Swahili na Waswahili

Swahili na Waswahili
Waswahili na Mswahili Rachel Siwa...Pamoja Daima!!

Tuesday 17 December 2019

Kikombe Cha Asubuhi; Yeremia 12....


Shalom,Habari za Asubuhi,Hamjambo,Mmeamkaje?

Tumshukuru Mungu wetu katika yote...

Asante  Mungu wetu kwa wema na fadhili zako kwetu
Asante kwa ulinzi wako kwetu wakati wote
Asante kwa kutuchagua tena na kutupa
kibali cha kuendelea kuiona leo hii
Asante kwa pumzi/uzima,afya na kuwatayari kwa majukumu yetu



Utukuzwe ee Mungu wetu,usifiwe Baba wa Mbinguni

Neema yako yatutosha  Mungu wetu..!

“Na sasa basi, ninawaweka nyinyi chini ya ulinzi wa Mungu na ujumbe wa neema yake. Yeye anao uwezo wa kuwajenga na kuwawezesha mzipate zile baraka alizowawekea watu wake. Mimi sikutamani hata mara moja fedha, wala dhahabu, wala nguo za mtu yeyote.
Baba wa Mbinguni tunakuja mbele zako tukijinyenyekeza,
tukijishusha na kujiachilia mikononi mwako

Mungu wetu tunaomba utusamehe dhambi zetu zote
Baba wa Mbinguni nasi tunaomba utupe neema ya kuweza kuwasamehe wale wote waliotukosea,Usitutie majaribuni Mungu wetu tunaomba utuepushe na yule mwovu na kazi zake zote,Jehovah ututakase miili yetu na akili zetu Baba wa Mbinguni tunaomba utufunike kwa  Damu ya Bwana na Mwokozi wetu Yesu Kristo wa Nazareti,
Yeye aliteseka kwanza ili sisi tupate kupona....

Mnajua nyinyi wenyewe kwamba nimefanya kazi kwa mikono yangu mwenyewe, ili kujipatia mahitaji yangu na ya wenzangu. Nimekuwa nikiwapeni daima mfano kwamba kwa kufanya kazi mithili hiyo tunapaswa kuwasaidia walio dhaifu, tukikumbuka maneno ya Bwana Yesu mwenyewe: ‘Heri zaidi kutoa kuliko kupokea.’”
Mungu wetu tunaomba ukabariki kazi za mikono yetu
Baba wa Mbinguni tunaomba ukatupe ubunifu na maarifa 
katika utendaji
Jehovah nasi tukatende sawasawa na mapenzi yako
Baba wa Mbinguni tunaomba ukabariki ridhiki zetu
ziingiazo/zitokazo
Mungu wetu nasi tunaomba ukatupe neema ya kuweza
kuwabariki wenye kuhitaji
Yahweh tusipungukiwe katika mahitaji yetu
Mungu wetu ukatupe kama inavyokupendeza wewe



Jehovah tunayaweka maisha yetu mikononi mwako
Baba wa Mbinguni tunaomba ukabariki nyumba/ndoa zetu,
watoto,wazazi wetu,familia/ndugu na wote wanaotuzunguka
Jehovah tunaomba ulinzi wako kwetu na kwa vyote tunavyo vimiliki
Yahweh tunaomba ukatubariki tuingiapo/tutokapo
Mungu wetu tunaomba ukavibariki vyote tunavyoenda kugusa/kutumia
Baba wa Mbinguni ukavitakase kwa Damu ya Bwana wetu Yesu Kristo
Mungu wetu ukatamalaki na kutuatamia
Baba wa Mbinguni tukawe salama rohoni
Mfalme wa amani amani yako ikatawale katika maisha yetu
Mungu wetu ukatupe macho ya kuona na masikio ya kusikia 
sauti yako na kuitii
Baba wa Mbinguni tunaomba ukatupe neema ya kufuata njia zako
Yahweh tukasimamie Neno lako amri na sheria zako siku zote 
za maisha yetu

Mungu  wetu ukaonekane katika maisha yetu popote tupitapo na ikajulikane kwamba upo 

Neema zako zikawe nasi Nuru yako ikaangaze katika maisha yetu
Ukatufanye barua njema ee Mungu wetu nasi tukasomeke kama
inavyokupendeza wewe
Roho Mtakatifu akatuongoze katika yote na tukawe na kiasi...

Baada ya kusema hayo, Paulo alipiga magoti pamoja nao wote, akasali. Wote walikuwa wanalia, na kumwaga kwa kumkumbatia na kumbusu. Jambo lililowahuzunisha zaidi lilikuwa neno alilosema kwamba hawangemwona tena. Basi, wakamsindikiza hadi melini.
Tazama wenye shida/tabu,Mungu wetu tunaomba
 ukawaguse kila mmoja na mahitaji yake
Baba wa Mbinguni tunaomba ukawasamehe pale walipokwenda
kinyume nawe
Mungu wetu ukawape neema ya kujiombea,macho ya rohoni,masikio yakusikia sauti yako,wakafuate njia zako nazo zikawaweke huru
Mungu wetu tunaomba ukasikie kulia kwao
Baba wa Mbinguni tunomba ukawafute machozi yao
Nuru yako ikaangaze katika maisha yao
Mungu wetu tunaomba ukawatendee sawasawa na mapenzi yako
Kwakuwa Ufalme ni wako Nguvu na Utukufu hata Milele
Amina....!!!


