Swahili na Waswahili

Swahili na Waswahili
Waswahili na Mswahili Rachel Siwa...Pamoja Daima!!

Tuesday 18 February 2020

Kikombe Cha Asubuhi; Maombolezo 5....


Shalom,Habari za Asubuhi,Hamjambo,Mmeamkaje?

Tumshukuru Mungu wetu katika yote...

Asante  Mungu wetu kwa wema na fadhili zako kwetu
Asante kwa ulinzi wako kwetu wakati wote
Asante kwa kutuchagua tena na kutupa
kibali cha kuendelea kuiona leo hii
Asante kwa pumzi/uzima,afya na kuwatayari kwa majukumu yetu


Utukuzwe ee Mungu wetu,usifiwe Baba wa Mbinguni

Neema yako yatutosha  Mungu wetu..!

Basi, Yesu akawauliza, “Je, nyinyi hamwelewi mfano huu? Mtawezaje basi, kuelewa mfano wowote? Mpanzi hupanda neno la Mungu. Watu wengine ni kama walio njiani ambapo neno lilipandwa. Lakini mara tu baada ya kulisikia, Shetani huja na kuliondoa neno hilo lililopandwa ndani yao.
Baba wa Mbinguni tunakuja mbele zako tukijinyenyekeza,
tukijishusha na kujiachilia mikononi mwako

Mungu wetu tunaomba utusamehe dhambi zetu zote
Baba wa Mbinguni nasi tunaomba utupe neema ya kuweza kuwasamehe wale wote waliotukosea,Usitutie majaribuni Mungu wetu tunaomba utuepushe na yule mwovu na kazi zake zote,Jehovah ututakase miili yetu na akili zetu Baba wa Mbinguni tunaomba utufunike kwa  Damu ya Bwana na Mwokozi wetu Yesu Kristo wa Nazareti,
Yeye aliteseka kwanza ili sisi tupate kupona....


Watu wengine ni kama zile mbegu zilizopandwa penye mawe. Mara tu walisikiapo hilo neno hulipokea kwa furaha. Lakini haliwaingii na kuwa na mizizi ndani yao; huendelea kulizingatia kwa kitambo tu, na wakati taabu au udhalimu vinapotokea kwa sababu ya hilo neno, mara wanakata tamaa. Watu wengine ni kama zile mbegu zilizoanguka penye miti ya miiba. Huo ni mfano wa wale wanaosikia hilo neno,
Mungu wetu tunaomba ukabariki kazi za mikono yetu
Baba wa Mbinguni tunaomba ukatupe ubunifu na maarifa 
katika utendaji
Jehovah nasi tukatende sawasawa na mapenzi yako
Baba wa Mbinguni tunaomba ukabariki ridhiki zetu
ziingiazo/zitokazo
Mungu wetu nasi tunaomba ukatupe neema ya kuweza
kuwabariki wenye kuhitaji
Yahweh tusipungukiwe katika mahitaji yetu
Mungu wetu ukatupe kama inavyokupendeza wewe



Jehovah tunayaweka maisha yetu mikononi mwako
Baba wa Mbinguni tunaomba ukabariki nyumba/ndoa zetu,
watoto,wazazi wetu,familia/ndugu na wote wanaotuzunguka
Jehovah tunaomba ulinzi wako kwetu na kwa vyote tunavyo vimiliki
Yahweh tunaomba ukatubariki tuingiapo/tutokapo
Mungu wetu tunaomba ukavibariki vyote tunavyoenda kugusa/kutumia
Baba wa Mbinguni ukavitakase kwa Damu ya Bwana wetu Yesu Kristo
Mungu wetu ukatamalaki na kutuatamia
Baba wa Mbinguni tukawe salama rohoni
Mfalme wa amani amani yako ikatawale katika maisha yetu
Mungu wetu ukatupe macho ya kuona na masikio ya kusikia 
sauti yako na kuitii
Baba wa Mbinguni tunaomba ukatupe neema ya kufuata njia zako
Yahweh tukasimamie Neno lako amri na sheria zako siku zote 
za maisha yetu

Mungu  wetu ukaonekane katika maisha yetu popote tupitapo na ikajulikane kwamba upo 

Neema zako zikawe nasi Nuru yako ikaangaze katika maisha yetu
Ukatufanye barua njema ee Mungu wetu nasi tukasomeke kama
inavyokupendeza wewe
Roho Mtakatifu akatuongoze katika yote na tukawe na kiasi...


lakini wasiwasi wa ulimwengu huu, anasa za mali na tamaa za kila namna huwaingia na kulisonga hilo neno, nao hawazai matunda. Lakini wengine ni kama zile mbegu zilizopandwa katika udongo mzuri. Hawa hulisikia hilo neno, wakalipokea, wakazaa matunda: Wengine thelathini, wengine sitini na wengine mia.”
Tazama wenye shida/tabu,Mungu wetu tunaomba
 ukawaguse kila mmoja na mahitaji yake
Baba wa Mbinguni tunaomba ukawasamehe pale walipokwenda
kinyume nawe
Mungu wetu ukawape neema ya kujiombea,macho ya rohoni,masikio yakusikia sauti yako,wakafuate njia zako nazo zikawaweke huru
Mungu wetu tunaomba ukasikie kulia kwao
Baba wa Mbinguni tunomba ukawafute machozi yao
Nuru yako ikaangaze katika maisha yao
Mungu wetu tunaomba ukawatendee sawasawa na mapenzi yako
Kwakuwa Ufalme ni wako Nguvu na Utukufu hata Milele
Amina....!!!


