Swahili na Waswahili

Swahili na Waswahili
Waswahili na Mswahili Rachel Siwa...Pamoja Daima!!

Friday 31 August 2012

Watoto na Malezi;Mtoto na Commando na Mtoto na Wachezaji!!!


Waunngwana Wazazi/Walezi;"Watoto na Malezi" Huyu anacheza na wachezaji,huyu anatupatia Picha la Commando!!!.

Duhh Huyu wa Commando kiboko...........Wewe unasemaje kuhusu mtoto mdogo na Wachezaji? na wa Commando jee? Kipaji,Ufuatiliaji mzuri au..
Vipi wewe ulikuwa wapenda nini Utotoni?

Tunasubiri Mtazamo wako.Maoni,Ushauri na Kuelimishana kwa Upendo.
"Swahili NA Waswahili" Pamoja Daima.

Thursday 30 August 2012

Jikoni Leo ni Tupike Pamoja-Mapishi ya Creme Caramel - Recipe of (Swahili)!!!!




Waungwana ni "Jikoni Leo" na da'Sophi wa "Tupike Pamoja" Mapishi ya Leo ni  Creme Caramel. Maneno yasiwe meengi, angalia hiyo Video.
 kama unaswali au Ushauri unakaribishwa.
pia ukitaka kujua Zaidi ungana naye kupitia;www.tupikepamoja.com au  unaweza kuungana naye You TubeTupike Pamoja.

"Swahili NA Waswahili" Karibuni Wooote.

Tuesday 28 August 2012

Pitapita ya Mswahili Mitaani-Coventry!!!!

                                   Alikutana na Wapiga Ngoma
                                   Ikapigwa na Akacheza
Mswahili mtoto akapiga ngoma nae


Banda la Wazungu, wanauza vitu kutoka kwa Waswahili wa KENYA



                            Banda la M'SENEGAL,Ameshona hizo Nguo na hivyo vidude wanatengeneza.

Waungwana ni "Pitapita ya Mswahili Mitaani" Ilikuwa Coventry.  kulikuwa na Mabanda mbalimbali ya Bidhaa , Vyakula na Michezo.

Kwabahati mbaya WaTanzania hatukuwa na Banda.
Nimatumaini yangu siku/wakati mwingine tutakuwa na Banda hata la Mchezo wa Bao,Kijiwe cha Kahawa ile Chunguu yanywewa kwa Vikombe Vidoogo na Kashata.

 Ndugu wa mimi/Blogger Mwenza EMU wa Three.Mmmhhh Ushauri wako Naufanyia Kazi.Hahahaha Eti Ndugu wa mimi ananishauri  nijiunge na Michezo kama Miereka,Judo,Sarakasi ,Kuogelea na.........Uwiiii Kweli umenichoka, Sikuweza Mikundeni itakuwa Michorokoni? hhahaha na Uzee huu mwili umekomaaa.Hahah Usichekeshe walionuna.

Sina Meengi,Unalolote la kuongezea,Maoni,Ushauri?
Pamoja sana "Swahili NA Waswahili"

Sunday 26 August 2012

Mswahili Wetu Leo;AIKAROSE MWASHA-Anaishi BELGIUM;NYOTA TUMAINI LETU!!!

NYOTA TUMAINI LETU





Jina: AikaRose Mwasha
Jinsia:Kike
Miaka:12
Utaifa:TANZANIA
Mchezo: Taekwando 
KILO: 28 kg- beginners FEMALE
Club: Nong Jang
MAKAZI: Leuven Belgium
MAFANIKIO: MEDALI YA FEDHA & DHAHABU


Kijana wa kitanzania mwenye ndoto ya kuwakilisha nchi yake kwenye mashindano ya kimataifa hapo usoni kwa kupitia mchezo wa mbinu za kujihami wa TAEKWANDO ,anamapenzi makubwa na mchezo huu aliouanza angali mdogo akiwa na umri wa  miaka 9 ,ameshashiriki mashindano madogo madogo nchini Belgium na kupata mafanikio makubwa kufikia medali ya fedha. Hivi karibuni alifanikiwa kupata medali ya dhahabu katika mashindano ya Olympic open Brussels yaliyofanyika Rue Du Lombartzyde Brussels Belgium tarehe  27 May 2012.
Sasa hivi anajiandaa na team yake kwenda Copenhagen kwenye  mashindano ya Wonderfull Copenhagen yatakayofanyika mwezi ujao.
Wito wake hasa kwa vijana wadogo akitilia mkazo jinsia ya kike ni kujifunza michezo mbalimbali na kuwa na ndoto ya kuwa mabalozi kwa taifa lao la TANZANIA.
VIPAJI HUINUA TAIFA

"Swahili NA Waswahili" Tunakutakia kila la kheri.

Mario Van Peebles Exclusive Interview - Tanzania Films Critics Associati...!!!!!!


Mario Van Peebles interview with Tanzania Films Critics Association (TFCA 


The link above is about 15 Question and Answer of video Insightful interview with Film maker/Director/Producer, Actor Mario Van Peebles and Michael Cohen, talk about their new Movie "We the Party" and general view of Tanzania Film Industry in including Copyright aspects in combating piracy problems and their view of films activities here in Tanzania.
Tanzania Films Critics Association (TFCA)
----------------------------------------------

Nawatakia J'Pili yenye baraka na Amani.Burudani- Mwamba Rock Choir!!!!


Wapendwa Nawatakia J'Pili yenye Baraka,Upendo,Umoja, Amani na Malezi mema.

Basi wakamletea watoto wadogo ili awaguse;Wanafunzi wake wakawakemea.Ila YESU alipoona alichukizwa sana,akawaambia,Waacheni Watoto wadogo waje kwangu,msiwazuie;Kwamaana Watoto kama hawa Ufalme wa MUNGU ni wao.

Neno La Leo:Marko Mtakatifu:10:13-16

"Swahili NA Waswahili" MUNGU ATUBARIKI SOTE.

Saturday 25 August 2012

Chaguo La Mswahili Leo;Bob Rudala,Ali Kiba,,2berry,20 Percent!!!!!!!

Waungwana "Chaguo La Mswahili Leo" ni Kina Kaka hao wakilalamika juu ya Mapenzi.
Kwa Mtazamo wangu naona kama Tanzania[bongo]Nyimbo nyingi zinazungumzia Mapenzi.Jee ndizo Zinawapenzi wengi,Rahisi Kutunga na Kuimba,Au...?

Mpenzi mimi sina Mengi Zaidi ni kutoka kwako.
Karibuni sana Kwa Maoni,Ushauri na Kuelimishana kwa Upendo.

"Swahili NA Waswahili" Pamoja Daima.