Swahili na Waswahili

Swahili na Waswahili
Waswahili na Mswahili Rachel Siwa...Pamoja Daima!!

Tuesday 27 August 2019

Kikombe Cha Asubuhi; Wimbo Ulio Bora6...


Shalom,Habari za Asubuhi,Hamjambo,Mmeamkaje?

Tumshukuru Mungu wetu katika yote...

Asante  Mungu wetu kwa wema na fadhili zako kwetu
Asante kwa ulinzi wako kwetu wakati wote
Asante kwa kutuchagua tena na kutupa
kibali cha kuendelea kuiona leo hii
Asante kwa pumzi/uzima,afya na kuwatayari kwa majukumu yetu


Utukuzwe ee Mungu wetu,usifiwe Baba wa Mbinguni

Neema yako yatutosha  Mungu wetu..!

Mungu atafanya jambo la haki: Atawalipa mateso wale wanaowatesa nyinyi na kuwapeni nafuu nyinyi mnaoteseka, na sisi pia. Atafanya jambo hilo wakati Bwana atakapotokea kutoka mbinguni pamoja na malaika wake wenye nguvu
Baba wa Mbinguni tunakuja mbele zako tukijinyenyekeza,tukijishusha na kujiachilia mikononi mwako
Mungu wetu tunaomba utusamehe dhambi zetu zote
Baba wa Mbinguni nasi tunaomba utupe neema ya kuweza kuwasamehe wale wote waliotukosea,Usitutie majaribuni Mungu wetu tunaomba utuepushe na yule mwovu na kazi zake zote,Jehovah ututakase miili yetu na akili zetu Baba wa Mbinguni tunaomba utufunike kwa  Damu ya Bwana na Mwokozi wetu Yesu Kristo wa Nazareti,
Yeye aliteseka kwanza ili sisi tupate kupona....

na miali ya moto, kuwaadhibu wale wanaomkataa Mungu na wale wasiotii Habari Njema ya Bwana wetu Yesu. Adhabu yao itakuwa kuangamizwa milele na kutengwa mbali na utukufu wake mkuu,
Mungu wetu tunaomba ukabariki kazi za mikono yetu
Baba wa Mbinguni tunaomba ukatupe ubunifu na maarifa 
katika utendaji
Jehovah nasi tukatende sawasawa na mapenzi yako
Baba wa Mbinguni tunaomba ukabariki ridhiki zetu
ziingiazo/zitokazo
Mungu wetu nasi tunaomba ukatupe neema ya kuweza
kuwabariki wenye kuhitaji
Yahweh tusipungukiwe katika mahitaji yetu
Mungu wetu ukatupe kama inavyokupendeza wewe

Jehovah tunayaweka maisha yetu mikononi mwako
Baba wa Mbinguni tunaomba ukabariki nyumba/ndoa zetu,
watoto,wazazi wetu,familia/ndugu na wote wanaotuzunguka
Jehovah tunaomba ulinzi wako kwetu na kwa vyote tunavyo vimiliki
Yahweh tunaomba ukatubariki tuingiapo/tutokapo
Mungu wetu tunaomba ukavibariki vyote tunavyoenda kugusa/kutumia
Baba wa Mbinguni ukavitakase kwa Damu ya Bwana wetu Yesu Kristo
Mungu wetu ukatamalaki na kutuatamia
Baba wa Mbinguni tukawe salama rohoni
Mfalme wa amani amani yako ikatawale katika maisha yetu
Mungu wetu ukatupe macho ya kuona na masikio ya kusikia 
sauti yako na kuitii
Baba wa Mbinguni tunaomba ukatupe neema ya kufuata njia zako
Yahweh tukasimamie Neno lako amri na sheria zako siku zote 
za maisha yetu

Mungu  wetu ukaonekane katika maisha yetu popote tupitapo na ikajulikane kwamba upo 

Neema zako zikawe nasi Nuru yako ikaangaze katika maisha yetu
Ukatufanye barua njema ee Mungu wetu nasi tukasomeke kama
inavyokupendeza wewe
Roho Mtakatifu akatuongoze katika yote na tukawe na kiasi...


wakati atakapokuja siku ile kupokea utukufu kutoka kwa watu wake na heshima kutoka kwa wote wanaoamini. Nyinyi pia mtakuwa miongoni mwao, kwani mmeuamini ule ujumbe tuliowaletea.
Tazama wenye shida/tabu,Mungu wetu tunaomba
 ukawaguse kila mmoja na mahitaji yake
Baba wa Mbinguni tunaomba ukawasamehe pale walipokwenda
kinyume nawe
Mungu wetu ukawape neema ya kujiombea,macho ya rohoni,masikio yakusikia sauti yako,wakafuate njia zako nazo zikawaweke huru
Mungu wetu tunaomba ukasikie kulia kwao
Baba wa Mbinguni tunomba ukawafute machozi yao
Nuru yako ikaangaze katika maisha yao
Mungu wetu tunaomba ukawatendee sawasawa na mapenzi yako
Kwakuwa Ufalme ni wako Nguvu na Utukufu hata Milele
Amina....!!!


Wapendwa katika Kristo Yesu asanteni sana
kwakuwanami/kunisoma

Mungu Baba aendelee kuwabariki na kuwatendea
kama inavyompendeza yeye
Amani ya Bwana wetu Yesu Kristo na upendo wa Mungu Baba
ukae nanyi daima....

Nawapenda.


Wanawake
1Ewe mwanamke uliye mzuri sana;
amekwenda wapi huyo mpenzi wako?
Ameelekea wapi mpenzi wako
ili tupate kushirikiana nawe katika kumtafuta?
Bibi arusi
2Mpenzi wangu amekwenda bustanini mwake,
mahali ambapo rihani hustawi.
Yeye analisha kondoo wake
na kukusanya yungiyungi.
3Mimi ni wake mpenzi wangu, naye ni wangu;
yeye huwalisha kondoo wake penye yungiyungi.
Shairi la tano
Bwana arusi
4Mpenzi wangu, wewe u mzuri kama Tirza,
wapendeza kama Yerusalemu,
unatisha kama jeshi lenye bendera.
5Hebu tazama kando tafadhali;
ukinitazama nahangaika.
Nywele zako ni kama kundi la mbuzi,
wateremkao chini ya milima ya Gileadi.
6Meno yako kama kundi la kondoo majike
wanaoteremka baada ya kuogeshwa.
Kila mmoja amezaa mapacha,
na hakuna yeyote aliyefiwa.
7Mashavu yako ni kama nusu mbili za komamanga,
nyuma ya shela lako.
8Wapo malkia sitini, masuria themanini,
na wasichana wasiohesabika!
9Hua wangu, mzuri wangu, ni mmoja tu,
na ni kipenzi cha mama yake;
yeye ni wa pekee kwa mama yake.
Wasichana humtazama na kumwita heri,
nao malkia na masuria huziimba sifa zake.
10Nani huyu atazamaye kama pambazuko?
Mzuri kama mwezi, mwangavu kama jua,
na anatisha kama jeshi lenye bendera.
11Nimeingia katika bustani ya milozi
kutazama machipuko ya bondeni,
kuona kama mizabibu imechanua,
na mikomamanga imechanua maua.
12Bila kutazamia, mpenzi wangu,
akanitia katika gari la mkuu.6:12 aya ya 12 Kiebrania si dhahiri.
Wanawake
13Rudi, rudi ewe msichana wa Mshulami.
Rudi, rudi tupate kukutazama.
Bibi arusi
Mbona mwataka kunitazama miye Mshulami
kana kwamba mnatazama ngoma
kati ya majeshi mawili?


Wimbo Ulio Bora6;1-13

Biblia Habari Njema kwa Watu Wote(BHN)

"Swahili Na Waswahili"Mbarikiwe.

Monday 26 August 2019

Kikombe Cha Asubuhi; Wimbo Ulio Bora5...


Shalom,Habari za Asubuhi,Hamjambo,Mmeamkaje?

Haleluyah ni siku/wiki nyingine tena Mungu wetu ametuchagua

na kutupa kibali cha kuendelea kuiona leo hii
Si kwamba sisi tumetenda mema sana wala si kwa nguvu zetu
si kwa utashi wetu wala si kwa akili zetu si kwamba sisi
ni wazuri mno si kwa uwezo wetu sisi kuwa hivi tulivyo leo hii
Ni kwa rehema/neema zake ni kwa mapenzi yake Mungu wetu....

