Swahili na Waswahili

Swahili na Waswahili
Waswahili na Mswahili Rachel Siwa...Pamoja Daima!!

Monday 15 October 2018

Kikombe Cha Asubuhi ;Yobu 15...



Shalom,Habari za Asubuhi,Hamjambo,Mmeamkaje?

Haleluyah ni siku/wiki nyingine tena Mungu wetu ametuchagua
na kutupa kibali cha kuendelea kuiona leo hii
Si kwamba sisi tumetenda mema sana wala si kwa nguvu zetu
si kwa utashi wetu wala si kwa akili zetu si kwamba sisi
ni wazuri mno si kwa uwezo wetu sisi kuwa hivi tulivyo leo hii
Ni kwa rehema/neema zake ni kwa mapenzi yake Mungu wetu....

Tumshukuru Mungu wetu katika yote...

Asante Mungu wetu kwa wema na fadhili zako kwetu
Asante kwa ulinzi wako kwetu wakati wote
Asante kwa pumzi/uzima,afya na kuwa tayari kwa majukumu yetu
Sifa na Utukufu tunakurudshia Mungu wetu....!!

Tunapomshukuru Mungu kwa kikombe kile cha baraka, je, huwa hatushiriki damu ya Kristo? Na tunapoumega mkate, je, huwa hatushiriki mwili wa Kristo? Kwa kuwa mkate huo ni mmoja, sisi, ingawa ni wengi, tu mwili mmoja; maana sote twashiriki mkate huohuo. Angalieni kwa mfano Wayahudi wenyewe: Wale wanaokula tambiko wanaungana na hiyo madhabahu. Nataka kusema nini, basi? Kwamba chakula kilichotambikiwa sanamu ni kitu zaidi ya chakula? Na hizo sanamu, je, ni kitu kweli zaidi ya sanamu?



Tazama jana imepita ee Mungu wetu leo ni siku mpya na kesho ni siku nyingine
Jehovah tunakuja mbele zako tukijinyenyekeza,tukijishusha na kujiachilia mikononi mwako
 Mungu wetu tunaomba utusamehe dhambi zetu zote tulizozifanya kwakuwaza,kwakunena,kwakutenda,kwakujua/kutojua
Baba wa Mbinguni nasi tunaomba utupe neema ya kuweza kuwasamehe wale wote waliotukosea
Jehovah usitutie majaribu Mungu wetu tunaomba utuepushe na yule mwovu na kazi zake zote
Yahweh tunaomba ututakase miili yetu na akili zetu
Baba wa Mbinguni utufunike kwa Damu ya Bwana na Mwokozi wetu Yesu Kristo wa Nazareti
yeye aliteseka kwanza ili sisi tupate kupona
Kwakupigwa kwake sisi tumepata kupona...

Hata kidogo! Ninachosema ni kwamba tambiko wanazotoa watu wasiomjua Mungu wanawatolea pepo, sio Mungu. Sipendi kamwe nyinyi muwe na ushirika na pepo. Hamwezi kunywa kikombe cha Bwana na kikombe cha pepo; hamwezi kushiriki katika Karamu ya Bwana na katika meza ya pepo. Au je, tunataka kumfanya Bwana awe na wivu? Mnadhani tuna nguvu zaidi kuliko yeye?

Yahweh tunaomba ukabariki kazi za mikono yetu
Baba wa Mbinguni tunaomba ukatupe ubunifu na maarifa 
katika utendaji
Jehovah nasi tukatende sawasawa na mapenzi yako
Baba wa Mbinguni tunaomba ukabariki ridhiki zetu
ziingiazo/zitokazo
Mungu wetu nasi tunaomba ukatupe neema ya kuweza
kuwabariki wenye kuhitaji
Yahweh tusipungukiwe katika mahitaji yetu
Mungu wetu ukatupe kama inavyokupendeza wewe

Baba wa Mbinguni tunayaweka maisha yetu mikononi mwako
Mungu wetu tunaomba ukabariki nyumba/ndoa zetu,
watoto,wazazi wetu,familia/ndugu na wote wanaotuzunguka
Jehovah tunaomba ulinzi wako kwetu na kwa vyote tunavyo vimiliki
Yahweh tunaomba ukatubariki tuingiapo/tutokapo
Mungu wetu tunaomba ukavibariki vyote tunavyoenda kugusa/kutumia
Baba wa Mbinguni ukavitakase kwa Damu ya Bwana wetu Yesu Kristo
Mungu wetu ukatamalaki na kutuatamia
Baba wa Mbinguni tukawe salama rohoni
Mfalme wa amani amani yako ikatawale katika maisha yetu
Mungu wetu ukatupe macho ya kuona na masikio ya kusikia 
sauti yako na kuitii
Baba wa Mbinguni tunaomba ukatupe neema ya kufuata njia zako
Yahweh tukasimamie Neno lako amri na sheria zako siku zote 
za maisha yetu
Mungu wetu ukaonekane katika maisha yetu
Neema zako zikawe nasi Nuru yako ikaangaze katika maisha yetu
ukatuguse kwa mkono wako wenye nguvu
Ukatufanye chombo chema ee Mungu wetu nasi tukatumike kama
inavyokupendeza wewe
Roho Mtakatifu akatuongoze katika yote na tukawe na kiasi...


Vitu vyote ni halali, lakini si vyote vinafaa. Vitu vyote ni halali lakini si vyote vinajenga. Mtu asitafute faida yake mwenyewe, ila faida ya mwenzake. Kuleni chochote kile kiuzwacho sokoni bila ya kuulizauliza kwa sababu ya dhamiri zenu; maana Maandiko yasema: “Dunia na vyote vilivyomo ni mali ya Bwana.” Kama mtu ambaye si mwaamini akiwaalikeni nanyi mkakubali kwenda, basi, kuleni vyote atakavyowaandalieni bila kuulizauliza kwa sababu ya dhamiri zenu. Lakini mtu akiwaambieni: “Chakula hiki kimetambikiwa sanamu,” basi, kwa ajili ya huyo aliyewaambieni hivyo na kwa ajili ya dhamiri, msile. Nasema, “kwa ajili ya dhamiri,” si dhamiri yenu, bali dhamiri yake huyo aliyewaambieni. Mtaniuliza: “Kwa nini uhuru wangu utegemee dhamiri ya mtu mwingine? Ikiwa mimi nashiriki chakula hicho huku namshukuru Mungu, kwa nini nilaumiwe kwa chakula ambacho kwa ajili yake nimemshukuru Mungu?” Basi, chochote mfanyacho iwe ni kula au kunywa, fanyeni yote kwa ajili ya utukufu wa Mungu. Msiwe kikwazo kwa Wayahudi au kwa Wagiriki au kwa kanisa la Mungu. Muwe kama mimi; najaribu kuwapendeza wote kwa kila njia, bila kutafuta faida yangu mwenyewe ila faida ya wote, wapate kuokolewa.

Mungu wetu tunawaweka mikononi mwako wenye shida/tabu,wote wanaopotia magumu/majaribu mbalimbali
watoto wako wanaokuomba kwa bidii na imani
Mungu wetu tunaomba ukawaguse kwa mkono wako wenye nguvu
 kila mmoja na mahitaji yake 
Yahweh tunaomba ukaonekane katika maisha yao
Jehovah tunaomba ukawaokoe,ukawavushe salama na  kuwalinda
Mungu wetu tunaomba ukawasamehe pale walipokwenda kinyume nawe
Baba wa Mbinguni ukawape neema ya kujiombea,kufuata njia zako
wakasimaie Neno lako nalo likaweke huru
Mungu wetu tunaomba ukasikie kuomba kwetu
Baba wa Mbinguni ukapokee sala/maombi yetu
Mungu wetu ukawatendee sawasawa na mapenzi yako
Kwakuwa Ufalme ni wako Nguvu na Utukufu hata Milele
Amina...!!

Asanteni sana wapendwa katika Kristo Yesu kwakuwa nami
Mungu Baba aendelee kuwabariki na kuwatendea 
kama inavyompendeza yeye....
Nawapenda.



Hoja ya pili ya Elifazi

(15:1–21:34)

1Kisha Elifazi, Mtemani, akajibu:
2“Je, mtu wa hekima hujibu kwa maneno ya upuuzi?
Je, mtu huyo amejaa maneno matupu?
3Je, mwenye hekima hujitetea kwa maneno yasiyofaa,
au kwa maneno yasiyo na maana?
4Lakini wewe unapuuza uchaji wa Mungu;
na kuzuia kutafakari mbele ya Mungu.
5Uovu wako ndio unaokifundisha kinywa chako,
nawe wachagua kusema kama wadanganyifu.
6Maneno yako mwenyewe yanakuhukumu, sio mimi;
matamshi yako yashuhudia dhidi yako.
7Je, wewe ni mtu wa kwanza kuzaliwa?
Je, wewe ulizaliwa kabla ya kuweko vilima?
8Je, ulipata kuweko katika halmashauri ya Mungu?
au, wewe ndiwe peke yako mwenye hekima?
9Unajua kitu gani tusichokijua sisi?
Unafahamu kitu gani tusichokifahamu sisi?
10Miongoni mwetu wapo wazee wenye hekima,
wenye miaka mingi kuliko baba yako.
11Je, faraja anazokupa Mungu ni ndogo mno?
Au je, neno lake la upole kwako si kitu?
12Mbona moyo unakusukuma kukasirika
na kutoa macho makali,
13hata kumwasi Mungu
na kusema maneno mabaya kama hayo?
14 Taz Yobu 25:4-6 Mtu ni nini hata aweze kuwa mwadilifu?
au yule aliyezaliwa na mwanamke hata aweze kuwa mwema?
15Ikiwa Mungu hawaamini hata watakatifu wake,
nazo mbingu si safi mbele yake,
16sembuse binadamu aliye kinyaa na mpotovu
binadamu atendaye uovu kama kunywa maji!
17“Sasa nisikilize, nami nitakuonesha,
nitakuambia yale niliyoyaona,
18mafundisho ya wenye hekima,
mambo ambayo wazee wao hawakuyaficha,
19ambao Mungu aliwapa hiyo nchi peke yao,
wala hakuna mgeni aliyepita miongoni mwao.
20Mwovu atateseka kwa maumivu siku zote,
miaka yote waliyopangiwa wakatili.
21Sauti za vitisho zitampigia kelele masikioni,
anapodhani amestawi mwangamizi atamvamia.
22Mwovu hana tumaini la kutoka gizani;
mwisho wake ni kufa kwa upanga.
23Hutangatanga kutafuta chakula,
akisema, ‘Kiko wapi?’
Ajua kwamba siku ya giza inamkaribia.
24Taabu na uchungu, vyamtisha;
vyamkabili kama jeshi la mfalme anayeshambulia.
25Kwa sababu amenyosha mkono wake dhidi ya Mungu;
akadiriki kumpinga huyo Mungu mwenye nguvu;
26alikimbia kwa kiburi kumshambulia,
huku ana ngao yenye mafundo makubwa.
27Uso wake ameunenepesha kwa mafuta,
na kiuno chake kimejaa mafuta.
28Ameishi katika miji iliyoachwa tupu,
katika nyumba zisizokaliwa na mtu;
nyumba zilizotakiwa ziwe lundo la uharibifu.
29Mtu huyo kamwe hatakuwa tajiri;
wala utajiri wake hautadumu duniani.
30Hatalikwepa giza la kifo.
Ndimi za moto zitakausha chipukizi zake,
maua yake yatapeperushwa na upepo.
31Heri aache kutumainia upuuzi na kujidanganya,
maana upuuzi ndio utakaokuwa tuzo lake.
32Atalipwa kikamilifu kabla ya kufa kwake,
na wazawa wake hawatadumu.
33Atakuwa kama mzabibu unaopukutisha zabibu mbichi,
kama mzeituni unaoangusha maua yake.
34Wote wasiomcha Mungu hawatapata watoto,
moto utateketeza mahema ya wala rushwa.
35Wanatunga udanganyifu na kuzaa uovu.
Mioyo yao hupanga udanganyifu.”



