Swahili na Waswahili

Swahili na Waswahili
Waswahili na Mswahili Rachel Siwa...Pamoja Daima!!

Tuesday 15 October 2019

Kikombe Cha Asubuhi;Isaya 33....


Shalom,Habari za Asubuhi,Hamjambo,Mmeamkaje?

Tumshukuru Mungu katika yote....

Mungu wetu Baba yetu,Muumba wetu Muumba wa Mbingu na Nchi
Muumba wa vyote vilivyomo vinavyoonekana na visivyoonekana
Mungu wa walio hai,Mungu  mwenye huruma,Mungu wa upendo
Mungu wa Abrahamu,Isaka na Yakobo...
Asante kwa wema na fadhili zako kwetu
Asante kwa ulinzi wako kwetu wakati wote
Asante kwa kutuchagua tena na kutupa
kibali cha kuendelea kuiona leo hii
Asante kwa pumzi/uzima,afya na kuwatayari kwa majukumu yetu

Neema yako yatutosha ee Mungu wetu....!!

Mfalme Ahasuero alitoza kodi watu wa bara na pwani. Matendo yake yote makuu na ya ajabu, pamoja na simulizi kamili kuhusu jinsi alivyompandisha cheo Mordekai na kumtunukia heshima kuu, yote yameandikwa katika Kitabu cha Kumbukumbu za wafalme wa Media na Persia.
Baba wa Mbinguni tunakuja mbele zako tukijinyenyekeza,tukijishusha na kujiachilia mikononi mwako
Mungu wetu tunaomba utusamehe dhambi zetu zote 
Baba wa Mbinguni nasi tunaomba ukatupe neema
ya kuweza kuwasamehe wale wote waliotukosea
Usitutie majaribuni Mungu wetu tunaomba utuepushe
na yule mwovu na kazi zake zote
Jehovah ututakase miili yetu na akili zetu
Baba wa Mbinguni tunaomba utufunike kwa Damu
ya Bwana na Mwokozi wetu Yesu Kristo wa Nazareti
yeye aliteseka kwanza ili sisi tupate kupona....
Mungu wetu tunaomba ukabariki kazi za mikono yetu
Baba wa Mbinguni tunaomba ukatupe ubunifu na maarifa katika utendaji
Jehovah nasi tukatende sawasawa na mapenzi yako
Yahweh tunaomba ukabariki ridhiki zetu ziingiazo/zitokazo
Mungu wetu nasi tunaomna ukatupe neema ya kuweza kuwabariki wenye kuhitaji
Tusipungukiwe katika mahitaji yetu
Baba wa Mbinguni tunaomba ukatupe kama inavyokupendeza wewe...


Yahweh tunayaweka maisha yetu mikononi mwako
Mungu wetu tunaomba ukabariki nyumba/ndoa zetu,
Jehovah tunaomba ulinzi wako kwetu na kwa vyote tunavyovimiliki
Yahweh tunaomba ukatubariki tuingiapo/tutokapo
Mungu wetu tunaomba ukavibariki vyote tunavyoenda kugusa/kutumia
Baba wa Mbinguni ukavitakase kwa Damu ya Bwana wetu Yesu Kristo
Mungu wetu ukatamalaki na kutuatamia
Baba wa Mbinguni tukawe salama rohoni
Yahwe ukatupe akili ya kutambua mema na mabaya
Mfalme wa amani amani yako ikatawale katika maisha yetu
Mungu wetu ukatupe macho ya kuona,masikio ya kusikia sauti yako na kuitii..
Baba wa Mbinguni  tunaomba ukatupe neema ya kufuata
njia zako,tukasimamie Neno lako,amri na sheria zako
siku zote za maisha yetu...
Ukatuguse kwa mkono wako wenye nguvu,ukatufanye chombo chema
ee Mungu wetu nasi tukatumike kama inavyokupendeza wewe
Roho Mtakatifu akatuongoze katika yote na tukawe na kiasi....

Mordekai, Myahudi, alikuwa wa kwanza chini ya mfalme Ahasuero katika madaraka. Alipendwa na kuheshimiwa na Wayahudi, maana aliwafanyia mema watu wake na kuwatakia amani wazawa wao wote.
Tazama watoto wako wenye shida/tabu,wote wanaopitia magumu/majaribu mbalimbali
Mungu wetu tunaomba ukawaguse kwa mkono wako wenye nguvu
kila mmoja na mahitaji yake
Mungu wetu tunaomba ukawasamehe pale walipo kwenda kinyume nawe
Yahweh tunaomba ukawape neema ya kuweza kujiombea,kufuata njia zako nazo zikawaweke huru...
Baba wa Mbinguni tunayaweka haya yote mikononi mwako
Kwakuwa Ufalme ni wako Nguvu na Utukufu hata Milele...
Amina...!!


Asanteni sana wapendwa katika Kristo Yesu kwakuwa nami,Baba wa Mbinguni aendelee kuwatendea sawasawa na mapenzi yake...
Nawapenda.


Maafa kwa mwangamizi
1Ole wako ewe mwangamizi,
unayeangamiza bila wewe kuangamizwa!
Ole wako wewe mtenda hila,
ambaye hakuna aliyekutendea hila!
Utakapokwisha kuangamiza
wewe utaangamizwa!
Utakapomaliza kuwatendea watu hila
wewe utatendewa hila.
2Ee Mwenyezi-Mungu, utuonee huruma,
kwako tumeliweka tumaini letu.
Uwe kinga yetu kila siku,
wokovu wetu wakati wa taabu.
3Kwa kishindo cha sauti yako watu hukimbia;
unapoinuka tu, mataifa hutawanyika.
4Maadui zao wanakusanya mateka,
wanayarukia kama panzi.
5Mwenyezi-Mungu ametukuka,
yeye anaishi juu mbinguni.
Ameujaza Siyoni haki na uadilifu.
6Enyi watu wa Yerusalemu,
Mwenyezi-Mungu atawajalieni usalama,
atawaokoa na kuwapa hekima na maarifa.
Hazina yenu kuu ni kumcha Mwenyezi-Mungu.
7Haya, mashujaa wao wanalia,
wajumbe wa amani wanaomboleza.
8Barabara kuu zimebaki tupu;
hamna anayesafiri kupitia humo.
Mikataba inavunjwa ovyo,
mashahidi wanadharauliwa.
Hamna anayejali tena maisha ya binadamu.
9Nchi inaomboleza na kunyauka;
misitu ya Lebanoni imekauka,
bonde zuri la Sharoni limekuwa jangwa,
huko Bashani na mlimani Karmeli
miti imepukutika majani yake.
Mwenyezi-Mungu awaonya maadui zake
10Mwenyezi-Mungu asema hivi:
“Sasa mimi nitainuka;
sasa nitajiweka tayari;
sasa mimi nitatukuzwa.
11Mipango yenu yote ni kama makapi,
na matokeo yake ni takataka tupu.
Pumzi yangu33:11 Pumzi yangu: Kadiri ya hati kadhaa za kale; makala ya Kiebrania ina pumzi yenu. itawaangamiza kama moto.
12Watu watakuwa kama wamechomwa kuwa majivu,
kama miiba iliyokatwa na kuteketezwa motoni.
13Sikilizeni mambo mliyofanya enyi mlio mbali,
nanyi mlio karibu kirini uwezo wangu.”
14Wenye dhambi katika Siyoni wanaogopa,
wasiomcha Mungu wanatetemeka na kusema:
“Nani awezaye kuukaribia moto huu mkali?
Nani awezaye kustahimili miali ya moto wa milele?”
15Ni mtu aishiye kwa uadilifu na asemaye ukweli;
mtu anayedharau kabisa utajiri wa dhuluma,
anayekataa hongo kata kata,
asiyekubali kamwe kusikia mipango ya mauaji,
wala hakubali macho yake yaone maovu.
16Mtu wa namna hiyo anaishi juu,
mahali salama penye ngome na miamba;
chakula chake atapewa daima,
na maji yake ya kunywa hayatakosekana.
Wakati mzuri ujao
17Mtaweza kumwona mfalme katika fahari yake,
mtaiona nchi anayotawala, kubwa na pana.
18Mtafikiria tisho lililopita na kujiuliza,
“Wako wapi wale waliokadiria na kukisia kodi?
Wako wapi wale waliopeleleza ulinzi wetu?”
19Hamtawaona tena watu wale wenye kiburi,
wanaozungumza lugha isiyoeleweka.
20Tazameni Siyoni tunamofanya sikukuu zetu;
tazameni mji Yerusalemu, makao matulivu, hema imara;
vigingi vyake havitangolewa kamwe,
kamba zake hazitakatwa hata moja.
21Humo Mwenyezi-Mungu atatuonesha ukuu wake.
Kutakuwa na mito mikubwa na vijito,
ambamo meli za vita hazitapita,
wala meli kubwa kuingia.
22Maana Mwenyezi-Mungu ni hakimu wetu,
yeye ni mtawala wetu;
Mwenyezi-Mungu ni mfalme wetu,
yeye ndiye anayetuokoa.
23Ewe Siyoni, kamba zako zimelegea,
haziwezi kushikilia matanga yake,
wala kuyatandaza.
Lakini nyara nyingi zitagawanywa;
hata vilema wataweza kuchukua sehemu yao.
24Hakuna atakayesema tena ni mgonjwa;
watu watasamehewa uovu wao wote.

Isaya33;1-24

Biblia Habari Njema kwa Watu Wote(BHN)

"Swahili Na Waswahili"Mbarikiwe.

Monday 14 October 2019

Kikombe Cha Asubuhi;Isaya 32....



Shalom,Habari za Asubuhi,Hamjambo,Mmeamkaje?

Haleluyah ni siku/wiki nyingine tena Mungu wetu ametuchagua

na kutupa kibali cha kuendelea kuiona leo hii
Si kwamba sisi tumetenda mema sana wala si kwa nguvu zetu
si kwa utashi wetu wala si kwa akili zetu si kwamba sisi
ni wazuri mno si kwa uwezo wetu sisi kuwa hivi tulivyo leo hii
Ni kwa rehema/neema zake ni kwa mapenzi yake Mungu wetu....

