Swahili na Waswahili

Swahili na Waswahili
Waswahili na Mswahili Rachel Siwa...Pamoja Daima!!

Tuesday 19 November 2019

Kikombe Cha Asubuhi;Isaya 58....


Shalom,Habari za Asubuhi,Hamjambo,Mmeamkaje?

Tumshukuru Mungu katika yote....

Mungu wetu Baba yetu,Muumba wetu Muumba wa Mbingu na Nchi
Muumba wa vyote vilivyomo vinavyoonekana na visivyoonekana
Mungu wa walio hai,Mungu  mwenye huruma,Mungu wa upendo
Mungu wa Abrahamu,Isaka na Yakobo...
Asante kwa wema na fadhili zako kwetu
Asante kwa ulinzi wako kwetu wakati wote
Asante kwa kutuchagua tena na kutupa
kibali cha kuendelea kuiona leo hii
Asante kwa pumzi/uzima,afya na kuwatayari kwa majukumu yetu

Neema yako yatutosha ee Mungu wetu....!!

Tulijaribu kuuponya Babuloni, lakini hauwezi kuponywa. Uacheni, twendeni zetu, kila mmoja katika nchi yake, maana hukumu yake ni kuu mno imeinuka mpaka mawinguni. Mwenyezi-Mungu amethibitisha kuwa hatuna hatia. Twendeni Siyoni tukatangaze matendo ya Mwenyezi-Mungu, Mungu wetu.
Baba wa Mbinguni tunakuja mbele zako tukijinyenyekeza,tukijishusha na kujiachilia mikononi mwako
Mungu wetu tunaomba utusamehe dhambi zetu zote 
Baba wa Mbinguni nasi tunaomba ukatupe neema
ya kuweza kuwasamehe wale wote waliotukosea
Usitutie majaribuni Mungu wetu tunaomba utuepushe
na yule mwovu na kazi zake zote
Jehovah ututakase miili yetu na akili zetu
Baba wa Mbinguni tunaomba utufunike kwa Damu
ya Bwana na Mwokozi wetu Yesu Kristo wa Nazareti
yeye aliteseka kwanza ili sisi tupate kupona....


Mwenyezi-Mungu amezichochea roho za wafalme wa Media, kwa maana amenuia kuiangamiza Babuloni. Naam, hicho ndicho kisasi cha Mwenyezi-Mungu; analipiza kisasi kwa ajili ya hekalu lake. Noeni mishale yenu! Chukueni ngao! Twekeni bendera ya vita kushambulia kuta za Babuloni. Imarisheni ulinzi; wekeni walinzi; tayarisheni mashambulizi. Mwenyezi-Mungu amepanga na kutekeleza mambo aliyosema juu ya wakazi wa Babuloni.
Mungu wetu tunaomba ukabariki kazi za mikono yetu
Baba wa Mbinguni tunaomba ukatupe ubunifu na maarifa katika utendaji
Jehovah nasi tukatende sawasawa na mapenzi yako
Yahweh tunaomba ukabariki ridhiki zetu ziingiazo/zitokazo
Mungu wetu nasi tunaomna ukatupe neema ya kuweza kuwabariki wenye kuhitaji
Tusipungukiwe katika mahitaji yetu
Baba wa Mbinguni tunaomba ukatupe kama inavyokupendeza wewe...


Yahweh tunayaweka maisha yetu mikononi mwako
Mungu wetu tunaomba ukabariki nyumba/ndoa zetu,
Jehovah tunaomba ulinzi wako kwetu na kwa vyote tunavyovimiliki
Yahweh tunaomba ukatubariki tuingiapo/tutokapo
Mungu wetu tunaomba ukavibariki vyote tunavyoenda kugusa/kutumia
Baba wa Mbinguni ukavitakase kwa Damu ya Bwana wetu Yesu Kristo
Mungu wetu ukatamalaki na kutuatamia
Baba wa Mbinguni tukawe salama rohoni
Yahwe ukatupe akili ya kutambua mema na mabaya
Mfalme wa amani amani yako ikatawale katika maisha yetu
Mungu wetu ukatupe macho ya kuona,masikio ya kusikia sauti yako na kuitii..
Baba wa Mbinguni  tunaomba ukatupe neema ya kufuata
njia zako,tukasimamie Neno lako,amri na sheria zako
siku zote za maisha yetu...
Ukatuguse kwa mkono wako wenye nguvu,ukatufanye chombo chema
ee Mungu wetu nasi tukatumike kama inavyokupendeza wewe
Roho Mtakatifu akatuongoze katika yote na tukawe na kiasi....