Wapendwa katika Kristo Yesu asanteni sana
kwakuwanami/kunisoma

Mungu Baba aendelee kuwabariki na kuwatendea
kama inavyompendeza yeye
Amani ya Bwana wetu Yesu Kristo na upendo wa Mungu Baba
ukae nanyi daima....

Nawapenda.


Yeremia anamhoji Mwenyezi-Mungu
1Ee Mwenyezi-Mungu, wewe ni mwadilifu,
ingawa nakulalamikia.
Lakini ningependa kutoa hoja zangu mbele yako:
Kwa nini waovu hufanikiwa katika mambo yao?
Mbona wote wenye hila hustawi?
2Unawaotesha nao wanaota;
wanakua na kuzaa matunda.
Wanakutaja kwa maneno yao,
lakini mioyo yao iko mbali nawe.
3Lakini wewe ee Mwenyezi-Mungu wanijua;
wayathibiti maelekeo yangu kwako.
Uwaokote hao kama kondoo wa kuchinjwa,
watenge kwa ajili ya wakati wa kuuawa.
4Mpaka lini nchi itaomboleza kwa ukame,
na nyasi za mashamba yote kunyauka?
Wanyama na ndege wanakufa kwa uovu wa wakazi wake;
wanasema: “Mungu hataona mwisho wetu.”12:4 Kiebrania: Mwisho wetu; baadhi ya tafsiri nyingine: Yale tunayofanya.
5Mwenyezi-Mungu asema,
“Ikiwa umeshindana na waendao kwa miguu ukachoka,
utawezaje kushindana na farasi?
Kama unaanguka katika nchi isiyo na vizuizi,
utafanyaje katika msitu wa Yordani?
6Hata ndugu zako, jamaa yako mwenyewe,
nao pia wamekutendea mambo ya hila;
wanakukemea waziwazi.
Usiwaamini hata kidogo,
japo wanakuambia maneno mazuri.”
Mungu anaiacha nyumba yake na watu wake
7Mwenyezi-Mungu asema hivi:
“Nimeiacha nyumba yangu;
nimeitupa mali yangu mimi mwenyewe.
Israeli, mpenzi wangu wa moyo,
nimemtia mikononi mwa maadui zake.
8Wateule wangu wamenigeuka,
wamekuwa kama simba porini,
wameningurumia mimi;
ndiyo maana nawachukia.
9Wateule wangu wamekuwa ndege mzuri
wanaoshambuliwa na kozi pande zote.
Nenda ukawakusanye wanyama wote wakali
waje kushiriki katika karamu.
10Wachungaji wengi wameharibu shamba langu la mizabibu,
wamelikanyagakanyaga chini lililo mali yangu;
shamba langu zuri wamelifanya jangwa.
11Wamelifanya kuwa tupu;
katika ukiwa wake lanililia.
Nchi yote imekuwa jangwa,
wala hakuna mtu anayejali.
12Juu ya milima yote jangwani,
watu wamefika kuangamiza.
Upanga wangu unapita kuiangamiza nchi,
toka upande mmoja hadi mwingine,
wala hakuna mtu atakayeishi kwa amani.
13Walipanda ngano, lakini walivuna magugu;
walifanya bidii, lakini hawakupata kitu.
Kwa sababu ya hasira yangu kali,
mavuno watakayoyapata yatakuwa aibu tupu.”
Mungu na majirani wa Israeli
14Mwenyezi-Mungu asema hivi juu ya jirani wabaya wa watu wangu: “Wamekigusa kile kilicho changu, kile nilichowapa watu wangu Israeli! Basi nitawangoa kutoka katika nchi yao. Hata watu wa Yuda nitawangoa katika nchi yao. 15Lakini baada ya kuwangoa, nitawahurumia tena; nitalirudisha kila taifa katika sehemu yake na katika nchi yake. 16Na kama watajifunza njia za watu wangu kwa moyo wote, kama wataapa kwa jina langu kwa kusema, ‘Kama aishivyo Mwenyezi-Mungu,’ kama vile walivyowafundisha watu wangu kuapa kwa jina la mungu Baali, basi watajengeka miongoni mwa watu wangu. 17Lakini taifa lolote ambalo halitanitii, nitalingoa kabisa na kuliangamiza. Mimi Mwenyezi-Mungu nimesema.”



Yeremia12;1-17

Biblia Habari Njema kwa Watu Wote(BHN)

"Swahili Na Waswahili"Mbarikiwe.

Monday 16 December 2019

Kikombe Cha Asubuhi; Yeremia 11....


Shalom,Habari za Asubuhi,Hamjambo,Mmeamkaje?

Haleluyah ni siku/wiki
Nyingine tena Mungu wetu ametuchagua

na kutupa kibali cha kuendelea kuiona leo hii
Si kwamba sisi tumetenda mema sana wala si kwa nguvu zetu
si kwa utashi wetu wala si kwa akili zetu si kwamba sisi
ni wazuri mno si kwa uwezo wetu sisi kuwa hivi tulivyo leo hii
Ni kwa rehema/neema zake ni kwa mapenzi yake Mungu wetu....

Tumshukuru Mungu wetu katika yote...

Asante Mungu wetu kwa wema na fadhili zako kwetu

Asante kwa ulinzi wako kwetu wakati wote
Asante kwa pumzi/uzima,afya na kuwa tayari kwa majukumu yetu
Sifa na Utukufu tunakurudshia Mungu wetu....!!

