Swahili na Waswahili

Swahili na Waswahili
Waswahili na Mswahili Rachel Siwa...Pamoja Daima!!

Thursday 10 October 2019

Kikombe Cha Asubuhi;Isaya 30....


Shalom,Habari za Asubuhi,Hamjambo,Mmeamkaje?

Tumshukuru Mungu katika yote....

Mungu wetu Baba yetu,Muumba wetu Muumba wa Mbingu na Nchi
Muumba wa vyote vilivyomo vinavyoonekana na visivyoonekana
Mungu wa walio hai,Mungu  mwenye huruma,Mungu wa upendo
Mungu wa Abrahamu,Isaka na Yakobo...
Asante kwa wema na fadhili zako kwetu
Asante kwa ulinzi wako kwetu wakati wote
Asante kwa kutuchagua tena na kutupa
kibali cha kuendelea kuiona leo hii
Asante kwa pumzi/uzima,afya na kuwatayari kwa majukumu yetu

Neema yako yatutosha ee Mungu wetu....!!

Kisha mfalme Daudi akaingia ndani ya hema na kuketi mbele ya Mwenyezi-Mungu, halafu akaomba, “Mimi ni nani, ee Mwenyezi-Mungu, na nyumba yangu ni nini hata unitukuze hivi? Isitoshe, umenifanyia mengine zaidi: Umenitolea ahadi juu ya vizazi vyangu vijavyo ee Mwenyezi-Mungu! Nikuambie nini zaidi, mimi Daudi mtumishi wako, kwa kunitukuza hivyo? Wewe unanijua mimi mtumishi wako.
Baba wa Mbinguni tunakuja mbele zako tukijinyenyekeza,tukijishusha na kujiachilia mikononi mwako
Mungu wetu tunaomba utusamehe dhambi zetu zote 
Baba wa Mbinguni nasi tunaomba ukatupe neema
ya kuweza kuwasamehe wale wote waliotukosea
Usitutie majaribuni Mungu wetu tunaomba utuepushe
na yule mwovu na kazi zake zote
Jehovah ututakase miili yetu na akili zetu
Baba wa Mbinguni tunaomba utufunike kwa Damu
ya Bwana na Mwokozi wetu Yesu Kristo wa Nazareti
yeye aliteseka kwanza ili sisi tupate kupona....

Ee Mwenyezi-Mungu, kwa ajili ya mtumishi wako na kwa kufuatana na moyo wako mwenyewe, umeyatenda hayo makuu yote, ili yajulikane hayo matendo makuu yote. Hakuna mwingine kama wewe, ee Mwenyezi-Mungu, na yote tunayoyasikia yanathibitisha kwamba hakuna Mungu mwingine ila wewe.
Mungu wetu tunaomba ukabariki kazi za mikono yetu
Baba wa Mbinguni tunaomba ukatupe ubunifu na maarifa katika utendaji
Jehovah nasi tukatende sawasawa na mapenzi yako
Yahweh tunaomba ukabariki ridhiki zetu ziingiazo/zitokazo
Mungu wetu nasi tunaomna ukatupe neema ya kuweza kuwabariki wenye kuhitaji
Tusipungukiwe katika mahitaji yetu
Baba wa Mbinguni tunaomba ukatupe kama inavyokupendeza wewe...


Yahweh tunayaweka maisha yetu mikononi mwako
Mungu wetu tunaomba ukabariki nyumba/ndoa zetu,
Jehovah tunaomba ulinzi wako kwetu na kwa vyote tunavyovimiliki
Yahweh tunaomba ukatubariki tuingiapo/tutokapo
Mungu wetu tunaomba ukavibariki vyote tunavyoenda kugusa/kutumia
Baba wa Mbinguni ukavitakase kwa Damu ya Bwana wetu Yesu Kristo
Mungu wetu ukatamalaki na kutuatamia
Baba wa Mbinguni tukawe salama rohoni
Yahwe ukatupe akili ya kutambua mema na mabaya
Mfalme wa amani amani yako ikatawale katika maisha yetu
Mungu wetu ukatupe macho ya kuona,masikio ya kusikia sauti yako na kuitii..
Baba wa Mbinguni  tunaomba ukatupe neema ya kufuata
njia zako,tukasimamie Neno lako,amri na sheria zako
siku zote za maisha yetu...
Ukatuguse kwa mkono wako wenye nguvu,ukatufanye chombo chema
ee Mungu wetu nasi tukatumike kama inavyokupendeza wewe
Roho Mtakatifu akatuongoze katika yote na tukawe na kiasi....

Tena ni watu gani duniani ambao wanaweza kulinganishwa na watu wako wa Israeli ambao peke yao Mungu wao alikwenda kuwakomboa ili wawe watu wake? Wewe ulijifanyia jina kwa kutenda mambo makubwa na ya ajabu hapo ulipoyafukuza mataifa mbele ya watu wako ambao uliwakomboa kutoka Misri. Hata umejifanyia watu wako wa Israeli kuwa watu wako milele; nawe ee Mwenyezi-Mungu, umekuwa Mungu wao.
Tazama watoto wako wenye shida/tabu,wote wanaopitia magumu/majaribu mbalimbali
Mungu wetu tunaomba ukawaguse kwa mkono wako wenye nguvu
kila mmoja na mahitaji yake
Mungu wetu tunaomba ukawasamehe pale walipo kwenda kinyume nawe
Yahweh tunaomba ukawape neema ya kuweza kujiombea,kufuata njia zako nazo zikawaweke huru...
Baba wa Mbinguni tunayaweka haya yote mikononi mwako
Kwakuwa Ufalme ni wako Nguvu na Utukufu hata Milele...
Amina...!!


Asanteni sana wapendwa katika Kristo Yesu kwakuwa nami,Baba wa Mbinguni aendelee kuwatendea sawasawa na mapenzi yake...
Nawapenda.



1Mwenyezi-Mungu asema hivi:
“Ole wao watoto wanaoniasi,
wanaotekeleza mipango yao na si mipango yangu,
wanaofanya mikataba kinyume cha matakwa yangu!
Naam, wanarundika dhambi juu ya dhambi.
2Bila kunitaka shauri, wanafunga safari kwenda Misri,
kukimbilia usalama katika ulinzi wa Farao,
kupata mahali pa usalama nchini Misri.
3Lakini ulinzi wa Farao utakuwa aibu yenu,
na usalama nchini Misri utakuwa fedheha yenu.
4Maana ingawa maofisa wao wamefika Soani,
na wajumbe wao mpaka Hanesi,
5wote wataaibishwa na hao wasioweza kuwasaidia,
watu ambao hawawezi kuwapa msaada au faida,
ila tu kuwapa aibu na fedheha.”
6Kauli ya Mungu juu ya wanyama wa pande za Negebu:30:6 Negebu: Au, kusini. Namna nyingine ya kutaja Misri.
“Wajumbe wanapita katika nchi ya taabu na shida,
yenye simba, nyoka wa sumu na majoka.
Wamewabebesha wanyama wao mali zao,
kuwapelekea watu wasioweza kuwafaa kitu.
7Maana msaada wa Misri ni bure, haufai kitu;
kwa hiyo nimeipanga Misri jina:
‘Joka30:7 Joka: Kiebrania: Rahabu. lisilo na nguvu!’”
Watu wasiotii
8Mungu aliniambia:
“Sasa chukua kibao cha kuandikia,
uandike jambo hili mbele yao,
liwe ushahidi wa milele:
9Watu hawa ni waasi, watoto wasioaminika;
watu wasiopenda kusikia mafunzo ya Mwenyezi-Mungu.
10Huwaambia waonaji: ‘Msione maono’,
na manabii: ‘Msitutangazie ukweli,
bali tuambieni mambo ya kupendeza,
toeni unabii wa mambo ya udanganyifu tu.
11Geukeni na kuiacha njia ya ukweli;
msituambie tena juu ya Mungu, Mtakatifu wa Israeli.’”
12Kwa hiyo Mungu, Mtakatifu wa Israeli asema:
“Nyinyi mmeukataa ujumbe wangu;
mkapania kufanya dhuluma na udanganyifu.
13Basi, dhambi hii itawaleteeni maangamizi
kama ufa mkubwa katika ukuta mrefu;
utabomoka mara na kuanguka chini ghafla.
14Kuporomoka kwa ukuta huo,
ni kama kupasuka kwa chungu
ambacho kimepasuliwa vibaya sana,
bila kusalia kigae cha kuchukulia moto mekoni,
au kuchotea maji kisimani.”
15Bwana Mungu, Mtakatifu wa Israeli, asema:
“Mkinirudia na kutulia mtaokolewa;
kwa utulivu na kunitumainia mtapata nguvu.”
Lakini nyinyi hamkutaka.
16Badala yake mlisema,
“La! Sisi tutakimbia na farasi wenye mbio.”
Sawa, mtakimbia na farasi wenye mbio,
lakini farasi wa maadui zenu wana mbio zaidi.
17Watu wenu elfu moja watamkimbia askari mmoja adui;
na askari watano maadui watawakimbizeni nyote.
Mwishowe, watakaosalia
watakuwa kama mlingoti wa bendera mlimani,
kama alama iliyo juu ya kilima.
Wakati wa wokovu
18Hata hivyo, Mwenyezi-Mungu anangoja awafadhili,
atainuka na kuwaonea huruma.
Maana, Mwenyezi-Mungu ni Mungu atendaye haki.
Heri wote wale wanaomtumainia.
19Enyi watu wa Siyoni, enyi watu wa Yerusalemu, hakika nyinyi hamtaomboleza tena. Kweli Mungu atawahurumia; mara tu atakaposikia kilio chenu atawaitikeni. 20Ingawa Bwana atawalisha taabu na kuwanywesha dhiki, yeye ndiye Mwalimu wenu na hatajificha tena; nanyi mtamwona kwa macho yenu wenyewe. 21Mkienda kulia au kushoto, mtasikia sauti nyuma yenu ikisema, “Njia ni hii; ifuateni.” 22Mtavifanya haramu vinyago vyenu vya miungu vilivyopakwa fedha na sanamu zenu zilizopakwa dhahabu. Mtazitupilia mbali kama vitu najisi, mkisema, “Poteleeni mbali!” 23Mtakapopanda mbegu zenu, Mwenyezi-Mungu atanyesha mvua kwa wakati wake, nazo zitakua na kuwapa mavuno mengi. Mifugo yenu nayo itapata malisho kwa wingi. 24Mafahali na punda wenu wa kulimia watapata malisho yaliyochambuliwa vizuri na kutiwa chumvi. 25Wakati utakapofika ambapo maadui watauawa na ngome zao kubomolewa, vijito vya maji vitatiririka kutoka kila mlima na kilima. 26Tena mwezi utawaka kama jua, nao mwanga wa jua utakuwa mara saba ya mwanga wake wa kawaida, kana kwamba mwanga wa siku saba umeangaza katika siku moja. Mambo haya yote yatatukia wakati Mwenyezi-Mungu atakapoyafunga na kuyaponya majeraha aliyowaletea watu wake.
Mungu ataiadhibu nchi ya Ashuru
27Tazameni, Mwenyezi-Mungu mwenyewe anakuja toka mbali!
Amewaka hasira na moshi wafuka;
midomo yake yaonesha ghadhabu yake,
maneno anayosema ni kama moto uteketezao.
28Pumzi yake ni kama mafuriko ya mto
ambao maji yake yanafika hadi shingoni.
Anakuja kuyachekecha mataifa kwa chekecheke ya maangamizi,
kuwafunga lijamu na kuwapeleka wasikotaka.
29Lakini nyinyi watu wa Yerusalemu mtaimba kwa furaha kama mfanyavyo wakati wa mkesha wa sikukuu. Mtajaa furaha kama watu wanaotembea kwa mdundo wa muziki wa filimbi kwenda mlimani kwa Mwenyezi-Mungu, Mwamba wa Israeli.
30Mwenyezi-Mungu atawafanya watu wote waisikie sauti yake tukufu na pigo la nguvu yake lionekane kwa hasira nyingi. Kutakuwa na ndimi za moto mkali, ngurumo, dhoruba na mvua ya mawe. 31Waashuru watajaa hofu watakaposikia sauti ya Mwenyezi-Mungu wakati atakapowachapa na fimbo yake. 32Kila pigo la adhabu ya Mwenyezi-Mungu juu ya Waashuru litaandamana na mdundo wa ngoma na zeze. Yeye mwenyewe binafsi atapigana na Waashuru. 33Naam, mahali pa kumteketeza mfalme wa Ashuru pamekwisha tayarishwa muda mrefu uliopita. Mahali penyewe ni shimo kubwa na pana. Moto upo na kuni kwa wingi. Mwenyezi-Mungu ataupulizia pumzi yake kama kijito cha madini ya kiberiti na kuuwasha.