Tumshukuru Mungu wetu katika yote...

Asante Mungu wetu kwa wema na fadhili zako kwetu

Asante kwa ulinzi wako kwetu wakati wote
Asante kwa pumzi/uzima,afya na kuwa tayari kwa majukumu yetu
Sifa na Utukufu tunakurudshia Mungu wetu....!!

Tunakushukuru, ee Mungu, tunakushukuru! Tunatangaza ukuu wa jina lako na kusimulia juu ya matendo yako makuu.
Tazama jana imepita ee Mungu wetu leo ni siku mpya na kesho ni siku nyingine Jehovah tunakuja mbele zako tukijinyenyekeza,tukijishusha na kujiachilia mikononi mwako
 Mungu wetu tunaomba utusamehe dhambi zetu zote tulizozifanya kwakuwaza,kwakunena,kwakutenda,kwakujua/kutojua
Baba wa Mbinguni nasi tunaomba utupe neema ya kuweza kuwasamehe wale wote waliotukosea
Jehovah usitutie majaribu Mungu wetu tunaomba utuepushe na yule mwovu na kazi zake zote
Yahweh tunaomba ututakase miili yetu na akili zetu
Baba wa Mbinguni utufunike kwa Damu ya Bwana na Mwokozi wetu Yesu Kristo wa Nazareti
yeye aliteseka kwanza ili sisi tupate kupona
Kwakupigwa kwake sisi tumepata kupona....

Mungu asema: “Mimi nimeweka wakati maalumu! Wakati huo nitahukumu kwa haki. Nchi ikitetemeka na vyote vilivyomo, mimi ndiye ninayeitegemeza misingi yake. Nawaambia wenye kiburi: ‘Acheni kujigamba’; na waovu: ‘Msioteshe pembe za kiburi! Msijione kuwa watu wa maana sana, wala kusema maneno ya majivuno.’”
Yahweh tunaomba ukabariki kazi za mikono yetu
Baba wa Mbinguni tunaomba ukatupe ubunifu na maarifa 
katika utendaji
Jehovah nasi tukatende sawasawa na mapenzi yako
Baba wa Mbinguni tunaomba ukabariki ridhiki zetu
ziingiazo/zitokazo
Mungu wetu nasi tunaomba ukatupe neema ya kuweza
kuwabariki wenye kuhitaji
Yahweh tusipungukiwe katika mahitaji yetu
Mungu wetu ukatupe kama inavyokupendeza wewe

Baba wa Mbinguni tunayaweka maisha yetu mikononi mwako
Mungu wetu tunaomba ukabariki nyumba/ndoa zetu,
watoto,wazazi wetu,familia/ndugu na wote wanaotuzunguka
Jehovah tunaomba ulinzi wako kwetu na kwa vyote tunavyo vimiliki
Yahweh tunaomba ukatubariki tuingiapo/tutokapo
Mungu wetu tunaomba ukavibariki vyote tunavyoenda kugusa/kutumia
Baba wa Mbinguni ukavitakase kwa Damu ya Bwana wetu Yesu Kristo
Mungu wetu ukatamalaki na kutuatamia
Baba wa Mbinguni tukawe salama rohoni
Mfalme wa amani amani yako ikatawale katika maisha yetu
Mungu wetu ukatupe macho ya kuona na masikio ya kusikia 
sauti yako na kuitii
Baba wa Mbinguni tunaomba ukatupe neema ya kufuata njia zako
Yahweh tukasimamie Neno lako amri na sheria zako siku zote 
za maisha yetu
Mungu wetu ukaonekane katika maisha yetu
Neema zako zikawe nasi Nuru yako ikaangaze katika maisha yetu
ukatuguse kwa mkono wako wenye nguvu
Ukatufanye chombo chema ee Mungu wetu nasi tukatumike kama
inavyokupendeza wewe
Roho Mtakatifu akatuongoze katika yote na tukawe na kiasi...


Hukumu haitoki mashariki au magharibi; wala haitoki nyikani au mlimani. Mungu mwenyewe ndiye hakimu; humshusha mmoja na kumkweza mwingine. Mwenyezi-Mungu, anashika kikombe mkononi, kimejaa divai kali ya hasira yake; anaimimina na waovu wote wanainywa; naam, wanainywa mpaka tone la mwisho. Lakini mimi nitafurahi milele, nitamwimbia sifa Mungu wa Yakobo. Atavunja nguvu zote za watu waovu; lakini nguvu za waadilifu ataziimarisha.
Mungu wetu tunawaweka mikononi mwako wenye shida/tabu,wote wanaopitia magumu/majaribu mbalimbali
Mungu wetu tunaomba ukawaguse kwa mkono wako wenye nguvu
 kila mmoja na mahitaji yake 
Mungu wetu tunaomba ukawasamehe pale walipokwenda kinyume nawe
Baba wa Mbinguni ukawape neema ya kujiombea,kufuata njia zako
wakasimamie Neno lako nalo likaweke huru
Mungu wetu tunaomba ukasikie kuomba kwetu
Mungu wetu ukawatendee sawasawa na mapenzi yako
Kwakuwa Ufalme ni wako Nguvu na Utukufu hata Milele
Amina...!!

Asanteni sana wapendwa katika Kristo Yesu kwakuwa nami
Mungu Baba aendelee kuwabariki na kuwatendea 
kama inavyompendeza yeye....
Nawapenda.

Mfalme mwadilifu
1Kutatokea mfalme atakayetawala kwa uadilifu,
nao viongozi wataongoza kwa kufuata haki.
2Kila mmoja atakuwa kama mahali pa kujikinga na upepo,
kama mahali pa kujificha wakati wa tufani.
Watakuwa kama vijito vya maji katika nchi kame,
kama kivuli cha mwamba mkubwa jangwani.
3Macho hayatafumbwa tena,
masikio yatabaki wazi.
4Wafanyao mambo kwa hamaki wataamua kwa busara,
wenye kigugumizi wataongea sawasawa.
5Wapumbavu hawataitwa tena waungwana,
wala walaghai hawataitwa tena waheshimiwa.
6Wapumbavu hunena upumbavu,
na fikira zao hupanga kutenda uovu,
kutenda mambo yasiyo mema,
kusema mambo ya kumkufuru Mwenyezi-Mungu.
Huwaacha wenye njaa bila chakula,
na wenye kiu huwanyima kinywaji.
7Ulaghai wa walaghai ni mbaya;
hao huzua visa viovu,
na kumwangamiza maskini kwa maneno ya uongo,
hata kama madai ya maskini ni halali.
8Lakini waungwana hutenda kiungwana,
nao hutetea mambo ya kiungwana.
Mawaidha kwa wanawake wa Yerusalemu
9Inukeni, enyi wanawake mnaostarehe, mnisikilize;
sikilizeni ninayosema enyi mabinti mlioridhika.
10Katika mwaka mmoja hivi mtatetemeka nyinyi mliotosheka;
maana hamtapata mavuno yoyote,
na mavuno ya zabibu yatatoweka.
11Tetemekeni kwa woga, enyi mnaojikalia tu;
tetemekeni kwa hofu, enyi mnaostarehe!
Vueni nguo zenu, mbaki uchi,
mjifunge vazi la gunia viunoni mwenu.
12Jipigeni vifua kwa huzuni,
ombolezeni, kwa sababu ya bustani zilizokuwa nzuri,
kwa mizabibu iliyokuwa ikizaa sana,
13kwa ardhi ya watu wangu inayoota miiba na mbigili,
kwa nyumba zote zilizojaa watu wenye furaha,
kwa mji uliokuwa na shangwe.
14Maana ikulu ya mfalme itaachwa mahame,
mji huo wa watu wengi utahamwa.
Mlima na mnara wa ulinzi utakuwa mapango milele,
pundamwitu watapitapita huko kwa furaha,
kondoo watapata malisho yao humo.
Nyakati za amani
15Hali itaendelea kuwa hivyo
mpaka tumiminiwe roho ya Mungu kutoka juu.
Hapo jangwa litakuwa shamba la rutuba tena,
na mashamba ya rutuba yatakuwa msitu.
16Haki itadumu katika nchi iliyokuwa nyika,
uadilifu utatawala katika mashamba yenye rutuba.
17Kutokana na uadilifu watu watapata amani,
utulivu na usalama utadumu milele.
18Watu wangu watakaa katika makao ya amani,
katika maskani salama na mazingira matulivu.
19Msitu wa adui utatoweka kabisa,32:19 Msitu … utatoweka kabisa: Au Patanyesha mvua ya mawe msitu utakapoanguka.
na mji wake utaangamizwa.
20Lakini heri yenu nyinyi:
Mtapanda mbegu zenu popote penye maji,
ng'ombe na punda wenu watatembeatembea watakavyo.


Isaya32;1-20

Biblia Habari Njema kwa Watu Wote(BHN)

"Swahili Na Waswahili"Mbarikiwe.

Friday 11 October 2019

Kikombe Cha Asubuhi;Isaya 31....


Shalom,Habari za Asubuhi,Hamjambo,Mmeamkaje?

Tumshukuru Mungu wetu katika yote...

Asante  Mungu wetu kwa wema na fadhili zako kwetu
Asante kwa ulinzi wako kwetu wakati wote
Asante kwa kutuchagua tena na kutupa
kibali cha kuendelea kuiona leo hii
Asante kwa pumzi/uzima,afya na kuwatayari kwa majukumu yetu


Utukuzwe ee Mungu wetu,usifiwe Baba wa Mbinguni

Neema yako yatutosha  Mungu wetu..!

