Swahili na Waswahili

Swahili na Waswahili
Waswahili na Mswahili Rachel Siwa...Pamoja Daima!!

Wednesday, 3 July 2019

Kikombe Cha Asubuhi ; Methali 10...

Shalom,Habari za Asubuhi,Hamjambo,Mmeamkaje?

Tumshukuru Mungu wetu katika yote...

Asante  Mungu wetu kwa wema na fadhili zako kwetu
Asante kwa ulinzi wako kwetu wakati wote
Asante kwa kutuchagua tena na kutupa
kibali cha kuendelea kuiona leo hii
Asante kwa pumzi/uzima,afya na kuwatayari kwa majukumu yetu


Utukuzwe ee Mungu wetu,usifiwe Baba wa Mbinguni

Neema yako yatutosha  Mungu wetu..!

Naye akajibu, “Bwana, mimi sina mtu wa kunipeleka majini wakati yanapotibuliwa. Kila nikijaribu kuingia, mtu mwingine hunitangulia.” Yesu akamwambia, “Inuka, chukua mkeka wako utembee.” Mara huyo mtu akapona, akachukua mkeka wake, akatembea. Jambo hili lilifanyika siku ya Sabato.
Baba wa Mbinguni tunakuja mbele zako tukijinyenyekeza,tukijishusha na kujiachilia mikononi mwako
Mungu wetu tunaomba utusamehe dhambi zetu zote
Baba wa Mbinguni nasi tunaomba utupe neema ya kuweza kuwasamehe wale wote waliotukosea,Usitutie majaribuni Mungu wetu tunaomba utuepushe na yule mwovu na kazi zake zote,Jehovah ututakase miili yetu na akili zetu Baba wa Mbinguni tunaomba utufunike kwa  Damu ya Bwana na Mwokozi wetu Yesu Kristo wa Nazareti,
Yeye aliteseka kwanza ili sisi tupate kupona....

Kwa hiyo baadhi ya Wayahudi wakamwambia huyo mtu aliyeponywa, “Leo ni Sabato, si halali kubeba mkeka wako.” Lakini yeye akawaambia, “Yule mtu aliyeniponya ndiye aliyeniambia: ‘Chukua mkeka wako, utembee.’”
Mungu wetu tunaomba ukabariki kazi za mikono yetu
Baba wa Mbinguni tunaomba ukatupe ubunifu na maarifa 
katika utendaji
Jehovah nasi tukatende sawasawa na mapenzi yako
Baba wa Mbinguni tunaomba ukabariki ridhiki zetu
ziingiazo/zitokazo
Mungu wetu nasi tunaomba ukatupe neema ya kuweza
kuwabariki wenye kuhitaji
Yahweh tusipungukiwe katika mahitaji yetu
Mungu wetu ukatupe kama inavyokupendeza wewe

Jehovah tunayaweka maisha yetu mikononi mwako
Baba wa Mbinguni tunaomba ukabariki nyumba/ndoa zetu,
watoto,wazazi wetu,familia/ndugu na wote wanaotuzunguka
Jehovah tunaomba ulinzi wako kwetu na kwa vyote tunavyo vimiliki
Yahweh tunaomba ukatubariki tuingiapo/tutokapo
Mungu wetu tunaomba ukavibariki vyote tunavyoenda kugusa/kutumia
Baba wa Mbinguni ukavitakase kwa Damu ya Bwana wetu Yesu Kristo
Mungu wetu ukatamalaki na kutuatamia
Baba wa Mbinguni tukawe salama rohoni
Mfalme wa amani amani yako ikatawale katika maisha yetu
Mungu wetu ukatupe macho ya kuona na masikio ya kusikia 
sauti yako na kuitii
Baba wa Mbinguni tunaomba ukatupe neema ya kufuata njia zako
Yahweh tukasimamie Neno lako amri na sheria zako siku zote 
za maisha yetu

Mungu  wetu ukaonekane katika maisha yetu popote tupitapo na ikajulikane kwamba upo 

Neema zako zikawe nasi Nuru yako ikaangaze katika maisha yetu
Ukatufanye barua njema ee Mungu wetu nasi tukasomeke kama
inavyokupendeza wewe
Roho Mtakatifu akatuongoze katika yote na tukawe na kiasi...