Tumshukuru Mungu wetu katika yote...

Asante Mungu wetu kwa wema na fadhili zako kwetu
Asante kwa ulinzi wako kwetu wakati wote
Asante kwa pumzi/uzima,afya na kuwa tayari kwa majukumu yetu
Sifa na Utukufu tunakurudshia Mungu wetu....!!

Mimi Paulo, Silwano na Timotheo, kwa jumuiya ya kanisa la Thesalonike, ambayo ni watu wake Mungu Baba yetu na wa Bwana Yesu Kristo. Tunawatakieni neema na amani kutoka kwa Mungu Baba yetu na kwa Bwana Yesu Kristo.
Tazama jana imepita ee Mungu wetu leo ni siku mpya na kesho ni siku nyingine Jehovah tunakuja mbele zako tukijinyenyekeza,tukijishusha na kujiachilia mikononi mwako
 Mungu wetu tunaomba utusamehe dhambi zetu zote tulizozifanya kwakuwaza,kwakunena,kwakutenda,kwakujua/kutojua
Baba wa Mbinguni nasi tunaomba utupe neema ya kuweza kuwasamehe wale wote waliotukosea
Jehovah usitutie majaribu Mungu wetu tunaomba utuepushe na yule mwovu na kazi zake zote
Yahweh tunaomba ututakase miili yetu na akili zetu
Baba wa Mbinguni utufunike kwa Damu ya Bwana na Mwokozi wetu Yesu Kristo wa Nazareti
yeye aliteseka kwanza ili sisi tupate kupona
Kwakupigwa kwake sisi tumepata kupona....

Ndugu, tunapaswa kumshukuru Mungu daima kwa ajili yenu. Inafaa kwetu kufanya hivyo kwani imani yenu inakua sana na kupendana kwenu kunaongezeka sana. Ndio maana sisi tunajivunia nyinyi katika makanisa ya Mungu. Tunaona fahari juu ya jinsi mnavyoendelea kuamini na kustahimili katika udhalimu wote na mateso mnayopata.
Yahweh tunaomba ukabariki kazi za mikono yetu
Baba wa Mbinguni tunaomba ukatupe ubunifu na maarifa 
katika utendaji
Jehovah nasi tukatende sawasawa na mapenzi yako
Baba wa Mbinguni tunaomba ukabariki ridhiki zetu
ziingiazo/zitokazo
Mungu wetu nasi tunaomba ukatupe neema ya kuweza
kuwabariki wenye kuhitaji
Yahweh tusipungukiwe katika mahitaji yetu
Mungu wetu ukatupe kama inavyokupendeza wewe

Baba wa Mbinguni tunayaweka maisha yetu mikononi mwako
Mungu wetu tunaomba ukabariki nyumba/ndoa zetu,
watoto,wazazi wetu,familia/ndugu na wote wanaotuzunguka
Jehovah tunaomba ulinzi wako kwetu na kwa vyote tunavyo vimiliki
Yahweh tunaomba ukatubariki tuingiapo/tutokapo
Mungu wetu tunaomba ukavibariki vyote tunavyoenda kugusa/kutumia
Baba wa Mbinguni ukavitakase kwa Damu ya Bwana wetu Yesu Kristo
Mungu wetu ukatamalaki na kutuatamia
Baba wa Mbinguni tukawe salama rohoni
Mfalme wa amani amani yako ikatawale katika maisha yetu
Mungu wetu ukatupe macho ya kuona na masikio ya kusikia 
sauti yako na kuitii
Baba wa Mbinguni tunaomba ukatupe neema ya kufuata njia zako
Yahweh tukasimamie Neno lako amri na sheria zako siku zote 
za maisha yetu
Mungu wetu ukaonekane katika maisha yetu
Neema zako zikawe nasi Nuru yako ikaangaze katika maisha yetu
ukatuguse kwa mkono wako wenye nguvu
Ukatufanye chombo chema ee Mungu wetu nasi tukatumike kama
inavyokupendeza wewe
Roho Mtakatifu akatuongoze katika yote na tukawe na kiasi...