Wapendwa katika Kristo Yesu asanteni sana
kwakuwanami/kunisoma

Mungu Baba aendelee kuwabariki na kuwatendea
kama inavyompendeza yeye
Amani ya Bwana wetu Yesu Kristo na upendo wa Mungu Baba
ukae nanyi daima....

Nawapenda.

Kuomba huruma
1Ukumbuke ee Mwenyezi-Mungu, mambo yaliyotupata!
Utuangalie, uone jinsi tulivyoaibishwa!
2Nchi yetu imekabidhiwa wageni,
nyumba zetu watu wengine.
3Tumekuwa yatima, bila baba,
mama zetu wameachwa kama wajane.
4Maji yetu tunayapata kwa fedha,
kuni zetu kwa kuzinunua.
5Tunalazimishwa kufanya kazi kama punda,
tumechoka lakini haturuhusiwi kupumzika.
6Wamisri na Waashuru tumewanyoshea mikono,
ili tupate chakula cha kutosha.
7Wazee wetu walitenda dhambi na hawapo tena;
nasi tunateseka kwa sababu ya makosa yao.
8Watumwa ndio wanaotutawala,
wala hakuna wa kutuokoa mikononi mwao.
9Chakula chetu twapata kwa kuhatarisha maisha yetu,
maana wauaji wanazurura huko mashambani.
10Ngozi zetu zawaka moto kama tanuri
kwa sababu ya njaa inayotuchoma.
11Wanawake wetu wanashikwa kwa nguvu mjini Siyoni,
binti zetu katika vijiji vya Yuda.
12Wakuu wetu wametungikwa kwa mikono yao;
wazee wetu hawapewi heshima yoyote.
13Vijana wanalazimishwa kusaga nafaka kwa mawe,
wavulana wanayumbayumba kwa mizigo ya kuni.
14Wazee wameacha kutoa mashauri yao,
vijana wameacha kuimba.
15Furaha ya mioyo yetu imetoweka,
ngoma zetu zimegeuzwa kuwa ombolezo.
16Fahari tuliyojivunia imetokomea.
Ole wetu kwa kuwa tumetenda dhambi!
17Kwa ajili hiyo tumeugua moyoni,
kwa mambo hayo macho yetu yamefifia.
18Maana mlima Siyoni umeachwa tupu,
mbweha wanazurura humo.
19Lakini wewe Mwenyezi-Mungu watawala milele,
utawala wako wadumu vizazi vyote.
20Mbona umetuacha muda mrefu hivyo?
Mbona umetutupa siku nyingi hivyo?
21Uturekebishe ee Mwenyezi-Mungu, nasi tukurudie,
uturudishie fahari yetu kama zamani.
22Au, je, umetukataa kabisa?
Je, umetukasirikia mno?


Maombolezo5;1-22

Biblia Habari Njema kwa Watu Wote(BHN)

"Swahili Na Waswahili"Mbarikiwe.

Monday 17 February 2020

Kikombe Cha Asubuhi; Maombolezo 4....


Shalom,Habari za Asubuhi,Hamjambo,Mmeamkaje?

Haleluyah ni siku/wiki nyingine tena Mungu wetu ametuchagua

na kutupa kibali cha kuendelea kuiona leo hii
Si kwamba sisi tumetenda mema sana wala si kwa nguvu zetu
si kwa utashi wetu wala si kwa akili zetu si kwamba sisi
ni wazuri mno si kwa uwezo wetu sisi kuwa hivi tulivyo leo hii
Ni kwa rehema/neema zake ni kwa mapenzi yake Mungu wetu....

Tumshukuru Mungu wetu katika yote...

Asante Mungu wetu kwa wema na fadhili zako kwetu

Asante kwa ulinzi wako kwetu wakati wote
Asante kwa pumzi/uzima,afya na kuwa tayari kwa majukumu yetu
Sifa na Utukufu tunakurudshia Mungu wetu....!!


Yesu alipokuwa peke yake, baadhi ya wale waliomsikia walimwendea pamoja na wale kumi na wawili, wakamwuliza juu ya hiyo mifano.
Tazama jana imepita ee Mungu wetu leo ni siku mpya na kesho ni siku nyingine Jehovah tunakuja mbele zako tukijinyenyekeza,tukijishusha na kujiachilia mikononi mwako
 Mungu wetu tunaomba utusamehe dhambi zetu zote tulizozifanya kwakuwaza,kwakunena,kwakutenda,kwakujua/kutojua
Baba wa Mbinguni nasi tunaomba utupe neema ya kuweza kuwasamehe wale wote waliotukosea
Jehovah usitutie majaribu Mungu wetu tunaomba utuepushe na yule mwovu na kazi zake zote
Yahweh tunaomba ututakase miili yetu na akili zetu
Baba wa Mbinguni utufunike kwa Damu ya Bwana na Mwokozi wetu Yesu Kristo wa Nazareti
yeye aliteseka kwanza ili sisi tupate kupona
Kwakupigwa kwake sisi tumepata kupona....

Naye akawaambia, “Nyinyi mmejaliwa kujua siri ya ufalme wa Mungu, lakini wale walio nje wataambiwa kila kitu kwa mifano,
Yahweh tunaomba ukabariki kazi za mikono yetu
Baba wa Mbinguni tunaomba ukatupe ubunifu na maarifa 
katika utendaji
Jehovah nasi tukatende sawasawa na mapenzi yako
Baba wa Mbinguni tunaomba ukabariki ridhiki zetu
ziingiazo/zitokazo
Mungu wetu nasi tunaomba ukatupe neema ya kuweza
kuwabariki wenye kuhitaji
Yahweh tusipungukiwe katika mahitaji yetu
Mungu wetu ukatupe kama inavyokupendeza wewe

Baba wa Mbinguni tunayaweka maisha yetu mikononi mwako
Mungu wetu tunaomba ukabariki nyumba/ndoa zetu,
watoto,wazazi wetu,familia/ndugu na wote wanaotuzunguka
Jehovah tunaomba ulinzi wako kwetu na kwa vyote tunavyo vimiliki
Yahweh tunaomba ukatubariki tuingiapo/tutokapo
Mungu wetu tunaomba ukavibariki vyote tunavyoenda kugusa/kutumia
Baba wa Mbinguni ukavitakase kwa Damu ya Bwana wetu Yesu Kristo
Mungu wetu ukatamalaki na kutuatamia
Baba wa Mbinguni tukawe salama rohoni
Mfalme wa amani amani yako ikatawale katika maisha yetu
Mungu wetu ukatupe macho ya kuona na masikio ya kusikia 
sauti yako na kuitii
Baba wa Mbinguni tunaomba ukatupe neema ya kufuata njia zako
Yahweh tukasimamie Neno lako amri na sheria zako siku zote 
za maisha yetu
Mungu wetu ukaonekane katika maisha yetu
Neema zako zikawe nasi Nuru yako ikaangaze katika maisha yetu
ukatuguse kwa mkono wako wenye nguvu
Ukatufanye chombo chema ee Mungu wetu nasi tukatumike kama
inavyokupendeza wewe
Roho Mtakatifu akatuongoze katika yote na tukawe na kiasi...


ili, ‘Watazame kweli, lakini wasione. Wasikie kweli, lakini wasielewe. La sivyo, wangemgeukia Mungu, naye angewasamehe.’”
Mungu wetu tunawaweka mikononi mwako wenye shida/tabu,wote wanaopitia magumu/majaribu mbalimbali
Mungu wetu tunaomba ukawaguse kwa mkono wako wenye nguvu
 kila mmoja na mahitaji yake 
Mungu wetu tunaomba ukawasamehe pale walipokwenda kinyume nawe
Baba wa Mbinguni ukawape neema ya kujiombea,kufuata njia zako
wakasimamie Neno lako nalo likaweke huru
Mungu wetu tunaomba ukasikie kuomba kwetu
Mungu wetu ukawatendee sawasawa na mapenzi yako
Kwakuwa Ufalme ni wako Nguvu na Utukufu hata Milele
Amina...!!

Asanteni sana wapendwa katika Kristo Yesu kwakuwa nami
Mungu Baba aendelee kuwabariki na kuwatendea 
kama inavyompendeza yeye....
Nawapenda.


