Swahili na Waswahili

Swahili na Waswahili
Waswahili na Mswahili Rachel Siwa...Pamoja Daima!!

Monday 17 December 2018

Kikombe Cha Asubuhi ;Zaburi 18...

Shalom,Habari za Asubuhi,Hamjambo,Mmeamkaje?
Haleluyah ni siku/wiki  nyingine tena Mungu wetu ametuchagua

na kutupa kibali cha kuendelea kuiona leo hii
Si kwamba sisi tumetenda mema sana wala si kwa nguvu zetu
si kwa utashi wetu wala si kwa akili zetu si kwamba sisi
ni wazuri mno si kwa uwezo wetu sisi kuwa hivi tulivyo leo hii
Ni kwa rehema/neema zake ni kwa mapenzi yake Mungu wetu....

Tumshukuru Mungu wetu katika yote...

Asante Mungu wetu kwa wema na fadhili zako kwetu
Asante kwa ulinzi wako kwetu wakati wote
Asante kwa pumzi/uzima,afya na kuwa tayari kwa majukumu yetu
Sifa na Utukufu tunakurudshia Mungu wetu....!!

Yesu aliwaambia, “Msifadhaike mioyoni mwenu. Mwaminini Mungu, niaminini na mimi pia. Nyumbani mwa Baba yangu mna makao mengi; kama isingekuwa hivyo, ningalikwisha waambieni. Sasa nakwenda kuwatayarishieni nafasi. Na nikienda na kuwatayarishieni nafasi, nitarudi na kuwachukueni kwangu, ili nanyi muwe pale nilipo mimi. Mnajua njia ya kwenda huko ninakokwenda.”

Tazama jana imepita ee Mungu wetu leo ni siku mpya na kesho ni siku nyingine Jehovah tunakuja mbele zako tukijinyenyekeza,tukijishusha na kujiachilia mikononi mwako
 Mungu wetu tunaomba utusamehe dhambi zetu zote tulizozifanya kwakuwaza,kwakunena,kwakutenda,kwakujua/kutojua
Baba wa Mbinguni nasi tunaomba utupe neema ya kuweza kuwasamehe wale wote waliotukosea
Jehovah usitutie majaribu Mungu wetu tunaomba utuepushe na yule mwovu na kazi zake zote
Yahweh tunaomba ututakase miili yetu na akili zetu
Baba wa Mbinguni utufunike kwa Damu ya Bwana na Mwokozi wetu Yesu Kristo wa Nazareti
yeye aliteseka kwanza ili sisi tupate kupona
Kwakupigwa kwake sisi tumepata kupona...

Thoma akamwuliza, “Bwana, hatujui unakokwenda, tutawezaje basi, kuijua hiyo njia?” Yesu akamjibu, “Mimi ni njia, na ukweli na uhai. Hakuna awezaye kwenda kwa Baba ila kwa kupitia kwangu. Ikiwa mnanijua mimi, mnamjua na Baba yangu pia. Na tangu sasa, mnamjua, tena mmekwisha mwona.”
Yahweh tunaomba ukabariki kazi za mikono yetu
Baba wa Mbinguni tunaomba ukatupe ubunifu na maarifa 
katika utendaji
Jehovah nasi tukatende sawasawa na mapenzi yako
Baba wa Mbinguni tunaomba ukabariki ridhiki zetu
ziingiazo/zitokazo
Mungu wetu nasi tunaomba ukatupe neema ya kuweza
kuwabariki wenye kuhitaji
Yahweh tusipungukiwe katika mahitaji yetu
Mungu wetu ukatupe kama inavyokupendeza wewe

Baba wa Mbinguni tunayaweka maisha yetu mikononi mwako
Mungu wetu tunaomba ukabariki nyumba/ndoa zetu,
watoto,wazazi wetu,familia/ndugu na wote wanaotuzunguka
Jehovah tunaomba ulinzi wako kwetu na kwa vyote tunavyo vimiliki
Yahweh tunaomba ukatubariki tuingiapo/tutokapo
Mungu wetu tunaomba ukavibariki vyote tunavyoenda kugusa/kutumia
Baba wa Mbinguni ukavitakase kwa Damu ya Bwana wetu Yesu Kristo
Mungu wetu ukatamalaki na kutuatamia
Baba wa Mbinguni tukawe salama rohoni
Mfalme wa amani amani yako ikatawale katika maisha yetu
Mungu wetu ukatupe macho ya kuona na masikio ya kusikia 
sauti yako na kuitii
Baba wa Mbinguni tunaomba ukatupe neema ya kufuata njia zako
Yahweh tukasimamie Neno lako amri na sheria zako siku zote 
za maisha yetu
Mungu wetu ukaonekane katika maisha yetu
Neema zako zikawe nasi Nuru yako ikaangaze katika maisha yetu
ukatuguse kwa mkono wako wenye nguvu
Ukatufanye chombo chema ee Mungu wetu nasi tukatumike kama
inavyokupendeza wewe
Roho Mtakatifu akatuongoze katika yote na tukawe na kiasi...

