Swahili na Waswahili

Swahili na Waswahili
Waswahili na Mswahili Rachel Siwa...Pamoja Daima!!

Thursday 27 October 2011

ANGALIZO KWA WATANZANIA WOTE, UTAPELI HUU UNAANZA KUOTA MIZIZI.






KUNA TAARIFA ZA WANIGERIA AMBAO WAMEWEKA MASKANI MAENEO YA SINZA, SHUGHULI AMBAZO WANAFANYA WANAIGERIA HAWA BADO HAZIELEWEKI, NI TATA.
MUDA MWINGI HASA VIPINDI VYA JIONI WANAPENDA KUSHINDA KATIKA BAA KADHAA AMBAZO ZINA AMBAA AMBAA NA BARA BARA YA SHEKILANGO, KUANZIA MAENEO YA URAFIKI MPAKA BAMAGA.

HIVI KARIBUNI WATUMIAJI WENGI WA SIMU ZA KIGANJANI NA INTERNET WAMEKUWA WAKITUMIWA MESEJI MBALI MBALI ZA KUSHINDA ZAWADI FLANI, MFANO WATUMIAJI WA SIMU ZA KIGANJANI WAMEKUWA WAKIPATA MSG AMBAYO INAWAONYESHA WAMESHINDA ZAWADI KUTOKA KAMPUNI YA NOKIA, WAKATI UNAKUTA ULIOTUMIWA MSG HIYO MUDA HUO UNATUMIA SIMU YA MCHINA AMBAYO HAINA HATA JINA, NA WALE WATUMIAJI WA INTERNET WANAPATA EMAIL ZA KUTAKA WAINGIZE DETAIL ZAO ZA AKAUNTI ZAO ZA BENKI, HIYO EMAIL INAKUONYESHA KAMA VILE ULICHEZA BAHATI NASIBU FLANI.

WATANZANIA WOTE KAENI CHONJO, KAPINGAZ Blog BADO INAWAFUATILIA HAWA JAMAA ILI KUWEZA KUJUA UNDANI WAO, NA VILE VILE TUNAVIOMBA VYOMBO VYA USALAMA NAVYO VIWEZE KUJUA HAWA JAMAA WANAFANYA NINI, HOFU YETU INAWEZEKANA WAO NDIO WANAJIHUSISHA NA UTAPELI HUU AMBAO NAAMINI WATANZANIA WENGI BADO HAWAJAUJUA VIZURI WIZI HUU WA KUTUMIA MITANDAO.
  
  Habari hii nimetumiwa na Kapingaz Blog

Asante sana.

Tuesday 25 October 2011

Watoto wa Kike na Mitindo!!!!!!

                                 da'Nadia na poziiiii.
                              da'Nadia na Tabasam...
                                     da'Ester kapoziiii....
                                   da'Ester yupo makini....
                                         da'Miriam na poziiii....
                                 da'Naomi  dadalao kwa mitindo sijui Jina.....

Waungwana mnasemaje? Watoto wetu wakipendeza nasi pia roho nyeupeeeee!!!
Mpendwa wewe unapendelea watoto wakitoka vipi/wakivaa vipi?
Nini wewe ulikuwa Unapenda kutinga/kuvaa ulipokuwa mdogo?

Wengi enzi za Utoto kulikuwa na nguo maalum, yaani ya Kanisani/Jumapili, Hospitali,Siku Kuu,Yakutokea kwenda kwa ndugu na jamaaa na yaKushindia/ukiwa nyumbani au kuchezea Rede kama si mpira wa Miguuu!!!!Hahahahhha Tumetokambali mwehhhh.

Lakini Watoto wa Leo wengi wao hakuna Masharti sana kila wakati Wamependeza tuu.

Karibuni Sana Tukumbushane ya Utoto na kutoa Maoni/Mawazo yako kwani Yanathamani kwetu!!!









Sunday 23 October 2011

Mwanamke na Kujiamini!!!!

Wanawake Tufunguke,Tujitoe,Tuamke,Tushikamane,Tupendane,Tuelimishane,Tujifunze na Tujiamini,
Hakuna kitu rahisi, Lakini ukiamua na kujituma utafanikiwa, Hatua moja huanzisha na nyingine,Tusisite kuulizana na kuomba Ushauri pale unapoona umekwama.Pale ulipo na unaweza kufanya kitu ili kusaidiana na kina baba pamoja na Familia,Jamii. Kila mmoja anamuhitaji mwenzie kwanamna moja au nyingine,Kama wewe unafanya kazi na kuna mwingine anafanya biashara.Unaweza kutamani Vitumbua na pengine unajua kupika lakini umechoka au hujui basi kuna mama yupo nyumbani yeye anapika na akakuuzia nayeakapata pesa kidogo nawe umepata mlo,Binadamu kila mmoja anajua hiki na mwingine anajua kile.WANAWAKE TUSILALE.

Nawatakia Jumapili Njema!!!.


Wednesday 19 October 2011

Nimekumbuka Kwetu,Nyumbani ni Nyumbani!!!!!!!!!!!!

                Nimewakumbuka Rafiki Zangu.
               Nimewakumbuka wa kaka wa Mitaa ya Kwetu.
                           Nimewakumbuka Ndugu zangu.
          Nimewakumbuka Vijana wa Mitaa ya Kwetu.
      Nimekumbuka hata Usafiri Wetu.
Nimekumbuka  Maembe,Mabungo na Matunda yote na Wauzaji wake.Hasa Magenge ya Karibu!!!!!

Wapendwa mimi Leo nimekumbuka Kwetu/Nyumbani, yaani ukiniuliza sana machozi yanaweza kunitoka.
Nanimekumbuka meeeeengiiiiii yakwetu.

Zamani ikiwa Likizo tunapelekwa kwa bibi mzaa mama[bi' Mwalimu], sasa ukiona naanza kuandika majina ya ndugu zangu,marafiki na wazazi wangu ujue kumekucha, nikimaliza kuandika bibi ajiandae kunirudisha.Na kila j'Mosi tunapelekwa kwa bibi mzaa baba[bi'MwanaPenza],yeye alikuwa mzee kidogo hawezi kutuhudumia, Hatukai sana huko, nae akiona narudi rudi ndani kunywa maji ajiandae na maswali baba alisema atakuja saangapi?akizugazuga tuu nitamuangushia kilioooo mpaka atuja kwanini tulienda.

Duuhhhh sasa huku nilipo sasa na Ukubwa huu sijui nifanye nini??
Nimeimba leo kuanzia Nyimbo za mchakamchaka,za mwalimu Kachale,Kibuzi,Ukuti na zote za utoto,
Nikahamia Youtube na Cd zote za Nyumbani, lakini nikaona Haitoshi ngoja nishiriki nanyi.

Jee Mpendwa nawe kunasiku yanakukuta haya na je unafanya nini ili kusahau?au unajifariji vipi?

Karibuni sana kwa mchango wa mawazo na Ushauri!!!!!!!!!


Tuesday 18 October 2011

AIBU GANI HII BADO INAENDELEA KULIKUMBA TAIFA LETU!!




Jeshi la Polisi nchini (PT) kupitia Inspekta Generali wake Said Mwema(Pichani) imetangaza dau la Shilingi Milioni 5 kwa mtu yeyote atakaefanikisha kupatikana kwa mtu aliyemjeruhi mtoto Adam Robert (14) ambaye ni Albino huko Geita ambapo mtu asiyejulikana alimvamia mtoto huyo na kuanza kumkata kata mikono na kisha kutoweka na vidole vya Albino huyo.
Tukio hilo lilitokea usiku wa kuamkia mwishoni mwawiki katika Kijiji cha Nyaruguguna, Kata na Tarafa ya Nyang'hwale ambapo mlemavu huyo, Adam Robert (14), mwanafunzi wa darasa la nne, alivamiwa na kukatwa mkono wa kulia na kisha kunyofolewa vidole vitatu vya mkono wa kushoto.
Ni jambo la kusikitisha sana kuona vitendo hivi vinaendelea kutokea na mwisho wa siku jeshi linataka kutumia fedha za walipa kodi kwa ajili ya kuwapata wahalifu hao, mi nadhani hii njia sio sahihi, sidhani kama Jeshi la polisi wanashindwa kuwapata hawa wanaowatuma wahalifu kwenda kuwadhuru maalbino hawa. Jambo la msingi hapa sio kutangaza dau ni kuhakikisha wale wanaowatuma ndio wanakamatwa na ninaamini jeshi la polisi likishirikiana na usalama wa Taifa inawezekana kuwakamata hawa na kuwatokomeza kabisa, usalama wa Taifa wanafanya kazi gani kama sio pia na kuangalia usalama wa Watanzania hawa!
Ni aibu kubwa kwa Taifa letu vitendo hivi vinavyoendelea.
                                                            
                                                                          Habari hii nimetumiwa na KapingaZ Blog
                                                             Asante sana kaka Kapinga.

YUSTA MSOKA, MWANASHERIA ALIYEFANIKIWA KUTIMIZA MOJA YA NDOTO ZAKE.




Advocate Yusta Msoka

Yusta Msoka akiwa amesimama nyuma, mbele ya dirisha la pili upande wa kulia, akiwa katika picha ya pamoja na Wanasheria wenzake baada ya kula kiapo cha kuwa Advocate (Wakili)

KAPINGAZ Blog inapenda kumpongeza sana Dada Yusta kwa kufanikiwa kufika hapo alipofikia, vile vile inamshauri asiishie hapo aendelee zaidi mpaka aweze kufikia level ambayo ni ya kimataifa.

Kwa kutambua uhaba mkubwa wa Mawakili katika Taifa letu tunapenda kuwapongeza wale wote walioweza kufanikiwa kuwa Mawakili, tunawaomba wakafanye kazi zao kwa uadilifu na kuliletea sifa na mafanikio mazuri taifa letu, hasa hasa kuwa makini katika mikataba mikubwa ambayo taifa letu sasa linaangamia kutokana na mikataba hiyo.
                                                                             Habari hii nimetumiwa na Kapingaz Blog
                                                              Hongera da' Yusta.