Yerusalemu baada ya kuangamia
1Jinsi gani dhahabu yetu ilivyochujuka,
dhahabu safi kabisa ilivyobadilika!
Mawe ya thamani yametawanywa
yamesambaa barabarani kote.
2Watoto wa Siyoni waliosifika sana,
waliothaminiwa kama dhahabu safi,
jinsi gani sasa wamekuwa kama vyombo vya udongo,
kazi ya mikono ya mfinyanzi!
3Hata mbwamwitu huwa na hisia za mama
na kuwanyonyesha watoto wao;
lakini watu wangu wamekuwa wakatili,
hufanya kama mbuni nyikani.
4Midomo ya watoto wachanga imekauka kwa kiu,
watoto wanaomba chakula lakini hakuna anayewapa.
5Watu waliojilisha vyakula vinono
sasa wanakufa njaa barabarani.
Waliolelewa na kuvikwa kifalme
sasa wanafukua kwa mikono kwenye majaa.
6 Taz Mwa 19:24 Watu wangu wamepata adhabu kubwa
kuliko watu wa mji wa Sodoma
mji ambao uliteketezwa ghafla
bila kuwa na muda wa kunyosha mkono.
7Vijana wa Siyoni walikuwa safi kuliko theluji,
walikuwa weupe kuliko maziwa.
Miili yao ilikuwa myekundu kama matumbawe,
uzuri wa viwiliwili vyao kama johari ya rangi ya samawati.
8Sasa sura zao ni nyeusi kuliko makaa,
wanapita barabarani bila kujulikana;
ngozi yao imegandamana na mifupa yao
imekauka, imekuwa kama kuni.
9Afadhali waliouawa kwa upanga
kuliko waliokufa kwa njaa,
ambao walikufa polepole
kwa kukosa chakula.
10 Taz Kumb 38:57; Eze 5:10 Kina mama ambao huwa na huruma kuu
waliwapika watoto wao wenyewe,
wakawafanya kuwa chakula chao
wakati watu wangu walipoangamizwa.
11Mwenyezi-Mungu alionesha uzito wa ghadhabu yake,
aliimimina hasira yake kali;
aliwasha moto huko mjini Siyoni
ambao uliteketeza misingi yake.
12Wafalme duniani hawakuamini
wala wakazi wowote wa ulimwenguni,
kwamba mvamizi au adui
angeweza kuingia malango ya Yerusalemu.
13Hayo yalisababishwa na dhambi za manabii wake,
yalitukia kwa sababu ya uovu wa makuhani wake
ambao walimwaga damu ya waadilifu mjini kwake.
14Walitangatanga barabarani kama vipofu,
walikuwa wamekuwa najisi kwa damu,
hata asiwepo mtu yeyote wa kuwagusa.
15Watu waliwapigia kelele wakisema:
“Tokeni, nendeni zenu enyi mlio najisi!
Tokeni, tokeni, msiguse chochote.”
Hivyo wakawa wakimbizi na kutangatanga;
watu wa mataifa walitamka:
“Hawa hawatakaribishwa kukaa kwetu!”
16Mwenyezi-Mungu mwenyewe aliwatawanya,
wala hatawajali tena.
Makuhani hawatapata tena heshima,
wazee hawatapendelewa tena.
17Tulichoka kukaa macho kungojea msaada;
tulikesha na kungojea kwa hamu
taifa ambalo halikuweza kutuokoa.
18Watu walifuatilia hatua zetu,
tukashindwa kupita katika barabara zetu.
Siku zetu zikawa zimetimia;
mwisho wetu ukawa umefika.
19Waliotufuatia walikuwa wepesi kuliko tai,
walitukimbiza milimani,
walituvizia huko nyikani.
20Walimnasa yule ambaye maisha yetu yalimtegemea,
yule mfalme aliyewekwa wakfu wa Mwenyezi-Mungu,
yule ambaye tulisema: “Chini ya ulinzi wake
tutaishi miongoni mwa mataifa.”
21Wakazi wa Edomu, mwaweza kushangilia kwa sasa,
mwaweza kwa sasa kufurahi enyi wakazi wa Uzi;
lakini kikombe hiki cha adhabu kitawajia pia,
nanyi pia mtakinywa na kulewa,
hata mtayavua mavazi yenu!
22Adhabu ya uovu wako ewe Siyoni imekamilika;
Mwenyezi-Mungu hatawaacha zaidi uhamishoni.
Lakini nyinyi Waedomu atawaadhibu kwa uovu wenu,
atazifichua dhambi zenu.



Maombolezo4;1-22

Biblia Habari Njema kwa Watu Wote(BHN)

"Swahili Na Waswahili"Mbarikiwe.

Friday 14 February 2020

Kikombe Cha Asubuhi; Maombolezo 3....



Shalom,Habari za Asubuhi,Hamjambo,Mmeamkaje?

Tumshukuru Mungu katika yote....

Mungu wetu Baba yetu,Muumba wetu Muumba wa Mbingu na Nchi
Muumba wa vyote vilivyomo vinavyoonekana na visivyoonekana
Mungu wa walio hai,Mungu  mwenye huruma,Mungu wa upendo
Mungu wa Abrahamu,Isaka na Yakobo...
Asante kwa wema na fadhili zako kwetu
Asante kwa ulinzi wako kwetu wakati wote
Asante kwa kutuchagua tena na kutupa
kibali cha kuendelea kuiona leo hii
Asante kwa pumzi/uzima,afya na kuwatayari kwa majukumu yetu

Neema yako yatutosha ee Mungu wetu....!!


Yesu alianza kufundisha tena akiwa kando ya ziwa. Umati mkubwa wa watu ulimzunguka hata ikambidi aingie katika mashua na kuketi. Watu wote wakawa wamekaa katika nchi kavu, kando ya ziwa. Aliwafundisha mambo mengi kwa mifano, na katika mafundisho yake aliwaambia,
Baba wa Mbinguni tunakuja mbele zako tukijinyenyekeza,
tukijishusha na kujiachilia mikononi mwako

Mungu wetu tunaomba utusamehe dhambi zetu zote 
Baba wa Mbinguni nasi tunaomba ukatupe neema
ya kuweza kuwasamehe wale wote waliotukosea
Usitutie majaribuni Mungu wetu tunaomba utuepushe
na yule mwovu na kazi zake zote
Jehovah ututakase miili yetu na akili zetu
Baba wa Mbinguni tunaomba utufunike kwa Damu
ya Bwana na Mwokozi wetu Yesu Kristo wa Nazareti
yeye aliteseka kwanza ili sisi tupate kupona....


“Sikilizeni! Mpanzi alikwenda kupanda mbegu. Alipokuwa akipanda mbegu, nyingine zilianguka njiani, ndege wakaja wakazila. Nyingine zilianguka penye mawe pasipokuwa na udongo mwingi, zikaota mara kwa kuwa udongo haukuwa na kina. Jua lilipochomoza, zikateketea; na kwa kuwa mizizi yake haikuwa na nguvu, zikanyauka.
Mungu wetu tunaomba ukabariki kazi za mikono yetu
Baba wa Mbinguni tunaomba ukatupe ubunifu na maarifa katika utendaji
Jehovah nasi tukatende sawasawa na mapenzi yako
Yahweh tunaomba ukabariki ridhiki zetu ziingiazo/zitokazo
Mungu wetu nasi tunaomna ukatupe neema ya kuweza kuwabariki wenye kuhitaji
Tusipungukiwe katika mahitaji yetu
Baba wa Mbinguni tunaomba ukatupe kama inavyokupendeza wewe...


Yahweh tunayaweka maisha yetu mikononi mwako
Mungu wetu tunaomba ukabariki nyumba/ndoa zetu,
Jehovah tunaomba ulinzi wako kwetu na kwa vyote tunavyovimiliki
Yahweh tunaomba ukatubariki tuingiapo/tutokapo
Mungu wetu tunaomba ukavibariki vyote tunavyoenda kugusa/kutumia
Baba wa Mbinguni ukavitakase kwa Damu ya Bwana wetu Yesu Kristo
Mungu wetu ukatamalaki na kutuatamia
Baba wa Mbinguni tukawe salama rohoni
Yahwe ukatupe akili ya kutambua mema na mabaya
Mfalme wa amani amani yako ikatawale katika maisha yetu
Mungu wetu ukatupe macho ya kuona,masikio ya kusikia sauti yako na kuitii..
Baba wa Mbinguni  tunaomba ukatupe neema ya kufuata
njia zako,tukasimamie Neno lako,amri na sheria zako
siku zote za maisha yetu...
Ukatuguse kwa mkono wako wenye nguvu,ukatufanye chombo chema
ee Mungu wetu nasi tukatumike kama inavyokupendeza wewe
Roho Mtakatifu akatuongoze katika yote na tukawe na kiasi....

Nyingine zilianguka kwenye miti ya miiba, nayo ikakua na kuzisonga, nazo hazikuzaa nafaka. Nyingine zilianguka katika udongo mzuri, zikamea, zikakua na kuzaa: Moja punje thelathini, moja sitini na nyingine mia.” Kisha akawaambia, “Mwenye masikio na asikie!”
Tazama watoto wako wenye shida/tabu,wote wanaopitia magumu/majaribu mbalimbali
Mungu wetu tunaomba ukawaguse kwa mkono wako wenye nguvu
kila mmoja na mahitaji yake
Mungu wetu tunaomba ukawasamehe pale walipo kwenda kinyume nawe
Yahweh tunaomba ukawape neema ya kuweza kujiombea,kufuata njia zako nazo zikawaweke huru...
Baba wa Mbinguni tunayaweka haya yote mikononi mwako
Kwakuwa Ufalme ni wako Nguvu na Utukufu hata Milele...
Amina...!!


Asanteni sana wapendwa katika Kristo Yesu kwakuwa nami,Baba wa Mbinguni aendelee kuwatendea sawasawa na mapenzi yake...
Nawapenda.

