Swahili na Waswahili

Swahili na Waswahili
Waswahili na Mswahili Rachel Siwa...Pamoja Daima!!

Wednesday 11 December 2019

Kikombe Cha Asubuhi; Yeremia 8....


Shalom,Habari za Asubuhi,Hamjambo,Mmeamkaje?

Tumshukuru Mungu katika yote....

Mungu wetu Baba yetu,Muumba wetu Muumba wa Mbingu na Nchi
Muumba wa vyote vilivyomo vinavyoonekana na visivyoonekana
Mungu wa walio hai,Mungu  mwenye huruma,Mungu wa upendo
Mungu wa Abrahamu,Isaka na Yakobo...
Asante kwa wema na fadhili zako kwetu
Asante kwa ulinzi wako kwetu wakati wote
Asante kwa kutuchagua tena na kutupa
kibali cha kuendelea kuiona leo hii
Asante kwa pumzi/uzima,afya na kuwatayari kwa majukumu yetu

Neema yako yatutosha ee Mungu wetu....!!


Jumamosi jioni tulikutana ili kumega mkate. Kwa vile Paulo alikuwa amekusudia kuondoka kesho yake, aliwahutubia watu na kuendelea kuongea nao hadi usiku wa manane. Katika chumba tulimokuwa, ghorofani, kulikuwa na taa nyingi zinawaka.
Baba wa Mbinguni tunakuja mbele zako tukijinyenyekeza,tukijishusha na kujiachilia mikononi mwako
Mungu wetu tunaomba utusamehe dhambi zetu zote 
Baba wa Mbinguni nasi tunaomba ukatupe neema
ya kuweza kuwasamehe wale wote waliotukosea
Usitutie majaribuni Mungu wetu tunaomba utuepushe
na yule mwovu na kazi zake zote
Jehovah ututakase miili yetu na akili zetu
Baba wa Mbinguni tunaomba utufunike kwa Damu
ya Bwana na Mwokozi wetu Yesu Kristo wa Nazareti
yeye aliteseka kwanza ili sisi tupate kupona....


Kijana mmoja aitwaye Eutuko alikuwa ameketi dirishani wakati Paulo alipokuwa anaendelea kuhutubu. Eutuko alianza kusinzia kidogokidogo na hatimaye usingizi ukambana, akaanguka chini kutoka ghorofa ya tatu. Wakamwokota amekwisha kufa. Lakini Paulo alishuka chini, akainama, akamkumbatia na kusema, “Msiwe na wasiwasi maana kuna uhai bado ndani yake.”
Mungu wetu tunaomba ukabariki kazi za mikono yetu
Baba wa Mbinguni tunaomba ukatupe ubunifu na maarifa katika utendaji
Jehovah nasi tukatende sawasawa na mapenzi yako
Yahweh tunaomba ukabariki ridhiki zetu ziingiazo/zitokazo
Mungu wetu nasi tunaomna ukatupe neema ya kuweza kuwabariki wenye kuhitaji
Tusipungukiwe katika mahitaji yetu
Baba wa Mbinguni tunaomba ukatupe kama inavyokupendeza wewe...


Yahweh tunayaweka maisha yetu mikononi mwako
Mungu wetu tunaomba ukabariki nyumba/ndoa zetu,
Jehovah tunaomba ulinzi wako kwetu na kwa vyote tunavyovimiliki
Yahweh tunaomba ukatubariki tuingiapo/tutokapo
Mungu wetu tunaomba ukavibariki vyote tunavyoenda kugusa/kutumia
Baba wa Mbinguni ukavitakase kwa Damu ya Bwana wetu Yesu Kristo
Mungu wetu ukatamalaki na kutuatamia
Baba wa Mbinguni tukawe salama rohoni
Yahwe ukatupe akili ya kutambua mema na mabaya
Mfalme wa amani amani yako ikatawale katika maisha yetu
Mungu wetu ukatupe macho ya kuona,masikio ya kusikia sauti yako na kuitii..
Baba wa Mbinguni  tunaomba ukatupe neema ya kufuata
njia zako,tukasimamie Neno lako,amri na sheria zako
siku zote za maisha yetu...
Ukatuguse kwa mkono wako wenye nguvu,ukatufanye chombo chema
ee Mungu wetu nasi tukatumike kama inavyokupendeza wewe
Roho Mtakatifu akatuongoze katika yote na tukawe na kiasi....


Kisha akapanda tena ghorofani, akamega mkate, akala. Aliendelea kuhubiri kwa muda mrefu hadi alfajiri, halafu akaondoka. Wale watu walimchukua yule kijana hadi nyumbani akiwa mzima kabisa, wakapata kitulizo kikubwa.
Tazama watoto wako wenye shida/tabu,wote wanaopitia magumu/majaribu mbalimbali
Mungu wetu tunaomba ukawaguse kwa mkono wako wenye nguvu
kila mmoja na mahitaji yake
Mungu wetu tunaomba ukawasamehe pale walipo kwenda kinyume nawe
Yahweh tunaomba ukawape neema ya kuweza kujiombea,kufuata njia zako nazo zikawaweke huru...
Baba wa Mbinguni tunayaweka haya yote mikononi mwako
Kwakuwa Ufalme ni wako Nguvu na Utukufu hata Milele...
Amina...!!


Asanteni sana wapendwa katika Kristo Yesu kwakuwa nami,Baba wa Mbinguni aendelee kuwatendea sawasawa na mapenzi yake...
Nawapenda.



