Swahili na Waswahili

Swahili na Waswahili
Waswahili na Mswahili Rachel Siwa...Pamoja Daima!!

Wednesday 7 June 2017

Kikombe Cha Asubuhi;Mambo Ya Walawi..9...



Shalom,Habari za Asubuhi,Hamjambo,Mmeamkaje Wapendwa/Waungwana?

Tumshukuru Mungu wetu katika yote...
Mtakatifu..!Mtakatifu..!Mtakatifu.! Baba wambinguni Tunakushukuru na kukusifu..
Asante kwa wema na fadhili zako,
Asante kwa ulinzi wako wakati wote na kutuamsha salama..

Asante kwa kutuchagua na kutupa kibali cha kuendelea kuiona leo hii.
Tunakuja mbele zako Mfamle wa Amani tukijinyenyekeza,tukijishusha na kujiachilia mokononi mwako Mungu wetu..
Tunaomba utusamehe pale tulipokwenda kinyume nawe Mungu wetu....kwakuwaza,kwakunena,kwakutenda,kwakujua/kutojua..Mfalme wa Amani tunaomba nasi utupe neema ya kuweza kuwasamehe waliotukosea..
Utuepushe katika majaribu,Utuokoe na yule mwovu na kazi zake Baba wa Mbinguni..
Ututakase na kutufunika kwa Damu ya mwanao mpendwa Bwana na mwokozi wetu Yesu Kristo wa Nazareti yeye aliteseka ili sisi tupate kupona..

Roho Mtakatifu akatuongoze katika yote na tukawe na kiasi..
Utupe moyo wenye Hekima,Busara,Amani ya moyo,Upendo wa kweli,kuchukuliana/kuvumiliana,kusameheana na Upole Kiasi..
Tupate kujitambua/kutambua..
Tukawe chombo chema na tukatumike sawasawa na mapenzi yako..
Baba wa Mbinguni tunaiweka siku hii mikononi mwako,Ukatubariki,ukatamalaki maishani mwetu na ukatuatamie..
Ikawe siku njema na yenye kukupendeza wewe..
Ukabariki Kazi zetu,Biashara,Masomo,vilaji/vinywaji,kuingia/kutoka kwetu,vyombo vya usafiri na tutembeapo hatua zetu ziwe nawe Jehovah..
Ukabariki ridhiki zetu ziingiazo/zitokazo nasi ukatupe neema ya kuwabariki wenye kuhitaji..
Tazama wenyeshida/tabu,wanaopitia magumu/majarubu mbalimbali,waliokatika vifungo mbalimbali,wagonjwa,wafiwa ukawe mfariji wao..Baba wa Mbinguni tunaomba ukawaguse na mkono wako wenye nguvu,ukawaponye na kuwaoko,ukaonekane kwenye mahitaji yao,wakapate kupona kimwili na kiroho pia..


Ee Mungu wetu tunaweka Nchi hii tunayoishi mikononi mwako Ukaibariki na kuwabariki watu wote tunaoshia humu,Ukatusamehe pale tulipokwenda kinyume,pale tulipokuasi na kufuata mambo yetu wenyewe..Ee Baba ukasikie kulia kwetu,ukasikie maombi yetu,ukasimame nasi katika yote,Ukatuepushe na Udini/ukabila,chuki na hasira,ukawabariki Viongozi wetu wa KIROHO Baba wa Mbinguni ukawape macho ya rohoni, ukabariki Familia zao pia,Ukawabariki na wanaotuongoza Baba wa Mbinguni wakatuongoze katika haki na kweli..
 Tuungane pamoja kuombea Amani kwenye Taifa hili,Mungu wetu ukaonekane na kutawala Milele...

Ee Mungu wetu tunaiweka Tanzania mikononi mwako,Amani ya kweli,Upendo wa Kweli,Ukaibariki na kuwabariki watu wake popote walipo,walio ndani ya Nchi na walio nje kwa sababu ya kusoma,kwa sababu ya kutafuta maisha,waliokatika matibabu na mengine yote Mfalme wa Amani ukatawale maisha yao, Ukatuongoze vyema na ukatupe mwanga katika maisha yetu,ukaonekane Mungu wetu,Kuna sababu ya kuwa Wa Tanzania haijalishi watu wanaishi wapi,wako wapi Mungu wetu yupo nasi..
Mungu wetu tunaiweka Afrika yote yote mikononi mwako waafrika popote walipo Baraka na Amani ziwafuate..
Mungu wetu tunaiweka Dunia hii mikononi mwako wewe ukawe mtawala mkuu na ukawabariki na kuwaongoza wote wanaotuongoza, Kiroho na kidunia wakatuongoze vyema kwa misingi yako Mungu wetu..

Wapendwa/waungwana tusikome kuombea Mtaifa yetu,watu wetu,Viongozi wetu wa KIROHO na wakimataifa/kidunia..
Tusichoke kuombeana mema hata kama tulikoseana tuombane msamaha na kuendela vyema katika maisha yetu,Muombee mwenzio mema,Ombea watoto wa wenzio,Tuombee Nchi tunazoishi na tulipotokea/zaliwa na watu wake Kwani Amani ikitawala hapo ulipo au ulipotokea/zaliwa nawe utakuwa na Amani ya moyo..
Ombea kazi,Karama za wengine walizobarikiwa na Mungu nawe una zako pia wengnine hawana hizo,Mungu wetu ni muweza wa yote..
Ombea adui yako,Samehe kama Mungu anavyotusamehe..
Tuachane na wivu,visasi na kukwamishana utachelewesha tuu kwani vinamwisho Mungu akimbariki mtu amembariki..

Mungu akatulinde na mabaya yote yaliyonenwa,yaliyotendwa kwa sababu yetu..Mungu akabariki vinywa vyetu na kutusamehe..tulipowanenea mabaya wengine,Tulipoadhibu,Tulipo hukumu na kusababisha makwazo kwa wengine..
Mungu akatubariki katika yote na tukajue kweli..

“Katika mwaka Dario mwana wa Ahasuero, Mmedi, alipoanza kutawala juu ya milki ya Wakaldayo, mimi Danieli nilikuwa nikivisoma kwa makini vitabu vitakatifu, na humo nikaelewa maana ya jambo lile Mwenyezi-Mungu alilomfahamisha nabii Yeremia kuhusu ile miaka sabini, muda ambao utahusika na kuharibiwa kwa Yerusalemu. Nilimwomba Mwenyezi-Mungu, kwa moyo, nikimtolea dua pamoja na kufunga, nikavaa vazi la gunia na kuketi kwenye majivu. Nilimwomba Mwenyezi-Mungu, Mungu wangu, na kuungama, nikisema: “Ee Bwana, wewe ni Mungu mkuu na wa kuogofya. Wewe ni mwaminifu kwa agano lako na unawafadhili wakupendao na kuzitii amri zako. Tumetenda dhambi, tumekosa, tumetenda maovu na kukuasi. Tumezikiuka amri zako na kanuni zako. Hatukuwasikiliza watumishi wako manabii, ambao kwa jina lako waliongea na wafalme wetu, wakuu wetu, wazee wetu na taifa letu lote. Kwako, ee Bwana, kuna uadilifu, lakini sisi daima tumejaa aibu. Jambo hili ni kweli kwetu sote tuishio Yudea, wakazi wa mji wa Yerusalemu na Waisraeli wote ambao umewatawanya katika nchi za mbali na za karibu kwa sababu ya kukosa uaminifu kwako. Aibu, ee Bwana, ni juu yetu, wafalme wetu, wakuu wetu na wazee wetu, kwa sababu tumekukosea. Wewe, Bwana Mungu wetu, una huruma na msamaha, ingawa sisi tumekuasi. Tulikataa kukusikiliza, ee Bwana, Mungu wetu; hatukuishi kulingana na sheria zako ulizotupa kwa njia ya watumishi wako manabii. Waisraeli wote wameiasi sheria yako, wamekuacha wakakataa kukutii. Kwa sababu tumekukosea, tumemwagiwa laana na viapo vilivyoandikwa katika sheria ya Mose, mtumishi wako. Umethibitisha yale uliyosema utatutenda sisi pamoja na watawala wetu kwa kuuadhibu mji wa Yerusalemu vikali zaidi ya mji mwingine wowote duniani. Umetuadhibu kama ilivyoandikwa katika sheria ya Mose, lakini mpaka sasa, ee Mwenyezi-Mungu, Mungu wetu, hatukuomba msamaha wako kwa kuziacha dhambi zetu na kutafakari uaminifu wako. Kwa hiyo, ee Mwenyezi-Mungu, Mungu wetu, ulikuwa tayari kutuadhibu, na ukafanya hivyo, kwa kuwa daima unafanya yaliyo ya haki, nasi hatukukusikiliza. “Na sasa ee Bwana, Mungu wetu, uliyewatoa watu wako nchini Misri kwa nguvu yako kuu na kulifanya jina lako litukuke mpaka sasa, tunasema kwamba tumetenda dhambi; tumefanya maovu. Ee Bwana, kwa kadiri ya matendo yako ya haki usiukasirikie wala kuughadhibikia mji wako wa Yerusalemu, mlima wako mtakatifu. Watu wote wa nchi za jirani wanaudharau mji wa Yerusalemu na watu wako, kwa sababu ya dhambi zetu na maovu waliyotenda wazee wetu. Kwa hiyo, ee Mungu, isikilize sala yangu na maombi yangu mimi mtumishi wako. Kwa hisani yako, uifadhili tena maskani yako iliyoharibiwa. Tega sikio, ee Mungu wangu; angalia uone taabu tulizo nazo na jinsi unavyotaabika huo mji uitwao kwa jina lako. Tunakutolea maombi yetu si kwa sababu tumetenda haki, bali kwa sababu wewe una huruma nyingi. Ee Mwenyezi-Mungu, utusikie; utusamehe ee Mwenyezi-Mungu. Ee Mwenyezi-Mungu, kwa hisani yako utusikie na kuchukua hatua, wala usikawie, ee Mungu wangu, kwa ajili ya mji huu na watu hawa wanaoitwa kwa jina lako!
Sifa na Utukufu tunakurudishia Mungu wetu..
Tunayaweka haya yote  mikononi mwako Mungu wetu..
Kwakua Ufalme ni wako Nguvu na Utukufu hata Milele..
Amina..!

Asanteni sana wote mnaotembelea hapa..
sina neno zuri lakusema..zaidi ya kuwaombea
Baraka na Amani zikamiminike katika maisha yenu..
Nawapenda.