“Nimepita miongoni mwenu nyote nikiuhubiri ufalme wa Mungu. Sasa lakini, najua hakuna hata mmoja wenu atakayeniona tena. Hivyo, leo hii ninawathibitishieni rasmi kwamba ikijatokea akapotea mmoja wenu, mimi sina lawama yoyote. Kwa maana sikusita hata kidogo kuwatangazieni azimio lote la Mungu.
Tazama jana imepita ee Mungu wetu leo ni siku mpya na kesho ni siku nyingine Jehovah tunakuja mbele zako tukijinyenyekeza,tukijishusha na kujiachilia mikononi mwako
 Mungu wetu tunaomba utusamehe dhambi zetu zote tulizozifanya kwakuwaza,kwakunena,kwakutenda,kwakujua/kutojua
Baba wa Mbinguni nasi tunaomba utupe neema ya kuweza kuwasamehe wale wote waliotukosea
Jehovah usitutie majaribu Mungu wetu tunaomba utuepushe na yule mwovu na kazi zake zote
Yahweh tunaomba ututakase miili yetu na akili zetu
Baba wa Mbinguni utufunike kwa Damu ya Bwana na Mwokozi wetu Yesu Kristo wa Nazareti
yeye aliteseka kwanza ili sisi tupate kupona
Kwakupigwa kwake sisi tumepata kupona....

Jihadharini wenyewe; lilindeni lile kundi ambalo Roho Mtakatifu amewaweka nyinyi muwe walezi wake. Lichungeni kanisa la Mungu ambalo amejipatia kwa damu ya Mwanae. Nafahamu vizuri sana kwamba baada ya kuondoka kwangu mbwamwitu wakali watawavamieni, na hawatakuwa na huruma kwa kundi hilo.
Yahweh tunaomba ukabariki kazi za mikono yetu
Baba wa Mbinguni tunaomba ukatupe ubunifu na maarifa 
katika utendaji
Jehovah nasi tukatende sawasawa na mapenzi yako
Baba wa Mbinguni tunaomba ukabariki ridhiki zetu
ziingiazo/zitokazo
Mungu wetu nasi tunaomba ukatupe neema ya kuweza
kuwabariki wenye kuhitaji
Yahweh tusipungukiwe katika mahitaji yetu
Mungu wetu ukatupe kama inavyokupendeza wewe

Baba wa Mbinguni tunayaweka maisha yetu mikononi mwako
Mungu wetu tunaomba ukabariki nyumba/ndoa zetu,
watoto,wazazi wetu,familia/ndugu na wote wanaotuzunguka
Jehovah tunaomba ulinzi wako kwetu na kwa vyote tunavyo vimiliki
Yahweh tunaomba ukatubariki tuingiapo/tutokapo
Mungu wetu tunaomba ukavibariki vyote tunavyoenda kugusa/kutumia
Baba wa Mbinguni ukavitakase kwa Damu ya Bwana wetu Yesu Kristo
Mungu wetu ukatamalaki na kutuatamia
Baba wa Mbinguni tukawe salama rohoni
Mfalme wa amani amani yako ikatawale katika maisha yetu
Mungu wetu ukatupe macho ya kuona na masikio ya kusikia 
sauti yako na kuitii
Baba wa Mbinguni tunaomba ukatupe neema ya kufuata njia zako
Yahweh tukasimamie Neno lako amri na sheria zako siku zote 
za maisha yetu
Mungu wetu ukaonekane katika maisha yetu
Neema zako zikawe nasi Nuru yako ikaangaze katika maisha yetu
ukatuguse kwa mkono wako wenye nguvu
Ukatufanye chombo chema ee Mungu wetu nasi tukatumike kama
inavyokupendeza wewe
Roho Mtakatifu akatuongoze katika yote na tukawe na kiasi...


Hata kutoka miongoni mwenu watatokea watu ambao watasema mambo ya uongo ili kuwapotosha watu na kuwafanya wawafuate wao tu. Kwa hiyo, muwe macho mkikumbuka kwamba kwa muda wa miaka mitatu, usiku na mchana, sikuchoka kumwonya kila mmoja wenu kwa machozi.
Mungu wetu tunawaweka mikononi mwako wenye shida/tabu,wote wanaopitia magumu/majaribu mbalimbali
Mungu wetu tunaomba ukawaguse kwa mkono wako wenye nguvu
 kila mmoja na mahitaji yake 
Mungu wetu tunaomba ukawasamehe pale walipokwenda kinyume nawe
Baba wa Mbinguni ukawape neema ya kujiombea,kufuata njia zako
wakasimamie Neno lako nalo likaweke huru
Mungu wetu tunaomba ukasikie kuomba kwetu
Mungu wetu ukawatendee sawasawa na mapenzi yako
Kwakuwa Ufalme ni wako Nguvu na Utukufu hata Milele
Amina...!!

Asanteni sana wapendwa katika Kristo Yesu kwakuwa nami
Mungu Baba aendelee kuwabariki na kuwatendea 
kama inavyompendeza yeye....
Nawapenda.