Isaya30;1-33

Biblia Habari Njema kwa Watu Wote(BHN)

"Swahili Na Waswahili"Mbarikiwe.

Wednesday 9 October 2019

Kikombe Cha Asubuhi;Isaya 29....

Shalom,Habari za Asubuhi,Hamjambo,Mmeamkaje?

Tumshukuru Mungu wetu katika yote...

Asante  Mungu wetu kwa wema na fadhili zako kwetu
Asante kwa ulinzi wako kwetu wakati wote
Asante kwa kutuchagua tena na kutupa
kibali cha kuendelea kuiona leo hii
Asante kwa pumzi/uzima,afya na kuwatayari kwa majukumu yetu


Utukuzwe ee Mungu wetu,usifiwe Baba wa Mbinguni

Neema yako yatutosha  Mungu wetu..!

Kwa hiyo basi, mwambie mtumishi wangu Daudi: ‘Mwenyezi-Mungu wa majeshi anasema hivi: Nilikutoa malishoni ulipokuwa unawachunga kondoo, ili uwe mkuu wa watu wangu Israeli. Tangu wakati huo nimekuwa pamoja nawe kokote ulikokwenda na nimewaangamiza maadui zako wote mbele yako. Nitakufanya kuwa maarufu kama wakuu wengine wa dunia.
Baba wa Mbinguni tunakuja mbele zako tukijinyenyekeza,
tukijishusha na kujiachilia mikononi mwako

Mungu wetu tunaomba utusamehe dhambi zetu zote
Baba wa Mbinguni nasi tunaomba utupe neema ya kuweza kuwasamehe wale wote waliotukosea,Usitutie majaribuni Mungu wetu tunaomba utuepushe na yule mwovu na kazi zake zote,Jehovah ututakase miili yetu na akili zetu Baba wa Mbinguni tunaomba utufunike kwa  Damu ya Bwana na Mwokozi wetu Yesu Kristo wa Nazareti,
Yeye aliteseka kwanza ili sisi tupate kupona....

Nami nitawachagulia watu wangu wa Israeli mahali pa kuishi niwapandikize, ili waishi mahali pao wenyewe, wasisumbuliwe tena. Nao watu wakatili wanaotumia nguvu hawatawatesa tena kama hapo awali, tangu wakati nilipowateua waamuzi juu ya watu wangu Israeli; mimi nitawashinda maadui zako wote. Zaidi ya yote, mimi Mwenyezi-Mungu nakutangazia kuwa nitakujengea nyumba.
Mungu wetu tunaomba ukabariki kazi za mikono yetu
Baba wa Mbinguni tunaomba ukatupe ubunifu na maarifa 
katika utendaji
Jehovah nasi tukatende sawasawa na mapenzi yako
Baba wa Mbinguni tunaomba ukabariki ridhiki zetu
ziingiazo/zitokazo
Mungu wetu nasi tunaomba ukatupe neema ya kuweza
kuwabariki wenye kuhitaji
Yahweh tusipungukiwe katika mahitaji yetu
Mungu wetu ukatupe kama inavyokupendeza wewe



Jehovah tunayaweka maisha yetu mikononi mwako
Baba wa Mbinguni tunaomba ukabariki nyumba/ndoa zetu,
watoto,wazazi wetu,familia/ndugu na wote wanaotuzunguka
Jehovah tunaomba ulinzi wako kwetu na kwa vyote tunavyo vimiliki
Yahweh tunaomba ukatubariki tuingiapo/tutokapo
Mungu wetu tunaomba ukavibariki vyote tunavyoenda kugusa/kutumia
Baba wa Mbinguni ukavitakase kwa Damu ya Bwana wetu Yesu Kristo
Mungu wetu ukatamalaki na kutuatamia
Baba wa Mbinguni tukawe salama rohoni
Mfalme wa amani amani yako ikatawale katika maisha yetu
Mungu wetu ukatupe macho ya kuona na masikio ya kusikia 
sauti yako na kuitii
Baba wa Mbinguni tunaomba ukatupe neema ya kufuata njia zako
Yahweh tukasimamie Neno lako amri na sheria zako siku zote 
za maisha yetu

Mungu  wetu ukaonekane katika maisha yetu popote tupitapo na ikajulikane kwamba upo 

Neema zako zikawe nasi Nuru yako ikaangaze katika maisha yetu
Ukatufanye barua njema ee Mungu wetu nasi tukasomeke kama
inavyokupendeza wewe
Roho Mtakatifu akatuongoze katika yote na tukawe na kiasi...

Siku zako zitakapotimia za kujiunga na babu zako, nitamfanya mmoja wa watoto wako, wewe mwenyewe awe mfalme; nami nitauimarisha ufalme wake. Yeye ndiye atakayenijengea nyumba; nami nitahakikisha kwamba ufalme wake unadumu milele. Mimi nitakuwa baba yake, naye atakuwa mwanangu; lakini sitamwondolea fadhili zangu kama vile nilivyomwondolea Shauli aliyekutangulia. Bali nitamwimarisha katika nyumba yangu na katika ufalme wangu milele, na kiti chake cha enzi kitakuwa imara daima.’” Nathani alimwelezea Daudi mambo yote haya kulingana na maono yote.
Tazama wenye shida/tabu,Mungu wetu tunaomba
 ukawaguse kila mmoja na mahitaji yake
Baba wa Mbinguni tunaomba ukawasamehe pale walipokwenda
kinyume nawe
Mungu wetu ukawape neema ya kujiombea,macho ya rohoni,masikio yakusikia sauti yako,wakafuate njia zako nazo zikawaweke huru
Mungu wetu tunaomba ukasikie kulia kwao
Baba wa Mbinguni tunomba ukawafute machozi yao
Nuru yako ikaangaze katika maisha yao
Mungu wetu tunaomba ukawatendee sawasawa na mapenzi yako
Kwakuwa Ufalme ni wako Nguvu na Utukufu hata Milele
Amina....!!!


Wapendwa katika Kristo Yesu asanteni sana
kwakuwanami/kunisoma

Mungu Baba aendelee kuwabariki na kuwatendea
kama inavyompendeza yeye
Amani ya Bwana wetu Yesu Kristo na upendo wa Mungu Baba
ukae nanyi daima....

Nawapenda.


Ujumbe dhidi ya Yerusalemu
1Ole wako Yerusalemu, madhabahu ya Mungu;29:1 madhabahu ya Mungu; ni tafsiri ya neno la Kiebrania Arieli ambalo katika Ezekieli 43:15,16 linamaanisha sehemu ya juu ya madhabahu. Arieli hapa ni jina la kishairi la Yerusalemu!
mji ambamo Daudi alipiga kambi yake!
Miaka yaja na kupita,
na sikukuu zako zaendelea kufanyika;
2lakini mimi Mungu nitauhuzunisha Yerusalemu,
nako kutakuwa na vilio na maombolezo,
mji wenyewe utakuwa kama madhabahu
iliyolowa damu ya watu waliouawa.
3Mimi nitapanga jeshi dhidi ya Yerusalemu,
nami nitauzingira na kuushambulia.
4Utaangushwa mbali sana ndani ya ardhi;
kutoka huko mbali utatoa sauti;
maneno yako yatatoka huko chini mavumbini;
sauti yako itatoka ardhini kama ya mzimu.
5Kundi la maadui zako litakuwa kama vumbi laini,
waliokutendea ukatili watakuwa kama makapi.
Hayo yatafanyika ghafla.
6Mwenyezi-Mungu wa majeshi atakuja kukusaidia;
atakuja na ngurumo, tetemeko la ardhi na sauti kubwa;
atakuja na kimbunga, tufani na moto uunguzao.
7Hapo, kundi la mataifa yote yanayoshambulia Yerusalemu,
wote wanaoshambulia ngome yake na kuutia wasiwasi,
watatoweka kama ndoto, kama maono ya usiku.
8Mataifa yote yanayoushambulia mji wa Yerusalemu
yatakuwa kama mtu mwenye njaa anayeota anakula
lakini aamkapo bado anaumwa na njaa!
Au mtu mwenye kiu anayeota kuwa anakunywa,
lakini anaamka mdhaifu, bado ana kiu.
Hatari ya kupuuza maonyo
9Endeleeni kuwa wapumbavu na kuduwaa!
Jipofusheni na kuwa vipofu!
Leweni lakini si kwa divai;
pepesukeni lakini si kwa pombe.
10Mwenyezi-Mungu amewamiminia hali ya usingizi mzito;
ameyafumba macho yenu enyi manabii,
amefunika vichwa vyenu enyi waonaji.
11Basi, kwenu nyinyi maono yote haya ni kama ujumbe ulioandikwa katika kitabu kilichofungwa kwa mhuri. Ukimpelekea mtu yeyote ajuaye kusoma, ukamwambia, “Hebu nisomee kitabu hiki,” atasema, “Siwezi kukisoma kwani kimefungwa kwa mhuri.” 12Na ukimpa mtu yeyote asiyejua kusoma, ukamwambia, “Hebu nisomee kitabu hiki,” atakuambia, “Sijui kusoma.”
13 29:13 Taz Mat 15:8-9 Marko 7:6-7 Bwana asema,
“Watu hawa huja kuniabudu kwa maneno matupu,
hali mioyo yao iko mbali nami.
Wananiheshimu kulingana na mapokeo ya watu tu,
jambo walilojifunza wao wenyewe.
14Hivyo, nitawatenda tena watu hawa maajabu,
mambo ya ajabu na ya kushangaza.
Nao wenye hekima wao wataishiwa hekima,
na busara ya wenye busara wao itatoweka.
Tumaini siku za usoni
15“Ole mnaomficha Mwenyezi-Mungu mipango yenu,
mnaotenda matendo yenu gizani
na kusema: ‘Hamna atakayetuona;
nani awezaye kujua tunachofanya?’
16 29:16 Taz Isa 45:9; Rom 9:20 Nyinyi mnafanya mambo kinyume kabisa!
Je, mfinyanzi na udongo ni hali moja?
Chombo hakiwezi kumwambia aliyekitengeneza:
‘Wewe hukunitengeneza.’
Kilichofinyangwa hakiwezi kumwambia aliyekiumba,
‘Wewe hujui chochote.’”
Marekebisho makubwa
17Bado kidogo tu,
msitu wa Lebanoni utageuzwa kuwa shamba lenye rutuba,
na shamba lenye rutuba kuwa msitu.
18Siku hiyo viziwi watasikia ujumbe ukisomwa kitabuni
na kutoka gizani vipofu wataanza kuona.
19Wanyofu watapata furaha mpya kwa Mwenyezi-Mungu,
na maskini wa watu watashangilia kwa furaha
kwa sababu ya Mungu, Mtakatifu wa Israeli.
20Majitu makatili yataangamizwa,
wenye kumdhihaki Mungu watakwisha,
wote wanaootea kutenda maovu watatokomezwa.
21Watatoweka wale wanaopotosha kesi ya mtu mahakamani,
watu wanaowafanyia hila mahakimu
na wasemao uongo kuwanyima haki yao wasio na hatia.
22Kwa hiyo, Mwenyezi-Mungu aliyemkomboa Abrahamu,
asema hivi kuhusu wazawa wa Yakobo:
“Wazawa wa Yakobo hawataaibishwa tena,
hawatainamisha vichwa vyao tena kwa aibu.
23Watakapowaona watoto wao,
watoto niliowajalia mimi mwenyewe,
watalitukuza jina langu mimi Mtakatifu wa Yakobo;
watakuwa na uchaji kwangu mimi Mungu wa Israeli.
24Waliopotoka rohoni watapata maarifa
na wenye kununa watakubali kufunzwa.”

Isaya29;1-24

Biblia Habari Njema kwa Watu Wote(BHN)

"Swahili Na Waswahili"Mbarikiwe.

Tuesday 8 October 2019

Kikombe Cha Asubuhi;Isaya 28....


Shalom,Habari za Asubuhi,Hamjambo,Mmeamkaje?

Tumshukuru Mungu katika yote....

Mungu wetu Baba yetu,Muumba wetu Muumba wa Mbingu na Nchi
Muumba wa vyote vilivyomo vinavyoonekana na visivyoonekana
Mungu wa walio hai,Mungu  mwenye huruma,Mungu wa upendo
Mungu wa Abrahamu,Isaka na Yakobo...
Asante kwa wema na fadhili zako kwetu
Asante kwa ulinzi wako kwetu wakati wote
Asante kwa kutuchagua tena na kutupa
kibali cha kuendelea kuiona leo hii
Asante kwa pumzi/uzima,afya na kuwatayari kwa majukumu yetu

Neema yako yatutosha ee Mungu wetu....!!

Wakati mfalme Daudi alipokuwa akikaa katika ikulu, siku moja alimwita nabii Nathani, na kumwambia, “Hebu tazama, mimi ninakaa kwenye nyumba nzuri iliyojengwa kwa mwerezi, lakini sanduku la agano la Mwenyezi-Mungu linakaa hemani.” Nathani akamwambia Daudi, “Fanya chochote unachofikiria moyoni mwako, kwa kuwa Mungu yu pamoja nawe.”
Baba wa Mbinguni tunakuja mbele zako tukijinyenyekeza,tukijishusha na kujiachilia mikononi mwako
Mungu wetu tunaomba utusamehe dhambi zetu zote 
Baba wa Mbinguni nasi tunaomba ukatupe neema
ya kuweza kuwasamehe wale wote waliotukosea
Usitutie majaribuni Mungu wetu tunaomba utuepushe
na yule mwovu na kazi zake zote
Jehovah ututakase miili yetu na akili zetu
Baba wa Mbinguni tunaomba utufunike kwa Damu
ya Bwana na Mwokozi wetu Yesu Kristo wa Nazareti
yeye aliteseka kwanza ili sisi tupate kupona....

Lakini usiku uleule, neno la Mwenyezi-Mungu lilimjia Nathani, kusema, “Nenda ukamwambie mtumishi wangu Daudi, ‘Mwenyezi-Mungu anasema hivi: Wewe hutanijengea nyumba ya kukaa.
Mungu wetu tunaomba ukabariki kazi za mikono yetu
Baba wa Mbinguni tunaomba ukatupe ubunifu na maarifa katika utendaji
Jehovah nasi tukatende sawasawa na mapenzi yako
Yahweh tunaomba ukabariki ridhiki zetu ziingiazo/zitokazo
Mungu wetu nasi tunaomna ukatupe neema ya kuweza kuwabariki wenye kuhitaji
Tusipungukiwe katika mahitaji yetu
Baba wa Mbinguni tunaomba ukatupe kama inavyokupendeza wewe...


Yahweh tunayaweka maisha yetu mikononi mwako
Mungu wetu tunaomba ukabariki nyumba/ndoa zetu,
Jehovah tunaomba ulinzi wako kwetu na kwa vyote tunavyovimiliki
Yahweh tunaomba ukatubariki tuingiapo/tutokapo
Mungu wetu tunaomba ukavibariki vyote tunavyoenda kugusa/kutumia
Baba wa Mbinguni ukavitakase kwa Damu ya Bwana wetu Yesu Kristo
Mungu wetu ukatamalaki na kutuatamia
Baba wa Mbinguni tukawe salama rohoni
Yahwe ukatupe akili ya kutambua mema na mabaya
Mfalme wa amani amani yako ikatawale katika maisha yetu
Mungu wetu ukatupe macho ya kuona,masikio ya kusikia sauti yako na kuitii..
Baba wa Mbinguni  tunaomba ukatupe neema ya kufuata
njia zako,tukasimamie Neno lako,amri na sheria zako
siku zote za maisha yetu...
Ukatuguse kwa mkono wako wenye nguvu,ukatufanye chombo chema
ee Mungu wetu nasi tukatumike kama inavyokupendeza wewe
Roho Mtakatifu akatuongoze katika yote na tukawe na kiasi....

Tangu wakati ule nilipowaongoza watu wa Israeli kutoka Misri mpaka hivi leo, sijaishi kwenye nyumba. Nimekuwa nikihama toka hema hadi hema, na toka makao hadi makao mengine. Je, kila mahali ambako nimekwenda na Waisraeli, nimepata kumwuliza mwamuzi wao yeyote niliyemwamuru awachunge watu wangu, “Kwa nini hukunijengea nyumba ya mierezi?” ’
Tazama watoto wako wenye shida/tabu,wote wanaopitia magumu/majaribu mbalimbali
Mungu wetu tunaomba ukawaguse kwa mkono wako wenye nguvu
kila mmoja na mahitaji yake
Mungu wetu tunaomba ukawasamehe pale walipo kwenda kinyume nawe
Yahweh tunaomba ukawape neema ya kuweza kujiombea,kufuata njia zako nazo zikawaweke huru...
Baba wa Mbinguni tunayaweka haya yote mikononi mwako
Kwakuwa Ufalme ni wako Nguvu na Utukufu hata Milele...
Amina...!!


Asanteni sana wapendwa katika Kristo Yesu kwakuwa nami,Baba wa Mbinguni aendelee kuwatendea sawasawa na mapenzi yake...
Nawapenda.

Onyo kwa ufalme wa kaskazini
1Ole wenye majivuno na walevi wa Efraimu,
fahari yake inatoweka kama ua linalonyauka!
Naam, fahari iliyotawala bondeni kwenye rutubarutuba;
na vichwani kwao walio watu walevi kupindukia!
2Bwana amejichagulia mtu wake shujaa na mwenye nguvu,
ambaye ni kama mvua ya mawe na dhoruba kali,
kama tufani ya mafuriko makubwa;
kwa mkono wake atawatupa chini ardhini.
3Majivuno na fahari ya walevi wa Efraimu
yatakanyagwakanyagwa ardhini,
4fahari yake inatoweka kama ua linalonyauka;
fahari iliyotawala bondeni kwenye rutuba
itakuwa kama tini za mwanzo kabla ya kiangazi;
mtu akiziona huzichuma na kuzila mara moja.
5Siku ile Mwenyezi-Mungu wa majeshi atakuwa taji tukufu,
kama kilemba kizuri kwa watu wake watakaobaki hai.
6Waamuzi mahakamani atawaongoza kutenda haki,
nao walinzi wa mji atawapa nguvu.
Isaya na manabii walevi wa Yuda
7Lakini wako wengine waliolewa divai
na kuyumbayumba kwa sababu ya pombe;
naam, makuhani na manabii wamelewa mvinyo,
wamevurugika kwa divai.
Wanayumbayumba kwa pombe kali;
maono yao yamepotoka,
wanapepesuka katika kutoa hukumu.
8Meza zote zimetapakaa matapishi,
hakuna mahali popote palipo safi.
9Wao wananidhihaki na kuuliza:
“Huyu nabii ataka kumfundisha nani?
Je, anadhani atatueleza sisi ujumbe wake?
Je, sisi ni watoto wachanga
walioachishwa kunyonya juzijuzi?
10Anatufundisha kama watoto wadogo:
Sheria baada ya sheria,
mstari baada ya mstari;
mara hiki, mara kile!”
11 28:11-12 Taz 1Kor 14:21 Haya basi!
Mwenyezi-Mungu ataongea na watu hawa
kwa njia ya watu wa lugha tofauti
wanaoongea lugha ngeni.
12Hata hivyo yeye alikuwa amewaahidi:
“Nitawaonesheni pumziko,
nitawapeni pumziko enyi mliochoka.
Hapa ni mahali pa pumziko.”
Lakini wao hawakutaka kunisikiliza.
13Kwa hiyo kwao neno la Mwenyezi-Mungu litakuwa tu:
Sheria sheria, mstari mstari;
mara hiki, mara kile!
Nao watalazimika kukimbia
lakini wataanguka nyuma;
watavunjika, watanaswa na kutekwa.
Jiwe la msingi Siyoni
14Basi, sikilizeni neno la Mwenyezi-Mungu,
enyi wenye madharau mnaotawala watu wa Yerusalemu,
15“Nyinyi mnajidai mmefanya mkataba na kifo,
mmefanya mapatano na Kuzimu!
Nyinyi mwasema eti balaa lijapo halitawapata,
kwa sababu mmefanya uongo kuwa tegemeo lenu,
na udanganyifu kuwa kinga yenu!”
16 28:16 Taz Zab 118:22-23; Rom 9:33; 10:11; 1Pet 2:6 Basi, hivi ndivyo asemavyo Mwenyezi-Mungu:
“Tazama! Naweka mjini Siyoni jiwe la msingi,
jiwe ambalo limethibitika.
Jiwe la pembeni, la thamani,
jiwe ambalo ni la msingi thabiti;
jiwe lililo na maandishi haya:
‘Anayeamini hatatishika.’
17Nitatumia haki kama kipimo changu,
nitatumia uadilifu kupimia.”
Mvua ya mawe itaufagilia mbali uongo mnaoutegemea,
na mafuriko yataharibu kinga yenu.
18Hapo mkataba wenu na kifo utabatilishwa,
na mapatano yenu na Kuzimu yatafutwa.
Janga lile kuu litakapokuja
litawaangusheni chini.
19Kila litakapopitia kwenu litawakumba;
nalo litapita kila asubuhi, mchana na usiku.
Kusikia ujumbe huu tu kutakuwa kitisho.
20Kwenu itakuwa kama ajinyoshaye juu ya kitanda kifupi mno,
au kujifunika kwa blanketi lililo dogo mno!
21 28:21 Taz Yos 10:10-12; 2Sam 5:20; 1Nya 14:11 Maana Mwenyezi-Mungu atainuka kama kule mlimani Perazimu;
atawaka hasira kama kule bondeni Gibeoni.
Atatekeleza mpango wake wa ajabu;
atatenda kazi yake ya kustaajabisha.
22Basi, nyinyi msiwe na madharau
vifungo vyenu visije vikakazwa zaidi.
Maana nimesikia kuwa Mwenyezi-Mungu wa majeshi
ameazimia kuiangamiza nchi yote.
Hekima ya Mungu
23Tegeni sikio msikilize ninayowaambieni;
sikilizeni kwa makini hotuba yangu.
24Je, alimaye ili kupanda hulima tu?
Je, huendelea kulima na kusawazisha shamba lake?
25La! Akisha lisawazisha shamba lake,
hupanda mbegu za bizari na jira,
akapanda ngano na shayiri katika safu,
na mipakani mwa shamba mimea mingineyo.
26Mtu huyo huwa anajua la kufanya,
kwa sababu Mungu wake humfundisha.
27Bizari haipurwi kwa mtarimbo
wala jira kwa gari la ng'ombe!
Ila bizari hupurwa kwa kijiti
na jira kwa fimbo.
28Mkulima apurapo ngano yake,
haendelei kuipura mpaka kuvunja punje zake.
Anajua jinsi ya kuipura kwa gurudumu,
bila kuziharibu punje za ngano.
29Ujuzi huu nao watoka kwa Mwenyezi-Mungu wa majeshi.
Mipango yake Mungu ni ya ajabu,
hekima yake ni kamilifu kabisa.

Isaya28;1-29

Biblia Habari Njema kwa Watu Wote(BHN)

"Swahili Na Waswahili"Mbarikiwe.

Monday 7 October 2019

Kikombe Cha Asubuhi;Isaya 27....


Shalom,Habari za Asubuhi,Hamjambo,Mmeamkaje?

Haleluyah ni siku/wiki nyingine tena Mungu wetu ametuchagua

na kutupa kibali cha kuendelea kuiona leo hii
Si kwamba sisi tumetenda mema sana wala si kwa nguvu zetu
si kwa utashi wetu wala si kwa akili zetu si kwamba sisi
ni wazuri mno si kwa uwezo wetu sisi kuwa hivi tulivyo leo hii
Ni kwa rehema/neema zake ni kwa mapenzi yake Mungu wetu....

Tumshukuru Mungu wetu katika yote...

Asante Mungu wetu kwa wema na fadhili zako kwetu

Asante kwa ulinzi wako kwetu wakati wote
Asante kwa pumzi/uzima,afya na kuwa tayari kwa majukumu yetu
Sifa na Utukufu tunakurudshia Mungu wetu....!!

Bwana, ni nani asiyekucha wewe? Nani asiyelitukuza jina lako? Wewe peke yako ni Mtakatifu. Mataifa yote yatakujia na kukuabudu maana matendo yako ya haki yamedhihirishwa.”
Tazama jana imepita ee Mungu wetu leo ni siku mpya na kesho ni siku nyingine Jehovah tunakuja mbele zako tukijinyenyekeza,tukijishusha na kujiachilia mikononi mwako
 Mungu wetu tunaomba utusamehe dhambi zetu zote tulizozifanya kwakuwaza,kwakunena,kwakutenda,kwakujua/kutojua
Baba wa Mbinguni nasi tunaomba utupe neema ya kuweza kuwasamehe wale wote waliotukosea
Jehovah usitutie majaribu Mungu wetu tunaomba utuepushe na yule mwovu na kazi zake zote
Yahweh tunaomba ututakase miili yetu na akili zetu
Baba wa Mbinguni utufunike kwa Damu ya Bwana na Mwokozi wetu Yesu Kristo wa Nazareti
yeye aliteseka kwanza ili sisi tupate kupona
Kwakupigwa kwake sisi tumepata kupona....

Baada ya hayo nikaona hekalu limefunguliwa mbinguni, na ndani yake hema ya kuwapo kwa Mungu. Basi, wale malaika saba wenye mabaa saba wakatoka humo hekaluni, wakiwa wamevaa nguo za kitani safi zenye kung'aa na kanda za dhahabu vifuani mwao.
Yahweh tunaomba ukabariki kazi za mikono yetu
Baba wa Mbinguni tunaomba ukatupe ubunifu na maarifa 
katika utendaji
Jehovah nasi tukatende sawasawa na mapenzi yako
Baba wa Mbinguni tunaomba ukabariki ridhiki zetu
ziingiazo/zitokazo
Mungu wetu nasi tunaomba ukatupe neema ya kuweza
kuwabariki wenye kuhitaji
Yahweh tusipungukiwe katika mahitaji yetu
Mungu wetu ukatupe kama inavyokupendeza wewe

Baba wa Mbinguni tunayaweka maisha yetu mikononi mwako
Mungu wetu tunaomba ukabariki nyumba/ndoa zetu,
watoto,wazazi wetu,familia/ndugu na wote wanaotuzunguka
Jehovah tunaomba ulinzi wako kwetu na kwa vyote tunavyo vimiliki
Yahweh tunaomba ukatubariki tuingiapo/tutokapo
Mungu wetu tunaomba ukavibariki vyote tunavyoenda kugusa/kutumia
Baba wa Mbinguni ukavitakase kwa Damu ya Bwana wetu Yesu Kristo
Mungu wetu ukatamalaki na kutuatamia
Baba wa Mbinguni tukawe salama rohoni
Mfalme wa amani amani yako ikatawale katika maisha yetu
Mungu wetu ukatupe macho ya kuona na masikio ya kusikia 
sauti yako na kuitii
Baba wa Mbinguni tunaomba ukatupe neema ya kufuata njia zako
Yahweh tukasimamie Neno lako amri na sheria zako siku zote 
za maisha yetu
Mungu wetu ukaonekane katika maisha yetu
Neema zako zikawe nasi Nuru yako ikaangaze katika maisha yetu
ukatuguse kwa mkono wako wenye nguvu
Ukatufanye chombo chema ee Mungu wetu nasi tukatumike kama
inavyokupendeza wewe
Roho Mtakatifu akatuongoze katika yote na tukawe na kiasi...


Kisha, mmojawapo wa wale viumbe wanne akawapa hao malaika saba mabakuli ya dhahabu yaliyojaa ghadhabu ya Mungu, aishiye milele na milele. Hekalu likajaa moshi uliosababishwa na utukufu na nguvu ya Mungu, na hakuna mtu aliyeweza kuingia hekaluni mpaka mwisho wa mabaa saba ya wale malaika saba.
Mungu wetu tunawaweka mikononi mwako wenye shida/tabu,wote wanaopitia magumu/majaribu mbalimbali
Mungu wetu tunaomba ukawaguse kwa mkono wako wenye nguvu
 kila mmoja na mahitaji yake 
Mungu wetu tunaomba ukawasamehe pale walipokwenda kinyume nawe
Baba wa Mbinguni ukawape neema ya kujiombea,kufuata njia zako
wakasimamie Neno lako nalo likaweke huru
Mungu wetu tunaomba ukasikie kuomba kwetu
Mungu wetu ukawatendee sawasawa na mapenzi yako
Kwakuwa Ufalme ni wako Nguvu na Utukufu hata Milele
Amina...!!

Asanteni sana wapendwa katika Kristo Yesu kwakuwa nami
Mungu Baba aendelee kuwabariki na kuwatendea 
kama inavyompendeza yeye....
Nawapenda.

 Siku hiyo, Mwenyezi-Mungu atautwaa upanga wake mkubwa, mkali na imara, na kuliadhibu dude Lewiyathani27:1 Lewiyathani: Joka la kutisha katika hadithi za kale, hapa latumiwa kutajia mataifa yaliyokandamiza Israeli. joka lirukalo na danganyifu; Mwenyezi-Mungu ataliua joka liishilo baharini.
2Siku hiyo, Mwenyezi-Mungu atasema hivi:
“Imbeni utenzi wa shamba langu zuri la mizabibu!27:2 shamba la mizabibu: Mfano wa Waisraeli, watu wa Mungu.
3Mimi, Mwenyezi-Mungu, ni mkulima wake;
nalimwagilia maji kila wakati,
ninalilinda usiku na mchana,
lisije likaharibiwa na mtu yeyote.
4Silikasirikii tena shamba hili;
kama miiba na mbigili ingelilivamia,
mimi ningepambana nayo na kuichoma moto.
5Maadui za watu wangu wakitaka ulinzi wangu,
basi, na wafanye amani nami;
naam, wafanye amani nami.”
6Itakuja siku wazawa wa Yakobo watashika mizizi;
naam, watu wa Israeli watachanua na kuchipua,
na kuijaza dunia yote kwa matunda.
7Mungu hakuwaadhibu Waisraeli vikali
kama alivyowaadhibu maadui wake;
Waisraeli waliopotea vitani,
ni wachache kuliko wale wa maadui zake.
8Aliwaadhibu watu wake kwa kuwapeleka uhamishoni.
Wakati wa upepo mkali wa mashariki,
aliwaondoa kwa kipigo kikali.
9Hivi ndivyo uovu wa wazawa wa Yakobo utakavyoondolewa,
hivi ndivyo dhambi yake itakavyofutwa kabisa:
Ataziharibu madhabahu za miungu;
mawe yake yatasagwasagwa kama chokaa;
Ashera, wala madhabahu za kufukizia ubani hazitabaki.
10Mji ule wa ngome sasa umekuwa mtupu,
umeachwa na kuhamwa kama jangwa,
humo ndama wanalisha na kupumzika.
11Matawi ya miti yamekauka na kuvunjika;
kina mama huyaokota wakawashia moto.
Watu hawa hawajaelewa kitu,
kwa hiyo Mungu, Muumba wao, hatawahurumia,
yeye aliyewafanya, hatawafadhili.
12Siku hiyo, kutoka mto Eufrate hadi mpakani mwa Misri, Mwenyezi-Mungu ataipura nafaka yake, nanyi Waisraeli mtakusanywa mmojammoja. 13Siku hiyo, tarumbeta kubwa itapigwa na watu wote wa Israeli waliopotea nchini Ashuru au waliotawanywa nchini Misri watarudi na kumwabudu Mwenyezi-Mungu juu ya mlima mtakatifu huko Yerusalemu.

Isaya27;1-13

Biblia Habari Njema kwa Watu Wote(BHN)

"Swahili Na Waswahili"Mbarikiwe.