Swahili na Waswahili

Swahili na Waswahili
Waswahili na Mswahili Rachel Siwa...Pamoja Daima!!

Thursday 25 July 2019

Kikombe Cha Asubuhi ; Methali 26...


Shalom,Habari za Asubuhi,Hamjambo,Mmeamkaje?

Tumshukuru Mungu katika yote....

Mungu wetu Baba yetu,Muumba wetu Muumba wa Mbingu na Nchi
Muumba wa vyote vilivyomo vinavyoonekana na visivyoonekana
Mungu wa walio hai,Mungu  mwenye huruma,Mungu wa upendo
Mungu wa Abrahamu,Isaka na Yakobo...
Asante kwa wema na fadhili zako kwetu
Asante kwa ulinzi wako kwetu wakati wote
Asante kwa kutuchagua tena na kutupa
kibali cha kuendelea kuiona leo hii
Asante kwa pumzi/uzima,afya na kuwatayari kwa majukumu yetu

Neema yako yatutosha ee Mungu wetu....!!

Lakini kama sadaka hiyo ya amani ni ya nadhiri au ya hiari, italiwa siku hiyohiyo inapotolewa na sehemu nyingine yaweza kuliwa kesho yake. Lakini nyama yoyote ya sadaka hiyo inayobaki hadi siku ya tatu itateketezwa.
Baba wa Mbinguni tunakuja mbele zako tukijinyenyekeza,tukijishusha na kujiachilia mikononi mwako
Mungu wetu tunaomba utusamehe dhambi zetu zote 
Baba wa Mbinguni nasi tunaomba ukatupe neema
ya kuweza kuwasamehe wale wote waliotukosea
Usitutie majaribuni Mungu wetu tunaomba utuepushe
na yule mwovu na kazi zake zote
Jehovah ututakase miili yetu na akili zetu
Baba wa Mbinguni tunaomba utufunike kwa Damu
ya Bwana na Mwokozi wetu Yesu Kristo wa Nazareti
yeye aliteseka kwanza ili sisi tupate kupona....

Tena nyama yoyote ya sadaka ya amani ikiliwa siku ya tatu, haitakubaliwa, wala haitapokelewa kwa faida yake mtu aliyeitoa. Nyama hiyo ni chukizo na mtu atakayeila atawajibika kwa uovu wake.
Mungu wetu tunaomba ukabariki kazi za mikono yetu
Baba wa Mbinguni tunaomba ukatupe ubunifu na maarifa katika utendaji
Jehovah nasi tukatende sawasawa na mapenzi yako
Yahweh tunaomba ukabariki ridhiki zetu ziingiazo/zitokazo
Mungu wetu nasi tunaomna ukatupe neema ya kuweza kuwabariki wenye kuhitaji
Tusipungukiwe katika mahitaji yetu
Baba wa Mbinguni tunaomba ukatupe kama inavyokupendeza wewe...

Yahweh tunayaweka maisha yetu mikononi mwako
Mungu wetu tunaomba ukabariki nyumba/ndoa zetu,
Jehovah tunaomba ulinzi wako kwetu na kwa vyote tunavyovimiliki
Yahweh tunaomba ukatubariki tuingiapo/tutokapo
Mungu wetu tunaomba ukavibariki vyote tunavyoenda kugusa/kutumia
Baba wa Mbinguni ukavitakase kwa Damu ya Bwana wetu Yesu Kristo
Mungu wetu ukatamalaki na kutuatamia
Baba wa Mbinguni tukawe salama rohoni
Yahwe ukatupe akili ya kutambua mema na mabaya
Mfalme wa amani amani yako ikatawale katika maisha yetu
Mungu wetu ukatupe macho ya kuona,masikio ya kusikia sauti yako na kuitii..
Baba wa Mbinguni  tunaomba ukatupe neema ya kufuata
njia zako,tukasimamie Neno lako,amri na sheria zako
siku zote za maisha yetu...
Ukatuguse kwa mkono wako wenye nguvu,ukatufanye chombo chema
ee Mungu wetu nasi tukatumike kama inavyokupendeza wewe
Roho Mtakatifu akatuongoze katika yote na tukawe na kiasi....

“Nyama yoyote inayogusa kitu najisi isiliwe. Nyama hiyo itateketezwa kwa moto. Wote walio safi wanaweza kula nyama iliyotolewa sadaka ya amani kwa Mwenyezi-Mungu. Lakini mtu yeyote aliye najisi, akila nyama hiyo, atatengwa na watu wake.
Tazama watoto wako wenye shida/tabu,wote wanaopitia magumu/majaribu mbalimbali
Mungu wetu tunaomba ukawaguse kwa mkono wako wenye nguvu
kila mmoja na mahitaji yake
Mungu wetu tunaomba ukawasamehe pale walipo kwenda kinyume nawe
Yahweh tunaomba ukawape neema ya kuweza kujiombea,kufuata njia zako nazo zikawaweke huru...
Baba wa Mbinguni tunayaweka haya yote mikononi mwako
Kwakuwa Ufalme ni wako Nguvu na Utukufu hata Milele...
Amina...!!


Asanteni sana wapendwa katika Kristo Yesu kwakuwa nami,Baba wa Mbinguni aendelee kuwatendea sawasawa na mapenzi yake...
Nawapenda.

1Heshima apewayo mpumbavu haimfai;
ni kama theluji ya kiangazi,
au mvua ya wakati wa mavuno.
2Kama shomoro au mbayuwayu wasiotua,
kadhalika laana asiyostahili mtu haimtui.
3Mjeledi kwa farasi, lijamu kwa punda,
na fimbo kwa mgongo wa mpumbavu.
4Usimjibu mpumbavu kipumbavu,
usije ukafanana naye.
5Mjibu mpumbavu kama ustahilivyo upumbavu wake,
asije akajiona kuwa mwenye hekima zaidi.
6Kumtuma mpumbavu ujumbe,
ni kama kujikata miguu au kujitafutia shida.
7Methali mdomoni mwa mpumbavu,
ni kama miguu ya kiwete inayoninginia.
8Kumpa mpumbavu heshima,
ni kama kufunga jiwe kwenye kombeo.
9Mpumbavu anayejaribu kutumia methali,
ni kama mlevi anayejaribu kungoa mwiba mkononi.
10Mtu amwajiriye mpumbavu au mlevi,
ni kama mpiga upinde anayejeruhi kila mtu.26:10 aya ya 10 makala ya Kiebrania si dhahiri.
11Mpumbavu anayerudiarudia upumbavu wake,
ni kama mbwa anayekula matapishi yake.
12Wamwona mtu ajionaye kuwa mwenye hekima?
Nakuambia mpumbavu ni nafuu kuliko huyo.
13Mvivu husema: “Huko nje kuna simba;
siwezi kwenda huko.”
14Kama vile mlango uzungukiapo bawaba zake,
ndivyo mvivu juu ya kitanda chake.
15Mvivu huutia mkono wake katika sahani ya chakula,
lakini hawezi kuuinua hadi mdomoni.
16Mvivu hujiona kuwa mwenye hekima
kuliko watu saba wawezao kujibu kwa busara.
17Ajiingizaye katika ugomvi usiomhusu,
ni kama mtu amshikaye masikio mbwa anayepita.
18Kama mwendawazimu achezeavyo mienge,
au mishale ya kifo,
19ndivyo alivyo mtu ampotoshaye jirani,
kisha aseme, “Nilikuwa natania tu!”
20Bila kuni, moto huzimika;
bila mchochezi, ugomvi humalizika.
21Kama vile makaa au kuni huchochea moto,
ndivyo mgomvi achocheavyo ugomvi.
22Maneno ya msengenyaji ni kama kitoweo;
hushuka mpaka ndani kabisa tumboni.
23Kama rangi angavu iliyopakwa kigae,
ndivyo yalivyo maneno matamu yenye nia mbaya.
24Mwenye chuki huficha chuki yake kwa maneno mazuri,
lakini huwa ana hila moyoni mwake.
25Akiongea vizuri usimwamini,
moyoni mwake mna chuki chungu nzima.
26Huenda akaficha chuki yake,
lakini nia zake mbaya zitajulikana kwa wote.
27Amchimbiaye mwenzake shimo, hutumbukia mwenyewe;
abingirishaye jiwe litamrudia mwenyewe.
28Asemaye uongo huwachukia hao anaowaumiza,
naye abembelezaye huleta maangamizi.

Methali26;1-28

Biblia Habari Njema kwa Watu Wote(BHN)

"Swahili Na Waswahili"Mbarikiwe.

Wednesday 24 July 2019

Kikombe Cha Asubuhi ; Methali 25...

Shalom,Habari za Asubuhi,Hamjambo,Mmeamkaje?

Tumshukuru Mungu wetu katika yote...

Asante  Mungu wetu kwa wema na fadhili zako kwetu
Asante kwa ulinzi wako kwetu wakati wote
Asante kwa kutuchagua tena na kutupa
kibali cha kuendelea kuiona leo hii
Asante kwa pumzi/uzima,afya na kuwatayari kwa majukumu yetu


Utukuzwe ee Mungu wetu,usifiwe Baba wa Mbinguni

Neema yako yatutosha  Mungu wetu..!

“Ufuatao ni mwongozo wa ibada kuhusu sadaka za amani ambazo mtu aweza kumtolea Mwenyezi-Mungu. Ikiwa mtu anatoa sadaka hiyo ya kumshukuru Mungu, basi, ataitoa pamoja na maandazi yasiyotiwa chachu yaliyopakwa mafuta, mikate myembamba iliyopakwa mafuta na maandazi ya unga laini uliochanganywa na mafuta.
Baba wa Mbinguni tunakuja mbele zako tukijinyenyekeza,tukijishusha na kujiachilia mikononi mwako
Mungu wetu tunaomba utusamehe dhambi zetu zote
Baba wa Mbinguni nasi tunaomba utupe neema ya kuweza kuwasamehe wale wote waliotukosea,Usitutie majaribuni Mungu wetu tunaomba utuepushe na yule mwovu na kazi zake zote,Jehovah ututakase miili yetu na akili zetu Baba wa Mbinguni tunaomba utufunike kwa  Damu ya Bwana na Mwokozi wetu Yesu Kristo wa Nazareti,
Yeye aliteseka kwanza ili sisi tupate kupona....

Pamoja na sadaka hiyo yake ya amani ya kumshukuru Mungu, ataleta maandazi yaliyotiwa chachu. Kutokana na maandazi hayo, atamtolea Mwenyezi-Mungu andazi moja kutoka kila sadaka; maandazi hayo yatakuwa yake kuhani anayeirashia madhabahu damu ya sadaka za amani.
Mungu wetu tunaomba ukabariki kazi za mikono yetu
Baba wa Mbinguni tunaomba ukatupe ubunifu na maarifa 
katika utendaji
Jehovah nasi tukatende sawasawa na mapenzi yako
Baba wa Mbinguni tunaomba ukabariki ridhiki zetu
ziingiazo/zitokazo
Mungu wetu nasi tunaomba ukatupe neema ya kuweza
kuwabariki wenye kuhitaji
Yahweh tusipungukiwe katika mahitaji yetu
Mungu wetu ukatupe kama inavyokupendeza wewe

Jehovah tunayaweka maisha yetu mikononi mwako
Baba wa Mbinguni tunaomba ukabariki nyumba/ndoa zetu,
watoto,wazazi wetu,familia/ndugu na wote wanaotuzunguka
Jehovah tunaomba ulinzi wako kwetu na kwa vyote tunavyo vimiliki
Yahweh tunaomba ukatubariki tuingiapo/tutokapo
Mungu wetu tunaomba ukavibariki vyote tunavyoenda kugusa/kutumia
Baba wa Mbinguni ukavitakase kwa Damu ya Bwana wetu Yesu Kristo
Mungu wetu ukatamalaki na kutuatamia
Baba wa Mbinguni tukawe salama rohoni
Mfalme wa amani amani yako ikatawale katika maisha yetu
Mungu wetu ukatupe macho ya kuona na masikio ya kusikia 
sauti yako na kuitii
Baba wa Mbinguni tunaomba ukatupe neema ya kufuata njia zako
Yahweh tukasimamie Neno lako amri na sheria zako siku zote 
za maisha yetu

Mungu  wetu ukaonekane katika maisha yetu popote tupitapo na ikajulikane kwamba upo 

Neema zako zikawe nasi Nuru yako ikaangaze katika maisha yetu
Ukatufanye barua njema ee Mungu wetu nasi tukasomeke kama
inavyokupendeza wewe
Roho Mtakatifu akatuongoze katika yote na tukawe na kiasi...

Nyama ya sadaka hiyo ya amani ya kumshukuru Mungu italiwa siku hiyohiyo inapotolewa; hataacha hata sehemu yake hadi asubuhi.
Tazama wenye shida/tabu,Mungu wetu tunaomba
 ukawaguse kila mmoja na mahitaji yake
Baba wa Mbinguni tunaomba ukawasamehe pale walipokwenda
kinyume nawe
Mungu wetu ukawape neema ya kujiombea,macho ya rohoni,masikio yakusikia sauti yako,wakafuate njia zako nazo zikawaweke huru
Mungu wetu tunaomba ukasikie kulia kwao
Baba wa Mbinguni tunomba ukawafute machozi yao
Nuru yako ikaangaze katika maisha yao
Mungu wetu tunaomba ukawatendee sawasawa na mapenzi yako
Kwakuwa Ufalme ni wako Nguvu na Utukufu hata Milele
Amina....!!!