Yeremia na agano
1Neno lilimjia Yeremia kutoka kwa Mwenyezi-Mungu; 2“Sikiliza masharti ya agano hili, kisha nenda ukawatangazie watu wa Yuda na wakazi wa Yerusalemu. 3Utawaambia hivi: Mwenyezi-Mungu, Mungu wa Israeli, asema hivi: Na alaaniwe mtu yeyote asiyejali masharti ya agano hili. 4Hili ni agano nililowapa wazee wenu nilipowatoa nchini Misri, kutoka katika tanuri la chuma. Niliwaambia wanitii na kufanya yote niliyowaamuru, na kwamba wakifanya hivyo, watakuwa watu wangu, nami nitakuwa Mungu wao. 5Wakifuata masharti hayo, mimi nitatimiza ahadi niliyowapa wazee wenu, kwamba nitawapa nchi inayotiririka maziwa na asali, kama ilivyo hadi leo.” Nami nikajibu: “Na iwe hivyo, ee Mwenyezi-Mungu.”
6Mwenyezi-Mungu akaniambia: “Tangaza masharti hayo yote katika miji ya Yuda na katika barabara za Yerusalemu. Waambie watu wayasikilize masharti ya agano hili na wayatekeleze. 7Maana niliwaonya vikali wazee wao nilipowatoa katika nchi ya Misri, na nimeendelea kuwaonya wanitii mpaka siku hii ya leo. 8Lakini wao hawakunitii, wala hawakunisikiliza. Badala yake, kila mmoja wao alizidi kuwa mkaidi na mwovu. Basi, niliwaadhibu kulingana na masharti ya agano hili nililowaamuru walishike, lakini hao wakakataa kulishika.”
9Tena Mwenyezi-Mungu aliniambia: “Watu wa Yuda na wakazi wa Yerusalemu wanafanya njama za kuniasi. 10Wameurudia uovu wa wazee wao ambao walikataa kusikiliza maneno yangu; wameiabudu miungu mingine na kuitumikia. Watu wa Israeli na watu wa Yuda wamevunja agano nililofanya na wazee wao. 11Kwa hiyo, sasa, mimi Mwenyezi-Mungu ninawaonya kwamba nitawaletea maafa ambayo hawataweza kuepukana nayo. Hata kama wakinililia namna gani, sitawasikiliza. 12Hapo ndipo watu wa Israeli na Yerusalemu watakapoiendea miungu yao ambayo wanaifukizia ubani. Lakini miungu hiyo haitaweza kuwaokoa wakati huo wa taabu zao. 13Miungu yako, ewe Yuda imekuwa mingi kama ilivyo miji yako; kama zilivyo nyingi barabara za Yerusalemu, ndivyo zilivyo nyingi madhabahu walizomjengea mungu kinyaa Baali, ili kumfukizia ubani. 14Basi, wewe Yeremia, usiwaombee watu hawa, usinililie kwa ajili yao, wala usiwaombee dua. Maana, hata wakiniomba wanapotaabika, mimi sitawasikiliza.”
15Mwenyezi-Mungu asema: “Watu niwapendao wana haki gani kuingia hekaluni mwangu wakati wametenda maovu? Je, wanadhani nadhiri11:15 nadhiri: Kiebrania: Nyingi. na nyama zilizowekwa wakfu zitawaondolea maafa? Je, hayo yatawafurahisha? 16Wakati fulani, mimi nilisema, wao ni mzeituni wenye majani mabichi, mzeituni mzuri na wenye matunda mema; lakini sasa, kwa ngurumo ya dhoruba kubwa, nitauchoma moto na kuyateketeza matawi yake. 17Mimi Mwenyezi-Mungu wa majeshi niliuotesha huu mzeituni; lakini natangaza maafa dhidi yake kwa sababu ya maovu ambayo watu wa Israeli na Yuda wameyafanya. Wamenikasirisha kwa kumfukizia ubani mungu Baali.”
Njama za kumuua Yeremia
18Mwenyezi-Mungu alinijulisha, nami nikaelewa;
Mwenyezi-Mungu alinijulisha njama zao.
19Nami nilikuwa kama kondoo mpole anayepelekwa machinjoni;
sikujua kuwa njama walizofanya zilikuwa dhidi yangu.
Walisema: “Na tuuharibu mti pamoja na matunda yake,
tumkatilie mbali kutoka nchi ya walio hai,
kamwe jina lake lisikumbukwe tena.”
20Lakini, ee Mwenyezi-Mungu wa majeshi,
wewe unayehukumu kwa haki,
unayepima mioyo na akili za watu,
unijalie kuona ukiwalipiza kisasi,
maana kwako nimekiweka kisa changu.
21Ndiyo maana Mwenyezi-Mungu wa majeshi anacho cha kusema juu ya watu wa Anathothi ambao wanataka kuniua na kuniambia: “Usitoe unabii kwa jina la Mwenyezi-Mungu, la sivyo tutakuua.” 22Mwenyezi-Mungu wa majeshi asema hivi: “Nitawaadhibu watu hao. Vijana wao watauawa vitani; watoto wao wa kiume na wa kike watakufa kwa njaa. 23Nimepanga muda wa kuleta maangamizi juu ya watu wa Anathothi. Wakati huo utakapofika, hakuna hata mmoja wao atakayebaki hai.”



Yeremia11;1-23

Biblia Habari Njema kwa Watu Wote(BHN)

"Swahili Na Waswahili"Mbarikiwe.

Friday 13 December 2019

Kikombe Cha Asubuhi; Yeremia 10....


Shalom,Habari za Asubuhi,Hamjambo,Mmeamkaje?

Tumshukuru Mungu wetu katika yote...