Filipo akamwambia, “Bwana, tuoneshe Baba, nasi tutatosheka.” Yesu akamwambia, “Nimekaa nanyi muda wote huu, nawe Filipo hujanijua? Aliyekwisha niona mimi amemwona Baba. Unawezaje basi, kusema: ‘Tuoneshe Baba?’ Je, huamini kwamba mimi niko ndani ya Baba, naye Baba yuko ndani yangu? Maneno ninayowaambieni siyasemi kwa mamlaka yangu; Baba aliye ndani yangu anafanya kazi yake.

Mungu wetu tunawaweka mikononi mwako wenye shida/tabu,wote wanaopotia magumu/majaribu mbalimbali
watoto wako wanaokuomba kwa bidii na imani
Mungu wetu tunaomba ukawaguse kwa mkono wako wenye nguvu
 kila mmoja na mahitaji yake 
Yahweh tunaomba ukaonekane katika maisha yao
Jehovah tunaomba ukawaokoe,ukawavushe salama na  kuwalinda
Mungu wetu tunaomba ukawasamehe pale walipokwenda kinyume nawe
Baba wa Mbinguni ukawape neema ya kujiombea,kufuata njia zako
wakasimaie Neno lako nalo likaweke huru
Mungu wetu tunaomba ukasikie kuomba kwetu
Baba wa Mbinguni ukapokee sala/maombi yetu
Mungu wetu ukawatendee sawasawa na mapenzi yako
Kwakuwa Ufalme ni wako Nguvu na Utukufu hata Milele
Amina...!!

Asanteni sana wapendwa katika Kristo Yesu kwakuwa nami
Mungu Baba aendelee kuwabariki na kuwatendea 
kama inavyompendeza yeye....
Nawapenda.


