Swahili na Waswahili

Swahili na Waswahili
Waswahili na Mswahili Rachel Siwa...Pamoja Daima!!

Saturday 9 November 2013

[AUDIO] DAKIKA 90 ZA DUNIA: Athari za vita baada ya kumalizika mapigano‏


Wakati vita ya Congo
ikionekana kuelekea ukingoni, bado tunakumbushwa kuwa athari za vita
katika nchi mbalimbali huendelea kuwaathiri wahusika na hasa wananchi wa
nchi hizo kwa miaka mingi baada ya kumalizika kwa vita hivyo.

Baadhi
ya athari huwa wazi sana. Mfano ni majengo yaliyoharibika wakati wa
mapigano, watu wanaouawa wakati wa mapigano na hata uchumi unaozorota
kutokana na watu kutofanya kazi wakati wa mapigano hayo.

Lakini pia kuna athari ambazo hazionekani ama kutopewa kipaumbele machoni mwa watu wengi baada ya vita hivyo.

Hivi karibuni, waMarekani wamekumbushwa kuhusu hili

Hii
ni sehemu ya ripoti ya Jamii Production kwenye kipindi cha DAKIKA 90 ZA
DUNIA kinachorushwa na kituo cha Radio cha Capital FM cha Dar Es Salaam
Tanzania kila Jumamosi kuanzia saa moja na nusu asubuhi (7:30 AM).



Bahati Alex (L) Capital Radio Jijini Dar es Salaam na Mubelwa Bandio (R) wa Jamii Production Washington DC
Hii ilikuwa ripoti ya Novemba 9, 2013



*JAMII PRODUCTION*
"Usahihi wa fikra ndio fikra sahihi"

No comments: