Swahili na Waswahili

Swahili na Waswahili
Waswahili na Mswahili Rachel Siwa...Pamoja Daima!!

Tuesday 6 November 2018

Kikombe Cha Asubuhi ;Yobu 31...


Shalom,Habari za Asubuhi,Hamjambo,Mmeamkaje?

Tumshukuru Mungu katika yote....

Mungu wetu Baba yetu,Muumba wetu Muumba wa Mbingu na Nchi
Muumba wa vyote vilivyomo vinavyoonekana na visivyoonekana
Mungu wa walio hai,Mungu  mwenye huruma,Mungu wa upendo
Mungu wa Abrahamu,Isaka na Yakobo..
Yahweh..!Jehovah..! Adonai..!Elohim..!El Olam..!El Qanna..!
El Elyon..!El shaddai..!Emanueli...!-Mungu pamoja nasi...
Unastahili sifa Mungu wetu,Unastahili kuabudiwa Jehovah,
Unastahili kuhimidiwa Yahweh,Unastahili Kutukuzwa Baba wa Mbinguni....!



Asante kwa wema na fadhili zako kwetu
Asante kwa ulinzi wako kwetu wakati wote
Asante kwa kutuchagua tena na kutupa
kibali cha kuendelea kuiona leo hii
Asante kwa pumzi/uzima,afya na kuwatayari kwa majukumu yetu

Neema yako yatutosha ee Mungu wetu....!!

Basi, ikiwa mmefufuka pamoja na Kristo, panieni mambo ya juu, kule Kristo aliko, ameketi upande wa kulia wa Mungu. Muwe na hamu ya mambo ya huko juu, na siyo mambo ya hapa duniani. Maana nyinyi mmekufa na uhai wenu umefichwa pamoja na Kristo katika Mungu. Uhai wenu halisi ni Kristo, na wakati atakapotokea ndipo nanyi pia mtakapotokea pamoja naye katika utukufu.

Baba wa Mbinguni tunakuja mbele zako tukijinyenyekeza,tukijishusha na kujiachilia mikononi mwako
Mungu wetu tunaomba utusamehe dhambi zetu zote tulizo zifanya
Kwakuwaza,kwakunena,kwakutenda,kwakujua/kutojua
Baba wa Mbinguni nasi tunaomba ukatupe neema
ya kuweza kuwasamehe wale wote waliotukosea
Usitutie majaribu Mungu wetu tunaomba utuepushe
na yule mwovu na kazi zake zote
Jehovah ututakase miili yetu na akili zetu
Baba wa Mbinguni tunaomba utufunike kwa Damu
ya Bwana na Mwokozi wetu Yesu Kristo wa Nazaretiyeye aliteseka kwanza ili sisi tupate kupona....


Basi, ueni chochote kilicho ndani yenu ambacho ni cha kidunia: Uasherati, uchafu, shauku, tamaa mbaya na uchu (ambao ni sawa na kuabudu sanamu). Kwa sababu ya mambo hayo hasira ya Mungu huwajia wote wanaomwasi. Wakati mmoja nyinyi pia mliishi kufuatana na mambo hayo, mlipotawaliwa nayo. Lakini sasa mnapaswa kuachana na mambo haya yote: Hasira, tamaa na uovu; kufuru au maneno yasiyofaa yasitoke kamwe vinywani mwenu. Msiambiane uongo, kwani nyinyi mmekwisha vua ule utu wa kale pamoja na matendo yake yote, mkavaa utu mpya. Huu unaendelea kurekebishwa na Mungu, Muumba wake, kadiri ya mfano wake, ili mpate kumjua Mungu kwa ukamilifu.

Mungu wetu tunaomba ukabariki kazi za mikono yetu
Baba wa Mbinguni tunaomba ukatupe ubunifu na maarifa katika utendaji

Jehovah nasi tukatende sawasawa na mapenzi yako
Yahweh tunaomba ukabariki ridhiki zetu ziingiazo/zitokazo
Mungu wetu nasi tunaomba ukatupe neema ya kuweza
kuwabariki wenye kuhitaji
Tusipungukiwe katika mahitaji yetu Baba wa Mbinguni
tunaomba ukatupe kama inavyokupendeza wewe....



Yahweh  tunayaweka maisha yetu mikononi mwako
Mungu wetu tunaomba ukabariki nyumba/ndoa zetu,
watoto,wazazi wetu,familia/ndugu na wote wanaotuzunguka
Jehovah tunaomba ulinzi wako kwetu na kwa vyote tunavyo vimiliki
Yahweh tunaomba ukatubariki tuingiapo/tutokapo
Mungu wetu tunaomba ukavibariki vyote tunavyoenda kugusa/kutumia
Baba wa Mbinguni ukavitakase kwa Damu ya Bwana wetu Yesu Kristo
Mungu wetu ukatamalaki na kutuatamia
Baba wa Mbinguni tukawe salama rohoni

Yahweh ukatupe akili ya kutambua mema na mabaya
Mfalme wa amani amani yako ikatawale katika maisha yetu
Mungu wetu ukatupe macho ya kuona na masikio ya kusikia 
sauti yako na kuitii
Baba wa Mbinguni tunaomba ukatupe neema ya kufuata njia zako
Yahweh tukasimamie Neno lako amri na sheria zako siku zote 
za maisha yetu
Mungu wetu ukaonekane katika maisha yetu
Baba wa Mbinguni tukanene yaliyo yako
Neema zako zikawe nasi Nuru yako ikaangaze katika maisha yetu
ukatuguse kwa mkono wako wenye nguvu
Ukatufanye chombo chema ee Mungu wetu nasi tukatumike kama
inavyokupendeza wewe
Roho Mtakatifu akatuongoze katika yote na tukawe na kiasi...



Katika hali hii, hakuna tena tofauti kati ya Mgiriki na Myahudi, aliyetahiriwa na asiyetahiriwa, msomi na asiye msomi, mtumwa na mtu aliye huru. Kristo ni kila kitu, na yumo katika yote.

Tazama watoto wako wanaokutafuta/kukuomba kwa bidii na imani, Mungu wetu tunawaweka mikononi mwako wenye shida/tabu,
wote wanaopitia magumu/majaribu mbalimbali
Mungu wetu tunaomba ukawaguse kwa mkono wako wenye nguvu
kila mmoja na mahitaji yake
Baba wa Mbinguni tunaomba ukaonekane katika maisha yao
Mungu wetu tunaomba ukawasamehe pale walipokwenda
kinyume nawe Yahweh tunaomba ukawape neema ya kujiombea
Kufuata njia zako nazo zikawaweke huru
Ukawape macho ya rohoni ee Mungu wetu na masikio ya kusikia
sauti yako,Ukawaokoe na kuwalinda,ukawaponye kimwili na kiroho
Nuru yako ikaangaze katika maisha yao,Amani ikatawale katika maisha yao,Upendo ukadumu kati yao
 

Baba wa Mbinguni tunayaweke haya yote mikono mwako
tukiamini Mungu wetu utawatendea sawasawa na mapenzi yako
Kwakuwa Ufalme ni wako Nguvu na Utukufu hata Milele
Amina...!!



Asanteni sana wapendwa katika Kristo Yesu
kwakuwanami/kunisoma Mungu Baba aendelee
kuwabariki na kuwatendea kama inavyompendeza yeye
Amani ya Bwana wetu Yesu Kristo na Upendo wa Mungu Baba
ukae nanyi daima
Nawapenda. 


1“Nimejifunga rasmi mimi mwenyewe,
macho yangu yasimtazame msichana kwa tamaa.
2Au je, nangojea nini kutoka kwa Mungu aliye juu?
Mungu Mwenye Nguvu ameniwekea kitu gani?
3Je, maafa hayawapati watu waovu
na maangamizi wale watendao mabaya?
4Je, Mungu haoni njia zangu,
na kujua hatua zangu zote?
5“Kama nimeishi kwa kufuata uongo,
kama nimekuwa mbioni kudanganya watu,
6Mungu na anipime katika mizani ya haki,
naye ataona kwamba sina hatia.
7Kama hatua zangu zimepotoka,
moyo wangu ukafuata tamaa za macho yangu;
kama mikono yangu imechafuliwa na dhambi,
8jasho langu na liliwe na mtu mwingine,
mazao yangu shambani na yangolewe.
9“Kama moyo wangu umevutwa kwa mke wa mtu,
kama nimenyemelea mlangoni kwa jirani yangu,
10basi, mke wangu na ampikie mume mwingine,
na wanaume wengine wamtumie.
11Jambo hilo ni kosa kuu la jinai,
uovu ambao hakimu lazima atoe adhabu.
12Kosa langu lingekuwa kama moto,
wa kuniteketeza na kuangamiza,
na kuchoma kabisa mapato yangu yote.
13Kama nimekataa kesi ya mtumishi wangu
wa kiume au wa kike,
waliponiletea malalamiko yao,
14nitafanya nini basi Mungu atakaponikabili?
Je, akinichunguza nitamjibu nini?
15Maana Mungu ndiye aliyeniumba mimi na mtumishi wangu;
yeye ndiye aliyetuumba sisi wote.
16 Taz Yobu 4:7-11,16 “Je, nimepata kumnyima maskini mahitaji yake
au kuwafanya wajane watumaini bure?
17Je, nimekula chakula changu peke yangu,
bila kuwaachia yatima nao wapate chochote?
18La! Tangu ujana wangu nimekuwa mlezi wao,
tangu utoto wangu nimewaongoza wajane.
19Je, nilimwona mtu anakufa kwa kukosa nguo,
au maskini ambaye hana nguo ya kuvaa,
20bila kumpa joto kwa mavazi ya manyoya ya kondoo wangu
naye akanitakia baraka za shukrani ya moyo?
21Kama nimenyosha mkono mahakamani dhidi ya yatima,
nikijua nitapendelewa na mahakimu,
22basi, bega langu na lingoke,
mkono wangu na ukwanyuke kiwikoni mwake.
23Maana maafa kutoka kwa Mungu ni kitisho kwangu;
mimi siwezi kuukabili ukuu wake.
24 Taz Sir 31:5-10 “Je, tumaini langu nimeliweka katika dhahabu,
au, nimeiambia dhahabu safi, ‘Wewe ni usalama wangu?’
25Je, nimepata kufurahia wingi wa utajiri wangu
au kujivunia mapato ya mikono yangu?
26Kama nimeliangalia jua likiangaza,
na mwezi ukipita katika uzuri wake,
27na moyo wangu ukashawishika kuviabudu,
nami nikaibusu mikono yangu kwa heshima yake,
28huo pia ungekuwa uovu wa kuadhibiwa na mahakimu
maana ningekuwa mwongo mbele ya Mungu aliye juu.
29“Je, nimefurahia kuangamia kwa adui yangu,
au kufurahi alipopatwa na maafa?
30La! Sikuruhusu kinywa changu kumtakia mabaya,
kwa kumlaani ili afe.
31Watumishi wangu wote wanasema wazi
kila mgeni amekaribishwa nyumbani mwangu.
32Msafiri hakulala nje ya nyumba yangu,
nilimfungulia mlango mpita njia.
33Je nimeficha makosa yangu kama wengine?
Je nimekataa kukiri dhambi zangu?
34Sijaogopa kusimama mbele ya umati wa watu,
wala kukaa kimya au kujifungia ndani,
eti kwa kuogopa kutishwa na dharau zao.
35Laiti angekuwapo mtu wa kunisikiliza!
Naweza kutia sahihi yangu katika kila nilichosema.
Namwambia Mungu Mwenye Nguvu anijibu!
Laiti mashtaka wanayonitolea maadui zangu yangeandikwa!
36Ningeyavaa kwa maringo mabegani
na kujivisha kichwani kama taji.
37Ningemhesabia Mungu kila kitu nilichofanya,
ningemwendea kama mwana wa mfalme.
38Kama nimeiiba ardhi ninayoilima,
nikasababisha mifereji yake iomboleze,
39kwa kufaidika na mazao yake bila kulipa
na kusababisha kifo cha wenyewe,
40basi miiba na iote humo badala ya ngano,
na magugu badala ya shayiri.”
Mwisho wa hoja za Yobu.



Yobu31;1-40

Biblia Habari Njema kwa Watu Wote(BHN)

"Swahili Na Waswahili"Mbarikiwe.

Monday 5 November 2018

Kikombe Cha Asubuhi ;Yobu 30...

Shalom,Habari za Asubuhi,Hamjambo,Mmeamkaje?

Haleluyah ni siku/wiki/mwezi  mwingine tena Mungu wetu ametuchagua
na kutupa kibali cha kuendelea kuiona leo hii
Si kwamba sisi tumetenda mema sana wala si kwa nguvu zetu
si kwa utashi wetu wala si kwa akili zetu si kwamba sisi
ni wazuri mno si kwa uwezo wetu sisi kuwa hivi tulivyo leo hii
Ni kwa rehema/neema zake ni kwa mapenzi yake Mungu wetu....

Tumshukuru Mungu wetu katika yote...

Asante Mungu wetu kwa wema na fadhili zako kwetu
Asante kwa ulinzi wako kwetu wakati wote
Asante kwa pumzi/uzima,afya na kuwa tayari kwa majukumu yetu
Sifa na Utukufu tunakurudshia Mungu wetu....!!



“Mimi siwezi kufanya kitu kwa uwezo wangu mwenyewe. Mimi ninahukumu kama ninavyosikia kutoka kwa Baba, nayo hukumu yangu ni ya haki. Nia yangu si kufanya nipendavyo mwenyewe, bali apendavyo yule aliyenituma. Nikijishuhudia mimi mwenyewe, ushahidi wangu hauwezi kukubaliwa kuwa wa kweli. Lakini yuko mwingine ambaye hutoa ushahidi juu yangu, nami najua kwamba yote anayosema juu yangu ni ya kweli. Nyinyi mlituma ujumbe kwa Yohane naye aliushuhudia ukweli. Si kwamba mimi nautegemea ushahidi wa wanadamu, lakini nasema mambo haya ili mpate kuokolewa.


Tazama jana imepita ee Mungu wetu leo ni siku mpya na kesho ni siku nyingine Jehovah tunakuja mbele zako tukijinyenyekeza,tukijishusha na kujiachilia mikononi mwako
 Mungu wetu tunaomba utusamehe dhambi zetu zote tulizozifanya kwakuwaza,kwakunena,kwakutenda,kwakujua/kutojua
Baba wa Mbinguni nasi tunaomba utupe neema ya kuweza kuwasamehe wale wote waliotukosea
Jehovah usitutie majaribu Mungu wetu tunaomba utuepushe na yule mwovu na kazi zake zote
Yahweh tunaomba ututakase miili yetu na akili zetu
Baba wa Mbinguni utufunike kwa Damu ya Bwana na Mwokozi wetu Yesu Kristo wa Nazareti
yeye aliteseka kwanza ili sisi tupate kupona
Kwakupigwa kwake sisi tumepata kupona...

Yohane alikuwa kama taa iliyokuwa ikiwaka na kuangaza, nanyi mlikuwa tayari kufurahia mwanga huo kwa kitambo. Lakini mimi nina ushahidi juu yangu ambao ni mkuu zaidi kuliko ule wa Yohane. Kwa maana kazi ninazofanya, kazi alizonipa Baba nizifanye, ndizo zinazonishuhudia kwamba Baba ndiye aliyenituma. Naye Baba aliyenituma hunishuhudia. Nyinyi hamjapata kamwe kusikia sauti yake, wala kuuona uso wake, na ujumbe wake haukai ndani yenu maana hamkumwamini yule aliyemtuma. Nyinyi huyachunguza Maandiko Matakatifu mkidhani kwamba ndani yake mtapata uhai wa milele; na kumbe maandiko hayohayo yananishuhudia! Hata hivyo, nyinyi hamtaki kuja kwangu ili mpate uhai.
Yahweh tunaomba ukabariki kazi za mikono yetu
Baba wa Mbinguni tunaomba ukatupe ubunifu na maarifa 
katika utendaji
Jehovah nasi tukatende sawasawa na mapenzi yako
Baba wa Mbinguni tunaomba ukabariki ridhiki zetu
ziingiazo/zitokazo
Mungu wetu nasi tunaomba ukatupe neema ya kuweza
kuwabariki wenye kuhitaji
Yahweh tusipungukiwe katika mahitaji yetu
Mungu wetu ukatupe kama inavyokupendeza wewe