Nchi hiyo imejaa mito na hazina tele, lakini mwisho wake umefika, uzi wa uhai wake umekatwa. Mwenyezi-Mungu wa majeshi ameapa kwa nafsi yake: “Hakika nitakujaza majeshi mengi kama nzige, nayo yatapiga vigelegele vya ushindi juu yako”
Tazama watoto wako wenye shida/tabu,wote wanaopitia magumu/majaribu mbalimbali
Mungu wetu tunaomba ukawaguse kwa mkono wako wenye nguvu
kila mmoja na mahitaji yake
Mungu wetu tunaomba ukawasamehe pale walipo kwenda kinyume nawe
Yahweh tunaomba ukawape neema ya kuweza kujiombea,kufuata njia zako nazo zikawaweke huru...
Baba wa Mbinguni tunayaweka haya yote mikononi mwako
Kwakuwa Ufalme ni wako Nguvu na Utukufu hata Milele...
Amina...!!


Asanteni sana wapendwa katika Kristo Yesu kwakuwa nami,Baba wa Mbinguni aendelee kuwatendea sawasawa na mapenzi yake...
Nawapenda.

Mfungo wa kweli
1Mwenyezi-Mungu asema:
“Piga kelele, wala usijizuie;
paza sauti yako kama tarumbeta.
Watangazie watu wangu makosa yao,
waambie wazawa wa Yakobo dhambi zao.
2Siku hata siku wananijia kuniabudu,
wanatamani kujua mwongozo wangu,
kana kwamba wao ni taifa litendalo haki,
taifa lisilosahau sheria za Mungu wao.
Wananitaka niamue kwa haki,
na kutamani kukaa karibu na Mungu.
3“Nyinyi mnaniuliza:
‘Mbona tunafunga lakini wewe huoni?
Mbona tunajinyenyekesha, lakini wewe hujali?’
“Ukweli ni kwamba wakati mnapofunga,
mnatafuta tu furaha yenu wenyewe,
na kuwakandamiza wafanyakazi wenu!
4Mnafunga, na kugombana na kupigana ngumi.
Mkifunga namna hiyo
maombi yenu hayatafika kwangu juu.
5Mfungapo, nyinyi mnajitaabisha;
mnaviinamisha vichwa vyenu kama unyasi,
na kulalia nguo za magunia na majivu.
Je, huo ndio mnaouita mfungo?
Je, hiyo ni siku inayokubaliwa nami?
6“La! Mfungo ninaotaka mimi ni huu:
Kuwafungulia waliofungwa bila haki,
kuziondoa kamba za utumwa,
kuwaachia huru wanaokandamizwa,
na kuvunjilia mbali udhalimu wote!
7 58:7 Taz Mat 25:35 Mfungo wa kweli ni kuwagawia wenye njaa chakula chako,
kuwakaribisha nyumbani kwako maskini wasio na makao,
kuwavalisha wasio na nguo,
bila kusahau kuwasaidia jamaa zenu.
8“Mkifanya hivyo mtangara kama pambazuko,
mkiwa wagonjwa mtapona haraka.
Matendo yenu mema yatawatangulia,
nami nitawalindeni kutoka nyuma kwa utukufu wangu.
9Ndipo mtakapoomba,
nami Mwenyezi-Mungu nitawaitikia;
mtalia kwa sauti kuomba msaada,
nami nitajibu, ‘Niko hapa!’
“Kama mkiiondoa dhuluma kati yenu,
mkiacha kudharau wengine na kusema maovu,
10mkiwapa chakula kwa ukarimu wenye njaa,
mkitosheleza mahitaji ya wenye dhiki,
mwanga utawaangazia nyakati za giza,
giza lenu litakuwa kama mchana.
11Mimi Mwenyezi-Mungu nitawaongozeni daima,
nitatosheleza mahitaji yenu wakati wa shida.58:11 maana ya neno hili Kiebrania si dhahiri.
Nitawaimarisha mwilini,
nanyi mtakuwa kama bustani iliyomwagiliwa maji,
kama chemchemi ya maji
ambayo maji yake hayakauki kamwe.
12Magofu yenu ya kale yatajengwa;
mtajenga upya juu ya misingi iliyoachwa zamani.
Nanyi mtaitwa watu waliotengeneza upya kuta,
watu waliozifanya barabara za mji zipitike tena.
Tuzo kwa kuiadhimisha Sabato
13“Kama ukiacha kufanya kazi siku ya Sabato,
ukaacha shughuli zako siku yangu hiyo takatifu;
kama ukiifanya siku yangu kuwa ya furaha,
ukaiheshimu siku hiyo takatifu ya Mwenyezi-Mungu,
ukaacha na shughuli58:13 shughuli: Au anasa. zako na kupiga domo,
14utapata furaha yako kwangu mimi Mwenyezi-Mungu,
nitakupatia ushindi katika kila pingamizi nchini,
nitakulisha mali ya Yakobo, babu yako.
Mimi, Mwenyezi-Mungu, nimesema.”


Isaya58;1-14

Biblia Habari Njema kwa Watu Wote(BHN)

"Swahili Na Waswahili"Mbarikiwe.

Monday 18 November 2019

Kikombe Cha Asubuhi;Isaya 57....


Shalom,Habari za Asubuhi,Hamjambo,Mmeamkaje?

Haleluyah ni siku/wiki
Nyingine tena Mungu wetu ametuchagua

na kutupa kibali cha kuendelea kuiona leo hii
Si kwamba sisi tumetenda mema sana wala si kwa nguvu zetu
si kwa utashi wetu wala si kwa akili zetu si kwamba sisi
ni wazuri mno si kwa uwezo wetu sisi kuwa hivi tulivyo leo hii
Ni kwa rehema/neema zake ni kwa mapenzi yake Mungu wetu....

Tumshukuru Mungu wetu katika yote...

Asante Mungu wetu kwa wema na fadhili zako kwetu

Asante kwa ulinzi wako kwetu wakati wote
Asante kwa pumzi/uzima,afya na kuwa tayari kwa majukumu yetu
Sifa na Utukufu tunakurudshia Mungu wetu....!!

Mwenyezi-Mungu asema hivi: “Nitachochea upepo wa kuangamiza dhidi ya Babuloni, dhidi ya wakazi wa Kaldayo. Nitawapeleka wapepetaji Babuloni, nao watampepeta; watamaliza kila kitu katika nchi yake watakapofika kuishambulia toka kila upande wakati wa maangamizi yake.” Usiwape nafasi wapiga mshale wa Babuloni; usiwaache wavute upinde, wala kuvaa mavazi yao ya vita. Usiwahurumie vijana wake; liangamize kabisa jeshi lake.
Tazama jana imepita ee Mungu wetu leo ni siku mpya na kesho ni siku nyingine Jehovah tunakuja mbele zako tukijinyenyekeza,tukijishusha na kujiachilia mikononi mwako
 Mungu wetu tunaomba utusamehe dhambi zetu zote tulizozifanya kwakuwaza,kwakunena,kwakutenda,kwakujua/kutojua
Baba wa Mbinguni nasi tunaomba utupe neema ya kuweza kuwasamehe wale wote waliotukosea
Jehovah usitutie majaribu Mungu wetu tunaomba utuepushe na yule mwovu na kazi zake zote
Yahweh tunaomba ututakase miili yetu na akili zetu
Baba wa Mbinguni utufunike kwa Damu ya Bwana na Mwokozi wetu Yesu Kristo wa Nazareti
yeye aliteseka kwanza ili sisi tupate kupona
Kwakupigwa kwake sisi tumepata kupona....

Wataanguka na kuuawa katika nchi ya Wakaldayo, watajeruhiwa katika barabara zake. Lakini Israeli na Yuda hawakuachwa na Mungu wao Mwenyezi-Mungu wa majeshi, ingawa nchi yao imejaa hatia mbele yake yeye Mtakatifu wa Israeli. Kimbieni kutoka Babuloni, kila mtu na ayaokoe maisha yake! Msiangamizwe katika adhabu yake, maana huu ndio wakati wa Mungu wa kulipa kisasi, anaiadhibu Babuloni kama inavyostahili.
Yahweh tunaomba ukabariki kazi za mikono yetu
Baba wa Mbinguni tunaomba ukatupe ubunifu na maarifa 
katika utendaji
Jehovah nasi tukatende sawasawa na mapenzi yako
Baba wa Mbinguni tunaomba ukabariki ridhiki zetu
ziingiazo/zitokazo
Mungu wetu nasi tunaomba ukatupe neema ya kuweza
kuwabariki wenye kuhitaji
Yahweh tusipungukiwe katika mahitaji yetu
Mungu wetu ukatupe kama inavyokupendeza wewe

Baba wa Mbinguni tunayaweka maisha yetu mikononi mwako
Mungu wetu tunaomba ukabariki nyumba/ndoa zetu,
watoto,wazazi wetu,familia/ndugu na wote wanaotuzunguka
Jehovah tunaomba ulinzi wako kwetu na kwa vyote tunavyo vimiliki
Yahweh tunaomba ukatubariki tuingiapo/tutokapo
Mungu wetu tunaomba ukavibariki vyote tunavyoenda kugusa/kutumia
Baba wa Mbinguni ukavitakase kwa Damu ya Bwana wetu Yesu Kristo
Mungu wetu ukatamalaki na kutuatamia
Baba wa Mbinguni tukawe salama rohoni
Mfalme wa amani amani yako ikatawale katika maisha yetu
Mungu wetu ukatupe macho ya kuona na masikio ya kusikia 
sauti yako na kuitii
Baba wa Mbinguni tunaomba ukatupe neema ya kufuata njia zako
Yahweh tukasimamie Neno lako amri na sheria zako siku zote 
za maisha yetu
Mungu wetu ukaonekane katika maisha yetu
Neema zako zikawe nasi Nuru yako ikaangaze katika maisha yetu
ukatuguse kwa mkono wako wenye nguvu
Ukatufanye chombo chema ee Mungu wetu nasi tukatumike kama
inavyokupendeza wewe
Roho Mtakatifu akatuongoze katika yote na tukawe na kiasi...


Babuloni ilikuwa kikombe cha dhahabu mkononi mwa Mwenyezi-Mungu, ambacho kiliilewesha dunia nzima. Mataifa yalikunywa divai yake, hata yakapatwa wazimu. Ghafla Babuloni imeanguka na kuvunjikavunjika; ombolezeni kwa ajili yake! Leteni dawa kutuliza maumivu yake; labda utaweza kuponywa.
Mungu wetu tunawaweka mikononi mwako wenye shida/tabu,wote wanaopitia magumu/majaribu mbalimbali
Mungu wetu tunaomba ukawaguse kwa mkono wako wenye nguvu
 kila mmoja na mahitaji yake 
Mungu wetu tunaomba ukawasamehe pale walipokwenda kinyume nawe
Baba wa Mbinguni ukawape neema ya kujiombea,kufuata njia zako
wakasimamie Neno lako nalo likaweke huru
Mungu wetu tunaomba ukasikie kuomba kwetu
Mungu wetu ukawatendee sawasawa na mapenzi yako
Kwakuwa Ufalme ni wako Nguvu na Utukufu hata Milele
Amina...!!

Asanteni sana wapendwa katika Kristo Yesu kwakuwa nami
Mungu Baba aendelee kuwabariki na kuwatendea 
kama inavyompendeza yeye....
Nawapenda.


Onyo dhidi ya ibada za sanamu
1Mtu mwadilifu akifa,
hakuna mtu anayejali;
mtu mwema akifariki,
hakuna mtu anayefikiri na kusema:
“Mtu huyo mwema ameondolewa asipatwe na maafa,
2ili apate kuingia kwenye amani.”
Watu wanaofuata njia ya haki,
watakuwa na amani na kupumzika.
3Lakini Mwenyezi-Mungu asema:
“Njoni hapa nyinyi wana wa wachawi;
nyinyi wazawa wa wachawi, wazinzi na malaya.
4Je, mnadhani mnamdhihaki nani?
Mnamfyonya nani na kumtolea ulimi?
Nyinyi wenyewe ni wahalifu tangu mwanzo,
nyinyi ni kizazi kidanganyifu.
5Nyinyi mnawaka tamaa kwenye miti ya mialoni,
na katika kila mti wa majani mabichi.
Mnawachinja watoto wenu
na kuwatambika katika mabonde na nyufa za majabali.
6Mnachagua mawe laini mabondeni,
na kuyafanya kitovu cha maisha yenu.
Mnayamiminia tambiko ya kinywaji
na kuyapelekea tambiko ya nafaka!
Je, mimi nitaridhishwa kwa vitu hivyo?
7Mmeweka vitanda vyenu juu ya milima mikubwa,
na kwenda huko kutoa tambiko.
8Nyuma ya milango na miimo
mmetundika kinyago chenu.
Nyinyi mnaniacha mimi
na kutandika na kuvipanua vitanda vyenu.
Mnafanya mapatano na hao mliopenda vitanda vyao.
Humo mnazitosheleza tamaa zenu mbaya,
huku mnakodolea macho kinyago chenu.57:8 huku … chenu: Maana katika Kiebrania si dhahiri.
9Mnajitia marashi na manukato kwa wingi
kisha mnakwenda kumwabudu Moleki.57:9 Moleki: Au Mfalme.
Mnawatuma wajumbe wenu huko na huko,
kujitafutia miungu ya kuabudu;
hata kuzimu walifika.
10Mlichoshwa na safari zenu ndefu,
hata hivyo hamkukata tamaa;
mlijipatia nguvu mpya,
ndiyo maana hamkuzimia.
11“Mlimwogopa na kutishwa na nani
hata mkasema uongo,
mkaacha kunikumbuka mimi
na kuacha kabisa kunifikiria?
Mimi sikuwaambia kitu kwa muda mrefu;
ndio maana labda mkaacha kuniheshimu!
12Mnafikiri mnafanya sawa,
lakini nitayafichua matendo yenu,
nayo miungu yenu haitawafaa kitu.
13Mtakapolia kuomba msaada,
rundo la vinyago vyenu na liwaokoe!
Upepo utavipeperushia mbali;
naam, pumzi itavitupilia mbali.
Lakini watakaokimbilia usalama kwangu,
wataimiliki nchi,
mlima wangu mtakatifu utakuwa mali yao.”
Huruma ya Mungu
14Mwenyezi-Mungu asema hivi:
“Jengeni! Jengeni! Tayarisheni njia!
Ondoeni vikwazo vyote njiani mwa watu wangu!”
15Hivi ndivyo asemavyo Mungu aliye juu kabisa,
aishiye milele na ambaye jina lake ni “Mtakatifu”:
“Mimi nakaa huko juu, mahali patakatifu,
nakaa pia na wenye majuto na wanyenyekevu.
Mimi nitawatia moyo walio wanyenyekevu
na kuwapa nguvu wenye majuto.
16Maana sitaendelea kuwalaumu
wala kuwakasirikia daima.
La sivyo hao niliowaumba watadhoofika mbele yangu,
nami ndiye niliyewapa pumzi yangu ya uhai.
17Niliwakasirikia kwa sababu ya uovu na tamaa zao;
niliwaadhibu, nikauficha uso wangu na kukasirika.
Lakini wao waliendelea kufuata njia zao wenyewe.
18Niliiona mienendo yao, lakini nitawaponya;
nitawaongoza na kuwapa faraja,
nitawatuliza hao wanaoomboleza.
19Mimi nitawapa amani,
amani kwa walio mbali na walio karibu!
Mimi nitawaponya.
20Lakini waovu ni kama bahari iliyochafuka,
ambayo haiwezi kutulia;
mawimbi yake hutupa tope na takataka.”
21Mungu wangu asema hivi:
“Watu waovu sitawapa amani.”



Isaya57;1-21

Biblia Habari Njema kwa Watu Wote(BHN)

"Swahili Na Waswahili"Mbarikiwe.

Friday 15 November 2019

Kikombe Cha Asubuhi;Isaya 56....


Shalom,Habari za Asubuhi,Hamjambo,Mmeamkaje?

Tumshukuru Mungu wetu katika yote...

Asante  Mungu wetu kwa wema na fadhili zako kwetu
Asante kwa ulinzi wako kwetu wakati wote
Asante kwa kutuchagua tena na kutupa
kibali cha kuendelea kuiona leo hii
Asante kwa pumzi/uzima,afya na kuwatayari kwa majukumu yetu


Utukuzwe ee Mungu wetu,usifiwe Baba wa Mbinguni

Neema yako yatutosha  Mungu wetu..!



Kwa nguvu yako uliisimika milima mahali pake. Wewe una nguvu mno! Watuliza mshindo wa bahari na wa mawimbi yake, wakomesha ghasia za watu. Ulimwengu wote washangazwa na matendo yako. Wasababisha furaha kila mahali, toka mashariki hata magharibi.
Baba wa Mbinguni tunakuja mbele zako tukijinyenyekeza,
tukijishusha na kujiachilia mikononi mwako

Mungu wetu tunaomba utusamehe dhambi zetu zote
Baba wa Mbinguni nasi tunaomba utupe neema ya kuweza kuwasamehe wale wote waliotukosea,Usitutie majaribuni Mungu wetu tunaomba utuepushe na yule mwovu na kazi zake zote,Jehovah ututakase miili yetu na akili zetu Baba wa Mbinguni tunaomba utufunike kwa  Damu ya Bwana na Mwokozi wetu Yesu Kristo wa Nazareti,
Yeye aliteseka kwanza ili sisi tupate kupona....


