Swahili na Waswahili

Swahili na Waswahili
Waswahili na Mswahili Rachel Siwa...Pamoja Daima!!

Saturday 23 June 2012

Jikoni Leo;Tupike Pamoja, Video Mpya-How to cook Donuts [in Swahili]!!!!!!!

Waungwana "JIKONI LEO"
Ni "TUPIKE PAMOJA" Wametoa Video mpya Jinsi ya Kupika Donuts.kama una Swali,Ushauri Usisite kuwasiliana nao kupitia.www.tupikepamoja.com.

"SWAHILI na WASWAHILI"
Pamoja Sana!!!!!

Thursday 21 June 2012

Watoto na Malezi;Violence Against Children [Ukatili Kwa Watoto]!!!!!!!


Makala hii inaonyesha ukatili dhidi ya watoto na jitihada zinazofanywa na serikali ya Tanzania kupitia Wizara ya Maendeleo ya Jamii, Jinsia na Watoto pamoja na Wizara ya Afya na Ustawi wa Jamii wakishirikiana na wadau mbalimbali kutokomeza ukatili dhidi ya watoto.

Makala hii imetengenezwa ikiwa ni mwitikio wa hali ya unyanyasaji na ukatili ambayo watoto wanakabiliana nayo. Makala hii imeandaliwa sambamba na uzinduzi wa ripoti ya ukatili kwa watoto ambalo ni agizo la Katibu Mkuu wa Umoja wa Mataifa kutokomeza ukatili kwa watoto. Ripoti hii ilizinduliwa na Dr. Asha Rose Migiro, Naibu Katibu Mkuu wa Umoja wa Mataifa.

Waungwana;Wazazi/Walezi Mnamaoni,Ushaurigani katika haya?


Shime Wazazi/Walezi;"Tutokomeze Ukatili  kwa watoto" Tuungane Pamoja katika kuwapenda,kuwatunza,kuwapa Malezi bora,kuwapatia Elimu na Kuwasikiliza.
"Mtoto wa mwenzio ni wako".
"SWAHILI na WASWAHILI" Pamoja sana!!!!

Wednesday 20 June 2012

RATIBA YA KUUAGA MWILI WA MAREHEMU WILLIAM FOFO MAPUNDA!!!!!





WILLIAM FOFO MAPUNDA (FOFO)

MWILI WA MAREHEMU WILLIAM FOFO MAPUNDA UTAAGWA RASMI LEO TAREHE 20/06/2012 NYUMBANI KWAKE TABATA KISUKULU TAYARI KWA KUPELEKWA NYUMBANI KWAO MANDA LUDEWA KWA MAZISHI, AMBAYO YATAFANYIKA KESHO TAREHE 21/06/2012 SIKU YA ALHAMISI.

RATIBA:

SAA 5.00 ASUBUHI: - MWILI KUWASILI NYUMBANI KWAKE TABATA KISUKULU

SAA 6.00 - 7.00 MCHANA: - CHAKULA KWA WOTE

SAA 7.00 - 8.30 MCHANA: - SALAMU ZA MWISHO (LAST RESPECT)

SAA 8.30 - 9.00 ALASIRI: - MWILI KUFIKA KANISANI (KANISA LA ANGLIKANA TABATA KISUKULU KARIBU NA BAR YA MAZDA)

SAA 9.00 - 10.30 JIONI: - IBADA NA KUAGA KWA WALE AMBAO WATAKUWA WAMECHELEWA NYUMBANI

SAA 10.30 JIONI: - KUANZA SAFARI YA KWENDA MANDA LUDEWA

WILLIAM FOFO MAPUNDA ALIFARIKI GAFLA USIKU WA KUAMKIA JANA NYUMBANI KWAKE TABATA KISUKULU, KWA TAARIFA TULIZOZIPATA KUTOKA KWA MADAKTARI WA HOSPITALI YA AMANA ILALA, KIFO CHAKE KIMESABABISHWA NA KUPATWA NA BLOOD PRESSURE GAFLA.

KWA TAARIFA YOYOTE PIGA NAMBA: 0713-254553

Tuesday 19 June 2012

TAARIFA YA MSIBA: WILLIAM FOFO MAPUNDA HATUNAYE TENA!!!!!!


Marehemu William Fofo enzi za uhai wake.

Taarifa ambazo zimetufikia hivi punde Ndugu yetu, Rafiki yetu William Fofo maarufu kwa jina la FOFO amefariki dunia usiku huu akiwa nyumbani kwake Tabata.

Taarifa kamili za sababu ya kifo chake bado hatujazipata, pindi tutakapozipata tutawajulisha, kwa sasa taratibu zote inaendelea nyumbani kwake Tabata na mwili wake umehifadhiwa katika Hospitali ya Amana Ilala Dar es salaam.

Monday 18 June 2012

Wa Afrika na Sherehe zao,LeoTupo Malawi ni-Kachitsa na Farayi;Tradditional Wedding!!!!


Mwenyewe bi Arusi Mtarajiwa,da'Farayi
Bwana Arusi Mtarajiwa kaka Willy Kachitsa,Huingii hapo mmpaka utoe pesa!!!
MmePendeza sana Wapendwa!!!!!
Mmmmhh Mapenzi Motomoto!!!!
Waungwana Leo Tupo Malawi, kaka KACHITSA na da'FARAYI wanatarajia kuwa mwili mmoja hivi karibuni.
Nasi tunawatakia kila lililojema katika maandalizi yao.Mungu asimamie kila hatua na Twasubiri kwa Hamu siku yenyewe!!!!!.

Waungwana; Sherehe hizi za WaAfrika zinafanana eehh? vipi kuhusu mambo ya kutoa pesa/Kufichua kabla ujaingia kwa wakwe na Mengine Meengi, Mila/Tamaduni za ndoa. zipi ninyi mnatumia/mlitumia?
 jee bado zina nguvu/Kufaa/Kufuatwa au mmezitupa?.

Jee wewe una Maoni ,Ushauri,gani kuhusu Tamaduni/Mila hizo nivyema kuzitunza na kuzifuata au Zimepitwa na Wakati?.

[To; Willy&farayi;May Good bless you!!!
We are still waiting for the big day!!
With Love From Isaac's Family.]


"SWAHILI na WASWAHLI"Pamoja sana!!!

Sunday 17 June 2012

Tumalize J'Pili vyema,Burudani-Anita John (Jehovah Jireh) swahili !!!!!!!!!

Waswahili wakisifu na Kuabudu,Da'Anita mwenye blauzi ya maua yenye pink
Natumaini mlikuwa na J'pili njema, Mungu azidi kuwabariki wooote!!!
Tumalizie siku na Zaburi ya 23:1-6;Bwana ndiye Mchungaji wangu,Sitapungukiwa na kitu!.!!!!!
Nawapenda Wooote.!
"SWAHILI na WASWAHILI"   Pamoja sana....

EXTRA BONGO WAZEE WA KIZIGO WAZIDI KULITIKISA JIJI NDANI YA MEEDA SINZA.




Ally Choki akiwaburudisha washabiki na wapenzi wa Extra Bongo ndani ya Meeda usiku wa kuamkia leo
Choki akichea show na wanenguaji wake wa Extra bongo ndani ya Meeda Sinza.
Banza Stone Mwana wa Masanja - AKA Jenerale akiimba nyimbo yake ndani ya Meeda Sinza.

Mmiliki wa KAPINGAZ Blog Henry Kapinga alikuwepo ndani ya Meeda Sinza, hapa akishoo luv na kuwapa Big Up Ally Choki na Banza Stone wakati Extra Bongo walipokuwa wanapamofu usiku wa kuamkia leo ndani ya ukumbi huo.
Rapa maarufu namba moja Afrika mashariki wa Extra Bongo Kaba Tano akirap ndani ya Meeda Sinza usiku wa kuamkia leo