Swahili na Waswahili

Swahili na Waswahili
Waswahili na Mswahili Rachel Siwa...Pamoja Daima!!

Monday 1 May 2017

Kikombe Cha Asubuhi;Kutoka 23...



Shalom,Habari za Asubuhi,Hamjambo,Mmeamkaje Wapendwa/Waungwana?
Tunamshukuru sana Mungu wetu kwa Neema/Rehema hii ya kutuchagua tena kuendelea kuiona siku/wiki/mwezi huu..si kwa uwezo wetu bali ni kwa mapenzi yake..
Tunaomba Baba wa Mbinguni ukatubariki,Tazama  mwezi/wiki/siku mwingine/nyingine tena Baba tukakuja mbele zako tukishukuru kwa mema yote uliyotutendea na unayoendelea kututendea..Asante kwa pumzi na afya,Asante kwa ridhiki zako ,wema na fadhili zako,Asante kwa yote na tunaanza nawe Baba wa mbinguni kwa kila jambo, maisha yetu yapo mikononi mwako,Tunaomba ukatubariki na kututendea sawasawa na mapenzi yako..Tunaomba utuokoe na mwovu na kazi zake zote..Tunaomba utubariki tuingiapo/tutokapo,vyombo vya usafiri na tutembeapo hatua zetu ziwe nawe Baba, kazi zetu,Biashara,Masomo,vilaji/vinywaji na vyote tunavyoenda kugusa/kutumia ukavitakase kwa Damu ya mwanao mpendwa Bwana na Mwokozi wetu Yesu Kristo yeye aliteseka ili sisi tupate kupona...Baba ukatutakase Akili na Miili yetu pia..
Roho Mtakatifu akatuongoze kwenye kunena/kutenda,kutambua/kujitambua na tukawe na kiasi...
Tunaomba utusamehe pale tulipokwenda kinyume nawe Mfalme wa Amani kwakuwaza,kwakunena,kwakutenda,kwakujua/kutojua..
Tunaomba na sisi utupe Neema ya kuweza kuwasamehe waliotukosea na tuwe na kiasi ili tusikwazane tena..
Tunawaweka mikononi mwako wote wanaopitia magumu/majaribu..Baba tazama wenye Shida/Tabu, wagonjwa,Wafiwa ukawe mfariji wao,waliokatika vifungo mbalimbali, waliokataliwa,waliokata tamaa,wenye mashaka/hofu,waliomizwa moyoni,Baba wa mbinguni ukawaguse na kuwaponya..
Tazama Yatima na wajane,wanaotafuta watoto Mfalme wa Amani,wanaotafuta wenza mke/mume ukawapatie walio wao na kuwabariki katika mahitaji yao..
Baba tunaomba ukabariki Ridhiki zetu ziingiazo na zitokazo ukazifanye baraka na kuweza kusaidia wengine..
Yesu Anakataliwa na Wayahudi...!!
Huko Yerusalemu kulikuwa na sikukuu ya kutabaruku. Wakati huo ulikuwa wa baridi. Naye Yesu akawa anatembea hekaluni katika ukumbi wa Solomoni. Basi, Wayahudi wakamzunguka, wakamwuliza, “Utatuacha katika mashaka mpaka lini? Kama wewe ndiwe Kristo, basi, tuambie wazi.” Yesu akawajibu, “Nimewaambieni, lakini hamsadiki. Kazi ninazozifanya mimi kwa jina la Baba yangu zinanishuhudia. Lakini nyinyi hamsadiki kwa sababu nyinyi si kondoo wangu. Kondoo wangu huisikia sauti yangu; mimi nawajua, nao hunifuata. Mimi nawapa uhai wa milele; nao hawatapotea milele, wala hakuna mtu atakayeweza kuwatoa mkononi mwangu. Baba yangu ambaye ndiye aliyenipa hao ni mkuu kuliko wote, wala hakuna awezaye kuwatoa mikononi mwake Baba. Mimi na Baba, tu mmoja.” Basi, Wayahudi wakachukua mawe ili wamtupie. Yesu akawaambia, “Nimewaonesheni kazi nyingi kutoka kwa Baba. Ni ipi kati ya hizo inayowafanya mnipige mawe?” Wayahudi wakamjibu, “Hatukupigi mawe kwa ajili ya kazi njema, ila kwa sababu ya kumkufuru Mungu! Maana wajifanya kuwa Mungu hali wewe ni binadamu tu.” Yesu akawajibu, “Je, haikuandikwa katika sheria yenu: ‘Mimi nimesema, nyinyi ni miungu?’ Mungu aliwaita miungu wale waliopewa ujumbe wake; nasi twajua kwamba Maandiko Matakatifu yasema ukweli daima. Je, yeye ambaye Baba alimweka wakfu na kumtuma ulimwenguni, mnamwambia: ‘Unakufuru,’ eti kwa sababu nilisema: ‘Mimi ni Mwana wa Mungu?’ Kama sifanyi kazi za Baba yangu, msiniamini. Lakini ikiwa ninazifanya, hata kama hamniamini, walau ziaminini hizo kazi, mpate kujua na kutambua kwamba Baba yuko ndani yangu, nami niko ndani yake.” Wakajaribu tena kumkamata lakini akachopoka mikononi mwao. Yesu akaenda tena ngambo ya mto Yordani, mahali Yohane alipokuwa akibatiza, akakaa huko. Watu wengi walimwendea wakasema, “Yohane hakufanya ishara yoyote. Lakini yale yote Yohane aliyosema juu ya mtu huyu ni kweli kabisa.” Watu wengi mahali hapo wakamwamini.
Mwamini Mungu ndugu yangu..katika shida zako mwite yeye,katika Raha,Furaha mshukuru yeye...Yeye asiye lala wala kusinzia hatokuacha daima, binadamu hubadirika lakini Mungu yeye habadiriki kamwe ukimtumainia yeye na kufuata njia zake kamwe hutojuta....
Sifa na utukufu ni wako Mungu wetu, tunayaweka yote mikononi mwako,tukishukuru na kuamini wewe ni Mungu wetu..
Amina..!!
Asanteni sana kwa wote mliopita hapa Mungu Baba muweza wa yote aendelee kuonekana katika mahitaji yenu na aendelee kuwabariki..
Nawapenda.

Haki na usawa

1“Usitoe habari za uongo. Usishirikiane na mtu mwovu ili kuwa shahidi mbaya. 2Usifuate genge la watu kutenda uovu, wala usijumuike na genge la watu kutoa ushahidi mahakamani ili kupotosha haki. 3Taz Lawi 19:15 Usiwe na upendeleo katika kesi ya maskini.
4“Ukimkuta ng'ombe au punda wa adui yako amepotea, utamrudishia mwenyewe. 5Ukimwona punda wa mtu anayekuchukia ameanguka na mzigo wake, msaidie mtu huyo kumsimamisha punda wake, wala usimwache na kwenda zako.
6“Usiipotoshe haki anayostahili maskini katika kesi yake. 7Jitenge mbali na mashtaka ya uongo wala usiwaue wasio na hatia na waadilifu, maana mimi sitamsamehe mtu mwovu. 8Usipokee rushwa, maana rushwa huwapofusha wakuu na kupotosha mambo ya wenye haki.
9“Usimdhulumu mgeni; nyinyi mwajua hali ya kuwa mgeni, maana mlikuwa wageni nchini Misri.

Mwaka wa saba

10“Kwa muda wa miaka sita utapanda mashamba yako na kuvuna mazao yake. 11Lakini mnamo mwaka wa saba, utayaacha mashamba yako bila kupanda mbegu, ili maskini miongoni mwa watu wako wapate chakula kilichosalia humo, na wanyama wa porini wale. Utafanya vivyo hivyo katika shamba lako la mizabibu na la mizeituni.
12“Kwa siku sita utafanya kazi zako, lakini siku ya saba utapumzika, ili ng'ombe wako na punda wako pia wapate kupumzika; na watumwa wako na watumishi wa kigeni wapate kustarehe. 13Yazingatie yote niliyokuambia. Usiyataje hata kidogo majina ya miungu mingine; hayo yasisikike kinywani mwako.
Sikukuu tatu kubwa

(Kut 34:18-26; Kumb 16:1-17)

14“Mara tatu kila mwaka mtafanya sikukuu kwa heshima yangu. 15Taz Kut 12:14-20; Lawi 23:6-8; Hes 28:17-25 Mtaadhimisha sikukuu ya mikate isiyotiwa chachu: Kama nilivyowaagiza, mtakula mikate isiyotiwa chachu kwa siku saba wakati uliopangwa katika mwezi wa Abibu, kwa sababu katika mwezi huo mlitoka Misri. Mtu yeyote asije mbele yangu mikono mitupu. 16Taz Lawi 23:15-21, 39-43; Hes 28:26-31 Mtaadhimisha sikukuu ya mavuno ya kwanza ya kazi zenu na ya mavuno ya mashamba yenu. Mtaadhimisha sikukuu ya kukusanya mavuno23:16 sikukuu ya kukusanya mavuno: Au sikukuu ya vibanda. mwishoni mwa mwaka mnapokusanya mazao ya kazi zenu. 17Mara tatu kwa mwaka wanaume wote watakusanyika mbele zangu mimi Bwana Mwenyezi-Mungu.
18“Usinitolee damu ya tambiko yangu pamoja na mkate uliotiwa chachu, wala usiyaache mafuta ya sikukuu yangu yabaki mpaka asubuhi.
19 Taz Kut 34:26; Kumb 14:21; 26:2 “Mazao ya kwanza ya ardhi yako utayaleta nyumbani kwangu mimi Mwenyezi-Mungu, Mungu wako.
“Usimchemshe mwanakondoo au mwanambuzi katika maziwa ya mama yake.23:19 desturi hiyo ilifanyika katika mila za kidini za Wakanaani.

Ahadi na maagizo

20“Tazameni, mimi namtuma malaika awatangulie safarini ili awalinde na kuwafikisha katika nchi niliyowatayarishia. 21Msikilizeni na kutii atakachosema, wala msimwasi, kwani hatawasamehe uasi wenu maana nimemtuma kwa jina langu. 22Lakini mkimsikiliza kwa makini na kufanya yote asemayo, mimi nitakuwa adui wa adui zenu na mpinzani wa wapinzani wenu. 23Malaika wangu atakapowaongoza na kuwafikisha katika nchi ya Waamori, Wahiti, Waperizi, Wakanaani, Wahivi na Wayebusi, nami nikawaangamiza hao wote, 24msiiname mbele ya miungu yao kuiabudu, wala kuitumikia, wala msiige mambo yao. Bali mtawaangamiza kabisa na kuzivunjavunja nguzo zao. 25Mtanitumikia mimi Mwenyezi-Mungu, Mungu wenu, nami nitawabariki kwa chakula na maji na kuyaondoa magonjwa kati yenu. 26Hakutakuwa na mwanamke yeyote atakayepoteza mimba wala kuwa tasa katika nchi yenu. Nami nitawajalia maisha marefu.
27“Nitapeleka kitisho mbele yenu na kuwavuruga watu wote mtakaowakabili, na adui zenu nitawafanya wageuke na kuwakimbia. 28Nitapeleka manyigu mbele yenu ambao watawafukuza Wahivi, Wakanaani na Wahiti. 29Sitawaondoa watu hao katika mwaka mmoja, nchi isije ikabaki tupu na wanyama wa porini wakaongezeka mno na kuwazidi nguvu. 30Lakini nitawaondoa kidogokidogo mpaka hapo mtakapoongezeka na kuimiliki nchi hiyo. 31Mipaka ya nchi yenu itakuwa kutoka bahari ya Shamu hadi bahari ya Mediteranea, na kutoka jangwani mpaka mto Eufrate, maana nitawatia wakazi wa nchi hiyo mikononi mwenu, nanyi mtawafukuza wawaondoke. 32Msifanye agano lolote nao, wala na miungu yao. 33Msiwaruhusu waishi nchini mwenu wasije wakawafanya mtende dhambi dhidi yangu; maana kama mkiitumikia miungu yao, hakika hiyo itakuwa mtego wa kuwanasa.”

Kutoka23;1-33

Biblia Habari Njema kwa Watu Wote(BHN)

"Swahili Na Waswahili"Mbarikiwe.

Friday 28 April 2017

Kikombe Cha Asubuhi;Kutoka 22...

Shalom,Habari za Asubuhi,Hamjambo,Mmeamkaje Wapendwa/Waungwana?
Tushuke mbele za Mungu tukishukuru na kusifu..
Mtakatifu..!!Mtakatifu..!!Mtakatifu..!! Baba wa Mbinguni,Mungu wetu na Muumba wetu, Muumba wa  Mbingu na Nchi na vyote vilivyomo ni mali yako, hata sisi Baba ni Mali yako, Hatuna Mungu mwingine zaidi yako, Hakuna wa kuabudiwa kama wewe, Hakuna Mlinzi na Muamuzi katika maisha yetu zaidi yako..Mungu wa Abrahamu,Isaka na Yakobo..
Tunakushukuru na kukusifu daima, Asante kwa ulinzi wako Usiku mzima..
Asante kwa Fadhili na wema wako Baba,Asante kwa Kibali chako na  Kutuchagua tena  kuendela kuiona siku hii..si kwanguvu zetu au ujuzi wetu Baba ni kwa Neema/Rehema zako Mfalme wa Amani..

Tazama Jana imepita Baba Leo ni siku mpya na Kesho ni siku nyingine Jehovah..!!
Tunajiachilia mikononi mwako tukijinyenyekeza na kuomba Utamalaki na kutuatamia Yaweh... katika Nyumba zetu,watoto wetu,familia zetu na maisha yetu yapo mikononi mwako Jehovah..!


Yesu Mchungaji Mwema..!!
Basi, akasema tena, “Kweli nawaambieni, mimi ni mlango wa kondoo. Wale wengine wote waliokuja kabla yangu ni wezi na wanyanganyi, nao kondoo hawakuwasikiliza. Mimi ni mlango. Anayeingia kwa kupitia kwangu ataokolewa; ataingia na kutoka, na kupata malisho. Mwizi huja kwa shabaha ya kuiba, kuua na kuharibu. Mimi nimekuja mpate kuwa na uhai – uhai kamili. “Mimi ni mchungaji mwema. Mchungaji mwema huutoa uhai wake kwa ajili ya kondoo wake. Mtu wa kuajiriwa ambaye si mchungaji, na wala kondoo si mali yake, anapoona mbwamwitu anakuja, huwaacha kondoo na kukimbia, kisha mbwamwitu huwakamata na kuwatawanya. Yeye hajali kitu juu ya kondoo kwa sababu yeye ni mtu wa mshahara tu. Mimi ni mchungaji mwema. Nawajua walio wangu, nao walio wangu wananijua mimi, kama vile Baba anijuavyo, nami nimjuavyo Baba. Mimi nayatoa maisha yangu kwa ajili yao. Tena ninao kondoo wengine ambao hawamo zizini humu. Inanibidi kuwaleta hao pia, nao wataisikia sauti yangu, na kutakuwako kundi moja na mchungaji mmoja. “Baba ananipenda kwani nautoa uhai wangu ili nipate kuupokea tena. Hakuna mtu anayeninyanganya uhai wangu; mimi nautoa kwa hiari yangu mwenyewe. Ninao uwezo wa kuutoa na uwezo wa kuuchukua tena. Hivi ndivyo Baba alivyoniamuru nifanye.” Kukawa tena na mafarakano kati ya Wayahudi kwa sababu ya maneno haya. Wengi wao wakasema, “Ana pepo; tena ni mwendawazimu! Ya nini kumsikiliza?” Wengine wakasema, “Haya si maneno ya mwenye pepo. Je, pepo anaweza kuyafumbua macho ya vipofu?”