1“Wakati huo, nasema mimi Mwenyezi-Mungu, mifupa ya wafalme wa Yuda, mifupa ya wakuu wao, mifupa ya makuhani, mifupa ya manabii na mifupa ya wakazi wote wa Yerusalemu itachimbuliwa makaburini mwao. 2Itaachwa imetandazwa mbele ya jua na mwezi na sayari zote za mbinguni, vitu ambavyo walivipenda na kuvitumikia, wakavitaka shauri na kuviabudu. Mifupa hiyo haitakusanywa wala kuzikwa, bali itakuwa kama mavi juu ya ardhi. 3Watu wote waliobaki wa jamaa hii mbovu, mahali popote pale nilipowatawanya, wataona heri kufa kuliko kuishi. Ndivyo nisemavyo mimi Mwenyezi-Mungu wa majeshi.
Dhambi na adhabu
4“Wewe Yeremia utawaambia
kuwa mimi Mwenyezi-Mungu nasema hivi:
Mtu akianguka, je hainuki tena?
Mtu akipotea, je, hairudii tena njia yake?
5Mbona basi, watu hawa wameacha njia iliyo sawa
na kuendelea katika upotovu wao?
Wanashikilia miungu yao ya uongo,
na kukataa kunirudia mimi!
6Mimi nilisikiliza kwa makini,
lakini wao hawakusema ukweli wowote.
Hakuna mtu anayetubu uovu wake,
wala kujiuliza; ‘Nimefanya nini?’
Kila mmoja wao anashika njia yake,
kama farasi akimbiliavyo moja kwa moja vitani.
7Hata korongo anajua wakati wa kuhama;
njiwa, mbayuwayu na koikoi,
hufuata majira yao ya kurudi.
Lakini watu wangu hawa hawajui kitu
juu ya amri zangu mimi Mwenyezi-Mungu.
8Mnawezaje kusema: ‘Sisi tuna hekima,
sisi tunayo sheria ya Mwenyezi-Mungu,’
hali waandishi wa sheria,
wameipotosha sheria yangu?
9Wenye hekima wenu wataaibishwa;
watafadhaishwa na kunaswa.
Wamelikataa neno la Mwenyezi-Mungu;
je, ni hekima gani hiyo waliyo nayo?
10Kwa hiyo, wake zao nitawapa watu wengine,
mashamba yao nitawapa wengine.
Maana, tangu mdogo hadi mkubwa,
kila mmoja ana tamaa ya faida haramu.
Tangu manabii hadi makuhani,
kila mmoja anatenda kwa udanganyifu.
11Wameliponya jeraha la watu wangu juujuu,
wakisema, ‘Kuna amani, kuna amani’,
kumbe hakuna amani yoyote!
12Je, waliona aibu walipotenda machukizo hayo?
La hasha! Hawakuona aibu hata kidogo.
Hata hawajui kuona haya.
Kwa hiyo, wataanguka pamoja na wale walioanguka;
nitakapowaadhibu, wataangamia.
Mimi Mwenyezi-Mungu nimesema.
13“Mimi Mwenyezi-Mungu nasema:
Nilipotaka kukusanya chochote kutoka kwao,
sikupata zabibu hata moja juu ya mzabibu,
sikupata tini zozote juu ya mtini;
hata majani yao yamekauka.
Hata nilichokuwa nimewapa kimetoweka.”8:13 nimewapa … kimetoweka: Maana katika Kiebrania si dhahiri.
14“Watu wanauliza: Kwa nini sisi tunakaa tu hapa?
Kusanyikeni, tuingie katika miji yenye ngome,
tukaangamie huko!
Mwenyezi-Mungu, Mungu wetu, ametupangia tuangamie,
ametupa maji yenye sumu tunywe,
kwa kuwa tumemkosea yeye.
15Tulitazamia kupata amani,
lakini hakuna jema lililotokea.
Tulitazamia wakati wa kuponywa,
badala yake tukapata vitisho.
16Sauti za farasi wao zinasikika,
kwa mlio wa farasi wao wa vita,
nchi nzima inatetemeka.
Wanafika na kuiharibu nchi na vyote vilivyomo,
kuangamiza mji pamoja na wote waishio humo.
(Mwenyezi-Mungu)
17“Basi nitawaleteeni nyoka;
nyoka wenye sumu wasioweza kurogwa na walozi,
nao watawauma nyinyi.
Mimi Mwenyezi-Mungu nimesema.”
Huzuni ya Yeremia
18Huzuni yangu haiwezi kutulizwa,8:18 huzuni … kutulizwa: Maana katika Kiebrania si dhahiri.
moyo wangu wasononeka ndani yangu.
19Sikiliza kilio cha watu wangu,
kutoka kila upande katika nchi.
“Je, Mwenyezi-Mungu hayuko Siyoni?
Je, mfalme wake hayuko tena huko?”
(Mwenyezi-Mungu)
“Mbona wamenikasirisha kwa sanamu zao za miungu,
na vinyago vyao vya miungu ya kigeni?”
(Yeremia)
20“Mavuno yamepita, kiangazi kimekwisha,
nasi bado hatujaokolewa!
21Jeraha la watu wangu limeniumiza moyoni,
ninaomboleza na kufadhaika.
22Je, hakuna dawa ya kupaka huko Gileadi?
Je, hakuna mganga huko?
Mbona basi watu wangu hawajaponywa?


Yeremia8;1-22

Biblia Habari Njema kwa Watu Wote(BHN)

"Swahili Na Waswahili"Mbarikiwe.

Tuesday 10 December 2019

Kikombe Cha Asubuhi; Yeremia 7....


Shalom,Habari za Asubuhi,Hamjambo,Mmeamkaje?

Tumshukuru Mungu wetu katika yote...

Asante  Mungu wetu kwa wema na fadhili zako kwetu
Asante kwa ulinzi wako kwetu wakati wote
Asante kwa kutuchagua tena na kutupa
kibali cha kuendelea kuiona leo hii
Asante kwa pumzi/uzima,afya na kuwatayari kwa majukumu yetu



Utukuzwe ee Mungu wetu,usifiwe Baba wa Mbinguni

Neema yako yatutosha  Mungu wetu..!


Ile ghasia ya Efeso ilipokwisha tulia Paulo aliwaita pamoja wale waumini, akawatia moyo. Kisha akawaaga, akasafiri kwenda Makedonia. Alipitia sehemu za nchi zile akiwatia watu moyo kwa maneno mengi. Halafu akafika Ugiriki ambako alikaa kwa miezi mitatu. Alipokuwa anajitayarisha kwenda Siria, aligundua kwamba Wayahudi walikuwa wanamfanyia mpango mbaya; hivyo aliamua kurudi kwa kupitia Makedonia.
Baba wa Mbinguni tunakuja mbele zako tukijinyenyekeza,
tukijishusha na kujiachilia mikononi mwako

Mungu wetu tunaomba utusamehe dhambi zetu zote
Baba wa Mbinguni nasi tunaomba utupe neema ya kuweza kuwasamehe wale wote waliotukosea,Usitutie majaribuni Mungu wetu tunaomba utuepushe na yule mwovu na kazi zake zote,Jehovah ututakase miili yetu na akili zetu Baba wa Mbinguni tunaomba utufunike kwa  Damu ya Bwana na Mwokozi wetu Yesu Kristo wa Nazareti,
Yeye aliteseka kwanza ili sisi tupate kupona....


Sopatro, mwana wa Pirho, kutoka Berea, aliandamana naye; pia Aristarko na Sekundo kutoka Thesalonike, Gayo kutoka Derbe, Timotheo, Tukiko na Trofimo wa mkoa wa Asia. Hao walitutangulia na kutungojea kule Troa.
Mungu wetu tunaomba ukabariki kazi za mikono yetu
Baba wa Mbinguni tunaomba ukatupe ubunifu na maarifa 
katika utendaji
Jehovah nasi tukatende sawasawa na mapenzi yako
Baba wa Mbinguni tunaomba ukabariki ridhiki zetu
ziingiazo/zitokazo
Mungu wetu nasi tunaomba ukatupe neema ya kuweza
kuwabariki wenye kuhitaji
Yahweh tusipungukiwe katika mahitaji yetu
Mungu wetu ukatupe kama inavyokupendeza wewe



Jehovah tunayaweka maisha yetu mikononi mwako
Baba wa Mbinguni tunaomba ukabariki nyumba/ndoa zetu,
watoto,wazazi wetu,familia/ndugu na wote wanaotuzunguka
Jehovah tunaomba ulinzi wako kwetu na kwa vyote tunavyo vimiliki
Yahweh tunaomba ukatubariki tuingiapo/tutokapo
Mungu wetu tunaomba ukavibariki vyote tunavyoenda kugusa/kutumia
Baba wa Mbinguni ukavitakase kwa Damu ya Bwana wetu Yesu Kristo
Mungu wetu ukatamalaki na kutuatamia
Baba wa Mbinguni tukawe salama rohoni
Mfalme wa amani amani yako ikatawale katika maisha yetu
Mungu wetu ukatupe macho ya kuona na masikio ya kusikia 
sauti yako na kuitii
Baba wa Mbinguni tunaomba ukatupe neema ya kufuata njia zako
Yahweh tukasimamie Neno lako amri na sheria zako siku zote 
za maisha yetu

Mungu  wetu ukaonekane katika maisha yetu popote tupitapo na ikajulikane kwamba upo 

Neema zako zikawe nasi Nuru yako ikaangaze katika maisha yetu
Ukatufanye barua njema ee Mungu wetu nasi tukasomeke kama
inavyokupendeza wewe
Roho Mtakatifu akatuongoze katika yote na tukawe na kiasi...


Sisi, baada ya sikukuu ya mikate isiyotiwa chachu, tulipanda meli kutoka Filipi na baada ya siku tatu tukawafikia kule Troa. Huko tulikaa kwa muda wa juma moja.
Tazama wenye shida/tabu,Mungu wetu tunaomba
 ukawaguse kila mmoja na mahitaji yake
Baba wa Mbinguni tunaomba ukawasamehe pale walipokwenda
kinyume nawe
Mungu wetu ukawape neema ya kujiombea,macho ya rohoni,masikio yakusikia sauti yako,wakafuate njia zako nazo zikawaweke huru
Mungu wetu tunaomba ukasikie kulia kwao
Baba wa Mbinguni tunomba ukawafute machozi yao
Nuru yako ikaangaze katika maisha yao
Mungu wetu tunaomba ukawatendee sawasawa na mapenzi yako
Kwakuwa Ufalme ni wako Nguvu na Utukufu hata Milele
Amina....!!!


Wapendwa katika Kristo Yesu asanteni sana
kwakuwanami/kunisoma

Mungu Baba aendelee kuwabariki na kuwatendea
kama inavyompendeza yeye
Amani ya Bwana wetu Yesu Kristo na upendo wa Mungu Baba
ukae nanyi daima....

Nawapenda.

Yeremia anahubiri hekaluni
1Mwenyezi-Mungu alimwamuru Yeremia aende kusimama 2kwenye lango la hekalu lake Mwenyezi-Mungu na kutangaza ujumbe huu: “Sikilizeni neno la Mwenyezi-Mungu enyi watu wa Yuda mnaoingia humu kumwabudu Mwenyezi-Mungu. 3Mwenyezi-Mungu wa majeshi, Mungu wa Israeli, asema hivi: Rekebisheni mienendo yenu na matendo yenu, nami nitawaacha mwendelee kukaa mahali hapa. 4Msitumainie maneno haya ya uongo: ‘Hili ni hekalu la Mwenyezi-Mungu, hekalu la Mwenyezi-Mungu, naam hekalu la Mwenyezi-Mungu.’
5“Ila kama mkibadili mienendo yenu na matendo yenu, mkitendeana haki kwa dhati; 6kama mkiacha kuwadhulumu wageni, yatima au wajane au kuwaua watu wasio na hatia katika nchi hii; kama mkiacha kuabudu miungu mingine na kujiangamiza wenyewe, 7basi mimi nitawaacha daima mkae mahali hapa, katika nchi niliyowapa wazee wenu tangu zamani.
8“Lakini kumbe, mnayaamini maneno ya uongo bure. 9Mnaiba, mnaua, mnafanya uzinzi, mnaapa uongo, mnamfukizia mungu Baali ubani na kuabudu miungu mingine ambayo hamjapata kuijua. 10Kisha, mnakuja na kusimama mbele yangu, katika hekalu hili linalojulikana kwa jina langu na kusema; ‘Tuko salama,’ huku mnaendelea kufanya mambo hayo yanayonichukiza. 11Je, hekalu hili linalojulikana kwa jina langu limekuwa pango la wanyanganyi? Jueni kuwa mimi nimeyaona yote mnayofanya! 12Nendeni mahali pangu kule Shilo,7:12 Shilo: Mji ambamo liliwekwa sanduku la agano nyakati za Eli (taz 1Sam 1:3). Mji huu uliangamizwa, pengine na Wafilisti. mahali nilipopachagua niabudiwe hapo awali, mkaone maangamizi niliyoyafanya huko kwa sababu ya uovu wa watu wangu, Israeli. 13Nyinyi mmefanya mambo hayo yote, na hata niliposema nanyi tena na tena hamkunisikiliza. Nilipowaiteni hamkuitika. 14Kwa hiyo, kama nilivyoutendea mji wa Shilo, ndivyo nitakavyolitendea hekalu hili linalojulikana kwa jina langu, hekalu ambalo nyinyi mnalitegemea; naam, mahali hapa ambapo niliwapa nyinyi na wazee wenu. 15Nitawafukuzeni mbali nami kama nilivyowatupilia mbali ndugu zenu, wazawa wote wa Efraimu.
Kutotii kwa watu
16“Nawe, Yeremia, usiwaombee watu hawa, usinililie kwa ajili yao, usiwaombee dua wala usinisihi kwa ajili yao, maana sitakusikiliza. 17Je, wewe huoni mambo wanayofanya katika miji ya Yuda na katika mitaa ya Yerusalemu? 18Watoto huokota kuni, akina baba huwasha moto na akina mama hukanda unga ili waoke mikate kwa ajili ya mungu wa kike wanayemwita malkia wa mbinguni. Tena wanaimiminia miungu mingine tambiko ya divai ili kuniudhi. 19Lakini je, wanamwudhi nani? Mimi? Hata kidogo! Wanajiumiza wao wenyewe na kuchanganyikiwa! 20Kwa hiyo, mimi Mwenyezi-Mungu nasema hivi: Nitaimwaga hasira yangu na ghadhabu yangu mahali hapa, juu ya wanadamu na wanyama, miti mashambani na mazao ya nchi. Itawaka na wala haitaweza kuzimwa.”
21Mwenyezi-Mungu wa majeshi, Mungu wa Israeli, asema hivi: “Haya, ongezeni tambiko zenu za kuteketezwa juu ya sadaka zenu na kula nyama yake! 22Maana, siku nilipowatoa wazee wenu nchini Misri, sikuwaambia kitu wala kuwapa amri yoyote juu ya tambiko za kuteketezwa na sadaka. 23Lakini niliwapa amri hii: Waitii sauti yangu ili niwe Mungu wao, nao wawe watu wangu. Niliwaamuru pia waishi kama nilivyowaagiza, ili mambo yao yawaendee vema. 24Lakini wao hawakunitii wala kunitegea sikio. Badala yake wakafuata fikira zao wenyewe na ukaidi wa mioyo yao, wakarudi nyuma badala ya kusonga mbele. 25Tangu siku ile wazee wenu walipotoka nchini Misri hadi leo, sijakoma kuwatuma kwenu watumishi wangu, manabii. 26Lakini hamkunisikiliza wala kunitegea sikio, ila mlizidi kuwa wakaidi, mkawa waasi kuliko hata wazee wenu.
27“Basi, wewe Yeremia utawaambia maneno haya yote, lakini wao hawatakusikiliza. Utawaita, lakini hawatakuitikia. 28Utawaambia; ‘Nyinyi ni taifa ambalo halikutii sauti ya Mwenyezi-Mungu, Mungu wenu, wala kukubali kuwa na nidhamu. Kwenu uaminifu umekufa; umetoweka kabisa katika maneno yenu.’
Maovu katika Bonde la Hinomu
29“Nyoeni nywele zenu enyi wakazi wa Yerusalemu, mzitupe;
fanyeni maombolezo juu ya vilele vya milima,
maana, mimi Mwenyezi-Mungu nimewakataa nyinyi,
mlio kizazi kilichosababisha hasira yangu!
30“Watu wa Yuda wametenda uovu mbele yangu. Wameweka vinyago vyao vya kuchukiza ndani ya nyumba hii ijulikanayo kwa jina langu, wakaitia unajisi. 31Wamejenga madhabahu iitwayo ‘Tofethi’ huko kwenye bonde la mwana wa Hinomu, wapate kuwachoma sadaka watoto wao wa kiume na wa kike humo motoni. Mimi sikuwa nimewaamuru kamwe kufanya jambo hilo, wala halikunijia akilini mwangu. 32Kwa sababu hiyo, siku zaja ambapo hawataliita tena ‘Tofethi,’ au ‘Bonde la Mwana wa Hinomu,’ bali wataliita ‘Bonde la Mauaji.’ Huko ndiko watakakozika watu, kwa sababu hapatakuwa na mahali pengine pa kuzikia. 33Maiti za watu hao zitakuwa chakula cha ndege wa angani na wanyama wa porini, na hapatakuwa na mtu atakayewafukuza. 34Nchi itakuwa jangwa na katika miji ya Yuda na mitaa ya Yerusalemu nitakomesha sauti zote za vicheko na furaha, sauti za bwana arusi na bibi arusi, kwa sababu nchi itakuwa ukiwa.

Yeremia7;1-34

Biblia Habari Njema kwa Watu Wote(BHN)

"Swahili Na Waswahili"Mbarikiwe.

Monday 9 December 2019

Kikombe Cha Asubuhi; Yeremia 6....


Shalom,Habari za Asubuhi,Hamjambo,Mmeamkaje?

Haleluyah ni siku/wiki
Nyingine tena Mungu wetu ametuchagua

na kutupa kibali cha kuendelea kuiona leo hii
Si kwamba sisi tumetenda mema sana wala si kwa nguvu zetu
si kwa utashi wetu wala si kwa akili zetu si kwamba sisi
ni wazuri mno si kwa uwezo wetu sisi kuwa hivi tulivyo leo hii
Ni kwa rehema/neema zake ni kwa mapenzi yake Mungu wetu....

Tumshukuru Mungu wetu katika yote...

Asante Mungu wetu kwa wema na fadhili zako kwetu

Asante kwa ulinzi wako kwetu wakati wote
Asante kwa pumzi/uzima,afya na kuwa tayari kwa majukumu yetu
Sifa na Utukufu tunakurudshia Mungu wetu....!!


Baada ya siku mbili Yesu aliondoka hapo, akaenda Galilaya. Maana Yesu mwenyewe alisema waziwazi kwamba, “Nabii hapati heshima katika nchi yake.” Basi, alipofika Galilaya, Wagalilaya wengi walimkaribisha. Maana nao pia walikuwa kwenye sikukuu ya Pasaka, wakayaona mambo yote Yesu aliyotenda huko Yerusalemu wakati wa sikukuu hiyo.
Tazama jana imepita ee Mungu wetu leo ni siku mpya na kesho ni siku nyingine Jehovah tunakuja mbele zako tukijinyenyekeza,tukijishusha na kujiachilia mikononi mwako
 Mungu wetu tunaomba utusamehe dhambi zetu zote tulizozifanya kwakuwaza,kwakunena,kwakutenda,kwakujua/kutojua
Baba wa Mbinguni nasi tunaomba utupe neema ya kuweza kuwasamehe wale wote waliotukosea
Jehovah usitutie majaribu Mungu wetu tunaomba utuepushe na yule mwovu na kazi zake zote
Yahweh tunaomba ututakase miili yetu na akili zetu
Baba wa Mbinguni utufunike kwa Damu ya Bwana na Mwokozi wetu Yesu Kristo wa Nazareti
yeye aliteseka kwanza ili sisi tupate kupona
Kwakupigwa kwake sisi tumepata kupona....

Yesu alifika tena huko mjini Kana, mkoani Galilaya, mahali alipogeuza maji kuwa divai. Kulikuwa na ofisa mmoja aliyekuwa na mtoto mgonjwa huko Kafarnaumu. Basi, huyo ofisa aliposikia kuwa Yesu alikuwa ametoka Yudea na kufika Galilaya, alimwendea akamwomba aende kumponya mtoto wake aliyekuwa mgonjwa mahututi. Yesu akamwambia, “Msipoona ishara na maajabu hamtaamini!” Huyo ofisa akamwambia, “Bwana, tafadhali twende kabla mwanangu hajafa.” Yesu akamwambia, “Nenda tu, mwanao ataishi.” Huyo mtu akaamini maneno ya Yesu, akaenda zake.
Yahweh tunaomba ukabariki kazi za mikono yetu
Baba wa Mbinguni tunaomba ukatupe ubunifu na maarifa 
katika utendaji
Jehovah nasi tukatende sawasawa na mapenzi yako
Baba wa Mbinguni tunaomba ukabariki ridhiki zetu
ziingiazo/zitokazo
Mungu wetu nasi tunaomba ukatupe neema ya kuweza
kuwabariki wenye kuhitaji
Yahweh tusipungukiwe katika mahitaji yetu
Mungu wetu ukatupe kama inavyokupendeza wewe

Baba wa Mbinguni tunayaweka maisha yetu mikononi mwako
Mungu wetu tunaomba ukabariki nyumba/ndoa zetu,
watoto,wazazi wetu,familia/ndugu na wote wanaotuzunguka
Jehovah tunaomba ulinzi wako kwetu na kwa vyote tunavyo vimiliki
Yahweh tunaomba ukatubariki tuingiapo/tutokapo
Mungu wetu tunaomba ukavibariki vyote tunavyoenda kugusa/kutumia
Baba wa Mbinguni ukavitakase kwa Damu ya Bwana wetu Yesu Kristo
Mungu wetu ukatamalaki na kutuatamia
Baba wa Mbinguni tukawe salama rohoni
Mfalme wa amani amani yako ikatawale katika maisha yetu
Mungu wetu ukatupe macho ya kuona na masikio ya kusikia 
sauti yako na kuitii
Baba wa Mbinguni tunaomba ukatupe neema ya kufuata njia zako
Yahweh tukasimamie Neno lako amri na sheria zako siku zote 
za maisha yetu
Mungu wetu ukaonekane katika maisha yetu
Neema zako zikawe nasi Nuru yako ikaangaze katika maisha yetu
ukatuguse kwa mkono wako wenye nguvu
Ukatufanye chombo chema ee Mungu wetu nasi tukatumike kama
inavyokupendeza wewe
Roho Mtakatifu akatuongoze katika yote na tukawe na kiasi...


Alipokuwa bado njiani, watumishi wake walikutana naye, wakamwambia kwamba mwanawe alikuwa mzima. Naye akawauliza saa mtoto alipopata nafuu; nao wakamwambia, “Jana saa saba mchana, homa ilimwacha.” Huyo baba akakumbuka kwamba ilikuwa ni saa ileile ambapo Yesu alimwambia: “Mwanao ataishi.” Hapo yeye akaamini pamoja na jamaa yake yote. Hii ilikuwa ishara ya pili aliyoifanya Yesu alipokuwa anatoka Yudea kwenda Galilaya.
Mungu wetu tunawaweka mikononi mwako wenye shida/tabu,wote wanaopitia magumu/majaribu mbalimbali
Mungu wetu tunaomba ukawaguse kwa mkono wako wenye nguvu
 kila mmoja na mahitaji yake 
Mungu wetu tunaomba ukawasamehe pale walipokwenda kinyume nawe
Baba wa Mbinguni ukawape neema ya kujiombea,kufuata njia zako
wakasimamie Neno lako nalo likaweke huru
Mungu wetu tunaomba ukasikie kuomba kwetu
Mungu wetu ukawatendee sawasawa na mapenzi yako
Kwakuwa Ufalme ni wako Nguvu na Utukufu hata Milele
Amina...!!

Asanteni sana wapendwa katika Kristo Yesu kwakuwa nami
Mungu Baba aendelee kuwabariki na kuwatendea 
kama inavyompendeza yeye....
Nawapenda.



Yerusalemu imezingirwa na maadui
1Enyi watu wa Benyamini,
ondokeni Yerusalemu mkimbilie usalama!
Pigeni tarumbeta mjini Tekoa;
onesheni ishara huko Beth-hakeremu,
maana maafa na maangamizi makubwa
yanakuja kutoka upande wa kaskazini.
2Mji wa Siyoni ni mzuri na mwororo,
lakini utaangamizwa.
3Watu wataujia kama wachungaji na makundi yao,
watapiga hema zao kuuzunguka kila mmoja sehemu yake,
wapate kuyaongoza makundi yao.
4Watasema: “Jitayarisheni kuushambulia Siyoni.
Haya! Tuanze kushambulia adhuhuri!
Bahati mbaya; jua linatua!
Kivuli cha jioni kinarefuka.
5Basi, tutaushambulia usiku;
tutayaharibu majumba yake ya kifalme.”
6Mwenyezi-Mungu wa majeshi asema:
“Kateni miti yake,
rundikeni udongo kuuzingira Yerusalemu.
Mji huu ni lazima uadhibiwe,
maana hamna lolote ndani yake ila dhuluma.
7Kama kisima kinavyohifadhi maji yake yakabaki safi,
ndivyo Yerusalemu unavyohifadhi uovu wako.
Ukatili na uharibifu vyasikika ndani yake,
magonjwa na majeraha yake nayaona daima.
8Hilo na liwe onyo kwako ee Yerusalemu,
la sivyo nitakutupa kabisa kwa chuki;
nikakufanya uwe jangwa,
mahali pasipokaliwa na mtu.”
Watu wasiopenda kusikia
9Mwenyezi-Mungu wa majeshi asema hivi:
“Kusanyeni watu wote wa Israeli waliobaki
kama watu wakusanyavyo zabibu zote;
kama afanyavyo mchumazabibu,
pitisheni tena mikono yenu katika matawi yake.”
10Nitaongea na nani nipate kumwonya,
ili wapate kunisikia?
Tazama, masikio yao yameziba,6:10 yameziba: Kiebrania: Hayajatahiriwa.
hawawezi kusikia ujumbe wako.
Kwao neno lako, ee Mwenyezi-Mungu,
limekuwa jambo la dhihaka,
hawalifurahii hata kidogo.
11Nimejaa hasira ya Mwenyezi-Mungu dhidi yao.
Nashindwa kuizuia ndani yangu.
Mwenyezi-Mungu akaniambia:
“Imwage hasira barabarani juu ya watoto
na pia juu ya makundi ya vijana;
wote, mume na mke watachukuliwa,
kadhalika na wazee na wakongwe.
12Nyumba zao zitapewa watu wengine,
kadhalika na mashamba yao na wake zao;
maana nitaunyosha mkono wangu,
kuwaadhibu wakazi wa nchi hii.
Mimi Mwenyezi-Mungu nimesema.
13Wote, tangu mdogo hadi mkubwa kabisa,
kila mmoja anatamani kupata faida isiyo halali.
Tangu manabii hadi makuhani,
kila mmoja wao ni mdanganyifu.
14Wameliponya jeraha la watu wangu juujuu,
wanasema; ‘Amani, amani’,
kumbe hakuna amani yoyote!
15Je, waliona aibu walipofanya machukizo hayo?
La! Hawakuona aibu hata kidogo.
Hawakujua hata namna ya kuona aibu.
Kwa hiyo wataanguka pamoja na wale waangukao;
wakati nitakapowaadhibu,
wataangamizwa kabisa.
Mimi Mwenyezi-Mungu nimesema.”
Israeli akataa njia ya Mungu
16Mwenyezi-Mungu asema hivi:
“Simameni katika njia panda, mtazame.
Ulizeni mjue juu ya matukio ya zamani.
Tafuteni mahali ilipo njia nzuri
muifuate nanyi mtapumzisha nafsi zenu.
Lakini wao wakasema:
‘Hatutafuata njia hiyo.’
17Kisha nikawawekea walinzi, nikawaambia:
‘Sikilizeni ishara ya tarumbeta.’
Lakini wao wakasema: ‘Hatutaisikiliza.’
18“Kwa hiyo, sikilizeni enyi mataifa;
enyi jumuiya ya watu jueni yatakayowapata.
19Sikiliza ee dunia!
Mimi nitawaletea maafa watu hawa
kulingana na nia zao mbaya.
Maana hawakuyajali maneno yangu,
na mafundisho yangu nayo wameyakataa.
20Ya nini kuniletea ubani kutoka Sheba,
na udi wa harufu nzuri kutoka nchi ya mbali?
Sadaka zenu za kuteketezwa hazikubaliki,
wala tambiko zenu hazinipendezi.
21Kwa hiyo mimi Mwenyezi-Mungu nasema hivi:
Tazama, nitawawekea watu hawa vikwazo
ambavyo vitawakwaza na kuwaangusha chini.
Akina baba na watoto wao wa kiume wataangamia,
kadhalika na majirani na marafiki.”
Mashambulizi kutoka kaskazini
22Mwenyezi-Mungu asema hivi:
“Tazameni, watu wanakuja toka nchi ya kaskazini;
taifa kubwa linajitayarisha kutoka mbali duniani.
23Wamezishika pinde zao na mikuki,
watu wakatili wasio na huruma.
Vishindo vyao ni kama ngurumo ya bahari.
Wamepanda farasi,
wamejipanga tayari kwa vita,
dhidi yako ewe Siyoni!”
24Waisraeli wanasema,
“Tumesikia habari zao,
mikono yetu imelegea;
tumeshikwa na dhiki na uchungu,
kama mwanamke anayejifungua.
25Hatuwezi kwenda mashambani,
wala kutembea barabarani;
maadui wameshika silaha mikononi,
vitisho vimejaa kila mahali.”
26Mwenyezi-Mungu asema,
“Jivikeni mavazi ya gunia, enyi watu wangu
na kugaagaa katika majivu.
Ombolezeni kwa uchungu,
kama mtu anayemwombolezea mwana wa pekee,
maana mwangamizi atakuja,
na kuwashambulia ghafla.
27Yeremia, wewe nimekuweka kuwa mchunguzi
na mpimaji wa watu wangu,
ili uchunguze na kuzijua njia zao.
28Wote ni waasi wakaidi,
ni watu wanaopitapita wakisengenya wengine,
wagumu kama shaba nyeusi au chuma;
wote hutenda kwa ufisadi.
29Mifuo inafukuta kwa nguvu,
risasi inayeyukia humohumo motoni;
ni bure kuendelea kuwatakasa watu wangu,
waovu hawawezi kuondolewa uchafu wao.
30Wataitwa ‘Takataka za fedha’,
maana mimi Mwenyezi-Mungu nimewakataa.”


Yeremia6;1-30

Biblia Habari Njema kwa Watu Wote(BHN)

"Swahili Na Waswahili"Mbarikiwe.

Friday 6 December 2019

Kikombe Cha Asubuhi; Yeremia 5....


Shalom,Habari za Asubuhi,Hamjambo,Mmeamkaje?

Tumshukuru Mungu wetu katika yote...

Asante  Mungu wetu kwa wema na fadhili zako kwetu
Asante kwa ulinzi wako kwetu wakati wote
Asante kwa kutuchagua tena na kutupa
kibali cha kuendelea kuiona leo hii
Asante kwa pumzi/uzima,afya na kuwatayari kwa majukumu yetu


Utukuzwe ee Mungu wetu,usifiwe Baba wa Mbinguni

Neema yako yatutosha  Mungu wetu..!

Nyinyi mwasema: ‘Bado miezi minne tu, na wakati wa mavuno utafika!’ Lakini mimi nawaambieni, angalieni mkaone jinsi mashamba yalivyo tayari kuvunwa. Mvunaji anapata mshahara wake, na anakusanya mavuno kwa ajili ya uhai wa milele; hivyo mpandaji na mvunaji watafurahi pamoja.
Baba wa Mbinguni tunakuja mbele zako tukijinyenyekeza,
tukijishusha na kujiachilia mikononi mwako

Mungu wetu tunaomba utusamehe dhambi zetu zote
Baba wa Mbinguni nasi tunaomba utupe neema ya kuweza kuwasamehe wale wote waliotukosea,Usitutie majaribuni Mungu wetu tunaomba utuepushe na yule mwovu na kazi zake zote,Jehovah ututakase miili yetu na akili zetu Baba wa Mbinguni tunaomba utufunike kwa  Damu ya Bwana na Mwokozi wetu Yesu Kristo wa Nazareti,
Yeye aliteseka kwanza ili sisi tupate kupona....


Kwa sababu hiyo msemo huu ni kweli: ‘Mmoja hupanda na mwingine huvuna.’ Mimi nimewatuma mkavune mavuno ambayo hamkuyatolea jasho; wengine walifanya kazi, lakini nyinyi mnafaidika kutokana na jasho lao.”
Mungu wetu tunaomba ukabariki kazi za mikono yetu
Baba wa Mbinguni tunaomba ukatupe ubunifu na maarifa 
katika utendaji
Jehovah nasi tukatende sawasawa na mapenzi yako
Baba wa Mbinguni tunaomba ukabariki ridhiki zetu
ziingiazo/zitokazo
Mungu wetu nasi tunaomba ukatupe neema ya kuweza
kuwabariki wenye kuhitaji
Yahweh tusipungukiwe katika mahitaji yetu
Mungu wetu ukatupe kama inavyokupendeza wewe



Jehovah tunayaweka maisha yetu mikononi mwako
Baba wa Mbinguni tunaomba ukabariki nyumba/ndoa zetu,
watoto,wazazi wetu,familia/ndugu na wote wanaotuzunguka
Jehovah tunaomba ulinzi wako kwetu na kwa vyote tunavyo vimiliki
Yahweh tunaomba ukatubariki tuingiapo/tutokapo
Mungu wetu tunaomba ukavibariki vyote tunavyoenda kugusa/kutumia
Baba wa Mbinguni ukavitakase kwa Damu ya Bwana wetu Yesu Kristo
Mungu wetu ukatamalaki na kutuatamia
Baba wa Mbinguni tukawe salama rohoni
Mfalme wa amani amani yako ikatawale katika maisha yetu
Mungu wetu ukatupe macho ya kuona na masikio ya kusikia 
sauti yako na kuitii
Baba wa Mbinguni tunaomba ukatupe neema ya kufuata njia zako
Yahweh tukasimamie Neno lako amri na sheria zako siku zote 
za maisha yetu

Mungu  wetu ukaonekane katika maisha yetu popote tupitapo na ikajulikane kwamba upo 

Neema zako zikawe nasi Nuru yako ikaangaze katika maisha yetu
Ukatufanye barua njema ee Mungu wetu nasi tukasomeke kama
inavyokupendeza wewe
Roho Mtakatifu akatuongoze katika yote na tukawe na kiasi...

Wasamaria wengi wa kijiji kile walimwamini kwa sababu ya maneno aliyosema huyo mama: “Ameniambia mambo yote niliyofanya.” Wasamaria walimwendea Yesu wakamwomba akae nao; naye akakaa hapo siku mbili. Watu wengi zaidi waliamini kwa sababu ya ujumbe wake. Wakamwambia yule mama, “Sisi hatuamini tu kwa sababu ya maneno yako; sisi wenyewe tumesikia, na tunajua kwamba huyu ndiye kweli Mwokozi wa ulimwengu.”
Tazama wenye shida/tabu,Mungu wetu tunaomba
 ukawaguse kila mmoja na mahitaji yake
Baba wa Mbinguni tunaomba ukawasamehe pale walipokwenda
kinyume nawe
Mungu wetu ukawape neema ya kujiombea,macho ya rohoni,masikio yakusikia sauti yako,wakafuate njia zako nazo zikawaweke huru
Mungu wetu tunaomba ukasikie kulia kwao
Baba wa Mbinguni tunomba ukawafute machozi yao
Nuru yako ikaangaze katika maisha yao
Mungu wetu tunaomba ukawatendee sawasawa na mapenzi yako
Kwakuwa Ufalme ni wako Nguvu na Utukufu hata Milele
Amina....!!!


Wapendwa katika Kristo Yesu asanteni sana
kwakuwanami/kunisoma

Mungu Baba aendelee kuwabariki na kuwatendea
kama inavyompendeza yeye
Amani ya Bwana wetu Yesu Kristo na upendo wa Mungu Baba
ukae nanyi daima....

Nawapenda.


