,amri na sheria zako
siku zote za maisha yetu...
Ukatuguse kwa mkono wako wenye nguvu,ukatufanye chombo chema
ee Mungu wetu nasi tukatumike kama inavyokupendeza wewe
Roho Mtakatifu akatuongoze katika yote na tukawe na kiasi....

Enyi watu! Sikilizeni ninachosema mimi Mwenyezi-Mungu: Je, nimekuwa jangwa kwa Israeli au nchi yenye giza nene? Kwa nini basi watu wangu waseme: ‘Sisi tu watu huru; hatutakuja kwako tena!’
Tazama watoto wako wenye shida/tabu,wote wanaopitia magumu/majaribu mbalimbali
Mungu wetu tunaomba ukawaguse kwa mkono wako wenye nguvu
kila mmoja na mahitaji yake
Mungu wetu tunaomba ukawasamehe pale walipo kwenda kinyume nawe
Yahweh tunaomba ukawape neema ya kuweza kujiombea,kufuata njia zako nazo zikawaweke huru...
Baba wa Mbinguni tunayaweka haya yote mikononi mwako
Kwakuwa Ufalme ni wako Nguvu na Utukufu hata Milele...
Amina...!!


Asanteni sana wapendwa katika Kristo Yesu kwakuwa nami,Baba wa Mbinguni aendelee kuwatendea sawasawa na mapenzi yake...

Nawapenda.

1Sikilizeni neno hili,
enyi wanawake ng'ombe wa Bashani
mlioko huko mlimani Samaria;
nyinyi mnaowaonea wanyonge,
mnaowakandamiza maskini,
na kuwaambia waume zenu:4:1 zenu: Au zao.
“Tuleteeni divai tunywe!”
Sikilizeni ujumbe huu:
2Mimi Bwana Mwenyezi-Mungu Mtakatifu nimeapa:
“Tazama, siku zaja,
ambapo watu watawakokoteni kwa kulabu,
kila mmoja wenu kama samaki kwenye ndoana.
3Mtaburutwa hadi ukutani palipobomolewa,
na kutupwa nje.4:3 katika Kiebrania pameongezwa neno hapa ambalo maana yake si dhahiri.
Nasema mimi Mwenyezi-Mungu.
Israeli haijajirekebisha bado
4“Enyi Waisraeli,
nendeni basi huko Betheli mkaniasi!
Nendeni Gilgali mkalimbikize makosa yenu!
Toeni sadaka zenu kila asubuhi,
na zaka zenu kila siku ya tatu.
5Toeni tambiko ya shukrani ya mikate iliyochachushwa.
Tangazeni popote kwamba mmetoa kwa hiari;
kwani ndivyo mnavyopenda kufanya!
Mimi Bwana Mungu nimenena.
6“Mimi niliwanyima chochote cha kutafuna,
nikasababisha ukosefu wa chakula popote.
Hata hivyo hamkunirudia.
Nasema mimi Mwenyezi-Mungu.
7“Tena niliwanyima mvua
miezi mitatu tu kabla ya mavuno.
Niliunyeshea mvua mji mmoja,
na mji mwingine nikaunyima.
Shamba moja lilipata mvua,
na lingine halikupata, likakauka.
8Watu wa miji miwili, mitatu wakakimbilia mji mwingine,
wapate maji, lakini hayakuwatosha.
Hata hivyo hamkunirudia.
Nasema mimi Mwenyezi-Mungu.
9“Niliwapiga pigo la ukame na ukungu;
nikakausha bustani na mashamba yenu ya mizabibu;
nzige wakala mitini na mizeituni yenu.
Hata hivyo hamkunirudia.
Nasema mimi Mwenyezi-Mungu.
10“Niliwaleteeni ugonjwa wa tauni
kama ule nilioupelekea Misri.
Niliwaua vijana wenu vitani,
nikawachukua farasi wenu wa vita.
Maiti zilijaa katika kambi zenu,
uvundo wake ukajaa katika pua zenu.
Hata hivyo hamkunirudia.
Nasema mimi Mwenyezi-Mungu.
11“Niliwaangusha baadhi yenu kwa maangamizi
kama nilivyoangamiza Sodoma na Gomora.
Wale walionusurika miongoni mwenu,
walikuwa kama kijiti kilichookolewa motoni.
Hata hivyo hamkunirudia.
Nasema mimi Mwenyezi-Mungu.
12“Kwa hiyo, enyi Waisraeli, nitawaadhibu.
Na kwa kuwa nitafanya jambo hilo,
kaeni tayari kuikabili hukumu yangu!”
13Mungu ndiye aliyeifanya milima,
na kuumba upepo;
ndiye amjulishaye mwanadamu mawazo yake;
ndiye ageuzaye mchana kuwa usiku,
na kukanyaga vilele vya dunia.
Mwenyezi-Mungu wa Majeshi ndilo jina lake!

