Swahili na Waswahili

Swahili na Waswahili
Waswahili na Mswahili Rachel Siwa...Pamoja Daima!!

Sunday 13 March 2016

Wapendwa Natumaini Jumapili ni Njema;Burudani-Anchor - Hillsong Live,My God is Awesome - Charles Jenkins,Break Every Chain (Live) - Tasha Cobbs,


Wapendwa;Ni Jumapili nyingine tena Mungu ametupa kibali cha kuwa pamoja tena....
Natumai wote wazima na jumapili ilikuwa/inaendelea vyema..
Tumshukuru Mungu kwa kila jambo,Hakuna na hatokuwepo kama yeye..

 "Basi, tusichoke kutenda mema; maana tusipolegea tutavuna mavuno kwa wakati wake."
Neno La Leo;Wagatia:6:1-18
Tuvumiliane na kusaidiana
1Ndugu, kama mkimwona mtu fulani amekosea, basi, nyinyi mnaoongozwa na Roho mwonyeni mtu huyo ajirekebishe; lakini fanyeni hivyo kwa upole, mkiwa na tahadhari msije nanyi wenyewe mkajaribiwa. 2Saidianeni kubeba mizigo yenu na hivyo mtatimiza sheria ya Kristo.3
                      3Mtu akijiona kuwa ni kitu, na kumbe si kitu, huyo anajidanganya mwenyewe. 4Lakini kila mmoja na aupime vizuri mwenendo wake mwenyewe. Ukiwa mwema, basi, anaweza kuona fahari juu ya alichofanya bila kuwa na sababu ya kujilinganisha na mtu mwingine. 5Maana kila mmoja anapaswa kuubeba mzigo wake mwenyewe.
                        Mwenye kufundishwa neno la Mungu na amshirikishe mwalimu wake riziki zake.
7Msidanganyike; Mungu hafanyiwi dhihaka. Alichopanda mtu ndicho atakachovuna. 8Apandaye katika tamaa za kidunia, atavuna humo uharibifu; lakini akipanda katika Roho, atavuna kutoka kwa Roho uhai wa milele. 9Basi, tusichoke kutenda mema; maana tusipolegea tutavuna mavuno kwa wakati wake. 10Kwa hiyo, tukiwa bado na wakati, tuwatendee watu wote mema, na hasa ndugu wa imani yetu.
                           Mawaidha ya mwisho na salamu
11Tazameni jinsi nilivyoandika kwa herufi kubwa, kwa mkono wangu mwenyewe. 12Wale wanaotaka kuonekana wazuri kwa mambo ya mwili ndio wanaotaka kuwalazimisha nyinyi mtahiriwe. Wanafanya hivyo kwa sababu moja tu: Kusudi wao wenyewe wasije wakadhulumiwa kwa sababu ya msalaba wa Kristo.13Maana, hao wenyewe waliotahiriwa hawaishiki sheria; huwataka nyinyi mtahiriwe wapate kujivunia alama hiyo mwilini mwenu. 14Lakini mimi sitajivunia kamwe chochote isipokuwa msalaba wa Bwana wetu Yesu Kristo; maana kwa njia ya msalaba huo ulimwengu umesulubiwa kwangu, nami nimesulubiwa kwa ulimwengu

        15Kutahiriwa au kutotahiriwa si kitu; cha maana ni kuwa kiumbe kipya.16Wanaoufuata mwongozo huo nawatakia amani na huruma; amani na huruma kwa Israeli – watu wa Mungu.
17Basi, sasa mtu yeyote asinisumbue tena, maana alama nilizo nazo mwilini mwangu ni zile za Yesu.
18Ndugu, neema ya Bwana wetu Yesu Kristo iwe nanyi. Amina.










"Swahili Na Waswahili"Pamoja Daima.

Sunday 6 March 2016

Natumai JumaPili ilikuwa njema;Happy Mother's Day..Burudani-Miriam Paul-Nipe Macho,Mvua ya Baraka......