Nao wakamwuliza, “Huyo mtu aliyekuambia: ‘Chukua mkeka wako, utembee,’ ni nani?” Lakini yeye hakumjua huyo mtu aliyemponya, maana Yesu alikuwa amekwisha ondoka mahali hapo, kwani palikuwa na umati mkubwa wa watu. Basi, baadaye Yesu alimkuta huyo aliyeponywa hekaluni, akamwambia, “Sasa umepona; usitende dhambi tena, usije ukapatwa na jambo baya zaidi.” Huyo mtu akaenda, akawaambia viongozi wa Wayahudi kwamba Yesu ndiye aliyemponya.
Tazama wenye shida/tabu,Mungu wetu tunaomba
 ukawaguse kila mmoja na mahitaji yake
Baba wa Mbinguni tunaomba ukawasamehe pale walipokwenda
kinyume nawe
Mungu wetu ukawape neema ya kujiombea,macho ya rohoni,masikio yakusikia sauti yako,wakafuate njia zako nazo zikawaweke huru
Mungu wetu tunaomba ukasikie kulia kwao
Baba wa Mbinguni tunomba ukawafute machozi yao
Nuru yako ikaangaze katika maisha yao
Mungu wetu tunaomba ukawatendee sawasawa na mapenzi yako
Kwakuwa Ufalme ni wako Nguvu na Utukufu hata Milele
Amina....!!!


Wapendwa katika Kristo Yesu asanteni sana
kwakuwanami/kunisoma

Mungu Baba aendelee kuwabariki na kuwatendea
kama inavyompendeza yeye
Amani ya Bwana wetu Yesu Kristo na upendo wa Mungu Baba
ukae nanyi daima....

Nawapenda.

Methali za Solomoni
1Hizi ni methali za Solomoni:
Mtoto mwenye hekima ni furaha ya baba yake;
lakini mtoto mpumbavu ni huzuni ya mama yake.
2Mali iliyopatikana kwa njia mbaya haifai,
lakini uadilifu huokoa mtu kutoka kifoni.
3Mwenyezi-Mungu hawaachi waadilifu wapate njaa,
lakini huzipinga tamaa za waovu.
4Uvivu husababisha umaskini,
lakini mkono wa mtu wa bidii hutajirisha.
5Mwenye busara hukusanya wakati wa mavuno,
kulala wakati wa kuvuna ni aibu.
6Mwadilifu hujiletea baraka yeye mwenyewe,
lakini kinywa cha mwovu kimesongwa na ukatili.
7Waadilifu hukumbukwa kwa baraka,
lakini waovu watasahaulika kabisa.
8Mwenye hekima moyoni hutii amri,
lakini mpumbavu aropokaye ataangamia.
9Aishiye kwa unyofu huishi salama,
apotoshaye maisha yake atagunduliwa.
10Akonyezaye kwa nia mbaya huzusha taabu,
lakini aonyaye kwa ujasiri huleta amani.
11Kinywa cha mwadilifu ni chemchemi ya uhai,
lakini kinywa cha mwovu kimesongwa na ukatili.
12 Taz Yak 5:20; 1Pet 4:8 Chuki huzusha ugomvi,
lakini upendo hufunika makosa yote.
13Kinywani mwa mwenye ufahamu mna hekima,
lakini wasio na akili watachapwa viboko mgongoni.
14Wenye hekima huhifadhi maarifa,
lakini kuropoka kwa mpumbavu huleta maangamizi haraka.
15Mali ya tajiri ndio ngome yake,
umaskini wa maskini humletea maangamizi.
16Tuzo la mtu mwema ni uhai,
lakini mwovu huishia katika dhambi.
17Anayekubali maonyo anaelekea kwenye uhai,
lakini anayekataa kuonywa amepotoka.
18Amchukiaye mwingine kwa siri ni mnafiki,
anayemsingizia mtu ni mpumbavu.
19Penye maneno mengi hapakosekani makosa,
lakini aneyeuzuia ulimi wake ana busara.
20Maneno ya mwadilifu ni kama fedha bora;
akili ya mtu mwovu haina thamani yoyote.
21Maneno ya mwadilifu huwafaa watu wengi,
lakini wapumbavu hufa kwa kukosa akili.
22Baraka za Mwenyezi-Mungu ndizo ziletazo fanaka,
juhudi za mtu haziongezi hapo chochote.10:22 huzuni … nazo: Au na haongezi hapo huzuni.
23Kwa mpumbavu kutenda maovu ni kama mchezo;
lakini watu wenye busara hufurahia hekima.
24Anachoogopa mtu mwovu ndicho kitakachompata,
lakini anachotamani mwadilifu ndicho atakachopewa.
25Kimbunga hupita na mwovu hutoweka,
lakini mwadilifu huimarishwa milele.
26Kama ilivyo siki kwa meno au moshi machoni,
ndivyo alivyo mvivu kwa bwana wake.
27Kumcha Mwenyezi-Mungu hurefusha maisha,
lakini miaka ya waovu itakuwa mifupi.
28Tumaini la mwadilifu huishia kwenye furaha,
lakini tazamio la mwovu huishia patupu.
29Mwenyezi-Mungu ni ngome ya wanyofu,
lakini watendao maovu atawaangamiza.
30Waadilifu kamwe hawataondolewa nchini,
lakini waovu hawatakaa katika nchi.
31Kinywa cha mwadilifu hutoa mambo ya hekima,
lakini ulimi wa mtu mbaya utakatiliwa mbali.
32Midomo ya waadilifu hujua yanayokubalika,
lakini vinywa vya waovu husema tu maovu.

