Tuesday, 3 April 2012
NDG. OMARY MJENGA MWAKILISHI WA UNOPS NCHINI SIERA LEONE AMALIZA ZIARA YAKE NCHINI.
Ndg. Omary Mjenga akipiga picha ya kumbukumbu wakati alipokwenda kumtembelea na kumuaga Rais Jakaya Kikwete jana Ikulu.
Hapa ndugu Mjenga akipiga picha na Naibu Waziri wa Jinsia, Watoto na maendeleo ya jamii, wakati alipokwenda kumtembelea.
Baada ya kutoka kuonana na Viongozi hao alishiriki Dinner Party na Wanafunzi wenzake aliosoma nao Shule ya Sekondari Songea Boys ndani ya viunga vya Rose Garden akiwemo na Naibu Waziri wa Elimu na Ufundi Mh. Philipo Mulugo.
Picha zaidi mtazipata baadae za tukio hili la kihistoria, ambalo kwa mara ya kwanza lilifanyika katika Pub ya KAPINGAZ Pub wakati huo tukimpongeza Naibu Waziri Mh. Mulugo kwa kuteuliwa.
Wana BOX 2 (Wana Luhila) walimpendekeza Ndg. Henry O. Kapinga kuwa Mwenyekiti wa Jumuiya hiyo mpaka pale tutakapo itisha uchaguzi Rasmi.
Omary Mjenga anaondoka leo kurudi Siera Leone tayari kwa kuendelea na kazi zake za UNOPS.
Habari kutoka http://kapingaz.blogspot.co.uk/
Ahsante sana.
Habari kutoka http://kapingaz.blogspot.co.uk/
Ahsante sana.
Sunday, 1 April 2012
Saturday, 31 March 2012
Chaguo la Mswahili Leo,mambo ya Taarab-Utalijua Jiji!
Friday, 30 March 2012
Thursday, 29 March 2012
MAZISHI YA MAREHEMU DENIS OSWALD KAPINGA
Ndg. Joseph Oswald Kapinga
Ndugu Joseph Kapinga pichani hapo juu anapenda kuwajulisha ndugu, jamaa na marafiki kuwa Ratiba ya mazishi ya mpendwa mdogo wetu Denis O. Kapinga yatafanyika leo Tarehe 29/03/2012 katika makaburi ya Sinza karibu na ukumbi wa mwika.
Ratiba itakuwa kama ifuatavyo:
Mwili wa marehemu utafika Nyumbani maeneo ya Sinza karibu na New White Inn Bar bara bara ya Sinza uzuri mnamo saa 6.00 Mchana kutoka Hospitali ya Mwananyamala.
Mwili utaagwa nyumbani saa 7.00 Mchana na baadae utapelekwa kanisa la Roman Catholic Sinza kwa Ibada.
Baada ya hapo Saa 8.30 Mchana mwili wa marehemu utapelekwa Makaburi ya Sinza kwenye nyumba yake ya milele.
"BWANA ALITOA NA BWANA
Poleni sana Familia ya Kapinga.
Swahili na Waswahili tunaungana nanyi katika wakati huu mgumu kwenu.
Mungu awatie Nguvu.
Ulale kwa Amani kaka Denis.O.Kapinga.
Poleni sana Familia ya Kapinga.
Swahili na Waswahili tunaungana nanyi katika wakati huu mgumu kwenu.
Mungu awatie Nguvu.
Ulale kwa Amani kaka Denis.O.Kapinga.
Tuesday, 27 March 2012
Jikoni Leo-Ni kwa Mama Mwakitalu!!!Pata na Burudani ya Ngoma!!!!![Mwanamke jiko au Mwaume Jiko?]
![]() |
| Da'Masika/mama Mwakitalu |
![]() |
| Mboga za Majani Mchanganyiko,Majani ya Kunde na Majani ya Maboga |
![]() |
| Mchuzi wa Samaki Umeungwa/wekwa Nazi na nyanyachungu |
Maandaziiiiii na hapo chini ni Mahindi ya Kuchemsha.
Kwani Utamu/Radha ya chakula wewe unaweza kupendezwa nacho na mwingine asipendezwe nacho.
Jee Kazi/Ujuzi wa Kupika ni kwa Wanawake tuu?Kwani mara nyingi utasikia Mwanamke jiko na si Mwanaume Jiko,Hasa kwa Maisha ya Leo,
kwa Maisha ya Zamani wengi wao Mama/Dada kazi yao kubwa ni Upishi na Baba wengi ndiyo walikuwa wanafanya Kazi hasa Mijini, Kwa Vijijini Woote BABA na MAMA Wanaenda shambani lakini Kupika ni MAMA.Jee Leo Tunaweza Thubutu kusema MWANAUME JIKO? AU TUTAKUA TUMEWADHALILISHA?Kwani wapo Wanakarangiza haswaaaa kutushinda au Hamjakutana nao?.
Karibuni Waumgwana kwa Mawazo na Kuelimisha na Kwa upendo.
Subscribe to:
Comments (Atom)