Wewe waitunza nchi kwa kuinyeshea mvua, waijalia rutuba na kuistawisha; mto wako umejaa maji tele, waifanikisha nchi na kuipatia mavuno. Hivi ndivyo uitengenezavyo nchi: Mashamba wayanyeshea mvua kwa wingi, na kuyalowanisha kwa maji; ardhi wailainisha kwa manyunyu, na kuibariki mimea ichipue.
Mungu wetu tunaomba ukabariki kazi za mikono yetu
Baba wa Mbinguni tunaomba ukatupe ubunifu na maarifa 
katika utendaji
Jehovah nasi tukatende sawasawa na mapenzi yako
Baba wa Mbinguni tunaomba ukabariki ridhiki zetu
ziingiazo/zitokazo
Mungu wetu nasi tunaomba ukatupe neema ya kuweza
kuwabariki wenye kuhitaji
Yahweh tusipungukiwe katika mahitaji yetu
Mungu wetu ukatupe kama inavyokupendeza wewe



Jehovah tunayaweka maisha yetu mikononi mwako
Baba wa Mbinguni tunaomba ukabariki nyumba/ndoa zetu,
watoto,wazazi wetu,familia/ndugu na wote wanaotuzunguka
Jehovah tunaomba ulinzi wako kwetu na kwa vyote tunavyo vimiliki
Yahweh tunaomba ukatubariki tuingiapo/tutokapo
Mungu wetu tunaomba ukavibariki vyote tunavyoenda kugusa/kutumia
Baba wa Mbinguni ukavitakase kwa Damu ya Bwana wetu Yesu Kristo
Mungu wetu ukatamalaki na kutuatamia
Baba wa Mbinguni tukawe salama rohoni
Mfalme wa amani amani yako ikatawale katika maisha yetu
Mungu wetu ukatupe macho ya kuona na masikio ya kusikia 
sauti yako na kuitii
Baba wa Mbinguni tunaomba ukatupe neema ya kufuata njia zako
Yahweh tukasimamie Neno lako amri na sheria zako siku zote 
za maisha yetu

Mungu  wetu ukaonekane katika maisha yetu popote tupitapo na ikajulikane kwamba upo 

Neema zako zikawe nasi Nuru yako ikaangaze katika maisha yetu
Ukatufanye barua njema ee Mungu wetu nasi tukasomeke kama
inavyokupendeza wewe
Roho Mtakatifu akatuongoze katika yote na tukawe na kiasi...


Wautunukia mwaka wote mema yako, kila ulipopitia pamejaa fanaka. Mbuga za majani zimejaa mifugo, milima nayo imejaa furaha. Malisho yamejaa kondoo, mabonde yamefunikwa kwa ngano. Kila kitu kinashangilia kwa furaha.
Tazama wenye shida/tabu,Mungu wetu tunaomba
 ukawaguse kila mmoja na mahitaji yake
Baba wa Mbinguni tunaomba ukawasamehe pale walipokwenda
kinyume nawe
Mungu wetu ukawape neema ya kujiombea,macho ya rohoni,masikio yakusikia sauti yako,wakafuate njia zako nazo zikawaweke huru
Mungu wetu tunaomba ukasikie kulia kwao
Baba wa Mbinguni tunomba ukawafute machozi yao
Nuru yako ikaangaze katika maisha yao
Mungu wetu tunaomba ukawatendee sawasawa na mapenzi yako
Kwakuwa Ufalme ni wako Nguvu na Utukufu hata Milele
Amina....!!!


Wapendwa katika Kristo Yesu asanteni sana
kwakuwanami/kunisoma

Mungu Baba aendelee kuwabariki na kuwatendea
kama inavyompendeza yeye
Amani ya Bwana wetu Yesu Kristo na upendo wa Mungu Baba
ukae nanyi daima....

Nawapenda.

Wote wanakaribishwa
1Mwenyezi-Mungu asema:
“Zingatieni haki na kutenda mema,
maana nitawaokoeni hivi karibuni,
watu wataona wazi kwamba ninawakomboeni.
2Heri mtu anayezingatia kikamilifu ninayosema,
anayeshika sheria ya Sabato kwa heshima
na kuepa kutenda uovu wowote.
3“Mgeni anayenitambua mimi Mwenyezi-Mungu asifikiri:
‘Hakika Mwenyezi-Mungu atanitenga na watu wake.’
Naye towashi asiseme:
‘Mimi ni mti mkavu tu!’
4Maana mimi Mwenyezi-Mungu nasema:
Towashi ashikaye sheria zangu za Sabato,
anayefanya mambo yanayonipendeza,
na kulizingatia agano langu,
5nitampa nafasi maalumu na ya sifa
katika nyumba yangu na kuta zake;
nafasi bora kuliko kuwa na watoto wa kiume na wa kike:
Nitampa jina la kukumbukwa daima,
na ambalo halitafutwa kamwe.
6“Watu wageni watakaonikiri mimi Mwenyezi-Mungu,
watakaoniheshimu, wakapenda jina langu na kuwa watumishi wangu,
wote watakaoshika Sabato bila kuikufuru,
watu watakaozingatia agano langu,
7hao nitawaleta katika mlima wangu mtakatifu,
na kuwafurahisha katika nyumba yangu ya sala;
tambiko na sadaka zao zitakubaliwa madhabahuni pangu.
Maana nyumba yangu itaitwa:
‘Nyumba ya sala kwa ajili ya watu wote’.
8“Hii ni kauli yangu mimi Bwana Mwenyezi-Mungu
ninayewakusanya Waisraeli waliotawanyika.
Licha ya hao niliokwisha kukusanya,
nitawakusanya watu wengine wajumuike nao.”
Viongozi wa Israeli walaumiwa
9Enyi wanyama wote wakali,
nanyi wanyama wote wa mwituni,
njoni muwatafune watu wangu.
10Maana viongozi wao wote ni vipofu;
wote hawana akili yoyote.
Wote ni kama mbwa bubu wasiobweka,
hulala tu na kuota ndoto,
hupenda sana kusinzia!
11Hao ni kama mbwa wenye uchu sana,
wala hawawezi kamwe kutoshelezwa.
Wachungaji hao hawana akili yoyote;
kila mmoja hutafuta faida yake mwenyewe.
12Huambiana, “Njoni, twende kutafuta divai;
njoni tunywe tushibe pombe!
Kesho itakuwa kama leo,
tena itakuwa sikukuu kubwa zaidi.”


Isaya56;1-12

Biblia Habari Njema kwa Watu Wote(BHN)

"Swahili Na Waswahili"Mbarikiwe.

Thursday 14 November 2019

Kikombe Cha Asubuhi;Isaya 55....


Shalom,Habari za Asubuhi,Hamjambo,Mmeamkaje?

Tumshukuru Mungu katika yote....

Mungu wetu Baba yetu,Muumba wetu Muumba wa Mbingu na Nchi
Muumba wa vyote vilivyomo vinavyoonekana na visivyoonekana
Mungu wa walio hai,Mungu  mwenye huruma,Mungu wa upendo
Mungu wa Abrahamu,Isaka na Yakobo...
Asante kwa wema na fadhili zako kwetu
Asante kwa ulinzi wako kwetu wakati wote
Asante kwa kutuchagua tena na kutupa
kibali cha kuendelea kuiona leo hii
Asante kwa pumzi/uzima,afya na kuwatayari kwa majukumu yetu

Neema yako yatutosha ee Mungu wetu....!!

Wastahili sifa, ee Mungu, huko Siyoni, watu watakutimizia wewe ahadi zao, maana wewe wajibu sala zetu. Binadamu wote watakujia wewe.
Baba wa Mbinguni tunakuja mbele zako tukijinyenyekeza,
tukijishusha na kujiachilia mikononi mwako

Mungu wetu tunaomba utusamehe dhambi zetu zote 
Baba wa Mbinguni nasi tunaomba ukatupe neema
ya kuweza kuwasamehe wale wote waliotukosea
Usitutie majaribuni Mungu wetu tunaomba utuepushe
na yule mwovu na kazi zake zote
Jehovah ututakase miili yetu na akili zetu
Baba wa Mbinguni tunaomba utufunike kwa Damu
ya Bwana na Mwokozi wetu Yesu Kristo wa Nazareti
yeye aliteseka kwanza ili sisi tupate kupona....

Tunapolemewa na makosa yetu, wewe mwenyewe watusamehe. Heri wale unaowachagua na kuwaleta karibu, waishi katika maskani yako. Sisi tutatoshelezwa na mema ya nyumba yako; mema ya hekalu lako takatifu.
Mungu wetu tunaomba ukabariki kazi za mikono yetu
Baba wa Mbinguni tunaomba ukatupe ubunifu na maarifa katika utendaji
Jehovah nasi tukatende sawasawa na mapenzi yako
Yahweh tunaomba ukabariki ridhiki zetu ziingiazo/zitokazo
Mungu wetu nasi tunaomna ukatupe neema ya kuweza kuwabariki wenye kuhitaji
Tusipungukiwe katika mahitaji yetu
Baba wa Mbinguni tunaomba ukatupe kama inavyokupendeza wewe...