Asante  Mungu wetu kwa wema na fadhili zako kwetu
Asante kwa ulinzi wako kwetu wakati wote
Asante kwa kutuchagua tena na kutupa
kibali cha kuendelea kuiona leo hii
Asante kwa pumzi/uzima,afya na kuwatayari kwa majukumu yetu


Utukuzwe ee Mungu wetu,usifiwe Baba wa Mbinguni

Neema yako yatutosha  Mungu wetu..!

Kutoka Mileto Paulo alituma ujumbe kwa wazee wa Efeso wakutane naye. Walipofika kwake aliwaambia, “Mnajua jinsi nilivyokaa nanyi siku zote tangu siku ile ya kwanza nilipofika Asia.
Baba wa Mbinguni tunakuja mbele zako tukijinyenyekeza,
tukijishusha na kujiachilia mikononi mwako

Mungu wetu tunaomba utusamehe dhambi zetu zote
Baba wa Mbinguni nasi tunaomba utupe neema ya kuweza kuwasamehe wale wote waliotukosea,Usitutie majaribuni Mungu wetu tunaomba utuepushe na yule mwovu na kazi zake zote,Jehovah ututakase miili yetu na akili zetu Baba wa Mbinguni tunaomba utufunike kwa  Damu ya Bwana na Mwokozi wetu Yesu Kristo wa Nazareti,
Yeye aliteseka kwanza ili sisi tupate kupona....


Mnajua jinsi nilivyomtumikia Bwana kwa unyenyekevu wote, kwa machozi na matatizo yaliyonipata kutokana na mipango ya hila ya Wayahudi. Mnajua kwamba sikusita hata kidogo kuwahubiria hadharani na nyumbani mwenu na kuwafundisha chochote ambacho kingewasaidieni.
Mungu wetu tunaomba ukabariki kazi za mikono yetu
Baba wa Mbinguni tunaomba ukatupe ubunifu na maarifa 
katika utendaji
Jehovah nasi tukatende sawasawa na mapenzi yako
Baba wa Mbinguni tunaomba ukabariki ridhiki zetu
ziingiazo/zitokazo
Mungu wetu nasi tunaomba ukatupe neema ya kuweza
kuwabariki wenye kuhitaji
Yahweh tusipungukiwe katika mahitaji yetu
Mungu wetu ukatupe kama inavyokupendeza wewe



Jehovah tunayaweka maisha yetu mikononi mwako
Baba wa Mbinguni tunaomba ukabariki nyumba/ndoa zetu,
watoto,wazazi wetu,familia/ndugu na wote wanaotuzunguka
Jehovah tunaomba ulinzi wako kwetu na kwa vyote tunavyo vimiliki
Yahweh tunaomba ukatubariki tuingiapo/tutokapo
Mungu wetu tunaomba ukavibariki vyote tunavyoenda kugusa/kutumia
Baba wa Mbinguni ukavitakase kwa Damu ya Bwana wetu Yesu Kristo
Mungu wetu ukatamalaki na kutuatamia
Baba wa Mbinguni tukawe salama rohoni
Mfalme wa amani amani yako ikatawale katika maisha yetu
Mungu wetu ukatupe macho ya kuona na masikio ya kusikia 
sauti yako na kuitii
Baba wa Mbinguni tunaomba ukatupe neema ya kufuata njia zako
Yahweh tukasimamie Neno lako amri na sheria zako siku zote 
za maisha yetu

Mungu  wetu ukaonekane katika maisha yetu popote tupitapo na ikajulikane kwamba upo 

Neema zako zikawe nasi Nuru yako ikaangaze katika maisha yetu
Ukatufanye barua njema ee Mungu wetu nasi tukasomeke kama
inavyokupendeza wewe
Roho Mtakatifu akatuongoze katika yote na tukawe na kiasi...

Niliwaonya wote – Wayahudi, kadhalika na watu wa mataifa, wamgeukie Mungu na kumwamini Bwana wetu Yesu. Sasa, sikilizeni! Mimi, nikiwa ninamtii Roho, nakwenda Yerusalemu bila kufahamu yatakayonipata huko. Ninachojua tu ni kwamba Roho Mtakatifu ananithibitishia katika kila mji kwamba vifungo na mateso ndivyo vinavyoningojea. Lakini, siuthamini uhai wangu kuwa kitu sana kwangu mradi tu nikamilishe ule utume wangu na ile kazi aliyonipa Bwana Yesu niifanye, yaani nishuhudie Habari Njema ya neema ya Mungu.
Tazama wenye shida/tabu,Mungu wetu tunaomba
 ukawaguse kila mmoja na mahitaji yake
Baba wa Mbinguni tunaomba ukawasamehe pale walipokwenda
kinyume nawe
Mungu wetu ukawape neema ya kujiombea,macho ya rohoni,masikio yakusikia sauti yako,wakafuate njia zako nazo zikawaweke huru
Mungu wetu tunaomba ukasikie kulia kwao
Baba wa Mbinguni tunomba ukawafute machozi yao
Nuru yako ikaangaze katika maisha yao
Mungu wetu tunaomba ukawatendee sawasawa na mapenzi yako
Kwakuwa Ufalme ni wako Nguvu na Utukufu hata Milele
Amina....!!!


Wapendwa katika Kristo Yesu asanteni sana
kwakuwanami/kunisoma

Mungu Baba aendelee kuwabariki na kuwatendea
kama inavyompendeza yeye
Amani ya Bwana wetu Yesu Kristo na upendo wa Mungu Baba
ukae nanyi daima....