“Basi sasa, ewe Mwenyezi-Mungu, liimarishe milele neno lako ulilosema kunihusu mimi mtumishi wako na kuhusu jamaa yangu. Nalo jina lako litatukuzwa milele, nao watu watasema, ‘Mwenyezi-Mungu wa majeshi, Mungu wa Israeli, ndiye Mungu wa Israeli!’ Na jamaa yangu, mimi Daudi mtumishi wako, itaimarika mbele yako.
Baba wa Mbinguni tunakuja mbele zako tukijinyenyekeza,tukijishusha na kujiachilia mikononi mwako
Mungu wetu tunaomba utusamehe dhambi zetu zote
Baba wa Mbinguni nasi tunaomba utupe neema ya kuweza kuwasamehe wale wote waliotukosea,Usitutie majaribuni Mungu wetu tunaomba utuepushe na yule mwovu na kazi zake zote,Jehovah ututakase miili yetu na akili zetu Baba wa Mbinguni tunaomba utufunike kwa  Damu ya Bwana na Mwokozi wetu Yesu Kristo wa Nazareti,
Yeye aliteseka kwanza ili sisi tupate kupona....

Maana ee Mungu wangu nimepata ujasiri kukuomba kwa sababu wewe, umenifunulia ukisema ya kwamba utanijengea nyumba. Sasa ee Mwenyezi-Mungu, wewe ndiwe Mungu, umeniahidi mimi mtumishi wako jambo hili jema;
Mungu wetu tunaomba ukabariki kazi za mikono yetu
Baba wa Mbinguni tunaomba ukatupe ubunifu na maarifa 
katika utendaji
Jehovah nasi tukatende sawasawa na mapenzi yako
Baba wa Mbinguni tunaomba ukabariki ridhiki zetu
ziingiazo/zitokazo
Mungu wetu nasi tunaomba ukatupe neema ya kuweza
kuwabariki wenye kuhitaji
Yahweh tusipungukiwe katika mahitaji yetu
Mungu wetu ukatupe kama inavyokupendeza wewe



Jehovah tunayaweka maisha yetu mikononi mwako
Baba wa Mbinguni tunaomba ukabariki nyumba/ndoa zetu,
watoto,wazazi wetu,familia/ndugu na wote wanaotuzunguka
Jehovah tunaomba ulinzi wako kwetu na kwa vyote tunavyo vimiliki
Yahweh tunaomba ukatubariki tuingiapo/tutokapo
Mungu wetu tunaomba ukavibariki vyote tunavyoenda kugusa/kutumia
Baba wa Mbinguni ukavitakase kwa Damu ya Bwana wetu Yesu Kristo
Mungu wetu ukatamalaki na kutuatamia
Baba wa Mbinguni tukawe salama rohoni
Mfalme wa amani amani yako ikatawale katika maisha yetu
Mungu wetu ukatupe macho ya kuona na masikio ya kusikia 
sauti yako na kuitii
Baba wa Mbinguni tunaomba ukatupe neema ya kufuata njia zako
Yahweh tukasimamie Neno lako amri na sheria zako siku zote 
za maisha yetu

Mungu  wetu ukaonekane katika maisha yetu popote tupitapo na ikajulikane kwamba upo 

Neema zako zikawe nasi Nuru yako ikaangaze katika maisha yetu
Ukatufanye barua njema ee Mungu wetu nasi tukasomeke kama
inavyokupendeza wewe
Roho Mtakatifu akatuongoze katika yote na tukawe na kiasi...

kwa hiyo nakuomba uibariki nyumba yangu, mimi mtumishi wako, ili idumu milele mbele yako; kwani unachobariki wewe, huwa kimebarikiwa milele.”
Tazama wenye shida/tabu,Mungu wetu tunaomba
 ukawaguse kila mmoja na mahitaji yake
Baba wa Mbinguni tunaomba ukawasamehe pale walipokwenda
kinyume nawe
Mungu wetu ukawape neema ya kujiombea,macho ya rohoni,masikio yakusikia sauti yako,wakafuate njia zako nazo zikawaweke huru
Mungu wetu tunaomba ukasikie kulia kwao
Baba wa Mbinguni tunomba ukawafute machozi yao
Nuru yako ikaangaze katika maisha yao
Mungu wetu tunaomba ukawatendee sawasawa na mapenzi yako
Kwakuwa Ufalme ni wako Nguvu na Utukufu hata Milele
Amina....!!!


Wapendwa katika Kristo Yesu asanteni sana
kwakuwanami/kunisoma

Mungu Baba aendelee kuwabariki na kuwatendea
kama inavyompendeza yeye
Amani ya Bwana wetu Yesu Kristo na upendo wa Mungu Baba
ukae nanyi daima....

Nawapenda.


