Swahili na Waswahili

Swahili na Waswahili
Waswahili na Mswahili Rachel Siwa...Pamoja Daima!!
Showing posts with label wa Tanzania/Waswahili. Show all posts
Showing posts with label wa Tanzania/Waswahili. Show all posts

Wednesday 9 May 2018

PICHA NA HABARI ZA USIKU WA WASATU, BIRMINGHAM, UINGEREZA, APRILI 28



Na Freddy Macha


Jumuiya ya wasanii Watanzania Uingereza (WASATU) ilichemsha supu, ukumbi wa Heartlands , Birmigham, Uingereza Jumamosi iliyopita. Makutano haya yalikuwa pia sehemu ya mchango mahususi kusaidia wasichana wanaopewa mimba kabla ya kuwa watu wazima, kitongoji cha Tengeru, Arusha. Fedha zilikusanywa na mjasiria mali mkazi wa Birmingham, Mtanzania Sia Travel. Sia alijaa mlangoni akihakikisha kila senti iiliyolipwa na wahudhuriaji watashiba chakula , sanaa usiku kucha na kuwafariji vigoli wetu.
WASATU iliyoundwa mwaka 2016 chini ya udhamini wa Balozi wetu Uingereza, Mhe Asha Rose Migiro, inakutanisha wasanii wa ala mbalimbali chini ya viongozi- mwanamuziki na mcheza sarakasi mwenye nidhamu ya hali yajuu, Fab Moses na mtangaza mapishi ya Kitanzania, Uingereza, Bi Neema Kitilya, aliyetulizana kama shingo ya twiga.
Mwaka jana, 2017, shughuli hii ilifanywa Northampton na asilimia 20 ya kipato iliwafikia Watanzania waliofikwa na maafa ya mafuriko ya maji.







Warembo wa kujitolea, walioonesha mavazi yaliyoandaliwa na kampuni ya “All Things African” (inayoendeshwa na Mtanzania, mchapa kazi, asiyejua uvivu kabila gani, Hamida Mbaga). Toka kushoto, Yvonne Waweru, Georgeous Katega, Victoire Koleilas, Maureen Tibenda

Viongozi wa WASATU – Neema Kitilya na Fab Moses wakijadiliana huku shughuli zikikwea minazi na kuta

Fahari ya Tanzania – imesambazwa meza ya bidhaa mseto na “All Things African”

Mcheza ngoma aliyepitia mitihani mikali na vikundi maarufu vya mila zetu- Kibisa na Muungano - Likiwa Ismail- akionesha SINDIMBA – bila aibu, staha wala wasiwasi.


Rama Sax akipuliza vitu. Zamani alipiga na Simba Wanyika akashiriki kurekodi wimbo wa “Sina Makosa”. Rama Sax ni pia mwimbaji mahiri

Baadhi ya vyakula vya Kitanzania

Msanii wa mapishi Neema John aliyechangia kazi njema na Neema Kitilya.

Wageni toka Tanzania na Uganda. Huyo Mganda (kushoto) ni mwanafunzi wa lugha ya Kiswahili

Mpiga Gitaa mkuu wetu, Jioni Ticha na kipande cha kuku baada ya kazi jukwaani. Alisafiri toka Leeds. Mbali sana na hapa

Watanzania wakichangamkia shughuli
Sia Travel akihamasika. Hakupitwa

Mwanamuziki Saidi Kanda,(aliyesimama) mbabe na mtukuzaji wa vyombo asilia vya muziki wa Kitanzania, akijumuika na Wabongo nadhif, waliokuwemo

Mwandishi na mwanamuziki, F Macha pamoja na wasanii Likiwa Ismail (ngoma) na Rama Sax.



Shukrani...
kwa habari na Matukio nitumie kupitia Email;rasca@hotmail.co.uk

"Swahili Na Waswahili"Pamoja Daima.







Saturday 2 January 2016

ASYA IDAROUS KHAMSINI ANOGESHA MKESHA WA MWAKA MPYA DMV


Mlimbwende akipita mbele ya mashabiki wa mitindo kuoka kwa gwiji la mitindo Tanzania mama Asya Idarous Khamsini aliponogesha mkesha wa mwaka mpya 2016 uliofanyika Lahnam, Maryaland nchini Marekani. PICHA NA KILIMANJARO STUDIO
Mlimbwende akipita mbele ya mashabiki.
Ni vivazi vya mama wa mitindo Asya Idarous Khamisni.
Mtoto manshallah akiwa ndani ya vazi la mama wa mitindo Asya Idarous Khamsini.
Mlimbwende akipita mbele ya mashabiki wa vivazi.
Ilikua ni vivazi kwa kwenda mbele.
Kijana akijitanashati na kivazi cha Asya Idarous Khamsini.
Gwiji la mitindo na walimbwende wake.
Kwa picha zaidi bofya HAPA

Saturday 1 August 2015

WATANZANIA CALIFORNIA WAMUAGA BALOZI LIBERATA MULAMULA


 Watanzania California wakiongozwa na Balozi wa Heshima Mhe. Ahmed Issa walijumuika pamoja siku ya Ijumaa na kumuaga Balozi Liberata Mulamula anayemaliza muda wake kama Balozi wa Tanzania nchini Marekani na Mexico na kurudi nyumbani kwenda kulitumikia taifa kama Katibu Mkuu wa Wizara ya Mambo ya Nje na Ushirikiano wa Kimataifa.
 Watanzania wa California wakipiga picha ya pamoja na Mhe. Balozi Libarata Mulamula (wapili toka kushoto) siku ya Ijumaa July 31, 2015 walipomuaga rasmi.
 Balozi Liberata Mulamula akimkabidhi zawadi yake Afisa Ubalozi Swahiba Mdeme mara tu baada ya kukabidhiwa na Watanzania California siku ya Ijumaa July 31, 2015 walipomualika rasmi kwa ajili ya kumuaga.
 Balozi Liberata Mulamula akicheza na kuburudika kwenye moja ya nyimbo zilizopigwa kwenye tafrija hiyo.
 Balozi Liberata akipiga makofi
Moja wa kikundi maarufu cha ngomma ya asili kikitoa burudani

Sunday 19 April 2015

BALOZI LIBERATA MULAMULA AHUDHURIA MKUTANO MKUU WA WASABATO WAISHIO NCHINI MAREKANI




Mchungaji Wilbert Nfubhusa akihubiri kwenye mkutano mkubwa wa neno la Mungu wa Wasababto waishio nchini Marekani uliofanyika siku ya Jumamosi April 18, 2015 Silver Spring, Maryland. Kulia ni Michael Mwasumbi akitafsiri mahubiri kwa lugha ya Kiingereza.Mkutano huu umehudhuriwa na Watanzania kutoka majimbo mbalimbali wakiwemo wengine kutoka Tanzania.
 Mhe. Liberata Mulamula. Balozi wa Tanzania nchini Marekani akiushukuru uongozi wa Wasabato nchini Marekani kwa kuweza kufanikisha mkutano wao na kuweza kumleta mchungaji Wilbert Nfubhusa na kuelezea amefurahishwa kwa makaribisho mazuri na kuwatakia mkutano mwema huku akiomba Mwenye Mungu aushushie baraka zake.


Mhe. Balozi Liberata Mulamula akimtambulisha mdogo wake  Joycelyne Rutageruka ambaye amekuja kumtembelea Mhe. Balozi toka nyumbani Tanzania nae akitoa neno kwenye mkutano mkuu wa Wasabato wa Watanzania waishio nchini Marekani uliofanyika siku ya Jumamosi April 18, 2015 Silver Spring, Maryland.  


Nchungaji Herry Mhando akifanya mamombi maalum kabla ya kumkaribisha mchungaji Wilbert Nfubhusa kutoa mahubiri,


Mshereheshaji Magoma akifafanua jambo


Mhahubiri yakiendelea
Kwa picha zaidi bofya soma zaidi

Wednesday 18 March 2015

Niambie Live Show....Ep1‏


Omby Nyongole, Salma Moshi na Queen Mkelemi
Karibu kwenye kipindi hiki cha NIAMBIE LIVE

Kipindi kinachozungumzia mambo mbalimbali yaliyochukua nafasi za juu kwenye mitandao ya kijamii. Pia kupata Tip ya siku / wiki kusaidia kuboresha maisha yako.

Ni Niambie Live....

KARIBU

Wednesday 19 November 2014

MISHUMAA YA KALE...Kipindi kipya kutoka VIJIMAMBO na KWANZA PRODUCTION


Photo Credits: Ye Olde Vivyl Shoppe
Baada ya pilika za wiki nzima, na mchamchaka wa maisha, sasa unakuja wakati wa kuburudika na muziki halisi wa zamani.

Katika kipindi hiki, utaweza "kuruka majoka" na "kula mangoma" kwa kusikiliza nyimbo ziliotamba miaka ya zamani, kupata historia ya wasanii na vikundi mbalimbali na pia kusikiliza mazungumzo na maDj na wasanii mbalimbali wa zamani.

Ungana na MixMaster Dj Luke Joe kwenye "one and two" na Mubelwa Bandio nyuma ya kipaza sauti kwenye kipindi kipya cha MISHUMAA YA KALE kitakachokujia kila Ijumaa kuanzia saa 11 kamili jioni mpaka saa 1 kamili usiku kwa majira ya Marekani ya Mashariki (5:00pm - 7:00pm EST)

Ungana nasi kupitia www.kwanzaproduction.com

MixMaster DJ Luke Joe. Photo Credits: IskaJojo Studios
Mubelwa Bandio