Adhabu, toba na tumaini
1Mimi ni mtu niliyepata mateso
kwa fimbo ya ghadhabu yake Mungu.
2Amenichukua akanipeleka
mpaka gizani kusiko na mwanga.
3Amenyosha mkono wake dhidi yangu mimi tu,
akanichapa tena na tena mchana kutwa.
4Amenichakaza ngozi na nyama,
mifupa yangu ameivunja.
5Amenizingira na kunizungushia
uchungu na mateso.
6Amenikalisha gizani
kama watu waliokufa zamani.
7Amenizungushia ukuta nisitoroke,
amenifunga kwa minyororo mizito.
8Ingawa naita na kulilia msaada
anaizuia sala yangu isimfikie.
9Njia zangu ameziziba kwa mawe makubwa
amevipotosha vichochoro vyangu.
10Yeye ni kama dubu anayenivizia;
ni kama simba aliyejificha.
11Alinifukuza njiani mwangu,
akanilemaza na kuniacha mkiwa.
12Aliuvuta upinde wake,
akanilenga mshale wake.
13Alinichoma moyoni kwa mishale,
kutoka katika podo lake.
14Nimekuwa kitu cha dhihaka kwa watu wote,
mchana kutwa nimekuwa mtu wa kuzomewa.
15Amenijaza taabu,
akanishibisha uchungu.
16Amenisagisha meno katika mawe,
akanifanya nigaegae majivuni.
17Moyo wangu haujui tena amani,
kwangu furaha ni kitu kigeni.
18Nimewaza “Nimekata tamaa kabisa,
tumaini langu kwa Mwenyezi-Mungu limetoweka.”
19Kukumbuka taabu na kutangatanga kwangu
kwanipa uchungu kama wa nyongo.
20Nayafikiria hayo daima,
nayo roho yangu imejaa majonzi.
21Lakini nakumbuka jambo hili moja,
nami ninalo tumaini:
22Kwamba fadhili za Mwenyezi-Mungu hazikomi,
huruma zake hazina mwisho.
23Kila kunapokucha ni mpya kabisa,
uaminifu wake ni mkuu mno.
24Mwenyezi-Mungu ndiye hazina yangu
hivyo nitamwekea tumaini langu.
25Mwenyezi-Mungu ni mwema kwa wanaomtegemea,
ni mwema kwa wote wanaomtafuta.
26Ni vema mtu kungojea kwa saburi
ukombozi utokao kwa Mwenyezi-Mungu.
27Ni vema mtu kujifunza uvumilivu
tangu wakati wa ujana wake.
28Heri kukaa peke na kimya,
mazito yanapompata kutoka kwa Mungu.
29Yampasa kuinama na kujinyenyekesha,
huenda ikawa tumaini bado lipo.
30Yampasa kumgeuzia shavu mwenye kumpiga,
na kuwa tayari kupokea matusi yake.
31Mwenyezi-Mungu hatatutupa milele.
32Ingawa atufanya tuhuzunike,
atakuwa na huruma tena
kadiri ya wingi wa fadhili zake.
33Yeye hapendelei kuwatesa
wala kuwahuzunisha wanadamu.
34Wafungwa wote nchini
wanapodhulumiwa na kupondwa;
35haki za binadamu zinapopotoshwa
mbele yake Mungu Mkuu,
36kesi ya mtu inapopotoshwa mahakamani,
je, Mwenyezi-Mungu haoni hayo?
37Nani awezaye kuamuru kitu kifanyike
Mwenyezi-Mungu asipopanga iwe hivyo?
38Maafa na mema hutokea tu
kwa amri yake Mungu Mkuu.
39Kwa nini mtu anung'unike,
ikiwa ameadhibiwa kwa dhambi zake?
40Na tupime na kuchunguza mwenendo wetu,
tupate kumrudia Mwenyezi-Mungu.
41Tumfungulie Mungu huko mbinguni
mioyo yetu na kumwomba:
42“Sisi tulikukosea na kukuasi
nawe bado hujatusamehe.
43“Umejizungushia hasira yako ukatufuatia,
ukatuua bila huruma.
44Umejizungushia wingu zito,
sala yeyote isiweze kupenya humo.
45Umetufanya kuwa takataka na uchafu
miongoni mwa watu wa mataifa.
46“Maadui zetu wote wanatuzomea.
47Kitisho na hofu vimetuandama,
tumepatwa na maafa na maangamizi.
48Macho yangu yabubujika mito ya machozi
kwa sababu ya kuangamizwa kwa watu wangu.
49“Machozi yatanitoka bila kikomo,
50mpaka Mwenyezi-Mungu kutoka huko mbinguni
aangalie chini na kuona.
51Nalia na kujaa majonzi,
kuona yaliyowapata kina mama wa mji wangu.
52“Nimewindwa kama ndege
na hao wanichukiao bila sababu.
53Walinitupa shimoni nikiwa hai
na juu yangu wakarundika mawe.
54Maji yalianza kunifunika kichwa,
nami nikafikiri, ‘Huu ni mwisho wangu.’
55“Kutoka chini shimoni
nilikulilia ee Mwenyezi-Mungu.
56Wewe umenisikia nikikulilia:
‘Usiache kusikia kilio changu cha msaada
bali unipatie nafuu.’
57Nilipokuita ulinijia karibu
ukaniambia, ‘Usiogope!’
58“Umenitetea katika kisa changu ee Mwenyezi-Mungu,
umeyakomboa maisha yangu.
59Umeuona uovu niliotendewa ee Mwenyezi-Mungu,
uniamulie kwa wema kisa changu.
60Umeuona uovu wa maadui zangu,
na mipango yao yote ya hila dhidi yangu.
61“Umesikia matukano yao ee Mwenyezi-Mungu,
na mipango yao yote ya hila dhidi yangu.
62Maneno na mawazo ya maadui zangu siku nzima
ni juu ya kuniangamiza mimi.
63Wakati wote, wamekaa au wanakwenda,
mimi ndiye wanayemzomea.
64Uwalipize, ee Mwenyezi-Mungu
kadiri ya hayo matendo yao,
kadiri ya mambo waliyotenda wenyewe.
65Uipumbaze mioyo yao,
na laana yako iwashukie.
66Uwafuatie kwa hasira, uwaangamize,
uwafanye watoweke ulimwenguni.”


Maombolezo3;1-66

Biblia Habari Njema kwa Watu Wote(BHN)

"Swahili Na Waswahili"Mbarikiwe.

Thursday 13 February 2020

Kikombe Cha Asubuhi; Maombolezo 2....


Shalom,Habari za Asubuhi,Hamjambo,Mmeamkaje?

Tumshukuru Mungu wetu katika yote...