Wapendwa katika Kristo Yesu asanteni sana
kwakuwanami/kunisoma

Mungu Baba aendelee kuwabariki na kuwatendea
kama inavyompendeza yeye
Amani ya Bwana wetu Yesu Kristo na upendo wa Mungu Baba
ukae nanyi daima....

Nawapenda.

Methali zaidi za Solomoni
1Hizi nazo ni methali nyingine za mfalme Solomoni walizonakili watu wa Hezekia, mfalme wa Yuda.
2Mungu hutukuzwa kwa kuficha mambo,
lakini mfalme hutukuzwa kwa yale anayoeleza.
3Kama zilivyo mbali mbingu na kirefu kina cha ardhi
ndivyo zisivyochunguzika akili za mfalme.
4Toa takataka katika fedha,
na mhunzi atakutengenezea chombo kizuri.
5Waondoe waovu mbele ya mfalme,
na utawala wake utaimarika katika haki.
6Usijipendekeze kwa mfalme,
wala usijifanye mtu mkubwa,
7maana ni heri kuambiwa, “Njoo huku mbele”,
kuliko kuporomoshwa mbele ya mkuu.
Mambo uliyoyaona kwa macho yako,
8usiharakishe kuyapeleka mahakamani;
maana utafanya nini hapo baadaye,
shahidi mwingine akibatilisha hayo usemayo?
9Suluhisha ugomvi na mwenzako peke yake,
na kila mmoja wenu asitoe siri ya mwenzake;
10watu wasije wakajua kuna siri,
ukajiharibia jina lako daima.
11Neno lisemwalo wakati unaofaa,
ni kama nakshi za dhahabu juu ya madini ya fedha.
12Onyo la mwenye hekima kwa mtu msikivu,
ni bora kuliko pete au vito vya dhahabu safi.
13Mjumbe mwaminifu humfurahisha yule aliyemtuma,
kama maji baridi wakati wa joto la mavuno.
14Kama vile mawingu na upepo bila mvua,
ndivyo alivyo mtu anayejigamba kutoa zawadi asiitoe.
15Kwa uvumilivu mtawala huweza kushawishika;
ulimi laini huvunja mifupa.
16Upatapo asali kula kiasi cha kukutosha,
usije ukaikinai na kuitapika.
17Usimtembelee jirani yako mara kwa mara,
usije ukamchosha naye akakuchukia.
18Mtu atoaye ushahidi wa uongo dhidi ya mwenziwe,
ni hatari kama rungu, upanga au mshale mkali.
19Kumtegemea mtu asiyeaminika wakati wa taabu,
ni kama jino bovu au mguu ulioteguka.
20Kumwimbia mtu mwenye huzuni,
ni kama kuvua nguo wakati wa baridi,
au kutia siki katika kidonda.
21Adui yako akiwa na njaa, mpe chakula;
akiwa na kiu, mpe maji ya kunywa.
22Hivyo utafanya apate aibu kali,
kama makaa ya moto kichwani pake,
naye Mwenyezi-Mungu atakutuza.
23Upepo wa kusi huleta mvua,
hali kadhalika masengenyo huleta chuki.
24Afadhali kuishi pembeni juu ya paa,
kuliko kuishi nyumbani pamoja na mwanamke mgomvi.
25Kama vile maji baridi kwa mwenye kiu,
ndivyo habari njema kutoka mbali.
26Mwadilifu akubaliye kufuata mambo ya mwovu,
ni chemchemi iliyochafuliwa au kisima kilichotibuliwa.
27Si vizuri kula asali nyingi mno;
kadhalika haifai kujipendekeza mno.25:27 kadhalika … mno: Maana katika Kiebrania si dhahiri.
28Mtu asiyeweza kuzuia hasira yake,
ni kama mji usio na ulinzi unaposhambuliwa.

Methali25;1-28

Biblia Habari Njema kwa Watu Wote(BHN)

"Swahili Na Waswahili"Mbarikiwe.

Tuesday 23 July 2019

Kikombe Cha Asubuhi ; Methali 24...


Shalom,Habari za Asubuhi,Hamjambo,Mmeamkaje?

Tumshukuru Mungu katika yote....

Mungu wetu Baba yetu,Muumba wetu Muumba wa Mbingu na Nchi
Muumba wa vyote vilivyomo vinavyoonekana na visivyoonekana
Mungu wa walio hai,Mungu  mwenye huruma,Mungu wa upendo
Mungu wa Abrahamu,Isaka na Yakobo...

Asante kwa wema na fadhili zako kwetu

Asante kwa ulinzi wako kwetu wakati wote
Asante kwa kutuchagua tena na kutupa
kibali cha kuendelea kuiona leo hii
Asante kwa pumzi/uzima,afya na kuwatayari kwa majukumu yetu

Neema yako yatutosha ee Mungu wetu....!!

