Swahili na Waswahili

Swahili na Waswahili
Waswahili na Mswahili Rachel Siwa...Pamoja Daima!!

Wednesday 4 December 2013

HUYU NA YULE: Mahojiano na waTanzania Evans Mhando na Fatuma Matulanga wakiwa CHINA‏


WaTanzania Evans Mhando (L) na Fatuma Matulanga (M) walipokutana jijini Beijing nchini China. Wiki hii walikuwa wageni katika kipindi cha HUYU NA YULE kinachotayarishwa na Mubelwa Bandio (R) wa Jamii Production

Katika huyu na yule wiki hii, nimepata nafasi ya kuzungumza na vijawa
wawili wa kiTanzania wanaosoma nchini China. Nao ni Fatuma Matulanga
aliyeko Beijing na Evans Mhando aliyeko Nanchang ambao kwa pamoja
tumejadili mambo kadhaa na zaidi kuhusu vijana

Wameeleza mengi wakioanisha kijana na maisha ya China na Tanzania ikiwemo

1: TOFAUTI KATI YA KIJANA WA CHINA NA TANZANIA

2:TOFAUTI
KATI YA ELIMU YA CHINA NA KWINGINE. Ni kweli kuwa China haifunzi
ubunifu na ndio maana wanasifika kwa kuendeleza kuliko kubuni?

3: MALALAMIKO KUWA BIDHAA ZA CHINA HAZINA UBORA, YANATAZAMWA VIPI HUKO CHINA?

4: NI KIPI WANACHOJUA SASA KUHUSU CHINA AMBACHO HAWAKUJUA KABLA HAWAKWENDA CHINA?

5: MABADILIKO YA SERA YA MTOTO MMOJA MNAONA IMEPOKELEWA VIPI HAPO?

6: NI KIPI WANACHOTAMANI KINGETOKA CHINA KWENDA TANZANIA (HASA KATIKA TASNIA YA HABARI?)

Na mengine mengi

Ni
huyu na Yule ya Mubelwa Bandio wa Jamii Production akihojiana na Fatuma
Matulanga na Evans Mhando, wanahabari wa shirika la utangazaji la
Tanzania (TBC) wanaojiendeleza kielimu nchini China


Kwa maoni ama ushauri, usisite kutuandikia kupitia jamiiproduction@gmail.com
--
*JAMII PRODUCTION*
"Usahihi wa fikra ndio fikra sahihi"

Tuesday 3 December 2013

Kipindi cha familia kutoka Jamii Productuion...Majukumu ya Baba katika Familia‏


Karibu katika kipindi hiki cha FAMILIA kutoka Jamii Production.

Katika kipindi cha wiki hii, mjadala wa WAJIBU WA BABA KATIKA FAMILIA umefungua mfululizo wetu wa mijadala kuhusu wajibu wa mzazi kwa familia yake

Mbali na washiriki waliokuwemo studio, pia tumeshirikisha maoni toka kwa wasikilizaji wetu wapendwa waliyotoa kwenye ukurasa wa Facebook
Msimamizi wa kipindi Abou Shatry akifuatilia mjadala

Karibu uungane nasi



Mjadala ukiendelea
Mgeni wetu katika mjadala huu Isidory Lyamuya


--
*JAMII PRODUCTION*
"Usahihi wa fikra ndio fikra sahihi"

Kifuatacho Jamii Production...Fatuma Matulanga na Evans Mhando‏



Katika kipengele hiki cha HUYU NA YULE  wiki hii, nimepata nafasi ya kuzungumza na vijawa
wawili wa kiTanzania wanaosoma nchini China. Nao ni Fatuma Matulanga
aliyeko Beijing na Evans Mhando aliyeko Nanchang ambao kwa pamoja
tumejadili mambo kadhaa na zaidi kuhusu vijana

Wameeleza mengi wakioanisha kijana na maisha ya China na Tanzania ikiwemo

1: TOFAUTI KATI YA KIJANA WA CHINA NA TANZANIA

2:TOFAUTI KATI YA ELIMU YA CHINA NA KWINGINE. Ni kweli kuwa China haifunzi ubunifu na ndio maana wanasifika kwa kuendeleza kuliko kubuni?

3: MALALAMIKO KUWA BIDHAA ZA CHINA HAZINA UBORA, YANATAZAMWA VIPI HUKO CHINA?

4: NI KIPI WANACHOJUA SASA KUHUSU CHINA AMBACHO HAWAKUJUA KABLA HAWAKWENDA CHINA?

5: MABADILIKO YA SERA YA MTOTO MMOJA MNAONA IMEPOKELEWA VIPI HAPO?

6: NI KIPI WANACHOTAMANI KINGETOKA CHINA KWENDA TANZANIA (HASA KATIKA TASNIA YA HABARI?)

Na mengine mengi

Usikose kutembelea mtandao huu siku ya Jumatano ili kusikiliza mahojiano kamili

Ni huyu na Yule ya Mubelwa Bandio wa Jamii Production akihojiana na Fatuma
Matulanga na Evans Mhando, wanahabari wa shirika la utangazaji la
Tanzania (TBC) wanaojiendeleza kielimu nchini China

Monday 2 December 2013

[AUDIO]: Maandalizi ya matembezi ya hisani: NCHI YANGU, WAJIBU WANGU, TAIFA KWANZA‏


 Matukio Chuma, muandaaji wa matembezi ya hisani akizungumzia matembezi hayo yatakayofanyika Januari 11, 2014 yenye kauli mbiu Nchi yangu, wajibu wangu, taifa kwanza.

Katika mahojiano haya Chuma anazungumzia mambo mbalimbali kuhusu matembezi hayo, ikiwemo sababu ya kuyaandaa, sababu za kuyafanya katika njia waliyoamua kuyafanya (Dar-Moro), mambo ya kufanya kabla hujashiriki matembezi haya na mengine mengi.

Unaweza kuwasiliana nao kwa simu namba 0784 311-056, 0772 545-562 ama barua pepe ambayo ni kwetutanzania@yahoo.com

--
*JAMII PRODUCTION*
"Usahihi wa fikra ndio fikra sahihi"

Sunday 1 December 2013

Nawatakia J'Pili Njema yenye Baraka;Burudani-Bahati Bukuku,Naomba niulize na Nyingine!!!

Wapendwa muwe na J'Pili Njema yenye,Shukrani,Imani,Upendo na Furaha...
Ninyi ni chumvi ya dunia,lakini chumvi ikiwa imeharibika itatiwa nini hata ikolee?
Neno La Leo;Mathayo Mtakatifu:5:11-16.
Vivyo hivyo nuru yenu na iangaze mbele ya watu, wapate kuyaona matendo yenu mema, wamtukuze Baba yenu aliye Mbinguni.








"Swahili Na Waswahili" Mbarikiwe Sana.

Saturday 30 November 2013

[AUDIO]: Kuzagaa kwa silaha za moto na kuongezeka kwa mauaji Tanzania‏


Picha kwa hisani ya thehabari.com
Si jambo geni tena hivi sasa nchini Tanzania kusikia fulani kashambuliwa au kauawa kwa risasi.
Silaha za moto hapa nchini hasa zile zinazomilikiwa kiholela zimekuwa zikimilikiwa na kila anayetaka... kama vocha za simu.

Hata mtu mwenye uwezo kidogo, na asiye na sababu ya kuwa na silaha anaweza kumiliki silaha nyumbani kwake .

Bastola kwa sasa zimekuwa kama bidhaa ya utashi na watu wanazimiliki kama wanavyomiliki simu za mkononi.


Ungana
na Sophia Kessy (L) na Mubelwa Bandio (R) katika sehemu hii ya kwanza kuangalia
tatizo hili linaloonekana kuzidi kuathiri na kutishia maisha ya
waTanzania wengi.



--
*JAMII PRODUCTION*
"Usahihi wa fikra ndio fikra sahihi"

Wednesday 27 November 2013

Jikoni Leo;[Street food]Chipsi Vumbi Na Hapa kwetu!!!!!!!


Hapa tunapokumbukia Chipsi za Nyumbani, Ma binti zangu hupenda sana Chipsi Mayai[ZEGE]Na sasa wanapika wenyewe kama unavyoona hapo juu,Nyama Choma Baba anawasaidia...

Waungwana;Jikoni Leo Mtaani na Kwa Da'Rachel..
Vipi Chipsi Vumbi/za Mitaani Zina Raha gani? Na Karaha Gani?

Kuna mtu hajawahi kula Chipsi hizi?

Jee wewe uliyekula/Unayekula Wapi KIJIWE bomba Cha Chipsi upendacho?

Pale Dar,Ilala  Kulikuwa kwa Ndago,Barafaa....
Pale Iringa,Kulikuwa kwa Baba Nusa...


Hizi ni Chache tuu nawe Waweza Kuongezea....





"Swahili Na Waswahili"Pamoja Sana.