Swahili na Waswahili

Swahili na Waswahili
Waswahili na Mswahili Rachel Siwa...Pamoja Daima!!

Monday 18 November 2013

Dr Donald Thomas alipohojiwa na Jamii Production‏


Katika kipengele hiki cha HUYU NA YULE, wiki hii utasikia mahojiano niliyowahi kufanya na Dr Donald Thomas. Mhandisi na mwanaanga wa Marekani.

 Ilimchukua miaka 33 kutimiza ndoto zake za kuelekea kwenye Orbit. Na baada ya kwenda kwenye Orbit mara nne, akastaafu na sasa anahimiza wanafunzi wa chekechea kujiunga na masomo ya Sayansi na Hesabu kwa manufaa ya kizazi kijacho

Nilipata fursa ya kuhojiana naye ambapo alieleza mengi mema



Kwa maoni, ushauri, nk usisite kutuandikia jamiiproduction@gmail.com

--
*JAMII PRODUCTION*
"Usahihi wa fikra ndio fikra sahihi"

Sunday 17 November 2013

Tumalizie J'Pili hii Vyema;Burudani-Kutoka,One Nation Gospel Na Gisubizo Choir!!!


Tumalizie J'Pili hii vyema.. Iwe Yenye Neema,Baraka,Upendo na Amani....BWANA asipojenga nyumba Waijengao wafanya kazi bure.BWANA asipoulinda mji Yeye aulindaye akesha bure.........

Neno La Leo;Zaburi:127:1-5





"Swahili Na Waswahili" Pamoja Sana

Saturday 16 November 2013

[AUDIO] DAKIKA 90 ZA DUNIA: Hatari ya bunduki za kuchapishwa nchini Marekani‏





Bunduki ya plastiki iliyotengenezwa kwa mashine ya 3D ikifyatua risasi wakaati wa majaribio

Photo credits: Screenshot from ATF Video


Kama tulivyoripoti katika ripoti hii ya Septemba 21, mauaji ya kutumia bunduki ni kati ya matatizo makubwa nchini Marekani.



Lakini pia, uwezo wa nchi hiyo katika teknolojia umesaidia kupunguza madhara ya vifo hivyo kwa kuwezesha kukamatwa kwa silaha kabla hazijafanya madhara.

Hii inajumuisha pia kutumia vifaa maalum vya kugundua vitu vya chuma ambavyo mtu anaweza kuwa ameficha.

Hata hivyo, kukua huko kwa teknolijia pia kuna athari katika mapambano dhidi ya uhalifu.


Wiki hii, kitengo kinachojishughulisha na udhibiti wa Pombe, Tumbaku, Bunduki na Milipuko nchini Marekani (ATF) kimetoa ripoti kuhusu athari ama madhara yanayoweza kusababishwa na bastola za plastiki zinazochapishwa katika umbo halisi (3D Guns)



Hii ni sehemu ya ripoti ya Jamii Production kwenye kipindi cha DAKIKA 90 ZA DUNIA kinachorushwa na kituo cha Radio cha Capital FM cha Dar Es Salaam Tanzania kila Jumamosi kuanzia saa moja na nusu asubuhi (7:30 AM).


Bahati Alex (L) Capital Radio Jijini Dar es Salaam na Mubelwa Bandio (R) wa Jamii Production Washington DC

Hii ilikuwa ripoti ya Novemba 16, 2013



Kwa maoni, ushauri, nk usisite kutuandikia jamiiproduction@gmail.com

--
*JAMII PRODUCTION*
"Usahihi wa fikra ndio fikra sahihi"

Friday 15 November 2013

Wanawake Na Mitindo Ya Nywele!!!!

Waungwana;Wanawake na Mitindo Ya Nywele...
Hivi ni kweli Nywele ndiyo pambo kubwa kwa Mwanamke?
Kujua/Kuona Zaidi nifuate huku;
http://mitindoafrica-abroad.blogspot.co.uk/

"Swahili NA Waswahili" Pamoja Daima.

Thursday 14 November 2013

HUYU NA YULE: Mjadala kuhusu MAJUKUMU NA WAJIBU WA KIJANA KWA NCHI YAKE.‏


Katika kipengele cha HUYU NA YULE, wiki hii tuliungana na VIJANA WATATU


Liberatus Mwang'ombe, Peter Walden na Ally Badawy kujadili MAJUKUMU NA WAJIBU WA KIJANA KWA NCHI YAKE.


Ali Badawi (kushoto), Peter Walden (kati(na Liberatus Mwang'ombe (kulia) wakiendelea na mjadala ndani ya studio za Jamii Production

Ulikuwa ni mjadala mrefu na huru ambao ulikuwa na mengi ya kufunzana


Karibu uungane nasi


Wakati tukimalizia mjadala kuhusu MAJUKUMU NA WAJIBU WA KIJANA KWA NCHI YAKE, Peter Walden alimuuliza Liberatus Mwang'ombe swali kuhusu kufunguliwa kwa matawi ya vyama vya siasa nje ya nchi.

Liberatus ni Katibu Mkuu wa Tawi la Chadema hapa Washington DC

Hapo pakawa na ka-mjadala kadoooogo ambako hata Ally Badawy na mwongozaji wa kipindi Mubelwa Bandio wakachangia.

Karibu usikilize



Kwa maoni, ushauri, nk usisite kutuandikia jamiiproduction@gmail.com

--
*JAMII PRODUCTION*
"Usahihi wa fikra ndio fikra sahihi"

Tuesday 12 November 2013

Mahojiano na mwanamuziki Dekula Kahanga a.k.a Vumbi‏


Hivi karibuni Jamii Production ilipata nafasi ya kuhojiana na mmoja wa wanamuziki waliojipatia umaarufu katika ucharazaji gitaa nchini Tanzania Dekula Kahanga aliye maarufu kwa jina la Vumbi.
Mahojiano haya "mepesi" yamegusa mambo mbalimbali kuhusu maisha yake kimuziki
Amehojiana na Jamii Production akiwa Sweden yalipo makazi yake ya sasa
KARIBU UUNGANE NASI

Kwa maoni, ushauri, nk usisite kutuandikia jamiiproduction@gmail.com

--
*JAMII PRODUCTION*
"Usahihi wa fikra ndio fikra sahihi"

Sunday 10 November 2013

Muendelee na J'Pili hii Vyema;Burudani Mchanganyiko-Hear My Cry Oh Lord,Blessed be the Name of the LORD,Na....!!!!

Wapendwa;Nimatumaini yangu  J'Pili inaendeleavyema...
MUNGU ni Pendo.Mimi nakupenda sana wewe uliyepita hapa/Unayepita hapa na Woooote....Muwe na Amani,Furaha na Upendo wa kweli...
Wapenzi na Mpendane;kwakuwa pendo latoka kwa MUNGU, na kila apendaye amezaliwa na MUNGU,naye anamjua MUNGU.

Neno La Leo;Waraka wa Kwanza wa Yohana:4:7-21











"Swahili Na Waswahili" Pamoja Sana.