Wapendwa waungwana; Habari za siku nyingi,Natumaini hamjambo na mnaendelea vyema na mwaka huu mpya..
Tunamshukuru Mungu kwa yote,Mungu yu mwema sana..nimeadimika kidogo mambo ni mengi familia imeongezeka
basi na majukumu yameongezeka,Lakini Mungu yu pamoja nasi na tupo pamoja tena..
Natumaini jumapili ilikuwa/inaendelea vyema
turudishe utukufu wa Mungu muumba wa yote...
"Happy Mother's Day" kwa wamama wote, Mungu atupe hekima,Busara katika Malezi ya Watoto wetu..
Mungu pia awaguse wenzetu wanaohitaji watoto ,akawape furaha hii nao wakafurahi pamoja na wengine..
Pia akawape sawasawa na mapenzi yake..
kuna ambao hawana kabisa ,Mungu yu pamoja nanyi,
Kuna walionao wa jinsia moja kike/kiume ,Mungu anamakusudi yake.
Kuna walionao lakini hawawajali/wameterekeza.Mungu awaguse mkumbuke majukumu yenu...

1Maneno ya mfalme Lemueli. Mawaidha aliyofundishwa na mama yake:

2Nikuambie nini mwanangu?
Nikuambie nini mwanangu niliyekuzaa?
Nikuambie nini wewe niliyekuomba kwa Mungu?


 Neno La Leo;Methali 31:1-31

Mawaidha kwa mfalme
1Maneno ya mfalme Lemueli. Mawaidha aliyofundishwa na mama yake:
2Nikuambie nini mwanangu?
Nikuambie nini mwanangu niliyekuzaa?
Nikuambie nini wewe niliyekuomba kwa Mungu?
3Usimalize nguvu zako kwa wanawake,
usiwape mali yako hao wanaoangamiza wafalme.
4Haifai ee Lemueli, haifai wafalme kunywa divai,
wala wakuu kutamani vileo.
5Wakinywa watasahau maagizo ya sheria,
na kuwanyima haki wenye taabu.
6Mpe kileo mtu anayekufa,
wape divai wale wenye huzuni tele;
7wanywe na kusahau umaskini wao,
wasikumbuke tena taabu yao.
8Lakini wewe, lazima useme kwa ajili ya wote walio bubu;
na kutetea haki za wote wasiojiweza.
9Sema kwa ajili yao na kuamua kwa haki,
linda haki za maskini na fukara.




Mke mwema
10Mke mwema kweli, apatikana wapi?
Huyo ana thamani kuliko johari!
11Mumewe humwamini kwa moyo,
kwake atapata faida daima.
12Kamwe hamtendei mumewe mabaya,
bali humtendea mema maisha yake yote.
13Hutafuta sufu na kitani,
na kufanya kazi kwa mikono yake kwa bidii.
14Yeye ni kama meli za biashara:
Huleta chakula chake kutoka mbali.
15Huamka kabla ya mapambazuko,
akaitayarishia jamaa yake chakula,
na kuwagawia kazi watumishi wake.
16Hufikiria kununua shamba, kisha hulinunua,
na kulima zabibu kwa faida ya jasho lake.
17Huwa tayari kufanya kazi kwa nguvu
na kuiimarisha mikono yake.
18Hutambua kwamba shughuli zake zina faida;
hufanya kazi hata usiku kwa mwanga wa taa yake.
19Husokota nyuzi kwa mikono yake mwenyewe,
kwa vidole vyake mwenyewe husuka nguo zake.
20Huufungua mkono wake kuwapa maskini,
hunyosha mkono kuwasaidia fukara.
21Hawahofii watu wake ijapo baridi ya kipupwe,
maana kila mmoja anazo nguo za kutosha.
22Hujitengenezea matandiko,
mavazi yake ni ya zambarau ya kitani safi.
23Mume wake ni mtu mashuhuri barazani,
anakoshiriki vikao vya wazee wa nchi.
24Mwanamke huyo hutengeneza nguo na kuziuza,
huwauzia wafanyabiashara mishipi.
25Nguvu na heshima ndizo sifa zake,
hucheka afikiriapo wakati ujao.
26Hufungua kinywa kunena kwa hekima,
huwashauri wengine kwa wema.
27Huchunguza yote yanayofanyika nyumbani mwake,
kamwe hakai bure hata kidogo.
28Watoto wake huamka na kumshukuru,
mumewe huimba sifa zake.
29Husema, “Wanawake wengi wametenda mambo ya ajabu,
lakini wewe umewashinda wote.”
30Madaha huhadaa na uzuri haufai,
bali mwanamke amchaye Mwenyezi-Mungu atasifiwa.
31Jasho lake lastahili kulipwa,
shughuli zake hazina budi kuheshimiwa popote.