Nawapenda.

Ibada za sanamu na ibada za kweli
1Sikilizeni neno analowaambieni Mwenyezi-Mungu,
enyi Waisraeli!
2Mwenyezi-Mungu asema hivi:
“Msijifunze mienendo ya mataifa mengine,
wala msishangazwe na ishara za mbinguni;
yaacheni mataifa mengine yashangazwe nazo.
3Maana, mila za dini za watu hawa ni za uongo.
Mtu hukata mti msituni
fundi akachonga kinyago cha mungu kwa shoka.
4Kisha watu hukipamba kwa fedha na dhahabu
wakakipigilia misumari kwa nyundo
ili kisije kikaanguka.
5Vinyago vyao ni kama vinyago vya kutishia ndege
katika shamba la matango,
havina uwezo wa kuongea;
ni lazima vibebwe
maana haviwezi kutembea.
Msiviogope vinyago hivyo,
maana haviwezi kudhuru,
wala haviwezi kutenda lolote jema.”
6Ee Mwenyezi-Mungu, hakuna aliye kama wewe;
wewe ni mkuu na nguvu yako yajulikana.
7Nani asiyekuogopa wewe, ee mfalme wa mataifa?
Wewe wastahili kuheshimiwa.
Miongoni mwa wenye hekima wote wa mataifa,
na katika falme zao zote,
hakuna hata mmoja aliye kama wewe.
8Wote ni wajinga na wapumbavu
mafunzo ya vinyago ni upuuzi mtupu!
9Vinyago hivyo hupambwa kwa fedha kutoka Tarshishi,
na dhahabu kutoka Ofiri;
kazi ya mafundi stadi na wafua dhahabu.
Zimevishwa nguo za samawati na zambarau,
zilizofumwa na wafumaji stadi.
10Lakini Mwenyezi-Mungu ni Mungu wa kweli;
Mungu aliye hai, mfalme wa milele.
Akikasirika, dunia hutetemeka,
mataifa hayawezi kustahimili hasira yake.
11Basi, utawaambia hivi: “Miungu ambayo haikuumba mbingu na dunia, itaangamia. Itatoweka kabisa duniani na chini ya mbingu.”
Wimbo wa kumsifu Mungu
12Mwenyezi-Mungu aliiumba dunia kwa nguvu zake;
kwa hekima yake aliuimarisha ulimwengu,
kwa akili yake alizitandaza mbingu.
13Anapotoa sauti yake, maji hunguruma mbinguni,
huzusha ukungu kutoka mipaka ya dunia.
Huufanya umeme umulike wakati wa mvua,
na kuutoa upepo katika ghala zake.
14Binadamu ni mjinga na mpumbavu;
kila mfua dhahabu huaibishwa na vinyago vyake;
maana, vinyago hivyo ni uongo mtupu.
Havina uhai wowote ndani yao.
15Havina thamani, ni udanganyifu mtupu;
wakati vitakapoadhibiwa vyote vitaangamia.
16Lakini Mungu wa Yakobo si kama vinyago hivyo,
maana, yeye ndiye aliyeumba vitu vyote,
na Israeli ni taifa lililo mali yake;
Mwenyezi-Mungu wa majeshi ndilo jina lake.
Uhamisho unakaribia
17Kusanyeni vitu vyenu enyi watu mliozingirwa.
18Maana Mwenyezi-Mungu asema hivi:
“Wakati huo nitawatupa nje ya nchi hii,
nitawataabisha asibaki mtu yeyote.”
19Ole wangu mimi Yerusalemu maana nimejeruhiwa!
Jeraha langu ni baya sana!
Lakini nilisema: “Hakika haya ni mateso,
na sina budi kuyavumilia.”
20Lakini hema langu limebomolewa,
kamba zake zote zimekatika;
watoto wangu wameniacha, na kwenda zao,
wala hawapo tena;
hakuna wa kunisimikia tena hema langu,
wala wa kunitundikia mapazia yangu.
21Nami Yeremia nikasema:
Wachungaji wamekuwa wajinga,
hawakuomba shauri kwa Mwenyezi-Mungu;
kwa sababu hiyo, hawakufanikiwa,
na kondoo wao wote wametawanyika.
22Sikilizeni sauti! Habari zinatufikia.
Kuna kishindo kutoka kaskazini.
Taifa kutoka kaskazini linakuja,
kuifanya miji ya Yuda kuwa jangwa
ambamo kutakuwa na mapango ya mbweha!
23Najua, ee Mwenyezi-Mungu,
binadamu hana uwezo na maisha yake;
hakuna mtu awezaye kuyaongoza maisha yake.
24Utukosoe, ee Mwenyezi-Mungu, lakini si kwa ghadhabu,
wala kwa hasira yako, tusije tukaangamia.
25Imwage hasira yako juu ya mataifa yasiyokuabudu,
na juu ya watu ambao hawakutambui.
Maana, wamewaua wazawa wa Yakobo;
wamewaua na kuwaangamiza kabisa,
na nchi yao wameiacha magofu.


Yeremia10;1-25

Biblia Habari Njema kwa Watu Wote(BHN)

"Swahili Na Waswahili"Mbarikiwe.

Thursday 12 December 2019

Kikombe Cha Asubuhi; Yeremia 9....



Shalom,Habari za Asubuhi,Hamjambo,Mmeamkaje?