Karibu kwenye mioyo yetu  utawale na kutuongoza katika yote,utupe macho ya rohoni Mfalme wa Amani tupate kutambua na kujitambua..Tukawe chombo chema na tukatumike sawasawa na mapenzi yako, tusiwe watu wa kujisifu wala kujitapa,tukawatendee wengine wema na tuwapende kama unavyotupenda sisi,tukawe na kiasi na utuokoe na kisasi Baba wa Mbinguni..
Tunaomba utusamehe pale tulipokwenda kinyume nawe Mfalme wa Amani kwakuwaza,kwakunena,kwakutenda,kwakujua au kutojua..
Tunaomba utupe  na sisi Neema ya kuweza kuwasamehe waliotukosea..
Baba tunaomba ukawaguse na kuwaponya wote wanaopitia majaribu/magumu,wenye shida/tabu, wagonjwa, wafiwa ukawe mfariji wao..ukawafungue walio kwenye vifungo mbali mbali Baba..wapate kupona kimwili na kiroho pia..
Yahweh..!! tunaomba ubariki kazi zetu, Biashara,Masomo,Vilaji/vinywaji,vyombo vya usafiri, tutembeapo hatua zetu ziwe nawe.. ututakase Miili yetu na Akili zetu na vyote tunavyoenda kugusa kutumia ukavitakase kwa Damu ya mwanao mpendwa Bwana na Mwokozi wetu Yesu Kristo wa Nazareti..yeye aliteseka ili sisi tupate kupona.
Tunayaweka haya mikononi mwako tukiamini na kukusifu daima..Tunashukuru na kukuabudu tukiamini wewe ni Mungu wetu Leo kesho na hata Milele..
Amina..!
Mungu awabariki sana na Asanteni sana kwa kupitia hapa
Nawapenda.



Maagizo juu ya malipo

1“Mtu akiiba ng'ombe au kondoo na kumchinja au kumwuza, atatozwa ng'ombe watano kwa kila ng'ombe, na kondoo wanne kwa kila kondoo. 2Mwizi akipatikana anavunja nyumba, akapigwa hata akafa, aliyemuua hana hatia ya mauaji. 3Lakini mwizi huyo akishikwa wakati jua limechomoza na kuuawa, aliyemuua atakuwa na hatia. Huyo mwizi anapaswa kulipa. Ikiwa hana kitu cha kulipa, basi, yeye mwenyewe atauzwa ili kulipia wizi wake. 4Kama mnyama aliyeibiwa atapatikana kwa huyo mwizi akiwa hai, basi, mwizi atalipa mara mbili, awe ni ng'ombe, punda au kondoo.
5“Mtu akiwalisha wanyama wake katika shamba la mizabibu au kumwachia mnyama wake kula katika shamba la mtu mwingine, atalipa hasara hiyo kwa mazao bora ya shamba lake mwenyewe au shamba lake la mizabibu.
6“Mtu akiwasha moto nao ukachoma miti ya miiba na kusambaa hadi kuteketeza miganda ya nafaka, au nafaka ya mtu mwingine ambayo bado haijavunwa, au shamba lote likateketea, aliyewasha moto huo lazima alipe hasara hiyo yote.
7“Mtu akimwachia mwenzake fedha au mali nyingine amtunzie, kisha ikaibiwa nyumbani mwake, mwizi akipatikana lazima alipe thamani yake mara mbili. 8Lakini mwizi asipopatikana, mwenye nyumba atakaribia mbele za Mungu ili kuthibitisha kwamba hakuhusika na wizi wa mali ya mwenzake.
9“Pakiwa na ubishi juu ya ng'ombe, au punda, au kondoo, au mavazi, au kitu chochote kilichopotea ambacho kila mmoja anadai ni chake, wanaohusika wataletwa mbele za Mungu. Yule ambaye Mungu ataamua amekosa, atamlipa mwenzake mara mbili.
10“Mtu akimkabidhi mwenzake punda, ng'ombe, kondoo au mnyama mwingine yeyote amtunzie, na mnyama huyo akafa au akaumia au akachukuliwa bila mtu yeyote kushuhudia, 11kiapo mbele ya Mwenyezi-Mungu kitaamua kati yao, kuonesha kwamba huyo aliyekabidhiwa hakuhusika na wizi wa mali ya mwenzake. Mwenye mnyama huyo atakubali hicho kiapo, na huyo mwenzake hatalipa malipo yoyote. 12Lakini kama aliibiwa kwake, ni lazima amlipe mwenyewe. 13Kama huyo mnyama aliraruliwa na wanyama wa porini, huyo mtu aliyekuwa amekabidhiwa lazima amlete kama ushahidi. Hatalipa malipo yoyote kwa ajili ya mnyama aliyeraruliwa na wanyama wa porini.
14“Mtu akiazima mnyama kwa mwenzake, kisha mnyama huyo akaumia au akafa wakati mwenyewe hayuko, aliyeazima mnyama huyo ni lazima alipe kikamilifu. 15Lakini kama mwenyewe alikuwako, basi aliyemwazima hatalipa chochote. Kama alikuwa ni mnyama aliyekodishwa, mwenyewe ataikubali tu bei ya kukodisha.

Sheria za maadili

16 Taz Kumb 22:28-29 “Mtu akimshawishi bikira ambaye hajaposwa, akalala naye, lazima atoe mahari na kumwoa msichana huyo. 17Baba wa huyo msichana akikataa katakata kumwoza binti yake, mtu huyo atalipa fedha ya mahari inayostahili msichana aliye bikira.
18“Usimwache mwanamke mchawi aishi.
19“Anayezini na mnyama lazima auawe.
20“Anayemtolea tambiko mungu mwingine badala ya Mwenyezi-Mungu pekee, lazima aangamizwe kabisa.
21“Msimdhulumu mgeni wala kumtesa, maana nanyi pia mlikuwa wageni nchini Misri. 22Msimtese mjane au yatima. 23Kama mkiwadhulumu hao nao wakanililia, hakika nitakisikiliza kilio chao, 24na hasira yangu itawaka, nami nitawaueni kwa upanga, na wake zenu watakuwa wajane na watoto wenu yatima.
25“Ukimkopesha fedha mtu yeyote miongoni mwa watu wangu walio maskini, usiwe kwake kama mdai, wala usimtoze riba. 26Ukilichukua vazi la mwenzako kuliweka rehani, lazima umrudishie kabla ya jua kutua, 27kwa kuwa hiyo ndiyo nguo yake ya pekee; ndiyo atakayojifunika nayo. Au wadhani atalalia nini? Akinililia nitamsikiliza, maana mimi ni mwenye huruma.
28“Usimtukane Mungu, wala kumlaani mkuu wa watu wako.
29“Usikawie kunitolea sehemu yangu kutokana na wingi wa mazao yako na divai yako. Mtanipa wazaliwa wenu wa kwanza wa kiume. 30Mtafanya vivyo hivyo kuhusu wazaliwa wa kwanza wa ng'ombe na kondoo wenu. Mtamwacha kila mzaliwa wa kwanza na mama yake kwa siku saba, na siku ya nane mtanitolea. 31Nyinyi mtakuwa watu waliowekwa wakfu kwangu. Kwa hiyo hamtakula nyama ya mnyama aliyeuawa na mnyama wa porini. Nyama hiyo mtawatupia mbwa.

Kutoka22;1-31

Biblia Habari Njema kwa Watu Wote(BHN)

"Swahili Na Waswahili"Mbarikiwe.

