Swahili na Waswahili

Swahili na Waswahili
Waswahili na Mswahili Rachel Siwa...Pamoja Daima!!

Thursday 13 October 2011

Mazishi ya Mpendwa Wetu; Baba Mzee Juma Penza, katika Picha

                       Marehemu Mzee Penza wakati wa Uhai wake.
     Kaka Mashaka akiweka Mchanga wa Mwisho.
       Kaka Mustapha akiweka Mchanga wa Mwisho.
               Kaka Iddy akiweka Mchanga wa Mwisho.
                   Rais Jakaya Kikwete akiweka Mchanga wa Mwisho.
               Mzee Janguo akiweka Mchangawa Mwisho.
             Meya wa Ilala Mstahiki Jerry Silaa, akiweka Mchanga wa Mwisho.
       Wajukuu nao hawakuwa nyuma kufanikisha Mazishi ya babu yao.


Shukrani kwa Wote Mliofanikisha Mazishi ya Mpendwa baba Yetu Mzee Juma Penza[JP].
MUNGU AILAZE ROHO YA MAREHEMU MAHALI PEMA PEPONI;AMINA.


Rachel-siwa[Mwanapenza]na Timu Yote ya SwahilinaWaswahili;MAJONZINI.




picha kwa hisani ya Michuzi blog,Asante sana.

Ulale kwa Amani baba Mzee Juma Penza!!!!!!!

Mzee wetu mpendwa Umetutoka tukiwa bado tunakuhitaji.
Leo sina mengi ya kusema;
Mungu akulaze mahali pema peponi Amina.

Poleni ndugu zangu wote mliopo nyumbani Tanzania na Wote tuliopo nje ya Tanzania,
Tuungane pamoja kwa wakati huu Mgumu kwetu Mgumu.

wako Rachel-Siwa[Mwanapenza].


Wednesday 12 October 2011

Tamara Sibusisiwe Phiri's birthday Party,Ilivyokuwa,Umewasikia Watoto wa Bondeni/Afrika kusini?Pata Uhondo!!!

HALI YA MTOTO CESILIA NI MBAYA ARUDI BILA KUFANYIWA OPERESHENI.




Mtoto Cecilia wakati akiwaomba wasamalia wema waweze kumsaidia.

Hapa Mtoto Cecilia akitoka Hospital ya Regency Dar akiwa ameshikwa mkono na afisa mmoja wa Channel Ten tayari kwa kuelekea Airport kuanza safari ya kwenda India.

Mtoto Cecilia alitangazwa hivi karibuni na Vituo mbali mbali vya habari akiomba msaada wa kusaidiwa pesa za matibabu ambazo zingeweza kumwezesha kufanyiwa operesheni ya moyo ambao umempelekea mpaka Tumbo lake kuvimba kama unavyoliona.

Taarifa za Cecilia ziliweza kutolewa na Miss Tanzania wa mwaka 2006 Bi .Hoyce Temu pale alipoamua kujitokeza na kumtangaza Cecilia akiomba msaada huo. Wasamaria wema walijitokeza na kumsaidia Cecilia mpaka akaweza kwenda India kwa matibabu, cha kusikitisha sana ni kwamba matibabu yake kwa njia ya operesheni yameshindikana kutokana na moyo wake kwa upande mmoja kuathirika na sumu ambayo madaktari wa India wamesema inasababishwa na Sumu ambayo ipo kwenye Mihogo, sumu hiyo huwaathiri sana watoto wenye umri kama wake.

Kwa hiyo imekuwa ni vigumu kumfanyia operesheni hiyo, wakashauri atumie dawa tu ili kuweza kuitoa sumu hiyo, Mtoto Cecilia mpaka sasa hali yake sio nzuri anawaomba watanzania mumuombee ili aweze kupona na aweze kutimiza azma yake ya kuwa Mwalimu. Watanzania tunashauriwa tukiona hali ambayo ni tofauti kwa watoto wetu tuwawaishe Hospitali mapemakwa uchunguzi tunaweza tukawahepusha na hali kama hii aliyofikia Cecilia.
Habari hii kutoka Kapingaz Blog

Tuesday 11 October 2011

Da'Tamara-Sibusisiwe Atimiza mwaka 1!!!!!!!!!

                    Da'Tamara kama anaota vile!!!!!!
  Duhhhh sasa nimetimiza mwaka, Hawa wazazi sijui watanipeleka Boarding..?
                            Mwenyewe mama Tamara!!
Baba Tamara [kaka Manyanya] naona  kajibebea Tamara wake.


Hongera da'Tamara kwa siku yako hii Muhimu, Mungu akubariki katika yote.
Baba na Mama Tamara; Hongereni  sana na Mungu awe nanyi daima katika malezi ya da'Tamara
na Maisha yenu.


Zaidi kuhusu Tamara na Wazazi wake na menginemengiiiii!!! Ingia http://ninaewapenda.blogspot.co