Hayo yote yanathibitisha kwamba hukumu ya Mungu ni ya haki, na matokeo yake, nyinyi mtastahili ufalme wake ambao kwa ajili yake mnateseka.
Mungu wetu tunawaweka mikononi mwako wenye shida/tabu,wote wanaopitia magumu/majaribu mbalimbali
Mungu wetu tunaomba ukawaguse kwa mkono wako wenye nguvu
 kila mmoja na mahitaji yake 
Mungu wetu tunaomba ukawasamehe pale walipokwenda kinyume nawe
Baba wa Mbinguni ukawape neema ya kujiombea,kufuata njia zako
wakasimamie Neno lako nalo likaweke huru
Mungu wetu tunaomba ukasikie kuomba kwetu
Mungu wetu ukawatendee sawasawa na mapenzi yako
Kwakuwa Ufalme ni wako Nguvu na Utukufu hata Milele
Amina...!!


Asanteni sana wapendwa katika Kristo Yesu kwakuwa nami
Mungu Baba aendelee kuwabariki na kuwatendea 
kama inavyompendeza yeye....
Nawapenda.

Bwana arusi
1Naingia bustanini mwangu,
dada yangu, bi arusi.
Nakusanya manemane na viungo,
nala sega langu la asali,
nanywa divai yangu na maziwa yangu.
Bibi arusi
Kuleni enyi marafiki, kunyweni;
kunyweni sana wapendwa wangu.
Shairi la nne
Bibi arusi
2Nililala, lakini moyo wangu haukulala.
Sauti ya mpenzi wangu anabisha hodi.
Bwana arusi
“Nifungulie, dada yangu mpenzi wangu, bibiarusi wangu,
hua wangu, usiye na kasoro.
Kichwa changu kimelowa umande
na nywele zangu manyunyu ya usiku.”
Bibi arusi
3Nimekwisha yavua mavazi yangu,
nitayavaaje tena?
Nimekwisha nawa miguu yangu,
niichafueje tena?
4Hapo mpenzi wangu akaugusa mlango,
moyo wangu ukajaa furaha.
5Niliinuka kumfungulia mpenzi wangu.
Mikono yangu imejaa manemane,
na vidole vyangu vyadondosha manemane,
nilipolishika komeo kufungua mlango.
6Nilimfungulia mlango mpenzi wangu,
lakini kumbe, alikuwa amekwisha toweka.
Moyo wangu ulifurahi alipokuwa akizungumza!
Nilimtafuta, lakini sikumpata;
nilimwita, lakini hakuniitikia.
7Walinzi wa mji waliniona,
walipokuwa wanazunguka mjini;
wakanipiga na kunijeruhi;
nao walinzi wa lango wakaninyanganya shela langu.
8Nawasihini, enyi wanawake wa Yerusalemu,
mkimwona mpenzi wangu,
mwelezeni kwamba naugua kwa mapenzi!
Wanawake
9Ewe upendezaye kuliko wanawake wote!
Kwani huyo mpenzi wako ana nini cha zaidi ya mpenzi mwingine,
hata utusihi kwa moyo kiasi hicho?
Bibi arusi
10Mpenzi wangu ni mzuri na mwenye nguvu,
mashuhuri miongoni mwa wanaume elfu kumi.
11Kichwa chake kizuri kama dhahabu safi,
nywele zake ni za ukoka,
nyeusi ti kama kunguru.
12Macho yake ni kama ya hua kandokando ya kijito,
ni kama njiwa waliooga maziwa kando ya kijito.5:12 kando ya kijito: Kiebrania si dhahiri.
13Mashavu yake ni kama matuta ya rihani
kama bustani iliyojaa manukato na manemane.
Midomo yake ni kama yungiyungi,
imelowa manemane kwa wingi.
14Mikono yake imewekwa bangili za dhahabu,
amevalia johari za Tarshishi.
Kiwiliwili chake ni kama pembe za ndovu
zilizopambwa kwa vito vya johari ya rangi ya samawati.
15Miguu yake ni kama nguzo za alabasta
zilizosimikwa katika misingi ya dhahabu.
Umbo lake ni kama Lebanoni,
ni bora kama miti ya mierezi.
16Kinywa chake kimejaa maneno matamu,
kwa ujumla anapendeza.
Basi, hivyo ndivyo alivyo mpenzi wangu,
naam, ndivyo alivyo rafiki yangu,
enyi wanawake wa Yerusalemu.

