Swahili na Waswahili

Swahili na Waswahili
Waswahili na Mswahili Rachel Siwa...Pamoja Daima!!

Friday 20 March 2015

Maisha na Malezi;Mama Mtumwa Wa Mapenzi..!!!


MAMA MALKIA WA UPENDO        💎
                                
💞MAMA MTUMWA WA MAPENZI💞          💎

🌾🍃Mwanadamu ulizaliwa katika hisia za kulia  ukiwa kichanga mwenye uchafu Asili ya upendo ipo kwa mama ulipofumbua macho ulikutana na tabasamu la mama.

🌾🍃Mama alitabasamu wakati unalia mama alijifanya uchizi ili kukufurahisha ghafla ungetokea kuwaona mtoto anapocheza na mama yake ungelidhani wote ni watoto kwa mapenzi ya mama.

🌾🍃Mwanadamu tambua unaweza umizwa na wengi lakini upendo wa mama ukakufanya utulie na hakuna mapenzi ya kweli kwa mtu kama mapenzi ya mama.

🌾🍃Mama juu yako baya likikukuta mama hulia mama yupo tayari kudanganya ulimwengu kukukomboa katika matatizo yako.

🌾🍃Alificha chakula wakati ukicheza udogoni na uliporejea ukamkuta amelala lakini aliacha maagizo utakuta wapo wa kukupashia yote mapenzi.

🌾🍃Mama alipoamka mwanzo alikuulizia ameshakula? Ima umekula atafurahi ima hujala atapita majumba ya watu kukuulizia hata kama atatoka miguu peku yote mapenzi tu.

🌾🍃Ulipoumwa usiku halali atataabika kwa kukaa na wewe ukiwa mikononi mwake huku akilalila ukuta pembeni mwa kitanda huku akitarajia pakikucha shingo limuume kwa kukesha na wewe yote mapenzi hayo.

🌾🍃Mtu yoyote akikupenda watu watamshangaa kwanini anakupenda sana? Lakini mapenzi ya mama hayaulizwi kwanini anampenda yote ni nguvu za hisia za upendo toka kwa mama.

🌾🍃Umekuwa sasa huenda hayupo tena mama amekuacha katika dunia ya mihangaiko na wala tambua hakuna tena kiumbe kitachokupenda kama alivokuwa mama.

🌾🍃Na ukiwa umebarikiwa upendo ulio hai kwako namaanisha uhai wa mama basi huenda amechokaa na anatembea kama mtoto sasa rudisha upendo wako kwa kumfanya nae afurahi japo hutoweza kulipiza yote.

🌾🍃Mama utamkumbuka utapomkosa utatamani kuita mama na hata ukipata wa kuwaita upendo hautatoka moyoni.

🌾🍃Wakati ulipotoka alitabasamu basi na wewe hakikisha wakati anakukimbia duniani mfanye atabasamu hata kama atatokwa na machozi .

🌾🍃Mtumie ujumbe huu Mama na kama hunae tena muombe kwa MOLA upatapo ujumbe huu watumie wenzako huenda wakafufua hisia kwa Mama.

🌾🍃HUYU NDIO MAMA MALIKIA WA UPENDO. 

 🌴🐪KISIWA CHA IMANI🐪🌴


Nimetumiwa na Rafiki Nami nimeileta hapa tujifunze sote.

"Swahili Na Waswahili" Pamoja Saima.

2 comments:

Yasinta Ngonyani said...

Imenigusa mno na nimemkumbuka sana mama........

Rachel Siwa said...

Pole da'Yasinta...