Swahili na Waswahili

Swahili na Waswahili
Waswahili na Mswahili Rachel Siwa...Pamoja Daima!!

Friday 4 October 2019

Kikombe Cha Asubuhi;Isaya 26....


Shalom,Habari za Asubuhi,Hamjambo,Mmeamkaje?

Tumshukuru Mungu wetu katika yote...

Asante  Mungu wetu kwa wema na fadhili zako kwetu
Asante kwa ulinzi wako kwetu wakati wote
Asante kwa kutuchagua tena na kutupa
kibali cha kuendelea kuiona leo hii
Asante kwa pumzi/uzima,afya na kuwatayari kwa majukumu yetu


Utukuzwe ee Mungu wetu,usifiwe Baba wa Mbinguni

Neema yako yatutosha  Mungu wetu..!

Kisha nikaona ishara nyingine mbinguni, kubwa na ya kushangaza. Palikuwa hapo malaika saba wenye mabaa saba ya mwisho. Kwa mabaa hayo saba, ghadhabu ya Mungu imekamilishwa.
Baba wa Mbinguni tunakuja mbele zako tukijinyenyekeza,tukijishusha na kujiachilia mikononi mwako
Mungu wetu tunaomba utusamehe dhambi zetu zote
Baba wa Mbinguni nasi tunaomba utupe neema ya kuweza kuwasamehe wale wote waliotukosea,Usitutie majaribuni Mungu wetu tunaomba utuepushe na yule mwovu na kazi zake zote,Jehovah ututakase miili yetu na akili zetu Baba wa Mbinguni tunaomba utufunike kwa  Damu ya Bwana na Mwokozi wetu Yesu Kristo wa Nazareti,
Yeye aliteseka kwanza ili sisi tupate kupona....

Kisha nikaona kitu kama bahari ya kioo, imechanganywa na moto. Nikawaona pia wale watu waliomshinda yule mnyama na sanamu yake na ambaye jina lake lilitajwa kwa ile tarakimu. Watu hao walikuwa wamesimama kando ya hiyo bahari ya kioo, wakiwa na vinubi walivyopewa na Mungu.
Mungu wetu tunaomba ukabariki kazi za mikono yetu
Baba wa Mbinguni tunaomba ukatupe ubunifu na maarifa 
katika utendaji
Jehovah nasi tukatende sawasawa na mapenzi yako
Baba wa Mbinguni tunaomba ukabariki ridhiki zetu
ziingiazo/zitokazo
Mungu wetu nasi tunaomba ukatupe neema ya kuweza
kuwabariki wenye kuhitaji
Yahweh tusipungukiwe katika mahitaji yetu
Mungu wetu ukatupe kama inavyokupendeza wewe



Jehovah tunayaweka maisha yetu mikononi mwako
Baba wa Mbinguni tunaomba ukabariki nyumba/ndoa zetu,
watoto,wazazi wetu,familia/ndugu na wote wanaotuzunguka
Jehovah tunaomba ulinzi wako kwetu na kwa vyote tunavyo vimiliki
Yahweh tunaomba ukatubariki tuingiapo/tutokapo
Mungu wetu tunaomba ukavibariki vyote tunavyoenda kugusa/kutumia
Baba wa Mbinguni ukavitakase kwa Damu ya Bwana wetu Yesu Kristo
Mungu wetu ukatamalaki na kutuatamia
Baba wa Mbinguni tukawe salama rohoni
Mfalme wa amani amani yako ikatawale katika maisha yetu
Mungu wetu ukatupe macho ya kuona na masikio ya kusikia 
sauti yako na kuitii
Baba wa Mbinguni tunaomba ukatupe neema ya kufuata njia zako
Yahweh tukasimamie Neno lako amri na sheria zako siku zote 
za maisha yetu

Mungu  wetu ukaonekane katika maisha yetu popote tupitapo na ikajulikane kwamba upo 

Neema zako zikawe nasi Nuru yako ikaangaze katika maisha yetu
Ukatufanye barua njema ee Mungu wetu nasi tukasomeke kama
inavyokupendeza wewe
Roho Mtakatifu akatuongoze katika yote na tukawe na kiasi...

Walikuwa wakiimba wimbo wa Mose, mtumishi wa Mungu na wa Mwanakondoo: “Bwana Mungu Mwenye Nguvu, matendo yako ni makuu na ya ajabu mno! Ewe Mfalme wa mataifa, njia zako ni za haki na za kweli!
Tazama wenye shida/tabu,Mungu wetu tunaomba
 ukawaguse kila mmoja na mahitaji yake
Baba wa Mbinguni tunaomba ukawasamehe pale walipokwenda
kinyume nawe
Mungu wetu ukawape neema ya kujiombea,macho ya rohoni,masikio yakusikia sauti yako,wakafuate njia zako nazo zikawaweke huru
Mungu wetu tunaomba ukasikie kulia kwao
Baba wa Mbinguni tunomba ukawafute machozi yao
Nuru yako ikaangaze katika maisha yao
Mungu wetu tunaomba ukawatendee sawasawa na mapenzi yako
Kwakuwa Ufalme ni wako Nguvu na Utukufu hata Milele
Amina....!!!


Wapendwa katika Kristo Yesu asanteni sana
kwakuwanami/kunisoma

Mungu Baba aendelee kuwabariki na kuwatendea
kama inavyompendeza yeye
Amani ya Bwana wetu Yesu Kristo na upendo wa Mungu Baba
ukae nanyi daima....

Nawapenda.


Wimbo wa ushindi
1Siku ile watu wataimba wimbo huu katika nchi ya Yuda:
Sisi tuna mji imara:
Mungu anatulinda kwa kuta na ngome.
2Fungueni malango ya mji,
taifa aminifu liingie;
taifa litendalo mambo ya haki.
3Ee Mungu, wawaweka katika amani walio thabiti,
wawaweka katika amani kwa kuwa wanakutegemea.
4Mtumaini Mwenyezi-Mungu siku zote
kwa maana yeye ni mwamba wa usalama milele.
5Amewaporomosha waliokaa pande za juu,
mji maarufu ameuangusha mpaka chini,
ameutupa mpaka mavumbini.
6Sasa mji huo unakanyagwakanyagwa
kwa miguu ya watu maskini na fukara.
7Njia ya watu wanyofu ni rahisi;
ewe Mungu mwadilifu, wasawazisha njia yao.
8Katika njia ya maamuzi yako
tunakungojea ee Mwenyezi-Mungu;
kulikumbuka jina lako ndiyo tamaa yetu.
9Moyo wangu wakutamani usiku kucha,
nafsi yangu yakutafuta kwa moyo.
Utakapoihukumu dunia,
watu wote ulimwenguni watajifunza haki.
10Lakini waovu hata wakipewa fadhili,
hawawezi kujifunza kutenda haki.
Hata katika nchi ya wanyofu,
wao bado wanatenda maovu,
wala hawajali ukuu wako wewe Mwenyezi-Mungu.
11Ee Mwenyezi-Mungu umeinua mkono kuwaadhibu,
lakini maadui zako hawauoni.
Waoneshe uwapendavyo watu wako nao wataaibika.
Moto wa hasira yako uwateketeze maadui zako!
12Wewe, ee Mwenyezi-Mungu, umetupatia amani;
umefanikisha shughuli zetu zote.26:12 umefanikisha … shughuli zetu zote: Au umetutendea kadiri ya matendo yetu.
13Ee Mwenyezi-Mungu, Mungu wetu,
tulipata kutawaliwa na watu wengine na miungu yao,
lakini twakiri wewe pekee kuwa Mungu wetu.
14Watu hao wamekufa, wala hawataishi tena;
wamekuwa mizimu, wala hawatafufuka.
Maana wewe umewaadhibu na kuwaangamiza,
hakuna atakayeweza kuwakumbuka tena.
15Umelikuza taifa letu, ee Mwenyezi-Mungu,
naam, umelizidisha taifa letu.
Umeipanua mipaka yote ya nchi,
kwa hiyo wewe watukuka.
16Ee Mwenyezi-Mungu, walipotaabika walikutafuta,
walikuomba msaada ulipowaadhibu.26:16 ulipowaadhibu: Maana yake katika Kiebrania si dhahiri.
17Kama vile mama mjamzito anayejifungua
hulia na kugaagaa kwa uchungu,
ndivyo tulivyokuwa kwa sababu yako, ee Mwenyezi-Mungu.
18Sisi tulipata maumivu ya kujifungua
lakini tukajifungua tu upepo!
Hatukupata ushindi wowote kwa ajili ya nchi yetu,
hatukuweza kuongeza idadi ya watu katika nchi.
19Wafu wako wataishi tena,
miili yao itafufuka.
Wanaolala mavumbini wataamka na kuimba kwa furaha!
Mungu atapeleka umande wake wa uhai,
nao walio kwa wafu watatoka hai.
Baada ya dhiki faraja
20Njoni watu wangu, ingieni majumbani mwenu,
mkajifungie humo ndani.
Jificheni kwa muda mfupi,
mpaka ifike ghadhabu ya Mwenyezi-Mungu.
21Maana Mwenyezi-Mungu aja kutoka kwake juu,
kutoka makao yake huko mbinguni;
kuwaadhibu wakazi wa dunia kwa uovu wao.
Nayo dunia haitaficha tena wale waliouawa,
ila itaufichua umwagaji damu wote.


Isaya26;1-21

Biblia Habari Njema kwa Watu Wote(BHN)

"Swahili Na Waswahili"Mbarikiwe.

Thursday 3 October 2019

Kikombe Cha Asubuhi;Isaya 25....


Shalom,Habari za Asubuhi,Hamjambo,Mmeamkaje?

Tumshukuru Mungu katika yote....

Mungu wetu Baba yetu,Muumba wetu Muumba wa Mbingu na Nchi
Muumba wa vyote vilivyomo vinavyoonekana na visivyoonekana
Mungu wa walio hai,Mungu  mwenye huruma,Mungu wa upendo
Mungu wa Abrahamu,Isaka na Yakobo...
Asante kwa wema na fadhili zako kwetu
Asante kwa ulinzi wako kwetu wakati wote
Asante kwa kutuchagua tena na kutupa
kibali cha kuendelea kuiona leo hii
Asante kwa pumzi/uzima,afya na kuwatayari kwa majukumu yetu

Neema yako yatutosha ee Mungu wetu....!!

Mwenyezi-Mungu akamwambia Mose, “Mwambie Aroni aichukue fimbo yake na kuinyosha juu ya maji ya Misri, juu ya mito yote, mifereji, madimbwi na mabwawa yao yote, nayo yatakuwa damu. Kutakuwa na damu nchini kote, na hata katika vyombo vyote vya mbao na vya mawe.”
Baba wa Mbinguni tunakuja mbele zako tukijinyenyekeza,tukijishusha na kujiachilia mikononi mwako
Mungu wetu tunaomba utusamehe dhambi zetu zote 
Baba wa Mbinguni nasi tunaomba ukatupe neema
ya kuweza kuwasamehe wale wote waliotukosea
Usitutie majaribuni Mungu wetu tunaomba utuepushe
na yule mwovu na kazi zake zote
Jehovah ututakase miili yetu na akili zetu
Baba wa Mbinguni tunaomba utufunike kwa Damu
ya Bwana na Mwokozi wetu Yesu Kristo wa Nazareti
yeye aliteseka kwanza ili sisi tupate kupona....

Mose na Aroni wakafanya kama Mwenyezi-Mungu alivyowaamuru. Aroni aliinua fimbo yake juu mbele ya Farao na maofisa wake, akayapiga maji ya mto Nili, na maji yote mtoni yakageuka kuwa damu. Samaki wakafa, mto ukanuka vibaya sana hata Wamisri wasiweze kunywa maji yake. Nchi nzima ikajaa damu.
Mungu wetu tunaomba ukabariki kazi za mikono yetu
Baba wa Mbinguni tunaomba ukatupe ubunifu na maarifa katika utendaji
Jehovah nasi tukatende sawasawa na mapenzi yako
Yahweh tunaomba ukabariki ridhiki zetu ziingiazo/zitokazo
Mungu wetu nasi tunaomna ukatupe neema ya kuweza kuwabariki wenye kuhitaji
Tusipungukiwe katika mahitaji yetu
Baba wa Mbinguni tunaomba ukatupe kama inavyokupendeza wewe...


Yahweh tunayaweka maisha yetu mikononi mwako
Mungu wetu tunaomba ukabariki nyumba/ndoa zetu,
Jehovah tunaomba ulinzi wako kwetu na kwa vyote tunavyovimiliki
Yahweh tunaomba ukatubariki tuingiapo/tutokapo
Mungu wetu tunaomba ukavibariki vyote tunavyoenda kugusa/kutumia
Baba wa Mbinguni ukavitakase kwa Damu ya Bwana wetu Yesu Kristo
Mungu wetu ukatamalaki na kutuatamia
Baba wa Mbinguni tukawe salama rohoni
Yahwe ukatupe akili ya kutambua mema na mabaya
Mfalme wa amani amani yako ikatawale katika maisha yetu
Mungu wetu ukatupe macho ya kuona,masikio ya kusikia sauti yako na kuitii..
Baba wa Mbinguni  tunaomba ukatupe neema ya kufuata
njia zako,tukasimamie Neno lako,amri na sheria zako
siku zote za maisha yetu...
Ukatuguse kwa mkono wako wenye nguvu,ukatufanye chombo chema
ee Mungu wetu nasi tukatumike kama inavyokupendeza wewe
Roho Mtakatifu akatuongoze katika yote na tukawe na kiasi....

Lakini wachawi wa Misri kwa kutumia uchawi wao wakafanya vivyo hivyo. Kwa hiyo moyo wa Farao ukabaki kuwa mgumu, naye hakuwasikiliza Mose na Aroni; ikawa kama Mwenyezi-Mungu alivyokuwa amesema. Basi, Farao akarudi nyumbani kwake, na hata haya yaliyotokea hakuyajali. Wamisri wote wakachimbachimba kandokando ya mto Nili ili wapate maji ya kunywa, kwani hawakuweza kunywa maji ya mto huo. Pigo hilo la mto Nili lilidumu siku saba.
Tazama watoto wako wenye shida/tabu,wote wanaopitia magumu/majaribu mbalimbali
Mungu wetu tunaomba ukawaguse kwa mkono wako wenye nguvu
kila mmoja na mahitaji yake
Mungu wetu tunaomba ukawasamehe pale walipo kwenda kinyume nawe
Yahweh tunaomba ukawape neema ya kuweza kujiombea,kufuata njia zako nazo zikawaweke huru...
Baba wa Mbinguni tunayaweka haya yote mikononi mwako
Kwakuwa Ufalme ni wako Nguvu na Utukufu hata Milele...
Amina...!!


Asanteni sana wapendwa katika Kristo Yesu kwakuwa nami,Baba wa Mbinguni aendelee kuwatendea sawasawa na mapenzi yake...
Nawapenda.


Wimbo wa sifa kwa Mungu
1Wewe, ee Mwenyezi-Mungu, ndiwe Mungu wangu;
nitakutukuza na kulisifu jina lako,
kwa maana umetenda mambo ya ajabu;
waitekeleza kwa uaminifu na kweli
mipango uliyoipanga tangu zamani.
2Umeufanya mji ule kuwa rundo la mawe,
mji wenye ngome kuwa uharibifu.
Majumba ya watu wageni yametoweka,
wala hayatajengwa tena upya.
3Kwa hiyo watu wenye nguvu watakutukuza,
miji ya mataifa katili itakuogopa.
4Maana wewe umekuwa ngome kwa maskini,
ngome kwa fukara katika taabu zao.
Wewe ni kimbilio wakati wa tufani,
kivuli wakati wa joto kali.
Kweli pigo la watu wakatili ni kali
kama tufani inayopiga ukuta;
5ni kama joto la jua juu ya nchi kavu.
Lakini wewe wakomesha fujo ya wageni.
Kama wingu lizimavyo joto la jua
ndivyo ukomeshavyo nyumba za ushindi za wakatili.
6Juu ya mlima Siyoni, Mwenyezi-Mungu wa majeshi atawafanyia watu wote karamu ya vinono na divai nzuri, nyama tamu na mafuta, pamoja na divai safi. 7Katika mlima huuhuu, Mwenyezi-Mungu ataliondoa wingu la huzuni lililowafunika watu wote, kifuniko cha uchungu juu ya mataifa yote. 825:8 Taz 1Kor 15:54; Ufu 7:17; 21:4 Bwana Mungu atakiangamiza kifo milele! Atayafuta machozi katika nyuso za watu wote na kuwaondolea watu wake aibu duniani kote. Bwana Mwenyezi-Mungu ametamka.
9Siku ile, watu wote watasema, “Huyu ndiye Mungu wetu! Tumemngojea atuokoe. Huyu ndiye Mwenyezi-Mungu tuliyemtazamia. Njoni tufurahi na kushangilia kwa kuwa ametuokoa.”
Mungu ataiadhibu Moabu
10Mwenyezi-Mungu ataulinda mlima wa Siyoni, lakini watu wa Moabu watakanyagwakanyagwa nchini mwao kama nyasi katika shimo la mbolea. 11Watainyosha mikono yao kama mtu anayejaribu kuogelea, lakini pamoja na ustadi wao, Mwenyezi-Mungu ataporomosha kiburi chao. 12Atayabomoa maboma ya miji ya Moabu yenye kuta ndefu na kuyabwaga chini mavumbini.


Isaya25;1-12

Biblia Habari Njema kwa Watu Wote(BHN)

"Swahili Na Waswahili"Mbarikiwe.

Wednesday 2 October 2019

Kikombe Cha Asubuhi;Isaya 24....


Shalom,Habari za Asubuhi,Hamjambo,Mmeamkaje?

Tumshukuru Mungu wetu katika yote...

Asante  Mungu wetu kwa wema na fadhili zako kwetu
Asante kwa ulinzi wako kwetu wakati wote
Asante kwa kutuchagua tena na kutupa
kibali cha kuendelea kuiona leo hii
Asante kwa pumzi/uzima,afya na kuwatayari kwa majukumu yetu


Utukuzwe ee Mungu wetu,usifiwe Baba wa Mbinguni

Neema yako yatutosha  Mungu wetu..!

Kisha Mwenyezi-Mungu akamwambia Mose, “Moyo wa Farao umekuwa mgumu. Anakataa kuwaacha Waisraeli waondoke. Basi, nenda ukakutane naye kesho asubuhi, wakati anapokwenda mtoni Nili. Mngojee kando ya mto. Chukua mkononi mwako ile fimbo iliyogeuka kuwa nyoka.
Baba wa Mbinguni tunakuja mbele zako tukijinyenyekeza,
tukijishusha na kujiachilia mikononi mwako

Mungu wetu tunaomba utusamehe dhambi zetu zote
Baba wa Mbinguni nasi tunaomba utupe neema ya kuweza kuwasamehe wale wote waliotukosea,Usitutie majaribuni Mungu wetu tunaomba utuepushe na yule mwovu na kazi zake zote,Jehovah ututakase miili yetu na akili zetu Baba wa Mbinguni tunaomba utufunike kwa  Damu ya Bwana na Mwokozi wetu Yesu Kristo wa Nazareti,
Yeye aliteseka kwanza ili sisi tupate kupona....

Kisha mwambie hivi, Mwenyezi-Mungu, Mungu wa Waebrania, amenituma kwako, naye asema hivi, ‘Waache watu wangu waende zao ili wanitumikie jangwani, lakini mpaka sasa wewe hupendi kutii.
Mungu wetu tunaomba ukabariki kazi za mikono yetu
Baba wa Mbinguni tunaomba ukatupe ubunifu na maarifa 
katika utendaji
Jehovah nasi tukatende sawasawa na mapenzi yako
Baba wa Mbinguni tunaomba ukabariki ridhiki zetu
ziingiazo/zitokazo
Mungu wetu nasi tunaomba ukatupe neema ya kuweza
kuwabariki wenye kuhitaji
Yahweh tusipungukiwe katika mahitaji yetu
Mungu wetu ukatupe kama inavyokupendeza wewe



Jehovah tunayaweka maisha yetu mikononi mwako
Baba wa Mbinguni tunaomba ukabariki nyumba/ndoa zetu,
watoto,wazazi wetu,familia/ndugu na wote wanaotuzunguka
Jehovah tunaomba ulinzi wako kwetu na kwa vyote tunavyo vimiliki
Yahweh tunaomba ukatubariki tuingiapo/tutokapo
Mungu wetu tunaomba ukavibariki vyote tunavyoenda kugusa/kutumia
Baba wa Mbinguni ukavitakase kwa Damu ya Bwana wetu Yesu Kristo
Mungu wetu ukatamalaki na kutuatamia
Baba wa Mbinguni tukawe salama rohoni
Mfalme wa amani amani yako ikatawale katika maisha yetu
Mungu wetu ukatupe macho ya kuona na masikio ya kusikia 
sauti yako na kuitii
Baba wa Mbinguni tunaomba ukatupe neema ya kufuata njia zako
Yahweh tukasimamie Neno lako amri na sheria zako siku zote 
za maisha yetu

Mungu  wetu ukaonekane katika maisha yetu popote tupitapo na ikajulikane kwamba upo 

Neema zako zikawe nasi Nuru yako ikaangaze katika maisha yetu
Ukatufanye barua njema ee Mungu wetu nasi tukasomeke kama
inavyokupendeza wewe
Roho Mtakatifu akatuongoze katika yote na tukawe na kiasi...

Basi, Mwenyezi-Mungu asema kwamba sasa utamtambua yeye ni nani. Nitayapiga maji ya mto Nili kwa fimbo hii, na maji yote yatageuka kuwa damu. Samaki waliomo mtoni Nili watakufa, mto wote utanuka vibaya, na Wamisri watachukia kabisa kunywa maji yake.’”
Tazama wenye shida/tabu,Mungu wetu tunaomba
 ukawaguse kila mmoja na mahitaji yake
Baba wa Mbinguni tunaomba ukawasamehe pale walipokwenda
kinyume nawe
Mungu wetu ukawape neema ya kujiombea,macho ya rohoni,masikio yakusikia sauti yako,wakafuate njia zako nazo zikawaweke huru
Mungu wetu tunaomba ukasikie kulia kwao
Baba wa Mbinguni tunomba ukawafute machozi yao
Nuru yako ikaangaze katika maisha yao
Mungu wetu tunaomba ukawatendee sawasawa na mapenzi yako
Kwakuwa Ufalme ni wako Nguvu na Utukufu hata Milele
Amina....!!!


Wapendwa katika Kristo Yesu asanteni sana
kwakuwanami/kunisoma

Mungu Baba aendelee kuwabariki na kuwatendea
kama inavyompendeza yeye
Amani ya Bwana wetu Yesu Kristo na upendo wa Mungu Baba
ukae nanyi daima....

Nawapenda.


Mwenyezi-Mungu ataiadhibu dunia
1Sasa Mwenyezi-Mungu anaiharibu dunia
na kuifanya tupu.
Atausokota uso wa dunia
na kuwatawanya wakazi wake.
2Kila mtu atapatwa na mambo yaleyale:
Mtu wa kawaida na kuhani;
mtumwa na bwana wake;
mjakazi na bibi yake;
mnunuzi na mwuzaji;
mkopeshaji na mkopaji;
mdai na mdaiwa.
3Dunia itaharibiwa kabisa na kuangamizwa;
Mwenyezi-Mungu ametamka hayo.
4Dunia inakauka na kunyauka;
ulimwengu unafadhaika na kunyauka;
mbingu zinafadhaika pamoja na dunia.
5Watu wameitia najisi dunia
maana wamezivunja sheria za Mungu,
wamezikiuka kanuni zake,
wamelivunja agano lake la milele.
6Kwa sababu hiyo laana inaitokomeza dunia,
wakazi wake wanateseka kwa makosa yao.
Wakazi wa dunia wamepungua,
ni watu wachache tu waliosalia.
7Mizabibu inanyauka,
divai inakosekana.
Wote waliokuwa wenye furaha
sasa wanasononeka kwa huzuni.
8Mdundo wa vigoma umekoma,
nderemo na vifijo vimetoweka;
midundo ya vinubi imekomeshwa.
9Hakuna tena kunywa divai na kuimba;
mvinyo umekuwa mchungu kwa wanywaji.
10Mji uliohamwa umejaa uharibifu;
kila nyumba imefungwa asiingie mtu.
11Kuna kilio barabarani kwa kukosa divai;
shangwe yote imekoma,
furaha imetoweka duniani.
12Mji ni magofu matupu;
malango yake yamevunjwavunjwa.
13Kama vile zeituni chache tu juu ya mzeituni
au tini chache tu juu ya mtini
baada ya kumaliza mavuno,
ndivyo itakavyokuwa katika nchi zote:
Watu wachache watabakia hai.
14Watakaosalia watapaza sauti,
wataimba kwa shangwe.
Kutoka magharibi watatangaza ukuu wa Mwenyezi-Mungu,
15nao wakazi wa mashariki watamsifu.
Watu wa mbali watalisifu
jina la Mwenyezi-Mungu, Mungu wa Israeli.
16Tunasikia nyimbo za sifa kutoka miisho ya dunia,
nyimbo za kumsifu Mungu aliye mwadilifu.
Lakini mimi ninanyongonyea,
naam, ninanyongonyea.
Ole wangu mimi!
Wasaliti wanaendelea kuwa wasaliti,
usaliti wao unazidi kuwa mbaya zaidi.
17Hofu, mashimo na mitego,
hivi ndivyo vinavyowangojeni enyi wakazi wa dunia.
18Atakayeikimbia hofu atatumbukia shimoni;
atakayetoka shimoni atanaswa mtegoni.
Madirisha ya mbinguni24:18 Madirisha ya mbinguni: Yaani tufani au gharika, Taz Mwa 7:11; 8:2. yamefunguliwa,
misingi ya dunia inatikisika.
19Dunia inavunjikavunjika,
inapasuka na kutikiswatikiswa.
20Inapepesuka kama mlevi,
inayumbayumba kama kibanda.
Imelemewa na mzigo wa dhambi zake
nayo itaanguka wala haitainuka tena.
21Siku ile Mwenyezi-Mungu ataliadhibu jeshi la angani24:21 jeshi la angani: Yaani jua, mwezi na nyota ambavyo baadhi ya watu wa nyakati hizo walifikiri kuwa pepo wabaya.
kadhalika na wafalme wa duniani.
22Wote watakusanywa kama wafungwa shimoni;
watafungwa gerezani pamoja kwa miaka mingi,
na baada ya muda huo atawaadhibu.
23Kisha mwezi utaaibishwa,
nalo jua litaona aibu kuangaza,
kwa kuwa Mwenyezi-Mungu wa majeshi
atatawala huko Yerusalemu katika mlima Siyoni;
ataonesha wazee wa watu wake utukufu wake.


Isaya24;1-23

Biblia Habari Njema kwa Watu Wote(BHN)

"Swahili Na Waswahili"Mbarikiwe.

Tuesday 1 October 2019

Kikombe Cha Asubuhi;Isaya 23....



Shalom,Habari za Asubuhi,Hamjambo,Mmeamkaje?

Haleluyah ni siku/wiki/mwezi mwingine tena Mungu wetu ametuchagua

na kutupa kibali cha kuendelea kuiona leo hii
Si kwamba sisi tumetenda mema sana wala si kwa nguvu zetu
si kwa utashi wetu wala si kwa akili zetu si kwamba sisi
ni wazuri mno si kwa uwezo wetu sisi kuwa hivi tulivyo leo hii
Ni kwa rehema/neema zake ni kwa mapenzi yake Mungu wetu....

Tumshukuru Mungu wetu katika yote...

Asante Mungu wetu kwa kutupa kibali cha kuona mwezi huu
Asante Mungu wetu kwa wema na fadhili zako kwetu

Asante kwa ulinzi wako kwetu wakati wote
Asante kwa pumzi/uzima,afya na kuwa tayari kwa majukumu yetu
Sifa na Utukufu tunakurudshia Mungu wetu....!!


Mwenyezi-Mungu aliwaambia Mose na Aroni, “Farao atakapowaambieni mthibitishe jambo hilo kwa kutenda miujiza, wewe utamwambia Aroni aichukue fimbo yake, aitupe mbele ya Farao, nayo itakuwa nyoka.”


Tazama jana imepita ee Mungu wetu leo ni siku mpya na kesho ni siku nyingine Jehovah tunakuja mbele zako tukijinyenyekeza,tukijishusha na kujiachilia mikononi mwako
 Mungu wetu tunaomba utusamehe dhambi zetu zote tulizozifanya kwakuwaza,kwakunena,kwakutenda,kwakujua/kutojua
Baba wa Mbinguni nasi tunaomba utupe neema ya kuweza kuwasamehe wale wote waliotukosea
Jehovah usitutie majaribu Mungu wetu tunaomba utuepushe na yule mwovu na kazi zake zote
Yahweh tunaomba ututakase miili yetu na akili zetu
Baba wa Mbinguni utufunike kwa Damu ya Bwana na Mwokozi wetu Yesu Kristo wa Nazareti
yeye aliteseka kwanza ili sisi tupate kupona
Kwakupigwa kwake sisi tumepata kupona....

Basi, Mose na Aroni wakamwendea Farao na kufanya kama walivyoamriwa na Mwenyezi-Mungu. Aroni aliitupa fimbo yake chini mbele ya Farao na maofisa wake, nayo ikawa nyoka. Lakini, Farao akawaita wenye hekima wake na wachawi; hao wachawi wa Misri wakafanya vivyo hivyo kwa uchawi wao.
Yahweh tunaomba ukabariki kazi za mikono yetu
Baba wa Mbinguni tunaomba ukatupe ubunifu na maarifa 
katika utendaji
Jehovah nasi tukatende sawasawa na mapenzi yako
Baba wa Mbinguni tunaomba ukabariki ridhiki zetu
ziingiazo/zitokazo
Mungu wetu nasi tunaomba ukatupe neema ya kuweza
kuwabariki wenye kuhitaji
Yahweh tusipungukiwe katika mahitaji yetu
Mungu wetu ukatupe kama inavyokupendeza wewe

Baba wa Mbinguni tunayaweka maisha yetu mikononi mwako
Mungu wetu tunaomba ukabariki nyumba/ndoa zetu,
watoto,wazazi wetu,familia/ndugu na wote wanaotuzunguka
Jehovah tunaomba ulinzi wako kwetu na kwa vyote tunavyo vimiliki
Yahweh tunaomba ukatubariki tuingiapo/tutokapo
Mungu wetu tunaomba ukavibariki vyote tunavyoenda kugusa/kutumia
Baba wa Mbinguni ukavitakase kwa Damu ya Bwana wetu Yesu Kristo
Mungu wetu ukatamalaki na kutuatamia
Baba wa Mbinguni tukawe salama rohoni
Mfalme wa amani amani yako ikatawale katika maisha yetu
Mungu wetu ukatupe macho ya kuona na masikio ya kusikia 
sauti yako na kuitii
Baba wa Mbinguni tunaomba ukatupe neema ya kufuata njia zako
Yahweh tukasimamie Neno lako amri na sheria zako siku zote 
za maisha yetu
Mungu wetu ukaonekane katika maisha yetu
Neema zako zikawe nasi Nuru yako ikaangaze katika maisha yetu
ukatuguse kwa mkono wako wenye nguvu
Ukatufanye chombo chema ee Mungu wetu nasi tukatumike kama
inavyokupendeza wewe
Roho Mtakatifu akatuongoze katika yote na tukawe na kiasi...


Kila mmoja akaitupa fimbo yake chini, ikawa nyoka. Lakini fimbo ya Aroni ikazimeza fimbo zao. Hata hivyo, moyo wa Farao bado ulibaki kuwa mgumu, wala hakuwasikiliza; ikawa kama alivyosema Mwenyezi-Mungu.
Mungu wetu tunawaweka mikononi mwako wenye shida/tabu,wote wanaopitia magumu/majaribu mbalimbali
Mungu wetu tunaomba ukawaguse kwa mkono wako wenye nguvu
 kila mmoja na mahitaji yake 
Mungu wetu tunaomba ukawasamehe pale walipokwenda kinyume nawe
Baba wa Mbinguni ukawape neema ya kujiombea,kufuata njia zako
wakasimamie Neno lako nalo likaweke huru
Mungu wetu tunaomba ukasikie kuomba kwetu
Mungu wetu ukawatendee sawasawa na mapenzi yako
Kwakuwa Ufalme ni wako Nguvu na Utukufu hata Milele
Amina...!!

Asanteni sana wapendwa katika Kristo Yesu kwakuwa nami
Mungu Baba aendelee kuwabariki na kuwatendea 
kama inavyompendeza yeye....
Nawapenda.


Angamizo la Tiro na Sidoni
1Kauli ya Mungu dhidi ya Tiro.
Ombolezeni, enyi mabaharia wa mbali baharini,
maana Tiro mji wenu umeharibiwa,
humo hamna tena makao wala bandari.
Mtazipokea habari hizo mtakaporejea kutoka Kupro.
2Nyamazeni kwa mshangao enyi wakazi wa pwani,
naam, tulieni enyi wafanyabiashara wa Sidoni,
ambao wajumbe wenu wanapita baharini,
3wakasafiri katika bahari nyingi.
Mapato yenu yalikuwa nafaka ya Misri,
mkaweza kufanya biashara na mataifa.
4Aibu kwako ewe Sidoni,
mji wa ngome kando ya bahari!
Bahari yenyewe yatangaza:
“Sijapata kuwa na uchungu wa kuzaa,
wala sijawahi kuzaa;
sijawahi kulea wavulana,
wala kutunza wasichana!”
5Habari zitakapoifikia Misri
kwamba Tiro imeangamizwa,
Wamisri watafadhaika sana.
6Ombolezeni enyi wenyeji wa Foinike!
Jaribuni kukimbilia Tarshishi.
7Je, huu ndio mji wa furaha wa Tiro,
mji ambao ulijengwa zamani za kale,
ambao wakazi wake walikwenda kumiliki nchi za mbali?
8Ni nani aliyepanga mambo haya dhidi ya Tiro,
mji uliowatawaza wafalme,
wafanyabiashara wake walikuwa wakuu,
wakaheshimiwa duniani kote?
9Ni Mwenyezi-Mungu wa majeshi!
Yeye ndiye aliyeyapanga haya yote.
Alifanya hivyo akiharibu kiburi chao
na kuwaaibisha waheshimiwa wake.
10Limeni sasa ardhi yenu enyi wakazi wa Tarshishi;
maana hamna tena bandari kwa ajili ya meli kubwa.23:10 aya 10 makala ya Kiebrania si dhahiri. Tafsiri ya hapa kulingana na makala ya Kiebrania iliyogunduliwa Kumrani.
11Mwenyezi-Mungu ameunyosha mkono wake juu ya bahari,
amezitetemesha falme;
ametoa amri kuziharibu ngome za Kanaani.
12Alisema: “Ewe binti Sidoni
hutaweza kufanya sherehe tena;
hata ukikimbilia Kupro,
huko nako hutapata pumziko!”
13(Ni Wakaldayo, wala si Waashuru, waliowaacha wanyama wa porini wauvamie mji wa Tiro. Wao ndio waliouzungushia mji huo minara ya kuushambulia, wakayabomoa majumba yake na kuufanya magofu.)23:13 aya 13 makala ya Kiebrania si dhahiri.
14Pigeni yowe enyi meli za Tarshishi,
maana kimbilio lenu limeharibiwa.
15Hapo mji wa Tiro utasahaulika kwa muda wa miaka sabini, muda wa maisha ya mfalme. Baada ya miaka hiyo sabini, mji wa Tiro utakumbwa na kile watu wanachoimba juu ya malaya:
16“Twaa kinubi chako
uzungukezunguke mjini,
ewe malaya uliyesahaulika!
Imba nyimbo tamutamu.
Imba nyimbo nyinginyingi
ili upate kukumbukwa tena.”
17Baada ya miaka hiyo sabini, Mwenyezi-Mungu atauadhibu mji wa Tiro, nao utarudia kufanya uzinzi kwa kujiuza kwa mataifa yote ya dunia. 18Fedha utakayopata itawekwa wakfu kwa Mwenyezi-Mungu. Mji wenyewe hautafaidika kwa fedha hiyo ila wale wanaomwabudu Mwenyezi-Mungu wataitumia kununulia chakula kingi na mavazi mazuri.


Isaya23;1-18

Biblia Habari Njema kwa Watu Wote(BHN)

"Swahili Na Waswahili"Mbarikiwe.