Methali10;1-32

Biblia Habari Njema kwa Watu Wote(BHN)

"Swahili Na Waswahili"Mbarikiwe.

Tuesday, 2 July 2019

Kikombe Cha Asubuhi ; Methali 9...

Shalom,Habari za Asubuhi,Hamjambo,Mmeamkaje?

Tumshukuru Mungu katika yote....

Mungu wetu Baba yetu,Muumba wetu Muumba wa Mbingu na Nchi
Muumba wa vyote vilivyomo vinavyoonekana na visivyoonekana
Mungu wa walio hai,Mungu  mwenye huruma,Mungu wa upendo
Mungu wa Abrahamu,Isaka na Yakobo...
Asante kwa wema na fadhili zako kwetu
Asante kwa ulinzi wako kwetu wakati wote
Asante kwa kutuchagua tena na kutupa
kibali cha kuendelea kuiona leo hii
Asante kwa pumzi/uzima,afya na kuwatayari kwa majukumu yetu

Neema yako yatutosha ee Mungu wetu....!!

Baada ya hayo kulikuwa na sikukuu ya Wayahudi, naye Yesu akaenda Yerusalemu. Huko Yerusalemu, karibu na mlango uitwao Mlango wa Kondoo, kulikuwa na bwawa la maji liitwalo kwa Kiebrania Bethzatha, ambalo lilikuwa na baraza tano zenye matao.
Baba wa Mbinguni tunakuja mbele zako tukijinyenyekeza,tukijishusha na kujiachilia mikononi mwako
Mungu wetu tunaomba utusamehe dhambi zetu zote 
Baba wa Mbinguni nasi tunaomba ukatupe neema
ya kuweza kuwasamehe wale wote waliotukosea
Usitutie majaribuni Mungu wetu tunaomba utuepushe
na yule mwovu na kazi zake zote
Jehovah ututakase miili yetu na akili zetu
Baba wa Mbinguni tunaomba utufunike kwa Damu
ya Bwana na Mwokozi wetu Yesu Kristo wa Nazareti
yeye aliteseka kwanza ili sisi tupate kupona....

Humo barazani mlikuwa na wagonjwa wengi wamekaa: Vipofu, viwete na waliopooza. [Walikuwa wakingojea maji yatibuliwe, maana mara kwa mara malaika alishuka majini nyakati fulani na kuyatibua. Mtu yeyote aliyekuwa wa kwanza kuingia majini baada ya maji kutibuliwa, alipona ugonjwa wowote aliokuwa nao.]
Mungu wetu tunaomba ukabariki kazi za mikono yetu
Baba wa Mbinguni tunaomba ukatupe ubunifu na maarifa katika utendaji
Jehovah nasi tukatende sawasawa na mapenzi yako
Yahweh tunaomba ukabariki ridhiki zetu ziingiazo/zitokazo
Mungu wetu nasi tunaomna ukatupe neema ya kuweza kuwabariki wenye kuhitaji
Tusipungukiwe katika mahitaji yetu
Baba wa Mbinguni tunaomba ukatupe kama inavyokupendeza wewe...

Yahweh tunayaweka maisha yetu mikononi mwako
Mungu wetu tunaomba ukabariki nyumba/ndoa zetu,
Jehovah tunaomba ulinzi wako kwetu na kwa vyote tunavyovimiliki
Yahweh tunaomba ukatubariki tuingiapo/tutokapo
Mungu wetu tunaomba ukavibariki vyote tunavyoenda kugusa/kutumia
Baba wa Mbinguni ukavitakase kwa Damu ya Bwana wetu Yesu Kristo
Mungu wetu ukatamalaki na kutuatamia
Baba wa Mbinguni tukawe salama rohoni
Yahwe ukatupe akili ya kutambua mema na mabaya
Mfalme wa amani amani yako ikatawale katika maisha yetu
Mungu wetu ukatupe macho ya kuona,masikio ya kusikia sauti yako na kuitii..
Baba wa Mbinguni  tunaomba ukatupe neema ya kufuata
njia zako,tukasimamie Neno lako,amri na sheria zako
siku zote za maisha yetu...
Ukatuguse kwa mkono wako wenye nguvu,ukatufanye chombo chema
ee Mungu wetu nasi tukatumike kama inavyokupendeza wewe
Roho Mtakatifu akatuongoze katika yote na tukawe na kiasi....

Basi, hapo palikuwa na mtu mmoja aliyekuwa mgonjwa kwa muda wa miaka thelathini na minane. Naye alipomwona huyo mtu amelala hapo na kujua kwamba alikuwa amekaa hapo kwa muda mrefu, akamwuliza, “Je, wataka kupona?”
Tazama watoto wako wenye shida/tabu,wote wanaopitia magumu/majaribu mbalimbali
Mungu wetu tunaomba ukawaguse kwa mkono wako wenye nguvu
kila mmoja na mahitaji yake
Mungu wetu tunaomba ukawasamehe pale walipo kwenda kinyume nawe
Yahweh tunaomba ukawape neema ya kuweza kujiombea,kufuata njia zako nazo zikawaweke huru...
Baba wa Mbinguni tunayaweka haya yote mikononi mwako
Kwakuwa Ufalme ni wako Nguvu na Utukufu hata Milele...
Amina...!!


Asanteni sana wapendwa katika Kristo Yesu kwakuwa nami,Baba wa Mbinguni aendelee kuwatendea sawasawa na mapenzi yake...
Nawapenda.

Hekima na upumbavu
1Hekima amejenga nyumba yake,
nyumba yenye nguzo saba.
2Amechinja wanyama wa karamu,
divai yake ameitayarisha,
ametandika meza yake.
3Amewatuma watumishi wake wa kike mjini,
waite watu kutoka kwenye vilele vya miinuko:
4“Yeyote aliye mjinga na aje hapa!”
Na yeyote aliye mpumbavu humwambia:
5“Njoo ukale chakula,
na unywe divai niliyotengeneza.
6Achana na ujinga upate kuishi;
fuata njia ya akili.”
7Anayemkosoa mwenye dharau hupata matusi,
amkaripiaye mwovu huishia kwa kuumizwa.
8Usimwonye mwenye dharau maana atakuchukia;
mwonye mwenye hekima naye atakupenda.
9Mfunze mwenye hekima naye atazidi kuwa na hekima;
mfundishe mwadilifu naye atazidi kuelimika.
10 Taz Yobu 28:28; Zab 111:10; Meth 1:7 Kumcha Mwenyezi-Mungu ni msingi wa hekima;
na kumjua yule Mtakatifu ni kupata akili.
11Kwa msaada wangu mimi Hekima siku zako zitaongezwa;
utaongezewa miaka mingi maishani mwako.
12Kama una hekima, itakufaa wewe mwenyewe;
kama ukiidharau, mwenyewe utapata hasara.
13Mwanamke mpumbavu ana kelele,
hajui kitu wala hana haya.9:13 aya 13 makala ya Kiebrania si dhahiri.
14Hukaa kitako mlangoni mwa nyumba yake,
huweka kiti chake mahali pa juu mjini,
15na kuwaita watu wapitao njiani,
watu wanaokwenda kwenye shughuli zao:
16“Yeyote aliye mjinga na aje hapa!”
Na yeyote aliye mpumbavu humwambia:
17“Maji ya wizi ni matamu sana;
mkate unaoliwa kwa siri ni mzuri sana.”
18Lakini mjinga hajui kwamba humo mna wafu,
wageni wa mwanamke huyo wamo chini Kuzimu.

Methali9;1-18

Biblia Habari Njema kwa Watu Wote(BHN)

"Swahili Na Waswahili"Mbarikiwe.

Monday, 1 July 2019

Kikombe Cha Asubuhi ; Methali 8...



Shalom,Habari za Asubuhi,Hamjambo,Mmeamkaje?
Haleluyah ni siku/wiki/mwezi mwingine tena Mungu wetu ametuchagua

na kutupa kibali cha kuendelea kuiona leo hii
Si kwamba sisi tumetenda mema sana wala si kwa nguvu zetu
si kwa utashi wetu wala si kwa akili zetu si kwamba sisi
ni wazuri mno si kwa uwezo wetu sisi kuwa hivi tulivyo leo hii
Ni kwa rehema/neema zake ni kwa mapenzi yake Mungu wetu....

