Swahili na Waswahili

Swahili na Waswahili
Waswahili na Mswahili Rachel Siwa...Pamoja Daima!!

Friday 21 December 2018

Kikombe Cha Asubuhi ;Zaburi 22...



Shalom,Habari za Asubuhi,Hamjambo,Mmeamkaje?

Tumshukuru Mungu katika yote....

Mungu wetu Baba yetu,Muumba wetu Muumba wa Mbingu na Nchi
Muumba wa vyote vilivyomo vinavyoonekana na visivyoonekana
Mungu wa walio hai,Mungu  mwenye huruma,Mungu wa upendo
Mungu wa Abrahamu,Isaka na Yakobo...
Asante kwa wema na fadhili zako kwetu
Asante kwa ulinzi wako kwetu wakati wote
Asante kwa kutuchagua tena na kutupa
kibali cha kuendelea kuiona leo hii
Asante kwa pumzi/uzima,afya na kuwatayari kwa majukumu yetu

Neema yako yatutosha ee Mungu wetu....!!


Basi ndugu, jihadharini asije akawako yeyote miongoni mwenu aliye na moyo mbaya hivyo na asiyeamini hata kujitenga na Mungu aliye hai. Maadamu hiyo “Leo” inayosemwa katika Maandiko bado inatuhusu sisi, mnapaswa kusaidiana daima, ili mtu yeyote miongoni mwenu asidanganywe na dhambi na kuwa mkaidi.

Baba wa Mbinguni tunakuja mbele zako tukijinyenyekeza,tukijishusha na kujiachilia mikononi mwako
Mungu wetu tunaomba utusamehe dhambi zetu zote tulizo zifanya
Kwakuwaza,kwakunena,kwakutenda,kwakujua/kutojua
Baba wa Mbinguni nasi tunaomba ukatupe neema
ya kuweza kuwasamehe wale wote waliotukosea
Usitutie majaribu Mungu wetu tunaomba utuepushe
na yule mwovu na kazi zake zote
Jehovah ututakase miili yetu na akili zetu
Baba wa Mbinguni tunaomba utufunike kwa Damu
ya Bwana na Mwokozi wetu Yesu Kristo wa Nazareti
yeye aliteseka kwanza ili sisi tupate kupona....

Maana sisi tunashirikiana na Kristo ikiwa tutazingatia kwa uthabiti tumaini tulilokuwa nalo mwanzoni. Maandiko yasema hivi: “Kama mkisikia sauti yake leo, msiwe wakaidi kama wakati ule waliponiasi.” Ni akina nani waliosikia sauti ya Mungu wakamwasi? Ni wale wote walioongozwa na Mose kutoka Misri.

Mungu wetu tunaomba ukabariki kazi za mikono yetu
Baba wa Mbinguni tunaomba ukatupe ubunifu na maarifa katika utendaji

Jehovah nasi tukatende sawasawa na mapenzi yako
Yahweh tunaomba ukabariki ridhiki zetu ziingiazo/zitokazo
Mungu wetu nasi tunaomba ukatupe neema ya kuweza
kuwabariki wenye kuhitaji
Tusipungukiwe katika mahitaji yetu Baba wa Mbinguni
tunaomba ukatupe kama inavyokupendeza wewe....



Yahweh  tunayaweka maisha yetu mikononi mwako
Mungu wetu tunaomba ukabariki nyumba/ndoa zetu,
watoto,wazazi wetu,familia/ndugu na wote wanaotuzunguka
Jehovah tunaomba ulinzi wako kwetu na kwa vyote tunavyo vimiliki
Yahweh tunaomba ukatubariki tuingiapo/tutokapo
Mungu wetu tunaomba ukavibariki vyote tunavyoenda kugusa/kutumia
Baba wa Mbinguni ukavitakase kwa Damu ya Bwana wetu Yesu Kristo
Mungu wetu ukatamalaki na kutuatamia
Baba wa Mbinguni tukawe salama rohoni

Yahweh ukatupe akili ya kutambua mema na mabaya
Mfalme wa amani amani yako ikatawale katika maisha yetu
Mungu wetu ukatupe macho ya kuona na masikio ya kusikia 
sauti yako na kuitii
Baba wa Mbinguni tunaomba ukatupe neema ya kufuata njia zako
Yahweh tukasimamie Neno lako amri na sheria zako siku zote 
za maisha yetu
Mungu wetu ukaonekane katika maisha yetu
Baba wa Mbinguni tukanene yaliyo yako
Neema zako zikawe nasi Nuru yako ikaangaze katika maisha yetu
ukatuguse kwa mkono wako wenye nguvu
Ukatufanye chombo chema ee Mungu wetu nasi tukatumike kama
inavyokupendeza wewe
Roho Mtakatifu akatuongoze katika yote na tukawe na kiasi....

Mungu aliwakasirikia akina nani kwa miaka arubaini? Aliwakasirikia wale waliotenda dhambi, maiti zao zikatapakaa kule jangwani. Mungu alipoapa: “Hawataingia mahali pangu pa pumziko,” alikuwa anawasema akina nani? Alikuwa anasema juu ya hao walioasi. Basi, twaona kwamba hawakuingia huko kwa sababu hawakuamini.

