Swahili na Waswahili

Swahili na Waswahili
Waswahili na Mswahili Rachel Siwa...Pamoja Daima!!

Wednesday 18 January 2012

Ulale kwa Amani da'Regia!!!!!



 Poleni sana Ndugu,Jamaa,Marafiki na Taifa pia.Bwana alitoa na Bwana Ametwaa.

Monday 16 January 2012

Utafiti;Eti kuangalia TV kwa saa Moja kunapunguza dakika22 za Maisha Yako!!!


  • Ukifuata kila linalosemwa na wanasayansi utashindwa kuishi. Leo watasema kunywa kahawa kunapunguza msongo wa mawazo. Kesho watasema kunywa kahawa  huko huko kunaongeza shinikizo la damu na uwezekano wa kupata pigo la kiharusi. Leo watasema hiki na kesho watasema kile ali mradi ni vurugu tupu. Kibaya zaidi ni ukimya wao kuhusu nini cha kufanya hasa pale tafiti zao zinapotoa matokeo yanayokinzana
  • Kwa vile nyingi ya tafiti hizi hufanyika huko Ulaya na Marekani, Waafrika inabidi kuyapokea matokeo ya tafiti hizi kwa uangalifu sana kwani huwa hayazingatii mazingira yetu na mtindo wetu wa maisha (japo sasa tunajitahidi sana kuwaiga kwa kila kitu).  
  • Utafiti uliofanywa mwaka jana na wanasayansi wa Chuo Kikuu cha Queenesland unaonyesha kwamba kuangalia runinga kwa watu wenye umri wa miaka 25 na kuendelea kuna madhara makubwa kiafya na kunapunguza muda wa kuishi. Utafiti huu unaonyesha kwamba kwa kila saa moja unayoitumia ukiangalia runinga basi unajipunguzia dakika 22 katika maisha yako. Hii ni sawa na kuvuta sigara mbili. 
  • Wanasayansi hawa wanasema kwamba tatizo hasa siyo kuangalia tv bali madhara ya kukaa mahali pamoja kwa muda mrefu ambako kunasababisha magonjwa ya moyo, kisukari, kunenepeana na matatizo mengine ya kiafya yanayosababishwa na mtindo wa maisha ya kubweteka (sedentary lifestyle). Kufanya mazoezi, hata kama ni dakika 15 tu kwa siku ni jambo la muhimu na kumeonyeshwa kuwa na faida nyingi za kiafya ikiwemo kuongeza siku tatu katika maisha yako.
              Kusoma zaidi habari hii ingia kwa  Blog ya kaka Matondo[MMN]http://www.matondo.blogspot.com
                                   Ahsante kaka Matondo.

Saturday 14 January 2012

Siku kama ya leo kaka Isaac Alizaliwa!!!!!!

Siku kama ya Leo miaka kadhaa iliyopita, Kaka Isaac, babake  Sandra na Tracey,Mume ya MadameRachel-siwa,Alizaliwaaa!!!
Tunamshukuru sana Mungu kwa yote juu yako,Mungu akubariki na kukulinda kila inapoitwa Leo.
Akuongezee Miaka Mingi na Ufanikishe malengo yako.Uzidi kuwa Baraka kwetu na Kwa Watu wote.
 Tunakupenda saaana,Wako Rachel,Sandra,Tracey[ Rasca].


Friday 13 January 2012

Wanawake na Urembo!!!!!!!!






Nimatumaini yangu woote wazima,
Haya Waungwana Wanawake na Urembo! Kuna mengi kwenye hizi picha na kwa Wanawake kwa Ujumla,
Mimi leo si msemaji saana,Kazi kwenu nyie na Mitazamo yenu,kipi wewe umependa hapo/Kukuvutia na kipi hujapenda hapo,yaani kama ingekuwa wewe hapo ungeongezea nini au ungepunguza nini,Pia wewe Mwanaume kama ni Mkeo,dada,shangazi na...Ungependa nini aongeze au  apunguze nini?Na jee labda unapenda lakini hujui ufanyeje uwe/awe kama hivyo,au kunakingine unapenda hapo hakipo,Basi usisite kusema/Kutoa Mawazo,Ushauri na Kuelimishana kwa Upendo.

Karibuni sana.


Tuesday 10 January 2012

Wazazi /Walezi wa sasa na Malezi!!!!!!




                        watoto kutusaidia jikoni.

kusafisha vyumba vyao.

kusaidia kusafisha na sehemu nyinngine
Wabaki na Furaha/Amani.
Ni matumaini yangu wote wazima,
Haya wapendwa,Wazazi/walezi wenzangu,vipi watoto kufanya/kusaidia kazi za nyumbani,
Hii imekaaje/wewe unaonaje?kazi kama kusafisha vyumba,kuosha vyombo,kuaanda vyakula na kazi nyingine nyingi,Jee wewe unafikiri ni Umri gani uliosahihi kwa mtoto kuanza  kumfundisha kazi ndogondogo?naje huu ni Unyanyasaji au ni malezi ya kawaida? naje Kuna kazi za watoto wa kiume na wakike?kama ndiyo jee sisi wenye watoto wa jinsia moja je?Unafikiri watoto wote wanapenda kazi? je kama hataki?.
Mimi binafsi kazi nyingine sikuwa nazipenda kufanya nilipokuwa mtoto,lakini mama alikuwa ananilazimisha, jee alikuwa ananikosea au ndiyo malezi?Jee wewe unapenda/ulipenda kazi zote ufanyazo/ulizokuwa unafanya?.
Mwana Umleavyo ndivyo akuavyo au.......

Karibuni sana Waungwana katika kusaidiana Kimawazo,Kujadili na Kuelekezana kwa Upendo!!












Thursday 5 January 2012

Waswahili na Maisha yao-Coventry Swahili Party/Mwaka Mpya[shukrani]!!!



                             Asanteni sana  Swahili dadazzzz.
                                   dada Esther Asante.
                                      Wapendwa Mungu awabariki sana.
                                       Mbarikiwe Malongazzzzz.
                                    Ahsante sana mamaKisa.
                                       Ahsante sana Dj Rik/blogger wa the network.





                   Chakula; Nyama choma na vyote,Vimepikwa kwa  da'Batuli.
Ahsanteni sana wote kwa Upendo na kutoa Muda wenu kwa kujumuika nasi ,  Mungu awabariki sana,Tunawatakia kila lililo jema.Kwaniaba ya da'Maggie ,da'Vick na Familia yangu,TUNAWAPENDA SANA.


Tuesday 3 January 2012

Waswahili na Maisha yao -Coventry Swahili Party/Mwaka Mpya[part-1]!!!
























Waswahili Wakijichanganya -Mkesha wa Mwaka mpya,Hebron Church!!!

                                      Ibada.
                                          Ibada.
                                          Utamaduni.
                                   Michezo mbalimbali.
                                                Mchukua matukio,da'Tracey.
Ahsante sana Mungu kwa Ulinzi wako,Wewe watosha maishani mwetu.
Mungu awabariki wote,Muwe na wakati mwema kila iitwapo leo.
       MUNGU NI PENDO,NASI TUNAWAPENDA WOTE!!!