Swahili na Waswahili

Swahili na Waswahili
Waswahili na Mswahili Rachel Siwa...Pamoja Daima!!

Monday 22 July 2019

Kikombe Cha Asubuhi ; Methali 23...

Shalom,Habari za Asubuhi,Hamjambo,Mmeamkaje?

Haleluyah ni siku/wiki nyingine tena Mungu wetu ametuchagua

na kutupa kibali cha kuendelea kuiona leo hii
Si kwamba sisi tumetenda mema sana wala si kwa nguvu zetu
si kwa utashi wetu wala si kwa akili zetu si kwamba sisi
ni wazuri mno si kwa uwezo wetu sisi kuwa hivi tulivyo leo hii
Ni kwa rehema/neema zake ni kwa mapenzi yake Mungu wetu....

Tumshukuru Mungu wetu katika yote...

Asante Mungu wetu kwa wema na fadhili zako kwetu
Asante kwa ulinzi wako kwetu wakati wote
Asante kwa pumzi/uzima,afya na kuwa tayari kwa majukumu yetu
Sifa na Utukufu tunakurudshia Mungu wetu....!!

“Ufuatao ni mwongozo wa ibada kuhusu sadaka ya kuondoa hatia. Sadaka hiyo ni takatifu kabisa. Mnyama wa sadaka ya kuondoa hatia atachinjiwa mahali wanapochinjiwa wanyama wa sadaka za kuteketezwa, na damu yake itarashiwa madhabahu pande zake zote.
Tazama jana imepita ee Mungu wetu leo ni siku mpya na kesho ni siku nyingine Jehovah tunakuja mbele zako tukijinyenyekeza,tukijishusha na kujiachilia mikononi mwako
 Mungu wetu tunaomba utusamehe dhambi zetu zote tulizozifanya kwakuwaza,kwakunena,kwakutenda,kwakujua/kutojua
Baba wa Mbinguni nasi tunaomba utupe neema ya kuweza kuwasamehe wale wote waliotukosea
Jehovah usitutie majaribu Mungu wetu tunaomba utuepushe na yule mwovu na kazi zake zote
Yahweh tunaomba ututakase miili yetu na akili zetu
Baba wa Mbinguni utufunike kwa Damu ya Bwana na Mwokozi wetu Yesu Kristo wa Nazareti
yeye aliteseka kwanza ili sisi tupate kupona
Kwakupigwa kwake sisi tumepata kupona....

Mafuta yake yote: Mafuta ya mkia na yale yanayofunika matumbo yatatolewa na kuteketezwa pamoja na zile figo mbili pamoja na mafuta yake na ile sehemu bora ya ini.
Yahweh tunaomba ukabariki kazi za mikono yetu
Baba wa Mbinguni tunaomba ukatupe ubunifu na maarifa 
katika utendaji
Jehovah nasi tukatende sawasawa na mapenzi yako
Baba wa Mbinguni tunaomba ukabariki ridhiki zetu
ziingiazo/zitokazo
Mungu wetu nasi tunaomba ukatupe neema ya kuweza
kuwabariki wenye kuhitaji
Yahweh tusipungukiwe katika mahitaji yetu
Mungu wetu ukatupe kama inavyokupendeza wewe

Baba wa Mbinguni tunayaweka maisha yetu mikononi mwako
Mungu wetu tunaomba ukabariki nyumba/ndoa zetu,
watoto,wazazi wetu,familia/ndugu na wote wanaotuzunguka
Jehovah tunaomba ulinzi wako kwetu na kwa vyote tunavyo vimiliki
Yahweh tunaomba ukatubariki tuingiapo/tutokapo
Mungu wetu tunaomba ukavibariki vyote tunavyoenda kugusa/kutumia
Baba wa Mbinguni ukavitakase kwa Damu ya Bwana wetu Yesu Kristo
Mungu wetu ukatamalaki na kutuatamia
Baba wa Mbinguni tukawe salama rohoni
Mfalme wa amani amani yako ikatawale katika maisha yetu
Mungu wetu ukatupe macho ya kuona na masikio ya kusikia 
sauti yako na kuitii
Baba wa Mbinguni tunaomba ukatupe neema ya kufuata njia zako
Yahweh tukasimamie Neno lako amri na sheria zako siku zote 
za maisha yetu
Mungu wetu ukaonekane katika maisha yetu
Neema zako zikawe nasi Nuru yako ikaangaze katika maisha yetu
ukatuguse kwa mkono wako wenye nguvu
Ukatufanye chombo chema ee Mungu wetu nasi tukatumike kama
inavyokupendeza wewe
Roho Mtakatifu akatuongoze katika yote na tukawe na kiasi...


Kuhani ataviteketeza juu ya madhabahu kama sadaka anayotolewa Mwenyezi-Mungu kwa moto. Hiyo ni sadaka ya kuondoa hatia. Wanaoruhusiwa kula sadaka hiyo ni wanaume wa ukoo wa makuhani peke yao; ni sadaka takatifu kabisa. Italiwa katika mahali patakatifu.
Mungu wetu tunawaweka mikononi mwako wenye shida/tabu,wote wanaopitia magumu/majaribu mbalimbali
Mungu wetu tunaomba ukawaguse kwa mkono wako wenye nguvu
 kila mmoja na mahitaji yake 
Mungu wetu tunaomba ukawasamehe pale walipokwenda kinyume nawe
Baba wa Mbinguni ukawape neema ya kujiombea,kufuata njia zako
wakasimaie Neno lako nalo likaweke huru
Mungu wetu tunaomba ukasikie kuomba kwetu
Mungu wetu ukawatendee sawasawa na mapenzi yako
Kwakuwa Ufalme ni wako Nguvu na Utukufu hata Milele
Amina...!!


Asanteni sana wapendwa katika Kristo Yesu kwakuwa nami
Mungu Baba aendelee kuwabariki na kuwatendea 
kama inavyompendeza yeye....
Nawapenda.

- 6 -
1Ukiketi kula pamoja na mtawala,
usisahau hata kidogo uko pamoja na nani.
2Zuia sana hamu yako,
ikiwa wewe wapenda sana kula.
3Usitamani vyakula vyake vizuri,
maana vyaweza kukudanganya.
- 7 -
4Ikiwa unayo hekima ya kutosha,
usijitaabishe kutafuta utajiri.
5Kufumba na kufumbua utajiri hutoweka,
huwa kama umepata mabawa ghafla,
ukaruka na kutowekea angani kama tai.
- 8 -
6Usile chakula cha mtu bahili,
wala usitamani mapochopocho yake,
7maana moyoni mwake anahesabu unachokula.23:7 maana … unachokula: Maana katika Kiebrania si dhahiri.
Atakuambia, “Kula, kunywa!”
Lakini moyoni mwake hayuko pamoja nawe.
8Utatapika vipande ulivyokula;
shukrani zako zote zitakuwa za bure.
- 9 -
9Usiseme maneno yako mbele ya mpumbavu,
maana atapuuza hekima ya maneno yako.
- 10 -
10Usiondoe alama ya mpaka wa zamani,
wala usiingilie mashamba ya yatima,
11maana Mungu, Mkombozi, ni mwenye nguvu,
naye ataitetea haki yao dhidi yako.
- 11 -
12Tumia akili zako kufuata mafundisho;
tumia masikio yako kusikiliza maarifa.
- 12 -
13Usiache kumrudi mtoto;
ukimchapa kiboko hatakufa.
14Ukimtandika kiboko,
utayaokoa maisha yake na kuzimu.
- 13 -
15Mwanangu, moyo wako ukiwa wenye busara,
moyo wangu pia utakuwa wenye furaha.
16Moyo wangu utashangilia,
mdomo wako utakaposema maneno yaliyo sawa.
- 14 -
17Moyo wako usiwaonee wivu wenye dhambi,
ila endelea kumcha Mwenyezi-Mungu siku zote.
18Hakika kuna kesho ya milele,
na tumaini lako halitakuwa bure.
- 15 -
19Sikia mwanangu, uwe na hekima;
fikiria sana jinsi unavyoishi.
20Usiwe mmoja wa walevi wa divai,
wala walafi wenye kupenda nyama,
21maana walevi na walafi wataishia kuwa maskini,
anayetumia siku yake kusinzia atavaa matambara.
- 16 -
22Msikilize baba yako aliyekuzaa,
wala usimdharau mama yako akizeeka.
23Nunua ukweli, wala usiuuze;
nunua hekima, mafunzo na busara.
24Baba wa mtoto mwadilifu atajaa furaha;
anayemzaa mtoto mwenye hekima atamfurahia.
25Wafurahishe baba na mama yako;
mama aliyekuzaa na afurahi.
- 17 -
26Mwanangu, nisikilize kwa makini,
shikilia mwenendo wa maisha yangu.
27Malaya ni shimo refu la kutega watu;
mwanamke mgeni ni kama kisima chembamba.
28Yeye hunyemelea kama mnyanganyi,
husababisha wanaume wengi kukosa uaminifu.
- 18 -
29Ni nani wapigao yowe?
Ni nani wenye huzuni?
Ni nani wenye ugomvi?
Ni nani walalamikao?
Ni nani wenye majeraha bila sababu?
Ni nani wenye macho mekundu?
30Ni wale ambao hawabanduki penye divai,
wale wakaao chonjo kuonja divai iliyokolezwa.
31Usiitamani divai hata kwa wekundu wake,
hata kama inametameta katika bilauri,
na kushuka taratibu unapoinywa.
32Mwishowe huuma kama nyoka;
huchoma kama nyoka mwenye sumu.
33Macho yako yataona mauzauza,
moyo wako utatoa mambo yaliyopotoka.
34Utakuwa kama mtu alalaye katikati ya bahari,
kama mtu alalaye juu ya mlingoti wa meli.
35Utasema, “Walinichapa, lakini sikuumia;
walinipiga, lakini sina habari.
Nitaamka lini?
Ngoja nitafute kinywaji kingine!”