Wimbo Ulio Bora5;1-16

Biblia Habari Njema kwa Watu Wote(BHN)

"Swahili Na Waswahili"Mbarikiwe.

Friday 23 August 2019

Kikombe Cha Asubuhi; Wimbo Ulio Bora4...


Shalom,Habari za Asubuhi,Hamjambo,Mmeamkaje?

Tumshukuru Mungu katika yote....

Mungu wetu Baba yetu,Muumba wetu Muumba wa Mbingu na Nchi
Muumba wa vyote vilivyomo vinavyoonekana na visivyoonekana
Mungu wa walio hai,Mungu  mwenye huruma,Mungu wa upendo
Mungu wa Abrahamu,Isaka na Yakobo...
Asante kwa wema na fadhili zako kwetu
Asante kwa ulinzi wako kwetu wakati wote
Asante kwa kutuchagua tena na kutupa
kibali cha kuendelea kuiona leo hii
Asante kwa pumzi/uzima,afya na kuwatayari kwa majukumu yetu

Neema yako yatutosha ee Mungu wetu....!!

Mungu mwenyewe ndiye mwenye kutuimarisha sisi na nyinyi pia katika Kristo, na ndiye anayetuweka wakfu;
Baba wa Mbinguni tunakuja mbele zako tukijinyenyekeza,tukijishusha na kujiachilia mikononi mwako
Mungu wetu tunaomba utusamehe dhambi zetu zote 
Baba wa Mbinguni nasi tunaomba ukatupe neema
ya kuweza kuwasamehe wale wote waliotukosea
Usitutie majaribuni Mungu wetu tunaomba utuepushe
na yule mwovu na kazi zake zote
Jehovah ututakase miili yetu na akili zetu
Baba wa Mbinguni tunaomba utufunike kwa Damu
ya Bwana na Mwokozi wetu Yesu Kristo wa Nazareti
yeye aliteseka kwanza ili sisi tupate kupona....

ndiye aliyetutia mhuri wa kuwa mali yake yeye na kutujalia Roho mioyoni mwetu kama dhamana ya mambo yote ambayo ametuwekea.
Mungu wetu tunaomba ukabariki kazi za mikono yetu
Baba wa Mbinguni tunaomba ukatupe ubunifu na maarifa katika utendaji
Jehovah nasi tukatende sawasawa na mapenzi yako
Yahweh tunaomba ukabariki ridhiki zetu ziingiazo/zitokazo
Mungu wetu nasi tunaomna ukatupe neema ya kuweza kuwabariki wenye kuhitaji
Tusipungukiwe katika mahitaji yetu
Baba wa Mbinguni tunaomba ukatupe kama inavyokupendeza wewe...

Yahweh tunayaweka maisha yetu mikononi mwako
Mungu wetu tunaomba ukabariki nyumba/ndoa zetu,
Jehovah tunaomba ulinzi wako kwetu na kwa vyote tunavyovimiliki
Yahweh tunaomba ukatubariki tuingiapo/tutokapo
Mungu wetu tunaomba ukavibariki vyote tunavyoenda kugusa/kutumia
Baba wa Mbinguni ukavitakase kwa Damu ya Bwana wetu Yesu Kristo
Mungu wetu ukatamalaki na kutuatamia
Baba wa Mbinguni tukawe salama rohoni
Yahwe ukatupe akili ya kutambua mema na mabaya
Mfalme wa amani amani yako ikatawale katika maisha yetu
Mungu wetu ukatupe macho ya kuona,masikio ya kusikia sauti yako na kuitii..
Baba wa Mbinguni  tunaomba ukatupe neema ya kufuata
njia zako,tukasimamie Neno lako,amri na sheria zako
siku zote za maisha yetu...
Ukatuguse kwa mkono wako wenye nguvu,ukatufanye chombo chema
ee Mungu wetu nasi tukatumike kama inavyokupendeza wewe
Roho Mtakatifu akatuongoze katika yote na tukawe na kiasi....

