(Lifestyle)Jamii,Tamaduni ,Matukio,Maisha ya Waswahili. Wapendao Kiswahili/Waswahili,Marafiki wa Swahili na Waswahili, Na Mengineyo ya Karibu, Yahitajikayo Kujuzwa Waswahili.Karibuni sana!!!!!!!
Swahili na Waswahili
Waswahili na Mswahili Rachel Siwa...Pamoja Daima!!
Showing posts with label Chaguo la Mswahili. Show all posts
Showing posts with label Chaguo la Mswahili. Show all posts
Waungwana; Chaguo La Mswahili Leo..Mambo ya.. Boyz 2 Men.... Thank you in Advance, On Bended Knee, A song for MAMA ..................... na Nyinginee.... Mhhh palikuwa hapatoshi...Vipi wewe kuna lolote unakumbuka ukisikia/kuangalia nyimbo hizi...Wapi na Nini?
"Swahili Na Waswahili" Zilipendwa/Zinapendwa...J'Mosi Njema.
Waungwana maneno meengi sinaaa..Mmmhhhh...Kitambo kidogo..walikugusa/Kuwapenda?Jee Bado wapo Juu? Nini /Wapi unakumbuka ukisikiliza Nyimbo hizi?.. Mimi ninawakumbuka watu wengi saana wengine wapo Hai na wengine washatangulia[Kufa].Wengine ninamawasiliano nao Wengine hata sijui wako wapi...Yote ni Maisha....... Twende Sote sasaaa....... "Swahili NA Waswahili" Pamoja Daima.
Waungwana;Chaguo La Mswahili Leo..Mhhhhh...motoo.mambo mchanganyiko.ya Kitambo kidogo.... Vipi hizi zinakukumbusha nini/wapi?.Zina kubamba/kuzipenda? Au hukupata kuzisikia?... Twende sote sasaa.....Balobakiee..na Imalobato lembiyeeeh........kusemasema walisema tumechokaaa..Muongo na mulozi ni watu wa kuchomaaaah....... Kujulikana kumbetabu mwana mbokaaa... Ukiwa shantii kama Mushedo wanashangaaaa....ukitembea peke yako wanasema wewe ndiyo mbayaaaa....Kujulikana kuna mamboooo....Lwambo wetu Franco wandugu eeehhhh....... Rafiki yake ananiaeeehh...wewe Mangwana ee...usiwafuate endelea jamani eehh...Ukipata Tabu omba kwa MUNGU eeeehhh Alafu MUNGU pekee yeye Milele na Milele eeehhh........ Wewe na mimi kisa gani ayaahh Ndugu nimekosea nini Angalia Makambooo eee....kama kuna mambo unielezee Taratibuuu eeehh kukorofisha mbele ya watu sitakieeeeehh sikia eeeeehhh......... "Swahili NA Waswahili"Pamoja sana.
w Waungwana;Chaguo la Mswahili Leo ni Mambo ya Mduara/Taarab..... Ralaralaaaaaa...lalalaaaahhhh..Mmmhh ....mimi sina Mengi kama wewe unayo Funguka /Ongea tuu. Swali la Kizushi;-Eti nyimbo za Taarab/Mduara nyingi zinauchochezi,Ushari,Vidongo na Umbea ......Haswa sa siku hizi.Za Zamani nyingi zilikuwa Kimapenzi Zaidi......Unasemaje Muungwana? "Swahili NA Waswahili" Twende Soteeee sasa.
Waungwana;"Chaguo La Mswahili Leo" ni "Wana wa SikindeNgoma Ya Ukaye".Maneno Meengii yanapunguza Uhondo na kujua Uhondo wa Ngoma Ingia Uchezeeee!!!! Waungwana kama zimekugusa/kuzipenda usikonde unaweza kutuambia Wimbo upi umekugusa na kwasababu ipi/Unakumbukia nini?
"Swahili NA Waswahili"Twende Sotee......Mv. Mapenzi Meli ya Wapendanao Moyo kama Bahari Manahodha mimi na wewe,x2.......Duniani kuna Mengi sawasawa na Bahariiii Kuna Papa na Nyangumi Tena wale wa Hatariii....... Mmhhhhh Sauti....?? Ngoja Niendelee na Chumvi..Lakini naweza pata SAFURA Bure Chumba cha kipaji cha Uimbaji Sikuingizwaaaaaa!!!!!!!!! Hahhahahaaaa..
Waungwana;"Chaguo La Mswahili Leo" Mmmmhhhh Motooo Afrika Mashariki Na Kati..... Wewe tuu utuambie Video ipi imekubamba/kuipenda? Kwa nini? Karibu sana....Swagger Swagger Swagger........... "Swahili NA Waswahili" Motooooooooo.