Thursday 27 April 2017

Kikombe Cha Asubuhi;Kutoka 21...


Shalom,Habari za Asubuhi,Hamjambo,Mmeamkaje Wapendwa/Waungwana?
Mungu wetu atosha yeye aliyetuchagua na kupatia kibali cha kuendelea kuiona leo hii.. Tunamrudishia Sifa na utukufu..
Sisi ni nani Baba wa Mbinguni, si kwamba ni wema sana hapana..Si kwamba wazuri mno hapana..si kwamba wajuaji na wenye nguvu sana ..hapana..ni kwa Neema/Rehema zako Mungu wetu umetuamsha tena na tukiwa na uwezo wa kuandika/kusoma Neno lako,Kutubu na kukutafuta wewe zaidi ya tunavyojua..

Tazama walio vitandani wakiwa wagonjwa, wengine wamekata kauli wanatamani hata kukuita Mungu kwa sauti zao lakina  wanashindwa kutubu,wengine wameshatangulia, si kwamba nao ni wabaya sana na si kwamba si wema sana..hapana,Baba wa mbinguni tunaomba ukawaguse kwa mkono wako wenye nguvu na ukawaponye na kuwaokoe..kwakuwa uponyaji una wewe Jehovah..!!

Tunaomba Baba ukatupe macho ya Rohoni na tupate kuuona wema na fadhili zako daima, Tukawe chombo chema na tukatumike sawasawa na mapenzi yako,
tunakwenda kinyume  na yule mwovu na kazi zake..
Tunakuja mbele zako Mungu wetu tujinyenyekeza na kuomba na utusamehe pale tulipokwenda kinyume nawe Yahweh..!
Nasi utupe Neema ya kuweza kuwasamehe waliotukosea..

Mchungaji Mwema..!!
“Kweli nawaambieni, yeyote yule asiyeingia katika zizi la kondoo kwa kupitia mlangoni, bali hupenya na kuingia kwa njia nyingine, huyo ni mwizi na mnyanganyi. Lakini anayeingia kwa kupitia mlangoni, huyo ndiye mchungaji wa kondoo. Mngojamlango wa zizi humfungulia, na kondoo husikia sauti yake; naye huwaita kondoo wake kila mmoja kwa jina lake, na kuwaongoza nje. Akisha watoa nje huwatangulia mbele, nao kondoo humfuata, kwani wanaijua sauti yake. Kondoo hao hawawezi kumfuata mgeni, bali watamkimbia kwa sababu hawaijui sauti yake.” Yesu aliwaambia mfano huo, lakini wao hawakuelewa alichotaka kuwaambia.

Tunaomba utubariki katika kazi zetu,Biashara,Masomo,Vyombo vya usafiri,Tuingiapo tutokapo,hatua zetu ziwe nawe Baba,Vilaji/vinywaji na vyote tunavyoenda kugusa/kutumia Mfalme wa Amani ukavitakase kwa Damu ya mwanao mpendwa Bwana na Mwokozi wetu Yesu Kristo wa Nazareti..
Ukatutakase Miili yetu na Akili zetu..
Roho Mtakatifu akatuongoze kwenye kunena/kutenda, kutambua na kujitambua..
Ukawaguse na kuwaponya wote wanaopitia magumu/majaribu mbalimbali na walio katika vifungo mbalimbali Baba ukawafungue na kuwaponya kimwili na kiroho pia..
Tunayaweka haya yote mikononi mwako tukiamini wewe ni Mungu wetu mwenye haki na Tunakushukuru na kukusifu Daima..
Amina..!!
Asanteni sana wote mnaopita hapa..Mungu aendelee kuwagusa na kuwabariki katika mahitaji yenu..
Nawapenda.


Maagizo kuhusu watumwa

(Kumb 15:12-18)

1“Haya ndiyo maagizo utakayowapa Waisraeli: 2Ukimnunua mtumwa Mwebrania, atakutumikia kwa miaka sita, lakini mwaka wa saba atakuwa huru na kuondoka, bila malipo. 3Kama alinunuliwa kabla hajaoa, ataondoka peke yake. Lakini kama alikuja na mkewe, basi, ataondoka na mkewe. 4Kama bwana wake alimwoza mke, akamzalia watoto wa kike au wa kiume, basi, huyo mwanamke na watoto wake watakuwa mali ya huyo bwana wake, na huyo mtumwa ataondoka peke yake. 5Lakini kama mtumwa huyo akisema kwamba anampenda bwana wake, mke wake na watoto wake na hataki kuondoka na kuwa huru, 6basi, bwana wake atamleta mbele ya Mungu. Kisha atampeleka kwenye mlango au kizingitini na kumtoboa sikio lake kwa shazia; naye atamtumikia bwana wake maisha yake yote.
7“Mtu akimwuza binti yake kuwa mtumwa, huyo hatapata uhuru wake kama watumwa wa kiume. 8Ikiwa huyo bwana wake alimnunua awe mmoja wa wake zake, kisha asipendezwe naye, huyo bwana atamwacha baba yake huyo mtumwa amkomboe. Huyo bwana hana haki ya kumwuza kwa watu wa mataifa mengine, kwa kuwa atakuwa amekosa uaminifu. 9Kama ataamua kumwoza kwa mwanawe, atamtendea mtumwa huyo kama binti yake. 10Kama huyo bwana akioa mke mwingine, lazima aendelee kumtosheleza mkewe wa kwanza kwa chakula, mavazi na haki zake za ndoa. 11Iwapo huyo bwana hatamtimizia haki hizo tatu, basi, mke ataondoka na kuwa huru bila malipo yoyote.

Maagizo kuhusu ukatili

12 Taz Lawi 24:17 “Ampigaye mtu na kumwua, lazima auawe. 13Lakini kama hakuwa amemvizia, bali ni kwa ajali, basi, huyo mwuaji ataweza kukimbilia usalama mahali nitakapowachagulieni. 14Lakini mtu akimshambulia mwenzake makusudi na kumwua kwa ujeuri, hata kama atakimbilia kwenye madhabahu, mtamtoa huko madhabahuni pangu na kumwua.
15“Ampigaye baba yake au mama yake lazima auawe.
16“Amtekaye mtu nyara ili kumwuza au kumfanya mtumwa wake lazima auawe.
17 Taz Lawi 20:9; Mat 15:4; Marko 7:10 “Amlaaniye baba yake au mama yake lazima auawe.
18“Watu wawili wakigombana, kisha mmoja akampiga mwenzake jiwe au ngumi bila kumwua, lakini akamjeruhi kiasi cha kumfanya augue na kulala kitandani, 19iwapo huyo aliyepigwa atapata nafuu na kuweza kutembea kwa kutegemea fimbo, huyo aliyemjeruhi atasamehewa. Lakini, atamlipa fidia ya muda alioupoteza kitandani, na kuhakikisha amemwuguza mpaka apone kabisa.
20“Mtu akimpiga mtumwa wake wa kiume au wa kike kwa fimbo na kumwua papo hapo, ni lazima aadhibiwe. 21Lakini mtumwa huyo akibaki hai siku moja au mbili, bwana wake hataadhibiwa, kwani huyo alikuwa ni mali yake.
22“Wanaume wakipigana na kumwumiza mwanamke mjamzito, hata mimba yake ikaharibika bila madhara mengine zaidi, yule aliyemwumiza atatozwa faini kama atakavyodai mumewe mwanamke huyo na kama mahakimu watakavyoamua. 23Lakini kama yatakuwapo madhara mengine, basi, lazima amlipe uhai kwa uhai, 24Taz Lawi 24:19-20; Kumb 19:21; Mat 5:38 jicho kwa jicho, jino kwa jino, mkono kwa mkono, mguu kwa mguu, 25kuchomwa moto kwa kuchomwa moto, jeraha kwa jeraha, na pigo kwa pigo.
26 Taz Lawi 25:39-46 “Mtu akimpiga jicho mtumwa wake wa kiume au wa kike na kuliharibu jicho lake, ni lazima amwachilie aende huru bila malipo kwa ajili ya jicho lake. 27Hali kadhalika, akimpiga hata kumngoa jino mtumwa wake wa kiume au wa kike, ni lazima amwachilie huru kwa ajili ya jino lake.

Maagizo kuhusu usalama wa wengine

28“Ngombe akimpiga mtu pembe na kumwua, ng'ombe huyo atauawa kwa kupigwa mawe na nyama yake haitaliwa. Mwenye ng'ombe huyo hatakuwa na lawama. 29Lakini kama ng'ombe huyo amezoea kupiga watu pembe, na mwenyewe akaonywa lakini hakumfunga, kama ng'ombe huyo akiua mtu lazima apigwe mawe, na mwenyewe lazima auawe. 30Hata hivyo, huyo mtu akitozwa faini ili kuyaokoa maisha yake, ni lazima alipe kiasi kamili atakachotozwa. 31Ngombe akimpiga pembe mtoto wa mtu mwingine, shauri hili litaamuliwa kwa njia hiyohiyo. 32Kama ng'ombe huyo akimpiga pembe mtumwa wa kiume au wa kike, mwenye ng'ombe atamlipa bwana wa huyo mtumwa fedha zenye thamani ya shekeli thelathini, na huyo ng'ombe lazima auawe kwa kupigwa mawe.
33“Mtu akiacha shimo wazi, ama akichimba shimo kisha asilifunike, halafu ng'ombe au punda akatumbukia humo, 34huyo mwenye shimo hilo lazima atoe fidia; atamlipa mwenye mnyama huyo fedha, na mnyama aliyekufa atakuwa wake.
35“Ngombe wa mtu akimwumiza ng'ombe wa mtu mwingine na kumwua, basi, watu watamwuza huyo ng'ombe aliyebaki hai na kugawana bei yake; vilevile watagawana yule ng'ombe aliyekufa. 36Lakini kama huyo ng'ombe alikuwa amezoea kupiga wengine pembe na mwenyewe hakumfunga, mwenyewe atalipa ng'ombe kwa ng'ombe, na yule aliyeuawa atakuwa wake.


Kutoka21;1-36

Biblia Habari Njema kwa Watu Wote(BHN)

"Swahili Na Waswahili"Mbarikiwe.

Wednesday 26 April 2017

Kikombe Cha Asubuhi;Kutoka 20...




Shalom,Habari za Asubuhi,Hamjambo,Mmeamkaje Wapendwa/Waungwana?
Tumshukuru Mungu wetu kwa mambo mengi na makuu ..

Asante Baba wa Mbinguni kwa kutuchagua na kutupa kibali cha kuendelea kuiona siku hii..
Tazama Jana imepita Baba Leo ni siku mpya na Kesho ni siku nyingine..!!
Tunaomba ukaibariki siku hii na ukatubariki katika maisha yetu..

Tunakuja mbele zako tukijinyenyekeza na kujiachilia mikononi mwako Baba wa Mbinguni,Maisha yetu yapo nawe  Yahweh..!! Amani inapatikana kwako, Upendo wa kweli una wewe Jehovah..!Furaha ipo kwako..!
Tumaini letu ni wewe jehovah..!!Mungu wetu,Muumba wetu,Mungu wa Abrahamu,Isaka na Yakobo..!!
Tunaomba ukabariki kazi zetu,Biashara,Masomo,Vyombo vya usafiri,Tuingiapo,tutokapo,hatua zetu ziwe nawe Jehovah..Vilaji/vinywaji,Ukabariki Ridhiki zetu ziingiazo na zitokazo, vyote tunavyoenda kugusa/kutumia Baba ukavitakase kwa Damu ya mwanao mpendwa Bwana wetu na mwakozi wetu Yesu Kristo yeye aliteseka ili sisi tupate kupona..Jehovah.. ukatutakase Miili yetu na Akili zetu, tupate kutambua/kujitambua..
Roho Mtakatifu ukatuongoze kwenye kunena/kutenda na tukawe na kiasi..
Tunakwenda kinyume na yule mwovu na kazi zake zote..
Baba wa mbinguni ukatuokoe na kutufunika na Damu ya Bwana wetu Yesu Kristo..
Tunakuja mbele zako Baba tunaomba utusamehe pale tulikwenda kinyume nawe,kwakuwaza,kwakutenda,kwakunena,kwakujua,kutojua..
Mfalme wa Amani tunaomba utupe na sisi Neeema ya kuweza kuwasamehe wote waliotukosea ..
Yahweh..ukawaguse na mkono wako wenye nguvu ,ukawaponye na kuwaokoa wote waliokwenye vifungo mbalimbali,Wagonjwa,wafiwa ukawemfariji wao,wenye shida/tabu,wanaopitia magumu/majaribu mbalimbali..Baba ukawaponye kimwili na kiroho..Baba ukaonekane kwenye shida zao..
Wapendwa tuendelee kuamini na kumtumaini Mungu wetu yeye atosha..

Yesu ni ufufuo na uhai..!!


Yesu alipofika huko alikuta Lazaro amekwisha kaa kaburini kwa siku nne. Kijiji cha Bethania kilikuwa karibu na Yerusalemu, umbali upatao kilomita tatu. Wayahudi wengi walikuwa wamefika kwa Martha na Maria kuwafariji kwa kifo cha kaka yao. Basi, Martha aliposikia kwamba Yesu alikuwa anakuja, akaenda kumlaki; lakini Maria alibaki nyumbani. Martha akamwambia Yesu, “Bwana, kama ungalikuwa hapa, kaka yangu hangalikufa! Lakini najua kwamba hata sasa chochote utakachomwomba Mungu, atakupa.” Yesu akamwambia, “Kaka yako atafufuka.” Martha akamjibu, “Najua kwamba atafufuka wakati wa ufufuo, siku ya mwisho.” Yesu akamwambia, “Mimi ndimi ufufuo na uhai. Anayeniamini mimi hata kama anakufa, ataishi; na kila anayeishi na kuniamini, hatakufa kamwe. Je, waamini hayo?” Martha akamwambia, “Ndiyo Bwana! Mimi naamini kwamba wewe ndiwe Kristo, Mwana wa Mungu, yule ajaye ulimwenguni.”

Tunayaweka haya yote mikononi mwako Baba wa Mbinguni tukiamini na kushukuru..
Amina..!
Asante kwa wote mliopita hapa Mungu aendelee kuwabariki na kuwaongoza katika maisha yenu..
Nawapenda.

Amri kumi
(Kumb 5:1-21)

1Mwenyezi-Mungu alizungumza maneno haya yote, akasema, 2“Mimi ndimi Mwenyezi-Mungu, Mungu wako, niliyekutoa nchini Misri, ambako ulikuwa mtumwa.
3“Usiwe na miungu mingine ila mimi.20:3 Usiwe … mimi: Au usiwe na miungu mingine zaidi yangu.
4 Taz Kut 34:17; Lawi 19:4; 26:1; Kumb 4:15-18; 27:15 “Usijifanyie sanamu ya miungu wa uongo, au kinyago cha chochote kilicho mbinguni, katika nchi au majini chini ya dunia. 5Taz Kut 34:6-7; Hes 14:18; Kumb 7:9-10 Usiisujudie wala kuitumikia; kwa kuwa mimi Mwenyezi-Mungu, Mungu wako, ni Mungu mwenye wivu. Nawapatiliza wana maovu ya baba zao, hata kizazi cha tatu na cha nne cha hao wanichukiao. 6Lakini nawafadhili maelfu ya wale wanipendao na kuzishika amri zangu.
7 Taz Lawi 19:12; Kumb 18:20; Roma 13:9; Yak 2:11 “Usilitaje bure jina langu mimi Mwenyezi-Mungu, Mungu wako. Maana mimi Mwenyezi-Mungu sitaacha kumwadhibu anayetumia jina langu vibaya.
8“Usisahau kuiweka takatifu siku ya Sabato. 9Siku sita fanya kazi na tenda mambo yako yote. 10Lakini siku ya saba ni Sabato ya Mwenyezi-Mungu, Mungu wako. Siku hiyo usifanye kazi yoyote, wewe, wala mwanao, wala binti yako, wala mtumwa wako, wala watumishi wako wa kike, wala mnyama wako wa kufugwa, wala mgeni aliye nyumbani mwako. 11Maana kwa siku sita mimi Mwenyezi-Mungu niliziumba mbingu na dunia, bahari na vyote vilivyomo, kisha nikapumzika siku ya saba. Kwa hiyo mimi Mwenyezi-Mungu niliibariki siku ya Sabato, nikaitakasa.
12“Waheshimu baba yako na mama yako, ili uishi maisha marefu katika nchi ninayokupa mimi Mwenyezi-Mungu, Mungu wako.
13“Usiue.
14“Usizini.
15 Taz Lawi 19:11; Mat 19:18; Marko 10:19; Luka 18:20; Roma 13:9 “Usiibe.
16 Taz Kut 23:1 Mat 19:18; Marko 10:19; Luka 18:20 “Usimshuhudie jirani yako uongo.
17“Usiitamani nyumba ya jirani yako, wala mke wake, wala mtumwa wake wa kiume au wa kike, wala ng'ombe wake, wala punda wake, wala chochote kilicho mali ya jirani yako.”
18Watu waliposikia ngurumo na kuona umeme ukiwaka na kuisikia sauti ya parapanda juu ya mlima uliokuwa unafuka moshi, wote waliogopa na kutetemeka. Wote walisimama mbali, 19wakamwambia Mose, “Ongea nasi wewe mwenyewe, nasi tutakusikiliza, lakini Mwenyezi-Mungu asiongee nasi, tusije tukafa.” 20Mose akawaambia, “Msiogope, maana Mungu amekuja kuwajaribu ili mpate kumcha yeye daima na msitende dhambi.”
21Watu wote walisimama mbali wakati Mose alipokaribia lile wingu zito alimokuwamo Mungu.

Sheria kuhusu madhabahu

22Mwenyezi-Mungu akamwambia Mose, “Waambie Waisraeli: ‘Mmejionea nyinyi wenyewe kwamba nimeongea nanyi kutoka mbinguni. 23Mtaniheshimu mimi peke yangu wala msijifanyie miungu ya fedha wala ya dhahabu. 24Nyinyi mtanijengea madhabahu ya udongo ambayo juu yake mtanitambikia kondoo wenu na ng'ombe wenu kama sadaka za kuteketezwa na sadaka za amani. Mahali popote nitakapowakumbusha watu jina langu, papo hapo mimi mwenyewe nitawajia na kuwabariki. 25Taz Kumb 27:5-7; Yosh 8:31 Kama mkinijengea madhabahu ya mawe, msiitengeneze kwa mawe ya kuchonga, maana mkitumia vyombo vya kuchongea mawe, mtaitia najisi. 26Wala msitengeneze madhabahu yenye ngazi za kupandia, mtu asije akauona uchi wa huyo anayepanda juu yake.’

Kutoka20;1-26

Biblia Habari Njema kwa Watu Wote(BHN)

"Swahili Na Waswahili"Mbarikiwe.

Tuesday 25 April 2017

Kikombe Cha Asubuhi;Kutoka 19...




Shalom,Habari za Asubuhi,Hamjambo,Mmeamkaje Wapendwa/Waungwana?
Mungu wetu ni muweza wa yote..Tumshukuru na Kumsifu daima..
Yeye aliyetuumba,Yeye aliyetupa kibali  cha kuendelea na kuiona tena Leo hii,Yeye kwa Mapenzi yake, Neema/Rehema zake ametuamsha tena,

yeye aliyetuchagua sisi,Yeye ni Mungu wetu,Muumba wetu,Muumba mbingu na Nchi, Mungu wa Abrahamu,Isaka na Yakobo, Baba yetu,Mfalme wa Amani, Muweza wa yote, Yeye ni mwanzo na yeye ni mwisho,Hakuna kama yeye na hatokuwepo,Yeye ni Alfa na Omega..Jehovah Nissi..!! Jehovah Rapha..!! Jehovah Jireh..!! Jehovah Shammah..!!El shaddah..!!!
Unatosha Baba, Neema  zako zatutosha, hakuna wa kufanana nawe Baba..!!Sifa na utukufu ni kwako daima..!!
Tunashuka mbele zako Baba ili wewe uinuliwe Daima... Tunakuja mbele zako, tunajiachilia mikononi mwako Baba na kujinyenyekeza...
Tunaomba utuokoe na kututakasa kwa Damu ya Mwanao mpendwa Bwana wetu  na Mwokozi wetu Yesu Kristo wa Nazareti..
Ututakase miili yetu na Akili zetu. tupate kujitambua/kutambua..
Ukabariki Kazi zetu,Biashara,Masomo , Vilaji/Vinywaji, Tuingiapo/tutokapo, Hatua zetu zikawe nawe Yahweh..!! Tazama vyote tunavyoenda kugusa/kutumia navyo tunaomba ukavitakase...
Tunaomba utusamehe pale tulipokwenda kinyume nawe Baba.. kwakuwaza,kwakunena, kwakutenda,kwakujua,kutojua..Mfalme wa Amani tunaomba nasi utupe Neema yakuweza kuwasamehe wote waliotukosea..
Tunakwenda kinyume na mwovu na kazi zake zote..

Baba wa Mbinguni utuokoe..
Baba wa Mbinguni tazama wenyeshida/tabu,wagonjwa,waliomagerezani pasipo na hatia,waliofungwa na mwovu Baba,wafiwa ukawe mfariji wao, Yatima na Wajane Mungu wangu na wote wanaopitia magumu/majaribu..
Tunaomba Baba ukawaponye na kuwaokoa, ukawaguse na mkono wako wenye nguvu..Uponyaji wa kweli una wewe..Ukawaweke huru Baba na wakapatekupona kimwili na kiroho.. Ukuu wako ukaonekane Baba wa Mbingu..
Asante Mungu wetu katika yote.. Maisha yetu yapo mikononi mwako..
Tukawe chombo chema na tukatumike sawasawa na mapenzi yako..
Tunayaweka haya yote mikononi mwako na Tunakushuru na kukusifu..
Tukiamini wewe ni Mungu wetu na Mlinzi wetu..kwako wewe hakuna linaloshindikana..Tunakuabu siku zote na Imani, Tumaini la kweli lipo kwako..


Utuonee huruma, ee Mungu, utubariki; utuelekezee uso wako kwa wema; dunia yote ipate kutambua njia yako, mataifa yote yajue nguvu yako ya kuokoa. Watu wote wakutukuze, ee Mungu; watu wote na wakusifu! Mataifa yote yafurahi na kuimba kwa furaha; maana wawahukumu watu kwa haki, na kuyaongoza mataifa duniani. Watu wote wakutukuze, ee Mungu; watu wote na wakusifu! Nchi imetoa mazao yake; Mungu, Mungu wetu, ametubariki. Mungu aendelee kutubariki. Watu wote duniani na wamche.
Amina..!!!

Asanteni wote mliopitia hapa Mungu aendelee kuwabariki katika mahitaji yenu.
Nawapenda.

Waisraeli mlimani Sinai

1Siku ya kwanza ya mwezi wa tatu tangu walipotoka nchini Misri, watu wa Israeli walifika katika jangwa la Sinai. 2Walipoondoka Refidimu na kufika jangwa la Sinai, huko walipiga kambi mbele ya mlima Sinai. 3Basi, Mose akapanda juu mlimani kwa Mungu. Hapo Mwenyezi-Mungu akamwita Mose kutoka huko juu mlimani, akamwambia, “Hivi ndivyo utakavyowaambia wazawa wa Yakobo, hao Waisraeli, 4‘Nyinyi wenyewe mmeona nilivyowatenda Wamisri na jinsi nilivyowachukua kama tai anavyochukua watoto wake kwa mabawa, nikawaleta kwangu. 5Taz Kumb 4:20; 7:6; 14:2; 26:18; Tito 2:14 Sasa basi, kama mkiitii sauti yangu na kulishika agano langu, mtakuwa watu wangu wateule kati ya mataifa yote, maana dunia yote ni yangu. 19:5-6 Taz 1Pet 2:9 6Taz Ufu 1:6; 5:10 Mtakuwa kwangu ufalme wa makuhani na taifa takatifu.’ Hayo ndiyo maneno utakayowaambia Waisraeli.”
7Basi, Mose akarudi, akawakusanya pamoja wazee wa Waisraeli na kuwaambia maneno hayo aliyoamriwa na Mwenyezi-Mungu. 8Watu wote wakaitikia kwa pamoja wakisema, “Mambo yote aliyoyasema Mwenyezi-Mungu, tutayafanya.” Mose akamjulisha Mwenyezi-Mungu jibu hilo la watu. 9Mwenyezi-Mungu akamwambia Mose, “Haya, mimi nitakujia katika wingu zito ili Waisraeli wapate kunisikia ninaposema nawe na kukuamini siku zote.”
Kisha Mose akamwambia Mungu jinsi watu walivyosema. 10Mwenyezi-Mungu akamwambia Mose, “Nenda kwa watu uwatakase leo na kesho. Waambie wayafue mavazi yao 11wawe tayari kwa kesho kutwa, maana siku hiyo ya tatu mimi Mwenyezi-Mungu nitashuka juu ya mlima Sinai mbele ya watu wote. 12Taz Ebr 12:18-20 Tena wewe utawawekea watu mpaka kuzunguka mlima. Utawakanya wajihadhari sana wasipande juu mlimani wala kuugusa mpaka wake. Yeyote atakayeugusa mlima, atauawa. 13Mtu asimguse mtu huyo; atauawa kwa kupigwa mawe au mshale awe ni mtu au ni mnyama, hataishi. Wakati mbiu itakapopigwa mfululizo, watu wote watakaribia mlimani.”
14Basi, Mose akashuka mlimani na kuwaendea watu, akawatakasa, nao wakayafua mavazi yao. 15Kisha akawaambia watu wote, “Kesho kutwa muwe tayari, na mwanamume yeyote asimkaribie mwanamke.”
16 Taz Ufu 4:5 Basi, siku ya tatu asubuhi, kukatokea ngurumo na umeme na wingu zito juu ya mlima. Ikasikika pia sauti kubwa ya mbiu ambayo iliwatetemesha watu wote kambini. 19:16-18 Taz Kumb 4:11-12 17Kisha Mose akawaongoza watu wote kutoka kambini, wakaenda kukutana na Mungu. Wote walikwenda wakajipanga chini ya mlima.
18Mlima wa Sinai ulikuwa umefunikwa na moshi kwa kuwa Mwenyezi-Mungu alishuka juu yake katika moto. Moshi wa moto huo ulipanda juu kama moshi wa tanuri kubwa na mlima wote ulitetemeka kwa nguvu. 19Sauti ya mbiu ilizidi kuongezeka, na Mose akaongea na Mungu. Mungu naye akamjibu katika ngurumo.
20Mwenyezi-Mungu alishuka juu ya mlima Sinai, akamwita Mose kutoka huko juu, naye Mose akapanda mlimani. 21Kisha Mwenyezi-Mungu akamwambia Mose, “Shuka chini ukawaonye watu wote wasije kunitazama; la sivyo wengi wao wataangamia. 22Hata makuhani ambao hunikaribia wanapaswa kujitakasa; la sivyo nitawaadhibu.” 23Mose akamwambia Mwenyezi-Mungu, “Watu hawa hawawezi kuupanda mlima wa Sinai kwani wewe mwenyewe ulituamuru tuweke mpaka kuuzunguka mlima.” 24Mwenyezi-Mungu akasema, “Teremka chini kisha urudi pamoja na Aroni. Lakini usiwaruhusu makuhani na watu wengine wapite mpaka na kuja kwangu, la sivyo nitawaadhibu.” 25Basi, Mose akashuka na kuwaambia Waisraeli mambo yote aliyoagizwa.

Kutoka19;1-25

Biblia Habari Njema kwa Watu Wote(BHN)

"Swahili Na Waswahili"Mbarikiwe.

Monday 24 April 2017

SHEREHE YA UBATIZO WA MTOTO ROSELYN HENRY KAPINGA KATIKA UKUMBI WA VIP WANYAMA HOTEL SINZA.


Cake maalum kwa ajili ya Ubatizo wa mtoto Roselyn Kapinga iliyoandaliwa na Aunt Agnes Makwati ikiwa tayari kwa kukatwa.
Aunt Eva (Doto) akiwa amembeba Roselyn kabla ya kuanza tukio la kukata Cake.
Mama wa Kiroho Aunt Esther Mbapila akitoa zawadi ya Roselyn kwa mama Roselyn
Cindy Makwati akimlisha cake Mama Roselyn kwa niaba ya Roselyn huku baba Roselyn akishuhudia tukio hilo.
Cindy akijiandaa kumlisha cake Aunt Agnes ambaye ni mama yake.
Babu Roselyn naye hakuwa nyuma katika kusherehekea Ubatizo wa mjukuu wake.




Mtoto Roselyn Henry Kapinga alipata Ubatizo siku ya Jumatatu ya Pasaka ya tarehe 17/04/2017 katika kanisa la Mt. Petro Oysterbay jijini Dar es salaam na baadae kufuatiwa na sherehe fupi iliyofanyika katika Ukumbi wa ndani katika Hoteli ya Wanyama Sinza jijini Dar es salaam.

Kikombe Cha Asubuhi;Kutoka 18...

Shalom,Habari za Asubuhi,Hamjambo,Mmeamkaje Wapendwa/Waungwana?
Ni siku nyingine tena Mungu ametuchagua na kutupa kibali cha kuendelea kuiona Leo hii..Tunamshukuru Mungu katika yote,ametulinda wiki nzima na usiku umepita, tumeamka tena..Asante kwa Neema/Rehema hii..
Tazama Jana imepita Baba Leo ni siku mpya na Kesho ni siku nyingine Jehovah..
Tunakuja mbele zako na tukijinyenyekeza, Tukishukuru na kukusifu Daima..
Tunaomba ukatulinde,ukatuponye,ukatutakase na kutufunika kwa Damu ya mwanao mpendwa Bwana wetu na Mwokozi wetu Yesu Kristo wa Nazareti.Maisha yetu yawe mikononi mwako Yahweh..
Roho Mtakatifu akatuongoze kwenye Kunena/kutenda na tukawe na kiasi..
Baba ukabariki kazi zetu,Biashara,Masomo na vyote tunavyoenda kugusa/kutumia Baba ukavitakase kwa Damu ya Bwana wetu Yesu Kristo..
Baba ukabariki Vilaji /vinywaji tuingiapo/tutokapo,tutembeapo hatua zetu ziwe nawe Jehovah..

Baba tazama wenye Shida/Tabu,Wanaopitia magumu/majaribu,Wagonjwa, wafiwa ukawe mfariji wao..Tunaomba ukawaguse na mkono wako wenye nguvu na ukawaponye na kuwaokoa wapate kupona kimwili na kiroho pia..
Jehovah..Utusamehe pale tulipo kwenda kinyume nawe..kwakujua/kutojua,kwakunena/kwakutenda,kwakuwaza..
Baba tunaomba nasi ukatupe Neema ya kuweza kuwasamehe wote waliotukosea..
Tunakwenda kinyume na yule Mwovu na kazi zake zote..

Baba ukatuokoe na kutulinda katika safari yetu ya maisha..
tukawe chombo chema na tukatumike sawasawa na mapenzi yako..

Baba tunaiweka Nchi hii tunayoishi mikononi mwako..Ukaibariki na kutubariki wote tunaoishi humu..ukawe mlinzi mkuu na ukatawale katika yote..
Tunaiweka Tanzania na watanzania wote  mikononi mwako ukawabariki na kuwabariki watu wake popote walipo..ukaonekane juu yao.. ukawe mtalawa mkuu..
Afrika na Dunia nzima iwe mikononi mwako, ukawe mtawala mkuu na ukawaongoze wanaotuongoza wakatuongoze katika haki kweli.
Tazama watoto wetu Leo wamerudi shule Baba ukaonekane kwenye masomo yako..wapate kuelewa na kukumbuka yote wanayofundishwa..

Ukawalinde katika ujana wao na wakawe na hofu yako Mungu..
waje kuwa watu wema mbele zako na jamii pia.
Neema yako yatutosha Yahweh..Furaha na Amani vipo kwako, Upendo wa kweli una wewe..Fadhili na wema ukokwako Jehovah..Uzima wa milele unapatikana kwako Mungu wetu, Muumba wetu, Mungu wa Abrahamu,Isaka na Yakobo..!!
Tunayaweka haya yote mikononi mwako.. tunakuabudu na Kuamini  wewe ni Mungu wetu na hatuna Mungu mwingine Leo kesho na hata Milele..
Amina..!
Asante kwa wote mliopita hapa natumaini hamtotoka watupu..
Mungu aendelee kuwaBariki..
Nawapenda.


Yethro anamtembelea Mose
(Kumb 1:9-18)
1Yethro, kuhani wa Midiani, baba mkwe wa Mose, alisikia juu ya mambo yote ambayo Mwenyezi-Mungu alimtendea Mose na Waisraeli alipowatoa katika nchi ya Misri. 2Taz Kut 2:21-22 Kwa hiyo Yethro, akiwa na Sipora, mkewe Mose, ambaye Mose alikuwa amemrudisha kwa baba yake, alimwendea Mose, 3Taz Mate 7:29 pamoja na watoto wawili wa Mose. Mtoto wa kwanza aliitwa Gershomu. Mose alimpa jina hili kwa vile alisema, “Nimekimbilia18:3 Nimekimbilia: Au nimekuwa mgeni, au mkimbizi Kiebrania: Ger. katika nchi ya kigeni.” 4Wa pili aliitwa Eliezeri,18:4 Eliezeri: Kiebrania “Eli” maana yake “Mungu wangu,” na “ezeri” maana yake “msaada.” kwa vile Mose alisema, “Mungu wa baba yangu ndiye aliyenisaidia nisiuawe na Farao.”
5Yethro, mkwewe Mose, alikuja pamoja na binti yake, yaani mkewe Mose, pamoja na watoto, akamkuta Mose jangwani alikokuwa amepiga kambi kwenye mlima wa Mungu. 6Mose alipoambiwa kuwa baba mkwe wake pamoja na mkewe na wanawe wawili wanakuja, 7alitoka kwenda kumlaki baba mkwe wake, akamwinamia na kumbusu. Wakasalimiana, kisha wakaingia hemani. 8Mose akamweleza mkwewe mambo yote Mwenyezi-Mungu aliyomtenda Farao na Wamisri kwa ajili ya Waisraeli. Alimwambia pia juu ya shida zote zilizowapata safarini na jinsi Mwenyezi-Mungu alivyowaokoa. 9Yethro akafurahishwa na yote aliyotenda Mwenyezi-Mungu kwa ajili ya Waisraeli, kwa kuwaokoa mikononi mwa Wamisri. 10Yethro akasema, “Na atukuzwe Mwenyezi-Mungu ambaye amewaokoa mikononi mwa Wamisri na kutoka utumwa wa Farao. 11Sasa najua kwamba Mwenyezi-Mungu ni mkuu kuliko miungu yote, kwani amewakomboa watu hawa mikononi mwa Wamisri ambao waliwatendea ujeuri.” 12Hapo Yethro, baba mkwe wa Mose, akamtolea Mungu sadaka za kuteketezwa na tambiko. Naye Aroni akaja pamoja na wazee wa Israeli ili kula chakula pamoja na Yethro, mbele ya Mwenyezi-Mungu.

Kuteuliwa kwa waamuzi
(Kumb 1:9-18)

13Kesho yake, Mose aliketi kuamua matatizo ya Waisraeli, nao wakasimama wakiwa wamemzunguka, tangu asubuhi mpaka jioni. 14Yethro, baba mkwe wa Mose, alipoyaona mambo yote ambayo Mose aliwafanyia Waisraeli, alimwuliza, “Kwa nini unawafanyia watu mambo haya? Mbona unaketi peke yako huku watu wamekuzunguka tangu asubuhi mpaka jioni?” 15Mose akamjibu mkwewe, “Kwa sababu watu huja kwangu kuuliza matakwa ya Mungu. 16Wakiwa na ugomvi wowote ule wao huja kwangu nami huamua kati ya mtu na mwenzake, na kuwafunza amri za Mungu na maamuzi yake.” 17Basi, Yethro akamwambia Mose, “Unavyofanya si vizuri! 18Utajidhuru mwenyewe na hawa watu kwa uchovu, kwani hii ni kazi ngumu usiyoweza kuifanya peke yako. 19Sikiliza shauri langu kwako, na Mungu awe pamoja nawe. Wewe utawawakilisha watu mbele ya Mungu na kumletea Mungu matatizo yao. 20Hali kadhalika utawafundisha amri na maamuzi ya Mungu na kuwaonesha jinsi inavyowapasa kuishi na kufanya. 21Lakini kuhusu mambo mengine, chagua miongoni mwa watu wote, watu wanaostahili, watu wanaomcha Mungu, waaminifu na wanaochukia kuhongwa. Wape hao mamlaka, wawe na jukumu la kuwasimamia watu katika makundi ya watu elfu, mia, hamsini na kumikumi. 22Hao ndio watakaokuwa na vikao kila siku kutatua matatizo ya watu. Matatizo magumu watakuletea wewe, lakini yale madogomadogo watayaamua wenyewe. Kwa njia hiyo utaweza kurahisisha kazi yako kwa vile watashirikiana nawe katika jukumu hilo. 23Ukifanya hivyo, na kama ndivyo atakavyo Mungu, utaweza kustahimili na watu hawa wote wataweza kurudi makwao kwa amani.”
24Mose alilisikiliza shauri hilo la mkwewe na kufanya kama alivyoshauriwa. 25Basi, akawateua watu wenye uwezo kati ya Waisraeli, akawafanya kuwa viongozi wa makundi ya watu elfu, watu mia, watu hamsini na watu kumikumi. 26Nao wakawa wanaamua matatizo ya watu kila wakati. Matatizo magumu walimletea Mose, lakini yale madogomadogo waliyatatua wao wenyewe. 27Baada ya kufanya hivyo, Mose na mkwewe wakaagana naye Yethro akarudi nchini kwake.
Kutoka18;1-27

Biblia Habari Njema kwa Watu Wote(BHN)

"Swahili Na Waswahili"Mbarikiwe.