Swahili na Waswahili

Swahili na Waswahili
Waswahili na Mswahili Rachel Siwa...Pamoja Daima!!
Showing posts with label Imani/waswahili. Show all posts
Showing posts with label Imani/waswahili. Show all posts

Thursday 17 August 2017

Mahojiano na Mch Absalom Nasuwa kuhusu Mkutano wa Askofu Gwajima DC



Karibu na asante kwa kujiunga nasi

Kanisa la Umoja International Outreach lililopo jijini Dallas Texas limeandaa mikutano ya injili katika maeneo ya Texas na Washington DNV.

Mwanzilishi na Mchungaji kiongozi wa kanisa hilo, Mch Absalom Nasuwa alizungumza na Mubelwa Bandio kuhusu mkutano huo

KARIBU



Pia Mch Nasuwa alizungumzia huduma yake

Monday 24 April 2017

SHEREHE YA UBATIZO WA MTOTO ROSELYN HENRY KAPINGA KATIKA UKUMBI WA VIP WANYAMA HOTEL SINZA.


Cake maalum kwa ajili ya Ubatizo wa mtoto Roselyn Kapinga iliyoandaliwa na Aunt Agnes Makwati ikiwa tayari kwa kukatwa.
Aunt Eva (Doto) akiwa amembeba Roselyn kabla ya kuanza tukio la kukata Cake.
Mama wa Kiroho Aunt Esther Mbapila akitoa zawadi ya Roselyn kwa mama Roselyn
Cindy Makwati akimlisha cake Mama Roselyn kwa niaba ya Roselyn huku baba Roselyn akishuhudia tukio hilo.
Cindy akijiandaa kumlisha cake Aunt Agnes ambaye ni mama yake.
Babu Roselyn naye hakuwa nyuma katika kusherehekea Ubatizo wa mjukuu wake.




Mtoto Roselyn Henry Kapinga alipata Ubatizo siku ya Jumatatu ya Pasaka ya tarehe 17/04/2017 katika kanisa la Mt. Petro Oysterbay jijini Dar es salaam na baadae kufuatiwa na sherehe fupi iliyofanyika katika Ukumbi wa ndani katika Hoteli ya Wanyama Sinza jijini Dar es salaam.