Swahili na Waswahili

Swahili na Waswahili
Waswahili na Mswahili Rachel Siwa...Pamoja Daima!!
Showing posts with label Chaguo la Mswahili. Show all posts
Showing posts with label Chaguo la Mswahili. Show all posts

Saturday 14 July 2012

Chaguo la Mswahili Leo-MATONYA feat LADY J.D - ANITA naNyingine Nyingii!!!!!

Waungwana Nimatumaini yangu woote Wazima.
Haya "Chaguo la Mswahili Leo" ni da'Judith[Lady Jayeed]
Vipi mwenzangu kuhusu dada huyu Amekipatia/Kujulia Kipaji chake?
Mimi huwa namkubali sana tuu kwa Muziki /Nyimbo zake.
Pia dada huyu anahusika na JIKONI, kwa hapo mimi siwezi semakitu kwani Sijawahi kufika"NYUMBANI  LOUNGE" Na sijawahi Kuonja Mkono wake[Mapishi yake].
Lakini nasikia ni Moto wa kuotea Mbali.

Jee unalolote unaweza kutuambia kuhusu kazi za dada huyu?
wewe anakubamba/unapenda kazi zake?.
Ngoja Tusikie kutoka kwako tusimalize Uhondo.

"Swahili NA Waswahili" Twende Sotee sasa... Natamanii kuwa Malaikaaa natamakuwa kuwa mtotoooo kohkohkoh Kibanda[Kipaji] hiki cha Kuimba mwenzangu mmhhh hahahha nimekumbuka Nyumbani nikiimba watu woote walala chini kwa kicheko haahahah Oiiiiiiiiiiiiiii 
ok nimekumbuka ngoja nilambe "chumvi" nitarudi tena

Saturday 7 July 2012

Chaguo la Mswahili Leo-Mafikizolo - ndihamba nawe na nyingine nyingiii!!!!!!

Waungwana; Leo ngoja tuwaangalie Hawa "Mafikizolo",
 Jee wewe wanakubamba/Unawapenda?
Nini zaidi kina kuvutia katika Muziki wao?.
Sina Mengi zaidi Nakusikiliza wewe.Twende sote sasa!!
"Swahili NA Waswahili" Pamoja Sana.

Saturday 23 June 2012

Chaguo la Mswahili Leo;DDC Mlimani Park na Tancut Almasi!!!!!!!!!

Waungwana "CHAGUO LA MSWAHILI LEO"
Turudi Nyuma kidogo Tuangalie/Tusikilize Nyimbo hizi kutoka kwenye Bendi zetu..
Jee unauonaje Mziki wa Bendi za sasa na Zamani?
Karibuni sana katika Yote!!!!!
"Swahili NA Waswahili" Twende Soteeeeeee.

Saturday 9 June 2012

Chaguo la Mswahli Leo;Mchanganyiko;ZAY B,DataZ,Mez B&RaYC,Cat-Z,AY,FA,Gk&Pauline Zongo na...Safi hiyooooo!!!!!!

Waungwana Leo hakuna Maneno Meengii, Ni Burudani tuu!!!!
Lakini hawa wengine wako wapi?
je Unakumbuka chochote kuhusu Burudani ya Leo?
 kibao kipi? na nini kinachokukumbusha?Tujuze basi.
Twende Sote sasa Safi hiyoooooo!!!!!!
"Swahili na Waswahili" Pamoja sana tuu.

Saturday 2 June 2012

Chaguo la Mswahili Leo-Tupo Burundi;Ndugu zangu wa Buyenzi Mpo?!!!!!

 Bibi na Bwana Billy.Hongereni sana Kwa kupata mtoto wa kiume.Mungu amlinde na kumkuza vyema.Nanyi awape hekima katika malezi yenu.Ngoja leo niwasogeze nyumbani.
 

Waungwana "CHAGUO LA MSWAHLI LEO" Nimewapeleka BURUNDI.
Haya umeona waRundi waishio CANADA wanavyofunza watoto wao Utamaduni wao?Jee wewe unaonaje kuhusu hili la kuwafundisha watoto mambo yakwenu?

Jee unao wakati wa kuwafundisha watoto hata Kibuzi,Kinyunyu,Ukuti,Rede,Nyimbo hata zile za Mchakamchaka?Au Muda hautoshi?

Nakumbuka kama wikimbili 2 tulikutana Waswahili kwenye Mnuso Mmoja hivi, Baada ya Kushiba Tukaanza kuimba hii Nyimbo.

Alisemaaa  Alisemaaa,Alisema Nyerere Alisema,Vijana wangu wote Mmeleegea, Sharti Tuanze Mchaka Mchaka.................Hahahahaa

 Swahili na Waswahili Waungwana.

 Kama unalolote utahitaji kuwajuza wenzio. Tutumie Kupitia Email.rasca@hotmail.co.uk.Pamoja sana!!!!!!