Asante  Mungu wetu kwa wema na fadhili zako kwetu
Asante kwa ulinzi wako kwetu wakati wote
Asante kwa kutuchagua tena na kutupa
kibali cha kuendelea kuiona leo hii
Asante kwa pumzi/uzima,afya na kuwatayari kwa majukumu yetu


Utukuzwe ee Mungu wetu,usifiwe Baba wa Mbinguni

Neema yako yatutosha  Mungu wetu..!

Yesu akawauliza, “Mnayo mikate mingapi?” Wakamjibu, “Saba na visamaki vichache.” Basi, Yesu akawaamuru watu wakae chini.
Baba wa Mbinguni tunakuja mbele zako tukijinyenyekeza,
tukijishusha na kujiachilia mikononi mwako

Mungu wetu tunaomba utusamehe dhambi zetu zote
Baba wa Mbinguni nasi tunaomba utupe neema ya kuweza kuwasamehe wale wote waliotukosea,Usitutie majaribuni Mungu wetu tunaomba utuepushe na yule mwovu na kazi zake zote,Jehovah ututakase miili yetu na akili zetu Baba wa Mbinguni tunaomba utufunike kwa  Damu ya Bwana na Mwokozi wetu Yesu Kristo wa Nazareti,
Yeye aliteseka kwanza ili sisi tupate kupona....

Akaitwaa ile mikate saba na vile visamaki, akamshukuru Mungu, akavimega, akawapa wanafunzi, nao wakawagawia watu. Wote wakala, wakashiba. Kisha wakakusanya mabaki, wakajaza vikapu saba.
Mungu wetu tunaomba ukabariki kazi za mikono yetu
Baba wa Mbinguni tunaomba ukatupe ubunifu na maarifa 
katika utendaji
Jehovah nasi tukatende sawasawa na mapenzi yako
Baba wa Mbinguni tunaomba ukabariki ridhiki zetu
ziingiazo/zitokazo
Mungu wetu nasi tunaomba ukatupe neema ya kuweza
kuwabariki wenye kuhitaji
Yahweh tusipungukiwe katika mahitaji yetu
Mungu wetu ukatupe kama inavyokupendeza wewe



Jehovah tunayaweka maisha yetu mikononi mwako
Baba wa Mbinguni tunaomba ukabariki nyumba/ndoa zetu,
watoto,wazazi wetu,familia/ndugu na wote wanaotuzunguka
Jehovah tunaomba ulinzi wako kwetu na kwa vyote tunavyo vimiliki
Yahweh tunaomba ukatubariki tuingiapo/tutokapo
Mungu wetu tunaomba ukavibariki vyote tunavyoenda kugusa/kutumia
Baba wa Mbinguni ukavitakase kwa Damu ya Bwana wetu Yesu Kristo
Mungu wetu ukatamalaki na kutuatamia
Baba wa Mbinguni tukawe salama rohoni
Mfalme wa amani amani yako ikatawale katika maisha yetu
Mungu wetu ukatupe macho ya kuona na masikio ya kusikia 
sauti yako na kuitii
Baba wa Mbinguni tunaomba ukatupe neema ya kufuata njia zako
Yahweh tukasimamie Neno lako amri na sheria zako siku zote 
za maisha yetu

Mungu  wetu ukaonekane katika maisha yetu popote tupitapo na ikajulikane kwamba upo 

Neema zako zikawe nasi Nuru yako ikaangaze katika maisha yetu
Ukatufanye barua njema ee Mungu wetu nasi tukasomeke kama
inavyokupendeza wewe
Roho Mtakatifu akatuongoze katika yote na tukawe na kiasi...

Hao waliokula walikuwa wanaume 4,000, bila kuhesabu wanawake na watoto. Basi, Yesu akawaaga watu, akapanda mashua, akaenda katika eneo la Magadani.
Tazama wenye shida/tabu,Mungu wetu tunaomba
 ukawaguse kila mmoja na mahitaji yake
Baba wa Mbinguni tunaomba ukawasamehe pale walipokwenda
kinyume nawe
Mungu wetu ukawape neema ya kujiombea,macho ya rohoni,masikio yakusikia sauti yako,wakafuate njia zako nazo zikawaweke huru
Mungu wetu tunaomba ukasikie kulia kwao
Baba wa Mbinguni tunomba ukawafute machozi yao
Nuru yako ikaangaze katika maisha yao
Mungu wetu tunaomba ukawatendee sawasawa na mapenzi yako
Kwakuwa Ufalme ni wako Nguvu na Utukufu hata Milele
Amina....!!!


Wapendwa katika Kristo Yesu asanteni sana
kwakuwanami/kunisoma

Mungu Baba aendelee kuwabariki na kuwatendea
kama inavyompendeza yeye
Amani ya Bwana wetu Yesu Kristo na upendo wa Mungu Baba
ukae nanyi daima....

Nawapenda.