Baba wa Mbinguni tunayaweka maisha yetu mikononi mwako
Mungu wetu tunaomba ukabariki nyumba/ndoa zetu,
watoto,wazazi wetu,familia/ndugu na wote wanaotuzunguka
Jehovah tunaomba ulinzi wako kwetu na kwa vyote tunavyo vimiliki
Yahweh tunaomba ukatubariki tuingiapo/tutokapo
Mungu wetu tunaomba ukavibariki vyote tunavyoenda kugusa/kutumia
Baba wa Mbinguni ukavitakase kwa Damu ya Bwana wetu Yesu Kristo
Mungu wetu ukatamalaki na kutuatamia
Baba wa Mbinguni tukawe salama rohoni
Mfalme wa amani amani yako ikatawale katika maisha yetu
Mungu wetu ukatupe macho ya kuona na masikio ya kusikia 
sauti yako na kuitii
Baba wa Mbinguni tunaomba ukatupe neema ya kufuata njia zako
Yahweh tukasimamie Neno lako amri na sheria zako siku zote 
za maisha yetu
Mungu wetu ukaonekane katika maisha yetu
Neema zako zikawe nasi Nuru yako ikaangaze katika maisha yetu
ukatuguse kwa mkono wako wenye nguvu
Ukatufanye chombo chema ee Mungu wetu nasi tukatumike kama
inavyokupendeza wewe
Roho Mtakatifu akatuongoze katika yote na tukawe na kiasi...


“Shabaha yangu si kupata sifa kutoka kwa watu. Lakini nawajua nyinyi, najua kwamba upendo kwa Mungu haumo mioyoni mwenu. Mimi nimekuja kwa mamlaka ya Baba yangu, lakini hamnipokei; bali mtu mwingine akija kwa mamlaka yake mwenyewe, mtampokea. Mwawezaje kuamini, hali nyinyi mnapenda kupokea sifa kutoka kwenu nyinyi wenyewe, wala hamtafuti sifa kutoka kwake yeye aliye peke yake Mungu? Msifikiri kwamba mimi nitawashtaki kwa Baba. Mose ambaye nyinyi mmemtumainia ndiye atakayewashtaki. Kama kweli mngemwamini Mose, mngeniamini na mimi pia, maana Mose aliandika juu yangu. Lakini hamyaamini yale aliyoandika; mtawezaje basi, kuamini maneno yangu?”

Mungu wetu tunawaweka mikononi mwako wenye shida/tabu,wote wanaopotia magumu/majaribu mbalimbali
watoto wako wanaokuomba kwa bidii na imani
Mungu wetu tunaomba ukawaguse kwa mkono wako wenye nguvu
 kila mmoja na mahitaji yake 
Yahweh tunaomba ukaonekane katika maisha yao
Jehovah tunaomba ukawaokoe,ukawavushe salama na  kuwalinda
Mungu wetu tunaomba ukawasamehe pale walipokwenda kinyume nawe
Baba wa Mbinguni ukawape neema ya kujiombea,kufuata njia zako
wakasimaie Neno lako nalo likaweke huru
Mungu wetu tunaomba ukasikie kuomba kwetu
Baba wa Mbinguni ukapokee sala/maombi yetu
Mungu wetu ukawatendee sawasawa na mapenzi yako
Kwakuwa Ufalme ni wako Nguvu na Utukufu hata Milele
Amina...!!

Asanteni sana wapendwa katika Kristo Yesu kwakuwa nami
Mungu Baba aendelee kuwabariki na kuwatendea 
kama inavyompendeza yeye....
Nawapenda.



1“Lakini sasa watu wananidhihaki,
tena watu walio wadogo kuliko mimi;
watu ambao baba zao niliwaona hawafai
hata kuwaangalia mbwa wangu wakilinda kondoo.
2Ningepata faida gani mikononi mwao,
watu ambao nguvu zao zilikuwa zimewaishia?
3Katika ufukara na njaa kali
walitafutatafuta cha kutafuna nyikani30:3 walitafutatafuta … nyikani: Tafsiri nyingine: Waliguguna huko nyikani.
sehemu tupu zisizokuwa na chakula.
4Walichuma mimea jangwani na majani msituni wakala,
walikula hata mizizi ya mti wa mfagio.
5Walifukuzwa mbali na watu,
watu waliwapigia kelele kama wezi.
6Iliwapasa kutafuta usalama mapangoni,
kwenye mashimo ardhini na miambani.
7Huko vichakani walilia kama wanyama,
walikusanyika pamoja chini ya upupu.
8Walikuwa wapumbavu wakuu na mabaradhuli
ambao walilazimika kufukuzwa nchini kwa kiboko.
9“Na sasa wamenitungia wimbo wa kunizomea,
nimekuwa kitu cha dhihaka kwao.
10Wananichukia na kuniepa;
wakiniona tu wanatema mate.
11Kwa kuwa Mungu amenidhoofisha na kuniaibisha,
wamekuwa huru kunitendea wapendavyo.
12Genge la watu lainuka kunishtaki30:12 kunishtaki: Au upande wangu wa kulia.
likitafuta kuniangusha kwa kunitegea.
Linanishambulia ili niangamie.
13Watu hao hukata njia yangu
huchochea balaa yangu,
na hapana mtu wa kuwazuia.30:13 kuwazuia: Kiebrania: Kuwasaidia.
14Wanakuja kama kwenye ufa mkubwa,
na baada ya shambulio wanasonga mbele.
15Hofu kuu imenishika;
hadhi yangu imetoweka kama kwa upepo,
na ufanisi wangu umepita kama wingu.
16“Sasa sina nguvu yoyote nafsini mwangu;
siku za mateso zimenikumba.
17Usiku mifupa yangu yote huuma,
maumivu yanayonitafuna hayapoi.
18Mungu amenikaba kwa mavazi yangu,
amenibana kama ukosi wa shati langu.30:18 aya hii ni ngumu sana kutafsiri.
19Amenibwaga matopeni;
nimekuwa kama majivu na mavumbi.
20Nakulilia, lakini hunijibu,
nasimama kuomba lakini hunisikilizi.
21Umegeuka kuwa mkatili kwangu,
wanitesa kwa mkono wako wenye nguvu.
22Wanitupa katika upepo na kunipeperusha;
wanisukasuka huku na huko katika dhoruba kali.
23Naam! Najua utanipeleka tu kifoni,
mahali watakapokutana wote waishio.
24“Je, mtu akikumbwa na maangamizi hainui mkono?
Je, mtu akiwa taabuni haombi msaada30:24 aya hii katika Kiebrania si dhahiri.
25Je, sikuwalilia wale waliokuwa na taabu?
Je, sikuona uchungu kwa ajili ya maskini?
26Lakini nilipotazamia mema, mabaya yalinipata,
nilipongojea mwanga, giza lilikuja.
27Moyo wangu wahangaika wala hautulii kamwe;
siku za mateso zimekumbana nami.
28Napitapita nikiomboleza, kwangu hamna jua.
Nasimama hadharani kuomba msaada.
29Kwa kilio nimekuwa ndugu yake mbwamwitu,
mimi na mbuni hamna tofauti.
30Ngozi yangu imebambuka
mifupa yangu inaungua kwa homa.
31Kinubi changu kimekuwa cha kufanya matanga
filimbi yangu kwa ajili ya kuomboleza.




Yobu30;1-31

Biblia Habari Njema kwa Watu Wote(BHN)

"Swahili Na Waswahili"Mbarikiwe.

Friday 2 November 2018

Kikombe Cha Asubuhi ;Yobu 29...



Shalom,Habari za Asubuhi,Hamjambo,Mmeamkaje?
Tumshukuru Mungu wetu katika yote...

Asante kwa wema na fadhili zako kwetu
Asante

 kwa ulinzi wako kwetu wakati wote
Asante kwa kutuchagua tena na kutupa
kibali cha kuendelea kuiona leo hii
Asante kwa pumzi/uzima,afya na kuwatayari kwa majukumu yetu


Utukuzwe ee Mungu wetu,usifiwe Baba wa Mbinguni

Jehovah  Jireh..!Jehovah Nissi..!Jehovah Raah..!
Jehovah Rapha..!Jehovah Shammah..!Jehovah Shamlom..!
Emanuel-Mungu pamohja nasi..!!
Neema yako yatutosha Baba wa Mbinguni..!

Kwa vile Yesu alifanya jambo hilo siku ya Sabato, Wayahudi walianza kumdhulumu. Basi, Yesu akawaambia, “Baba yangu anafanya kazi daima, nami pia nafanya kazi.” Kwa sababu ya maneno haya, viongozi wa Wayahudi walizidi kutafuta njia ya kumuua Yesu; si kwa kuwa aliivunja Sheria ya Sabato tu, bali pia kwa kuwa alisema kwamba Mungu ni Baba yake, na hivyo akajifanya sawa na Mungu.

Baba wa Mbinguni tunakuja mbele zako tukijinyenyekeza,tukijishusha
na kujiachilia mikononi mwako
Mungu wetu tunaomba utusamehe dhambi zetu zote tulizo zifanya
Kwakuwaza,kwakunena,kwakutenda,kwakujua/kutojua
Baba wa Mbinguni nasi tunaomba ukatupe neema
ya kuweza kuwasamehe wale wote waliotukosea
Usitutie majaribu Mungu wetu tunaomba utuepushe
na yule mwovu na kazi zake zote
Jehovah ututakase miili yetu na akili zetu
Baba wa Mbinguni tunaomba utufunike kwa Damu
ya Bwana na Mwokozi wetu Yesu Kristo wa Nazareti
yeye aliteseka kwanza ili sisi tupate kupona...

Yesu akawaambia, “Kweli nawaambieni, Mwana hawezi kufanya kitu peke yake; anaweza tu kufanya kile anachomwona Baba akikifanya. Maana kile anachofanya Baba, Mwana hukifanya vilevile. Baba ampenda Mwana, na humwonesha kila kitu anachokifanya yeye mwenyewe, tena atamwonesha mambo makuu kuliko haya, nanyi mtastaajabu. Kama vile Baba huwafufua wafu na kuwapa uhai, vivyo hivyo naye Mwana huwapa uhai wale anaopenda. Baba hamhukumu mtu yeyote; shughuli yote ya hukumu amemkabidhi Mwana, ili watu wote wamheshimu Mwana kama vile wanavyomheshimu Baba. Asiyemheshimu Mwana hamheshimu Baba ambaye amemtuma.

Mungu wetu tunaomba ukabariki kazi za mikono yetu
Baba wa Mbinguni tunaomba ukatupe ubunifu na maarifa 
katika utendaji
Jehovah nasi tukatende sawasawa na mapenzi yako
Baba wa Mbinguni tunaomba ukabariki ridhiki zetu
ziingiazo/zitokazo
Mungu wetu nasi tunaomba ukatupe neema ya kuweza
kuwabariki wenye kuhitaji
Yahweh tusipungukiwe katika mahitaji yetu
Mungu wetu ukatupe kama inavyokupendeza wewe



Jehovah tunayaweka maisha yetu mikononi mwako
Baba wa Mbinguni tunaomba ukabariki nyumba/ndoa zetu,
watoto,wazazi wetu,familia/ndugu na wote wanaotuzunguka
Jehovah tunaomba ulinzi wako kwetu na kwa vyote tunavyo vimiliki
Yahweh tunaomba ukatubariki tuingiapo/tutokapo
Mungu wetu tunaomba ukavibariki vyote tunavyoenda kugusa/kutumia
Baba wa Mbinguni ukavitakase kwa Damu ya Bwana wetu Yesu Kristo
Mungu wetu ukatamalaki na kutuatamia
Baba wa Mbinguni tukawe salama rohoni
Mfalme wa amani amani yako ikatawale katika maisha yetu
Mungu wetu ukatupe macho ya kuona na masikio ya kusikia 
sauti yako na kuitii
Baba wa Mbinguni tunaomba ukatupe neema ya kufuata njia zako
Yahweh tukasimamie Neno lako amri na sheria zako siku zote 
za maisha yetu

Mungu wetu tunaomba ukatupe akili ya kutambua mema na mabaya Baba wa Mbinguni ukaonekane katika maisha yetu popote tupitapo na ikajulikane kwamba upo Mungu wetu

Neema zako zikawe nasi Nuru yako ikaangaze katika maisha yetu
ukatuguse kwa mkono wako wenye nguvu
Ukatufanye barua njema ee Mungu wetu nasi tukasomeke kama
inavyokupendeza wewe
Roho Mtakatifu akatuongoze katika yote na tukawe na kiasi...

“Kweli nawaambieni, anayesikia neno langu, na kumwamini yule aliyenituma, anao uhai wa milele. Hatahukumiwa kamwe, bali amekwisha pita kutoka kifoni na kuingia katika uhai. Kweli nawaambieni, wakati unakuja, tena umekwisha fika, ambapo wafu wataisikia sauti ya Mwana wa Mungu, nao watakaoisikia, wataishi. Kama vile Baba alivyo asili ya uhai, ndivyo pia alivyomjalia Mwanae kuwa asili ya uhai. Tena amempa mamlaka ya kuhukumu kwa sababu yeye ni Mwana wa Mtu. Msistaajabie jambo hili; maana wakati unakuja ambapo wote waliomo makaburini wataisikia sauti yake, nao watafufuka: Wale waliotenda mema watafufuka na kuishi, na wale waliotenda maovu watafufuka na kuhukumiwa.

Tazama wenye shida/tabu,watoto wako wanaokutafuta kwa bidii na imani
Mungu wetu tunaomba ukawaguse kwa mkono wako wenye nguvu
Yahweh tunaomba  ukawaguse kila mmoja na mahitaji yake
Mungu wetu  unajua haja za mioyo ya kila mmoja
Baba wa Mbinguni tunaomba ukawasamehe pale walipokwenda
kinyume nawe
Mungu wetu ukawape neema ya kujiombea,macho ya rohoni,masikio yakusikia sauti yako,wakafuate njia zako nazo zikawaweke huru
Mungu wetu tunaomba ukasikie kulia kwao
Baba wa Mbinguni tunomba ukawafute machozi yao
Jehovah ukaonekane katika maisha yao
Nuru yako ikaangaze katika maisha yao
Mungu wetu tunaomba ukawatendee sawasawa na mapenzi yako
Kwakuwa Ufalme ni wako Nguvu na Utukufu hata Milele
Amina....!!!


Wapendwa katika Kristo Yesu asanteni sana
kwakuwanami/kunisoma

Mungu Baba aendelee kuwabariki na kuwatendea
kama inavyompendeza yeye
Amani ya Bwana wetu Yesu Kristo na upendo wa Mungu Baba
ukae nanyi daima....
Nawapenda.





1Kisha Yobu akaendelea na hoja yake, akasema:
2“Laiti ningekuwa kama zamani,
wakati ule ambapo Mungu alinichunga;
3wakati taa yake iliponiangazia kichwani,
na kwa mwanga wake nikatembea gizani.
4Wakati huo nilifikia ukamilifu wa maisha,
wakati urafiki wa Mungu ulikaa nyumbani kwangu.
5Mungu Mwenye Nguvu alikuwa bado pamoja nami,
na watoto wangu walinizunguka.
6Nyakati hizo niliogelea kwenye ufanisi,
miamba ilinitiririshia vijito vya mafuta!
7Nilipokutana na wazee langoni mwa mji
na kuchukua nafasi yangu mkutanoni,
8vijana waliponiona walisimama kando,
na wazee walisimama wima kwa heshima.
9Wakuu waliponiona waliacha kuzungumza
waliweka mikono juu ya midomo kuwataka watu wakae kimya.
10Sauti za waheshimiwa zilinyamazishwa,
na vinywa vyao vikafumbwa.
11Kila aliyesikia habari zangu alinitakia heri
na aliponiona, alikubali habari hizo kuwa kweli:
12Nilimwokoa maskini aliyenililia msaada,
kadhalika na yatima asiyekuwa na wa kumsaidia.
13Waliokuwa karibu kuangamia walinitakia baraka,
niliwafanya wajane waone tena furaha moyoni.
14Uadilifu ulikuwa vazi langu;
kutenda haki kulikuwa kama joho na kilemba changu.
15Kwa vipofu nilikuwa macho ya kuwaonesha njia,
kwa viwete nilikuwa miguu yao.
16Kwa maskini nilikuwa baba yao,
nilifanya bidii kutetea haki za watu nisiowajua.
17Nilizivunja nguvu za watu waovu,
nikawafanya wawaachilie mateka wao.
18Kisha nikafikiri: Nitafia kiotani mwangu nimetulia;
siku za maisha yangu zitaongezeka kama mchanga.
19Mimi ni kama mti uliotandaza mizizi majini,
umande wa usiku huburudisha matawi yangu.
20Napata fahari mpya daima,
na nguvu zangu tayari kama mshale na upinde.
21“Wakati huo watu walinisikiliza na kungoja,
walikaa kimya kungojea shauri langu.
22Nilipomaliza kusema hawakuwa na cha kuongeza,
maneno yangu yaliwakolea kama matone ya mvua.
23Watu waliningojea kama wangojeavyo mvua,
walikuwa kama watu wanaotazamia msimu wa vuli.
24Walipokata tamaa niliwaonesha uso wa furaha,
uchangamfu wa uso wangu wakaungangania.
25Niliwatangulia kuwaongoza, nikawaonesha njia;
nilikuwa kwao kama mfalme kati ya majeshi yake;
kama mtu anayewafariji wenye msiba.


Yobu29;1-25

Biblia Habari Njema kwa Watu Wote(BHN)

"Swahili Na Waswahili"Mbarikiwe.

Thursday 1 November 2018

Kikombe Cha Asubuhi ;Yobu 28...


Shalom,Habari za Asubuhi,Hamjambo,Mmeamkaje?
Haleluyah Mungu wetu yu mwema sana..
Tumshukuru Mungu wetu katika yote....

Mungu wetu Baba yetu,Muumba wetu Muumba wa Mbingu na Nchi
Baba wa Upendo,Baba wa faraja,Baba wa huruma,Baba wa Baraka
Mungu mwenye nguvu,Mungu mwenye kuponya
Mungu wa Abrahamu,Isaka na Yakobo,Muweza wa yote
Wewe ni mwanzo na wewe ni mwisho,Alfa na Omega...!!


Asante kwa wema na fadhili zako kwetu
Asante kwa ulinzi wako kwetu wakati wote
Asante kwa kutuchagua tena na kutupa
kibali cha kuendelea kuiona leo hii


Baada ya hayo kulikuwa na sikukuu ya Wayahudi, naye Yesu akaenda Yerusalemu. Huko Yerusalemu, karibu na mlango uitwao Mlango wa Kondoo, kulikuwa na bwawa la maji liitwalo kwa Kiebrania Bethzatha, ambalo lilikuwa na baraza tano zenye matao. Humo barazani mlikuwa na wagonjwa wengi wamekaa: Vipofu, viwete na waliopooza. [Walikuwa wakingojea maji yatibuliwe, maana mara kwa mara malaika alishuka majini nyakati fulani na kuyatibua. Mtu yeyote aliyekuwa wa kwanza kuingia majini baada ya maji kutibuliwa, alipona ugonjwa wowote aliokuwa nao.]

Tazama Jana imepita ee Mungu wetu Leo ni siku mpya na kesho ni siku nyingineJehovah...
Yahweh tunakuja mbele zako tukijinyenyekeza,tukijishusha

na kujiachilia mikononi mwako
Mungu wetu tunaomba utusamehe dhambi zetu zote tulizo zifanya
Kwakuwaza,kwakunena,kwakutenda,kwakujua/kutojua
Baba wa Mbinguni nasi tunaomba ukatupe neema
ya kuweza kuwasamehe wale wote waliotukosea
Usitutie majaribu Mungu wetu tunaomba utuepushe
na yule mwovu na kazi zake zote
Jehovah ututakase miili yetu na akili zetu
Baba wa Mbinguni tunaomba utufunike kwa Damu
ya Bwana na Mwokozi wetu Yesu Kristo wa Nazareti

yeye aliteseka kwanza ili sisi tupate kupona





Basi, hapo palikuwa na mtu mmoja aliyekuwa mgonjwa kwa muda wa miaka thelathini na minane. Naye alipomwona huyo mtu amelala hapo na kujua kwamba alikuwa amekaa hapo kwa muda mrefu, akamwuliza, “Je, wataka kupona?” Naye akajibu, “Bwana, mimi sina mtu wa kunipeleka majini wakati yanapotibuliwa. Kila nikijaribu kuingia, mtu mwingine hunitangulia.” Yesu akamwambia, “Inuka, chukua mkeka wako utembee.” Mara huyo mtu akapona, akachukua mkeka wake, akatembea. Jambo hili lilifanyika siku ya Sabato.

Mungu wetu tunaomba ukabariki kazi za mikono yetu
Baba wa Mbinguni tunaomba ukatupe ubunifu na maarifa katika utendaji
Jehovah nasi tukatende sawasawa na mapenzi yako
Yahweh tunaomba ukabariki ridhiki zetu ziingiazo/zitokazo
Mungu wetu nasi tunaomba ukatupe neema ya kuweza
kuwabariki wenye kuhitaji
Tusipungukiwe katika mahitaji yetu Baba wa Mbinguni
tunaomba ukatupe kama inavyokupendeza wewe....



Baba wa Mbinguni tunayaweka maisha yetu mikononi mwako
Mungu wetu tunaomba ukabariki nyumba/ndoa zetu,
watoto,wazazi wetu,familia/ndugu na wote wanaotuzunguka
Jehovah tunaomba ulinzi wako kwetu na kwa vyote tunavyo vimiliki
Yahweh tunaomba ukatubariki tuingiapo/tutokapo
Mungu wetu tunaomba ukavibariki vyote tunavyoenda kugusa/kutumia
Baba wa Mbinguni ukavitakase kwa Damu ya Bwana wetu Yesu Kristo
Mungu wetu ukatamalaki na kutuatamia
Baba wa Mbinguni tukawe salama rohoni
Mfalme wa amani amani yako ikatawale katika maisha yetu
Mungu wetu ukatupe macho ya kuona na masikio ya kusikia 
sauti yako na kuitii

 Mungu wetu ukatupe akili ya kutambua mema na mabaya
Baba wa Mbinguni tunaomba ukatupe neema ya kufuata njia zako
Yahweh tukasimamie Neno lako amri na sheria zako siku zote 
za maisha yetu

Mungu wetu ukaonekane katika maisha yetu

Baba wa Mbinguni tukanene yaliyo yako
Neema zako zikawe nasi Nuru yako ikaangaze katika maisha yetu
ukatuguse kwa mkono wako wenye nguvu
Tukawe barua njema  ee Mungu wetu nasi tukasomeke kama
inavyokupendeza wewe
Roho Mtakatifu akatuongoze katika yote na tukawe na kiasi...

Kwa hiyo baadhi ya Wayahudi wakamwambia huyo mtu aliyeponywa, “Leo ni Sabato, si halali kubeba mkeka wako.” Lakini yeye akawaambia, “Yule mtu aliyeniponya ndiye aliyeniambia: ‘Chukua mkeka wako, utembee.’” Nao wakamwuliza, “Huyo mtu aliyekuambia: ‘Chukua mkeka wako, utembee,’ ni nani?” Lakini yeye hakumjua huyo mtu aliyemponya, maana Yesu alikuwa amekwisha ondoka mahali hapo, kwani palikuwa na umati mkubwa wa watu. Basi, baadaye Yesu alimkuta huyo aliyeponywa hekaluni, akamwambia, “Sasa umepona; usitende dhambi tena, usije ukapatwa na jambo baya zaidi.” Huyo mtu akaenda, akawaambia viongozi wa Wayahudi kwamba Yesu ndiye aliyemponya.

Mungu Baba tunawaweka mikononi mwako wenye shida/tabuwote wanaopotia magumu/majaribu mbalimbali
watoto wako wanaokuomba kwa bidii na imani
Mungu wetu tunaomba ukawaguse kwa mkono wako wenye nguvu
 kila mmoja na mahitaji yake 
Yahweh tunaomba ukaonekane katika maisha yao
Jehovah tunaomba ukawaokoe,ukawavushe salama na  kuwalinda
Mungu wetu tunaomba ukawasamehe pale walipokwenda kinyume nawe
Baba wa Mbinguni ukawape neema ya kujiombea,kufuata njia zako
wakasimaie Neno lako nalo likaweke huru
Mungu wetu tunaomba ukasikie kuomba kwetu
Baba wa Mbinguni ukapokee sala/maombi yetu
Mungu wetu ukawatendee sawasawa na mapenzi yako
Kwakuwa Ufalme ni wako Nguvu na Utukufu hata Milele
Amina...!!

Asanteni sana wapendwa katika Kristo Yesu kwakuwa nami
Mungu Baba aendelee kuwabariki na kuwatendea 
kama inavyompendeza yeye....
Nawapenda.






Sifa za hekima

1“Hakika kuna machimbo ya fedha,
na mahali ambako dhahabu husafishwa.
2Watu huchimba chuma ardhini,
huyeyusha shaba kutoka mawe ya madini.
3Wachimba migodi huleta taa gizani,
huchunguza vina vya ardhi
na kuchimbua mawe yenye madini gizani.
4Binadamu huchimba mashimo mbali na makazi ya watu,
mbali na watu mahali kusipofikika,
wachimba madini huninginia wamefungwa kamba.
5Kutoka udongoni chakula hupatikana,
lakini chini yake kila kitu huvurugwa kwa moto.
6Katika mawe yake ndimo vilimo vito vya rangi ya samawati
na udongo wake una vumbi la dhahabu.
7“Njia za kwenda kwenye migodi hiyo
hakuna ndege mla nyama azijuaye;
na wala jicho la tai halijaiona.
8Wanyama waendao kwa madaha hawajazikanyaga
wala simba hawajawahi kuzipitia.
9Binadamu huchimbua miamba migumu kabisa,
huichimbua milima na kuiondolea mbali.
10Hupasua mifereji kati ya majabali,
na jicho lake huona vito vya thamani.
11Huziba chemchemi zisitiririke,
na kufichua vitu vilivyofichika.
12 Taz Sir 1:6; Bar 3:15 “Lakini hekima itapatikana wapi?
Ni mahali gani panapopatikana maarifa?
13 Taz Bar 3:29-31 Hakuna mtu ajuaye thamani ya hekima,
wala hekima haipatikani nchini mwa walio hai.
14Vilindi vyasema, ‘Hekima haimo kwetu,’
na bahari yasema, ‘Haiko kwangu.’
15Hekima haiwezi kupatikana kwa dhahabu,
wala kwa kupima kiasi kingi cha fedha.
16Haiwezi kupimwa kwa dhahabu ya Ofiri,
wala kwa vito vya Sardoniki au vya rangi ya samawati,
17dhahabu au kioo havilingani nayo,
wala haiwezi kubadilishwa na vito vya dhahabu safi.
18Hekima ina thamani kuliko matumbawe na marijani,
thamani yake yashinda thamani ya lulu.
19Topazi ya Kushi haiwezi kulinganishwa nayo,
wala haiwezi kupewa bei ya dhahabu safi.
20“Basi, hekima yatoka wapi?
Ni wapi panapopatikana maarifa?
21Imefichika machoni pa viumbe vyote hai,
na ndege wa angani hawawezi kuiona.
22Abadoni na Kifo wasema,
‘Tumesikia uvumi wake kwa masikio yetu.’
23 Taz Bar 3:35-37 “Mungu aijua njia ya hekima,
anajua mahali inapopatikana.
24Maana yeye huona mpaka upeo wa dunia,
huona kila kitu chini ya mbingu.
25Alipoupa upepo uzito wake,
na kuyapimia maji mipaka yake;
26alipoamua mvua inyeshe wapi,
umeme na radi vipite wapi;
27 Taz Sira 1:9,19 hapo ndipo alipoiona hekima na kuitangaza,
aliisimika na kuichunguza.”
28 Taz Zab 111:10; Meth 1:7; 9:10 Kisha Mungu akamwambia mwanadamu:
“Tazama! Kumcha Bwana ndio hekima;
na kujitenga na uovu ndio maarifa.”



Yobu28;1-28

Biblia Habari Njema kwa Watu Wote(BHN)

"Swahili Na Waswahili"Mbarikiwe.