Saturday 19 May 2012

Chaguo la Mswahili Leo;Celine&R.kelly- I'm Your Angel, The Step in the Name of Love. Na nyingineee!!!



 Waungwana Nawatakia j'Mosi yenye Amani na Furaha daima!!.
Leo ngoja Tuangalie/twende Pande hii.
 Sina Mengi Zaidi Nakusikiliza wewe tuu.Baada ya Burudani, Umekumbuka nini,Umeguswa,Umefurahi,Umenuna au? "Swahili na Waswahili" Pamoja sana

Saturday 12 May 2012

Chaguo la Mswahili Leo;Kutoka kwa Familia ya Penza.Burudani;Diamond - Moyo wangu,Mbagala,Mawazo!!!!!



Diamond na Chance
Diamond na da'Phoibe[Mwana Penza]
Waungwana Leo sipo mbaali sana,yaani si za Kale,Kijana anabamba/anafanya vyema katika Kazi yake, au vipi.
Jee wewe Muungwana Kijana Almasi anakubamba/unapenda kazi yake?Zaidi ni Sauti,Maneno,Muonekano,Uchezaji, Manjonjooo kama si Vionjooo?

Twende Sootee sasaaa, Moyo Wanguuu ooh Moyo wanguuu oooohhh.....Makuti na Mkoleeeeee duuhh mpaka Mkoleeeee!!

Pamoja sana na muwe na J'Mosi njema!!!!!!

Friday 27 April 2012

Chaguo la Mswahili Leo-Sweet Mother ,Wagadu Gu,Colombia,!!!!!!!!



Wakaka na Karikiti!!!!
Haya Waungwa, yakale ni Dhahabu Waswahili wanasema au?
Kuna lolote unakumbuka hapa?


Inavuka soxxxx kinabakia kiatuuuu.
Muwe na wakati mwema!!!!!!!!

Saturday 21 April 2012

Chaguo la Mswahili Leo;Professor Jay -Anasema- hapo vipi?kama Ipo,Ndiyo Mzee!!!!!!!

Nawatakia J'Mosi Njema yenye Amani,Upendo,Uvumilivu na Umoja!!!
Burudani na Maneno muruwaaa kutoka kwake Mswahili Professor Jay-Msikilize kwa makini.NDIYO MZEE!!.
Pamoja Sana, Hapo Vipi?

Friday 13 April 2012

Chaguo la Mswahili Leo;Swahili Taarab Bi Malika - Sitaki sitaki na Vidonge,Isaa Matona-Msumeno!!

Waungwana Mwajionaje na Khariiii?Teheheheeheh .Nimatumaini yangu woote wazima,Leo nimewaletea Taarab za Zamani kidogo,Hizi Taarab hasa hizi za Zamani zinamafumbo sana, yaani kunamaneno mengine unaweza usiyaelewe anamaanisha nini.
Jee wewe ni mpenzi wa Taarab au huwa unasikiliza/kuangalia au kucheza?
Unaona tofauti gani kati ya Taarab za Zamani na sasa na jee Unafikiri Taarab za Zamani Zinamvuto zaidi ya sasa au Za Sasa Zinamvuto kuliko za Zamani?
Karibuni sana kama hujahi kuzisikia Leo jaribu, na Wapenzi wa Taarab Jimwageni Uwanjani au...Swahili na Waswahili.Pamoja sana tuu!!!!!

Saturday 31 March 2012

Chaguo la Mswahili Leo,mambo ya Taarab-Utalijua Jiji!

Haya Waungwana mambo hayo, hahaaaa Mambo ya Taarab... Swahili na Waswahili twende Sote sasa!!

Saturday 17 March 2012

Chaguo la Mswahili Leo-Congo - Pepe Kalle!!!!!!!

Nawatakieni J'mosi njema!Kumbuka Enzi zako, hahah wapi dada Mwasu KLM, my Wifi Neema Nyanyile, Mama Kisa na da' Nana Msilie wapendwa wangu,Enzi hairudi ikipita imepita, kumbukumbu ipo lakini..Waungwana nini Mnakumbuka kukisiliza nyimbo hizi?.Twende sote sasa Anakala Manzeeeeee!!!!!!!!.Pamoja sana.

Saturday 10 March 2012

Wanawake na Mitindo-da'Levina na Rafiki zake!! Chaguo la Mswahili-Yvonne Chaka - Mamaland na Umgombothi


                                         Da'Levina[Aliye shika kiuno] na Rafiki katika poziii
                                         Dadazzz mmependeza mnoo,Asanteni sana  kwa kutuwakilisha.Siku ya Wanawake ,Wao walijumuika na wenzao kwa Shamim.Duuhh kivazi cha kanga kikitengenezwa, kinapendeza haswaaa.Wanawatakia Wanawake Woote Duniani ,Baraka, Amani,Upendo na Umoja.WANAWAKE JUU!!!