Yobu15;1-35

Biblia Habari Njema kwa Watu Wote(BHN)

"Swahili Na Waswahili"Mbarikiwe.

Friday 12 October 2018

Kikombe Cha Asubuhi ;Yobu 14...


Shalom,Habari za Asubuhi,Hamjambo,Mmeamkaje?

Tumshukuru Mungu wetu katika yote...

Asante kwa wema na fadhili zako kwetu
Asante

 kwa ulinzi wako kwetu wakati wote
Asante kwa kutuchagua tena na kutupa
kibali cha kuendelea kuiona leo hii
Asante kwa pumzi/uzima,afya na kuwatayari kwa majukumu yetu


Utukuzwe ee Mungu wetu,usifiwe Baba wa Mbinguni

Jehovah  Jireh..!Jehovah Nissi..!Jehovah Raah..!
Jehovah Rapha..!Jehovah Shammah..!Jehovah Shamlom..!
Emanuel-Mungu pamohja nasi..!!
Neema yako yatutosha Baba wa Mbinguni..!

Ndugu, nataka mjue kwamba babu zetu wote walikuwa chini ya ulinzi wa lile wingu, na kwamba wote walivuka salama ile bahari. Wote walibatizwa katika umoja na Mose katika lile wingu na katika ile bahari. Wote walikula chakula kilekile cha kiroho, wakanywa pia kinywaji kilekile cha kiroho, maana walikunywa kutoka ule mwamba wa kiroho uliowafuata; mwamba huo ulikuwa Kristo mwenyewe. Hata hivyo, wengi wao hawakumpendeza Mungu, na maiti zao zilisambazwa jangwani.

Baba wa Mbinguni tunakuja mbele zako tukijinyenyekeza,tukijishusha
na kujiachilia mikononi mwako
Mungu wetu tunaomba utusamehe dhambi zetu zote tulizo zifanya
Kwakuwaza,kwakunena,kwakutenda,kwakujua/kutojua
Baba wa Mbinguni nasi tunaomba ukatupe neema
ya kuweza kuwasamehe wale wote waliotukosea
Usitutie majaribu Mungu wetu tunaomba utuepushe
na yule mwovu na kazi zake zote
Jehovah ututakase miili yetu na akili zetu
Baba wa Mbinguni tunaomba utufunike kwa Damu
ya Bwana na Mwokozi wetu Yesu Kristo wa Nazareti
yeye aliteseka kwanza ili sisi tupate kupona...

Sasa, mambo hayo yote ni mfano tu kwetu; yanatuonya sisi tusitamani ubaya kama wao walivyotamani. Msiwe waabudu sanamu kama baadhi yao walivyokuwa; kama yasemavyo Maandiko: “Watu waliketi kula na kunywa, wakasimama kucheza.” Wala tusizini kama baadhi yao walivyozini, wakaangamia siku moja watu 23,000. Tusimjaribu Bwana kama baadhi yao walivyomjaribu, wakauawa na nyoka. Wala msinungunike kama baadhi yao walivyonungunika, wakaangamizwa na Mwangamizi!

