Swahili na Waswahili

Swahili na Waswahili
Waswahili na Mswahili Rachel Siwa...Pamoja Daima!!

Monday 24 February 2014

Jikoni Leo;Jee Umeshawahi Kutumia Vitu Hivi?


Waungwana;"Jikoni Leo",Tukumbuke vifaa hivi vya kupikia na Kuhifadhia/Kuwekea Maji  ya Kunywa.
Mimi navijua kama Vyungu/Chungu na Mtungi.

Wewe unavijua kwa jina gani?
Jee Umewahi /Bado Unatumia?

Mtoto wangu Sandra Alipokuwa  mdogo alikuwa anaita Vyungu/Chungu.."KIMBONDO"

"Swahili NA Waswahili" Pamoja Sana.

Sunday 23 February 2014

Natumaini J'Pili Inaendelea Vyema;Burudani-Yesu Ni Bwana by E R Mwansasu Chidumule!!!




Natumaini J'Pili inaendelea vyema;Na asubuhi walipokuwa wakipita,waliuona ule mti umenyauka toka shinani.
Neno La Leo;Marko Mtakatifu:11:20-26.

Kwa sababu hiyo nawaambia,Yo yote myaombayo mkisali,aminini ya kwamba mnayapokea,nayo yatakuwa yenu.






"Swahili Na Waswahili"MUNGU  Atubariki Sote.

Saturday 22 February 2014

[AUDIO]: DAKIKA 90 ZA DUNIA: Kwanini Facebook imetumia dola bilioni 19 kununua WhatsApp?‏


Photo: Mobile88.com

Kama wewe ni mmoja wa wanaotumia njia ya mawasiliano iliyojipatia umaarufu ya
WhatsApp, basi ujue kuwa nawe ni miongoni mwa wateja takribani nusu
bilioni walioufanya mtandao huo kuwa maarufu zaidi duniani kwa kipindi
kifupi tu.

Ni umaarufu huu uliofanya kampuni kubwa ya mawasiliano
ya Facebook wiki hii kuona umuhimu wa kutumia dola za kimarekani bilioni
19 kununua WhatsApp.

Lakini kwanini kampuni itumie kiasi hicho kikubwa kwa kampuni kama hii?

Hii ni sehemu ya ripoti ya Jamii Production kwenye kipindi cha DAKIKA 90 ZA DUNIA kinachorushwa na kituo cha Radio cha Capital FM cha Dar Es Salaam Tanzania kila Jumamosi kuanzia saa moja na nusu asubuhi (7:30 AM).


Monday 17 February 2014

Tano Ladies Na Maadhimisho ya Siku Ya Wanawake Duniani;Tarehe 8.03.2014!!!!!!

Wakiwa na Mhe.Balozi ;Liberata Mulamula
Wakiwa na Mhe.January Makamba
Wenyewe Wanawake wa Shoka Tano Ladies!!!!

"Swahili Na Swahili"Tukiwa na Nia Moja,Pamoja Tunaweza.

Thursday 13 February 2014

Jikoni Leo; Tupo Sokoni-Zanzibar Market!!!!!









Waungwana; "Jikoni Leo" tupo sokoni.
Nini kimekufurahisha na nini kimekuchukiza katika masoko haya?
Kwa walio mbali na Nyumbani nini kimekukumbusha na unakikosa hapo ulipo?

"Swahili Na Waswahili" Pamoja Daima.

Wednesday 12 February 2014

Wanawake Na Urembo-Nywele,Makeup!!!!



Waungwana;Wanawake na Urembo, jee wewe kwako UREMBO ni nini?
Kila Mwanamke  anacho anachokipenda kukifanya,kuboresha UREMBO wake,Wapo wanaopenda kunyoa Nyusi,Kupaka Wanja,Rangi za mdomo,Kusuka,Kuweka Nywele Bandia,Kucha na Mengine meengi.Jee wewe Wapenda nini?

kwapicha zaidi ingia;http://www.mitindoafrica-abroad.blogspot.co.uk/


"Swahili NA Waswahili" Pamoja Daima.

Monday 10 February 2014

[AUDIO]: Kipindi cha familia kutoka Jamii Productuion...BAJETI KATIKA FAMILIA‏


Bwn Solomon, Sunday Shomari na Herriet Shangirai wakijadili jambo ndani ya studio za Jamii Production. Washington DC
Karibu katika kipindi cha FAMILIA kutoka Jamii Production.
Katika kipindi hiki, tumejadili suala la BAJETI KATIKA FAMILIA.
umuhimu wake, namna ya kulitekeleza na mengine mengi.

Wachangiaji studio walikuwa ni Herriet Shangirai, Sunday Shomari, Solomon na Mubelwa Bandio
KARIBU UUNGANE NASI