Swahili na Waswahili

Swahili na Waswahili
Waswahili na Mswahili Rachel Siwa...Pamoja Daima!!

Wednesday 4 September 2013

Mswahili wetu Leo;Prof.Ahmed Nabhany- Jukwaa La Mashairi


Waungwana; Jukwaa La Mashairi.Jukwaani Leo na Mshairi,Mswahili wetu ; Prof.Ahmed Nabhany, Anatuchambulia tofauti ya   Mashairi.
Wewe unapenda Mashairi? ni Mtunzi /unajua  Mashairi,Ngonjera au?

Karibu Sana.......






"Swahili Na Waswahili" Pamoja Daima.

Monday 2 September 2013

Unaijua Hii? Si Ya Kukosa kabisa ni-FAHARI PASSION 2013!!!!!!

FAHARI PASSION 2013

Tanzania Women's Association (TAWA)

Saturday, 7 September 2013 at 18:00 - Sunday, 8 September 2013 at 00:00 (BST)

London, United Kingdom




You are cordially invited to a fashion showcase to present a collection of upcoming Tanzanian designers who will be given the opportunity to participate in the International Fashion Showcase 2014 in conjunction with London Fashion Week Feb 2014.

This is a ticket only event. Please follow the link to get tickets.
www.faharipassion2013.eventbrite.com

If any tanzanian upcoming jewellery or fashion designer would like to get involved message the TAWA page

or email info@tawa-uk.com

or contact:

Rose Kiondo - +447881098020
Sara Abood - +447908185618
Monique Ferguson-Rowe - +447949267007
Mariam Mungula - +447770910901

Thanks and we hope to see you there!

Sunday 1 September 2013

Nawatakia J'Pili njema ;Tusifu na Kuabudu-Burudani-How Great Thou Art,Great is thy Faithfulness,To GOD be the Glory!!!!!!



Wapendwa sina Maneno Mengi ni Kusifu na Kuabudu..MUNGU wetu ni Mwema Saana;[14]Zaidi ya hayo yote jivikeni Upendo,ndio kifungo cha ukamilifu.

[16]Neno la kristo na likae kwa wingi ndani yenu katika hekima yote,mkifundishana na kuonyana kwa zaburi, na nyimbo na tenzi za rohoni;huku mkimwimbia MUNGU kwa neema mioyoni mwenu.









Neno La Leo;Wakolosai:3:12-17.Na kila mfanyalo,  kwa neno au kwa tendo,Fanyeni yote katika jina la BWANA  YESU,mkimshukuru MUNGU BABA kwa yeye.

"Swahili Na Waswahili" Mbarikiwe Sana.

Saturday 31 August 2013

Chaguo La Mswahili Leo;Makoma!!!!!!!



Waungwana;Mmmhhh Hawa ni "MAKOMA"Hili ndiyo "Chaguo La Mswahili Leo" Moooto.. Nawakubali.. Maneno Meengi sina Leo Nasikilizia kutoka Kwenu..Twende Sote  sasa -Butu Na Moyi na...Endeleaaa.







"Swahili Na Waswahili" Pamoja Sana

Wednesday 28 August 2013

Wanawake Na Majukumu;Vipaji/Ubunifu!!!!!









Waungwana;Wanawake Na Majukumu;Vipaji/Ubunifu/Ujuzi..

Wapo Wanawake weengi sana wanajua Vitu/Mambo Mbalimbali lakini Hawajulikani.

Unafikiri ni Kwanini?
Wewe mwenzangu unajua/Una kipaji/Ujuzi Gani /nini?

"Swahili Na Waswahili" Pamoja Daima


Sunday 25 August 2013

Tumalizie J'Pili hii kwa Amani na Upendo;Brudani-Angela Chibolonza!!!

Wapendwa;Tumalizie J'Pili hii Vyema.

Lakini,ndugu, kwa habari ya nyakati na majira,hamna haja niwaandikie..........
Neno La Leo;1:Wathesalaonike:5:1-28..
[4]Bali ninyi,ndugu, hammo gizani,hata siku ile iwapate kama mwivi[5]Kwakuwa ninyi nyote mmekuwa wana wa nuru, na wana wa mchana;sisi si wa usiku, wala wa giza.[6]Basi tusilale usingizi kama wengine,bali tukeshe na kuwa na kiasi.

[16]Furahini siku zote;[17]Ombeni bila kukoma;[18]Shukuruni kwa kila jambo;maana hayo ni mapenzi ya MUNGU kwenu katika Kristo YESU.

[25]Ndugu,tuombeeni.[26]Wasalimuni ndugu wote kwa busu takatifu.[27]Nawaapisha kwa BWANA, ndugu wote wasomewe waraka huu.

[28]Neema ya BWANA wetu YESU Kristona iwe pamoja nanyi.










"Swahili Na Waswhili" Mbarikiwe Wote.

Wednesday 21 August 2013

Kisa Cha Leo na Mswahili Emu-Three;Wema Hauozi-Sehemu ya 52!!!!!



Tulitoka nje ya lile pango huku tukiwa tumekata tamaa ya kumpata huyu mtu tena,ikizingatia kuwa yeye analifahamu hilo pango lilivyo, na sisi japokuwa tupo wengi, lakini njia za kupita zilihitajia mtu mmoja mmoja,…

Bado tukiwa na matumaini ya kumpata huyo mtu akiwa hai, tuliharakisha kutoka, ili kuungana na wenzetu waliokuwa wakijibisha risasi na huyo jamaa, na baadaye kukawa kimiya, ikiashiria kuwa huenda huyo mtu alishatoka nje,

Swali likawa je kama huyo mtu kawahi kutoka nje, itakuwaje, kwani hatukukumbuka kumuacha askari zaidi ya mwanasheria, wote tulikimbilia kuingia ndani..na je hiyo amri ya kutokutumia risasi huko nje, itawezaje kuepukika, na mtu kama huyo?

Tuendelee na kisa chetu......

Tukajitahidi na sisi kutoka nje kwa haraka haraka, na tulipofika nje, tuliwaona askari wetu wamesimama huku wameelekeza silaha zao upande wa pili, kama wanawinda kitu, na mkuu ndiye aliyekuwa wa kwanza kutoka na bastola yake mkononi, akawauliza vijana wake

‘Yupo wapi’ akauliza

‘Mkuu kaingia kwenye hicho kichaka, na cha ajabu haonekani tena, lakini tuna uhakika yupo hapo, na tunahisi kuwa hayupo peek yake,…’akasema mmoja wapo, na wote wakaelekea kwenye hicho kichaka na kwa mbele wakaona watu wawili wakiwa kwenye mapigano na kila mmoja akiwa kamshika mwenzake mkono, ili kuzuia silaha yake, isielekezwe kwake.

Msaidieni mwanasheria, lakini msitumie silaha, kumbukeni tulivyoambiwa, ….’akasema mkuu, huku nay eye akielekea kule ambapo mwanasheria alikuwa akipambana na huyo mtu, na ilikuwa vigumu kuingilia kwani zile silaha walizoshika zingeliweza kufyatuka na kuleta madhara kwa yule ambaye angeliwakaribia, kwahiyo ikawa kutafuta jinsi ya kusaidia.

Mwanadada ambaye alikuwa nyuma akiwa na yule binti, alifika eneo hilo na kuona hiyo hali, na hapo akasema;.

`Mbona mumesimama, hamumsaidi mwenzenu…’akasema mwanadada, akikimbilia kule kwenye mapigano kati ya mwanasheria na huyo jamaa na alipofika tu, akasikia mlipuko wa risasi,…..oh, mwanasheria akapanua mdomo, na kudondoka chini, na yule mtu alipoona hivyo, akainuka kutaka kukimbia, lakini hakuweza hata kuinua mguu.

Risasi ililengwa bara bara, kutoka kichani, na yule mtu akatoa macho ya uwoga, na kudondoka chini, na hapo mwanadada na mkuu, wakawa wameduwaa, ina maana kazi yote imekuwa ni bure, ina maana masharti ya msituni yamevunjwa, na haijulikani ni kitu gani kitatokea.

Mkuu akamkimbilia yule mtu, na kuhakikisha hana silaha, na akamshika kuangalia kama yupo hai, na akainua kichwa kumwangalia mwanadada na kusema;

soma zaidi ingia;http://miram3.blogspot.co.uk/

Tupo pia kwenye: Facebook, na Twitter, bofya hapa upate zaidi;
https://www.facebook.com/emu.three
https://twitter.com/emuthree



"Swahili Na Waswahili" Pamoja Daima.