Amosi4;1-13

Biblia Habari Njema kwa Watu Wote(BHN)

"Swahili Na Waswahili"Mbarikiwe

Tuesday 9 June 2020

Kikombe Cha Asubuhi; Amosi 3...

Shalom,Habari za Asubuhi,Hamjambo,Mmeamkaje?

Tumshukuru Mungu wetu katika yote...

Asante  Mungu wetu kwa wema na fadhili zako kwetu
Asante kwa ulinzi wako kwetu wakati wote
Asante kwa kutuchagua tena na kutupa
kibali cha kuendelea kuiona leo hii
Asante kwa pumzi/uzima,afya na kuwatayari kwa majukumu yetu


Utukuzwe ee Mungu wetu,usifiwe Baba wa Mbinguni

Neema yako yatutosha  Mungu wetu..!

“Kama vile mwizi aonavyo aibu akishikwa, ndivyo Waisraeli watakavyoona aibu; wao wenyewe, wafalme wao, wakuu wao, makuhani wao na manabii wao.
Baba wa Mbinguni tunakuja mbele zako tukijinyenyekeza,
tukijishusha na kujiachilia mikononi mwako

Mungu wetu tunaomba utusamehe dhambi zetu zote
Baba wa Mbinguni nasi tunaomba utupe neema ya kuweza kuwasamehe wale wote waliotukosea,Usitutie majaribuni Mungu wetu tunaomba utuepushe na yule mwovu na kazi zake zote,Jehovah ututakase miili yetu na akili zetu Baba wa Mbinguni tunaomba utufunike kwa  Damu ya Bwana na Mwokozi wetu Yesu Kristo wa Nazareti,
Yeye aliteseka kwanza ili sisi tupate kupona....

Hao huuambia mti: ‘Wewe u baba yangu,’ na jiwe: ‘Wewe ndiwe uliyenizaa;’ kwa maana wamenipa kisogo, wala hawakunielekezea nyuso zao. Lakini wakati wa shida husema: ‘Inuka utuokoe!’
Mungu wetu tunaomba ukabariki kazi za mikono yetu
Baba wa Mbinguni tunaomba ukatupe ubunifu na maarifa 
katika utendaji
Jehovah nasi tukatende sawasawa na mapenzi yako
Baba wa Mbinguni tunaomba ukabariki ridhiki zetu
ziingiazo/zitokazo
Mungu wetu nasi tunaomba ukatupe neema ya kuweza
kuwabariki wenye kuhitaji
Yahweh tusipungukiwe katika mahitaji yetu
Mungu wetu ukatupe kama inavyokupendeza wewe



Jehovah tunayaweka maisha yetu mikononi mwako
Baba wa Mbinguni tunaomba ukabariki nyumba/ndoa zetu,
watoto,wazazi wetu,familia/ndugu na wote wanaotuzunguka
Jehovah tunaomba ulinzi wako kwetu na kwa vyote tunavyo vimiliki
Yahweh tunaomba ukatubariki tuingiapo/tutokapo
Mungu wetu tunaomba ukavibariki vyote tunavyoenda kugusa/kutumia
Baba wa Mbinguni ukavitakase kwa Damu ya Bwana wetu Yesu Kristo
Mungu wetu ukatamalaki na kutuatamia
Baba wa Mbinguni tukawe salama rohoni
Mfalme wa amani amani yako ikatawale katika maisha yetu
Mungu wetu ukatupe macho ya kuona na masikio ya kusikia 
sauti yako na kuitii
Baba wa Mbinguni tunaomba ukatupe neema ya kufuata njia zako
Yahweh tukasimamie Neno lako amri na sheria zako siku zote 
za maisha yetu

Mungu  wetu ukaonekane katika maisha yetu popote tupitapo na ikajulikane kwamba upo 

Neema zako zikawe nasi Nuru yako ikaangaze katika maisha yetu
Ukatufanye barua njema ee Mungu wetu nasi tukasomeke kama
inavyokupendeza wewe
Roho Mtakatifu akatuongoze katika yote na tukawe na kiasi...