Mungu ndiye shahidi wangu; yeye anajua moyo wangu! Mimi sikuja tena Korintho kwa sababu tu ya kuwahurumieni. Hatutaki kutumia mabavu juu ya imani yenu; nyinyi mko imara katika imani yenu. Wajibu wetu ni kufanya kazi pamoja kwa ajili ya furaha yenu.
Tazama watoto wako wenye shida/tabu,wote wanaopitia magumu/majaribu mbalimbali
Mungu wetu tunaomba ukawaguse kwa mkono wako wenye nguvu
kila mmoja na mahitaji yake
Mungu wetu tunaomba ukawasamehe pale walipo kwenda kinyume nawe
Yahweh tunaomba ukawape neema ya kuweza kujiombea,kufuata njia zako nazo zikawaweke huru...
Baba wa Mbinguni tunayaweka haya yote mikononi mwako
Kwakuwa Ufalme ni wako Nguvu na Utukufu hata Milele...
Amina...!!


Asanteni sana wapendwa katika Kristo Yesu kwakuwa nami,Baba wa Mbinguni aendelee kuwatendea sawasawa na mapenzi yake...
Nawapenda.

Bwana arusi
1Hakika u mzuri ewe mpenzi wangu,
hakika u mzuri!
Macho yako ni kama ya hua
nyuma ya shela lako,
nywele zako ni kama kundi la mbuzi
washukao katika milima ya Gileadi.
2Meno yako ni kama kondoo majike waliokatwa manyoya
wanaoteremka baada ya kuogeshwa.
Kila mmoja amezaa mapacha,
na hakuna yeyote aliyefiwa.
3Midomo yako ni kama utepe mwekundu,
kinywa chako chavutia kweli.
Nyuma ya shela lako,
mashavu yako ni kama nusu mbili za komamanga.
4Shingo yako ni kama mnara wa Daudi,
uliojengwa ili kuhifadhia silaha,4:4 uliojengwa … silaha: Makala katika Kiebrania si dhahiri.
ambako zimetundikwa ngao elfu moja
zote zikiwa za mashujaa.
5Matiti yako ni kama paa mapacha,
ambao huchungwa penye yungiyungi.
6Nitakaa kwenye mlima wa manemane,
na kwenye kilima cha ubani,
hadi hapo kutakapopambazuka,
na giza kutoweka.
7Tazama ulivyo mzuri ee mpenzi wangu,
wewe huna kasoro yoyote.
8Njoo, bibiarusi wangu tuondoke Lebanoni;
na tuiachilie mbali Lebanoni.
Shuka toka kilele cha mlima Amana,
toka kilele cha Seniri na Hermoni,
toka mapango ya simba,
toka milima ya chui.
9Umefurahisha moyo wangu, dada yangu, bi arusi,
umefurahisha moyo wangu,
kwa kunitupia jicho mara moja tu,
na kwa huo mkufu wako shingoni.
10Dada yangu, bi arusi;
pendo lako ni tamu ajabu.
Ni bora kuliko divai,
marashi yako yanukia kuliko viungo vyote.
11Midomo yako yadondosha asali, ee bibiarusi wangu;
ulimi wako una asali na maziwa.
Harufu nzuri ya mavazi yako ni kama ya Lebanoni.
12Dada yangu, naam, bi arusi,
ni bustani iliyofichika,
bustani iliyosetiriwa;
chemchemi iliyotiwa mhuri.
13Machipukizi yako ni bustani ya mikomamanga
pamoja na matunda bora kuliko yote,
hina na nardo.
14Nardo na zafarani, mchai na mdalasini
manemane na udi,
na mimea mingineyo yenye harufu nzuri.
15U chemchemi ya bustani,
kisima cha maji yaliyo hai,
vijito vitiririkavyo kutoka Lebanoni.
Bibi arusi
16Vuma, ewe upepo wa kaskazi,
njoo, ewe upepo wa kusi;
vumeni juu ya bustani yangu,
mlijaze anga kwa manukato yake.
Mpenzi wangu na aje bustanini mwake,
ale matunda yake bora kuliko yote.