Misri haitaweza kusaidia
1Ole wao wale waendao Misri kuomba msaada,
ole wao wanaotegemea farasi,
wanaotegemea wingi wa magari yao ya vita,
na nguvu za askari wao wapandafarasi,
nao hawamtegemei Mtakatifu wa Israeli,
wala hawamwombi Mwenyezi-Mungu shauri!
2Mungu ni mwenye busara na huleta maangamizi.
Habadilishi tamko lake;
ila yuko tayari kuwakabili watu waovu
kadhalika na wasaidizi wa watendao mabaya.
3Wamisri ni binadamu tu wala si Mungu;
farasi wao nao ni wanyama tu, si roho.
Mwenyezi-Mungu akiunyosha mkono wake,
taifa linalotoa msaada litajikwaa,
na lile linalosaidiwa litaanguka;
yote mawili yataangamia pamoja.
Mungu ataulinda mji wa Yerusalemu
4Mwenyezi-Mungu aliniambia:
“Kama vile simba au mwanasimba angurumavyo
kuyakinga mawindo yake,
hata kundi la wachungaji likiitwa kumkabili,
yeye hatishiki kwa kelele zao,
wala hashtuki kwa sauti zao.
Ndivyo atakavyoshuka Mwenyezi-Mungu wa majeshi
kupigana juu ya mlima Siyoni na kilima chake.
5Kama ndege arukavyo juu ya viota vyake,
ndivyo Mwenyezi-Mungu atakavyoulinda Yerusalemu,
ataulinda na kuukomboa,
atauhifadhi na kuuokoa.
6Enyi Waisraeli,
mrudieni huyo mliyemsaliti vibaya.
7Wakati utafika ambapo nyote
mtavitupilia mbali vinyago vyenu
vya fedha na dhahabu ambavyo
mmejitengenezea kwa mikono yenu,
vikawakosesha.
8Hapo Waashuru watauawa kwa upanga,
lakini si kwa upanga wa binadamu;
naam, wataangamizwa kwa upanga
ambao ni zaidi ya ule wa binadamu.
Waashuru watakimbia
na vijana wao watafanyizwa kazi za kitumwa.
9Mfalme wao atatoroka kwa hofu,
na maofisa wao wataiacha bendera yao kwa woga.
Hayo ameyatamka Mwenyezi-Mungu
ambaye moto wake umo mjini Siyoni,
naam, tanuri lake limo mjini Yerusalemu.”


Isaya31;1-9

Biblia Habari Njema kwa Watu Wote(BHN)

"Swahili Na Waswahili"Mbarikiwe.

Thursday 10 October 2019

Kikombe Cha Asubuhi;Isaya 30....


Shalom,Habari za Asubuhi,Hamjambo,Mmeamkaje?

Tumshukuru Mungu katika yote....

Mungu wetu Baba yetu,Muumba wetu Muumba wa Mbingu na Nchi
Muumba wa vyote vilivyomo vinavyoonekana na visivyoonekana
Mungu wa walio hai,Mungu  mwenye huruma,Mungu wa upendo
Mungu wa Abrahamu,Isaka na Yakobo...
Asante kwa wema na fadhili zako kwetu
Asante kwa ulinzi wako kwetu wakati wote
Asante kwa kutuchagua tena na kutupa
kibali cha kuendelea kuiona leo hii
Asante kwa pumzi/uzima,afya na kuwatayari kwa majukumu yetu

Neema yako yatutosha ee Mungu wetu....!!

Kisha mfalme Daudi akaingia ndani ya hema na kuketi mbele ya Mwenyezi-Mungu, halafu akaomba, “Mimi ni nani, ee Mwenyezi-Mungu, na nyumba yangu ni nini hata unitukuze hivi? Isitoshe, umenifanyia mengine zaidi: Umenitolea ahadi juu ya vizazi vyangu vijavyo ee Mwenyezi-Mungu! Nikuambie nini zaidi, mimi Daudi mtumishi wako, kwa kunitukuza hivyo? Wewe unanijua mimi mtumishi wako.
Baba wa Mbinguni tunakuja mbele zako tukijinyenyekeza,tukijishusha na kujiachilia mikononi mwako
Mungu wetu tunaomba utusamehe dhambi zetu zote 
Baba wa Mbinguni nasi tunaomba ukatupe neema
ya kuweza kuwasamehe wale wote waliotukosea
Usitutie majaribuni Mungu wetu tunaomba utuepushe
na yule mwovu na kazi zake zote
Jehovah ututakase miili yetu na akili zetu
Baba wa Mbinguni tunaomba utufunike kwa Damu
ya Bwana na Mwokozi wetu Yesu Kristo wa Nazareti
yeye aliteseka kwanza ili sisi tupate kupona....

Ee Mwenyezi-Mungu, kwa ajili ya mtumishi wako na kwa kufuatana na moyo wako mwenyewe, umeyatenda hayo makuu yote, ili yajulikane hayo matendo makuu yote. Hakuna mwingine kama wewe, ee Mwenyezi-Mungu, na yote tunayoyasikia yanathibitisha kwamba hakuna Mungu mwingine ila wewe.
Mungu wetu tunaomba ukabariki kazi za mikono yetu
Baba wa Mbinguni tunaomba ukatupe ubunifu na maarifa katika utendaji
Jehovah nasi tukatende sawasawa na mapenzi yako
Yahweh tunaomba ukabariki ridhiki zetu ziingiazo/zitokazo
Mungu wetu nasi tunaomna ukatupe neema ya kuweza kuwabariki wenye kuhitaji
Tusipungukiwe katika mahitaji yetu
Baba wa Mbinguni tunaomba ukatupe kama inavyokupendeza wewe...


Yahweh tunayaweka maisha yetu mikononi mwako
Mungu wetu tunaomba ukabariki nyumba/ndoa zetu,
Jehovah tunaomba ulinzi wako kwetu na kwa vyote tunavyovimiliki
Yahweh tunaomba ukatubariki tuingiapo/tutokapo
Mungu wetu tunaomba ukavibariki vyote tunavyoenda kugusa/kutumia
Baba wa Mbinguni ukavitakase kwa Damu ya Bwana wetu Yesu Kristo
Mungu wetu ukatamalaki na kutuatamia
Baba wa Mbinguni tukawe salama rohoni
Yahwe ukatupe akili ya kutambua mema na mabaya
Mfalme wa amani amani yako ikatawale katika maisha yetu
Mungu wetu ukatupe macho ya kuona,masikio ya kusikia sauti yako na kuitii..
Baba wa Mbinguni  tunaomba ukatupe neema ya kufuata
njia zako,tukasimamie Neno lako,amri na sheria zako
siku zote za maisha yetu...
Ukatuguse kwa mkono wako wenye nguvu,ukatufanye chombo chema
ee Mungu wetu nasi tukatumike kama inavyokupendeza wewe
Roho Mtakatifu akatuongoze katika yote na tukawe na kiasi....

Tena ni watu gani duniani ambao wanaweza kulinganishwa na watu wako wa Israeli ambao peke yao Mungu wao alikwenda kuwakomboa ili wawe watu wake? Wewe ulijifanyia jina kwa kutenda mambo makubwa na ya ajabu hapo ulipoyafukuza mataifa mbele ya watu wako ambao uliwakomboa kutoka Misri. Hata umejifanyia watu wako wa Israeli kuwa watu wako milele; nawe ee Mwenyezi-Mungu, umekuwa Mungu wao.
Tazama watoto wako wenye shida/tabu,wote wanaopitia magumu/majaribu mbalimbali
Mungu wetu tunaomba ukawaguse kwa mkono wako wenye nguvu
kila mmoja na mahitaji yake
Mungu wetu tunaomba ukawasamehe pale walipo kwenda kinyume nawe
Yahweh tunaomba ukawape neema ya kuweza kujiombea,kufuata njia zako nazo zikawaweke huru...
Baba wa Mbinguni tunayaweka haya yote mikononi mwako
Kwakuwa Ufalme ni wako Nguvu na Utukufu hata Milele...
Amina...!!


Asanteni sana wapendwa katika Kristo Yesu kwakuwa nami,Baba wa Mbinguni aendelee kuwatendea sawasawa na mapenzi yake...
Nawapenda.



1Mwenyezi-Mungu asema hivi:
“Ole wao watoto wanaoniasi,
wanaotekeleza mipango yao na si mipango yangu,
wanaofanya mikataba kinyume cha matakwa yangu!
Naam, wanarundika dhambi juu ya dhambi.
2Bila kunitaka shauri, wanafunga safari kwenda Misri,
kukimbilia usalama katika ulinzi wa Farao,
kupata mahali pa usalama nchini Misri.
3Lakini ulinzi wa Farao utakuwa aibu yenu,
na usalama nchini Misri utakuwa fedheha yenu.
4Maana ingawa maofisa wao wamefika Soani,
na wajumbe wao mpaka Hanesi,
5wote wataaibishwa na hao wasioweza kuwasaidia,
watu ambao hawawezi kuwapa msaada au faida,
ila tu kuwapa aibu na fedheha.”
6Kauli ya Mungu juu ya wanyama wa pande za Negebu:30:6 Negebu: Au, kusini. Namna nyingine ya kutaja Misri.
“Wajumbe wanapita katika nchi ya taabu na shida,
yenye simba, nyoka wa sumu na majoka.
Wamewabebesha wanyama wao mali zao,
kuwapelekea watu wasioweza kuwafaa kitu.
7Maana msaada wa Misri ni bure, haufai kitu;
kwa hiyo nimeipanga Misri jina:
‘Joka30:7 Joka: Kiebrania: Rahabu. lisilo na nguvu!’”
Watu wasiotii
8Mungu aliniambia:
“Sasa chukua kibao cha kuandikia,
uandike jambo hili mbele yao,
liwe ushahidi wa milele:
9Watu hawa ni waasi, watoto wasioaminika;
watu wasiopenda kusikia mafunzo ya Mwenyezi-Mungu.
10Huwaambia waonaji: ‘Msione maono’,
na manabii: ‘Msitutangazie ukweli,
bali tuambieni mambo ya kupendeza,
toeni unabii wa mambo ya udanganyifu tu.
11Geukeni na kuiacha njia ya ukweli;
msituambie tena juu ya Mungu, Mtakatifu wa Israeli.’”
12Kwa hiyo Mungu, Mtakatifu wa Israeli asema:
“Nyinyi mmeukataa ujumbe wangu;
mkapania kufanya dhuluma na udanganyifu.
13Basi, dhambi hii itawaleteeni maangamizi
kama ufa mkubwa katika ukuta mrefu;
utabomoka mara na kuanguka chini ghafla.
14Kuporomoka kwa ukuta huo,
ni kama kupasuka kwa chungu
ambacho kimepasuliwa vibaya sana,
bila kusalia kigae cha kuchukulia moto mekoni,
au kuchotea maji kisimani.”
15Bwana Mungu, Mtakatifu wa Israeli, asema:
“Mkinirudia na kutulia mtaokolewa;
kwa utulivu na kunitumainia mtapata nguvu.”
Lakini nyinyi hamkutaka.
16Badala yake mlisema,
“La! Sisi tutakimbia na farasi wenye mbio.”
Sawa, mtakimbia na farasi wenye mbio,
lakini farasi wa maadui zenu wana mbio zaidi.
17Watu wenu elfu moja watamkimbia askari mmoja adui;
na askari watano maadui watawakimbizeni nyote.
Mwishowe, watakaosalia
watakuwa kama mlingoti wa bendera mlimani,
kama alama iliyo juu ya kilima.
Wakati wa wokovu
18Hata hivyo, Mwenyezi-Mungu anangoja awafadhili,
atainuka na kuwaonea huruma.
Maana, Mwenyezi-Mungu ni Mungu atendaye haki.
Heri wote wale wanaomtumainia.
19Enyi watu wa Siyoni, enyi watu wa Yerusalemu, hakika nyinyi hamtaomboleza tena. Kweli Mungu atawahurumia; mara tu atakaposikia kilio chenu atawaitikeni. 20Ingawa Bwana atawalisha taabu na kuwanywesha dhiki, yeye ndiye Mwalimu wenu na hatajificha tena; nanyi mtamwona kwa macho yenu wenyewe. 21Mkienda kulia au kushoto, mtasikia sauti nyuma yenu ikisema, “Njia ni hii; ifuateni.” 22Mtavifanya haramu vinyago vyenu vya miungu vilivyopakwa fedha na sanamu zenu zilizopakwa dhahabu. Mtazitupilia mbali kama vitu najisi, mkisema, “Poteleeni mbali!” 23Mtakapopanda mbegu zenu, Mwenyezi-Mungu atanyesha mvua kwa wakati wake, nazo zitakua na kuwapa mavuno mengi. Mifugo yenu nayo itapata malisho kwa wingi. 24Mafahali na punda wenu wa kulimia watapata malisho yaliyochambuliwa vizuri na kutiwa chumvi. 25Wakati utakapofika ambapo maadui watauawa na ngome zao kubomolewa, vijito vya maji vitatiririka kutoka kila mlima na kilima. 26Tena mwezi utawaka kama jua, nao mwanga wa jua utakuwa mara saba ya mwanga wake wa kawaida, kana kwamba mwanga wa siku saba umeangaza katika siku moja. Mambo haya yote yatatukia wakati Mwenyezi-Mungu atakapoyafunga na kuyaponya majeraha aliyowaletea watu wake.
Mungu ataiadhibu nchi ya Ashuru
27Tazameni, Mwenyezi-Mungu mwenyewe anakuja toka mbali!
Amewaka hasira na moshi wafuka;
midomo yake yaonesha ghadhabu yake,
maneno anayosema ni kama moto uteketezao.
28Pumzi yake ni kama mafuriko ya mto
ambao maji yake yanafika hadi shingoni.
Anakuja kuyachekecha mataifa kwa chekecheke ya maangamizi,
kuwafunga lijamu na kuwapeleka wasikotaka.
29Lakini nyinyi watu wa Yerusalemu mtaimba kwa furaha kama mfanyavyo wakati wa mkesha wa sikukuu. Mtajaa furaha kama watu wanaotembea kwa mdundo wa muziki wa filimbi kwenda mlimani kwa Mwenyezi-Mungu, Mwamba wa Israeli.
30Mwenyezi-Mungu atawafanya watu wote waisikie sauti yake tukufu na pigo la nguvu yake lionekane kwa hasira nyingi. Kutakuwa na ndimi za moto mkali, ngurumo, dhoruba na mvua ya mawe. 31Waashuru watajaa hofu watakaposikia sauti ya Mwenyezi-Mungu wakati atakapowachapa na fimbo yake. 32Kila pigo la adhabu ya Mwenyezi-Mungu juu ya Waashuru litaandamana na mdundo wa ngoma na zeze. Yeye mwenyewe binafsi atapigana na Waashuru. 33Naam, mahali pa kumteketeza mfalme wa Ashuru pamekwisha tayarishwa muda mrefu uliopita. Mahali penyewe ni shimo kubwa na pana. Moto upo na kuni kwa wingi. Mwenyezi-Mungu ataupulizia pumzi yake kama kijito cha madini ya kiberiti na kuuwasha.

Isaya30;1-33

Biblia Habari Njema kwa Watu Wote(BHN)

"Swahili Na Waswahili"Mbarikiwe.