“Lakini iko wapi miungu yako uliyojifanyia? Iinuke basi, kama inaweza kukusaidia, wakati unapokuwa katika shida. Ee Yuda, idadi ya miungu yako ni sawa na idadi ya miji yako!
Tazama wenye shida/tabu,Mungu wetu tunaomba
 ukawaguse kila mmoja na mahitaji yake
Baba wa Mbinguni tunaomba ukawasamehe pale walipokwenda
kinyume nawe
Mungu wetu ukawape neema ya kujiombea,macho ya rohoni,masikio yakusikia sauti yako,wakafuate njia zako nazo zikawaweke huru
Mungu wetu tunaomba ukasikie kulia kwao
Baba wa Mbinguni tunomba ukawafute machozi yao
Nuru yako ikaangaze katika maisha yao
Mungu wetu tunaomba ukawatendee sawasawa na mapenzi yako
Kwakuwa Ufalme ni wako Nguvu na Utukufu hata Milele
Amina....!!!


Wapendwa katika Kristo Yesu asanteni sana
kwakuwanami/kunisoma

Mungu Baba aendelee kuwabariki na kuwatendea
kama inavyompendeza yeye
Amani ya Bwana wetu Yesu Kristo na upendo wa Mungu Baba
ukae nanyi daima....

Nawapenda.

1Enyi Waisraeli, sikilizeni neno Mwenyezi-Mungu alilosema dhidi yenu, enyi taifa zima alilolitoa nchini Misri:
2“Kati ya mataifa yote ulimwenguni,
ni nyinyi tu niliowachagua.
Kwa hiyo nitawaadhibu nyinyi,
kwa sababu ya uovu wenu wote.”
Jukumu la nabii
3Je, watu wawili huanza safari pamoja,
bila ya kufanya mpango pamoja kwanza?
4Je, simba hunguruma porini
kama hajapata mawindo?
Je, mwanasimba hunguruma pangoni mwake
kama hajakamata kitu?
5Je, mtego bila chambo
utamnasa ndege?
Je, mtego hufyatuka
bila kuguswa na kitu?
6Je, baragumu ya vita hulia mjini
bila kutia watu hofu?
Je, mji hupatwa na janga
asilolileta Mungu?
7Hakika, Bwana Mwenyezi-Mungu hafanyi kitu
bila kuwafunulia watumishi wake manabii nia yake.
8Simba akinguruma,
ni nani asiyeogopa?
Bwana Mwenyezi-Mungu akinena,
ni nani atakataa kuutangaza ujumbe wake?
Kuangamizwa kwa Samaria
9Tangazeni katika ikulu za Ashdodi,
na katika ikulu za nchi ya Misri:
“Kusanyikeni kwenye milima
inayoizunguka nchi ya Samaria,
mkajionee msukosuko mkubwa
na dhuluma zinazofanyika humo.”
10Mwenyezi-Mungu asema hivi:
“Watu hawa wameyajaza majumba yao
vitu vya wizi na unyang'anyi.
Hawajui kabisa kutenda yaliyo sawa!
11Kwa hiyo, adui ataizingira nchi yao,
atapaharibu mahali pao pa kujihami,
na kuziteka nyara ikulu zao.”
12Mwenyezi-Mungu, asema hivi: “Kama vile mchungaji ampokonyavyo simba kinywani miguu miwili tu au kipande cha sikio la kondoo, ndivyo watakavyonusurika watu wachache tu wa Israeli wakaao Samaria, ambao sasa wanalalia vitanda vizuri na matandiko ya hariri.”3:12 vitanda vizuri na matandiko ya hariri: Maana katika Kiebrania si dhahiri.
13Bwana Mungu wa majeshi asema hivi:
“Sikilizeni, mkawaonye wazawa wa Yakobo:
14Siku nitakapowaadhibu Waisraeli
kwa sababu ya makosa yao,
nitayaharibu pia madhabahu ya mji wa Betheli.
Nitazikata pembe3:14 pembe: Hizi zilikuwa alama ya usalama.za kila madhabahu
na kuziangusha chini.
15Nitaziharibu nyumba zote mjini na vijijini;
nitazibomoa nyumba zilizopambwa kwa pembe,
majumba makubwamakubwa hayatasalia hata moja.
Mimi Mwenyezi-Mungu nimesema.”


Amosi3;1-15

Biblia Habari Njema kwa Watu Wote(BHN)

"Swahili Na Waswahili"Mbarikiwe