Wimbo Ulio Bora4;1-16

Biblia Habari Njema kwa Watu Wote(BHN)

"Swahili Na Waswahili"Mbarikiwe.

Thursday 22 August 2019

Kikombe Cha Asubuhi; Wimbo Ulio Bora3...


Shalom,Habari za Asubuhi,Hamjambo,Mmeamkaje?

Tumshukuru Mungu wetu katika yote...

Asante  Mungu wetu kwa wema na fadhili zako kwetu
Asante kwa ulinzi wako kwetu wakati wote
Asante kwa kutuchagua tena na kutupa
kibali cha kuendelea kuiona leo hii
Asante kwa pumzi/uzima,afya na kuwatayari kwa majukumu yetu


Utukuzwe ee Mungu wetu,usifiwe Baba wa Mbinguni

Neema yako yatutosha  Mungu wetu..!

Nikiwa na matumaini hayo, nilikusudia kuja kwenu hapo awali ili mpate baraka maradufu. Nilikusudia kupita kwenu nikiwa safarini kwenda Makedonia na wakati wa kurudi pia, ili nipate msaada wenu kwa safari yangu kwenda Yudea.
Baba wa Mbinguni tunakuja mbele zako tukijinyenyekeza,tukijishusha na kujiachilia mikononi mwako
Mungu wetu tunaomba utusamehe dhambi zetu zote
Baba wa Mbinguni nasi tunaomba utupe neema ya kuweza kuwasamehe wale wote waliotukosea,Usitutie majaribuni Mungu wetu tunaomba utuepushe na yule mwovu na kazi zake zote,Jehovah ututakase miili yetu na akili zetu Baba wa Mbinguni tunaomba utufunike kwa  Damu ya Bwana na Mwokozi wetu Yesu Kristo wa Nazareti,
Yeye aliteseka kwanza ili sisi tupate kupona....

Je, mnadhani nilipopanga hivyo nimekuwa kama mtu asiye na msimamo? Je, mnadhani kwamba ninafanya uamuzi wangu kwa fikira za kibinadamu na kwamba nasema “Ndiyo” na “Siyo” papo hapo?
Mungu wetu tunaomba ukabariki kazi za mikono yetu
Baba wa Mbinguni tunaomba ukatupe ubunifu na maarifa 
katika utendaji
Jehovah nasi tukatende sawasawa na mapenzi yako
Baba wa Mbinguni tunaomba ukabariki ridhiki zetu
ziingiazo/zitokazo
Mungu wetu nasi tunaomba ukatupe neema ya kuweza
kuwabariki wenye kuhitaji
Yahweh tusipungukiwe katika mahitaji yetu
Mungu wetu ukatupe kama inavyokupendeza wewe

Jehovah tunayaweka maisha yetu mikononi mwako
Baba wa Mbinguni tunaomba ukabariki nyumba/ndoa zetu,
watoto,wazazi wetu,familia/ndugu na wote wanaotuzunguka
Jehovah tunaomba ulinzi wako kwetu na kwa vyote tunavyo vimiliki
Yahweh tunaomba ukatubariki tuingiapo/tutokapo
Mungu wetu tunaomba ukavibariki vyote tunavyoenda kugusa/kutumia
Baba wa Mbinguni ukavitakase kwa Damu ya Bwana wetu Yesu Kristo
Mungu wetu ukatamalaki na kutuatamia
Baba wa Mbinguni tukawe salama rohoni
Mfalme wa amani amani yako ikatawale katika maisha yetu
Mungu wetu ukatupe macho ya kuona na masikio ya kusikia 
sauti yako na kuitii
Baba wa Mbinguni tunaomba ukatupe neema ya kufuata njia zako
Yahweh tukasimamie Neno lako amri na sheria zako siku zote 
za maisha yetu

Mungu  wetu ukaonekane katika maisha yetu popote tupitapo na ikajulikane kwamba upo 

Neema zako zikawe nasi Nuru yako ikaangaze katika maisha yetu
Ukatufanye barua njema ee Mungu wetu nasi tukasomeke kama
inavyokupendeza wewe
Roho Mtakatifu akatuongoze katika yote na tukawe na kiasi...