Dhambi ya Yerusalemu
1Kimbieni huko na huko mjini Yerusalemu;
pelelezeni na kujionea wenyewe!
Chunguzeni masoko yake
mwone kama kuna mtu atendaye haki
mtu atafutaye ukweli;
akiwako, basi Mwenyezi-Mungu atausamehe Yerusalemu.
2Ingawa wanaapa: “Kama Mwenyezi-Mungu aishivyo”,
viapo vyao ni vya uongo.
3Ee Mwenyezi-Mungu, wewe watafuta daima uaminifu.
Umewatwanga, lakini hawakuona uchungu;
umewateketeza, lakini walikataa kukosolewa.
Wamezifanya nyuso zao kuwa ngumu kuliko mwamba;
wamekataa kabisa kurudi kwako.
4Ndipo nilipowaza:
“Hawa ni watu duni hawana akili;
hawajui matakwa ya Mwenyezi-Mungu,
hawajui Sheria ya Mungu wao.
5Nitawaendea wakuu niongee nao;
bila shaka, wao wanajua matakwa ya Mwenyezi-Mungu;
wanajua sheria ya Mungu wao.”
Lakini wote waliivunja nira yao.
Waliikatilia mbali minyororo yao.
6Kwa hiyo simba kutoka msituni atawaua;
mbwamwitu kutoka jangwani atawararua.
Chui anaivizia miji yao.
Kila atokaye humo atararuliwa vipandevipande,
kwa sababu dhambi zao ni nyingi,
maasi yao ni makubwa.
7Mwenyezi-Mungu anauliza:
“Nitawezaje kukusamehe ee Yerusalemu?
Watu wako wameniasi;
wameapa kwa miungu ya uongo.
Nilipowashibisha kwa chakula,
wao walifanya uzinzi,
wakajumuika majumbani mwa makahaba.
8Walikuwa kama farasi walioshiba wenye tamaa,
kila mmoja akimtamani mke wa jirani yake.
9Je, nisiwaadhibu kwa mambo haya yote?
Nisilipize kisasi juu ya taifa kama hili?
10“Pandeni mpite katika mashamba yake ya mizabibu
mkaharibu kila kitu bila kumaliza kabisa.
Yakateni matawi yake,
kwani hayo si yangu mimi Mwenyezi-Mungu.
11Naam, watu wa Israeli na watu wa Yuda,
wamekosa kabisa uaminifu kwangu.
Mimi Mwenyezi-Mungu nimesema.”
Matokeo ya kuachwa na Mungu
12Wamesema uongo juu ya Mwenyezi-Mungu
wamesema: “Hatafanya kitu;
hatutapatwa na uovu wowote;
hatutashambuliwa wala kuona njaa.
13Manabii si kitu, ni upepo tu;
maana neno lake Mungu halimo ndani yao.”
Basi hayo na yawapate wao wenyewe!
14Mwenyezi-Mungu wa majeshi asema hivi:
“Kwa kuwa wao wamesema jambo hilo,
sasa nitayafanya maneno niliyokupa wewe Yeremia kuwa moto.
Watu hawa watakuwa kuni,
na moto huo utawateketeza.
15“Nami Mwenyezi-Mungu nasema juu yenu enyi Waisraeli:
Mimi naleta taifa moja kutoka mbali,
lije kuwashambulia.
Taifa ambalo halishindiki,
taifa ambalo ni la zamani,
ambalo lugha yake hamuifahamu,
wala hamwezi kuelewa wasemacho.
16Mishale yao husambaza kifo;
wote ni mashujaa wa vita.
17Watayala mazao yenu na chakula chenu;
watawamaliza watoto wenu wa kike na wa kiume.
Watachinja makundi yenu ya kondoo na ng'ombe;
wataiharibu mizabibu yenu na mitini yenu.
Miji yenu ya ngome mnayoitegemea,
wataiharibu kwa silaha zao.
18“Lakini, hata katika siku hizo mimi Mwenyezi-Mungu nasema, sitawaangamiza na kuwamaliza kabisa. 19Na watu wenu watakapouliza ‘Kwa nini Mwenyezi-Mungu, Mungu wetu, ametutendea mambo hayo yote?’ Wewe utawaambia, ‘Nyinyi mlimwacha Mwenyezi-Mungu, mkaitumikia miungu ya kigeni katika nchi yenu. Basi ndivyo mtakavyowatumikia watu wengine katika nchi isiyo yenu.’
Mungu awaonya watu wake
20“Watangazie wazawa wa Yakobo,
waambie watu wa Yuda hivi:
21Sikilizeni enyi wajinga na wapumbavu;
watu mlio na macho, lakini hamwoni,
mlio na masikio, lakini hamsikii.
22Mbona hamniogopi? Nauliza mimi Mwenyezi-Mungu!
Kwa nini hamtetemeki mbele yangu?
Mimi niliweka mchanga uwe mpaka wa bahari,
kizuizi cha daima ambacho bahari haiwezi kuvuka.
Ingawa mawimbi yanaupiga, hayawezi kuupita;
ingawa yananguruma, hayawezi kuuruka.
23Lakini watu hawa wana moyo wa ukaidi na uasi;
wameniacha wakaenda zao.
24Wala hawasemi mioyoni mwao;
‘Na tumche Mwenyezi-Mungu, Mungu wetu,
anayetujalia mvua kwa wakati wake,
anayetupatia mvua za masika na mvua za vuli;
na kutupa majira maalumu ya mavuno.’
25Makosa yenu yamewazuia msipate baraka hizo,
dhambi zenu zimewafanya msipate mema.
26Naam, kuna walaghai miongoni mwa watu wangu,
watu ambao hunyakua mali za wengine.
Wako kama wawindaji wa ndege:
Hutega mitego yao na kuwanasa watu.
27Kama vile kapu lililojaa ndege walionaswa,
ndivyo nyumba zao zilivyojaa mali za udanganyifu.
Ndiyo maana wamekuwa watu wakubwa na matajiri,
28wamenenepa na kunawiri.
Katika kutenda maovu hawana kikomo
hawahukumu yatima kwa haki wapate kufanikiwa,
wala hawatetei haki za watu maskini.
29“Je, nisiwaadhibu kwa mambo haya?
Je nitaacha kulipiza kisasi taifa kama hili?
30Jambo la ajabu na la kuchukiza
limetokea katika nchi hii:
31Manabii wanatabiri mambo ya uongo,
makuhani nao hutafuta faida yao wenyewe;5:31 hutafuta faida yao wenyewe: Tafsiri ya maneno magumu na ya pekee ya Kiebrania.
na watu wangu wanaona jambo hilo kuwa sawa. Lakini mwisho utakapofika mtafanyaje?”

Yeremia5;1-31

Biblia Habari Njema kwa Watu Wote(BHN)

"Swahili Na Waswahili"Mbarikiwe.