Methali23;1-35

Biblia Habari Njema kwa Watu Wote(BHN)

"Swahili Na Waswahili"Mbarikiwe.

Friday 19 July 2019

Kikombe Cha Asubuhi ; Methali 22...

Shalom,Habari za Asubuhi,Hamjambo,Mmeamkaje?

Tumshukuru Mungu wetu katika yote...

Asante  Mungu wetu kwa wema na fadhili zako kwetu
Asante kwa ulinzi wako kwetu wakati wote
Asante kwa kutuchagua tena na kutupa
kibali cha kuendelea kuiona leo hii
Asante kwa pumzi/uzima,afya na kuwatayari kwa majukumu yetu


Utukuzwe ee Mungu wetu,usifiwe Baba wa Mbinguni

Neema yako yatutosha  Mungu wetu..!

Labda Onesimo aliondoka kwako kwa kitambo tu, kusudi uweze tena kuwa naye daima. Na sasa yeye si mtumwa wa kawaida, ila ni bora zaidi ya mtumwa: Yeye ni ndugu yetu mpenzi. Ni wa maana sana kwangu mimi, na kwako atakuwa wa maana zaidi, kama mtumwa na kama ndugu katika Bwana.
Baba wa Mbinguni tunakuja mbele zako tukijinyenyekeza,tukijishusha na kujiachilia mikononi mwako
Mungu wetu tunaomba utusamehe dhambi zetu zote
Baba wa Mbinguni nasi tunaomba utupe neema ya kuweza kuwasamehe wale wote waliotukosea,Usitutie majaribuni Mungu wetu tunaomba utuepushe na yule mwovu na kazi zake zote,Jehovah ututakase miili yetu na akili zetu Baba wa Mbinguni tunaomba utufunike kwa  Damu ya Bwana na Mwokozi wetu Yesu Kristo wa Nazareti,
Yeye aliteseka kwanza ili sisi tupate kupona....

Basi, ikiwa wanitambua mimi kuwa mwenzako, mpokee tena kama vile ungenipokea mimi mwenyewe. Kama alikuwa amekukosea kitu, au alikuwa na deni lako, basi, unidai mimi. Naandika jambo hili kwa mkono wangu mwenyewe: Mimi Paulo nitalipa! (Tena sina haja ya kusema kwamba wewe unalo deni kwangu la nafsi yako). Naam, ndugu yangu, nifanyie jambo hilo kwa ajili ya jina la Bwana; burudisha moyo wangu kama ndugu katika Kristo.
Mungu wetu tunaomba ukabariki kazi za mikono yetu
Baba wa Mbinguni tunaomba ukatupe ubunifu na maarifa 
katika utendaji
Jehovah nasi tukatende sawasawa na mapenzi yako
Baba wa Mbinguni tunaomba ukabariki ridhiki zetu
ziingiazo/zitokazo
Mungu wetu nasi tunaomba ukatupe neema ya kuweza
kuwabariki wenye kuhitaji
Yahweh tusipungukiwe katika mahitaji yetu
Mungu wetu ukatupe kama inavyokupendeza wewe



Jehovah tunayaweka maisha yetu mikononi mwako
Baba wa Mbinguni tunaomba ukabariki nyumba/ndoa zetu,
watoto,wazazi wetu,familia/ndugu na wote wanaotuzunguka
Jehovah tunaomba ulinzi wako kwetu na kwa vyote tunavyo vimiliki
Yahweh tunaomba ukatubariki tuingiapo/tutokapo
Mungu wetu tunaomba ukavibariki vyote tunavyoenda kugusa/kutumia
Baba wa Mbinguni ukavitakase kwa Damu ya Bwana wetu Yesu Kristo
Mungu wetu ukatamalaki na kutuatamia
Baba wa Mbinguni tukawe salama rohoni
Mfalme wa amani amani yako ikatawale katika maisha yetu
Mungu wetu ukatupe macho ya kuona na masikio ya kusikia 
sauti yako na kuitii
Baba wa Mbinguni tunaomba ukatupe neema ya kufuata njia zako
Yahweh tukasimamie Neno lako amri na sheria zako siku zote 
za maisha yetu

Mungu  wetu ukaonekane katika maisha yetu popote tupitapo na ikajulikane kwamba upo 

Neema zako zikawe nasi Nuru yako ikaangaze katika maisha yetu
Ukatufanye barua njema ee Mungu wetu nasi tukasomeke kama
inavyokupendeza wewe
Roho Mtakatifu akatuongoze katika yote na tukawe na kiasi...

