Swahili na Waswahili

Swahili na Waswahili
Waswahili na Mswahili Rachel Siwa...Pamoja Daima!!

Monday 2 September 2019

Kikombe Cha Asubuhi;Isaya 2....



Shalom,Habari za Asubuhi,Hamjambo,Mmeamkaje?

Haleluyah ni siku/wiki/mwezi mwingine tena Mungu wetu ametuchagua

na kutupa kibali cha kuendelea kuiona leo hii
Si kwamba sisi tumetenda mema sana wala si kwa nguvu zetu
si kwa utashi wetu wala si kwa akili zetu si kwamba sisi
ni wazuri mno si kwa uwezo wetu sisi kuwa hivi tulivyo leo hii
Ni kwa rehema/neema zake ni kwa mapenzi yake Mungu wetu....

Tumshukuru Mungu wetu katika yote...

Asante Mungu wetu kwa wema na fadhili zako kwetu
Asante kwa ulinzi wako kwetu wakati wote
Asante kwa pumzi/uzima,afya na kuwa tayari kwa majukumu yetu
Sifa na Utukufu tunakurudshia Mungu wetu....!!

Hivyo, ee mfalme Dario, utoe amri hiyo na kuitia hati sahihi yako ili isibadilishwe. Nayo itakuwa sheria ya Wamedi na Wapersi, sheria ambayo haibatilishwi.” Hivyo, mfalme Dario akaitia sahihi hati ya sheria hiyo.
Tazama jana imepita ee Mungu wetu leo ni siku mpya na kesho ni siku nyingine Jehovah tunakuja mbele zako tukijinyenyekeza,tukijishusha na kujiachilia mikononi mwako
 Mungu wetu tunaomba utusamehe dhambi zetu zote tulizozifanya kwakuwaza,kwakunena,kwakutenda,kwakujua/kutojua
Baba wa Mbinguni nasi tunaomba utupe neema ya kuweza kuwasamehe wale wote waliotukosea
Jehovah usitutie majaribu Mungu wetu tunaomba utuepushe na yule mwovu na kazi zake zote
Yahweh tunaomba ututakase miili yetu na akili zetu
Baba wa Mbinguni utufunike kwa Damu ya Bwana na Mwokozi wetu Yesu Kristo wa Nazareti
yeye aliteseka kwanza ili sisi tupate kupona
Kwakupigwa kwake sisi tumepata kupona....

Danieli alipojua kuwa ile hati imetiwa sahihi, alirudi nyumbani kwake ghorofani katika chumba chake kilichokuwa na madirisha yaliyofunguka kuelekea Yerusalemu. Humo, Danieli, kama ilivyokuwa kawaida yake, alipiga magoti mara tatu kila siku akamwomba na kumshukuru Mungu wake.
Yahweh tunaomba ukabariki kazi za mikono yetu
Baba wa Mbinguni tunaomba ukatupe ubunifu na maarifa 
katika utendaji
Jehovah nasi tukatende sawasawa na mapenzi yako
Baba wa Mbinguni tunaomba ukabariki ridhiki zetu
ziingiazo/zitokazo
Mungu wetu nasi tunaomba ukatupe neema ya kuweza
kuwabariki wenye kuhitaji
Yahweh tusipungukiwe katika mahitaji yetu
Mungu wetu ukatupe kama inavyokupendeza wewe

Baba wa Mbinguni tunayaweka maisha yetu mikononi mwako
Mungu wetu tunaomba ukabariki nyumba/ndoa zetu,
watoto,wazazi wetu,familia/ndugu na wote wanaotuzunguka
Jehovah tunaomba ulinzi wako kwetu na kwa vyote tunavyo vimiliki
Yahweh tunaomba ukatubariki tuingiapo/tutokapo
Mungu wetu tunaomba ukavibariki vyote tunavyoenda kugusa/kutumia
Baba wa Mbinguni ukavitakase kwa Damu ya Bwana wetu Yesu Kristo
Mungu wetu ukatamalaki na kutuatamia
Baba wa Mbinguni tukawe salama rohoni
Mfalme wa amani amani yako ikatawale katika maisha yetu
Mungu wetu ukatupe macho ya kuona na masikio ya kusikia 
sauti yako na kuitii
Baba wa Mbinguni tunaomba ukatupe neema ya kufuata njia zako
Yahweh tukasimamie Neno lako amri na sheria zako siku zote 
za maisha yetu
Mungu wetu ukaonekane katika maisha yetu
Neema zako zikawe nasi Nuru yako ikaangaze katika maisha yetu
ukatuguse kwa mkono wako wenye nguvu
Ukatufanye chombo chema ee Mungu wetu nasi tukatumike kama
inavyokupendeza wewe
Roho Mtakatifu akatuongoze katika yote na tukawe na kiasi...

Watu wale waliofanya mpango dhidi ya Danieli waliingia ndani, wakamkuta Danieli akiomba dua na kumsihi Mungu wake.
Mungu wetu tunawaweka mikononi mwako wenye shida/tabu,wote wanaopitia magumu/majaribu mbalimbali
Mungu wetu tunaomba ukawaguse kwa mkono wako wenye nguvu
 kila mmoja na mahitaji yake 
Mungu wetu tunaomba ukawasamehe pale walipokwenda kinyume nawe
Baba wa Mbinguni ukawape neema ya kujiombea,kufuata njia zako
wakasimamie Neno lako nalo likaweke huru
Mungu wetu tunaomba ukasikie kuomba kwetu
Mungu wetu ukawatendee sawasawa na mapenzi yako
Kwakuwa Ufalme ni wako Nguvu na Utukufu hata Milele
Amina...!!


Asanteni sana wapendwa katika Kristo Yesu kwakuwa nami
Mungu Baba aendelee kuwabariki na kuwatendea 
kama inavyompendeza yeye....
Nawapenda.


Amani ya kudumu
(Mika 4:1-3)
1Neno alilopewa Isaya, mwana wa Amozi, kuhusu Yuda na Yerusalemu.
2Siku zijazo mlima wa nyumba ya Mwenyezi-Mungu
utaimarishwa kupita milima yote,
utainuliwa juu ya vilima vyote.
Mataifa yote yatamiminika huko,
3watu wengi wataujia na kusema,
“Njoni tupande mlima wa Mwenyezi-Mungu,
twende nyumbani kwa Mungu wa Yakobo,
apate kutufundisha njia zake,
nasi tuishi kadiri ya mwongozo wake.
Maana sheria itakuja kutoka Siyoni;
neno la Mwenyezi-Mungu kutoka Yerusalemu.”
4 2:4 Taz Yoe 3:10 Mungu atasuluhisha mizozo ya mataifa
atakata mashauri ya watu wengi.
Watu watafua panga za vita kuwa majembe
na mikuki yao kuwa miundu ya kupogolea.
Taifa halitapigana na taifa lingine
wala hayatafanya tena mazoezi ya vita.
5Sasa, enyi wazawa wa Yakobo, njoni,
tutembee katika mwanga wa Mwenyezi-Mungu.

Kiburi kitaondolewa
6Sasa, ee Mungu, umewatupa watu wako, wazawa wa Yakobo.
Maana kweli wachawi wa mashariki wamejaa kati yao,
wapo na wapiga ramli kama kwa Wafilisti.
Wanashirikiana na watu wageni.
7Nchi yao imejaa fedha na dhahabu,
hazina yao ni kubwa kupindukia.
Nchi yao imejaa farasi,
magari yao ya kukokotwa hayana idadi.
8Nchi yao imejaa vinyago vya miungu,
huabudu kazi ya mikono yao,
vitu walivyotengeneza wao wenyewe.
9Kwa hiyo, kila mtu ataaibishwa na kufedheheshwa.
Usiwasamehe hata kidogo, ee Mungu!
10 2:10 Taz Ufu 6:15; 2Thes 1:9 Ingieni katika mwamba,
mkajifiche mavumbini,
kuiepa hasira ya Mwenyezi-Mungu,
mbali na utukufu wa enzi yake.
11Siku yaja ambapo kiburi cha watu kitashushwa,
majivuno ya kila mtu yatavunjwa;
na Mwenyezi-Mungu peke yake atatukuzwa siku hiyo.
12Naam, yaja siku ya Mwenyezi-Mungu wa majeshi
dhidi ya wenye kiburi na majivuno,
dhidi ya wote wanaojikweza;
13dhidi ya mierezi yote ya Lebanoni,
ambayo ni mirefu na mizuri,
dhidi ya mialoni yote nchini Bashani;
14dhidi ya milima yote mirefu,
dhidi ya vilima vyote vya juu;
15dhidi ya minara yote mirefu,
dhidi ya kuta zote za ngome;
16dhidi ya meli zote za Tarshishi,
na dhidi ya meli zote nzuri.
17Kiburi chote cha watu kitakomeshwa,
majivuno ya kila mtu yatavunjwa.
Na Mwenyezi-Mungu peke yake atatukuzwa siku hiyo.
18Vinyago vyote vya miungu vitatoweka kabisa.
19Ingieni katika mapango miambani,
katika mashimo ardhini,
kuiepa hasira ya Mwenyezi-Mungu,
mbali na utukufu wa enzi yake,
atakapokuja kuitia hofu dunia.
20Siku hiyo, watu watawatupia panya na popo
vinyago vyao vya fedha na dhahabu
walivyojitengenezea ili kuviabudu.
21Nao wataingia katika mapango miambani
na kwenye nyufa za miamba,
kuiepa hasira ya Mwenyezi-Mungu,
mbali na utukufu wa enzi yake,
atakapokuja kuitia hofu dunia.
22Usimwamini binadamu,
uhai wake haudumu kama pumzi.
Yeye anafaa kitu gani?

Isaya2;1-22

Biblia Habari Njema kwa Watu Wote(BHN)

"Swahili Na Waswahili"Mbarikiwe.

Friday 30 August 2019

Kikombe Cha Asubuhi; Tunamshukuru Mungu kwa kumaliza Kitabu Cha Wimbo Ulio Bora ,Leo Tunaanza Kitabu Cha Isaya 1....


Shalom,Habari za Asubuhi,Hamjambo,Mmeamkaje?

Haleluyah Mungu wetu yu mwema sana..
Tunamshukuru Mungu kwa kutupa kibali cha

 kupitia kitabu cha "WIMBO ULIO BORA
"
Ni matumaini yangu kuna mengi tumejifunza/kufaidika
na kutupa mwanga/kuelewa kwenye kitabu hiki...


Leo tunapokwenda anza kupitia Kitabu cha"ISAYA"tunamuomba Mungu wetu akatupe kibali,macho ya rohoni
 na akili ya kuelewa katika kujifunza NENO lake...
Ee Mungu  tunaomba ukatuongoze...!!

Tumshukuru Mungu wetu katika yote...

Asante  Mungu wetu kwa wema na fadhili zako kwetu
Asante kwa ulinzi wako kwetu wakati wote
Asante kwa kutuchagua tena na kutupa
kibali cha kuendelea kuiona leo hii
Asante kwa pumzi/uzima,afya na kuwatayari kwa majukumu yetu

Utukuzwe ee Mungu wetu,usifiwe Baba wa Mbinguni
Neema yako yatutosha  Mungu wetu..!

Ndipo wakapatana hivi: “Hatutapata kisingizio chochote cha kumshtaki Danieli isipokuwa kama kisingizio hicho kitakuwa kinahusu sheria ya Mungu wake.”
Baba wa Mbinguni tunakuja mbele zako tukijinyenyekeza,tukijishusha na kujiachilia mikononi mwako
Mungu wetu tunaomba utusamehe dhambi zetu zote
Baba wa Mbinguni nasi tunaomba utupe neema ya kuweza kuwasamehe wale wote waliotukosea,Usitutie majaribuni Mungu wetu tunaomba utuepushe na yule mwovu na kazi zake zote,Jehovah ututakase miili yetu na akili zetu Baba wa Mbinguni tunaomba utufunike kwa  Damu ya Bwana na Mwokozi wetu Yesu Kristo wa Nazareti,
Yeye aliteseka kwanza ili sisi tupate kupona....

Basi, hao wakuu na maliwali kwa pamoja, wakamwendea mfalme na kumwambia, “Uishi ee mfalme Dario!
Mungu wetu tunaomba ukabariki kazi za mikono yetu
Baba wa Mbinguni tunaomba ukatupe ubunifu na maarifa 
katika utendaji
Jehovah nasi tukatende sawasawa na mapenzi yako
Baba wa Mbinguni tunaomba ukabariki ridhiki zetu
ziingiazo/zitokazo
Mungu wetu nasi tunaomba ukatupe neema ya kuweza
kuwabariki wenye kuhitaji
Yahweh tusipungukiwe katika mahitaji yetu
Mungu wetu ukatupe kama inavyokupendeza wewe



Jehovah tunayaweka maisha yetu mikononi mwako
Baba wa Mbinguni tunaomba ukabariki nyumba/ndoa zetu,
watoto,wazazi wetu,familia/ndugu na wote wanaotuzunguka
Jehovah tunaomba ulinzi wako kwetu na kwa vyote tunavyo vimiliki
Yahweh tunaomba ukatubariki tuingiapo/tutokapo
Mungu wetu tunaomba ukavibariki vyote tunavyoenda kugusa/kutumia
Baba wa Mbinguni ukavitakase kwa Damu ya Bwana wetu Yesu Kristo
Mungu wetu ukatamalaki na kutuatamia
Baba wa Mbinguni tukawe salama rohoni
Mfalme wa amani amani yako ikatawale katika maisha yetu
Mungu wetu ukatupe macho ya kuona na masikio ya kusikia 
sauti yako na kuitii
Baba wa Mbinguni tunaomba ukatupe neema ya kufuata njia zako
Yahweh tukasimamie Neno lako amri na sheria zako siku zote 
za maisha yetu

Mungu  wetu ukaonekane katika maisha yetu popote tupitapo na ikajulikane kwamba upo 

Neema zako zikawe nasi Nuru yako ikaangaze katika maisha yetu
Ukatufanye barua njema ee Mungu wetu nasi tukasomeke kama
inavyokupendeza wewe
Roho Mtakatifu akatuongoze katika yote na tukawe na kiasi...

Sisi wakuu uliotuweka, wasimamizi, maliwali, washauri na wakuu wa mikoa, sote tumepatana kuwa inafaa, ee mfalme, utoe amri na kuhakikisha inafuatwa kikamilifu. Amuru kwamba kwa muda wa siku thelathini kusiwe na mtu yeyote atakayeruhusiwa kuomba kitu chochote kwa mungu yeyote au kwa mtu yeyote, isipokuwa kutoka kwako wewe, ewe mfalme. Mtu yeyote atakayevunja sheria hii na atupwe katika pango la simba.
Tazama wenye shida/tabu,Mungu wetu tunaomba
 ukawaguse kila mmoja na mahitaji yake
Baba wa Mbinguni tunaomba ukawasamehe pale walipokwenda
kinyume nawe
Mungu wetu ukawape neema ya kujiombea,macho ya rohoni,masikio yakusikia sauti yako,wakafuate njia zako nazo zikawaweke huru
Mungu wetu tunaomba ukasikie kulia kwao
Baba wa Mbinguni tunomba ukawafute machozi yao
Nuru yako ikaangaze katika maisha yao
Mungu wetu tunaomba ukawatendee sawasawa na mapenzi yako
Kwakuwa Ufalme ni wako Nguvu na Utukufu hata Milele
Amina....!!!


Wapendwa katika Kristo Yesu asanteni sana
kwakuwanami/kunisoma

Mungu Baba aendelee kuwabariki na kuwatendea
kama inavyompendeza yeye
Amani ya Bwana wetu Yesu Kristo na upendo wa Mungu Baba
ukae nanyi daima....
Nawapenda.

1 Maono aliyoyaona Isaya, mwana wa Amozi, kuhusu Yuda na mji wa Yerusalemu, nyakati za utawala wa Uzia, Yothamu, Ahazi na Hezekia, wafalme wa Yuda.

Mungu awakemea watu wake
2Mwenyezi-Mungu asema hivi:
“Sikilizeni enyi mbingu,
tega sikio ee dunia.
Mimi nimewalea wanangu wakakua,
lakini sasa wameniasi!
3Ngombe humfahamu mwenyewe,
punda hujua kibanda cha bwana wake;
lakini Waisraeli hawajui,
watu wangu, hawaelewi!”
4Ole wako wewe taifa lenye dhambi,
watu waliolemewa na uovu,
wazawa wa wenye kutenda maovu,
watu waishio kwa udanganyifu!
Nyinyi mmemwacha Mwenyezi-Mungu,
mmemdharau Mtakatifu wa Israeli,
mmefarakana naye na kurudi nyuma.
5Kwa nini huachi uasi wako?
Mbona wataka kuadhibiwa bado?
Kichwa chote ni majeraha matupu,
na moyo wote unaugua!
6Toka wayo hadi kichwa hamna penye nafuu,
umejaa majeraha na vidonda vitoavyo damu,
navyo havikuoshwa, kufungwa wala kutiwa mafuta.
7Nchi yenu imeharibiwa kabisa;
miji yenu imeteketezwa kwa moto.
Wageni wananyakua nchi yenu mkiona kwa macho,
imeharibiwa kama uharibifu wa Sodoma.1:7 Sodoma: Kiebrania: Wageni, Taz Kumb 29:33; Yer 49:18.
8Mji Siyoni umeachwa kama kibanda shambani,
kama kitalu katika shamba la matango,
kama mji uliozingirwa.
9Mwenyezi-Mungu wa majeshi asingalituachia wachache,
tungalikwisha kuwa kama watu wa Sodoma,
tungalikuwa hali ileile ya Gomora.1:9 Gomora: Taz Mwa 19:24; Roma 9:29.
10Sikilizeni neno la Mwenyezi-Mungu
enyi watawala waovu kama wa Sodoma!
Sikilizeni mafunzo ya Mungu wetu
enyi watu waovu kama wa Gomora!
11 1:11-14 Taz Amo 5:21-22 Mwenyezi-Mungu asema hivi;
“Wingi wa tambiko zenu ni kitu gani kwangu?
Nimezichoka sadaka zenu za kondoo wa kuteketezwa
na mafuta ya wanyama wenu wanono.
Sipendezwi na damu ya fahali,
wala ya wanakondoo, wala ya beberu.
12Mnapokuja mbele yangu kuniabudu
nani aliyewataka mkanyagekanyage nyua zangu?
13Msiniletee tena matoleo yenu yasiyo na maana;
ubani ni chukizo kwangu.
Acheni kufanya sikukuu za mwezi mpya,
Sabato na mikutano mikubwa ya ibada;
sikubali ibada zilizochanganyika na dhambi.
14Sikukuu zenu za mwezi mpya na nyinginezo
moyo wangu wazichukia.
Zimekuwa mzigo mzito kwangu,
nami nimechoka kuzivumilia.
15“Mnapoinua mikono yenu kuomba
nitauficha uso wangu nisiwaone.
Hata mkiomba kwa wingi sitawasikia,
maana mikono yenu imejaa damu.
16Jiosheni, jitakaseni;
ondoeni uovu wa matendo yenu mbele yangu.
Acheni kutenda maovu,
17jifunzeni kutenda mema.
Tendeni haki,
ondoeni udhalimu,
walindeni yatima,
teteeni haki za wajane.”
18Mwenyezi-Mungu asema hivi:
“Njoni, basi, tuhojiane.
Ingawa mna madoa mekundu ya dhambi,
mtatakaswa na kuwa weupe kama theluji;
madoa yenu yajapokuwa mekundu kama damu,
mtakuwa weupe kama sufu.
19Mkiwa tayari kunitii,
mtakula mazao mema ya nchi.
20Lakini mkikaidi na kuniasi,
mtaangamizwa kwa upanga.
Mimi, Mwenyezi-Mungu, nimesema.”
Mji uliojaa dhambi
21Jinsi gani mji uliokuwa mwaminifu
sasa umegeuka kuwa kahaba!
Wakati mmoja haki ilitawala humo,
lakini sasa umejaa wauaji.
22Fedha yenu imekuwa takataka;
divai yenu imechanganyika na maji.
23Viongozi wako ni waasi;
wanashirikiana na wezi.
Kila mmoja anapenda hongo,
na kukimbilia zawadi.
Hawawatetei yatima,
haki za wajane si kitu kwao.
24Kwa hiyo asema Bwana Mwenyezi-Mungu,
Mwenye Nguvu wa Israeli:
“Nitawamwagia maadui zangu hasira yangu,
nitawalipiza kisasi wapinzani wangu.
25Nitanyosha mkono wangu dhidi yenu;
nitayeyusha uchafu wenu kabisa,
na kuondoa takataka yenu yote.
26Nitawapeni waamuzi wenu kama kwanza
na washauri wenu kama pale awali.
Ndipo Yerusalemu utakapoitwa ‘Mji wa Uadilifu’
utaitwa ‘Mji Mwaminifu’”
27Mji Siyoni utakombolewa kwa haki,
uadilifu utawaokoa watakaotubu humo.
28Lakini waasi na wenye dhambi
wote wataangamizwa pamoja;
wanaomwacha Mwenyezi-Mungu watateketezwa.
29Mtaionea aibu hiyo mialoni mliyoipenda sana;
mtafadhaika kwa sababu ya bustani mlizofurahia.
30Mtakuwa kama mwaloni unaonyauka majani;
kama shamba lisilo na maji.
31Wenye nguvu watakuwa kama majani makavu,
matendo yao yatakuwa kama cheche za moto.
Watateketea pamoja na matendo yao,
wala hapatakuwa na mtu wa kuwaokoa.

Isaya1;1-31

Biblia Habari Njema kwa Watu Wote(BHN)

"Swahili Na Waswahili"Mbarikiwe.

Thursday 29 August 2019

Kikombe Cha Asubuhi; Wimbo Ulio Bora 8...

Shalom,Habari za Asubuhi,Hamjambo,Mmeamkaje?

Tumshukuru Mungu wetu katika yote...

Asante  Mungu wetu kwa wema na fadhili zako kwetu
Asante kwa ulinzi wako kwetu wakati wote
Asante kwa kutuchagua tena na kutupa
kibali cha kuendelea kuiona leo hii
Asante kwa pumzi/uzima,afya na kuwatayari kwa majukumu yetu


Utukuzwe ee Mungu wetu,usifiwe Baba wa Mbinguni

Neema yako yatutosha  Mungu wetu..!

Mfalme Dario aliamua kuteua wakuu 120 kusimamia mambo ya utawala. Aliwateua pia wakuu watatu, Danieli akiwa mmojawapo, wawasimamie wale wakuu wengine na maslahi ya mfalme, asije akapata hasara.
Baba wa Mbinguni tunakuja mbele zako tukijinyenyekeza,tukijishusha na kujiachilia mikononi mwako
Mungu wetu tunaomba utusamehe dhambi zetu zote
Baba wa Mbinguni nasi tunaomba utupe neema ya kuweza kuwasamehe wale wote waliotukosea,Usitutie majaribuni Mungu wetu tunaomba utuepushe na yule mwovu na kazi zake zote,Jehovah ututakase miili yetu na akili zetu Baba wa Mbinguni tunaomba utufunike kwa  Damu ya Bwana na Mwokozi wetu Yesu Kristo wa Nazareti,
Yeye aliteseka kwanza ili sisi tupate kupona....

Muda si muda, Danieli akadhihirika kuwa bora kuliko wale wasimamizi wengine na wakuu wote kwa kuwa alikuwa na roho njema. Hivyo mfalme akanuia kumpa uongozi wa ufalme wote.
Mungu wetu tunaomba ukabariki kazi za mikono yetu
Baba wa Mbinguni tunaomba ukatupe ubunifu na maarifa 
katika utendaji
Jehovah nasi tukatende sawasawa na mapenzi yako
Baba wa Mbinguni tunaomba ukabariki ridhiki zetu
ziingiazo/zitokazo
Mungu wetu nasi tunaomba ukatupe neema ya kuweza
kuwabariki wenye kuhitaji
Yahweh tusipungukiwe katika mahitaji yetu
Mungu wetu ukatupe kama inavyokupendeza wewe

Jehovah tunayaweka maisha yetu mikononi mwako
Baba wa Mbinguni tunaomba ukabariki nyumba/ndoa zetu,
watoto,wazazi wetu,familia/ndugu na wote wanaotuzunguka
Jehovah tunaomba ulinzi wako kwetu na kwa vyote tunavyo vimiliki
Yahweh tunaomba ukatubariki tuingiapo/tutokapo
Mungu wetu tunaomba ukavibariki vyote tunavyoenda kugusa/kutumia
Baba wa Mbinguni ukavitakase kwa Damu ya Bwana wetu Yesu Kristo
Mungu wetu ukatamalaki na kutuatamia
Baba wa Mbinguni tukawe salama rohoni
Mfalme wa amani amani yako ikatawale katika maisha yetu
Mungu wetu ukatupe macho ya kuona na masikio ya kusikia 
sauti yako na kuitii
Baba wa Mbinguni tunaomba ukatupe neema ya kufuata njia zako
Yahweh tukasimamie Neno lako amri na sheria zako siku zote 
za maisha yetu

Mungu  wetu ukaonekane katika maisha yetu popote tupitapo na ikajulikane kwamba upo 

Neema zako zikawe nasi Nuru yako ikaangaze katika maisha yetu
Ukatufanye barua njema ee Mungu wetu nasi tukasomeke kama
inavyokupendeza wewe
Roho Mtakatifu akatuongoze katika yote na tukawe na kiasi...

Wale wakuu pamoja na maliwali wakatafuta kisingizio cha kumshtaki Danieli kuhusu mambo ya ufalme, lakini hawakuweza kupata sababu ya kumlaumu, wala kosa lolote, kwani Danieli alikuwa mwaminifu. Hakupatikana na kosa, wala hatia yoyote.
Tazama wenye shida/tabu,Mungu wetu tunaomba
 ukawaguse kila mmoja na mahitaji yake
Baba wa Mbinguni tunaomba ukawasamehe pale walipokwenda
kinyume nawe
Mungu wetu ukawape neema ya kujiombea,macho ya rohoni,masikio yakusikia sauti yako,wakafuate njia zako nazo zikawaweke huru
Mungu wetu tunaomba ukasikie kulia kwao
Baba wa Mbinguni tunomba ukawafute machozi yao
Nuru yako ikaangaze katika maisha yao
Mungu wetu tunaomba ukawatendee sawasawa na mapenzi yako
Kwakuwa Ufalme ni wako Nguvu na Utukufu hata Milele
Amina....!!!


Wapendwa katika Kristo Yesu asanteni sana
kwakuwanami/kunisoma

Mungu Baba aendelee kuwabariki na kuwatendea
kama inavyompendeza yeye
Amani ya Bwana wetu Yesu Kristo na upendo wa Mungu Baba
ukae nanyi daima....

Nawapenda.

1Laiti ungekuwa kaka yangu,
ambaye amenyonyeshwa na mama yangu!
Hivyo, hata kama ningekutana nawe nje,
ningekubusu na hakuna ambaye angenidharau.
2Ningekuongoza na kukufikisha nyumbani kwa mama mzazi,
mahali ambapo ungenifundisha upendo.
Ningekupa divai nzuri iliyokolezwa,
ningekupa divai yangu ya makomamanga yangu.
3Mkono wako wa kushoto u chini ya kichwa changu,
na mkono wako wa kulia wanikumbatia.
4Nawasihini, enyi wanawake wa Yerusalemu,
msiyachochee wala kuyaamsha mapenzi,
hadi hapo wakati wake utakapofika.
Shairi la sita
Wanawake
5Ni nani huyu ajaye kutoka mbugani,
huku anamwegemea mpenzi wake?
Bibi arusi
Chini ya mtofaa, mimi nilikuamsha,
pale ambapo mama yako aliona uchungu,
naam, pale ambapo mama yako alikuzaa.
6Nipige kama mhuri moyoni mwako,
naam, kama mhuri mikononi mwako.
Maana pendo lina nguvu kama kifo,
wivu nao ni mkatili kama kaburi.
Mlipuko wake ni kama mlipuko wa moto,
huwaka kama mwali wa moto.
7Maji mengi hayawezi kamwe kulizima,
mafuriko hayawezi kulizamisha.
Mtu akijaribu kununua pendo,
akalitolea mali yake yote,
atakachopata ni dharau tupu.
Ndugu za Bibi arusi
8Tunaye dada mdogo,
ambaye bado hajaota matiti.
Je, tumfanyie nini dada yetu
siku atakapoposwa?
9Kama angalikuwa ukuta,
tungalimjengea mnara wa fedha;
na kama angalikuwa mlango,
tungalimhifadhi kwa mbao za mierezi.
Bibi arusi
10Mimi nalikuwa ukuta,
na matiti yangu kama minara yake.
Machoni pake nalikuwa
kama mwenye kuleta amani.
Bwana arusi
11Solomoni alikuwa ana shamba la mizabibu,
mahali paitwapo Baal-hamoni.
Alilikodisha kwa walinzi;
kila mmoja wao alilipa vipande elfu vya fedha.
12Shamba langu la mizabibu ni shamba langu mwenyewe,
naam, ni shamba langu binafsi!
Basi, Solomoni, wewe ukae na elfu zako za fedha,
na kila mlinzi wa matunda akae na mia mbili zake.
13Ewe uliye shambani,
rafiki zangu wanasikiliza sauti yako;
hebu nami niisikie tafadhali!
Bibi arusi
14Njoo haraka ewe mpenzi wangu,
kama paa au mwanapaa dume juu ya milima ya manukato.

Wimbo Ulio Bora8;1-14

Biblia Habari Njema kwa Watu Wote(BHN)

"Swahili Na Waswahili"Mbarikiwe.

Wednesday 28 August 2019

Kikombe Cha Asubuhi; Wimbo Ulio Bora 7...


Shalom,Habari za Asubuhi,Hamjambo,Mmeamkaje?

Tumshukuru Mungu katika yote....

Mungu wetu Baba yetu,Muumba wetu Muumba wa Mbingu na Nchi
Muumba wa vyote vilivyomo vinavyoonekana na visivyoonekana
Mungu wa walio hai,Mungu  mwenye huruma,Mungu wa upendo
Mungu wa Abrahamu,Isaka na Yakobo...
Asante kwa wema na fadhili zako kwetu
Asante kwa ulinzi wako kwetu wakati wote
Asante kwa kutuchagua tena na kutupa
kibali cha kuendelea kuiona leo hii
Asante kwa pumzi/uzima,afya na kuwatayari kwa majukumu yetu

Neema yako yatutosha ee Mungu wetu....!!

Ndiyo maana tunawaombeeni daima. Tunamwomba Mungu wetu awawezesheni kustahili maisha aliyowaitia muyaishi. Tunamwomba, kwa uwezo wake, atimize nia yenu ya kutenda mema na kukamilisha kazi yenu ya imani.
Baba wa Mbinguni tunakuja mbele zako tukijinyenyekeza,tukijishusha na kujiachilia mikononi mwako
Mungu wetu tunaomba utusamehe dhambi zetu zote 
Baba wa Mbinguni nasi tunaomba ukatupe neema
ya kuweza kuwasamehe wale wote waliotukosea
Usitutie majaribuni Mungu wetu tunaomba utuepushe
na yule mwovu na kazi zake zote
Jehovah ututakase miili yetu na akili zetu
Baba wa Mbinguni tunaomba utufunike kwa Damu
ya Bwana na Mwokozi wetu Yesu Kristo wa Nazareti
yeye aliteseka kwanza ili sisi tupate kupona....
Mungu wetu tunaomba ukabariki kazi za mikono yetu
Baba wa Mbinguni tunaomba ukatupe ubunifu na maarifa katika utendaji
Jehovah nasi tukatende sawasawa na mapenzi yako
Yahweh tunaomba ukabariki ridhiki zetu ziingiazo/zitokazo
Mungu wetu nasi tunaomna ukatupe neema ya kuweza kuwabariki wenye kuhitaji
Tusipungukiwe katika mahitaji yetu
Baba wa Mbinguni tunaomba ukatupe kama inavyokupendeza wewe...

Yahweh tunayaweka maisha yetu mikononi mwako
Mungu wetu tunaomba ukabariki nyumba/ndoa zetu,
Jehovah tunaomba ulinzi wako kwetu na kwa vyote tunavyovimiliki
Yahweh tunaomba ukatubariki tuingiapo/tutokapo
Mungu wetu tunaomba ukavibariki vyote tunavyoenda kugusa/kutumia
Baba wa Mbinguni ukavitakase kwa Damu ya Bwana wetu Yesu Kristo
Mungu wetu ukatamalaki na kutuatamia
Baba wa Mbinguni tukawe salama rohoni
Yahwe ukatupe akili ya kutambua mema na mabaya
Mfalme wa amani amani yako ikatawale katika maisha yetu
Mungu wetu ukatupe macho ya kuona,masikio ya kusikia sauti yako na kuitii..
Baba wa Mbinguni  tunaomba ukatupe neema ya kufuata
njia zako,tukasimamie Neno lako,amri na sheria zako
siku zote za maisha yetu...
Ukatuguse kwa mkono wako wenye nguvu,ukatufanye chombo chema
ee Mungu wetu nasi tukatumike kama inavyokupendeza wewe
Roho Mtakatifu akatuongoze katika yote na tukawe na kiasi....

Kwa namna hiyo, jina la Bwana wetu Yesu litapata utukufu kutoka kwenu, nanyi mtapata utukufu kutoka kwake kwa neema ya Mungu wetu na ya Bwana Yesu Kristo.
Tazama watoto wako wenye shida/tabu,wote wanaopitia magumu/majaribu mbalimbali
Mungu wetu tunaomba ukawaguse kwa mkono wako wenye nguvu
kila mmoja na mahitaji yake
Mungu wetu tunaomba ukawasamehe pale walipo kwenda kinyume nawe
Yahweh tunaomba ukawape neema ya kuweza kujiombea,kufuata njia zako nazo zikawaweke huru...
Baba wa Mbinguni tunayaweka haya yote mikononi mwako
Kwakuwa Ufalme ni wako Nguvu na Utukufu hata Milele...
Amina...!!


Asanteni sana wapendwa katika Kristo Yesu kwakuwa nami,Baba wa Mbinguni aendelee kuwatendea sawasawa na mapenzi yake...
Nawapenda.

Bwana arusi
1Nyayo zako katika viatu zapendeza sana!
Ewe mwanamwali wa kifalme.
Mapaja yako ya mviringo ni kama johari,
kazi ya msanii hodari.
2Kitovu chako ni kama bakuli
lisilokosa divai iliyokolezwa.
Tumbo lako ni kama lundo la ngano
lililozungushiwa yungiyungi kandokando.
3Matiti yako ni kama paa mapacha,
ni kama swala wawili.
4Shingo yako ni kama mnara wa pembe za ndovu;
macho yako ni kama vidimbwi mjini Heshboni,
karibu na mlango wa Beth-rabi.
Pua yako ni kama mnara wa Lebanoni,
ambao unauelekea mji wa Damasko.
5Kichwa chako juu yako ni kama mlima Karmeli,
nywele zako za ukoka zangaa kama zambarau;
uzuri7:5 uzuri: Kiebrania si dhahiri. wako waweza kumteka hata mfalme.
6Tazama ulivyo mzuri na wa kuvutia!
Ewe mpenzi, mwali upendezaye!
7Umbo lako lapendeza kama mtende,
matiti yako ni kama shada za tende.
8Nilisema nitaupanda mtende na kuzichuma shada za tende.
Kwangu matiti yako ni kama shada za zabibu,
harufu nzuri ya pumzi yako ni kama matofaa;
9na kinywa chako ni kama divai tamu.
Bibi arusi
Basi divai na itiririke hadi kwa mpenzi wangu,
ipite juu ya midomo yake na meno yake!8:9 midomo yake na meno yake: Kiebrania: Midomo ya wale walalao.
10Mimi ni wake mpenzi wangu,
naye anionea sana shauku.
11Njoo ewe mpenzi wangu, twende mashambani,
twende zetu tukalale huko vijijini.
12Tutaamka mapema, twende kwenye mashamba ya mizabibu,
tukaone kama imeanza kuchipua,
na kama maua ya zabibu yamekwisha kuchanua,
pia kama mikomamanga imeanza kutoa maua.
Huko ndiko nitakapokupatia pendo langu.
13Harufu nzuri ya tunguja imejaa hewani
karibu na milango yetu kuna kila aina ya matunda bora,
yote mapya na ya siku za nyuma,
ambayo nimekuwekea wewe mpenzi wangu.

Wimbo Ulio Bora7;1-13

Biblia Habari Njema kwa Watu Wote(BHN)

"Swahili Na Waswahili"Mbarikiwe.