Adhabu ya Yerusalemu
1Mwenyezi-Mungu, kwa hasira yake,
amewaweka watu wa Siyoni gizani.
Fahari ya Israeli ameibwaga chini.
Siku ya hasira yake
alilitupilia mbali hata hekalu lake.
2Mwenyezi-Mungu ameharibu bila huruma
makazi yote ya wazawa wa Yakobo.
Kwa ghadhabu yake amezibomoa ngome za watu wa Yuda.
Ufalme wao na watawala wake
ameuporomosha chini kwa aibu.
3Nguvu yote ya Israeli ameivunja kwa hasira.
Hakunyosha mkono kuwasaidia
walipokutana na adui;
amewawakia watu wa Yakobo kama moto,
akateketeza kila kitu.
4Amevuta upinde wake kama adui,
na kuuweka mkono wake wa kulia tayari,
amewaua wote tuliowaonea fahari
katika maskani yetu watu wa Siyoni.
Ametumiminia hasira yake kama moto.
5Mwenyezi-Mungu amekuwa kama adui,
ameangamiza watu wa Israeli;
majumba yake yote ameyaharibu,
ngome zake amezibomoa.
Amewazidishia watu wa Yuda
matanga na maombolezo.
6Hekalu lake amelibomoa kama kitalu bustanini,
maskani yake ameiharibu.
Amefutilia mbali sikukuu na Sabato huko Siyoni,
kwa hasira yake kuu amewakataa mfalme na makuhani.
7Mwenyezi-Mungu ameipuuza madhabahu yake
na hekalu lake amelikataa.
Kuta za majumba mjini amewaachia maadui wazibomoe,
wakapiga kelele humo nyumbani kwa Mwenyezi-Mungu
kama kelele za wakati wa sikukuu.
8Mwenyezi-Mungu alipania kuubomoa ukuta wa mji wa Siyoni;
aliupima na kuhakikisha kila kitu kimeharibiwa;
minara na kuta za nje ya mji akazifanya ukiwa,
zote kwa pamoja zikaangamia.
9Malango yake yameanguka chini,
makomeo yake ameyaharibu na kuyavunjavunja.
Mfalme na wakuu wake wako uhamishoni kati ya mataifa.
Mwongozo wa sheria umetoweka kabisa,
manabii wake hawapati tena maono
kutoka kwake Mwenyezi-Mungu.
10Wazee wa Siyoni wameketi chini kimya,
wamejitia mavumbi vichwani
na kuvaa mavazi ya gunia.
Wasichana wa Yerusalemu wameinamisha vichwa.
11Macho yangu yamevimba kwa kulia,
roho yangu imechafuka.
Moyo wangu una huzuni nyingi
kwa sababu ya kuangamizwa kwa watu wangu
kwa sababu watoto wachanga wanazirai katika barabara za mji.
12Wanawalilia mama zao:
“Wapi chakula, wapi kinywaji?”
Huku wanazirai kama majeruhi
katika barabara za mjini,
na kukata roho mikononi mwa mama zao.
13Nikuambie nini ee Yerusalemu?
Nikulinganishe na nini?
Nikufananishe na kitu gani
ili niweze kukufariji,
ee Siyoni uliye mzuri?
Maafa yako ni mengi kama bahari.
Ni nani awezaye kukuponya?
14Manabii wako wamekuonea maono madanganyifu,
hawakufichua wazi uovu wako
ili wapate kukurekebisha,
bali walikuonea kauli ya uongo na ya kupotosha.
15Wapita njia wote wanakudhihaki;
wanakuzomea, ee Yerusalemu,
wakitikisa vichwa vyao kwa dharau na kusema:
“Je, huu ndio ule mji uliofikia upeo wa uzuri,
mji uliokuwa furaha ya dunia nzima?”
16Maadui zako wote wanakuzomea,
wanakufyonya na kukusagia meno,
huku wakisema, “Tumemwangamiza!
Kweli, siku ile tuliyoingojea kwa hamu
sasa imefika na tumeiona!”
17Mwenyezi-Mungu amefanya yale aliyokusudia,
ametekeleza yale aliyotishia;
kama alivyopanga tangu kale
ameangamiza bila huruma yoyote;
amewafanya maadui wafurahie adhabu yako,
amewakuza mashujaa wa maadui zako.
18Kuta zako, ee mji wa Siyoni, zimlilie Mwenyezi-Mungu!
Machozi na yatiririke kama mto mchana na usiku!
Lia na kuomboleza bila kupumzika!
19Usiku kucha uamkeamke ukalie.
Mfungulie Mwenyezi-Mungu yaliyo moyoni mwako.
Mwinulie mikono yako kuwaombea watoto wako,
watoto wanaozirai kwa njaa popote barabarani.
20Tazama ee Mwenyezi-Mungu uone!
Je, kuna yeyote uliyemtendea ulivyotutendea sisi?
Je, hata kina mama wawale watoto wao?
Je, nao makuhani wauawe hekaluni mwako?
21Maiti za vijana na wazee zimelala vumbini barabarani,
wasichana na wavulana wangu wameuawa kwa upanga;
umewaua bila huruma siku ya hasira yako.
22Umewaalika kama kwenye sikukuu
maadui zangu walionitisha kila upande.
Katika siku ya hasira yako ee Mwenyezi-Mungu,
hakuna aliyetoroka au kunusurika.
Wale niliowazaa na kuwalea
adui zangu wamewaangamiza.


Maombolezo2;1-22

Biblia Habari Njema kwa Watu Wote(BHN)

"Swahili Na Waswahili"Mbarikiwe.