Swahili na Waswahili

Swahili na Waswahili
Waswahili na Mswahili Rachel Siwa...Pamoja Daima!!

Tuesday 5 June 2012

SHUKRANI KUTOKA KWA MCHUNGAJI JOHN KUPAZA WA KANISA LA BAPTIST TANGA.


Marehemu Mama Mchungaji John Kupaza
Familia ya Mchungaji John Kupaza wa Kanisa la Baptist Kisosora Tanga anapenda kutoa shukrani zake za dhati kwa wale wote waliojaribu kuokoa maisha ya Mke wake Mpendwa Marehemu Mama Mchungaji Kupaza na wale walioshiriki kwa dhati katika shughuli za mazishi.
Mchungaji J. Kupaza anapenda shukrani zake za dhati ziwafikie Baptist Convention of Tanzania, Mwenyekiti wa Jumuiya Kuu ya Wanawake wa Baptist Tanzania, Dr. Lugano Mtafya, Umoja wa Makanisa ya Baptist Dar es salaam, Baptist Kanda ya Kaskazini, Umoja wa Makanisa Tanga, Manesi na Wauguzi wa Hospitali ya Muhimbili, Hospitali ya Cancer ya Ocean Road, Hospitali ya Bombo Tanga, Madaktari na wauguzi wa Magomeni Baptist Center, Majirani wote wa Mchungaji Kupaza na watoto wa Marehemu Sarah, Samwel, Rosemary, Dr. Lawi, Potinna, David na Tumaini wote kwa pamoja wanawashukuru wote mlioshirikiana nao katika kipindi hiki kigumu. Mungu awabariki wote.
Marehemu Mama Mchungaji Kupaza alifariki Tar. 18/05/2012 Jijini Dar es slaam na kuzikwa Tarehe 21/05/2012 Jijini Tanga katika makaburi ya Bombo.
BWANA ALITOA NA BWANA AMETWAA JINA LA BWANA LIHIMIDIWE
AMEN.

Monday 4 June 2012

Mambo ya Igatanzania!!Ungana nami kujua zaidi!!!!!!

Haya Waungwana mambo ya Igatanzania hayo!!!
Niwauzaji wa T-shirt,Jezi,Kanga,Vitenge,Viatu vya shanga,Bangili,Makembe na vitu vyooote vya urembo kutoka nyumbani Tanzania.

 Pia ni Wapishi wa vitafunwa/Vitafunio,Vyakula vyooote ujuavyo vya kiswahili.
Pata kitu Roho inapenda na waswahili wa "Igatanzania"

Wapo Coventry u.k.

kwa mawasiliano zaidi piga namba hii.07730008921.

KARIBUNI SANA WAUNGWANA.

Orijino Komedi na -OK Msuruhishi wa Muungano-Msudani.avi

Hahahhhaahahhahah haya,Waungwana Mambo ya Tanganyika na Zanzibar!!!!!!
[Watoto wa mujini wanasema Kimenuka huko].


Sina la zaidi Mengi Mtasema Wenyewe!!PaMoja sana "Swahili na

 Waswahili"
Mungu ibariki Tanzania.

Sunday 3 June 2012

Nawatakia J'Pili Njema,Burudani- Upendo Nkone,Abihudi Misholi!!!!!!


6.Lakini nasema neno hili,Apandaye haba atavuna haba;Apandae kwa Ukarimu Atavuna kwa Ukarimu.
7.Kila mtu na Atende kama alivyokusudia Moyoni mwake,si kwa Huzuni,wala si kwa Lazima;Maana Mungu humpenda yeye atoaye kwa Moyo wa Ukunjufu.
Neno la Leo:Wakorintho9:6-15.

Mungu atubariki Sote!!!!

Saturday 2 June 2012

Chaguo la Mswahili Leo-Tupo Burundi;Ndugu zangu wa Buyenzi Mpo?!!!!!

 Bibi na Bwana Billy.Hongereni sana Kwa kupata mtoto wa kiume.Mungu amlinde na kumkuza vyema.Nanyi awape hekima katika malezi yenu.Ngoja leo niwasogeze nyumbani.
 

Waungwana "CHAGUO LA MSWAHLI LEO" Nimewapeleka BURUNDI.
Haya umeona waRundi waishio CANADA wanavyofunza watoto wao Utamaduni wao?Jee wewe unaonaje kuhusu hili la kuwafundisha watoto mambo yakwenu?

Jee unao wakati wa kuwafundisha watoto hata Kibuzi,Kinyunyu,Ukuti,Rede,Nyimbo hata zile za Mchakamchaka?Au Muda hautoshi?

Nakumbuka kama wikimbili 2 tulikutana Waswahili kwenye Mnuso Mmoja hivi, Baada ya Kushiba Tukaanza kuimba hii Nyimbo.

Alisemaaa  Alisemaaa,Alisema Nyerere Alisema,Vijana wangu wote Mmeleegea, Sharti Tuanze Mchaka Mchaka.................Hahahahaa

 Swahili na Waswahili Waungwana.

 Kama unalolote utahitaji kuwajuza wenzio. Tutumie Kupitia Email.rasca@hotmail.co.uk.Pamoja sana!!!!!!

Wednesday 30 May 2012

Jikoni Leo; ni Wasomali na Darasa la Mapishi na Utamaduni wao;Wazazi wa Marekani.na Da'Mariam!!!!!!

Waungwana "Jikoni Leo" ni Wasomali;
Wazazi/Walezi wa Marekani Wakiwafundisha Watoto wao Jinsi ya Kupika na Tamaduni za Kwao.


Pia da'Mariam naye Hayuko Nyuma kuonyesha/Kuwafunza watu wengine Jinsi "East Africa" wapikavyo.
 

Hapa nimeona Wasomali wanajitahidi kuwafundisha kupika watoto wa kike tuu,Sijui watoto wa kiume kwao Hawapiki?au bado wanamambo yaleee mtoto wakike "LAKE JIKO".

Waungwana Mmejifunza nini kwa haya ya Wenzetu Wasomali?

Karibuni sana kwa Maoni,Ushauri na Kuelimishana kwa Upendo.

Pamoja sana."Swahili na Waswahili."

Tuesday 29 May 2012

Wa Afrika na Sherehe zao;Leo ni Wadigo wedding , Kenya!!!!!!

Hahhahahhah Kadala,Mwanamke wa shoka, Mwanakwetu,Kadoda,Ndugu wa mimi na Waungwana Woooote,
Mambo hayo ya kupetipeti!!
Sina lazaidi Mengi Mnayo Wenyewe Yakheeeeee!!!!


Karibuni sana. "Swahili na Waswahili".Pamoja sana tuu.