                Bible Society of Tanzania
Jifunze zaidi









Mungu awabariki wote mliopita hapa,
muwe na wakati mwema.








"Swahili Na Waswahili"Pamoja Daima.

Tuesday 26 January 2016

NesiWangu Show. Rev Kennedy on "OBAMACARE" registration before its deadline Jan 31, 2016


The Affordable Care Act (ACA) or OBAMA CARE is a United States federal
statute signed into law by President Barack Obama on March 23, 2010.
The ACA was enacted to increase the quality and affordability of
health insurance, lower the uninsured rate by expanding public and
private insurance coverage, and reduce the costs of healthcare for
individuals and the government”
This message is brought to you by HELP AFRICA, which is an organization that targets African Communities in abroad and at home.
We
urge you to register so you can access quality health services health
services, avoid penalties and strengthen the health of our communities.

Tuesday 19 January 2016

MSIBA NYUMBANI KWA MAREHEMU GEORGE SEBO BOWIE, MARYLAND NCHINI MAREKANI


Kushoto niAbdul Sebo  mtoto wa marehemu akipewa pole na moja ya ndugu, jamaa na marafiki waliofika nyumbani kwa marehemu Bowie kutoa pole na rambi rambi zao kwa wafiwa kutokana na kifo cha mpendwa wao Mzee George Sebo kilichotokea siku ya Jumatatu asubuhi January 18, 2016 katika Hospitali ya Prince George iliyopo Maryland nchini Marekani. Utaratibu na mipango tutajulishwa leo kwa sasa imetengenezwa GOFUNDME ambayo ni www.gofundme.com/8fjvpcns
Picha na Vijimambo/Kwanza Production
 Kati ni mke wa marehemu Aunty Grace akipewa pole na moja ya ndugu, jamaa na marafiki waliofika nyumbani kwa marehemu kujumika nao na kuwafariji katika kipindi hiki kigumu cha kuondokewa na mpendwa wao mzee wetu George Sebo

 Mmoja ya wanaDMV wakijumuika pamoja na kwa kutoa pole na kuwafariji wafiwa katika kipindi hiki kigumu cha kuondokewa na mpendwa wao. Kushoto ni Salma Moshi.

 WanaDMV na wanafamilia wakijumuika na kuwafariji wafiwa nyumbani kwao Bowie, Maryland nchini Marekani na kutoa pole na rambi rambi zao . Kutoka kushoto ni Sharif, Tuma, Salma, Justa, Aunty Grace na Iska wakiwa na mke wa marehemu Aunty Grace kumpa pole kwenye msiba wa kuondokewa na kipenzi mume wake Mzee George Sebo.

WanaDMV wakijumuika na wanafamilia nyumbani kwa marehemu Bowie, Maryland.

Saturday 2 January 2016

MISS TANZANIA USA AHUDHURIA MKESHA WA MWAKA MPYA DMV


Miss Tanzania USA Aeesha Kamara akipata picha ya upendeleo alipofika kwenye mkesha wa mwka mpya ulioandaliwa na Jumuiya ya Watanzania DMV siku ya Alhamisi Desemba 31, 2016 Lanham, Maryalnd nchini Marekani. PICHA NA KILIMANJARO STUDIO
Asha Hariz Kushoto) pamoja na mama wa mitindo Asya Idarous Khamsini wakipata picha ya pamoja na Miss Tanzania USA Pageant alipohudhuria mkesha wa mwaka mpya DMV.
 Aeesha Kamara katika picha ya pamoja na msanii Patience Ibembo wa Congo mwenye makzi yake Marekani kwa sasa ambaye zamani alikuamcheza show wa Koffi Olomide.

Kutoka kushoto ni Patience Ibembo, Aeesha Kamara, Mama Winny Casey Mratibu wa Miss Tanzania USA na Rukia Malipula ambaye ni mama mzazi wa Aeesha Kamara.
Aeesha Kamara akitangaza kalenda ya 2016 iliyotengenezwa na Miss Africa USA na pichga yake kutumika kwenye kalenda hiyo baada ya kuwashinda mamiss wengine wa Africa shindano lililofanyika New York Novemba 2015. 
KWA PICHA ZAIDI BOFYA HAPA