Sheria ni moja kuhusu sadaka ya kuondoa hatia na sadaka ya kuondoa dhambi: Kuhani anayefanya ibada ya upatanisho ndiye atakayeichukua.
Baba wa Mbinguni tunakuja mbele zako tukijinyenyekeza,tukijishusha na kujiachilia mikononi mwako
Mungu wetu tunaomba utusamehe dhambi zetu zote 
Baba wa Mbinguni nasi tunaomba ukatupe neema
ya kuweza kuwasamehe wale wote waliotukosea
Usitutie majaribuni Mungu wetu tunaomba utuepushe
na yule mwovu na kazi zake zote
Jehovah ututakase miili yetu na akili zetu
Baba wa Mbinguni tunaomba utufunike kwa Damu
ya Bwana na Mwokozi wetu Yesu Kristo wa Nazareti
yeye aliteseka kwanza ili sisi tupate kupona....

Kuhani anayetoa sadaka ya kuteketezwa ya mtu yeyote, atachukua ngozi ya mnyama aliyetolewa. Sadaka yoyote ya nafaka iliyookwa jikoni au katika sufuria au katika kikaango itakuwa mali ya kuhani anayeitoa.
Mungu wetu tunaomba ukabariki kazi za mikono yetu
Baba wa Mbinguni tunaomba ukatupe ubunifu na maarifa katika utendaji
Jehovah nasi tukatende sawasawa na mapenzi yako
Yahweh tunaomba ukabariki ridhiki zetu ziingiazo/zitokazo
Mungu wetu nasi tunaomna ukatupe neema ya kuweza kuwabariki wenye kuhitaji
Tusipungukiwe katika mahitaji yetu
Baba wa Mbinguni tunaomba ukatupe kama inavyokupendeza wewe...

Yahweh tunayaweka maisha yetu mikononi mwako
Mungu wetu tunaomba ukabariki nyumba/ndoa zetu,
Jehovah tunaomba ulinzi wako kwetu na kwa vyote tunavyovimiliki
Yahweh tunaomba ukatubariki tuingiapo/tutokapo
Mungu wetu tunaomba ukavibariki vyote tunavyoenda kugusa/kutumia
Baba wa Mbinguni ukavitakase kwa Damu ya Bwana wetu Yesu Kristo
Mungu wetu ukatamalaki na kutuatamia
Baba wa Mbinguni tukawe salama rohoni
Yahwe ukatupe akili ya kutambua mema na mabaya
Mfalme wa amani amani yako ikatawale katika maisha yetu
Mungu wetu ukatupe macho ya kuona,masikio ya kusikia sauti yako na kuitii..
Baba wa Mbinguni  tunaomba ukatupe neema ya kufuata
njia zako,tukasimamie Neno lako,amri na sheria zako
siku zote za maisha yetu...
Ukatuguse kwa mkono wako wenye nguvu,ukatufanye chombo chema
ee Mungu wetu nasi tukatumike kama inavyokupendeza wewe
Roho Mtakatifu akatuongoze katika yote na tukawe na kiasi....

Kila sadaka ya nafaka, iwe imechanganywa na mafuta au kavu, itakuwa ya wazawa wa Aroni, na wote wagawiwe kwa sawa.
Tazama watoto wako wenye shida/tabu,wote wanaopitia magumu/majaribu mbalimbali
Mungu wetu tunaomba ukawaguse kwa mkono wako wenye nguvu
kila mmoja na mahitaji yake
Mungu wetu tunaomba ukawasamehe pale walipo kwenda kinyume nawe
Yahweh tunaomba ukawape neema ya kuweza kujiombea,kufuata njia zako nazo zikawaweke huru...
Baba wa Mbinguni tunayaweka haya yote mikononi mwako
Kwakuwa Ufalme ni wako Nguvu na Utukufu hata Milele...
Amina...!!


Asanteni sana wapendwa katika Kristo Yesu kwakuwa nami,Baba wa Mbinguni aendelee kuwatendea sawasawa na mapenzi yake...
Nawapenda.

- 19 -
1Usiwaonee wivu watu waovu,
wala usitamani kuwa pamoja nao,
2maana fikira zao zote ni juu ya ukatili,
hamna jema lolote litokalo midomoni mwao.
- 20 -
3Nyumba hujengwa kwa hekima,
na kuimarishwa kwa busara.
4Kwa maarifa vyumba vyake hujazwa
vitu vya thamani na vya kupendeza.
- 21 -
5Kuwa na hekima ni bora kuliko kuwa na nguvu,24:5 Kuwa … nguvu: Au Mwenye hekima anampita mwenye nguvu.
naam, maarifa ni bora kuliko nguvu.
6Maana kwa mwongozo mzuri waweza kupigana vita,
na kwa washauri wengi ushindi hupatikana.
- 22 -
7Kwa mpumbavu hekima ni ngumu kuielewa;
penye mkutano wa mashauri hafungui mdomo.
- 23 -
8Afikiriaye kutenda maovu daima
ataitwa mtu mwenye fitina.
9Mpango anaofikiria mpumbavu ni dhambi;
mwenye dharau huchukiwa na kila mtu.
- 24 -
10Ukifa moyo wakati wa shida,
basi wewe ni dhaifu kweli.
- 25 -
11Mwokoe mtu anayechukuliwa kuuawa bure;
usisite kumwokoa anayeuawa bila hatia.
12Usiseme baadaye: “Hatukujua!”
Maana Mungu apimaye mioyo ya watu huona;
yeye atakulipa kulingana na matendo yako!
- 26 -
13Mwanangu, ule asali maana ni nzuri;
sega la asali ni tamu mdomoni.
14Ndivyo ilivyo hekima nafsini mwako;
ukiipata utakuwa na matazamio mema,
wala tumaini lako halitakuwa la bure.
- 27 -
15Usivizie kama mwovu kushambulia makao ya mtu mwema,
wala usijaribu kuiharibu nyumba yake,
16maana mtu mwema huanguka mara nyingi lakini huinuka,
lakini mtu mwovu huangamizwa na janga.
- 28 -
17Usishangilie kuanguka kwa adui yako;
usifurahie moyoni mwako kujikwaa kwake,
18maana Mwenyezi-Mungu aonaye hayo hatapendezwa;
huenda akaacha kumwadhibu.
- 29 -
19Usihangaike kwa sababu ya watenda mabaya,
wala usiwaonee wivu watu waovu,
20maana mwovu hatakuwa na mema baadaye;
taa ya uhai wake itazimwa.
- 30 -
21Mwanangu, umche Mwenyezi-Mungu na kumheshimu mfalme,
wala usishirikiane na wale wasio na msimamo,
22maana maangamizi yao huwapata ghafla.
Hakuna ajuaye maafa watakayozusha.24:22 Hakuna … watakayozusha: Au Hakuna ajuaye maafa yatakayosababishwa na Mungu au mfalme.
Misemo zaidi
23Ifuatayo pia ni misemo ya wenye hekima:
Kupendelea watu katika hukumu si vizuri.
24Anayemwachilia mtu mwenye hatia,
hulaaniwa na watu na kuchukiwa na mataifa.
25Lakini wanaowaadhibu waovu watapata furaha,
na baraka njema zitawajia.
26Jibu lililo la haki,
ni kama busu la rafiki.
27Kwanza fanya kazi zako nje,
tayarisha kila kitu shambani,
kisha jenga nyumba yako.
28Usishuhudie bure dhidi ya jirani yako,
wala usiseme uongo juu yake.
29Usiseme, “Nitamtenda kama alivyonitenda!
Ni lazima nilipize kisasi!”
30Nilipitia karibu na shamba la mvivu;
shamba la mzabibu la mtu mpumbavu.
31Nilishangaa kuona limemea miiba,
magugu yamefunika eneo lake lote,
na ukuta wake wa mawe umebomoka.
32Nilitazama, nikawaza,
mwishowe nikapata funzo:
33 Taz Meth 6:10-11 Lala tu kidogo; sinzia tu kidogo!
Kunja mikono yako tu upumzike!
34Lakini kumbuka kwamba uwapo usingizini,
umaskini utakuvamia kama mnyanganyi,
ufukara kama mtu mwenye silaha.


Methali24;1-34

Biblia Habari Njema kwa Watu Wote(BHN)

"Swahili Na Waswahili"Mbarikiwe.

Monday 22 July 2019

Kikombe Cha Asubuhi ; Methali 23...

Shalom,Habari za Asubuhi,Hamjambo,Mmeamkaje?

Haleluyah ni siku/wiki nyingine tena Mungu wetu ametuchagua

na kutupa kibali cha kuendelea kuiona leo hii
Si kwamba sisi tumetenda mema sana wala si kwa nguvu zetu
si kwa utashi wetu wala si kwa akili zetu si kwamba sisi
ni wazuri mno si kwa uwezo wetu sisi kuwa hivi tulivyo leo hii
Ni kwa rehema/neema zake ni kwa mapenzi yake Mungu wetu....

Tumshukuru Mungu wetu katika yote...

Asante Mungu wetu kwa wema na fadhili zako kwetu
Asante kwa ulinzi wako kwetu wakati wote
Asante kwa pumzi/uzima,afya na kuwa tayari kwa majukumu yetu
Sifa na Utukufu tunakurudshia Mungu wetu....!!

“Ufuatao ni mwongozo wa ibada kuhusu sadaka ya kuondoa hatia. Sadaka hiyo ni takatifu kabisa. Mnyama wa sadaka ya kuondoa hatia atachinjiwa mahali wanapochinjiwa wanyama wa sadaka za kuteketezwa, na damu yake itarashiwa madhabahu pande zake zote.
Tazama jana imepita ee Mungu wetu leo ni siku mpya na kesho ni siku nyingine Jehovah tunakuja mbele zako tukijinyenyekeza,tukijishusha na kujiachilia mikononi mwako
 Mungu wetu tunaomba utusamehe dhambi zetu zote tulizozifanya kwakuwaza,kwakunena,kwakutenda,kwakujua/kutojua
Baba wa Mbinguni nasi tunaomba utupe neema ya kuweza kuwasamehe wale wote waliotukosea
Jehovah usitutie majaribu Mungu wetu tunaomba utuepushe na yule mwovu na kazi zake zote
Yahweh tunaomba ututakase miili yetu na akili zetu
Baba wa Mbinguni utufunike kwa Damu ya Bwana na Mwokozi wetu Yesu Kristo wa Nazareti
yeye aliteseka kwanza ili sisi tupate kupona
Kwakupigwa kwake sisi tumepata kupona....

Mafuta yake yote: Mafuta ya mkia na yale yanayofunika matumbo yatatolewa na kuteketezwa pamoja na zile figo mbili pamoja na mafuta yake na ile sehemu bora ya ini.
Yahweh tunaomba ukabariki kazi za mikono yetu
Baba wa Mbinguni tunaomba ukatupe ubunifu na maarifa 
katika utendaji
Jehovah nasi tukatende sawasawa na mapenzi yako
Baba wa Mbinguni tunaomba ukabariki ridhiki zetu
ziingiazo/zitokazo
Mungu wetu nasi tunaomba ukatupe neema ya kuweza
kuwabariki wenye kuhitaji
Yahweh tusipungukiwe katika mahitaji yetu
Mungu wetu ukatupe kama inavyokupendeza wewe

Baba wa Mbinguni tunayaweka maisha yetu mikononi mwako
Mungu wetu tunaomba ukabariki nyumba/ndoa zetu,
watoto,wazazi wetu,familia/ndugu na wote wanaotuzunguka
Jehovah tunaomba ulinzi wako kwetu na kwa vyote tunavyo vimiliki
Yahweh tunaomba ukatubariki tuingiapo/tutokapo
Mungu wetu tunaomba ukavibariki vyote tunavyoenda kugusa/kutumia
Baba wa Mbinguni ukavitakase kwa Damu ya Bwana wetu Yesu Kristo
Mungu wetu ukatamalaki na kutuatamia
Baba wa Mbinguni tukawe salama rohoni
Mfalme wa amani amani yako ikatawale katika maisha yetu
Mungu wetu ukatupe macho ya kuona na masikio ya kusikia 
sauti yako na kuitii
Baba wa Mbinguni tunaomba ukatupe neema ya kufuata njia zako
Yahweh tukasimamie Neno lako amri na sheria zako siku zote 
za maisha yetu
Mungu wetu ukaonekane katika maisha yetu
Neema zako zikawe nasi Nuru yako ikaangaze katika maisha yetu
ukatuguse kwa mkono wako wenye nguvu
Ukatufanye chombo chema ee Mungu wetu nasi tukatumike kama
inavyokupendeza wewe
Roho Mtakatifu akatuongoze katika yote na tukawe na kiasi...


Kuhani ataviteketeza juu ya madhabahu kama sadaka anayotolewa Mwenyezi-Mungu kwa moto. Hiyo ni sadaka ya kuondoa hatia. Wanaoruhusiwa kula sadaka hiyo ni wanaume wa ukoo wa makuhani peke yao; ni sadaka takatifu kabisa. Italiwa katika mahali patakatifu.
Mungu wetu tunawaweka mikononi mwako wenye shida/tabu,wote wanaopitia magumu/majaribu mbalimbali
Mungu wetu tunaomba ukawaguse kwa mkono wako wenye nguvu
 kila mmoja na mahitaji yake 
Mungu wetu tunaomba ukawasamehe pale walipokwenda kinyume nawe
Baba wa Mbinguni ukawape neema ya kujiombea,kufuata njia zako
wakasimaie Neno lako nalo likaweke huru
Mungu wetu tunaomba ukasikie kuomba kwetu
Mungu wetu ukawatendee sawasawa na mapenzi yako
Kwakuwa Ufalme ni wako Nguvu na Utukufu hata Milele
Amina...!!


Asanteni sana wapendwa katika Kristo Yesu kwakuwa nami
Mungu Baba aendelee kuwabariki na kuwatendea 
kama inavyompendeza yeye....
Nawapenda.

- 6 -
1Ukiketi kula pamoja na mtawala,
usisahau hata kidogo uko pamoja na nani.
2Zuia sana hamu yako,
ikiwa wewe wapenda sana kula.
3Usitamani vyakula vyake vizuri,
maana vyaweza kukudanganya.
- 7 -
4Ikiwa unayo hekima ya kutosha,
usijitaabishe kutafuta utajiri.
5Kufumba na kufumbua utajiri hutoweka,
huwa kama umepata mabawa ghafla,
ukaruka na kutowekea angani kama tai.
- 8 -
6Usile chakula cha mtu bahili,
wala usitamani mapochopocho yake,
7maana moyoni mwake anahesabu unachokula.23:7 maana … unachokula: Maana katika Kiebrania si dhahiri.
Atakuambia, “Kula, kunywa!”
Lakini moyoni mwake hayuko pamoja nawe.
8Utatapika vipande ulivyokula;
shukrani zako zote zitakuwa za bure.
- 9 -
9Usiseme maneno yako mbele ya mpumbavu,
maana atapuuza hekima ya maneno yako.
- 10 -
10Usiondoe alama ya mpaka wa zamani,
wala usiingilie mashamba ya yatima,
11maana Mungu, Mkombozi, ni mwenye nguvu,
naye ataitetea haki yao dhidi yako.
- 11 -
12Tumia akili zako kufuata mafundisho;
tumia masikio yako kusikiliza maarifa.
- 12 -
13Usiache kumrudi mtoto;
ukimchapa kiboko hatakufa.
14Ukimtandika kiboko,
utayaokoa maisha yake na kuzimu.
- 13 -
15Mwanangu, moyo wako ukiwa wenye busara,
moyo wangu pia utakuwa wenye furaha.
16Moyo wangu utashangilia,
mdomo wako utakaposema maneno yaliyo sawa.
- 14 -
17Moyo wako usiwaonee wivu wenye dhambi,
ila endelea kumcha Mwenyezi-Mungu siku zote.
18Hakika kuna kesho ya milele,
na tumaini lako halitakuwa bure.
- 15 -
19Sikia mwanangu, uwe na hekima;
fikiria sana jinsi unavyoishi.
20Usiwe mmoja wa walevi wa divai,
wala walafi wenye kupenda nyama,
21maana walevi na walafi wataishia kuwa maskini,
anayetumia siku yake kusinzia atavaa matambara.
- 16 -
22Msikilize baba yako aliyekuzaa,
wala usimdharau mama yako akizeeka.
23Nunua ukweli, wala usiuuze;
nunua hekima, mafunzo na busara.
24Baba wa mtoto mwadilifu atajaa furaha;
anayemzaa mtoto mwenye hekima atamfurahia.
25Wafurahishe baba na mama yako;
mama aliyekuzaa na afurahi.
- 17 -
26Mwanangu, nisikilize kwa makini,
shikilia mwenendo wa maisha yangu.
27Malaya ni shimo refu la kutega watu;
mwanamke mgeni ni kama kisima chembamba.
28Yeye hunyemelea kama mnyanganyi,
husababisha wanaume wengi kukosa uaminifu.
- 18 -
29Ni nani wapigao yowe?
Ni nani wenye huzuni?
Ni nani wenye ugomvi?
Ni nani walalamikao?
Ni nani wenye majeraha bila sababu?
Ni nani wenye macho mekundu?
30Ni wale ambao hawabanduki penye divai,
wale wakaao chonjo kuonja divai iliyokolezwa.
31Usiitamani divai hata kwa wekundu wake,
hata kama inametameta katika bilauri,
na kushuka taratibu unapoinywa.
32Mwishowe huuma kama nyoka;
huchoma kama nyoka mwenye sumu.
33Macho yako yataona mauzauza,
moyo wako utatoa mambo yaliyopotoka.
34Utakuwa kama mtu alalaye katikati ya bahari,
kama mtu alalaye juu ya mlingoti wa meli.
35Utasema, “Walinichapa, lakini sikuumia;
walinipiga, lakini sina habari.
Nitaamka lini?
Ngoja nitafute kinywaji kingine!”


Methali23;1-35

Biblia Habari Njema kwa Watu Wote(BHN)

"Swahili Na Waswahili"Mbarikiwe.