Tumshukuru Mungu wetu katika yote...

Asante Mungu wetu kwa wema na fadhili zako kwetu
Asante kwa ulinzi wako kwetu wakati wote
Asante kwa pumzi/uzima,afya na kuwa tayari kwa majukumu yetu
Sifa na Utukufu tunakurudshia Mungu wetu....!!

Basi, tuzingatie kwa makini imani tunayoiungama. Maana tunaye Kuhani Mkuu aliyeingia mpaka mbinguni; Yesu, Mwana wa Mungu.
Tazama jana imepita ee Mungu wetu leo ni siku mpya na kesho ni siku nyingine Jehovah tunakuja mbele zako tukijinyenyekeza,tukijishusha na kujiachilia mikononi mwako
 Mungu wetu tunaomba utusamehe dhambi zetu zote tulizozifanya kwakuwaza,kwakunena,kwakutenda,kwakujua/kutojua
Baba wa Mbinguni nasi tunaomba utupe neema ya kuweza kuwasamehe wale wote waliotukosea
Jehovah usitutie majaribu Mungu wetu tunaomba utuepushe na yule mwovu na kazi zake zote
Yahweh tunaomba ututakase miili yetu na akili zetu
Baba wa Mbinguni utufunike kwa Damu ya Bwana na Mwokozi wetu Yesu Kristo wa Nazareti
yeye aliteseka kwanza ili sisi tupate kupona
Kwakupigwa kwake sisi tumepata kupona...
Huyu Kuhani Mkuu wetu anaelewa kabisa unyonge wetu; yeye mwenyewe alijaribiwa kama sisi kwa kila namna lakini hakutenda dhambi.
Yahweh tunaomba ukabariki kazi za mikono yetu
Baba wa Mbinguni tunaomba ukatupe ubunifu na maarifa 
katika utendaji
Jehovah nasi tukatende sawasawa na mapenzi yako
Baba wa Mbinguni tunaomba ukabariki ridhiki zetu
ziingiazo/zitokazo
Mungu wetu nasi tunaomba ukatupe neema ya kuweza
kuwabariki wenye kuhitaji
Yahweh tusipungukiwe katika mahitaji yetu
Mungu wetu ukatupe kama inavyokupendeza wewe

Baba wa Mbinguni tunayaweka maisha yetu mikononi mwako
Mungu wetu tunaomba ukabariki nyumba/ndoa zetu,
watoto,wazazi wetu,familia/ndugu na wote wanaotuzunguka
Jehovah tunaomba ulinzi wako kwetu na kwa vyote tunavyo vimiliki
Yahweh tunaomba ukatubariki tuingiapo/tutokapo
Mungu wetu tunaomba ukavibariki vyote tunavyoenda kugusa/kutumia
Baba wa Mbinguni ukavitakase kwa Damu ya Bwana wetu Yesu Kristo
Mungu wetu ukatamalaki na kutuatamia
Baba wa Mbinguni tukawe salama rohoni
Mfalme wa amani amani yako ikatawale katika maisha yetu
Mungu wetu ukatupe macho ya kuona na masikio ya kusikia 
sauti yako na kuitii
Baba wa Mbinguni tunaomba ukatupe neema ya kufuata njia zako
Yahweh tukasimamie Neno lako amri na sheria zako siku zote 
za maisha yetu
Mungu wetu ukaonekane katika maisha yetu
Neema zako zikawe nasi Nuru yako ikaangaze katika maisha yetu
ukatuguse kwa mkono wako wenye nguvu
Ukatufanye chombo chema ee Mungu wetu nasi tukatumike kama
inavyokupendeza wewe
Roho Mtakatifu akatuongoze katika yote na tukawe na kiasi...

Basi, na tukikaribie bila hofu kiti cha enzi cha Mungu mwenye neema, tupokee huruma na neema ya kutusaidia wakati wa shida.
Mungu wetu tunawaweka mikononi mwako wenye shida/tabu,wote wanaopotia magumu/majaribu mbalimbali
Mungu wetu tunaomba ukawaguse kwa mkono wako wenye nguvu
 kila mmoja na mahitaji yake 
Mungu wetu tunaomba ukawasamehe pale walipokwenda kinyume nawe
Baba wa Mbinguni ukawape neema ya kujiombea,kufuata njia zako
wakasimaie Neno lako nalo likaweke huru
Mungu wetu tunaomba ukasikie kuomba kwetu
Mungu wetu ukawatendee sawasawa na mapenzi yako
Kwakuwa Ufalme ni wako Nguvu na Utukufu hata Milele
Amina...!!

Asanteni sana wapendwa katika Kristo Yesu kwakuwa nami
Mungu Baba aendelee kuwabariki na kuwatendea 
kama inavyompendeza yeye....
Nawapenda.

Wito wa Hekima
1 Taz Meth 1:20-21 Sikilizeni! Hekima anaita!
Busara anapaza sauti yake!
2Juu penye mwinuko karibu na njia,
katika njia panda ndipo alipojiweka.
3Karibu na malango ya kuingilia mjini,
mahali wanapoingia watu anaita kwa sauti:
4“Enyi watu wote, nawaita nyinyi!
Wito wangu ni kwa ajili ya binadamu.
5Enyi wajinga, jifunzeni kuwa na akili;
sikilizeni kwa makini enyi wapumbavu.
6Sikilizeni maana nitakachosema ni jambo muhimu;
midomoni mwangu mtatoka mambo ya adili.
7Kinywa changu kitatamka kweli tupu;
uovu ni chukizo midomoni mwangu.
8Kinywa changu kitatamka maneno ya kweli,
udanganyifu ni haramu midomoni mwangu.
9Kwa mtu mwelewa kila kitu ni wazi,
kwa mwenye maarifa yote ni sawa.
10Chagua mafundisho yangu badala ya fedha;
na maarifa badala ya dhahabu safi.
11“Mimi Hekima nina thamani kuliko johari;
chochote unachotamani hakiwezi kulingana nami.
12Mimi Hekima ninao ujuzi;
ninayo maarifa na busara.
13Kumcha Mwenyezi-Mungu ni kuchukia uovu.
Nachukia kiburi, majivuno na maisha mabaya;
nachukia na lugha mbaya.
14Nina uwezo wa kushauri na nina hekima.
Ninao ujuzi na nina nguvu.
15Kwa msaada wangu wafalme hutawala,
watawala huamua yaliyo ya haki.
16Kwa msaada wangu viongozi hutawala,
wakuu na watawala halali.8:16 tafsiri nyingine: Wakuu, mahakimu wa dunia.
17Nawapenda wale wanaonipenda;
wanaonitafuta kwa bidii hunipata.
18Utajiri na heshima viko kwangu,
mali ya kudumu na fanaka.
19Matunda yangu ni mazuri kuliko dhahabu safi,
faida yangu yashinda ile ya fedha bora.
20Natembea katika njia ya uadilifu;
ninafuata njia za haki.
21Mimi huwatajirisha wanaonipenda,
huzijaza tele hazina zao wanipendao.
22 Taz Ufu 3:14 “Mwenyezi-Mungu aliniumba mwanzoni mwa kazi yake,8:22 kazi yake: Makala ya Kiebrania: Njia yake.
zama za zama kabla ya kuwako kitu chochote.
23Nilifanywa mwanzoni mwa nyakati,
nilikuwako kabla ya dunia kuanza.
24Nilizaliwa kabla ya vilindi vya bahari,
kabla ya chemchemi zibubujikazo maji.
25Kabla ya milima haijaumbwa,
na vilima kusimamishwa mahali pake,
mimi nilikuwako tayari.
26Kabla Mungu hajaumba dunia na mashamba yake,
wala chembe za kwanza za mavumbi ya dunia.
27Nilikuwako wakati alipoziweka mbingu,
wakati alipopiga duara juu ya bahari;
28wakati alipoimarisha mawingu mbinguni,
alipozifanya imara chemchemi za bahari;
29wakati alipoiwekea bahari mpaka wake,
maji yake yasije yakavunja amri yake;
wakati alipoiweka misingi ya dunia.
30Nilikuwa pamoja naye kama fundi stadi,8:30 fundi stadi: Au Mtoto mdogo.
nilikuwa furaha yake kila siku,
nikishangilia mbele yake daima,
31nikifurahia dunia na wakazi wake,
na kupendezwa kuwa pamoja na wanadamu.
32“Sasa basi wanangu, nisikilizeni:
Heri wale wanaofuata njia zangu.
33Sikilizeni mafunzo mpate hekima,
wala msiyakatae.
34Heri mtu anayenisikiliza,
anayekaa kila siku mlangoni pangu,
anayekesha karibu na milango yangu.
35Anayenipata mimi amepata uhai,
amepata upendeleo kwa Mwenyezi-Mungu.
36Asiyenipata anajidhuru mwenyewe;
wote wanaonichukia wanapenda kifo.”