Naandika nikitumaini kwamba utanikubalia ombi langu; tena najua kwamba utafanya hata zaidi ya haya ninayokuomba. Pamoja na hayo, nitayarishie chumba kwani natumaini kwamba kwa sala zenu, Mungu atanijalia niwatembeleeni. Epafra, mfungwa mwenzangu kwa ajili ya Kristo Yesu, anakusalimu. Nao akina Marko, Aristarko, Dema na Luka, wafanyakazi wenzangu, wanakusalimu. Nawatakieni nyinyi nyote neema ya Bwana Yesu Kristo.
Tazama wenye shida/tabu,Mungu wetu tunaomba
 ukawaguse kila mmoja na mahitaji yake
Baba wa Mbinguni tunaomba ukawasamehe pale walipokwenda
kinyume nawe
Mungu wetu ukawape neema ya kujiombea,macho ya rohoni,masikio yakusikia sauti yako,wakafuate njia zako nazo zikawaweke huru
Mungu wetu tunaomba ukasikie kulia kwao
Baba wa Mbinguni tunomba ukawafute machozi yao
Nuru yako ikaangaze katika maisha yao
Mungu wetu tunaomba ukawatendee sawasawa na mapenzi yako
Kwakuwa Ufalme ni wako Nguvu na Utukufu hata Milele
Amina....!!!


Wapendwa katika Kristo Yesu asanteni sana
kwakuwanami/kunisoma

Mungu Baba aendelee kuwabariki na kuwatendea
kama inavyompendeza yeye
Amani ya Bwana wetu Yesu Kristo na upendo wa Mungu Baba
ukae nanyi daima....
Nawapenda.

1Afadhali kuwa na sifa nzuri kuliko mali nyingi;
wema ni bora kuliko fedha au dhahabu.
2Matajiri na maskini wana hali hii moja:
Mwenyezi-Mungu ni Muumba wao wote.
3Mtu mwangalifu huona hatari akajificha,
lakini wajinga hujitokeza mbele wakaumia.
4Ukinyenyekea na kumcha Mwenyezi-Mungu,
utapata tuzo: Fanaka, heshima na uhai.
5Njia ya waovu imejaa miiba na mitego;
anayetaka kuhifadhi maisha yake ataiepa.
6Mfunze mtoto namna ya kuishi vizuri,
naye hatasahau njia hiyo hata uzeeni.
7Tajiri humtawala maskini;
mkopaji ni mtumwa wa mkopeshaji.
8Apandaye dhuluma atavuna janga;
uwezo wake wa kutenda mabaya utavunjwa.
9Mtu mkarimu atabarikiwa,
maana chakula chake humgawia maskini.
10Mfukuze mwenye dharau na fujo itatoweka,
ugomvi na matusi vitakoma.
11Mwenye nia safi na maneno mazuri,
atakuwa rafiki wa mfalme.
12Mwenyezi-Mungu hulinda elimu ya kweli,
lakini huyavuruga maneno ya waovu.
13Mvivu husema, “Siwezi kutoka nje;
kuna simba huko, ataniua!”
14Kinywa cha mwasherati ni shimo refu;
anayechukiwa na Mwenyezi-Mungu atatumbukia humo.
15Mtoto hupenda mambo ya kijinga moyoni,
lakini fimbo ya nidhamu humwondolea hayo.
16Anayemdhulumu maskini atamfanya afaidike mwishowe,
anayewapa matajiri zawadi ataishia kuwa maskini.
Misemo thelathini ya wenye hekima
17Tega sikio usikie maneno ya wenye hekima,
elekeza moyo wako uzingatie maarifa yangu.
18Wewe utafurahi endapo utayaweka moyoni,
na kuyakariri kila wakati.
19Ninayependa kumfundisha leo ni wewe,
ili tegemeo lako liwe kwa Mwenyezi-Mungu.
20Nimekuandikia misemo thelathini,
misemo ya maonyo na maarifa,
21ili kukufundisha yaliyo sawa na kweli;
na mtu akikuuliza uweze kumpa jibu sahihi.
- 1 -
22Usimdhulumu maskini kwa kuwa ni maskini,
wala usimnyime fukara haki yake mahakamani.
23Maana Mwenyezi-Mungu atawatetea;
atawapokonya maisha yao wale watakaowadhulumu.
- 2 -
24Usifanye urafiki na mtu wa hasira,
wala usiandamane na mwenye ghadhabu,
25usije ukajifunza mwenendo wake,
ukajinasa kabisa katika mtego.
- 3 -
26Usiwe mmoja wao wenye kuweka ahadi,
watu ambao hujiweka wadhamini wa madeni.
27Ikiwa huna chochote cha kulipa,
hata kitanda unacholalia kitachukuliwa!
- 4 -
28Usiondoe alama ya mipaka ya zamani
ambayo iliwekwa na wazee wako.
- 5 -
29Je, yuko mtu mwenye maarifa kazini mwake?
Huyo atawatumikia wafalme;
hatawapa huduma yake watu wasiofaa.