Yahweh tunayaweka maisha yetu mikononi mwako
Mungu wetu tunaomba ukabariki nyumba/ndoa zetu,
Jehovah tunaomba ulinzi wako kwetu na kwa vyote tunavyovimiliki
Yahweh tunaomba ukatubariki tuingiapo/tutokapo
Mungu wetu tunaomba ukavibariki vyote tunavyoenda kugusa/kutumia
Baba wa Mbinguni ukavitakase kwa Damu ya Bwana wetu Yesu Kristo
Mungu wetu ukatamalaki na kutuatamia
Baba wa Mbinguni tukawe salama rohoni
Yahwe ukatupe akili ya kutambua mema na mabaya
Mfalme wa amani amani yako ikatawale katika maisha yetu
Mungu wetu ukatupe macho ya kuona,masikio ya kusikia sauti yako na kuitii..
Baba wa Mbinguni  tunaomba ukatupe neema ya kufuata
njia zako,tukasimamie Neno lako,amri na sheria zako
siku zote za maisha yetu...
Ukatuguse kwa mkono wako wenye nguvu,ukatufanye chombo chema
ee Mungu wetu nasi tukatumike kama inavyokupendeza wewe
Roho Mtakatifu akatuongoze katika yote na tukawe na kiasi....

Kwa matendo yako makuu watuitikia na kutuokoa, ewe Mungu wa wokovu wetu; wewe ndiwe tumaini la viumbe vyote, duniani kote na mbali baharini.
Tazama watoto wako wenye shida/tabu,wote wanaopitia magumu/majaribu mbalimbali
Mungu wetu tunaomba ukawaguse kwa mkono wako wenye nguvu
kila mmoja na mahitaji yake
Mungu wetu tunaomba ukawasamehe pale walipo kwenda kinyume nawe
Yahweh tunaomba ukawape neema ya kuweza kujiombea,kufuata njia zako nazo zikawaweke huru...
Baba wa Mbinguni tunayaweka haya yote mikononi mwako
Kwakuwa Ufalme ni wako Nguvu na Utukufu hata Milele...
Amina...!!


Asanteni sana wapendwa katika Kristo Yesu kwakuwa nami,Baba wa Mbinguni aendelee kuwatendea sawasawa na mapenzi yake...
Nawapenda.

Njoni hata kama hamna fedha
1Haya! Kila mwenye kiu na aje kwenye maji!
Njoni, nyote hata msio na fedha;
nunueni ngano mkale,
nunueni divai na maziwa.
Bila fedha, bila gharama!
2Mbona mnatumia fedha yenu
kwa ajili ya kitu kisicho chakula?
Ya nini kutoa jasho lenu kwa kitu kisichoshibisha?
Nisikilizeni mimi kwa makini,
nanyi mtakula vilivyo bora,
na kufurahia vinono.
3Tegeni sikio enyi watu wangu, mje kwangu;
nisikilizeni, ili mpate kuishi.
Nami nitafanya nanyi agano la milele;
nitawapeni fadhili nilizomwahidi Daudi.
4Mimi nilimfanya kiongozi na kamanda wa mataifa
ili yeye anishuhudie kwa watu wa mataifa.
5Sasa utayaita mataifa usiyoyajua,
watu wa mataifa yasiyokutambua watakujia mbio,
kwa sababu yangu mimi Mwenyezi-Mungu, Mungu wako;
kwa sababu yangu mimi Mtakatifu wa Israeli
niliyekufanya wewe utukuke.”
6Mtafuteni Mwenyezi-Mungu wakati bado anapatikana,
mwombeni msaada wakati yupo bado karibu.
7Waovu na waache njia zao mbaya,
watu wabaya waachane na mawazo yao mabaya;
wamrudie Mwenyezi-Mungu apate kuwahurumia,
wamwendee Mungu wetu maana atawasamehe.
8Maana, Mwenyezi-Mungu asema hivi:
“Mawazo yangu si kama mawazo yenu,
wala njia zangu si kama njia zenu.
9Kama vile mbingu zilivyo mbali na dunia,
ndivyo njia zangu zilivyo mbali na zenu,
na mawazo yangu mbali na mawazo yenu.
10Kama vile mvua na theluji ishukavyo toka mbinguni,
wala hairudi huko bali huinywesha ardhi,
ikaifanya ichipue mimea ikakua,
ikampatia mpanzi mbegu na kuwapa watu chakula,
11vivyo hivyo na neno langu mimi:
Halitanirudia bila mafanikio,
bali litatekeleza matakwa yangu,
litafanikiwa lengo nililoliwekea.
12“Mtatoka Babuloni kwa furaha;
mtaongozwa mwende kwa amani.
Milima na vilima mbele yenu vitapaza sauti na kuimba,
na miti yote mashambani itawapigia makofi.
13Badala ya michongoma kutamea misonobari,
na badala ya mbigili kutamea mihadasi.
Hilo litakuwa jambo litakalowakumbusha watu
juu ya mambo niliyotenda mimi Mwenyezi-Mungu;
ishara ya milele ambayo haitafutwa.”


Isaya55;1-13

Biblia Habari Njema kwa Watu Wote(BHN)

"Swahili Na Waswahili"Mbarikiwe.