Swahili na Waswahili

Swahili na Waswahili
Waswahili na Mswahili Rachel Siwa...Pamoja Daima!!

Sunday 9 August 2015

MISA YA KUMBUKUMBU YA MAREHEMU MZEE SAMUEL LUANGISA NEW YORK NCHINI MAREKANI.


Mchungaji Butiku akiongoza misa ya shukurani na arubaini ya
marehemu Mzee Samuel Luangisa iliyofanyika siku ya Jumamosi Aug 8,
2015 Mount Vernon, New York na kuhudhuriwa na ndugu, jamaa na marafiki
kutoka kila pembe ya Marekani.
Mrs Luangisa, mke wa marehemu akifuatilia misa.


Wanafamilia wakifuatilia misa.


Wajukuu wa marehemu wakifanya onesho la kumenzi babu yao.


Mtoto wa marehemu Mao Luangisa akitoa salamu za shukurani.


Mwenyekiti wa Jumuiya ya Watanzania New York Hajji Khamis akiongea
machache huku akisisitiza upendo na mshikmano kwenye Jumuiya za
Watanzania hususani zile zilizopo nje ya Tanzania kwani kwa kufanya
hivyo Jumuiya zitakua imara.


Mchungaji Butiku akiongoza misa.


Wakati wa maakuli.
Kwa picha zaidi bofya HAPA

Thursday 6 August 2015

BALOZI LIBERATA MULAMULA AONDOKA RASMI MAREKANI KURUDI TANZANIA.


 Balozi Liberata Mulamula kwenye picha ya pamoja  na baadhi ya Wafanyakazi wa Ubalozi wa Tanzania Washington DC walipokwenda kumuaga nyumbani kwake Bethesda Maryland.




                               Safari ya kuelekea Uwanja wa Ndege wa Kimataifa Dulles ikianza.

 Mhe Balozi Liberata Mulamula akisalimiana na Agnes Mutta Mke wa Mwambata wa Jeshi wa Ubalozi wa Tanzania Washington DC.

Mhe Balozi Liberata Mulamula pamoja na Mkuu wa Utawala Lily Munanka wakibadilishana mawazo pamoja na familia ya Mwambata wa Jeshi.

 Mhe Balozi Liberata Mulamula akiwa pamoja na Mwambata wa Jeshi Col. Adolph Mutta pamoja na Mkewe Agnes Mutta.

               Mhe Balozi Liberata Mulamula akitoa  pasi yake ya kusafiria kwaajili ya kujisajili tayari kwa kuondoka.

                        Mhe Balozi Liberata Mulamula  akiwa katika hatua za mwisho za usajili.

                           Mhe Balozi Liberata Mulamula tayari usajili ulipokamilika

Mhe. Katibu Mkuu Balozi Liberata Mulamula kwenye picha ya pamoja na baadhi ya wafanyakazi wa Ubalozi pamoja na familia zao.

Mhe. Katibu Mkuu Balozi Liberata Mulamula akiwa tayari anajiandaa kwa ukaguzi wa mwisho na kuelekea kwenye ndege.

 Kwa pamoja tunasema Safari Njema na Ubarikiwe Sana Balozi Mulamula daima tutakukumbuka.

                    PICHA ZOTE KWA HISANI YA CAMERA YA UBALOZI.

Tuesday 4 August 2015

BALOZI LIBERATA MULAMULA ATINGA NDANI YA STUDIO YA KILIMANJARO


 Balozi Liberata Mulamula akiwasili nje ya jengo lenye studio ya Kilimanjaro tayari kuongea LIVE katika kipindi cha Jukwaa langu kinachorushwa kila siku ya Jumatatu kuanzia saa 12 jioni mpaka saa 2 usiku saa za Mashariki za Marekanui. anayemfungulia mlango ni Abdul Malik

 Balozi Liberata Mulamula akiingia ndani ya studio akiwa amesindikizwa Harriet Shangarai (kushoto) ambaye pia ni Mkurugenzi wa studio hiyo, kulia ni Afisa Ubalozi Swahiba Mdeme na Abdul Malik
 Balozi Liberata Mulamula akipata maelezo kutoka kwa studio meneja ambaye pia ni mtangazaji na mtayarishaji wa kipindi cha Jukwaa langu, Bwn. Mubelwa Bandio (hayupo pichani) Kushoto ni Afisa Ubalozi Swahiba Mdeme akifuatilia maelezo hayo.
 Mhe. Liberata Mulamula akiendelea kusikiliza maelezo kutoka kwa meneja wa studio Mubelwa Bandio ambaye ni mtangazaji na mtayarishaji wa kipindi cha jukwaa lako. Kati ni matangazaji maarufu wa Radio ya Times FM na aliyewahi kutangaza  Radio One Bi. Rose Chitalah ambaye pia anamsaidia Mubelwa Bandio katika utangazaji na kuchangia hoja mbalimbali katika kipindi cha Jukwaa langu.
 Balozi Liberata Mulamula akiendelea kujibu maswali ya watangazaji mahiri Mubelwa Bandio (kulia) na Rose Chitalah (hayupo pichani ) na wasikilizaji waliokua na shahuku ya kumuuliza maswali.
  Balozi Liberata Mulamula akiendelea kujibu maswali ya watangazaji mahiri Bwn. Mubelwa Bandio (hayupo pichani ) na Rose Chitalah (kushoto)
 Afisa Ubalozi Swahiba Mdeme akisikiliza mahojiano na kunakili baadhi ya vipengele katika mahojiano hayo.
 Kutoka kushoto ni Afisa Ubalozi Swahiba Mdeme, Mhe. Balozi Liberata Mulamula na mtangazaji mahiri Rose Chitalah wakiwa katika picha ya pamoja.
 Kutoka kushoto ni Dj Luke Joe, Meneja wa studio ya Kilimanjaro,  Mubelwa Bandio, Mhe. Balozi Liberata Mulamula na mtangazaji mahiri Rose Chitalah wakipata picha ya kumbu kumbu na Balozi Liberata Mulamula anayemaliza muda wake kama Balozi wa Tanzania nchini Marejkani na Canada na sasa ni Katibu Mkuu wa Wizara ya Mambo ya Nje na Ushirikiano wa Kimataifa

Monday 3 August 2015

Mkutano wa Injili Washington DC [Aug 14 - 16 2015]


Kanisa la The Way of the Cross Gospel Ministries linapenda kuwaalika katika siku tatu za mkutano wa uamsho utakaofanyika hapa Washington DC.

Ni kati ya Agosti 14-16 2015




Mtumishi wa Mungu Emmanuel Mgaya ama Masanja Mkandamizaji alipohudumu kwa waumini wa jiji la Washington DC na vitongoji vyake siku ya Jumapili 07/07/2013 katika kanisa la THE WAY OF THE CROSS GOSPEL MINISTRIES

Sunday 2 August 2015

Muendelee Vyema na Jumapili Hii;Namshukuru Sana Mungu kwa mema Mengi,Burudani-Kinondoni Revival Choir Ninakushukuru na ....

Namshukuru sana Mungu baba muumba wa vyote,
Kwa mema yote aliyonitendea na ayonitendea..
Nimrudishie nini Mungu wangu?
Nasema Asante Mungu...
Jana tarehe 01/08 ilikuwa Siku ya kumbukumbu yangu ya Mimi kuja katika Dunia hii/Kuzaliwa.

Mungu yu mwema Sana!!!
Asante kwa Wazazi/Walezi kwa yote mliyoweza kufanikisha
Kwa nafasi yenu ili mimi niendelee.
Asante kwa Mume wangu kwa Nafasi yako pia.
Asante Watoto wangu, Dada/kaka,Ma Wifi/Ma Shemeji,Ndugu,Jamaa naMarafiki zangu pia kwa Nafasi zenu.
Asante kwa wote mlionitumia ujumbe,Maombi,Dua/Sala na mengine mengi..
Mungu azidi kuwabariki Sana katika yote.

Asante pia kwa wewe unayepita hapa...


"Sasa baba naja kwako najimimina maisha yangu niguseeeee!!!!!!!"""
Pendo Lako Calvary...!!!!!
Lanivutaaaa nipate Kuabuduuuu...!!!
Neno La Leo;Waebrania:11:1-40
Imani






"Swahili na Waswahili" Mbarikiwe wote.

Saturday 1 August 2015

WATANZANIA CALIFORNIA WAMUAGA BALOZI LIBERATA MULAMULA


 Watanzania California wakiongozwa na Balozi wa Heshima Mhe. Ahmed Issa walijumuika pamoja siku ya Ijumaa na kumuaga Balozi Liberata Mulamula anayemaliza muda wake kama Balozi wa Tanzania nchini Marekani na Mexico na kurudi nyumbani kwenda kulitumikia taifa kama Katibu Mkuu wa Wizara ya Mambo ya Nje na Ushirikiano wa Kimataifa.
 Watanzania wa California wakipiga picha ya pamoja na Mhe. Balozi Libarata Mulamula (wapili toka kushoto) siku ya Ijumaa July 31, 2015 walipomuaga rasmi.
 Balozi Liberata Mulamula akimkabidhi zawadi yake Afisa Ubalozi Swahiba Mdeme mara tu baada ya kukabidhiwa na Watanzania California siku ya Ijumaa July 31, 2015 walipomualika rasmi kwa ajili ya kumuaga.
 Balozi Liberata Mulamula akicheza na kuburudika kwenye moja ya nyimbo zilizopigwa kwenye tafrija hiyo.
 Balozi Liberata akipiga makofi
Moja wa kikundi maarufu cha ngomma ya asili kikitoa burudani

Wednesday 29 July 2015

Mazungumzo na mtangazaji Rose Chitallah kwenye kipindi cha JUKWAA LANGU


Mubelwa Bandio na Rose Chitallah studioni
Kipindi hiki ambacho kinakujia kila JUMATATU, kinajadili mambo mbalimbali na zaidi kuhusu UCHAGUZI MKUU WA TANZANIA 2015

Katika kipindi hiki utasikia mahojiano yetu na watu mbalimbali kuhusu DEMOKRASIA kuelekea uchaguzi nchini Tanzania

Katika kipindi cha wiki hii tumebahatika kuungana na mtangazaji Rose Chitallah

Karibu