Mungu wetu tunaomba ukabariki kazi za mikono yetu
Baba wa Mbinguni tunaomba ukatupe ubunifu na maarifa 
katika utendaji
Jehovah nasi tukatende sawasawa na mapenzi yako
Baba wa Mbinguni tunaomba ukabariki ridhiki zetu
ziingiazo/zitokazo
Mungu wetu nasi tunaomba ukatupe neema ya kuweza
kuwabariki wenye kuhitaji
Yahweh tusipungukiwe katika mahitaji yetu
Mungu wetu ukatupe kama inavyokupendeza wewe



Jehovah tunayaweka maisha yetu mikononi mwako
Baba wa Mbinguni tunaomba ukabariki nyumba/ndoa zetu,
watoto,wazazi wetu,familia/ndugu na wote wanaotuzunguka
Jehovah tunaomba ulinzi wako kwetu na kwa vyote tunavyo vimiliki
Yahweh tunaomba ukatubariki tuingiapo/tutokapo
Mungu wetu tunaomba ukavibariki vyote tunavyoenda kugusa/kutumia
Baba wa Mbinguni ukavitakase kwa Damu ya Bwana wetu Yesu Kristo
Mungu wetu ukatamalaki na kutuatamia
Baba wa Mbinguni tukawe salama rohoni
Mfalme wa amani amani yako ikatawale katika maisha yetu
Mungu wetu ukatupe macho ya kuona na masikio ya kusikia 
sauti yako na kuitii
Baba wa Mbinguni tunaomba ukatupe neema ya kufuata njia zako
Yahweh tukasimamie Neno lako amri na sheria zako siku zote 
za maisha yetu

Mungu wetu tunaomba ukatupe akili ya kutambua mema na mabaya Baba wa Mbinguni ukaonekane katika maisha yetu popote tupitapo na ikajulikane kwamba upo Mungu wetu

Neema zako zikawe nasi Nuru yako ikaangaze katika maisha yetu
ukatuguse kwa mkono wako wenye nguvu
Ukatufanye barua njema ee Mungu wetu nasi tukasomeke kama
inavyokupendeza wewe
Roho Mtakatifu akatuongoze katika yote na tukawe na kiasi...

Basi, mambo hayo yaliyowapata wao ni kielelezo kwa wengine, na yaliandikwa ili kutuonya sisi ambao mwisho wa nyakati unatukabili. Anayedhani amesimama imara ajihadhari asianguke. Majaribu mliyokwisha pata ni ya kawaida kwa binadamu. Mungu ni mwaminifu, naye hataruhusu mjaribiwe kupita nguvu zenu, ila pamoja na majaribu, yeye atawapeni pia nguvu ya kustahimili na njia ya kutoka humo salama. Kwa hiyo, wapenzi wangu, epeni ibada za sanamu. Naongea nanyi, watu wenye busara; jiamulieni wenyewe hayo nisemayo.

Tazama wenye shida/tabu,watoto wako wanaokutafuta kwa bidii na imani
Mungu wetu tunaomba ukawaguse kwa mkono wako wenye nguvu
Yahweh tunaomba  ukawaguse kila mmoja na mahitaji yake
Mungu wetu  unajua haja za mioyo ya kila mmoja
Baba wa Mbinguni tunaomba ukawasamehe pale walipokwenda
kinyume nawe
Mungu wetu ukawape neema ya kujiombea,macho ya rohoni,masikio yakusikia sauti yako,wakafuate njia zako nazo zikawaweke huru
Mungu wetu tunaomba ukasikie kulia kwao
Baba wa Mbinguni tunomba ukawafute machozi yao
Jehovah ukaonekane katika maisha yao
Nuru yako ikaangaze katika maisha yao
Mungu wetu tunaomba ukawatendee sawasawa na mapenzi yako
Kwakuwa Ufalme ni wako Nguvu na Utukufu hata Milele
Amina....!!!


Wapendwa katika Kristo Yesu asanteni sana
kwakuwanami/kunisoma

Mungu Baba aendelee kuwabariki na kuwatendea
kama inavyompendeza yeye
Amani ya Bwana wetu Yesu Kristo na upendo wa Mungu Baba
ukae nanyi daima....
Nawapenda.






1 Taz Hek 2:1; Sira 40:1-11; 41:1-4 “Mtu ni mtoto tu wa mwanamke;
huishi siku chache tena zilizojaa taabu.
2Huchanua kama ua, kisha hunyauka.
Hukimbia kama kivuli na kutoweka.
3Ee Mungu, kwa nini unajali hata kumwangalia
na kuanza kuhojiana naye?
4Nani awezaye kutoa kitu kisafi kutoka kitu kichafu?
Hakuna anayeweza.
5Siku za kuishi binadamu zimepimwa;
ee, Mungu umeipanga idadi ya miezi yake;
hawezi kupita kikomo ulichomwekea.
6Angalia pembeni basi, umwache;
ili apate kufurahia siku zake kama kibarua.
7Maana mti ukikatwa lipo tumaini la kuota,
waweza kuchipua tena.
8Japo mizizi yake itazeeka udongoni,
na shina lake kufia ardhini,
9lakini kwa harufu tu ya maji utachipua;
utatoa matawi kama chipukizi.
10Lakini mtu hufa na huo ndio mwisho wake.
Akisha toa roho anabakiwa na nini tena?
11“Kama vile maji yakaukavyo ziwani,
na mto unavyokoma kutiririka,
12ndivyo anavyokufa mtu, wala haamki tena;
hataamka tena wala kugutuka,
hata hapo mbingu zitakapotoweka.
13“Laiti ungenificha kuzimu;
ungenificha hadi ghadhabu yako ipoe;
nao muda ulionipimia ukiisha ungenikumbuka.
14Je, mtu akifa anaweza kuishi tena?
Siku zangu zote za kazi ningekungoja
hadi wakati wa kufunguliwa ufike.
15Hapo ungeniita, nami ningeitika,
wakati ungetaka kuniona mimi kiumbe chako.
16Ndipo ungeweza kuzihesabu hatua zangu,
ungeacha kuzichunguza dhambi zangu.
17Makosa yangu yangefungiwa katika mfuko,
nawe ungeufunika uovu wangu.
18“Lakini milima huanguka
majabali hungoka mahali pake.
19Mtiririko wa maji hula miamba,
mvua kubwa hufanya mmomonyoko wa ardhi.
Ndivyo nawe unavyoharibu tumaini la binadamu.
20Wewe wamwangusha binadamu, naye akatoweka milele;
waubadilisha uso wake na kumtupilia mbali.
21Watoto wake wakiheshimika, yeye hana habari.
Wakiporomoshwa, yeye haoni kabisa.
22Huhisi tu maumivu ya mwili wake,
na kuomboleza tu hali yake mbaya.”


Yobu14;1-22

Biblia Habari Njema kwa Watu Wote(BHN)

"Swahili Na Waswahili"Mbarikiwe.

Thursday 11 October 2018

Kikombe Cha Asubuhi ;Yobu 13...



Shalom,Habari za Asubuhi,Hamjambo,Mmeamkaje?


Haleluyah Mungu wetu yu mwema sana..
Tumshukuru Mungu wetu katika yote....

Mungu wetu Baba yetu,Muumba wetu Muumba wa Mbingu na Nchi
Baba wa Upendo,Baba wa faraja,Baba wa huruma,Baba wa Baraka
Mungu mwenye nguvu,Mungu mwenye kuponya
Mungu wa Abrahamu,Isaka na Yakobo,Muweza wa yote
Wewe ni mwanzo na wewe ni mwisho,Alfa na Omega...!!


Asante kwa wema na fadhili zako kwetu
Asante kwa ulinzi wako kwetu wakati wote
Asante kwa kutuchagua tena na kutupa
kibali cha kuendelea kuiona leo hii
Asante kwa pumzi/uzima,afya na kuwatayari kwa majukumu yetu

Sifa na Utukufu tunakurudishia wewe ee Mungu wetu....!!




Lakini nyinyi wapenzi wangu, kumbukeni yale mliyoambiwa hapo awali na mitume wa Bwana wetu Yesu Kristo. Waliwaambieni: “Siku za mwisho, watatokea watu watakaowadhihaki nyinyi, watu wafuatao tamaa zao mbaya.” Hao ndio wanaosababisha mafarakano, watu wa fikira za kidunia, wasio na Roho wa Mungu.

Tazama Jana imepita ee Mungu wetu Leo ni siku mpya na kesho ni siku nyingineJehovah...
Yahweh tunakuja mbele zako tukijinyenyekeza,tukijishusha

na kujiachilia mikononi mwako
Mungu wetu tunaomba utusamehe dhambi zetu zote tulizo zifanya
Kwakuwaza,kwakunena,kwakutenda,kwakujua/kutojua
Baba wa Mbinguni nasi tunaomba ukatupe neema
ya kuweza kuwasamehe wale wote waliotukosea
Usitutie majaribu Mungu wetu tunaomba utuepushe
na yule mwovu na kazi zake zote
Jehovah ututakase miili yetu na akili zetu
Baba wa Mbinguni tunaomba utufunike kwa Damu
ya Bwana na Mwokozi wetu Yesu Kristo wa Nazareti 

yeye aliteseka kwanza ili sisi tupate kupona



Lakini nyinyi, wapenzi wangu, jijengeni wenyewe juu ya imani yenu takatifu kabisa. Salini kwa nguvu ya Roho Mtakatifu, na kudumu katika upendo wa Mungu, mkimngojea Bwana wetu Yesu Kristo ambaye, kwa huruma yake, atawajalieni uhai wa milele. Muwe na huruma kwa watu walio na mashaka; waokoeni kwa kuwanyakua kutoka motoni. Lakini kwa wengine muwe na huruma pamoja na tahadhari, mkichukia hata mavazi yao yenye madoa ya tamaa zao mbaya.


Mungu wetu tunaomba ukabariki kazi za mikono yetu
Baba wa Mbinguni tunaomba ukatupe ubunifu na maarifa katika utendaji
Jehovah nasi tukatende sawasawa na mapenzi yako
Yahweh tunaomba ukabariki ridhiki zetu ziingiazo/zitokazo
Mungu wetu nasi tunaomba ukatupe neema ya kuweza
kuwabariki wenye kuhitaji
Tusipungukiwe katika mahitaji yetu Baba wa Mbinguni
tunaomba ukatupe kama inavyokupendeza wewe....



Baba wa Mbinguni tunayaweka maisha yetu mikononi mwako
Mungu wetu tunaomba ukabariki nyumba/ndoa zetu,
watoto,wazazi wetu,familia/ndugu na wote wanaotuzunguka
Jehovah tunaomba ulinzi wako kwetu na kwa vyote tunavyo vimiliki
Yahweh tunaomba ukatubariki tuingiapo/tutokapo
Mungu wetu tunaomba ukavibariki vyote tunavyoenda kugusa/kutumia
Baba wa Mbinguni ukavitakase kwa Damu ya Bwana wetu Yesu Kristo
Mungu wetu ukatamalaki na kutuatamia
Baba wa Mbinguni tukawe salama rohoni
Mfalme wa amani amani yako ikatawale katika maisha yetu
Mungu wetu ukatupe macho ya kuona na masikio ya kusikia 
sauti yako na kuitii

 Mungu wetu ukatupe akili ya kutambua mema na mabaya
Baba wa Mbinguni tunaomba ukatupe neema ya kufuata njia zako
Yahweh tukasimamie Neno lako amri na sheria zako siku zote 
za maisha yetu

Mungu wetu ukaonekane katika maisha yetu

Baba wa Mbinguni tukanene yaliyo yako
Neema zako zikawe nasi Nuru yako ikaangaze katika maisha yetu
ukatuguse kwa mkono wako wenye nguvu
Tukawe barua njema  ee Mungu wetu nasi tukasomeke kama
inavyokupendeza wewe
Roho Mtakatifu akatuongoze katika yote na tukawe na kiasi...




Kwake yeye awezaye kuwalinda msije mkaanguka, na kuwaleta nyinyi bila hatia mpaka mbele ya utukufu wake, kwake yeye aliye peke yake Mungu, Mkombozi wetu, uwe utukufu, ukuu, nguvu na mamlaka kwa njia ya Kristo Bwana wetu, tangu zama zote, sasa na hata milele! Amina.

Mungu Baba tunawaweka mikononi mwako wenye shida/tabuwote wanaopotia magumu/majaribu mbalimbali
watoto wako wanaokuomba kwa bidii na imani
Mungu wetu tunaomba ukawaguse kwa mkono wako wenye nguvu
 kila mmoja na mahitaji yake 
Yahweh tunaomba ukaonekane katika maisha yao
Jehovah tunaomba ukawaokoe,ukawavushe salama na  kuwalinda
Mungu wetu tunaomba ukawasamehe pale walipokwenda kinyume nawe
Baba wa Mbinguni ukawape neema ya kujiombea,kufuata njia zako
wakasimaie Neno lako nalo likaweke huru
Mungu wetu tunaomba ukasikie kuomba kwetu
Baba wa Mbinguni ukapokee sala/maombi yetu
Mungu wetu ukawatendee sawasawa na mapenzi yako
Kwakuwa Ufalme ni wako Nguvu na Utukufu hata Milele
Amina...!!

Asanteni sana wapendwa katika Kristo Yesu kwakuwa nami
Mungu Baba aendelee kuwabariki na kuwatendea 
kama inavyompendeza yeye....
Nawapenda.

Jibu la Yobu laendelea

1“Tazama, hayo yote nimeyaona kwa macho yangu;
nimeyasikia kwa masikio yangu mwenyewe na kuelewa.
2Yote mnayoyajua, mimi pia nayajua.
Mimi si mtu duni kuliko nyinyi.
3Lakini ningependa kusema na Mungu mwenye nguvu,
natamani kujitetea mbele zake Mungu.
4Lakini nyinyi mnaupakaa uongo chokaa;
nyinyi nyote ni waganga wasiofaa kitu.
5Laiti mngekaa kimya kabisa,
ikafikiriwa kwamba mna hekima!
6Sikilizeni basi hoja yangu,
nisikilizeni ninapojitetea.
7Je, mnadhani mwamtumikia Mungu kwa kusema uongo?
Mnafikiri kusema kwa hila kunamfaa yeye?
8Je, mnajaribu kumpendelea Mungu?
Je, mtamtetea Mungu mahakamani?
9Je, akiwakagua nyinyi mtapona?
Au mnadhani mnaweza kumdanganya Mungu kama watu?
10Hakika yeye atawakemea
kama mkionesha upendeleo kwa siri.
11Je, fahari yake haiwatishi?
Je, hampatwi na hofu juu yake?
12Misemo yenu ni methali za majivu,
hoja zenu ni ngome za udongo.
13“Nyamazeni, nami niongee.
Yanipate yatakayonipata.
14Niko tayari hata kuhatarisha
maisha yangu;13:14 kadiri ya tafsiri ya kale ya Kigiriki yaani Septuaginta. Kiebrania aya yaanza na “Kwa nini…?” Na msemo “Kushika nyama yangu katikati ya meno yangu” haupatikani penginepo na maana yake si dhahiri – lakini kutokana na aya hiyo maana yake ni sawa na kuhatarisha maisha.
15Mungu aniue akitaka, sina la kupoteza,
hata hivyo nitautetea mwenendo wangu mbele yake.
16Kama nikifaulu hapo nitakuwa nimeshinda,
maana mtu mwovu hawezi kwenda mbele yake.
17Sikilizeni kwa makini maneno yangu,
maelezo yangu na yatue masikioni mwenu.
18Kesi yangu nimeiandaa vilivyo,
nina hakika mimi sina hatia.
19“Nani atakayeipinga hoja yangu?
Niko tayari kunyamaza na kufa.
20Mungu wangu, nijalie tu haya mawili,
nami sitajificha mbali na wewe:
21Kwanza uniondolee mkono wako unaonipiga,
na usiniangamize kwa kitisho chako.
22“Uanze kutoa hoja yako nami nikujibu.
Au mimi nianze, nawe unijibu.
23Makosa na dhambi zangu ni ngapi?
Nijulishe hatia na dhambi yangu.
24“Mbona unaugeuza uso wako mbali nami?
Kwa nini unanitendea kama adui yako?
25Je, utalitisha jani linalopeperushwa,
au kuyakimbiza makapi?
26Wewe umetoa mashtaka makali dhidi yangu,
na kunibebesha dhambi za ujana wangu.
27 Taz Yobu 33:11 Wanifunga minyororo miguuni,
wazichungulia hatua zangu zote,
na nyayo zangu umeziwekea kikomo.
28Nami naishia kama mti uliooza,
mithili ya vazi lililoliwa na nondo.


Yobu13;1-28

Biblia Habari Njema kwa Watu Wote(BHN)

"Swahili Na Waswahili"Mbarikiwe.

Wednesday 10 October 2018

Kikombe Cha Asubuhi ;Yobu 12...




Shalom,Habari za Asubuhi,Hamjambo,Mmeamkaje?

Haleluyah Mungu wetu yu mwema sana
Tumshukuru Mungu wetu kila wakati
Asante Mungu wetu kwa wema na fadhili zako kwetu
Asante kwa ulinzi wako kwetu wakati wote
Asante kwa kutuchagua tena na kutupa
kibali cha kuendelea kuiona leo hii
Asante kwa pumzi/uzima,afya na kuwatayari kwa majukumu yetu



Utukuzwe ee Mungu wetu,usifiwe Baba wa Mbinguni
Uabudiwe Jehovah,Uhimidiwe Yahweh,Matendo yako ni makuu mno,
Matendo yako ni ya ajabu,Matendo yako yanatisha
Hakuna kama wewe ee Mungu wetu..

Neema yako yatutosha Baba wa Mbinguni...!!




Hivyo ndivyo pia walivyo watu hawa. Ndoto zao huwaongoza katika kuichafua miili yao wenyewe, kuyadharau mamlaka ya Mungu na kuvitukana viumbe vitukufu vya huko juu. Hata Mikaeli, malaika mkuu, hakufanya hivyo. Katika ule ubishi kati yake na Ibilisi juu ya mwili wa Mose, Mikaeli hakuthubutu kumhukumu Ibilisi kwa matusi, ila alisema: “Bwana mwenyewe na akukaripie.” Lakini watu hawa hutukana chochote wasichokielewa; wataangamizwa kwa mambo yaleyale wanayoyajua kwa silika kama wajuavyo wanyama wasio na akili.

Baba wa Mbinguni tunakuja mbele zako tukijinyenyekeza,tukijishusha
na kujiachilia mikononi mwako
Mungu wetu tunaomba utusamehe dhambi zetu zote tulizo zifanya
Kwakuwaza,kwakunena,kwakutenda,kwakujua/kutojua
Baba wa Mbinguni nasi tunaomba ukatupe neema
ya kuweza kuwasamehe wale wote waliotukosea
Usitutie majaribu Mungu wetu tunaomba utuepushe
na yule mwovu na kazi zake zote
Jehovah ututakase miili yetu na akili zetu
Baba wa Mbinguni tunaomba utufunike kwa Damu
ya Bwana na Mwokozi wetu Yesu Kristo wa Nazareti
yeye aliteseka kwanza ili sisi tupate kupona

Kwakupigwa kwake sisi tumepata kupona...



Ole wao! Watu hao wamefuata mwenendo uleule wa Kaini. Kwa ajili ya fedha, wamejiingiza katika mkosi uleule wa Balaamu. Wameasi kama Kora alivyoasi na wameangamizwa kama yeye alivyoangamizwa. Kwa makelele yao yasiyo na adabu, na kwa kujipendelea wao wenyewe, watu hao ni kama madoa machafu kwenye karamu mnazoshiriki kwa upendo. Wako kama mawingu yasiyo na mvua yanayopeperushwa na upepo. Wao ni kama miti iliyopukutika isiyozaa matunda, iliyokufa kabisa, iliyong'olewa. Watu hao ni kama mawimbi makali ya bahari, na matendo yao ya aibu yanatoka kama povu. Wao ni kama nyota zinazotangatanga ambazo zimewekewa milele mahali pa giza kuu.
Mungu wetu tunaomba ukabariki kazi za mikono yetu
Baba wa Mbinguni tunaomba ukatupe ubunifu na maarifa 
katika utendaji
Jehovah nasi tukatende sawasawa na mapenzi yako
Baba wa Mbinguni tunaomba ukabariki ridhiki zetu
ziingiazo/zitokazo
Mungu wetu nasi tunaomba ukatupe neema ya kuweza
kuwabariki wenye kuhitaji
Yahweh tusipungukiwe katika mahitaji yetu
Mungu wetu ukatupe kama inavyokupendeza wewe

Baba wa Mbinguni tunayaweka maisha yetu mikononi mwako
Mungu wetu tunaomba ukabariki nyumba/ndoa zetu,
watoto,wazazi wetu,familia/ndugu na wote wanaotuzunguka
Jehovah tunaomba ulinzi wako kwetu na kwa vyote tunavyo vimiliki
Yahweh tunaomba ukatubariki tuingiapo/tutokapo
Mungu wetu tunaomba ukavibariki vyote tunavyoenda kugusa/kutumia
Baba wa Mbinguni ukavitakase kwa Damu ya Bwana wetu Yesu Kristo
Mungu wetu ukatamalaki na kutuatamia
Baba wa Mbinguni tukawe salama rohoni
Mfalme wa amani amani yako ikatawale katika maisha yetu
Mungu wetu ukatupe macho ya kuona na masikio ya kusikia 
sauti yako na kuitii
 Mungu wetu ukatupe akili ya kutambua mema na mabaya
Baba wa Mbinguni tunaomba ukatupe neema ya kufuata njia zako
Yahweh tukasimamie Neno lako amri na sheria zako siku zote 
za maisha yetu
Mungu wetu ukaonekane katika maisha yetu
Neema zako zikawe nasi Nuru yako ikaangaze katika maisha yetu
ukatuguse kwa mkono wako wenye nguvu
Ukatufanye barua  njema ee Mungu wetu nasi tukasomeke kama
inavyokupendeza wewe

Roho Mtakatifu akatuongoze katika yote na tukawe na kiasi...





Naye Henoki, ambaye ni babu wa saba tangu Adamu, alibashiri hivi juu ya watu hao: “Sikilizeni! Bwana anakuja pamoja na maelfu ya malaika wake watakatifu kuwahukumu watu wote, na kuwaadhibu wote wasiomcha Mungu kwa ajili ya matendo yao yote maovu waliyotenda bila kumjali Mungu, na kwa ajili ya maneno yote mabaya ambayo watu waovu walimkashifu nayo.” Watu hawa hunung'unika daima, hulalamika, hufuata tamaa zao mbaya, hujigamba na kuwasifu watu wengine mno kwa faida yao wenyewe.



Baba wa Mbinguni tunawaweka mikononi mwako wenye shida/tabu
wote wanaopotia magumu/majaribu mbalimbali
watoto wako wanaokuomba kwa bidii na imani
Mungu wetu tunaomba ukawaguse kwa mkono wako wenye nguvu
 kila mmoja na mahitaji yake 
Yahweh tunaomba ukaonekane katika maisha yao
Jehovah tunaomba ukawaokoe,ukawavushe salama na  kuwalinda
Mungu wetu tunaomba ukawasamehe pale walipokwenda kinyume nawe
Baba wa Mbinguni ukawape neema ya kujiombea,kufuata njia zako
wakasimaie Neno lako nalo likaweke huru
Mungu wetu tunaomba ukasikie kuomba kwetu
Baba wa Mbinguni ukapokee sala/maombi yetu
Mungu wetu ukawatendee  kama inavyokupendeza wewe
Kwakuwa Ufalme ni wako Nguvu na Utukufu hata Milele
Amina...!!

Asanteni sana wapendwa katika Kristo Yesu kwakuwa nami
Mungu Baba aendelee kuwabariki na kuwatendea 
sawasawa na mapenzi yake....

Amani ya Bwana wetu Yesu Kristo na Upendo 
wa Mungu Baba ukae nanyi daima....


Nawapenda.

Jibu la Yobu

1Ndipo Yobu akajibu:
2“Sawa! Nyinyi ni watu wa hekima.
Hekima itakufa wakati ule mtakapokufa.
3Mimi nami ni mwelewa kama nyinyi.
Mimi si mtu duni kuliko nyinyi.
Yote mliyosema kila mtu anajua.
4Nimekuwa kichekesho kwa rafiki zangu:
Mimi niliyemwomba Mungu na akanijibu;
mimi niliye mwadilifu na bila lawama,
nimekuwa kichekesho kwa watu.
5Mtu anayestarehe hudharau msiba;
kwake, msiba huwajia wale wanaoteleza.
6Makao ya wanyanganyi yana amani;
wenye kumchokoza Mungu wako salama,
nguvu yao ni mungu wao.
7Lakini waulize wanyama nao watakufunza;
waulize ndege nao watakuambia.
8Au iulize mimea nayo itakufundisha;
sema na samaki nao watakuarifu.
9Nani kati ya viumbe hivyo,
asiyejua kwamba Mwenyezi-Mungu ametenda hayo?
10Uhai wa kila kiumbe hai umo mikononi mwake;
kadhalika na pumzi ya uhai wa binadamu.
11Je, sikio haliyapimi maneno
kama ulimi uonjavyo chakula?
12Hekima iko kwa watu wazee,
maarifa kwao walioishi muda mrefu.
13Lakini hekima na uwezo ni vyake Mungu,
yeye ana maarifa na ujuzi.
14Akibomoa, hakuna awezaye kujenga upya;
akimfunga mtu, hakuna awezaye kumfungua.
15Akizuia mvua, twapata ukame;
akiifungulia, nchi hupata mafuriko.
16Yeye ana nguvu na hekima;
wanaodanganywa na wanaodanganya ni wake.
17Huwaacha washauri waende zao uchi,
huwafanya waamuzi kuwa wapumbavu.
18Huwavua wafalme vilemba vyao;
na kuwafunga viunoni kamba za wafungwa;
19Huwaacha makuhani waende uchi;
na kuwaangusha wenye nguvu.
20Huwanyanganya washauri kipawa chao cha kuongea,
huwapokonya wazee hekima yao.
21Huwamwagia wakuu aibu,
huwaondolea wenye uwezo nguvu zao.
22Huvifunua vilindi vya giza,
na kuleta mwangani yaliyokuwa gizani.
23Huyakuza mataifa kisha huyaangamiza,
huyafanya yapanuke kisha huyatawanya.
24Huwaondolea viongozi wa watu ujuzi wao,
huwafanya watangetange nyikani kusiko na njia,
25wakapapasapapasa gizani kusiko na mwanga;
na kuwafanya wapepesuke kama walevi.


Yobu12;1-25

Biblia Habari Njema kwa Watu Wote(BHN)

"Swahili Na Waswahili"Mbarikiwe.