Utenzi wa ushindi
(Kwa Mwimbishaji. Zaburi ya Daudi, mtumishi wa Mungu, aliyomwimbia Mungu wakati alipomwokoa mkononi mwa Shauli na adui wengine)
1Nakupenda, ee Mwenyezi-Mungu, nguvu yangu!
2Mwenyezi-Mungu ni mwamba wangu,
ngome yangu na mkombozi wangu;
Mungu wangu, mwamba wangu ninayemkimbilia usalama;
ngao yangu, nguvu za wokovu wangu na ngome yangu.
3Namwita Mwenyezi-Mungu astahiliye sifa anisaidie,
nami naokolewa kutoka kwa maadui zangu.
4Kamba za kifo zilinizingira,
mawimbi ya maangamizi yalinivamia;
5kamba za kuzimu zilinizinga,
mitego ya kifo ilinikabili.
6Katika taabu yangu nilimwita Mwenyezi-Mungu,
nilimlilia Mungu wangu anisaidie.
Aliisikia sauti yangu hekaluni mwake;
kilio changu kilimfikia masikioni mwake.
7Hapo dunia ikatetemeka na kutikisika;
misingi ya milima ikayumbayumba,
kwani Mungu alikuwa amekasirika.
8Moshi ulifuka kutoka puani mwake,
moto uunguzao ukatoka kinywani mwake;
makaa ya moto yalilipuka kutoka kwake.
9Aliinamisha anga, akashuka chini;
na wingu jeusi chini ya miguu yake.
10Alipanda kiumbe chenye mabawa18:10 kiumbe chenye mabawa: Kiebrania: Kerubi. akaruka;
akapaa kasi juu ya mabawa ya upepo.
11Alijifunika giza pande zote,
mawingu mazito yaliyojaa maji yalimzunguka.
12Umeme ulimulika mbele yake;
kukatokea mawinguni mvua ya mawe na makaa ya moto.
13Mwenyezi-Mungu alinguruma kutoka mbinguni;
Mungu Mkuu akatoa sauti yake,
kukatokea mvua ya mawe na makaa ya moto.
14Aliwapiga maadui mishale yake, akawatawanya,
alirusha umeme, akawatimua.
15Ulipowakemea maadui zako ee Mwenyezi-Mungu,
ulipowatisha kwa ghadhabu yako,
vilindi vya bahari vilifunuliwa,
misingi ya dunia ikaonekana.
16Mungu alinyosha mkono kutoka juu akanichukua,
kutoka katika maji mengi alininyanyua.
17Aliniokoa kutoka kwa maadui zangu wenye nguvu nyingi,
aliniokoa kutoka kwa hao walionichukia,
maana walikuwa na nguvu kunishinda.
18Walinivamia nilipokuwa taabuni,
lakini Mwenyezi-Mungu alikuwa kinga yangu.
19Alinileta, akaniweka mahali pa usalama;
alinisalimisha, kwani alipendezwa nami.
20Mwenyezi-Mungu alinipa tuzo kadiri ya uadilifu wangu;
alinituza kwa vile mikono yangu haina hatia.
21Maana nimefuata njia za Mwenyezi-Mungu,
wala sikujitenga na Mungu wangu kwa uovu.
22Nimeshika maagizo yake yote,
sikuacha kufuata masharti yake.
23Mbele yake sikuwa na hatia;
nimejikinga nisiwe na hatia.
24Mwenyezi-Mungu amenituza kadiri ya uadilifu wangu;
yeye ajua kwamba mikono yangu haina hatia.
25Wewe ni mwaminifu kwa walio waaminifu;
mwema kwa wale walio wema.
26Wewe ni mkamilifu kwa walio wakamilifu;
lakini mkatili kwa watu walio waovu.
27Wewe wawaokoa walio wanyenyekevu,
lakini wenye majivuno huwaporomosha.
28Wewe ee Mwenyezi-Mungu, waniangazia;
walifukuza giza langu, ee Mwenyezi-Mungu, Mungu wangu.
29Kwa msaada wako nakishambulia kikosi;
wewe wanipa nguvu ya kuruka ukuta.
30Huyu Mungu matendo yake hayana dosari!
Ahadi ya Mwenyezi-Mungu ni ya kuaminika;
yeye ni ngao kwa wote wanaomkimbilia usalama.
31Nani aliye Mungu isipokuwa Mwenyezi-Mungu?
Nani aliye mwamba wa usalama ila Mungu wetu?
32Mungu ndiye anijaliaye nguvu kila upande;
ndiye anayeifanya salama njia yangu.
33Ameiimarisha miguu yangu kama ya paa,
na kuniweka salama juu ya vilele.
34Hunifunza kupigana vita,
mikono yangu iweze kuvuta upinde wa shaba.
35Umenipa ngao yako ya kuniokoa;
mkono wako wa kulia umenitegemeza;
wema wako umenifanikisha.
36Umenirahisishia njia yangu;
wala miguu yangu haikuteleza.
37Niliwafuatia adui zangu na kuwakamata;
sikurudi nyuma mpaka nimewaangamiza.
38Niliwaangusha chini wasiweze kuinuka tena;
walianguka chini ya miguu yangu.
39Wewe ulinijalia nguvu ya kupigana vita;
uliwaporomosha maadui chini yangu.
40Uliwafanya maadui zangu wakimbie,
na wale walionichukia niliwaangamiza.
41Walipiga yowe lakini hapakuwa na wa kuwaokoa;
walimlilia Mwenyezi-Mungu lakini hakuwajibu.
42Niliwatwanga wakawa kama vumbi inayopeperushwa na upepo;
niliwakanyaga18:42 niliwakanyaga: Kiebrania: Niliwatupa nje. kama tope la njiani.
43Wewe uliniokoa na mashambulizi ya watu,
ukanifanya mtawala wa mataifa.
Watu nisiowajua walinitumikia.
44Mara waliposikia habari zangu walinitii.
Wageni walinijia wakinyenyekea.
45Wageni walikufa moyo;
wakaja kutoka ngome zao wakitetemeka.
46Mwenyezi-Mungu yu hai!
Asifiwe mwamba wa usalama wangu;
atukuzwe Mungu wa wokovu wangu.
47Yeye ameniwezesha kulipiza kisasi;
na kuyashinda mataifa chini yangu.
48Ameniokoa kutoka kwa maadui zangu,
akanikuza juu ya wapinzani wangu,
na kunisalimisha mbali na watu wakatili.
49 Taz Rom 15:9 Kwa hiyo nitakutukuza kati ya mataifa,
ee Mwenyezi-Mungu nitaliimbia sifa jina lako.
50Mungu humjalia mfalme wake ushindi mkubwa;
humwonesha fadhili zake huyo mteule wake,
naam, humfadhili Daudi na wazawa wake milele.


Zaburi18;1-50

Biblia Habari Njema kwa Watu Wote(BHN)

"Swahili Na Waswahili"Mbarikiwe.

No comments: