Swahili na Waswahili

Swahili na Waswahili
Waswahili na Mswahili Rachel Siwa...Pamoja Daima!!

Monday 28 May 2012

Da'Tracey-Sarah,Atimiza Miaka 11!!!!!!!

Da'Tracey-Sarah
Da'Sandra akiandaa Keki
Tumtangulize Mungu kwanza katika Yote!!!

Leo umezima 11,mungu akulinde uzime 100!!!
Anaitwa Mkama; kwakuzima Mishumaa hayuko nyuma,Kama mtoto wako anasuasua kuzima,Tuwasiliane!!
da'Tracey akikata keki na da'Mija akihakikisha mambo yako sawa!!!

da'Elizabeth na da'Mija wakiandaa keki,watu tule!!kweli watoto wa Shoka,Mungu awabariki sana!!
Mama akimlisha Mwana!!
Da'Mija akilishwa na Rafiki yake kipenzi,Mungu azidi kuwaunganisha daima!!
Da'Tracey akilishwa na dada yake!!
Da'Sandra akilishwa na Mdogo wake, duuh kuna haja ya kuongeza sijui!!
Da'Anita akilishwa,Chezea yeye!!!
Da'Asiimwe akilishwa,huwa hana haraka wala maneno mengi,jicho tuu linaongea!!
Da'Manjula aliamua kupanda juu ya kiti,Ale kwa raha,nani anapenda Ufupi?
Kamanda Mkama a.k.a.Mzee wa Next,Akipata kipande chake!!!
Dada Mkubwa,Eliza naye akijipatia keki!!
Pamoja daima!!!!
Katuni/Vibonzo lazima tuangalie!!!
Mapoziiiiiii
Unahitaji wanamitindo? Tuwasiliane.....hahahahaha
Na muziki tulisakata, sikunyingine nitaweka Video!!!Lakini Zilipendwa waligomaaa!!!
Mwenyekiti wa Kamati ya Maandalizi,da'Mija[Mia] akipozi baada ya kazi kubwa!!
Da'Tracey[Sarah]Akipozi  na Kuwashukuru Wazazi,Ndugu,Jamaa na Marafiki kwa yooote!!!



Familia ya Isaac,Tunamshukuru sana Mungu kwa Mema Mengi aliyotutendea,Asante kwa kumtunza na kumlinda Mtoto wetu Tracey-Sarah na Familia pia.
Asante kwa Kumaliza SAT'S,Salama,wewe ulimlinda akiwa Shule ya Msingi pia Tunamuweka Mikononi mwako Aendapo Secondary.

Shukrani Nyingi Ziwaendee,Familia ya Nyotu[Kamau].Familia ya Manju[Da'Mija Mwanamke wa Shoka].Kaka Don,baba Eliza na Familia yako. Da'Maggie[dadake]Asante sana.

Mungu awabariki sana kwa Moyo wenu wa Upendo na Kutumia Muda wenu kuwa nasi.

Pamoja sana Wapendwa,MUNGU NI PENDO APENDA WATU.Nasi TUNAWAPENDA WOOOOOTE.

Friday 25 May 2012

Waswahili wetu Leo;WaTanzania na Madawa ya Kulevya!!!!!!!

Haya Waungwana;Hawa ni Ndugu zetu,Jamaa zetu,Rafiki zetu,
Jee nani Alaumiwe? Muuzaji au Mtumiaji?
"Swahili na Waswahili" Pamoja sana.

Tuesday 22 May 2012

Wa Afrika na Sherehe Zao;Nigerian Bride (Traditional Wedding) and Gele Styles!!!!

Swali; Jee WaTanzania tunaweza kuvaa nini kwenye Ndoa,Siku ya Posa,Siku ya kuagwa, K/party au Sherehe yoyote inayotakiwa Kuonyesha Utanzania Wetu?

Nimeshaona wengi wakivaa kimasi, Jee Vazi hili linaweza kututambulisha?

Waungwana karibuni sana katika Kuelimishana,Kushauriana  na Mapenzi yako katika Vazi la Nyumbani.
Pamoja sana .Swahili na Waswahli!!!!!

Monday 21 May 2012

Jikoni Leo. Mswahili; da'Sophi na Tupike Pamoja!!! Angalia Video!!!!




Karibuni "tupikepamoja.com"


Habari utakazo zipata katika tovuti hii ni picha za video na maelezo ya kina kuhusu namna ya kupika mapishi na vyakula vizuri vya kimataifa muhimu zaidi ni rahisi kupika.
Tovuti hii ni kwa ajili ya watu wanaopenda kupika, kujaribu vyakula vipya na ladha mpya ili kuwashangaza rafiki na familia zao kwa ladha hizo. Maelekezo ya mapishi utakayopata hapa ni kwa ajili ya meza kuu ingawa wakati mwingine tunashirikiana nawe katika vinywaji na viburudisho (deserts & sweets).
kwa kuanzia ni matumaini yetu utafurahia kupika kama sisi.
Pia usisahau kututumia maoni yako, maswali na ujumbe tuweze kuboresha na kutimiza mahitaji yako, Asante kwa ushirikiano wako
Furahia chakula chako!

Kujua zaidi Mtembelee.www.tupikepamoja.com
Haya Waungwana Mambo hayo kazi kwenu na "Tupike Pamoja"

Hongera da'Sophi kazi nzuri.

Sunday 20 May 2012

Nawatakia J'Pili Njema;Burudani;Sarah K - Liseme.The Christ Ambassadors-Moyoni Mwangu na Kazi Tufanye!!!!!!



Watoto wa KKkT Kijito Nyama
Nawatakia J'Pili yenye Baraka, Upendo,Amani, Umoja na Furaha.
1;Haleluya.Msifuni Mungu katika Patakatifu pake;
Msifuni katika anga la uweza wake.
Neno la Leo:Zaburi ya 150:1-6. 

6;Kila mwenye Pumzi na Amsifu BWANA.
Haleluya!!!!!!!!!.

Saturday 19 May 2012

Chaguo la Mswahili Leo;Celine&R.kelly- I'm Your Angel, The Step in the Name of Love. Na nyingineee!!!



 Waungwana Nawatakia j'Mosi yenye Amani na Furaha daima!!.
Leo ngoja Tuangalie/twende Pande hii.
 Sina Mengi Zaidi Nakusikiliza wewe tuu.Baada ya Burudani, Umekumbuka nini,Umeguswa,Umefurahi,Umenuna au? "Swahili na Waswahili" Pamoja sana

Friday 18 May 2012

MTANZANIA DR ENGINEER SHABAN KACHUA ATUNUKIWA RASMI SHAHADA YAKE YA UDAKTARI WA FALSAFA NCHINI CANADA.


Dr Engineer Shaban Kachua mwenye joho lenye rangi nyekundu na Bluu akiwa na waafrika wenzake wakati wa alipotunukiwa Shahada yake ya Udaktari wa falsafa Nchini Canada.
Hapa Dr Kachua akiwa amekaa mstari wa mbele kabisa na wahitimu wenzake.
Mama Mzazi wa Dr Kachua (mwenye blauzi nyeusi), akiwa na Mama mkwe wake, wote kwa pamoja walishiriki katika tukio la kihistoria la kutunukiwa Shahada ya PHD kwa mtoto wao nchini Canada.
Mrs Dr Shaban Kachua (Jemima) akiwa na furaha pamoja na watoto wao walishiriki katika shughuli ya kutunukiwa Mume wake shahada ya udaktari wa Falsafa (PHD).

Kwa sasa Dr Shaban Kachua anaishi Nchini Canada pamoja na familia yake. Sisi kama watanzania wenzake tunapenda kumpongeza sana kwa kuweza kuipeperusha vema Bendera yetu, tunapenda kumshauri pia, elimu yake hiyo aweze kuitumia pia kulisaidia Taifa lake la Tanzania hasa katika nyanja hiyo ya Sayansi, kwa kutambua zaidi tuna upungufu mkubwa wa wanasayansi katika Taifa letu.

HONGERA SANA
Asanteni sana KapingaZ http://kapingaz.blogspot.co.uk/