Aroni anatoa sadaka

1Siku ya nane baada ya siku saba za kuwekwa wakfu, Mose akamwita Aroni na wanawe pamoja na wazee wa Israeli. 2Mose akamwambia Aroni, “Chukua ndama dume kwa ajili ya sadaka ya kuondoa dhambi na kondoo dume kwa ajili ya sadaka ya kuteketezwa; wanyama wote wasiwe na dosari. Kisha watoe sadaka mbele ya Mwenyezi-Mungu. 3Waambie Waisraeli wachukue beberu mmoja kwa ajili ya sadaka ya kuondoa dhambi, na ndama mmoja na mwanakondoo mmoja wote wa umri wa mwaka mmoja na wasio na dosari kwa ajili ya sadaka ya kuteketezwa, 4fahali mmoja na kondoo dume mmoja kwa ajili ya sadaka za amani, wakamtolee Mwenyezi-Mungu pamoja na sadaka ya nafaka iliyochanganywa na mafuta kwa maana leo Mwenyezi-Mungu atawatokea.”
5Waisraeli wakaleta vyote hivyo mbele ya hema la mkutano kama Mose alivyowaamuru na jumuiya yote ikaenda kusimama mbele ya Mwenyezi-Mungu. 6Mose akawaambia, “Hili ndilo jambo ambalo Mwenyezi-Mungu aliwaamuru mlifanye ili utukufu wake uonekane kwenu.” 7Hapo Mose akamwambia Aroni, “Nenda kwenye madhabahu, utolee hapo sadaka yako ya kuondoa dhambi na sadaka ya kuteketezwa na kufanya ibada ya upatanisho kwa ajili yako na kwa ajili ya watu wa Israeli. Kisha tolea hapo sadaka za watu na kuwafanyia ibada ya upatanisho kama alivyoamuru Mwenyezi-Mungu.”
8Basi, Aroni akaikaribia madhabahu, akamchinja yule ndama aliyemtoa awe sadaka ya kuondoa dhambi yake mwenyewe. 9Wanawe wakamletea damu, naye akachovya kidole chake katika damu hiyo na kuzipaka pembe za madhabahu. Damu iliyosalia akaimwaga kwenye tako la madhabahu. 10Lakini mafuta na figo akaviteketeza vyote juu ya madhabahu kama Mwenyezi-Mungu alivyomwamuru Mose. 11Lakini ile ngozi akaiteketeza kwa moto nje ya kambi.
12Kisha Aroni akamchinja mnyama wa sadaka ya kuteketezwa. Wanawe wakamletea damu, naye akainyunyizia madhabahu pande zote. 13Kisha wakamletea sadaka ya kuteketezwa, kipande kimojakimoja, na kichwa; naye akaviteketeza juu ya madhabahu. 14Akaosha matumbo na miguu na kuiteketeza pamoja na ile sadaka ya kuteketezwa kwenye madhabahu.
15Kisha, Aroni akaweka mbele sadaka ya watu. Alimchukua mbuzi wa sadaka ya watu ya kuondoa dhambi, akamchinja na kumtoa sadaka ya kuondoa dhambi, kama alivyofanya kwa yule wa kwanza. 16Kisha akaweka mbele ile sadaka ya kuteketezwa akatolea sadaka hiyo kulingana na agizo. 17Kisha akaweka mbele sadaka ya nafaka akijaza konzi moja na kuiteketeza juu ya madhabahu pamoja na sadaka ya kuteketezwa ya kila asubuhi.
18 # Taz Lawi 3:1-11 Halafu Aroni akamchinja pia fahali na yule kondoo dume wa sadaka za amani kwa ajili ya watu. Wanawe wakamletea damu ambayo aliinyunyizia madhabahu pande zote. 19Mafuta ya fahali huyo na kondoo dume, mkia wa kondoo, mafuta yaliyofunika matumbo, figo na sehemu bora ya ini 20wakayaweka juu ya vidari, naye akaviteketeza kwenye madhabahu. 21Lakini vile vidari na ule mguu wa nyuma wa kulia, Aroni alifanya navyo ishara ya kumtolea Mwenyezi-Mungu, kama Mose alivyoamuru.
22 # Taz Hes 6:22-26 Aroni alipomaliza kutolea sadaka zote: Sadaka za kuondoa dhambi, sadaka za kuteketezwa na sadaka za amani, aliwainulia watu mikono, akawabariki, kisha akashuka chini. 23Ndipo Mose na Aroni wakaingia ndani ya hema la mkutano; walipotoka waliwabariki watu, nao utukufu wa Mwenyezi-Mungu ukaonekana kwa watu wote. 24Mwenyezi-Mungu akawasha moto ukaiteketeza sadaka ya kuteketezwa na mafuta yaliyokuwa juu ya madhabahu. Watu wote walipouona huo moto walipaza sauti na kusujudu.

Mambo Ya Walawi9;1-24


Biblia Habari Njema kwa Watu Wote(BHN)

"Swahili Na Waswahili"Mbarikiwe.

No comments: