Swahili na Waswahili

Swahili na Waswahili
Waswahili na Mswahili Rachel Siwa...Pamoja Daima!!

Tuesday 20 November 2018

Kikombe Cha Asubuhi ;Yobu 41...

Shalom,Habari za Asubuhi,Hamjambo,Mmeamkaje?

Tumshukuru Mungu katika yote....

Mungu wetu Baba yetu,Muumba wetu Muumba wa Mbingu na Nchi
Muumba wa vyote vilivyomo vinavyoonekana na visivyoonekana
Mungu wa walio hai,Mungu  mwenye huruma,Mungu wa upendo
Mungu wa Abrahamu,Isaka na Yakobo..
Yahweh..!Jehovah..! Adonai..!Elohim..!El Olam..!El Qanna..!
El Elyon..!El shaddai..!Emanueli...!-Mungu pamoja nasi...
Unastahili sifa Mungu wetu,Unastahili kuabudiwa Jehovah,
Unastahili kuhimidiwa Yahweh,Unastahili Kutukuzwa Baba wa Mbinguni....!



Asante kwa wema na fadhili zako kwetu
Asante kwa ulinzi wako kwetu wakati wote
Asante kwa kutuchagua tena na kutupa
kibali cha kuendelea kuiona leo hii
Asante kwa pumzi/uzima,afya na kuwatayari kwa majukumu yetu

Neema yako yatutosha ee Mungu wetu....!!


Wakafika mjini Kafarnaumu, na mara ilipofika Sabato, Yesu akaingia katika sunagogi, akaanza kufundisha. Watu wote waliomsikia walishangazwa na mafundisho yake, maana hakuwa anafundisha kama waalimu wao wa sheria, bali kama mtu mwenye mamlaka.

Baba wa Mbinguni tunakuja mbele zako tukijinyenyekeza,tukijishusha na kujiachilia mikononi mwako
Mungu wetu tunaomba utusamehe dhambi zetu zote tulizo zifanya
Kwakuwaza,kwakunena,kwakutenda,kwakujua/kutojua
Baba wa Mbinguni nasi tunaomba ukatupe neema
ya kuweza kuwasamehe wale wote waliotukosea
Usitutie majaribu Mungu wetu tunaomba utuepushe
na yule mwovu na kazi zake zote
Jehovah ututakase miili yetu na akili zetu
Baba wa Mbinguni tunaomba utufunike kwa Damu
ya Bwana na Mwokozi wetu Yesu Kristo wa Nazaretiyeye aliteseka kwanza ili sisi tupate kupona....


Mara akatokea mle ndani ya sunagogi mtu mmoja mwenye pepo mchafu, akapaza sauti, “Una nini nasi, wewe Yesu wa Nazareti? Je, umekuja kutuangamiza? Najua wewe ni nani: Wewe ni Mtakatifu wa Mungu!” Yesu akamkemea huyo pepo akisema, “Nyamaza! Mtoke mtu huyu.” Basi, huyo pepo mchafu akamtikisatikisa mtu huyo, kisha akalia kwa sauti kubwa, akamtoka.

Mungu wetu tunaomba ukabariki kazi za mikono yetu
Baba wa Mbinguni tunaomba ukatupe ubunifu na maarifa katika utendaji

Jehovah nasi tukatende sawasawa na mapenzi yako
Yahweh tunaomba ukabariki ridhiki zetu ziingiazo/zitokazo
Mungu wetu nasi tunaomba ukatupe neema ya kuweza
kuwabariki wenye kuhitaji
Tusipungukiwe katika mahitaji yetu Baba wa Mbinguni
tunaomba ukatupe kama inavyokupendeza wewe....



Yahweh  tunayaweka maisha yetu mikononi mwako
Mungu wetu tunaomba ukabariki nyumba/ndoa zetu,
watoto,wazazi wetu,familia/ndugu na wote wanaotuzunguka
Jehovah tunaomba ulinzi wako kwetu na kwa vyote tunavyo vimiliki
Yahweh tunaomba ukatubariki tuingiapo/tutokapo
Mungu wetu tunaomba ukavibariki vyote tunavyoenda kugusa/kutumia
Baba wa Mbinguni ukavitakase kwa Damu ya Bwana wetu Yesu Kristo
Mungu wetu ukatamalaki na kutuatamia
Baba wa Mbinguni tukawe salama rohoni

Yahweh ukatupe akili ya kutambua mema na mabaya
Mfalme wa amani amani yako ikatawale katika maisha yetu
Mungu wetu ukatupe macho ya kuona na masikio ya kusikia 
sauti yako na kuitii
Baba wa Mbinguni tunaomba ukatupe neema ya kufuata njia zako
Yahweh tukasimamie Neno lako amri na sheria zako siku zote 
za maisha yetu
Mungu wetu ukaonekane katika maisha yetu
Baba wa Mbinguni tukanene yaliyo yako
Neema zako zikawe nasi Nuru yako ikaangaze katika maisha yetu
ukatuguse kwa mkono wako wenye nguvu
Ukatufanye chombo chema ee Mungu wetu nasi tukatumike kama
inavyokupendeza wewe
Roho Mtakatifu akatuongoze katika yote na tukawe na kiasi...

Watu wote wakashangaa, wakaulizana, “Ni mambo gani haya? Je, ni mafundisho mapya? Mtu huyu anayo mamlaka ya kuamuru hata pepo wachafu, nao wanamtii!” Habari za Yesu zikaenea upesi kila mahali katika eneo la Galilaya.

Tazama watoto wako wanaokutafuta/kukuomba kwa bidii na imani, Mungu wetu tunawaweka mikononi mwako wenye shida/tabu,
wote wanaopitia magumu/majaribu mbalimbali
Mungu wetu tunaomba ukawaguse kwa mkono wako wenye nguvu
kila mmoja na mahitaji yake
Baba wa Mbinguni tunaomba ukaonekane katika maisha yao
Mungu wetu tunaomba ukawasamehe pale walipokwenda
kinyume nawe Yahweh tunaomba ukawape neema ya kujiombea
Kufuata njia zako nazo zikawaweke huru
Ukawape macho ya rohoni ee Mungu wetu na masikio ya kusikia
sauti yako,Ukawaokoe na kuwalinda,ukawaponye kimwili na kiroho
Nuru yako ikaangaze katika maisha yao,Amani ikatawale katika maisha yao,Upendo ukadumu kati yao
 

Baba wa Mbinguni tunayaweke haya yote mikono mwako
tukiamini Mungu wetu utawatendea sawasawa na mapenzi yako
Kwakuwa Ufalme ni wako Nguvu na Utukufu hata Milele
Amina...!!



Asanteni sana wapendwa katika Kristo Yesu
kwakuwanami/kunisoma Mungu Baba aendelee
kuwabariki na kuwatendea kama inavyompendeza yeye
Amani ya Bwana wetu Yesu Kristo na Upendo wa Mungu Baba
ukae nanyi daima
Nawapenda. 





1“Yeyote anayeliona hilo dude,
hufa moyo na kuzirai.
2Hakuna mtu yeyote mkali athubutuye kulishtua.
Nani, basi awezaye kusimama mbele yangu?
3Nani aliyenipa kitu, ili nitakiwe kumrudishia?
Chochote kilicho chini ya mbingu ni changu.41:3 maana katika makala ya Kiebrania si dhahiri.
4“Sitaacha kukueleza juu ya viungo vya hilo dude
au juu ya nguvu zake na umbo lake zuri.
5Nani awezaye kumbambua vazi lake la nje?
Nani awezaye kutoboa deraya lililovaa?
6Nani awezaye kufungua kinywa chake?
Meno yake pande zote ni kitisho!
7Mgongo41:7 Mgongo; kadiri ya Septuaginta: Makala ya Kiebrania: Fahari. wake umefanywa kwa safu za ngao
zilizoshikamana pamoja kama kwa mhuri,
8Kila moja imeshikamana na nyingine,
hata hewa haiwezi kupenya katikati yake.
9Yameunganishwa pamoja,
hata haiwezekani kuyatenganisha.
10Likipiga chafya, mwanga huchomoza,
macho yake humetameta kama jua lichomozapo.
11Kinywani mwake hutoka mienge iwakayo,
cheche za moto huruka nje.
12Puani mwake hufuka moshi,
kama vile chungu kinachochemka;
kama vile magugu yawakayo.
13Pumzi yake huwasha makaa;
mwali wa moto hutoka kinywani mwake.
14Shingo yake ina nguvu ajabu,
litokeapo watu hukumbwa na hofu.
15Misuli yake imeshikamana pamoja,
imara kama chuma wala haitikisiki.
16Moyo wake ni mgumu kama jiwe,
mgumu kama jiwe la kusagia.
17Linapoinuka, mashujaa hushikwa na woga,
kwa pigo moja huwa wamezirai.
18Hakuna upanga uwezao kulijeruhi,
wala mkuki, mshale au fumo.
19Kwake chuma ni laini kama unyasi,
na shaba kama mti uliooza.
20Mshale hauwezi kulifanya likimbie;
akitupiwa mawe ya teo huyaona kama makapi.
21Kwake, rungu ni kama kipande cha bua,
hucheka likitupiwa fumo kwa wingi.
22Tumbo lake ni kama limefunikwa na vigae vikali;
hukwaruza na kurarua udongo kama chombo cha kupuria.
23Bahari huisukasuka kama maji yachemkayo,
huifanya itoe povu kama chupa ya mafuta.
24Lipitapo huacha nyuma alama inayongaa;
povu jeupe huonekana limeelea baharini.
25Duniani hakuna kinachofanana nalo;
hilo ni kiumbe kisicho na hofu.
26Huwaona kuwa si kitu wote wenye kiburi;
hilo ni mfalme wa wanyama wote wakali.”



Yobu41;1-26

Biblia Habari Njema kwa Watu Wote(BHN)

"Swahili Na Waswahili"Mbarikiwe.

Monday 19 November 2018

Kikombe Cha Asubuhi ;Yobu 40...


Shalom,Habari za Asubuhi,Hamjambo,Mmeamkaje?

Haleluyah ni siku/wiki  nyingine tena Mungu wetu ametuchagua
na kutupa kibali cha kuendelea kuiona leo hii
Si kwamba sisi tumetenda mema sana wala si kwa nguvu zetu
si kwa utashi wetu wala si kwa akili zetu si kwamba sisi
ni wazuri mno si kwa uwezo wetu sisi kuwa hivi tulivyo leo hii
Ni kwa rehema/neema zake ni kwa mapenzi yake Mungu wetu....

Tumshukuru Mungu wetu katika yote...

Asante Mungu wetu kwa wema na fadhili zako kwetu
Asante kwa ulinzi wako kwetu wakati wote
Asante kwa pumzi/uzima,afya na kuwa tayari kwa majukumu yetu
Sifa na Utukufu tunakurudshia Mungu wetu....!!

Siku hizo, Yesu alifika kutoka Nazareti, mji wa Galilaya, akabatizwa na Yohane katika mto Yordani. Mara tu alipotoka majini, aliona mbingu zimefunguliwa, na Roho akishuka juu yake kama njiwa. Sauti ikasikika kutoka mbinguni: “Wewe ni Mwanangu mpendwa, nimependezwa nawe.” Mara akaongozwa na Roho kwenda jangwani, akakaa huko siku arubaini akijaribiwa na Shetani. Alikuwa huko pamoja na wanyama wa porini, nao malaika wakawa wanamhudumia.

Tazama jana imepita ee Mungu wetu leo ni siku mpya na kesho ni siku nyingine Jehovah tunakuja mbele zako tukijinyenyekeza,tukijishusha na kujiachilia mikononi mwako
 Mungu wetu tunaomba utusamehe dhambi zetu zote tulizozifanya kwakuwaza,kwakunena,kwakutenda,kwakujua/kutojua
Baba wa Mbinguni nasi tunaomba utupe neema ya kuweza kuwasamehe wale wote waliotukosea
Jehovah usitutie majaribu Mungu wetu tunaomba utuepushe na yule mwovu na kazi zake zote
Yahweh tunaomba ututakase miili yetu na akili zetu
Baba wa Mbinguni utufunike kwa Damu ya Bwana na Mwokozi wetu Yesu Kristo wa Nazareti
yeye aliteseka kwanza ili sisi tupate kupona
Kwakupigwa kwake sisi tumepata kupona...

Yohane alipokwisha fungwa gerezani, Yesu alikwenda Galilaya, akahubiri Habari Njema ya Mungu, akisema, “Wakati umetimia, na ufalme wa Mungu umekaribia. Tubuni na kuiamini Habari Njema!”
Yahweh tunaomba ukabariki kazi za mikono yetu
Baba wa Mbinguni tunaomba ukatupe ubunifu na maarifa 
katika utendaji
Jehovah nasi tukatende sawasawa na mapenzi yako
Baba wa Mbinguni tunaomba ukabariki ridhiki zetu
ziingiazo/zitokazo
Mungu wetu nasi tunaomba ukatupe neema ya kuweza
kuwabariki wenye kuhitaji
Yahweh tusipungukiwe katika mahitaji yetu
Mungu wetu ukatupe kama inavyokupendeza wewe

Baba wa Mbinguni tunayaweka maisha yetu mikononi mwako
Mungu wetu tunaomba ukabariki nyumba/ndoa zetu,
watoto,wazazi wetu,familia/ndugu na wote wanaotuzunguka
Jehovah tunaomba ulinzi wako kwetu na kwa vyote tunavyo vimiliki
Yahweh tunaomba ukatubariki tuingiapo/tutokapo
Mungu wetu tunaomba ukavibariki vyote tunavyoenda kugusa/kutumia
Baba wa Mbinguni ukavitakase kwa Damu ya Bwana wetu Yesu Kristo
Mungu wetu ukatamalaki na kutuatamia
Baba wa Mbinguni tukawe salama rohoni
Mfalme wa amani amani yako ikatawale katika maisha yetu
Mungu wetu ukatupe macho ya kuona na masikio ya kusikia 
sauti yako na kuitii
Baba wa Mbinguni tunaomba ukatupe neema ya kufuata njia zako
Yahweh tukasimamie Neno lako amri na sheria zako siku zote 
za maisha yetu
Mungu wetu ukaonekane katika maisha yetu
Neema zako zikawe nasi Nuru yako ikaangaze katika maisha yetu
ukatuguse kwa mkono wako wenye nguvu
Ukatufanye chombo chema ee Mungu wetu nasi tukatumike kama
inavyokupendeza wewe
Roho Mtakatifu akatuongoze katika yote na tukawe na kiasi...

Alipokuwa anapita kando ya ziwa Galilaya, aliwaona wavuvi wawili: Simoni na Andrea ndugu yake wakivua samaki kwa wavu. Yesu akawaambia, “Nifuateni nami nitawafanya nyinyi kuwa wavuvi wa watu.” Mara wakaziacha nyavu zao, wakamfuata. Alipokwenda mbele kidogo, aliwaona Yakobo na Yohane, wana wa Zebedayo. Nao pia walikuwa ndani ya mashua yao wakizitengeneza nyavu zao. Yesu akawaita mara, nao wakamwacha baba yao Zebedayo katika mashua pamoja na wafanyakazi, wakamfuata.
Mungu wetu tunawaweka mikononi mwako wenye shida/tabu,wote wanaopotia magumu/majaribu mbalimbali
watoto wako wanaokuomba kwa bidii na imani
Mungu wetu tunaomba ukawaguse kwa mkono wako wenye nguvu
 kila mmoja na mahitaji yake 
Yahweh tunaomba ukaonekane katika maisha yao
Jehovah tunaomba ukawaokoe,ukawavushe salama na  kuwalinda
Mungu wetu tunaomba ukawasamehe pale walipokwenda kinyume nawe
Baba wa Mbinguni ukawape neema ya kujiombea,kufuata njia zako
wakasimaie Neno lako nalo likaweke huru
Mungu wetu tunaomba ukasikie kuomba kwetu
Baba wa Mbinguni ukapokee sala/maombi yetu
Mungu wetu ukawatendee sawasawa na mapenzi yako
Kwakuwa Ufalme ni wako Nguvu na Utukufu hata Milele
Amina...!!

Asanteni sana wapendwa katika Kristo Yesu kwakuwa nami
Mungu Baba aendelee kuwabariki na kuwatendea 
kama inavyompendeza yeye....
Nawapenda.


1Mwenyezi-Mungu akaendelea kumwambia Yobu:
2“Je, wewe mwenye kuchunguza makosa utashindana na Mungu Mwenye Nguvu?
Wewe unayebishana nami Mungu, basi jibu mambo hayo!”
3Kisha Yobu akamjibu Mwenyezi-Mungu:
4“Mimi sifai kitu nitakujibu nini?
Naufunga mdomo wangu.
5Nilithubutu kusema na sitasema tena.
Nilisisitiza lakini sitaendelea kusema zaidi.”
6Hapo Mwenyezi-Mungu akamjibu kutoka kimbunga:
7“Jikaze kama mwanamume.
Nitakuuliza, nawe utanijibu.
8Je, unataka kweli kubatilisha hukumu yangu,
kuniona nina hatia ili wewe usiwe na hatia?
9Je, una nguvu kama mimi Mungu?
Waweza kunguruma kwa sauti kama yangu?
10“Basi, jioneshe kuwa na fahari na ukuu,
ujipambe kwa utukufu na fahari.
11Wamwagie watu hasira yako kuu;
mwangalie kila mwenye kiburi na kumwangusha.
12Mwangalie kila mwenye kiburi na kumporomosha,
uwakanyage waovu mahali walipo.
13Wazike wote pamoja ardhini;
mfunge kila mmoja kwa kifungo cha kifo.
14Hapo nitakutambua,
kwamba nguvu yako mwenyewe imekupa ushindi.
15“Liangalie lile dude Behemothi,40:15 Behemothi: Mnyama huyo huenda ni kiboko.
nililoliumba kama nilivyokuumba wewe.
Hilo hula nyasi kama ng'ombe,
16lakini mwilini lina nguvu ajabu,
na misuli ya tumbo lake ni imara.
17Huufanya mkia wake mgumu kama mwerezi,
mishipa ya mapaja yake imeshonwa pamoja.
18Mifupa yake ni mabomba ya shaba,
viungo vyake ni kama pao za chuma.
19“Hilo ni la kwanza la ajabu kati ya viumbe vyangu!40:19 Hilo … vyangu: Au hilo ndilo tunda la kwanza la kazi ya Mungu.
Ni mimi Muumba wake niwezaye kulishinda.
20Milima wanamocheza wanyama wote wa porini
hutoa chakula chake.
21Hujilaza chini ya vichaka vya miiba,
na kujificha kati ya matete mabwawani.
22Hujisitiri katika vivuli vya vichaka vya miiba
na vya miti iotayo kando ya vijito.
23Mto ukifurika haliogopi,
halitishiki hata mto Yordani ukilifurikia kinywani.
24Nani awezaye kuliziba macho na kuliteka?
Nani awezaye kulitoboa pua kwa mtego?
25 Taz Zab 74:14; 104:26; Isa 27:1 40:25 Kufuatana na Biblia ya Kiebrania; baadhi ya tafsiri ni 41:1 Je, waweza kuvua dude Lewiyathani40:25 Lewiyathani: Au Mamba. kwa ndoana,
au kuufunga ulimi wake kwa kamba?
26Je, unaweza kulitia kamba puani mwake,
au kulitoboa taya kwa kulabu?
27Je, wadhani litakusihi uliachilie?
Je, litazungumza nawe kwa upole?
28Je, litafanya mapatano nawe,
ulichukue kuwa mtumishi wako milele?
29Je, utacheza nalo kama ndege,
au kulifunga kamba licheze na wajakazi wako?
30Wadhani wavuvi watashindania bei yake?
Je, wafanyabiashara watathubutu kulikata na kugawana?
31Je, waweza kuichoma ngozi yake kwa mikuki,
au kichwa chake kwa mfumo wa kuvua samaki?
32Jaribu tu kuligusa, uone cha mtema kuni;
Kamwe hutarudia tena kufanya hivyo!


Yobu40;1-32

Biblia Habari Njema kwa Watu Wote(BHN)

"Swahili Na Waswahili"Mbarikiwe.

Friday 16 November 2018

Kikombe Cha Asubuhi ;Yobu 39...


Shalom,Habari za Asubuhi,Hamjambo,Mmeamkaje?

Tumshukuru Mungu wetu katika yote...

Asante kwa wema na fadhili zako kwetu
Asante

 kwa ulinzi wako kwetu wakati wote
Asante kwa kutuchagua tena na kutupa
kibali cha kuendelea kuiona leo hii
Asante kwa pumzi/uzima,afya na kuwatayari kwa majukumu yetu


Utukuzwe ee Mungu wetu,usifiwe Baba wa Mbinguni

Jehovah  Jireh..!Jehovah Nissi..!Jehovah Raah..!
Jehovah Rapha..!Jehovah Shammah..!Jehovah Shamlom..!
Emanuel-Mungu pamohja nasi..!!
Neema yako yatutosha Baba wa Mbinguni..!

Habari Njema ya Yesu Kristo, Mwana wa Mungu. Ilianza kama ilivyoandikwa katika kitabu cha nabii Isaya: “Mungu alisema, ‘Namtuma mjumbe wangu akutangulie, ambaye atakutayarishia njia yako.’ Sauti ya mtu anaita jangwani: ‘Mtayarishieni Bwana njia yake, nyosheni barabara zake.’”

Baba wa Mbinguni tunakuja mbele zako tukijinyenyekeza,tukijishusha

na kujiachilia mikononi mwako
Mungu wetu tunaomba utusamehe dhambi zetu zote tulizo zifanya
Kwakuwaza,kwakunena,kwakutenda,kwakujua/kutojua
Baba wa Mbinguni nasi tunaomba ukatupe neema
ya kuweza kuwasamehe wale wote waliotukosea
Usitutie majaribu Mungu wetu tunaomba utuepushe
na yule mwovu na kazi zake zote
Jehovah ututakase miili yetu na akili zetu
Baba wa Mbinguni tunaomba utufunike kwa Damu
ya Bwana na Mwokozi wetu Yesu Kristo wa Nazareti
yeye aliteseka kwanza ili sisi tupate kupona...

Yohane Mbatizaji alitokea jangwani, akahubiri kwamba watu watubu na kubatizwa ili Mungu awasamehe dhambi zao. Watu kutoka sehemu zote za Yudea na wenyeji wote wa Yerusalemu walimwendea, wakaziungama dhambi zao, naye akawabatiza katika mto Yordani.

Mungu wetu tunaomba ukabariki kazi za mikono yetu

Baba wa Mbinguni tunaomba ukatupe ubunifu na maarifa 
katika utendaji
Jehovah nasi tukatende sawasawa na mapenzi yako
Baba wa Mbinguni tunaomba ukabariki ridhiki zetu
ziingiazo/zitokazo
Mungu wetu nasi tunaomba ukatupe neema ya kuweza
kuwabariki wenye kuhitaji
Yahweh tusipungukiwe katika mahitaji yetu
Mungu wetu ukatupe kama inavyokupendeza wewe



Jehovah tunayaweka maisha yetu mikononi mwako
Baba wa Mbinguni tunaomba ukabariki nyumba/ndoa zetu,
watoto,wazazi wetu,familia/ndugu na wote wanaotuzunguka
Jehovah tunaomba ulinzi wako kwetu na kwa vyote tunavyo vimiliki
Yahweh tunaomba ukatubariki tuingiapo/tutokapo
Mungu wetu tunaomba ukavibariki vyote tunavyoenda kugusa/kutumia
Baba wa Mbinguni ukavitakase kwa Damu ya Bwana wetu Yesu Kristo
Mungu wetu ukatamalaki na kutuatamia
Baba wa Mbinguni tukawe salama rohoni
Mfalme wa amani amani yako ikatawale katika maisha yetu
Mungu wetu ukatupe macho ya kuona na masikio ya kusikia 
sauti yako na kuitii
Baba wa Mbinguni tunaomba ukatupe neema ya kufuata njia zako
Yahweh tukasimamie Neno lako amri na sheria zako siku zote 
za maisha yetu

Mungu wetu tunaomba ukatupe akili ya kutambua mema na mabaya Baba wa Mbinguni ukaonekane katika maisha yetu popote tupitapo na ikajulikane kwamba upo Mungu wetu

Neema zako zikawe nasi Nuru yako ikaangaze katika maisha yetu
ukatuguse kwa mkono wako wenye nguvu
Ukatufanye barua njema ee Mungu wetu nasi tukasomeke kama
inavyokupendeza wewe
Roho Mtakatifu akatuongoze katika yote na tukawe na kiasi...

Yohane alikuwa amevaa vazi lililofumwa kwa manyoya ya ngamia, na ukanda wa ngozi kiunoni mwake. Chakula chake kilikuwa nzige na asali ya mwituni. Naye alihubiri akisema, “Baada yangu anakuja mwenye nguvu zaidi kuliko mimi, ambaye mimi sistahili hata kuinama na kufungua kamba za viatu vyake. Mimi ninawabatiza kwa maji, lakini yeye atawabatiza kwa Roho Mtakatifu.”


Tazama wenye shida/tabu,watoto wako wanaokutafuta kwa bidii na imani
Mungu wetu tunaomba ukawaguse kwa mkono wako wenye nguvu
Yahweh tunaomba  ukawaguse kila mmoja na mahitaji yake
Mungu wetu  unajua haja za mioyo ya kila mmoja
Baba wa Mbinguni tunaomba ukawasamehe pale walipokwenda
kinyume nawe
Mungu wetu ukawape neema ya kujiombea,macho ya rohoni,masikio yakusikia sauti yako,wakafuate njia zako nazo zikawaweke huru
Mungu wetu tunaomba ukasikie kulia kwao
Baba wa Mbinguni tunomba ukawafute machozi yao
Jehovah ukaonekane katika maisha yao
Nuru yako ikaangaze katika maisha yao
Mungu wetu tunaomba ukawatendee sawasawa na mapenzi yako
Kwakuwa Ufalme ni wako Nguvu na Utukufu hata Milele
Amina....!!!


Wapendwa katika Kristo Yesu asanteni sana
kwakuwanami/kunisoma

Mungu Baba aendelee kuwabariki na kuwatendea
kama inavyompendeza yeye
Amani ya Bwana wetu Yesu Kristo na upendo wa Mungu Baba
ukae nanyi daima....
Nawapenda.

1“Je, wajua mbuzi wa milimani huzaa lini,
au umewahi kuona kulungu akizaa?
2Je, wajua huchukua mimba kwa muda gani,
au siku yenyewe ya kuzaa waijua?
3“Wajua wakati watakapochuchumaa kuzaa,
wakati wa kuzaa watoto wao?
4Watoto wao hupata nguvu,
hukua hukohuko porini,
kisha huwaacha mama zao na kwenda zao.
5“Nani aliyemwacha huru pundamwitu?
Nani aliyewaacha waende kwa kuwafungua?
6Mimi niliwapa jangwa liwe makao yao,
mbuga zenye chumvi kuwa makazi yao.
7Hujitenga kabisa na makelele ya miji,
hasikilizi kelele ya kumfanyisha kazi.
8Hutembeatembea milimani kupata malisho,
na kutafuta chochote kilicho kibichi.
9“Je, nyati atakubali kukutumikia?
Au je, atakubali kulala zizini mwako?
10Je, waweza kumfunga nyati kamba kulima shamba,
au avute jembe la kulimia?
11Je, utamtegemea kwa kuwa ana nguvu nyingi
na kumwacha akufanyie kazi zako nzito?
12Je, wamtazamia nyati akuvunie mavuno yako,
na kuleta nafaka mahali pa kupuria?
13“Mbuni hupigapiga mabawa yake kwa madaha,
lakini hawezi kuruka kama korongo.39:13 aya hii katika Kiebrania si dhahiri.
14Mbuni huyaacha mayai yake juu ya ardhi
ili yapate joto mchangani;
15lakini hajui kama yanaweza kukanyagwa,
au kuvunjwa na mnyama wa porini.
16Mbuni huwatendea wanawe ukatili kama si wake,
hata kazi yake ikiharibika yeye hana wasiwasi;
17kwa sababu nilimfanya asahau hekima yake,
wala sikumpa sehemu yoyote ya akili.
18Lakini akianza kukimbia,
humcheka hata farasi na mpandafarasi.
19“Je, Yobu, ndiwe uliyewapa farasi nguvu,
ukawavika shingoni manyoya marefu?
20Je, ni wewe unayemfanya farasi aruke kama nzige?
Mlio wake wa maringo ni wa ajabu!
21Huparapara ardhi mabondeni kwa pupa;
hukimbilia kwenye mapigano kwa nguvu zake zote.
22Farasi huicheka hofu, na hatishiki;
wala upanga hauwezi kumrudisha nyuma.
23Silaha wachukuazo wapandafarasi,
hugongana kwa sauti na kungaa juani.
24Farasi husonga mbele, akitetemeka kwa hasira;
tarumbeta iliapo, yeye hasimami.
25Kila ipigwapo tarumbeta, yeye hutoa sauti;
huisikia harufu ya vita toka mbali,
huusikia mshindo wa makamanda
wakitoa amri kwa makelele.
26“Je, mwewe amejifunza kwako jinsi ya kuruka,
na kunyosha mabawa yake kuelekea kusini?
27Je, tai hupaa juu kwa amri yako,
na kuweka kiota chake juu milimani?
28Tai hufanya makazi yake juu ya miamba mirefu,
na ncha kali za majabali ndizo ngome zake.
29Kutoka huko huotea mawindo,
macho yake huyaona kutoka mbali.
30 Taz Mat 24:28; Luka 17:37 Makinda yake hufyonza damu;
pale ulipo mzoga ndipo alipo tai.”


Yobu39;1-30

Biblia Habari Njema kwa Watu Wote(BHN)

"Swahili Na Waswahili"Mbarikiwe.

Thursday 15 November 2018

Kikombe Cha Asubuhi ;Yobu 38...


Shalom,Habari za Asubuhi,Hamjambo,Mmeamkaje?

Haleluyah Mungu wetu yu mwema sana..
Tumshukuru Mungu wetu katika yote....

Mungu wetu Baba yetu,Muumba wetu Muumba wa Mbingu na Nchi
Baba wa Upendo,Baba wa faraja,Baba wa huruma,Baba wa Baraka
Mungu mwenye nguvu,Mungu mwenye kuponya
Mungu wa Abrahamu,Isaka na Yakobo,Muweza wa yote
Wewe ni mwanzo na wewe ni mwisho,Alfa na Omega...!!


Asante kwa wema na fadhili zako kwetu
Asante kwa ulinzi wako kwetu wakati wote
Asante kwa kutuchagua tena na kutupa
kibali cha kuendelea kuiona leo hii


Yesu aliuita tena ule umati wa watu, akawaambia, “Nisikilizeni nyote, mkaelewe. Hakuna kitu kinachoingia ndani ya mtu kutoka nje kinachoweza kumtia mtu unajisi. Lakini kinachotoka ndani ya mtu ndicho kinachomtia mtu unajisi.” Mwenye masikio na asikie! Alipouacha umati wa watu na kuingia nyumbani, wanafunzi wake walimwuliza maana ya huo mfano. Naye akawaambia, “Je, hata nyinyi hamwelewi? Je, hamwelewi kwamba kitu kinachomwingia mtu kutoka nje, hakiwezi kumtia unajisi, kwa maana hakimwingii moyoni, ila tumboni, na baadaye hutolewa nje chooni?” (Kwa kusema hivyo, Yesu alihalalisha vyakula vyote.) Akaendelea kusema, “Kinachotoka ndani ya mtu ndicho kinachomtia unajisi. Maana kutoka ndani, moyoni mwa mtu, hutoka mawazo mabaya, uasherati, wizi, uuaji, uzinzi, uchoyo, uovu, udanganyifu, ufisadi, wivu, kashfa, kiburi na upumbavu. Maovu hayo yote yatoka ndani ya mtu, nayo humtia mtu unajisi.”

Tazama Jana imepita ee Mungu wetu Leo ni siku mpya na kesho ni siku nyingineJehovah...
Yahweh tunakuja mbele zako tukijinyenyekeza,tukijishusha
na kujiachilia mikononi mwako
Mungu wetu tunaomba utusamehe dhambi zetu zote tulizo zifanya
Kwakuwaza,kwakunena,kwakutenda,kwakujua/kutojua
Baba wa Mbinguni nasi tunaomba ukatupe neema
ya kuweza kuwasamehe wale wote waliotukosea
Usitutie majaribu Mungu wetu tunaomba utuepushe
na yule mwovu na kazi zake zote
Jehovah ututakase miili yetu na akili zetu
Baba wa Mbinguni tunaomba utufunike kwa Damu
ya Bwana na Mwokozi wetu Yesu Kristo wa Nazareti

yeye aliteseka kwanza ili sisi tupate kupona



Yesu aliondoka hapo, akaenda wilaya ya Tiro. Huko aliingia katika nyumba moja na hakutaka mtu ajue; lakini hakuweza kujificha. Hapo mwanamke mmoja ambaye binti yake alikuwa na pepo, alisikia habari za Yesu. Basi, akaja akajitupa chini mbele ya miguu yake. Mama huyo alikuwa Mgiriki, mwenyeji wa Sirofoinike. Basi, akamwomba Yesu amtoe binti yake pepo mchafu. Yesu akamwambia, “Kwanza watoto washibe; kwa maana si vizuri kuchukua chakula cha watoto na kuwatupia mbwa.” Lakini huyo mama akasema, “Ni kweli, Bwana; lakini hata mbwa walio chini ya meza hula makombo ya watoto.” Yesu akamwambia, “Kwa sababu ya neno hilo, nenda. Pepo amemtoka binti yako!” Basi, akaenda nyumbani kwake, akamkuta mtoto amelala kitandani, na pepo amekwisha mtoka.

Mungu wetu tunaomba ukabariki kazi za mikono yetu
Baba wa Mbinguni tunaomba ukatupe ubunifu na maarifa katika utendaji
Jehovah nasi tukatende sawasawa na mapenzi yako
Yahweh tunaomba ukabariki ridhiki zetu ziingiazo/zitokazo
Mungu wetu nasi tunaomba ukatupe neema ya kuweza
kuwabariki wenye kuhitaji
Tusipungukiwe katika mahitaji yetu Baba wa Mbinguni
tunaomba ukatupe kama inavyokupendeza wewe....



Baba wa Mbinguni tunayaweka maisha yetu mikononi mwako
Mungu wetu tunaomba ukabariki nyumba/ndoa zetu,
watoto,wazazi wetu,familia/ndugu na wote wanaotuzunguka
Jehovah tunaomba ulinzi wako kwetu na kwa vyote tunavyo vimiliki
Yahweh tunaomba ukatubariki tuingiapo/tutokapo
Mungu wetu tunaomba ukavibariki vyote tunavyoenda kugusa/kutumia
Baba wa Mbinguni ukavitakase kwa Damu ya Bwana wetu Yesu Kristo
Mungu wetu ukatamalaki na kutuatamia
Baba wa Mbinguni tukawe salama rohoni
Mfalme wa amani amani yako ikatawale katika maisha yetu
Mungu wetu ukatupe macho ya kuona na masikio ya kusikia 
sauti yako na kuitii

 Mungu wetu ukatupe akili ya kutambua mema na mabaya
Baba wa Mbinguni tunaomba ukatupe neema ya kufuata njia zako
Yahweh tukasimamie Neno lako amri na sheria zako siku zote 
za maisha yetu

Mungu wetu ukaonekane katika maisha yetu

Baba wa Mbinguni tukanene yaliyo yako
Neema zako zikawe nasi Nuru yako ikaangaze katika maisha yetu
ukatuguse kwa mkono wako wenye nguvu
Tukawe barua njema  ee Mungu wetu nasi tukasomeke kama
inavyokupendeza wewe
Roho Mtakatifu akatuongoze katika yote na tukawe na kiasi...


Kisha Yesu aliondoka wilaya ya Tiro, akapitia Sidoni, akafika ziwa Galilaya kwa kupitia nchi ya Dekapoli. Basi, wakamletea bubu kiziwi, wakamwomba amwekee mikono. Yesu akamtenga na umati wa watu, akamtia vidole masikioni, akatema mate na kumgusa ulimi. Kisha akatazama juu mbinguni, akapiga kite, akamwambia, “Efatha,” maana yake “Funguka.” Mara masikio yake yakafunguka na ulimi wake ukafunguliwa, akaanza kusema sawasawa. Yesu akawaamuru wasimwambie mtu juu ya jambo hilo. Lakini kadiri alivyowakataza, ndivyo walivyozidi kutangaza habari hiyo. Watu walishangaa sana, wakasema, “Amefanya yote vyema: Amewajalia viziwi kusikia, na mabubu kusema!”

Mungu Baba tunawaweka mikononi mwako wenye shida/tabuwote wanaopotia magumu/majaribu mbalimbali
watoto wako wanaokuomba kwa bidii na imani
Mungu wetu tunaomba ukawaguse kwa mkono wako wenye nguvu
 kila mmoja na mahitaji yake 
Yahweh tunaomba ukaonekane katika maisha yao
Jehovah tunaomba ukawaokoe,ukawavushe salama na  kuwalinda
Mungu wetu tunaomba ukawasamehe pale walipokwenda kinyume nawe
Baba wa Mbinguni ukawape neema ya kujiombea,kufuata njia zako
wakasimaie Neno lako nalo likaweke huru
Mungu wetu tunaomba ukasikie kuomba kwetu
Baba wa Mbinguni ukapokee sala/maombi yetu
Mungu wetu ukawatendee sawasawa na mapenzi yako
Kwakuwa Ufalme ni wako Nguvu na Utukufu hata Milele
Amina...!!

Asanteni sana wapendwa katika Kristo Yesu kwakuwa nami
Mungu Baba aendelee kuwabariki na kuwatendea 
kama inavyompendeza yeye....
Nawapenda.

Mungu anamjibu Yobu

1Hapo Mwenyezi-Mungu alimjibu Yobu kutoka dhoruba:
2“Nani wewe unayevuruga mashauri yangu
kwa maneno yasiyo na akili?
3Jikaze kama mwanamume,
nami nitakuuliza nawe utanijibu.
4“Ulikuwa wapi nilipoiweka misingi ya dunia?
Niambie, kama una maarifa.
5Ni nani aliyeweka vipimo vyake, wajua bila shaka!
Au nani aliyelaza kamba juu yake kuipima?
6Je, nguzo za dunia zimesimikwa juu ya nini,
au nani aliyeliweka jiwe lake la msingi,
7 Taz Bar 3:34 nyota za asubuhi zilipokuwa zikiimba pamoja,
na wana wa Mungu wakapaza sauti za shangwe?
8 Taz Yer 5:22 Ni nani aliyeyafunga mafuriko ya bahari
wakati yalipozuka na kuvuma kutoka vilindini?
9Mimi ndiye niliyeifunika bahari kwa mawingu
na kuiviringishia giza nene.
10Niliiwekea bahari mipaka,
nikaizuia kwa makomeo na milango,
11nikaiambia: ‘Mwisho wako ni hapa, si zaidi!
Mawimbi yako ya nguvu yatakomea hapa!’
12“Yobu, tangu uzaliwe umewahi kuamuru kupambazuke?
na kulifanya pambazuko lijue mahali pake,
13ili lipate kuikamata dunia kwa pembe zake
na kuwatimulia mbali waovu waliomo?
14Dunia hugeuka na kupata rangi kama vazi;
kama udongo wa mfinyanzi unavyogeuzwa na mhuri.
15Lakini waovu watanyimwa mwanga wao,
mkono wanaonyosha kupiga watu utavunjwa.
16“Je, umepata kufika kwenye chemchemi za bahari?
au kutembea juu ya sakafu ya kilindi cha bahari?
17Je, umewahi kuoneshwa malango ya kifo,
au kuyaona malango ya makazi ya giza nene?
18Je, wajua ukubwa wa dunia?
Niambie kama unajua haya yote.
19“Je, makao ya mwanga yako wapi?
Nyumbani kwa giza ni wapi,
20ili upate kulipeleka kwenye makao yake,
na kuifahamu njia ya kwenda huko kwake.
21Wewe unapaswa kujua,
wewe ambaye umekwisha ishi miaka mingi!
22“Je, umewahi kuingia katika bohari za theluji,
au kuona bohari za mvua ya mawe
23ambavyo nimevihifadhi kwa ajili ya wakati wa fujo,
kwa ajili ya siku ya mapigano na vita?
24Ipi njia ya kwenda mahali mwanga unapogawanywa,
au huko kunakotoka upepo wa mashariki ukasambazwa duniani?
25“Nani aliyechora angani njia kwa ajili ya mvua?
Nani aliyeionesha radi njia yake mawinguni,
26ikasababisha mvua kunyesha nchini kusikoishi mtu
na jangwani ambako hakuna mtu,
27ili kuiburudisha nchi kavu na kame
na kuifanya iote nyasi?
28“Je, mvua ina baba?
Au nani ameyazaa matone ya umande?
29Je, barafu ilitoka tumboni kwa nani?
Nani aliyeizaa theluji?
30Maji hugeuka kuwa magumu kama jiwe,
na uso wa bahari ukaganda.
31 Taz Yobu 9:9; Amo 5:8 “Angalia makundi ya nyota:
Je, unaweza kuifunga minyororo Kilimia,
au kuvilegeza vifungo vya Orioni?
32Je, waweza kuziongoza nyota katika majira yake,
au kumwongoza Dubu pamoja na watoto wake?
33Je, wazijua kanuni zinazotawala mbingu;
Je, waweza kuzipangia taratibu zao duniani?
34“Je, waweza kupaza sauti na kuyaamuru mawingu
yakufunike kwa mtiririko wa mvua?
35Je, wewe ukiamuru umeme umulike,
utakujia na kusema: ‘Nipo hapa?’
36Ni nani aliyemjulisha kwarara kujaa kwa mto Nili
au aliyemwambia jogoo kwamba mvua inakuja?38:36 aya hii si dhahiri. Ilifikiriwa zamani kwamba ndege kwarara na jogoo walikuwa wanaweza kujua majira fulani.
37Nani mwenye akili ya kuweza kuhesabu mawingu,
au kuinamisha viriba vya maji huko mbinguni?
38ili vumbi duniani igandamane
na udongo ushikamane na kuwa matope?
39“Je, waweza kumwindia simba mawindo yake
au kuishibisha hamu ya wana simba;
40wanapojificha mapangoni mwao,
au kulala mafichoni wakiotea?
41Ni nani awapaye kunguru chakula chao,
makinda yao yanaponililia mimi Mungu,
na kurukaruka huku na huko kwa njaa?



Yobu38;1-41

Biblia Habari Njema kwa Watu Wote(BHN)

"Swahili Na Waswahili"Mbarikiwe.