Methali22;1-29

Biblia Habari Njema kwa Watu Wote(BHN)

"Swahili Na Waswahili"Mbarikiwe.

Thursday 18 July 2019

Kikombe Cha Asubuhi ; Methali 21...


Shalom,Habari za Asubuhi,Hamjambo,Mmeamkaje?

Tumshukuru Mungu katika yote....

Mungu wetu Baba yetu,Muumba wetu Muumba wa Mbingu na Nchi
Muumba wa vyote vilivyomo vinavyoonekana na visivyoonekana
Mungu wa walio hai,Mungu  mwenye huruma,Mungu wa upendo
Mungu wa Abrahamu,Isaka na Yakobo...
Asante kwa wema na fadhili zako kwetu
Asante kwa ulinzi wako kwetu wakati wote
Asante kwa kutuchagua tena na kutupa
kibali cha kuendelea kuiona leo hii
Asante kwa pumzi/uzima,afya na kuwatayari kwa majukumu yetu

Neema yako yatutosha ee Mungu wetu....!!

Kwa sababu hiyo, ningeweza, kwa uhodari kabisa, nikiwa ndugu yako katika kuungana na Kristo, kukuamuru ufanye unachopaswa kufanya. Lakini kwa sababu ya upendo, ni afadhali zaidi nikuombe. Nafanya hivi ingawa mimi ni Paulo, balozi wa Kristo Yesu, na sasa pia mfungwa kwa ajili yake.
Baba wa Mbinguni tunakuja mbele zako tukijinyenyekeza,tukijishusha na kujiachilia mikononi mwako
Mungu wetu tunaomba utusamehe dhambi zetu zote 
Baba wa Mbinguni nasi tunaomba ukatupe neema
ya kuweza kuwasamehe wale wote waliotukosea
Usitutie majaribuni Mungu wetu tunaomba utuepushe
na yule mwovu na kazi zake zote
Jehovah ututakase miili yetu na akili zetu
Baba wa Mbinguni tunaomba utufunike kwa Damu
ya Bwana na Mwokozi wetu Yesu Kristo wa Nazareti
yeye aliteseka kwanza ili sisi tupate kupona....

Basi, ninalo ombi moja kwako kuhusu mwanangu Onesimo, ambaye ni mwanangu katika Kristo kwani nimekuwa baba yake nikiwa kifungoni. Ni Onesimo yuleyule ambaye wakati mmoja alikuwa hakufai kitu, lakini sasa ananifaa mimi na wewe pia.
Mungu wetu tunaomba ukabariki kazi za mikono yetu
Baba wa Mbinguni tunaomba ukatupe ubunifu na maarifa katika utendaji
Jehovah nasi tukatende sawasawa na mapenzi yako
Yahweh tunaomba ukabariki ridhiki zetu ziingiazo/zitokazo
Mungu wetu nasi tunaomna ukatupe neema ya kuweza kuwabariki wenye kuhitaji
Tusipungukiwe katika mahitaji yetu
Baba wa Mbinguni tunaomba ukatupe kama inavyokupendeza wewe...

Yahweh tunayaweka maisha yetu mikononi mwako
Mungu wetu tunaomba ukabariki nyumba/ndoa zetu,
Jehovah tunaomba ulinzi wako kwetu na kwa vyote tunavyovimiliki
Yahweh tunaomba ukatubariki tuingiapo/tutokapo
Mungu wetu tunaomba ukavibariki vyote tunavyoenda kugusa/kutumia
Baba wa Mbinguni ukavitakase kwa Damu ya Bwana wetu Yesu Kristo
Mungu wetu ukatamalaki na kutuatamia
Baba wa Mbinguni tukawe salama rohoni
Yahwe ukatupe akili ya kutambua mema na mabaya
Mfalme wa amani amani yako ikatawale katika maisha yetu
Mungu wetu ukatupe macho ya kuona,masikio ya kusikia sauti yako na kuitii..
Baba wa Mbinguni  tunaomba ukatupe neema ya kufuata
njia zako,tukasimamie Neno lako,amri na sheria zako
siku zote za maisha yetu...
Ukatuguse kwa mkono wako wenye nguvu,ukatufanye chombo chema
ee Mungu wetu nasi tukatumike kama inavyokupendeza wewe
Roho Mtakatifu akatuongoze katika yote na tukawe na kiasi....

Sasa namrudisha kwako, naye ni kama moyo wangu mimi mwenyewe. Ningependa akae nami hapa anisaidie badala yako wakati niwapo kifungoni kwa sababu ya Injili. Lakini sitafanya chochote bila kibali chako. Sipendi kukulazimisha unisaidie, kwani wema wako unapaswa kutokana na hiari yako wewe mwenyewe na si kwa kulazimika.
Tazama watoto wako wenye shida/tabu,wote wanaopitia magumu/majaribu mbalimbali
Mungu wetu tunaomba ukawaguse kwa mkono wako wenye nguvu
kila mmoja na mahitaji yake
Mungu wetu tunaomba ukawasamehe pale walipo kwenda kinyume nawe
Yahweh tunaomba ukawape neema ya kuweza kujiombea,kufuata njia zako nazo zikawaweke huru...
Baba wa Mbinguni tunayaweka haya yote mikononi mwako
Kwakuwa Ufalme ni wako Nguvu na Utukufu hata Milele...
Amina...!!


Asanteni sana wapendwa katika Kristo Yesu kwakuwa nami,Baba wa Mbinguni aendelee kuwatendea sawasawa na mapenzi yake...
Nawapenda.

1Moyo wa mfalme ni kama maji yanayotiririka;
Mwenyezi-Mungu, huuongoza popote apendapo.
2Matendo yote ya mtu ni sawa machoni pake,
lakini Mwenyezi-Mungu hupima mioyo.
3Kutenda mambo mema na ya haki,
humpendeza Mwenyezi-Mungu kuliko tambiko.
4Macho ya kiburi na moyo wa majivuno
huonesha wazi dhambi ya waovu.
5Mipango ya mtu wa bidii huleta mali kwa wingi,
lakini kila aliye na pupa huishia patupu.
6Mali ipatikanayo kwa udanganyifu,
ni mvuke upitao na mtego wa kifo.
7Ukatili wa wakatili utawafutilia mbali,
maana wanakataa kutenda yaliyo ya haki.
8Njia ya mtu mwenye hatia imepotoka,
lakini mwenendo wa mnyofu umenyooka.
9Afadhali kuishi pembeni juu ya paa,
kuliko kuishi nyumbani na mwanamke mgomvi.
10Anachopania kutenda mtu mbaya ni uovu;
hata kwa jirani yake hana huruma.
11Ukimwadhibu mwenye dhihaka, mjinga hupata hekima;
ukimfundisha mwenye hekima, unampatia maarifa.
12Mungu Mwadilifu21:12 Mungu Mwadilifu:Mungu. anajua wanayotenda waovu nyumbani kwao;
naye atawaangusha na kuwaangamiza.
13Anayekataa kusikiliza kilio cha maskini,
naye pia hatasikilizwa atakapolilia msaada.
14Hasira hutulizwa kwa zawadi ya siri;
tunu apewayo mtu imefichwa hupooza ghadhabu.
15Haki ikitekelezwa watu wema hufurahi,
lakini watu waovu hufadhaishwa.
16Anayetangatanga mbali na njia ya busara,
atajikuta ametua miongoni mwa wafu.
17Anayependa anasa atakuwa maskini;
anayefikiria tu kula na kunywa hatatajirika.
18Mwovu atapata pigo ambalo halitampata mtu mwema,
mkosefu ataadhibiwa badala ya mnyofu.
19Afadhali kuishi jangwani,
kuliko kukaa na mwanamke mgomvi na msumbufu.
20Nyumbani kwa mwenye busara mna hazina za thamani,
lakini mpumbavu huponda mali yake yote.
21Anayepania uadilifu na huruma,
ataishi maisha marefu na kuheshimiwa.
22Mwenye hekima aweza kuteka mji wa wenye nguvu,
na kuziporomosha ngome wanazozitegemea.
23Achungaye mdomo wake na ulimi wake,
hujiepusha na matatizo.
24Mwenye majivuno na kiburi jina lake ni “Madharau;”
matendo yake yamejaa majivuno ya ufidhuli wake.
25Mvivu hufa kwa kutotimizwa tamaa zake,
maana mikono yake milegevu haitaki kufanya kazi.
26Mchana kutwa mwovu hutamani kupata kitu,
lakini mwadilifu hutoa, tena kwa ukarimu.
27Tambiko ya mwovu ni kitu cha kuchukiza,
huchukiza zaidi akiitoa kwa nia mbaya.
28Shahidi mwongo ataangamia,
lakini msikivu hawezi kunyamazishwa.
29Mtu mwovu hujionesha kuwa jasiri,
lakini mwadilifu huhakikisha ametenda sawa.
30Hakuna hekima, maarifa, wala mawaidha yoyote ya mtu,
yawezayo kumshinda Mwenyezi-Mungu.
31Farasi hutayarishwa kwa vita,
lakini ushindi wamtegemea Mwenyezi-Mungu.

Methali21;1-31

Biblia Habari Njema kwa Watu Wote(BHN)

"Swahili Na Waswahili"Mbarikiwe.

Wednesday 17 July 2019

Kikombe Cha Asubuhi ; Methali 20...


Shalom,Habari za Asubuhi,Hamjambo,Mmeamkaje?

Tumshukuru Mungu wetu katika yote...

Asante  Mungu wetu kwa wema na fadhili zako kwetu
Asante kwa ulinzi wako kwetu wakati wote
Asante kwa kutuchagua tena na kutupa
kibali cha kuendelea kuiona leo hii
Asante kwa pumzi/uzima,afya na kuwatayari kwa majukumu yetu


Utukuzwe ee Mungu wetu,usifiwe Baba wa Mbinguni

Neema yako yatutosha  Mungu wetu..!

Mimi Paulo, mfungwa kwa ajili ya Kristo Yesu, na ndugu Timotheo, ninakuandikia wewe Filemoni mpendwa, mfanyakazi mwenzetu, na kanisa linalokutana nyumbani kwako, na wewe dada Afia, na askari mwenzetu Arkipo. Tunawatakieni neema na amani kutoka kwa Mungu Baba yetu, na kwa Bwana Yesu Kristo.
Baba wa Mbinguni tunakuja mbele zako tukijinyenyekeza,tukijishusha na kujiachilia mikononi mwako
Mungu wetu tunaomba utusamehe dhambi zetu zote
Baba wa Mbinguni nasi tunaomba utupe neema ya kuweza kuwasamehe wale wote waliotukosea,Usitutie majaribuni Mungu wetu tunaomba utuepushe na yule mwovu na kazi zake zote,Jehovah ututakase miili yetu na akili zetu Baba wa Mbinguni tunaomba utufunike kwa  Damu ya Bwana na Mwokozi wetu Yesu Kristo wa Nazareti,
Yeye aliteseka kwanza ili sisi tupate kupona....

Kila wakati ninaposali, nakukumbuka wewe Filemoni, na kumshukuru Mungu, maana nasikia habari za imani yako kwa Bwana Yesu na upendo wako kwa watu wote wa Mungu.
Mungu wetu tunaomba ukabariki kazi za mikono yetu
Baba wa Mbinguni tunaomba ukatupe ubunifu na maarifa 
katika utendaji
Jehovah nasi tukatende sawasawa na mapenzi yako
Baba wa Mbinguni tunaomba ukabariki ridhiki zetu
ziingiazo/zitokazo
Mungu wetu nasi tunaomba ukatupe neema ya kuweza
kuwabariki wenye kuhitaji
Yahweh tusipungukiwe katika mahitaji yetu
Mungu wetu ukatupe kama inavyokupendeza wewe

Jehovah tunayaweka maisha yetu mikononi mwako
Baba wa Mbinguni tunaomba ukabariki nyumba/ndoa zetu,
watoto,wazazi wetu,familia/ndugu na wote wanaotuzunguka
Jehovah tunaomba ulinzi wako kwetu na kwa vyote tunavyo vimiliki
Yahweh tunaomba ukatubariki tuingiapo/tutokapo
Mungu wetu tunaomba ukavibariki vyote tunavyoenda kugusa/kutumia
Baba wa Mbinguni ukavitakase kwa Damu ya Bwana wetu Yesu Kristo
Mungu wetu ukatamalaki na kutuatamia
Baba wa Mbinguni tukawe salama rohoni
Mfalme wa amani amani yako ikatawale katika maisha yetu
Mungu wetu ukatupe macho ya kuona na masikio ya kusikia 
sauti yako na kuitii
Baba wa Mbinguni tunaomba ukatupe neema ya kufuata njia zako
Yahweh tukasimamie Neno lako amri na sheria zako siku zote 
za maisha yetu

Mungu  wetu ukaonekane katika maisha yetu popote tupitapo na ikajulikane kwamba upo 

Neema zako zikawe nasi Nuru yako ikaangaze katika maisha yetu
Ukatufanye barua njema ee Mungu wetu nasi tukasomeke kama
inavyokupendeza wewe
Roho Mtakatifu akatuongoze katika yote na tukawe na kiasi...

Naomba ili imani hiyo unayoshiriki pamoja nasi ikuwezeshe kuwa na ujuzi mkamilifu zaidi wa baraka zote tunazopata katika kuungana kwetu na Kristo. Ndugu, upendo wako umeniletea furaha kubwa na kunipa moyo sana! Nawe umeichangamsha mioyo ya watu wa Mungu.
Tazama wenye shida/tabu,Mungu wetu tunaomba
 ukawaguse kila mmoja na mahitaji yake
Baba wa Mbinguni tunaomba ukawasamehe pale walipokwenda
kinyume nawe
Mungu wetu ukawape neema ya kujiombea,macho ya rohoni,masikio yakusikia sauti yako,wakafuate njia zako nazo zikawaweke huru
Mungu wetu tunaomba ukasikie kulia kwao
Baba wa Mbinguni tunomba ukawafute machozi yao
Nuru yako ikaangaze katika maisha yao
Mungu wetu tunaomba ukawatendee sawasawa na mapenzi yako
Kwakuwa Ufalme ni wako Nguvu na Utukufu hata Milele
Amina....!!!


Wapendwa katika Kristo Yesu asanteni sana
kwakuwanami/kunisoma

Mungu Baba aendelee kuwabariki na kuwatendea
kama inavyompendeza yeye
Amani ya Bwana wetu Yesu Kristo na upendo wa Mungu Baba
ukae nanyi daima....

Nawapenda.

1Divai huleta dhihaka na kileo huleta ugomvi;
yeyote anayevutiwa navyo hana hekima.
2Ghadhabu kali ya mfalme ni kama simba angurumaye;
anayemkasirisha anayahatarisha maisha yake.
3Ni jambo la heshima kuepa ugomvi;
wapumbavu ndio wanaogombana.
4Mvivu halimi wakati wa kulima;
wakati wa mavuno atatafuta asipate chochote.
5Fikira za mtu zimefichika kama kilindi cha maji;
lakini mtu mwenye busara ajua kuzichota humo.
6Watu wengi hujivunia kuwa wema,
lakini mwaminifu wa kweli apatikana wapi?
7Mtu mwadilifu akiishi kwa unyofu;
watoto wake atakaowaacha watabarikiwa.
8Mfalme mwema aketipo kutoa hukumu,
huupepeta uovu wote kwa macho yake.
9Nani athubutuye kusema: “Nimeutakasa moyo wangu;
mimi nimetakasika dhambi yangu?”
10Mizani ya udanganyifu na vipimo vya udanganyifu,
vyote ni chukizo kwa Mwenyezi-Mungu.
11Hata mtoto hujulikana kwa matendo yake,
kama tabia yake ni njema na aminifu.
12Sikio lisikialo na jicho lionalo,
yote mawili kayafanya Mwenyezi-Mungu.
13Usipende kulala tu usije ukawa maskini;
uwe macho nawe utakuwa na chakula kingi.
14“Hakifai, hakifai”, mnunuzi hulalamika,
lakini akiondoka hujisifu amepunguziwa bei.
15Kuna dhahabu na wingi wa mawe ya thamani kubwa;
lakini cha thamani kubwa zaidi ni maneno ya busara!
16Mtu akiahidi mbele yako kumdhamini mgeni,
chukua nguo yake;
mfanye awajibike kwa kuwadhamini wageni.
17Chakula kipatikanacho kwa udanganyifu ni kitamu,
lakini baadaye huwa kama mchanga kinywani.
18Mipango mizuri hufanyika kwa kushauriana;
ukitaka kuanza vita lazima kutafakari kwanza.
19Mpiga domo hafichi siri,
kwa hiyo mwepe mtu wa kuropoka.
20Anayemlaani baba yake au mama yake,
mwanga wa uhai wake utazimwa kama taa gizani.
21Mali iliyopatikana kwa haraka mwanzoni,
haitakuwa ya heri mwishoni.
22Usiseme, “Nitalipiza ubaya niliotendewa.”
Mtegemee Mwenyezi-Mungu naye atakusaidia.
23Mizani ya udanganyifu ni chukizo kwa Mwenyezi-Mungu,
na vipimo visivyo halali ni kitu kibaya.
24Hatua za mtu huongozwa na Mwenyezi-Mungu;
awezaje binadamu kujua njia ya kwenda?
25Ni hatari kusema kwa mzaha “Usiahidi kumpa Mungu kitu bila kufikiri,
la sivyo utaanza kusikitika baada ya nadhiri yako.”
26Mfalme mwenye busara huwapepeta waovu;
huwaadhibu bila huruma.
27Dhamiri ya mtu ni taa ya Mwenyezi-Mungu;
huchunguza nafsi yake mtu mpaka ndani kabisa.
28Wema na uaminifu humkinga mfalme;
utawala wake huimarishwa kwa uadilifu.
29Fahari ya vijana ni nguvu zao,
uzuri wa vikongwe ni mvi za uzee.
30Mapigo yanayoumiza ni dawa ya kuondoa uovu;
viboko husafisha nafsi mpaka ndani kabisa.

Methali20;1-30

Biblia Habari Njema kwa Watu Wote(BHN)

"Swahili Na Waswahili"Mbarikiwe.