Mungu ni ukweli tupu; basi, kile tulichowaambia nyinyi si jambo la “Ndiyo” na “Siyo”. Maana Kristo Yesu, Mwana wa Mungu, ambaye mimi, Silwano na Timotheo, tulimhubiri kwenu, hakuwa mtu wa “Ndiyo” na “Siyo;” bali yeye daima ni “Ndiyo” ya Mungu. Maana ndani yake ahadi zote za Mungu zimekuwa “Ndiyo”. Kwa sababu hiyo, “Amina” yetu husemwa kwa njia ya Kristo kwa ajili ya kumtukuza Mungu.
Tazama wenye shida/tabu,Mungu wetu tunaomba
 ukawaguse kila mmoja na mahitaji yake
Baba wa Mbinguni tunaomba ukawasamehe pale walipokwenda
kinyume nawe
Mungu wetu ukawape neema ya kujiombea,macho ya rohoni,masikio yakusikia sauti yako,wakafuate njia zako nazo zikawaweke huru
Mungu wetu tunaomba ukasikie kulia kwao
Baba wa Mbinguni tunomba ukawafute machozi yao
Nuru yako ikaangaze katika maisha yao
Mungu wetu tunaomba ukawatendee sawasawa na mapenzi yako
Kwakuwa Ufalme ni wako Nguvu na Utukufu hata Milele
Amina....!!!


Wapendwa katika Kristo Yesu asanteni sana
kwakuwanami/kunisoma

Mungu Baba aendelee kuwabariki na kuwatendea
kama inavyompendeza yeye
Amani ya Bwana wetu Yesu Kristo na upendo wa Mungu Baba
ukae nanyi daima....

Nawapenda.

1Usiku nikiwa kitandani mwangu,
niliota namtafuta nimpendaye moyoni mwangu;
nilimtafuta, lakini sikumpata.
2Niliamka nikazunguka mjini,
barabarani na hata vichochoroni,
nikimtafuta yule wangu wa moyo.
Nilimtafuta, lakini sikumpata.
3Walinzi wa mji waliniona
walipokuwa wanazunguka mjini.
Basi nikawauliza,
“Je, mmemwona mpenzi wangu wa moyo?”
4Mara tu nilipoachana nao,
nilimwona mpenzi wangu wa moyo;
nikamshika wala sikumwachia aondoke,
hadi nilipompeleka nyumbani kwa mama yangu,
hadi chumbani kwake yule aliyenizaa.
5Nawasihini, enyi wanawake wa Yerusalemu,
kama walivyo paa au swala,
msiyachochee wala kuyaamsha mapenzi,
hadi hapo wakati wake utakapofika.
Shairi la tatu
Bibi arusi
6Ni kitu gani kile kitokacho jangwani
kama mnara wa moshi,
kinukiacho manemane na ubani,
manukato yauzwayo na wafanyabiashara?
7Tazama! Ni machela ya Solomoni;
amebebwa juu ya kiti chake cha enzi;
amezungukwa na walinzi sitini,
mashujaa bora wa Israeli.
8Kila mmoja wao ameshika upanga,
kila mmoja wao ni hodari wa vita.
Kila mmoja ana upanga wake mkononi,
tayari kumkabili adui usiku.
9Mfalme Solomoni alijitengenezea machela,
kwa mbao nzuri kutoka Lebanoni.
10Nguzo zake zilitengenezwa kwa fedha;
mgongo wake kwa dhahabu;
mahali pa kukalia pamefunikwa vitambaa vya zambarau,
walichoshona kwa upendo wanawake wa Yerusalemu,
waliokishonea alama za upendo.
11Njoni basi enyi wanawake wa Siyoni,
mkamwone mfalme Solomoni.
Amevalia taji aliyovikwa na mama yake,
siku alipofanya harusi yake,
naam, siku ambayo moyo wake ulijaa furaha.

Wimbo Ulio Bora3;1-11

Biblia Habari Njema kwa Watu Wote(BHN)

"Swahili Na Waswahili"Mbarikiwe.