Tumshukuru Mungu katika yote....

Mungu wetu Baba yetu,Muumba wetu Muumba wa Mbingu na Nchi
Muumba wa vyote vilivyomo vinavyoonekana na visivyoonekana
Mungu wa walio hai,Mungu  mwenye huruma,Mungu wa upendo
Mungu wa Abrahamu,Isaka na Yakobo...
Asante kwa wema na fadhili zako kwetu
Asante kwa ulinzi wako kwetu wakati wote
Asante kwa kutuchagua tena na kutupa
kibali cha kuendelea kuiona leo hii
Asante kwa pumzi/uzima,afya na kuwatayari kwa majukumu yetu

Neema yako yatutosha ee Mungu wetu....!!


Sisi tulipanda meli tukatangulia kwenda Aso ambako tungemchukua Paulo. Ndivyo alivyopanga; maana alitaka kufika huko kwa kupitia nchi kavu. Basi, alitukuta kule Aso, tukampandisha melini, tukaenda Mitulene.
Baba wa Mbinguni tunakuja mbele zako tukijinyenyekeza,
tukijishusha na kujiachilia mikononi mwako

Mungu wetu tunaomba utusamehe dhambi zetu zote 
Baba wa Mbinguni nasi tunaomba ukatupe neema
ya kuweza kuwasamehe wale wote waliotukosea
Usitutie majaribuni Mungu wetu tunaomba utuepushe
na yule mwovu na kazi zake zote
Jehovah ututakase miili yetu na akili zetu
Baba wa Mbinguni tunaomba utufunike kwa Damu
ya Bwana na Mwokozi wetu Yesu Kristo wa Nazareti
yeye aliteseka kwanza ili sisi tupate kupona....

Kutoka huko tulisafiri tukafika Kio kesho yake. Siku ya pili, tulitia nanga Samo na kesho yake tukafika Mileto.
Mungu wetu tunaomba ukabariki kazi za mikono yetu
Baba wa Mbinguni tunaomba ukatupe ubunifu na maarifa katika utendaji
Jehovah nasi tukatende sawasawa na mapenzi yako
Yahweh tunaomba ukabariki ridhiki zetu ziingiazo/zitokazo
Mungu wetu nasi tunaomna ukatupe neema ya kuweza kuwabariki wenye kuhitaji
Tusipungukiwe katika mahitaji yetu
Baba wa Mbinguni tunaomba ukatupe kama inavyokupendeza wewe...


Yahweh tunayaweka maisha yetu mikononi mwako
Mungu wetu tunaomba ukabariki nyumba/ndoa zetu,
Jehovah tunaomba ulinzi wako kwetu na kwa vyote tunavyovimiliki
Yahweh tunaomba ukatubariki tuingiapo/tutokapo
Mungu wetu tunaomba ukavibariki vyote tunavyoenda kugusa/kutumia
Baba wa Mbinguni ukavitakase kwa Damu ya Bwana wetu Yesu Kristo
Mungu wetu ukatamalaki na kutuatamia
Baba wa Mbinguni tukawe salama rohoni
Yahwe ukatupe akili ya kutambua mema na mabaya
Mfalme wa amani amani yako ikatawale katika maisha yetu
Mungu wetu ukatupe macho ya kuona,masikio ya kusikia sauti yako na kuitii..
Baba wa Mbinguni  tunaomba ukatupe neema ya kufuata
njia zako,tukasimamie Neno lako,amri na sheria zako
siku zote za maisha yetu...
Ukatuguse kwa mkono wako wenye nguvu,ukatufanye chombo chema
ee Mungu wetu nasi tukatumike kama inavyokupendeza wewe
Roho Mtakatifu akatuongoze katika yote na tukawe na kiasi....

Paulo alikuwa amekusudia kuendelea na safari kwa meli bila kupitia Efeso ili asikawie zaidi huko Asia. Alikuwa na haraka ya kufika Yerusalemu kwa sikukuu ya Pentekoste kama ingewezekana.
Tazama watoto wako wenye shida/tabu,wote wanaopitia magumu/majaribu mbalimbali
Mungu wetu tunaomba ukawaguse kwa mkono wako wenye nguvu
kila mmoja na mahitaji yake
Mungu wetu tunaomba ukawasamehe pale walipo kwenda kinyume nawe
Yahweh tunaomba ukawape neema ya kuweza kujiombea,kufuata njia zako nazo zikawaweke huru...
Baba wa Mbinguni tunayaweka haya yote mikononi mwako
Kwakuwa Ufalme ni wako Nguvu na Utukufu hata Milele...
Amina...!!


Asanteni sana wapendwa katika Kristo Yesu kwakuwa nami,Baba wa Mbinguni aendelee kuwatendea sawasawa na mapenzi yake...
Nawapenda.