Methali8;1-36

Biblia Habari Njema kwa Watu Wote(BHN)

"Swahili Na Waswahili"Mbarikiwe.

Friday, 28 June 2019

Kikombe Cha Asubuhi ; Methali 7...

Shalom,Habari za Asubuhi,Hamjambo,Mmeamkaje?

Tumshukuru Mungu wetu katika yote...

Asante  Mungu wetu kwa wema na fadhili zako kwetu
Asante kwa ulinzi wako kwetu wakati wote
Asante kwa kutuchagua tena na kutupa
kibali cha kuendelea kuiona leo hii
Asante kwa pumzi/uzima,afya na kuwatayari kwa majukumu yetu


Utukuzwe ee Mungu wetu,usifiwe Baba wa Mbinguni

Neema yako yatutosha  Mungu wetu..!

Mungu aliweka siku nyingine ambayo inaitwa “Leo,” akasema baadaye kwa njia ya Daudi maneno yaliyokwisha tajwa: “Kama mkisikia sauti ya Mungu leo, msiwe wakaidi.”
Baba wa Mbinguni tunakuja mbele zako tukijinyenyekeza,tukijishusha na kujiachilia mikononi mwako
Mungu wetu tunaomba utusamehe dhambi zetu zote
Baba wa Mbinguni nasi tunaomba utupe neema ya kuweza kuwasamehe wale wote waliotukosea,Usitutie majaribuni Mungu wetu tunaomba utuepushe na yule mwovu na kazi zake zote,Jehovah ututakase miili yetu na akili zetu Baba wa Mbinguni tunaomba utufunike kwa  Damu ya Bwana na Mwokozi wetu Yesu Kristo wa Nazareti,
Yeye aliteseka kwanza ili sisi tupate kupona....

Kama Yoshua angekuwa amewapa watu hao hilo pumziko, Mungu hangalisema baadaye juu ya siku nyingine. Kwa hiyo, basi, bado kuna kupumzika kwa watu wa Mungu. Maana, kila aingiaye mahali pa pumziko la Mungu atapumzika kutoka katika kazi yake kama vile pia Mungu alivyopumzika kutoka kazi yake. Basi, tujitahidi kuingia katika pumziko hilo, ili asiwepo yeyote miongoni mwetu atakayekataa kutii kama walivyofanya wao.
Mungu wetu tunaomba ukabariki kazi za mikono yetu
Baba wa Mbinguni tunaomba ukatupe ubunifu na maarifa 
katika utendaji
Jehovah nasi tukatende sawasawa na mapenzi yako
Baba wa Mbinguni tunaomba ukabariki ridhiki zetu
ziingiazo/zitokazo
Mungu wetu nasi tunaomba ukatupe neema ya kuweza
kuwabariki wenye kuhitaji
Yahweh tusipungukiwe katika mahitaji yetu
Mungu wetu ukatupe kama inavyokupendeza wewe



Jehovah tunayaweka maisha yetu mikononi mwako
Baba wa Mbinguni tunaomba ukabariki nyumba/ndoa zetu,
watoto,wazazi wetu,familia/ndugu na wote wanaotuzunguka
Jehovah tunaomba ulinzi wako kwetu na kwa vyote tunavyo vimiliki
Yahweh tunaomba ukatubariki tuingiapo/tutokapo
Mungu wetu tunaomba ukavibariki vyote tunavyoenda kugusa/kutumia
Baba wa Mbinguni ukavitakase kwa Damu ya Bwana wetu Yesu Kristo
Mungu wetu ukatamalaki na kutuatamia
Baba wa Mbinguni tukawe salama rohoni
Mfalme wa amani amani yako ikatawale katika maisha yetu
Mungu wetu ukatupe macho ya kuona na masikio ya kusikia 
sauti yako na kuitii
Baba wa Mbinguni tunaomba ukatupe neema ya kufuata njia zako
Yahweh tukasimamie Neno lako amri na sheria zako siku zote 
za maisha yetu

Mungu  wetu ukaonekane katika maisha yetu popote tupitapo na ikajulikane kwamba upo 

Neema zako zikawe nasi Nuru yako ikaangaze katika maisha yetu
Ukatufanye barua njema ee Mungu wetu nasi tukasomeke kama
inavyokupendeza wewe
Roho Mtakatifu akatuongoze katika yote na tukawe na kiasi...

Neno la Mungu ni hai na lina nguvu; ni kali kuliko upanga wenye makali kuwili. Hukata kabisa mpaka mahali ambapo moyo na roho hukutana, mpaka pale vikutanapo viungo vya mwili na uboho. Neno hilo huchambua nia na fikira za mioyo ya watu. Hakuna kiumbe chochote kilichofichika mbele ya Mungu; kila kitu kimefunuliwa wazi mbele ya macho yake yeye ambaye kwake tutapaswa kutoa hoja ya matendo yetu.
Tazama wenye shida/tabu,Mungu wetu tunaomba
 ukawaguse kila mmoja na mahitaji yake
Baba wa Mbinguni tunaomba ukawasamehe pale walipokwenda
kinyume nawe
Mungu wetu ukawape neema ya kujiombea,macho ya rohoni,masikio yakusikia sauti yako,wakafuate njia zako nazo zikawaweke huru
Mungu wetu tunaomba ukasikie kulia kwao
Baba wa Mbinguni tunomba ukawafute machozi yao
Nuru yako ikaangaze katika maisha yao
Mungu wetu tunaomba ukawatendee sawasawa na mapenzi yako
Kwakuwa Ufalme ni wako Nguvu na Utukufu hata Milele
Amina....!!!


Wapendwa katika Kristo Yesu asanteni sana
kwakuwanami/kunisoma

Mungu Baba aendelee kuwabariki na kuwatendea
kama inavyompendeza yeye
Amani ya Bwana wetu Yesu Kristo na upendo wa Mungu Baba
ukae nanyi daima....
Nawapenda.

1Mwanangu, yashike maneno yangu,
zihifadhi kwako amri zangu.
2Zifuate amri zangu nawe utaishi;
yalinde mafundisho yangu kama mboni ya jicho lako.
3Yafunge vidoleni mwako;
yaandike moyoni mwako.
4Iambie Hekima: “Wewe ni dada yangu”,
na Busara “Wewe ni rafiki yangu”.
5Vitakulinda mbali na mwanamke mbaya,
vitakuepusha na maneno matamu ya mwanamke mgeni.

Mwanamke mwasherati
6Siku moja dirishani mwa nyumba yangu,
nilichungulia nje kupitia viunzi vya dirisha,
7nikawaona vijana wengi wajinga,
na mmoja hasa aliyekuwa mpumbavu.
8Huyo alikuwa akitembea kwenye barabara ile,
karibu na kona alikoishi mwanamke fulani.
Basi akashika njia iendayo nyumbani kwa mwanamke huyo.
9Ilikuwa yapata wakati wa jioni,
giza na usiku vilikuwa vimeanza kuingia.
10Punde kijana akakutana na huyo mwanamke;
amevalia kama malaya, ana mipango yake.
11Alikuwa mwanamke wa makelele na mkaidi;
miguu yake haitulii nyumbani:
12Mara barabarani, mara sokoni,
katika kila kona ya njia hakosekani akivizia.
13Alimkumbatia kijana huyo na kumbusu,
na kwa maneno matamu, akamwambia:
14“Ilinilazimu kutoa tambiko zangu;
leo hii nimekamilisha nadhiri yangu.
15Ndio maana nimetoka ili nikulaki,
nimekutafuta kwa hamu nikakupata.
16Nimetandika kitanda changu vizuri,
kwa shuka za rangi za kitani kutoka Misri.
17Nimekitia manukato, manemane, udi na mdalasini.
18Njoo tulale pamoja mpaka asubuhi;
njoo tujifurahishe kwa mahaba.
19Mume wangu hayumo nyumbani,
amekwenda safari ya mbali.
20Amechukua bunda la fedha;
hatarejea nyumbani karibuni.”
21Alimshawishi kwa maneno mengi ya kubembeleza;
kijana akashawishika kwa maneno yake matamu.
22Hapo akamfuata huyo mwanamke moja kwa moja,
kama ng'ombe aendaye machinjioni,
kama paa arukiaye mtegoni.
23Hakutambua kwamba hiyo itamgharimu maisha yake,
mpaka alipojikuta amekuwa kama amechomwa mshale moyoni,
amekuwa kama ndege aliyenaswa wavuni.
24Sasa wanangu, nisikilizeni;
yategeeni sikio maneno ya kinywa changu.
25Msikubali kuongozwa na mwanamke kama huyo,
wala msipitepite katika mapito yake.
26Maana amewaangusha wanaume wengi;
ni wengi mno hao aliowachinja.
27Nyumba yake ni njia ya kwenda kuzimu,
ni mahali pa kuteremkia mautini.

Methali7;1-27

Biblia Habari Njema kwa Watu Wote(BHN)

"Swahili Na Waswahili"Mbarikiwe.