Waungwana;"Chaguo la Mswahili Leo" Mambo ya Mnanda/Mchiriku na hii ya JIDE sijui niiteje Chakacha au........Naomba mnisaidie. Sina Meengi saana.Kama Umeguswa au unalolote unalokumbuka jimwage tuu.....
Twende Soote sasa. Ilala salamu zao...Migomigo salamu zao Temeke wasalimieeee oohh... Mmmhh huu Mnanda ukipigwa kigogo watu Ilala hamlali.. "Swahili NA Waswahili" Sereeeeebukaa.
Waungwana;Chaguo La Mswahili Leo""Mambo Ya zamani Kidogo.
Nakusikiliza wapi unakumbuka na nini kilikuwa kinavaliwa wakati huo? Scania,Mwanameka, Raizoniii,Fundi Nimwagie,Soroo, Vishati Vyembamba na Ulipiga Picha za Studio wewe? hahahah umeshika kiuno kwenye Maua!!!!
Waungwana;"Chaguo La Mswahili Leo"Mambo hayo ya Zilipendwa..Unakumbuka Nyimbo hizi ?Ulikuwa wapi na Umri Gani weee..Uliziimba na kuongezea maneno yako pale usipoelewa?Bado Zinakubamba/Kuzipenda?Enzi hizo Ulikuwa Unavaajeeee? Kama si Mwaka Wa Watoto Viatu Kutoka BORA au MORO Shuzzzzz..
Kaka Yangu Chacha o'Wambura ananiambia ukisikiliza nyimbo hizi Unajiona KIJEBA...Hahaah.......
Twende Sote sasa Jua Maisha ni Mulima eee, Kuna Kupanda na kushuka eee...Bali Kuteleza si kwanguka eee Mtoto wa Mama....Mmmmhhh ngoja niendelee kunywa Mayai Mabichi!!
Waungwana; "Chaguo la Mswahili Leo" Maneno si Meeengi ,jee wewe ulicheza nyimbo hizi, basi hata kuzisikia?Jee kuna lolote unakumbuka kupitia Mchanganyo wa Leo au Nyimbo moja kati ya hizo? Tuelezeeee. Karibu kwa Yoote..Twende Soote sasa....Aaaaaa aaaaaahhh aaahhhh... Mhhhh Sauti imegoma.......kaaaziii kwelikweli ngoja niendelee na Chumvi. "Swahili NA Waswahili" Pamoja sana
Mabibi wa [doti com] Kileo na Mambo Yao!!!!!!Mama Erik/Kadala.Ndugu wa mimi na Waungwana woote, hapo vipi? bibi katupiaaa.........Mabibi wa leo hawataki,Sangula,Vanga,Mganda,Lizombe,Mbeta, Mdumange. Nao wanaungana na mangoma ya sasa. Vipi ndiyo maendeleo au?
Waungwana; "Chaguo La Mswahili Leo"ni mambo Mchanganyiko.
Hunifahamu sikufahamu iweje leo unipakazie!!!........mambo ya Dully....Banana nae na mambo ya oohh oohh Nzela mwanamama!!!
mmhh ngoja nikanywe Maziwa kwanza...
Waungwana sina Meengi Twende sotee sasa, kuna lolote unalo lakuongezea,kukumbuka katika nyimbo za Leo?Tuhabarishe/tuelezee!!!!!
Waungwana"Chaguo LA Mswahili Leo"Leo ni Mswahili Q CHIEf.
Vipi Nyimbo zake zinakubamba/unazipenda?Jee kunakitu unakumbuka kupitia Nyimbo hizi?
Twende soote sasa..Kosa langu kosa langu ni lipi baba? ulinikana Tangu tumboni, Ulimkana mama yanguu...Si ulinizaa wewe Ukanikataa sasa iweje unaona mi Nafaaaaaaaa.... Endeleaa...
Jee vipi kama mtoto alikataliwa na BABA Yake ni Vyema nae MtotoKumtosa/kumkataa baba au...Jee Ingekuwa Wewe Ungefanyaje?.
Waungwana "CHAGUO LA MSWAHILI LEO" Turudi nyuma kidoogo Tuangalie/Tusikilize Bendi zetu , jee unaonaje Bendi hizi? Zinaklukumbusha nini na jee Zinakubamba/Unazipenda? Vipi Bendi za kileo na za zamani Tofauti iko wapi?
Na jee zasasa wanafanya vyema zaidi kwa sababu ya usasa au wanakwenda Kinyume?
Twende sote sasa....... oohh mwajuma pesa hupatikana kwatabu...oohh mwajuma pesa hupatikana kwa shidaaaaa...Bwana Mashakaaaa wachakulalamika oohh kama amekushinda mrudishe kwaooo.......