Swahili na Waswahili

Swahili na Waswahili
Waswahili na Mswahili Rachel Siwa...Pamoja Daima!!

Monday 25 November 2013

Sunday 24 November 2013

Nawatakia J'Pili Njema;Burudani-Here I am to Worship[Playlist]!!!!

Wapendwa;Muwe Na J'Pili yenye Baraka,Amani,Upendo na Furaha...
Lakini nafsini mwangu nalikusudia hivi,nisije kwenu tena kwa huzuni...
.Maana mimi nikiwatia huzuni,basi ni nani anifurahishaye mimi ila yeye ahuzunishwaye nami?
Neno La Leo;2Wakorintho:2:1-11.


"Swahili Na Waswahili" Mbarikiwe Sana.

Saturday 23 November 2013

Wa-Africa Na Mitindo Mchanganyiko!!!!!





Mhhhh..Mengi sina..ni Wa-Afrika na Mitindo...mimi naiita Mitindo TATA..
Vipi Inavalika? Si wanasema Wanawake tunavaa mavazi yanayo fanana na Yao..nawao jee?......haya na Nywele za dada kama hivyo.

Kuona Zaidi nifuate;http://www.mitindoafrica-abroad.blogspot.co.uk/

"Swahili Na Waswahili" Pamoja Daima.

[AUDIO] DAKIKA 90 ZA DUNIA: Miaka 50 tangu kuuawa kwa Rais John F Kennedy‏



 

Ijumaa wiki hii,
Marekani imeadhimisha nusu karne tangu kuuawa kwa Rais wa 35 wa taifa
hilo, John F Kennedy aliyeuawa Novemba 22, 1963 alipokuwa akisafiri kwenye gari la wazi jijini Dallas

Rais John F Kennedy akiwa katika gari la wazi muda mchache kabla hajauawa kwa risasi. Pembeni yake ni mkewe na mbele yake ni aliyekuwa Gavana wa Texas John Bowden Connally, Jr.ambaye pia alijeruhiwa katika shambulio hilo
Kwa wiki nzima, kumekuwa na shughuli mbalimbali kukumbuka tukio hili lililoshitua wengi nchini humo. Mambo mengi yametendeka. Vitabu vipya vimeandikwa na watu wamezungumzia kuuawa kwa Rais huyo pamoja na ufuasi alioacha kwenye uongozi mpaka sasa. Na kama ilivyotegemewa, Kengele ziligongwa, maua yaliwekwa kwenye kaburi, bendera zilipepea nusu mlingoti na nyimbo mbalimbali ziliimbwa

Rais Barak Obama, aliadhimisha kumbukumbu
hizo Jumatano wiki hii kwa kuweka shada la maua kwenye kaburi la Rais
Kennedy na pia kutoa tuzo za heshima kwa watu mbalimbali akiwemo Rais
mstaafu Bill Clinton, mwanahabari maarufu Oprah Winfrey na wengine 14.

Rais Barack Obama (wa pili kulia) akiwa na mkewe Michelle, Rais mstaafu Bill Clinton (wa tatu kulia) na mkewe Hillary Clinton wakitoa heshima mbele ya kaburi la JFK jumatano wiki hii.


Hii
ni sehemu ya ripoti ya Jamii Production kwenye kipindi cha DAKIKA 90 ZA
DUNIA kinachorushwa na kituo cha Radio cha Capital FM cha Dar Es Salaam
Tanzania kila Jumamosi kuanzia saa moja na nusu asubuhi (7:30 AM).

Bahati Alex (L) Capital Radio Jijini Dar es Salaam na Mubelwa Bandio (R) wa Jamii Production Washington DC
Hii ilikuwa ripoti ya Novemba 23, 2013




--
*JAMII PRODUCTION*
"Usahihi wa fikra ndio fikra sahihi"

Friday 22 November 2013

Jikoni Leo;African Market-Nima Market in Accra, Ghana!!!!




Waungwana;Jikoni Leo, Tupo sokoni  Ghana..haya tuangalie mahitahi...
Kuna vingine wewe huviwezi kula lakini wengine wanaweza.

Nini kimekuvutia?

"Swahili Na Waswahili" Pamoja Daima.

Wednesday 20 November 2013

Ana kwa Ana na Astronaut Dr Donald Thomas‏


Karibu katika mahojiano kamili na Dr Donald Thomas.

Mhandisi na mwanaanga wa Marekani

 Katika mahojiano haya, Dr Thomas anaeleza historia yake na namna ambavyo ALIHANGAIKA NA KUVUMILIA kabla hajapata nafasi ya kufanya kile alichokuwa akikipenda zaidi.

Ilimchukua miaka 9 tangu ajaribu kwa mara ya kwanza mpaka achaguliwe, na katika miaka hiyo, alituma maombi mara nne.

Ili kuongeza nafasi yake kufanikiwa akaamua kuchukua madarasa ya urubani, scuba diving, kufundisha, kuongeza elimu na mengine ili kufanikisha kile alichotaka kufanya japo hakukuwa na uhakika wa hilo.

Lakini aliamini katika atendalo.

Pia ameeleza maandalizi wanayofanya na mafunzo wanayopitia kuanzia wanapochaguliwa mpaka
wanapoenda kwenye mission hizo, hisia na uoga wake siku ya kwanza alipanda
space shuttle. Amezungumzia safari nzima na shughuli kuanzia
wanavyoondoka mpaka wanavyofika angani pamoja na changamoto za kuishi kwenye
orbit. Kuanzia kupika mpaka kutumia choo. Na pia, namna alivyopokea taarifa za
kulipuka kwa space shuttle Columbia. Shuttle aliyoitumia mara tatu kati ya nne
alizokwenda kwenye orbit.

Baada ya miaka 20 aliyofanya kazi kama mwanasayansi wa NASA, na safari nne kwenye Orbit, akastaafu na sasa ni Mkurugenzi wa Willard Hackerman Academy katika chuo kikuu cha Towson hapa Maryland ambapo anahimiza wanafunzi wa chekechea kujiunga na masomo ya Sayansi na Hesabu kwa manufaa ya kizazi kijacho

Nilipata fursa ya kuhojiana naye mwaka 2011




Kwa maoni, ushauri, nk usisite kutuandikia jamiiproduction@gmail.com


--
*JAMII PRODUCTION*
"Usahihi wa fikra ndio fikra sahihi"

Monday 18 November 2013

Kipindi Maalum Mazishi ya Bi.Martha Shani Tanzania




Tunawaletea kipindi maalum cha Mazishi ya mpendwa na kipenzi chetu Bi. Martha Shani aliyefariki ghafla nchini Marekani na kuja Kuzikwa nyumbani Tanzania. Katika Kipindi hiki utaona matukio mbalimbali katika safari ya mwisho ya Bi. Martha Shani.

"Swahili Na Waswahili";Mhhh...Pole sana kaka Alex,  Familia,Ndugu,Jamaa na Marafiki.

Ulale kwa Amani da'Martha Shani.