Swahili na Waswahili

Swahili na Waswahili
Waswahili na Mswahili Rachel Siwa...Pamoja Daima!!

Sunday 10 May 2015

TIMU TANZANIA YASHIRIKI MATEMBEZI YA SUSAN G. KOMEN WASHINGTON, DC




Timu Tanzania ikipata picha ya pamoja kabla ya kuanza matembezi ya saratani ya matiti ya Susan G. Komen yaliyofanyika Washington, DC siku ya Jumamosi May 9, 2015.


Wanusurika wa saratani ya matiti wakipata picha ya pamoja.


Matembezi yakianza.


Kushoto ni msaniii toka uingereza Matt Goss aliyeimba wimbo maalum wa Strong kwa ajili ya matembezi haya ya Susan G. Komen ambaye mwaka jana mama yake mzazi alifariki kutokana na maradhi ya saratani ya matiti akipeana mkono na watembeaji wa saratatani ya titi. Kati ni Nancy G. Brinker mdogo wake Susan G. Komen akipeana mkono na watembeaji siku ya maadhimisho ya matembezi ya saratani ya matiti kwa kumuenzi dada yake kwa kuanzisha oganaizesheni ya kupigana na gonjwa hili hatari mwaka 1982 kama ahadi aliyomwekea dada yake.


Mmoja ya watembeaji na mnusurika wa saratani ya titi akipatiwa huduma ya kwanza na watembeaji wenzake baada ya kuanguka na kupata majeraha kwenye paji la uso huku wakisubili gari la wagonjwa.


Timu Tanzania ikichanja mbuga kwenye matembezi hayo.


Mwanahabari wa Kwanza Production na Vijimambo Media Mubelwa Bandio(kulia) akiwa sambamba na mwimbaji Matt Goss na Nancy G. Brinker CEO wa Susan G. Komen


Timu Tanzania ikiwa imemaliza matembezi yao ya maili 3 takribani na kilomita 5


Watoto wa wazazi Watanzania wakipata picha ya pamoja baada ya kumaliza matembezi hayo na wazazi wao.


Picha ya pamoja ya kumaliza matembezi hayo pamoja na mmoja wa kikosi cha zima moto wa TDF aliyejumuika kupiga picha na timu Tanzania.

Picha zote na Kwanza Production na Vijimambo Media & Entertainment.
Kwa picha zaidi bofya HAPA

1 comment:

Mbele said...

Mimi kama m-Tanzania niliyeko hapa ughaibuni--na hata kama ningekuwa kwetu TZ--nimeguswa na taarifa na picha hizi. Nimeguswa na mshikamano wenu. Nimeguswa na namna mlivyowashirikisha watoto, taifa la kesho. Ni elimu bora kwao. Kwa yote hayo, nawapeni pongezi. Mungu aendelee kuwaongoza katika njia hii.