1Laiti kichwa changu kingekuwa kisima cha maji,
na macho yangekuwa chemchemi ya machozi
ili nipate kulia mchana na usiku,
kwa ajili ya watu wangu waliouawa!
2Laiti ningekuwa na mahali pa kukaa jangwani,
ambamo ningewaacha watu wangu na kwenda zangu.”
Mwenyezi-Mungu asema:
“Wote ni watu wazinzi,
ni genge la watu wahaini.
3Hupinda maneno yao kama pinde;
wameimarika kwa uongo na si kwa haki.
Huendelea kutoka uovu hata uovu,
wala hawanitambui mimi.
Mimi Mwenyezi-Mungu nimesema.
4Kila mmoja ajihadhari na jirani yake!
Hata ndugu yeyote haaminiki,
kila ndugu ni mdanganyifu,
na kila jirani ni msengenyaji.
5Kila mmoja humdanganya jirani yake,
hakuna hata mmoja asemaye ukweli.
Wamezifundisha ndimi zao kusema uongo;
hutenda uovu kiasi cha kushindwa kabisa kutubu.
6Wanarundika dhuluma juu ya dhuluma,
na udanganyifu juu ya udanganyifu.
Wanakataa kunitambua mimi.
Mimi Mwenyezi-Mungu nimesema.
7Kwa hiyo mimi Mwenyezi-Mungu wa majeshi nasema:
Tazama, nitawayeyusha na kuwajaribu!
Au, nifanye nini zaidi na watu wangu waovu?
8Ndimi zao ni kama mishale yenye sumu,
daima haziishi kudanganya;
kila mmoja huongea vema na jirani yake,
lakini moyoni mwake hupanga kumshambulia.
9Je, nisiwaadhibu kwa sababu ya mambo haya?
Je, nisilipe kisasi kwa taifa kama hili?
Mimi Mwenyezi-Mungu nimesema.”
Nyakati za kulia na kuomboleza
10Nitaililia na kuiomboleza milima;
nitayaombolezea malisho nyikani,
kwa sababu yamekauka kabisa,
hakuna mtu apitaye mahali hapo.
Hakusikiki tena sauti za ng'ombe;
ndege na wanyama wamekimbia na kutoweka.
11Mwenyezi-Mungu asema:
“Nitaifanya Yerusalemu magofu matupu,
naam, nitaifanya kuwa pango la mbweha;
na miji ya Yuda nitaifanya kuwa jangwa,
mahali pasipokaliwa na mtu yeyote.”
12Nami nikauliza, “Je kuna mtu mwenye hekima kiasi cha kuweza kueleza mambo haya? Mwenyezi-Mungu aliongea na nani hata huyo aweze kutangaza kitu hicho? Kwa nini nchi imeharibiwa na kufanywa tupu kama jangwa hata hakuna mtu apitaye humo?”
13Mwenyezi-Mungu akajibu: “Kwa kuwa wamekataa kushika sheria yangu niliyowapa, wamekataa kutii sauti yangu na kufuata matakwa yake. 14Badala yake wamefuata kwa ukaidi fikira za mioyo yao, wakaenda kuyaabudu Mabaali kama walivyofundishwa na wazee wao. 15Basi, mimi Mwenyezi-Mungu wa majeshi, Mungu wa Israeli, nasema hivi: Tazama nitawalisha watu hawa uchungu na kuwapa maji yenye sumu wanywe. 16Nitawatawanya kati ya mataifa ambayo wao wenyewe wala wazee wao hawakupata kuyajua; nitawafanya waandamwe na vita mpaka hapo nitakapowaangamiza wote.”
Watu wa Yerusalemu walilia msaada
17Mwenyezi-Mungu wa majeshi asema hivi:
“Fikirini na kuwaita wanawake waomboleze;
naam, waiteni wanawake hodari wa kuomboleza.
18Waambieni: ‘Njoni hima mkaomboleze juu yetu,
macho yetu yapate kuchuruzika machozi,
na kope zetu zibubujike machozi kama maji.’”
(Yeremia)
19Kilio kinasikika Siyoni:
“Tumeangamia kabisa!
Tumeaibishwa kabisa!
Lazima tuiache nchi yetu,
maana nyumba zetu zimebomolewa!
20Enyi wanawake, sikilizeni neno la Mwenyezi-Mungu!
Tegeni masikio msikie jambo analosema.
Wafundisheni binti zenu kuomboleza,
na jirani zenu wimbo wa maziko:
21‘Kifo kimepenya madirisha yetu,
kimeingia ndani ya majumba yetu;
kimewakatilia mbali watoto wetu barabarani,
vijana wetu katika viwanja vya mji.
22Maiti za watu zimetapakaa kila mahali
kama marundo ya mavi mashambani,
kama masuke yaliyoachwa na mvunaji,
wala hakuna atakayeyakusanya.’
Ndivyo alivyoniambia Mwenyezi-Mungu niseme.”
23Mwenyezi-Mungu asema hivi:
“Mwenye hekima asijivunie nguvu zake,
wala tajiri asijivunie utajiri wake.
24Anayetaka kujivuna na ajivunie jambo hili:
Kwamba ananifahamu
kwamba anajua Mwenyezi-Mungu hutenda mema,
hufanya mambo ya haki na uadilifu duniani.
Watu wa namna hiyo ndio wanipendezao.
Mimi Mwenyezi-Mungu nimesema.”
25Mwenyezi-Mungu asema: “Siku zaja ambapo nitawaadhibu wote waliotahiriwa mwilini tu: 26Wamisri, Wayuda, Waedomu, Waamoni, Wamoabu na wakazi wote wa jangwani wanaonyoa denge.9:26 wanaonyoa denge: Watu hao walinyoa denge kwa heshima ya mungu wao, desturi ambayo Waisraeli walikatazwa Maana watu hawa wote na Waisraeli wote hawakutahiriwa moyoni.”


Yeremia9;1-26

Biblia Habari Njema kwa Watu Wote(BHN)

"Swahili Na Waswahili"Mbarikiwe.