Tazama watoto wako wanaokutafuta/kukuomba kwa bidii na imani, Mungu wetu tunawaweka mikononi mwako wenye shida/tabu,
wote wanaopitia magumu/majaribu mbalimbali
Mungu wetu tunaomba ukawaguse kwa mkono wako wenye nguvu
kila mmoja na mahitaji yake
Baba wa Mbinguni tunaomba ukaonekane katika maisha yao
Mungu wetu tunaomba ukawasamehe pale walipokwenda
kinyume nawe Yahweh tunaomba ukawape neema ya kujiombea
Kufuata njia zako nazo zikawaweke huru
Ukawape macho ya rohoni ee Mungu wetu na masikio ya kusikia
sauti yako,Ukawaokoe na kuwalinda,ukawaponye kimwili na kiroho
Nuru yako ikaangaze katika maisha yao,Amani ikatawale katika maisha yao,Upendo ukadumu kati yao

Baba wa Mbinguni tunayaweka haya yote mikononi mikononi mwako,Kwakuwa Ufalme ni wako Nguvu na Utukufu hata Milele 
Amina!!
Asanteni sana wapendwa katika Kristo Yesu kwakuwa nami,Mungu Baba aendelee kuwatendea sawasawa na mapezni yake
Nawapenda.


Kilio
(Kwa Mwimbishaji: Mtindo wa utenzi wa kulungu wa alfajiri. Zaburi ya Daudi)
1 Taz Mat 27:46; Marko 15:34 Mungu wangu, Mungu wangu, mbona umeniacha?
Mbona uko mbali sana kunisaidia,
mbali na maneno ya kilio changu?
2Ee Mungu wangu, nalia mchana lakini hujibu;
napiga yowe usiku, lakini nafuu sipati.
3Hata hivyo, wewe ni mtakatifu;
wewe watawala na kusifiwa na Waisraeli.
4Wazee wetu walikutegemea;
walikutegemea, nawe ukawaokoa.
5Walikulilia wewe, wakaokolewa;
walikutegemea, nao hawakuaibika.
6Lakini mimi ni mdudu tu, wala si mtu;
nimepuuzwa na kudharauliwa na watu.
7 Taz Mat 27:39; Marko 15:29; Luka 23:35 Wote wanionao hunidhihaki;
hunifyonya na kutikisa vichwa vyao.
8 Taz Mat 27:43 Husema: “Alimtegemea Mwenyezi-Mungu,
basi, Mungu na amkomboe!
Kama Mungu anapendezwa naye,
basi, na amwokoe!”
9Lakini ndiwe uliyenitoa tumboni mwa mama yangu,
uliniweka salama kifuani pa mama yangu.
10Nimekutegemea tangu kuzaliwa kwangu.
Tangu nilipozaliwa wewe umekuwa Mungu wangu.
11Usikae mbali nami, kwani taabu imekaribia;
wala hakuna wa kunisaidia.
12Maadui wengi wanizunguka kama fahali;
wamenisonga kama fahali wakali wa Bashani!
13Wanafunua vinywa vyao kama simba,
tayari kushambulia na kurarua.
14Nimekwisha kama maji yaliyomwagika;
mifupa yangu yote imeteguka;
moyo wangu ni kama nta,
unayeyuka ndani mwangu.
15Koo22:15 Koo: Au Nguvu. langu limekauka kama kigae;
ulimi wangu wanata kinywani mwangu.
Umeniacha kwenye mavumbi ya kifo.
16Genge la waovu limenizunguka;
wananizingira kama kundi la mbwa;
wamenitoboa22:16 wamenitoboa: Baadhi ya hati za kale: Wamenifunga; Kiebrania: Kama simba. mikono na miguu.
17Nimebaki mifupa mitupu;
maadui zangu waniangalia na kunisimanga.
18 Taz Mat 27:15; Marko 15:24; Luka 23:34; Yoh 19:24 Wanagawana nguo zangu,
na kulipigia kura vazi langu.
19Lakini wewe ee Mwenyezi-Mungu, usikae mbali nami;
ewe msaada wangu, uje haraka kunisaidia.
20Iokoe nafsi yangu mbali na upanga,
yaokoe maisha yangu makuchani mwa mbwa hao!
21Uniokoe kinywani mwa simba;
iokoe nafsi yangu dhaifu22:21 nafsi yangu dhaifu: Kiebrania: Wewe umenisikiliza. toka pembe za nyati hao.
Wimbo wa shukrani
22 Taz Ebr 2:12 Nitawasimulia ndugu zangu matendo yako;
nitakusifu kati ya kusanyiko lao:
23Enyi mnaomcha Mwenyezi-Mungu, msifuni!
Mtukuzeni enyi wazawa wote wa Yakobo!
Mcheni Mungu enyi wazawa wote wa Israeli!
24Maana yeye hapuuzi au kudharau unyonge wa mnyonge;
wala hajifichi mbali naye,
ila humsikia anapomwomba msaada.
25Kwa sababu yako ninakusifu
katika kusanyiko kubwa la watu;
nitatimiza ahadi zangu mbele yao wakuchao.
26Maskini watakula na kushiba;
wanaomtafuta Mwenyezi-Mungu watamsifu.
Mungu awajalie kuishi milele!
27Ulimwengu wote utakumbuka na kumrudia Mwenyezi-Mungu;
jamaa zote za mataifa zitamwabudu.
28Maana Mwenyezi-Mungu ni mfalme;
yeye anayatawala mataifa.
29Wenye kiburi wote duniani watasujudu mbele yake;
wote ambao hufa watainama mbele yake,
wote ambao hawawezi kudumisha uhai wao.
30Vizazi vijavyo vitamtumikia;
watu watavisimulia habari za Mwenyezi-Mungu,
31watatangaza matendo yake ya wokovu.
Watu wasiozaliwa bado wataambiwa:
“Mwenyezi-Mungu ndiye aliyefanya hayo!”



Zaburi22;1-31

Biblia Habari Njema kwa Watu Wote(BHN)

"Swahili Na Waswahili"Mbarikiwe.

No comments: